Tuesday, March 29, 2011

BAADHI YA PICHA WAKATI WA MUSIC AWARD













20 PERCENT AWAANGUSHA MASHAROBARO - KILI MUSIC AWARDS



Abbas Hamis, marufu kama “20 percent” aliwashangaza masharobaro na kuibuka mfalme pale alipojinyakulia Tuzo tano katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, siku ya jumamosi usiku.

20 percent ambaye hakuwepo ukumbini, alijitwalia tuzo za Mwanamuziki wa mwaka wa kiume, Mwanamuziki bora wa kiume na Mwandishi bora wa Mwaka, ambapo nyimbo zake mbili “Tamaa mbaya” na “Ya nini Malumbano” zilipigiwa kura kwa Wimbo wa mwaka, na Wimbo bora wa Kiafrika. Nyota huyo ni Mwimbaji na mtunzi bora.

Tuzo za 20 percent zilipokelewa na producer wake Man Walter

Monday, March 21, 2011

Una kazi ya sanaa unataka kuitangaza?

Iwapo una kazi ya sanaa unayotaka kuitangaza, kama kwaya, muziki,ngoma, sanaa za maonyesho, n.k. tuma picha ya kazi hiyo pamoja na maelezo mafupi kwenda kwa wangahp@gmail.com. Kazi hiyo itawekwa katika blog bure. Ukiona tangazo hili mtaarifu na mwenzako.

Wednesday, March 2, 2011

Utafiti kwenye sanaa na wasanii

Napenda kufahamu kama kuna mtu aliyefanya utafiti (research) kwenye kuboresha maslahi ya wasanii na ubora wa kazi zao. Pia kama kuna mtu anayefahamu journal yeyote Tanzania, au Afrika inayohusu kazi za wasanii.