Tuesday, May 31, 2011

Blatter denies FIFA in crisis and will seek fourth term in charge


A defiant Sepp Blatter shrugged off allegations of corruption within FIFA Monday and said he would press ahead with his bid to be re-elected as president of football's world governing body for the fourth time.

Blatter will be the sole candidate in Wednesday's election in Zurich after Qatari Mohamed Bin Hammam, the only person standing against him, was suspended by the FIFA ethics committee Sunday, along with fellow leading official Jack Warner.

"We are not in a crisis, we are only in some difficulties and these can be solved inside our family," Blatter told a press conference Monday where he was continually pressed on both his own position and wider allegations of wrongdoing within FIFA.

"FIFA is strong enough to deal with our own problems," he asserted when asked if he had considered postponing Wednesday's vote by the 208-member FIFA Congress.

Fresh strikes in Libya as Zuma says Gadhafi is ready for cease-fire

Tripoli, Libya (CNN) -- Fresh explosions rang out early Tuesday near Tripoli, hours after South African President Jacob Zuma held talks with Moammar Gadhafi and signalled he was ready to accept an African Union plan for a cease-fire.

Around 12:45 a.m. Tuesday, a pair of large blasts were heard about five minutes apart, as jets flew over the capital of Tripoli.

A Libyan government official said the first strike hit Abu Sita, a former military turned construction site about 10 kilometers (6 miles) from the city center. There was no immediate indication of where the second explosion occurred. Nor was there an immediate response from NATO, which has conducted regular strikes as part of its stated mission to halt Libyan leader Gadhafi's forces from killing innocent civilians.

Hours before the blasts, Zuma emerged from a meeting with the longtime Libyan strongman convinced that Gadhafi was ready for an end to hostilities, including such airstrikes and the ongoing fight with the Benghazi-based opposition movement. But he gave no indication that Gadhafi was prepared to step aside, as rebel leaders have insisted is their primary demand.

"Brother leader took the position today that he is ready to implement the decision of the AU (that) there must be a cease-fire," Zuma told a scrum of reporters on the tarmac at Tripoli's Mitiga International Airport before boarding a jet. "The view is that that must include -- bombing by NATO must also come to an end," he said in the news conference, which was broadcast on Libyan state television.

Zuma added that Gadhafi said any cease-fire must apply to all parties, "but also, he makes the point that: Let the Libyan people be given a chance to talk among themselves. And therefore, he's ready to implement the road map of the AU."

Unlike some other world leaders, Zuma has not called for the longtime Libyan leader to step down. Neither has Zuma's African National Congress party nor the African Union, which he was representing and which Gadhafi once led. In fact, the AU has criticized the NATO airstrikes.

In April, Zuma led an AU delegation to Tripoli, where hopes were raised briefly when it was announced that Gadhafi had agreed, in principle, to the African Union's "road map" proposal for peace. But Gadhafi continued his attacks and the Libyan opposition rejected the proposal because it did not meet its demand that he give up the power he has held for 42 years.

A government official said Libyan Prime Minister Al-Baghdadi Ali al-Mahmudi also attended Monday's meeting. Baghdadi greeted Zuma upon his arrival at the airport, where dozens of Gadhafi supporters carried posters, some of which said, "May the leader be victorious" and "Thanks for great Africa."
The African Union has helped mediate peace talks before, including ones in Kenya and Zimbabwe that left the ruling powers in control.

It was not clear whether Zuma used the opportunity to press Gadhafi for information on the whereabouts of South African freelance photographer Anton Hammerl. Hammerl has been missing in Libya since April and is believed dead. South Africa has said it got assurances from Libya that the journalist was alive. But a Libyan government spokesman has said his whereabouts were unknown. "We never had him with us at any stage," spokesman Musa Ibrahim has said.

The meeting came as Gadhafi's grip on power appeared to continue to loosen. Eight generals from his army have defected to Italy, the Italian Foreign Ministry told CNN Monday. The generals were accompanied by more than 100 Libyan soldiers, a senior Italian official with firsthand knowledge of, and responsibility for, the operation said.

Marando: Tunamtaka Rais Kikwete mahakamani
















Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, WAKILI Mabere Marando anayemtetea Profesa Costa Mahalu aliyekuwa na Balozi wa Tanzania nchini Italia, amesema ataiomba mahakama imlazimishe Rais Jakaya Kikwete kufika mahakamani kumtetea mteja mteja wake iwapo hatakubali kwenda kutoa ushahidi baada ya kuombwa kufanya hivyo kwa barua.Marando ametoa kauli hiyo wakati Profesa Mahalu na mwenzake Grace Martin wakianza kujitetea leo.

Mbali na utetezi wao binafsi, wanatarajia pia kuwa na mashahidi kadhaa wa kuwatetea akiwamo Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa pamoja na Rais Kikwete.Tayari Rais Mkapa amewasilisha mahakamani hapo hati yake ya kiapo akimtetea Profesa Mahalu na mwenzake kuhusiana na tuhuma zinazowakabili huku akibainisha kuwa yuko tayari kufika mahakamani iwapo italazimu.

Lakini hadi jana, Rais Kikwete alikuwa hajajibu barua aliyoandikiwa na Wakili Marando kwa niaba ya wateja wake wakimwomba akubali wa kufika mahakamani kuwatetea au kuwasilisha kiapo chake ambacho kitatumika kama ushahidi wa utetezi dhidi yao.

Marando alisema jana kuwa Rais Kikwete alikuwa hajajibu barua hiyo, lakini akasema ikiwa Profesa Mahalu atamaliza kujitetea pamoja na mashahidi wengine kabla Rais Kikwete hajakubali, wataiomba mahakama imkumbushe.

“Kama atakaidi hata baada ya mahakama kumwandikia, basi tutaomba kesi hiyo iahirishwe hadi mwaka 2016 (wakati atakapokuwa amemaliza muda wake wa urais) ili imlazimishe kuja kutoa ushahidi huo,” alisema Marando.

Mei 3, mwaka huu Wakili Marando alimwandikia barua Rais Kikwete yenye kumbukumbu namba MM/PCRM/2011/1 kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, akibainisha kuwa ni miongoni mwa mashahidi muhimu ambao wateja wao wamewaagiza wamwite.

Barua hiyo inabainisha kuwa umuhimu wa Rais Kikwete katika ushahidi huo wa utetezi unatokana na ukweli kwamba nyumba hiyo ya Ubalozi wa Italia ilinunuliwa wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na kwamba alikuwa na taarifa zote kuhusu mchakato wa ununuzi wake.

Mchakato huo, kwa mujibu wa barua hiyo ni pamoja na nguvu ya kisheria aliyopewa mteja wao ambayo ilisainiwa na Rais Kikwete wakati huo akiwa Waziri Septemba 24, 2004 pamoja na hotuba yake aliyoitoa Bungeni Agosti 3, 2004 akithibitisha kuwa ununuzi wa jengo hilo haukuwa na mushkeli wowote.

Pia barua hiyo inaweka wazi kuwa kuna barua nyingi tu ambazo Profesa Mahalu alimwandikia Kikwete akiwa waziri, pamoja na katibu mkuu wa wizara hiyo, ambazo anapaswa kuzitambua mahakamani wakati wa utetezi.

“Kwa hiyo tunaomba kwa unyenyekevu kabisa, uweke barua yetu hii mbele ya Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania; aisome na akueleze utujibu kama hana pingamizi kuja kueleza ukweli mahakamani. Kama muda wake hauruhusu, kulingana na ratiba zake za kitaifa, tunaomba aturuhusu tumwandalie kiapo (affidavit) kitakachoeleza yaliyotekea ili tukiwasilishe mahakamani badala ya kumwita yeye mahakamani”, inasisitiza barua hiyo na kuongeza kuwa hakuna kifungu cha Katiba kinachozuia Rais kuitwa kutoa ushahidi mahakamani.

Katika kiapo chake alichokiwasilisha mahakamani, Mkapa anamtetea Mahalu na akidai kuwa amefanya naye kazi kwa muda mrefu na anamjua kuwa ni mtu mwaminifu, mtiifu na mchakapakazi. Mkapa alieleza katika hati yake hiyo kuwa mchakato wa ununuzi wa jengo hilo ulifanyika wakati wa uongozi wake na kwamba alikuwa akijua kila kilichokuwa kikiendelea kuhusiana na ununuzi huo na kwamba ulifanyika kwa mujibu wa sheria.

Alifafanua kuwa mpango wa ununuzi wa jengo hilo ulikuwa ni utekelezaji wa sera ya serikali wa kuwa na majengo yake ya kudumu katika kila ubalozi kwa kununua au kujenga ikiwa ni njia ya kupunguza gharama za upangaji. Aliongeza kuwa serikali yake ilimpa Profesa Mahalu mamlaka yote kupitia nguvu ya kisheria ya kusimamia na kutekeleza mchakato wa ununuzi wa jengo.

Mkapa alisisitiza kuwa kupitia utaratibu wa serikali, alikuwa akijua kuwa taarifa ya uthamini wa jengo hilo iliyofanywa na Wizara ya Ujenzi ilikuwa ni Dola za Marekani 3.0 milioni wakati Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ilikadiriwa Euro 5.5 milioni: “Kupitia utaratibu wa serikali nilifahamu kuwa jengo hilo lilinunuliwa kwa gharama ya Dola za Marekani 3.0milioni sawa na Euro 3,098,741.40,” alisema Mkapa.
Pia Mkapa alisisitiza kuwa alikuwa na bado anatambua taarifa ya serikali bungeni ya Agosti 3, 2004 iliyoeleza na kuthibitisha kuwa taratibu zote za ununuzi wa jengo hilo zilifuatwa kwa mujibu wa maelekezo ya serikali na kwamba dalali alilipwa kikamilifu.

“Kwa kipindi chote ambacho nimefanya kazi na Balozi Mahalu katika nafasi mbalimbali za utumishi wa serikali ameonyesha tabia thabiti na za dhati, uaminifu, utiifu, uchapakazi na ubora," alisema Mkapa.

Alisema kuwa sifa hizo zilimfanya atunukiwe na Rais wa Italia, Tuzo ya Heshima ya Juu wakati wa kuadhimisha Siku ya Taifa hilo, muda mrefu baada ya kuwa ameondoka nchini humo.

Profesa Mahalu na mwenzake, Martin aliyekuwa Ofisa Utawala wa ubalozi huo wanakabiliwa na mashtaka hayo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakidaiwa kuhujumu uchumi kwa kuisababishia Serikali hasara ya Euro 2,065,827.60. Wanadaiwa kusababisha hasara hiyo kupitia mchakato wa ununuzi wa jengo la ubalozi huo, wakati wa utumishi wao.

Kutokana na mashtaka hayo, leo wanadiplomasia hao wanaanza kujitetea baada ya mahakama hiyo kuwaona kuwa wana kesi ya kujibu.Mahalu na Martin wanadaiwa kula njama na kutenda makosa hayo katika tarehe tofauti na katika maeneo tofauti huko Italia, likiwamo la kumpotosha mwajiri wao katika hati ya matumizi.

Miongoni mwa mashtaka hayo ni kwamba Septemba 23, 2002 huko Rome, washtakiwa wakiwa waajiriwa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walisaini vocha yenye namba D2/9/23/9/02 ikionyesha kuwa bei ya ununuzi wa jengo la ubalozi ni Euro 3,098,741.58, maelezo ambayo yalikuwa ni ya uongo na yenye nia ya kumdanganya mwajiri wao.

Monday, May 30, 2011

Mtikila: Ridhiwani nenda mahakamani




Mchungaji Christopher Mtikila
LICHA ya mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani kuwaandikia barua ya kusudio la siku 10 kuwafikisha mahakamani Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa na Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameambiwa aende huko mahakamani.

Katika kusudio lake Ridhiwani amedai kuwa endapo watashindwa kumwomba radhi na kumlipa Sh2 bilioni atakwenda mahakamani.Katika kusudio hilo, Ridhiwani amewataka wanasiasa hao wamwombe radhi na kumlipa fidia hiyo ndani ya siku kumi kuanzia Mei 13, kwa madai waliyoyatoa hadharani kuwa yeye ni bilionea aliyetajirika kifisadi.

Katika kusudio hilo, Ridhiwani pia amehusisha gazeti la Tanzania Daima ambalo amedai limechangia kumchafua kwa kuripoti madai ya wanasiasa hao dhidi yake.

“Tumeelekezwa na mteja wetu kuwataka wote kwa pamoja kukanusha na kusahihisha tuhuma zote na kuchapisha habari hiyo ya kuomba radhi kwa uzito na herufi kubwa (bold print) katika kurasa za mbele  wa gazeti hilo (Tanzania Daima) kwa siku tatu mfululizo hadi Mei 23, 2011," alieleza wakili Sam Mapande wa Law Associates, anayemwakilisha Ridhiwani.Wakili huyo aliendelea, "Pia, wote kwa pamoja mnatakiwa kulipa fidia ya Sh2 bilioni kwa madhara ya jumla aliyopata mteja wetu.”

Barua hiyo ya kurasa sita  imetaja baadhi ya maneno yaliyoandikwa kwenye matoleo mawili ya gazeti la Tanzania Daima yakimkariri Dk Slaa na Mchungaji Mtikila, wakimhusisha pia Rais Jakaya Kikwete na mwanaye (Ridhwani) na watu wengine walio karibu yake na matukio ya ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka na ofisi ya umma. Kwa mujibu wa Ridhiwani, madai hayo yamemchafulia jina, kumdhalilisha, kumshushia hadhi na heshima yake katika jamii inayomzunguka.

Mhariri wa gazeti la Tanzania Daima, Absalom Kibanda amekiri kupokea barua hiyo, lakini akasema hawezi kusema chochote kwa jambo ambalo ni la kisheria. “Kwa kuwa bado hatujafikishwa mahakamani, siwezi kusema tumejiunga vipi. Tunasubiri tufikishwe mahakamani kwanza,” alisema Kibanda.

Mchungaji Christopher Mtikila amemtaka mtoto huyo wa rais kwenda mahakamani haraka akidai kuwa hana shaka kwa kuwa ana ushahidi mzito kuthibitisha madai yake.Mtikila aliwaambia waandishi wa habari mjini Arusha jana kuwa, kesi hiyo itakuwa ni ukombozi kwa taifa kwa sababu itampa yeye na mwenzake, Dk Slaa muda wa kueleza kile alichokiita madudu yanayofanywa na mtoto huyo wa rais.
Mtikila aliendelea kudai kuwa Ridhwani anatumia vibaya ofisi na madaraka ya baba yake (Rais Kikwete) kujilimbikizia mali kinyume cha sheria.

“Kitendo cha Ridhwani kutaka aombwe radhi na fidia ni njia na ngazi muhimu itakayosaidia mambo mengi yaliyojificha kuwekwa hadharani," alisema Mtikila na kuongeza:"Tutatumia sheria zilizopo kuwabana wote ambao majina yao yameandikishwa kwenye mali za vigogo nchini waeleze walivyopata mali hizo na hapo ndipo watakapowataja wahusika halisi,” alisema Mtikila.

Kiongozi huyo wa DP aliendelea kudai kuwa viongozi wengi nchini wamejilimbikizia mali kupitia wizi na ufisadi, wakitumia nafasi zao za umma huku wakiandikisha majina ya watu wengine kwenye mali hizo kuficha umiliki wao.

Alidai kuwa kesi anayotaka kuifungua Ridhiwani itaibua mambo mengi kwani walioandikishwa majina kwenye mali hizo, watawataja wamiliki halisi badala ya kufungwa jela kwa kumiliki mali inayodhaniwa kuwa ya wizi au kupatikana isivyo halali.

Kwa upande wake, Dk Slaa jana hakupatikana kuzungumzia kusudio hilo la Ridhiwani kutokana na simu yake ya kiganjani kutopatikana kwa siku nzima.

Jana, Ridhiwani alipotakiwa kueleza nini kinafuata baada ya muda aliotoa kuisha alijibu kwa ufupi kuwa asingependa kuzungumzia suala hilo kwa kuwa ni jambo la kisheria na kwamba sheria ina kanuni zake.

"Ndugu yangu, sitaki kuzungumzia hili kwa kuwa sheria ina kanuni zake. Hili litazungumzwa mahakamani."
Dk Slaa na Mtikila walikaririwa mwanzo wa Mei wakisema kuwa mtoto huyo wa rais ana utajiri mkubwa licha ya kumaliza shule miaka ya karibuni huku wakimtuhumu kutumia cheo na madaraka ya baba yake kujitajirisha.
 

Air France crash pilots lost vital speed data, say investigators

(CNN) -- Pilots of the Air France flight that crashed in 2009 and plummeted 38,000 feet in just three minutes and 30 seconds, lost vital speed data, France's Bureau of Investigation and Analysis (BEA) said Friday.
The pilots got conflicting air speeds in the minutes leading up to the crash, the interim reports states. The aircraft climbed to 38,000 feet when "the stall warning was triggered and the airplane stalled," the report says.
Aviation experts are asking why the pilots responded to the stall by pulling the nose up instead of pushing it down to recover.

Miles O'Brien, a pilot and aviation analyst, said: "You push down on the wheel to gain air speed, perhaps they (pilots) were getting information that the air speed was too high. Pulling the nose up will exacerbate an aerodynamic stall."

The speed displayed on the left primary flight display were "inconsistent" with those on the integrated standby instrument system (ISIS), the report says.

 
New details on cause of Air France crash
 
 
What caused the Air France crash?
 
 
Map: Air France Flight 447

The aircraft experienced some "rolling" before stalling and then descending rapidly into the ocean. The descent lasted 3 minutes and 30 seconds and the engines remained operational, said the report. It plunged at 10,912 feet (3,300 meters) per minute.

At the time of the descent, the two co-pilots and captain were in the aircraft cockpit.

Saturday, May 28, 2011

Basi la Sumry laua 15 Mbeya

Wimbi la ajali za barabarani limeendelea kuikumba nchi ambapo jana usiku majira ya saa nne usiku basi linalomilikiwa na kampuni ya Sumry lilipata ajali na kuua 15 papo hapo na kujeruhi wengine 20. Basi hilo lililokuwa linatoka Arusha kuelekea Mbeya lilipata ajali eneo la Igawa, Mbarari, Mbeya. Maiti na majeruhi waliwahishwa katika hospitali za Ilembula na Mbarari.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya Advocate Nyombi alisema chanzo cha ajali ni kupasuka kwa gurudumu la basi hilo. Dereva wa basi ni kati ya watu waliokufa katika ajali hiyo.

Friday, May 27, 2011

Tamko la Vijana Arusha lazidi kuivuruga CCM

















TAMKO la baadhi ya vijana wa UVCCM, Mkoa wa Arusha kutaka mafisadi wafukuzwe, limezidi kukivuruga chama hicho baada ya Katibu Mkuu, Wilson Mukama kusema hawezi kujiingiza 'kichwa kichwa' kuzungumzia suala hilo, huku baadhi ya watuhumiwa wakikataa kulizungumzia. Mukama alisema CCM inafuatilia kwa karibu mgogoro huo, lakini haiwezi kuuzungumzia sasa kwa kuwa hajapata taarifa rasmi kutoka umoja wa vijana.

Kwa mujibu wa Mukama, UVCCM ni jumuiya halali ya chama tawala yenye mamlaka kamili ya kuzungumzia matatizo yake, hivyo yeye kusema chochote itakuwa ni kuingilia kazi za jumuiya hiyo.
“Chama chetu kina utaratibu wake, UVCCM ni jumuiya ndani yake, hayo yaliyotokea kule Arusha siwezi kuyazungumzia, ila kesho (leo) tuna kikao, hivyo wao vijana watatupa taarifa zao,” alisema Mukama, huku akisoma ujumbe mfupi wa simu (sms) alioandikiwa na katibu mkuu wa umoja huo, Martin Shigella kuwa watatoa taarifa ya yaliyotokea Arusha.

“Suala la Arusha tunalifuatilia kwa ukaribu sana, ila utendaji tunawaachia wao (UV-CCM), nasi tukishapata taarifa zao ndio tutaweza kulizungumzia suala hilo, ila kwa sasa mtafute Shigella,” alielekeza Mukama.
Alipotafutwa kwa simu jana kuzungumzia tuhuma hizo, Shigella alisema kuwa hawezi kutolea ufafanuzi kwa kuwa alikuwa nje ya nchi kikazi. “Sikuwapo nchini, kwa hiyo sitaweza kuzungumza lolote, kuna mtu alikuwa akikaimu nafasi yangu, hivyo nikipata maelezo kutoka kwake nitakuwa tayari kuzungumza, nitafute kesho (leo),”alisema Shigella.

Naye makamu mwenyekiti wa umoja huo taifa, Benno Malisa alisema wamesikitishwa na kauli zilizotolewa na vijana wenzao wa Arusha, hivyo watatuma kamati ya maadili kwenda kuzungumza na makundi yanayolumbana. “Hivi karibuni Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM itakaa na kutoa uamuzi, lakini ni baada ya Kamati ya Maadili itakayotumwa kuzungumza na wanachama wanaolumbana huko Arusha kuleta ripoti makao makuu ya umoja wetu,”Alisema Malisa.

Akizungumzia adhabu wanazoweza kupewa wanachama wa umoja huo, Malisa alisema adhabu hizo zitatokana na aina ya makosa watakayokutwa nayo. “Suala hili liko ndani ya uwezo wetu na tutalifanyia kazi na kuchukua hatua kwa mujibu wa kanuni za UVCCM, kama kutakuwa na makosa makubwa zaidi yatapelekwa  ngazi za juu zaidi,”alisema Malisa.

Juzi, UVCCM Mkoa wa Arusha waliuomba uongozi wa juu wa chama tawala kuwafukuza uanachama viongozi watatu, wakiwamo Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na mwenzake wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge wanaotuhumiwa kwa ufisadi.

Vijana hao pia walikishauri chama hicho kupitia kamati yake ya maadili kuwaita na kuwahoji makada hao maarufu na baadaye kuwachukulia hatua, zikiwamo za kuwafukuza kwa maslahi ya chama na taifa. Tamko hilo lililosomwa na mjumbe wa baraza la umoja huo mkoani Arusha, Ali Babu lilitaka watuhumiwa hao waliowaita mapacha watatu, kuwa ndio chanzo cha kudhoofika kwa chama hicho tawala.

"Pia, tunasisitiza Andrew Chenge aondolewe kwenye Kamati ya Maadili ya CCM mara moja na kumtaka mtuhumiwa mwingine (jina tunalo) aondolewe pia kwenye uongozi wa ndani ya umoja wetu," ilieleza sehemu ya taarifa hiyo. Lakini, alipotafutwa jana kuzungumzia tuhuma hizo, Chenge alijibu kwa ufupi: "Kwa sasa sitaki kuzungumzia masuala hayo. Kila la heri."

Naye Lowassa alipotafutwa alisema kwa ufupi: ‘no comment’ akimaanisha kuwa hawezi kulizungumzia suala hilo.

Hata hivyo, wakati makada hao wakigoma kuzungumzia suala hilo, mwenyekiti wa umoja huo Mkoa wa Arusha, James ole Milya anayeshinikizwa kujiuzulu wadhifa huo, jana aliibuka na kudai kuwa tamko hilo lilitolewa na kundi la vijana aliowaita wahuni wa mitaani na wasiokuwa na kazi.

“Wale ni wahuni, hawana chochote wala lolote, wanapenda kukaa vijiweni hawana kazi za kufanya, tuna taarifa kwamba walitumwa na baadhi ya viongozi hapa Arusha kupindisha na kuvuruga hoja za umoja wetu mkoani  Arusha,” alisema Milya

Alisema kuwa vijana hao wakiongozwa na Ali Babu hawatambuliki ndani ya umoja huo, huku akisisitiza  kwamba hoja na malalamiko yote hupitishwa katika ngazi husika ili ziweze kufanyiwa kazi na sio kuibuka na kutoa matamshi yasiyo na tija.

Millya aliendeleza msimamo wake wa kutaka Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Mary Chatanda ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu aondoke madarakani kwa madai ya kusababisha jimbo kwenda upinzani (Chadema), huku akimtaka katibu huyo asikilize kilio chao (UVCCM) cha kumtaka aondoke. Alisema kuwa endapo kiongozi huyo ataendelea kung'ang'ania nafasi yake, basi atang’olewa kwa maandamano ya vijana yasiyokuwa na kikomo ambayo yatafanywa na wanachama wa umoja huo.

“Msimamo wetu uko pale pale, Chatanda ni lazima aondoke kwa kuwa amekivuruga chama chetu, ametuchonganisha na viongozi wa dini, lakini pia amesababisha Jimbo la Arusha Mjini liangukie upinzani kwa kukimbilia Tanga kusaka ubunge wa viti maalumu kipindi cha uchaguzi,”alisisitzia Milya.

Juzi,  katika mkutano wao wenye malengo makuu sita, vijana hao wa Mkoa wa Arusha walisema wanaunga mkono falsafa ya CCM ya kujivua gamba."Tunaipongeza na kuiunga mkono Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa kutambua kwamba mafisadi wamechangia sana kukidhoofisha na kukipotezea mvuto chama chetu mbele ya umma wa Watanzania," ilisema taarifa hiyo na kuongeza:
"Kwa mantiki hiyo tunatamka kwa kauli moja kwamba mapacha hao watatu wa ufisadi (wakiwataja kwa majina) na vibaraka wao wafukuzwe mara moja kwa maslahi ya CCM na Watanzania."

CUF yamtaka Nahodha ajiuzuru

*Ni kutokana na mauaji ya wananchi  watano Tarime 
*Yalaani, yasema huo ni ukiukwaji wa haki za binadamu


BARAZA Kuu la Chama cha Wananchi (CUF) limemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani kuwajibika kutokana na mauaji yaliyotokea wilayani Tarime lakini pia kufanyika kwa uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo.

Hatua hiyo ilifikiwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mapendekezo mbalimbali yaliyoazimiwa na kikao cha baraza hilo.

Alisema kuwa baraza hilo linalaani vitendo vya ukiukaji na uvunjaji wa haki za binadamu hususan mauaji ya raia yanayofanywa na Jeshi la Polisi ambayo yamekuwa yakiripotiwa kila mara.

"Inatuumiza sana kwa kuwa inaonekana jambo hili ni la kawaida kwa sababu watendaji wake hawachukuliwi hatua yoyote," alisema.

Prof. Lipumba alisema kuwa baraza hilo pia linamtaka Rais Jakaya Kikwete kutambua kuwa jukumu la kuleta maendeleo ya Watanzania ni la watu wote hivyo serikali yake isisite kutumia sera mbadala za CUF kwa maendeleo ya taifa.

Alisema serikali kupitia wizara ya Fedha na Uchumi na Wizara ya Nishati na Madini inatakiwa kuchukua hatua za kuhakikisha nchi na wananchi wake wananufaika na rasilimali za madini zilizopo hapa nchini hususani madini ya dhahabu ambayo bei yake katika soko la dunia imepanda.

"Dhahabu inayouzwa nje ni dola bilioni 1.5 kwa mwaka sawa na  asilimia 40  ya bidhaa za Tanzania zinazouzwa nje ya nchi," alisema.

Alisisitiza kuwa baraza hilo linataka kuona utajiri wa nchi unawanufaisha wananchi na kuisaidia nchi kujikomboa kutoka katika dimbwi la umasikini na kuacha kutegemea misaada kutoka nje ambayo imeifanya nchi kuwa tegemezi kwa miaka mingi.

Aliongeza kuwa baraza hilo linamtaka Waziri wa Nishati na Madini Bw.William Ngeleja kujiuzulu kwa kuwa ameshindwa kutumia vyanzo vya umeme vilivyopo nchini ili kukabiliana na tatizo sugu la nishati linaloikumba nchi yetu kwa sasa.

Alisema nchi imejaliwa vyanzo vingi ya umeme na maeneo mengi ya maporomoko ya maji, makaa ya mawe, madini na hata umeme wa jua ambao hauna gharama kubwa ya kufua.

"Ni miaka 50 tangu tupate uhuru hatuna sababu yoyote  ya kutokuwa na umeme wa uhakika, ni ufisadi tu ambao umekithiri katika serikali yetu," alisema.

Alisisitiza kuwa serikali ni lazima itambue kuwa hali ya kutokuwa na umeme wa uhakika imezorotesha uzalishaji viwanda,biashara,huduma katika hospitali na shule hivyo kusababisha uchumi wa nchi kuzorota.

Aliitaka serikali kuzingatia mapendekezo na hoja zinazotolewa na kamati ya Nishati na Madini ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania zinazolenga kupata ufumbuzi wa matatizo ya umeme.

Pia alisema baraza hilo linaitaka serikali kuwa makini katika suala zima la utunzaji na uhifadhi wa silaha nzito za kivita zenye madhara makubwa na kutaka zihifadhiwe mbali na makazi ya watu ili matukio ya milipuko ya mabomu ambayo yameshatokea mara mbili yasijirudie tena.  

Thursday, May 26, 2011

Lissu na wenzake marufuku Nyamongo

Maiti wazikwa, wananchi wataka kurejesha majeneza polisi



 
















MBUNGE wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria, na wenzake saba ambao juzi walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime na kusomewa mashtaka matatu ya kuingia eneo la hospitali bila kibali, kufanya mkutano na kuzuia watu kufanya kazi, wamepata dhamana lakini wamezuiwa kutembelea maeneo ya Nyamongo hadi kesi inayowakabili itakapokwisha.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya hiyo, Yusto Roboroga alitoa uamuzi huo akisema ni kwa mujibu wa kifungu cha Sheria Namba 148 cha Makosa ya Jinai, kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2002, ambacho kinatoa haki kwa watuhumiwa kupata dhamana. Alitoa uamuzi huo baada ya kupitia pingamizi lililowekwa na upande wa mashtaka kutaka wasipewe dhamana. Hata hivyo, alisema: “Washtakiwa wanazuiwa kutembelea maeneo ya Nyamongo mpaka kesi hiyo itakapokuwa imekwisha."

Hakimu huyo alisema kwa kuwa washtakiwa hao ni viongozi wakubwa wa chama walizuiwa ili kupunguza shinikizo la wanachama kutokana na tukio lililojitokeza, lakini kwa kuwa mazishi yameshafanyika, alisema wanaweza kudhaminiwa kama watakidhi masharti.

Hakimu Ruboroga alitaja masharti  ya dhamana hiyo kuwa ni kusaini mkataba wa dhamana wa Sh5 milioni kwa wadhamini wawili wanaoaminika.

Kwa wasio wakazi wa Tarime, alisema watatakiwa kupeleka mahakamani hati za mali isiyohamishika. Washtakiwa wote walikidhi masharti na kuachiwa kwa dhamana hadi Juni 26, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Juzi, Lissu na wenzake, Waitara Mwita Mwikwabe, Stanslaus Nyembea, Anderson Deogratias Chacha, Andrew Andalu Nyandu, Mwita Marwa Maswi, Bashiri Abdalllah Selemani na Ibrahimu Juma Kimu walifikishwa mbele ya mahakama hiyo na kusomewa mashtaka hayo matatu na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Casmir Kiria ambaye alisema, waliyatenda Mei 23, majira ya saa nne usiku. Wote walikana mashtaka hayo.

Wakati huo huo maiti wote waliokuwa wametelekezwa barabarani wamezikwa na ndugu zao huku baadhi ya familia zikikataa kuwazika kwa majeneza ya polisi na kutumia yale yaliyokuwa yameandaliwa huku wengine wakipanga kuyarudisha kwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Tarime, Constantine Massawe.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kewanja, Om’tima Tanzania alisema kuwa mmoja wa marehemu hao, Chacha Ngoka alizikwa na jamii. Hata hivyo, alisema polisi waliweka mwili wake ndani ya jeneza bila kuweka sanda hali ambayo iliwalazimu kumweka ndani ya jeneza lao na kumvika sanda. Hilo lilifanyika pia katika eneo la Nyakunguru alikozikwa marehemu Emmanuel Magige.

Katika Kijiji cha Bonchugu, Serengeti, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Mwikwabe Makena alidai kwamba walilazimika kuzika mwili wa marehemu Chawali Bhoke uliotelekezwa na polisi.


Alidai kwamba kabla ya kuutelekeza, walifyatua mabomu ya machozi na risasi hewani baada ya wananchi waliokuwa wamebeba pinde, mishale, mikuki na mapanga kujaribu kuzuia gari la polisi. Alisema walilazimika kuzika bila kuwapo kwa ndugu wa marehemu waliokuwa wameachwa Tarime.Hata hivyo, Kamanda Massawe na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Robert Boaz hakuwa tayari kuzungumzia madai hayo.

Wednesday, May 25, 2011

Polisi 'wapora' maiti mochwari

*Tundu Lisu akamatwa, afikishwa kortini Tarime

JESHI la Polisi limewakamata na kuwafikisha mahakamani Mbunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na maofisa wengine wa chama hicho baada ya kudaiwa kufanya mkusanyiko usio halali na kuzuia watu kuzika ndugu zao.

Sambamba na hatua hiyo jeshi hilo limedaiwa kuingia mochwari ya Hospitali ya Wilaya ya Tarime na kuchukua kwa nguvu maiti nne za watu waliouawa na polisi hivi karibuni na kwenda kuzitelekeza maeneo mbalimbali ili kuzuia mkusanyiko wa kuaga maiti hizo kwa pamoja, kwa kile wanachoeleza ni kuzuia uvunjifu wa amani.

Bw. Lisu na wenzake wanadaiwa kukutwa katika Hosptali ya Wilaya ya mjini hapo wakilinda miili hiyo baada ya kusikia tetesi kuwa polisi walikuwa na mpango wa kuichukua na kuisafirisha kusikojulikana.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya mahakama, Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Bw. Casmil Kria alisema watuhumiwa wanakabiliwa na mashtaka matatu, yaliyosomwa mbele ya Hakimu wa Wilaya, Bw. Yusto Ruboroga.

Mashtaka hayo ni kuingia eneo la hospitali bila kibali, kufanya mkusanyiko usio halali na kuzuia watu kuchukua miili ya ndugu zao.

Watuhumiwa hao ambao wanadaiwa kukutwa eneo hilo saa 4:00 usiku baada ya kusomewa mashtaka na kuyakana, walirudishwa rumande kwa 'sababu za kiusalama', na kesho watafikishwa tena mahakamani kwa ajili ya kupewa dhamana, endapo miili ya waliouawa itakuwa imeshazikwa.

Walioshtakiwa ni Mbunge wa Singida Magharibi, Bw. Tundu Lissu (43), Bw. Mwita Mwikwabe (36), Bw. Stancelaus Nyembea (33), Anderson Deogratias (35), Bw. Andrew Andaru (63), Bw. Mwita Marwa (48) Bw. Bashiri Abdallah Seremani (35) pamoja na Ibrahimu Juma Kimi (27) ambaye ni dereva wa Bw. Lissu.

Wakati huo huo, waandishi wanne wa habari pamoja na Mbunge Viti Maalumu, Bi. Ester Matiko (CHADEMA) nao walishikiliwa na Jeshi la Polisi katika Kituo Kidogo cha Nyamwaga na baadaye kuachiwa huru baada ya mahojiano.

Wandishi hao ni Bi. Beldina Nyakeke wa The Citizen, Anna Mroso (Nipashe), Bw. Anthony Mayunga (Mwananchi) pamoja na Mabere Makubi wa Chanel Ten ambao walikuwa kwenye msafara wa Bi. Matiko.

Waandishi wengine wa habari waliofika katika mahakama ya wilaya kufuatilia tukio hilo walizuiliwa kuingia na kutishiwa kupigwa
risasi na ofisa mmoja wa polisi.

Ofisa huyo ambaye hakufahamika jina aliwatimua waandishi hao, huku akiomba bunduki kutoka kwa askari mwenzake na kuiandaa mithili ya kupambana na adui.

“Toka! Toka! Naombeni bunduki yangu hapa naona nyinyi hamjui kufanya kazi, hatukuja kufanya mchezo hapa waondoe na wale watu upesi mahali hapa wasongee mbali huko hatutaki mtu hapa!” alisema.

Askari hao wakiwa wameziba njia huku ofisa huyo akiendelea kuelekeza bunduki yake kwa raia waliokuwa eneo hilo.

An exit strategy for Moammar Gadhafi

South Africa's President Jacob Zuma is reportedly to travel to Libya to discuss an exit strategy for Moammar Gadhafi

Tuesday, May 24, 2011

Sumaye aongoza harambee kuchangia ujenzi wa kituo cha TEKNOHAMA cha watoto yatima

  • Kaimu mkuu wa mkoa, Baba Askofu Mdegela, Mstahiki Meya, watu maarufu wahudhuria
  • Computers 4 africa wachangia kompyuta 105
  • Bonny Mwaitege, Christina Shushu, Bahati Bukuku, Jeniffer Mgeni, na Solomoni Mukubwa wawasha moto

Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Frederick Tluway Sumaye, juzi aliongoza harambee kabambe ya kuchangia ujenzi wa Kituo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano cha watoto yatima. Harambee hiyo ilifanyika katika uwanja wa Samora, manispaa ya Iringa mjini.

Katika uzinduzi huo, Mh. Sumaye alisisitiza Upendo, Huruma, Mshikamano na Kuwapa elimu bora watoto hasa yatima. Aidha Mh. Sumaye alisema kuwa wazo la kuwajengea watoto yatima kituo cha TEKNOHAMA limekuja muda muhafaka ambapo dunia imekuwa kama kijiji.

Mh. Sumaye aliongoza mnada wa vitu mbali mbali wakati wa harambee hiyo ambapo yeye mwenyewe alichangia kiasi cha shilingi milioni moja. Wengine waliochangia ni pamoja na Kaimu mkuu wa mkoa wa Iringa ambaye pia ni na mkuu wa wilaya ya Iringa kapteni mstaafu Aseri Msangi, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Iringa, Dk. Owdenburg Mdegela, MSTAHIKI meya wa Manispaa ya Iringa Amani Mwamwindi, watu maarufu kama Solanus Nichombe, na Dorah Sanga.

Taasisi ya Computers 4 Africa ya Uingereza, kupitia wawakilishi wake wa Tanzania wamechangia jumla ya kompyuta 105, na kuahidi kutoa mchango zaidi kupitia wataalamu wake.

Harambee hiyo iliwashwa moto na magwiji wa nyimbo za injili afrika ya mashariki wakiwamo Bonny Mwaitege, Christina Shushu, Bahati Bukuku, Jennifer Mgeni na Solomoni Mkubwa, ambao kwa pamoja walifanya umati uliohudhuria kusimama na kushangilia kwa nguvu katika harambee hiyo. Baba Askofu Dk. Owdenberg Mdegela alionyesha kipaji chake pale alipoweza kuimba kwa umahiri pamoja na waimbaji hao.

Awali mratibu wa kituo  cha TEKNOHAMA Bw. Majaliwa Mbonela alisema kuwa, taasisi ya "Children Care Development Organization" inashughulika na kazi ya kulea watoto wanaoishi katika mazingira magumu mkoani Iringa kupitia mafunzo ya Teknolojia ya Computer, ufundi wa kushona na kubuni mitindo mbalimbali ya nguo za jinsia zote za kike na kiume, lugha za kigeni (Kichina, Kifaransa, Kijerumani na Kiarabu), na kuimarisha uwezo wa jamii katika kukuza elimu ya afya na kupambana na vitendo vya ukiukwaji haki za watoto na akina mama.





















Friday, May 20, 2011

SHEIKH YAHAYA HUSEIN AFARIKI DUNIA


Mnajimu wa Afrika Mashariki Sheikh Yahaya Hussein amefariki dunia leo nyumbani kwake mwembe chai jijini Dar es salaam, saa 4 asubuhi

Sheikh Yahaya alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo.

OCD mbaroni kwa kumpiga risasi makalioni mhadhiri wa SUA



MKUU wa Polisi wa Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma, Onesmo Lianga ameshikiliwa na polisi mkoani Morogoro kwa muda na baadaye kuachiwa kwa
tuhuma za kumpiga risasi sehemu ya makalio mwalimu wa kikundi cha sanaa cha Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Dadie Kitururu (42).

Ndugu wa karibu na marafiki wa Bw. Kitururu alipigwa risasi Mei 11, mwaka huu majira ya jioni katika eneo la Forest wakati akiwa njiani kurejea nyumbani kwake, huku wakishangaa kwa nini polisi amtwange mtuhumiwa risasi badala ya kumtia mbaroni.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Bi. Adolphina Chialo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, akisema kuwa siku ya tukio majira ya jioni Bw. Kitururu akiendesha gari alimgonga mpanda baiskeli Salumu Chiga (58), mfanyakazi wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro mkazi wa Kichangani karibu na ofisi za Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Kilakala na kukimbia.

Alisema kuwa OCD huyo ambaye alikuwa nyuma ya Bw. Kitururu aliyekuwa akiendesha gari lenye namba za usajili T 320 ANQ Suzuki Samurai, naye akiwa na gari lenye namba T 630 BFZ aina ya Rav 4 alimkimbiza Kitururu hadi eneo hilo la Forest.

Kwa mujibu wa RPC, baada ya OCD kuona Kitururu anakimbia zaidi, alifyatua risasi kwa bastola yenye namba PA06897 aina ya Chinese na kupasua taili la mbele na risasi ikapenya hadi kumfikia Kitururu kwenye makalio.

Kamanda Chialo alisema, baada ya tukio hilo OCD alimkamata mtuhumiwa huyo na kumfikisha katika Kituo Kikuu cha Polisi mkoani Morogoro na kuwekwa rumande na baadaye polisi waligundua kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa na majeraha baada ya kuona akivuja damu, ndipo alipopelekwa hospitali kwa uchunguzi zaidi.

"Baada ya kufikishwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro mtuhumiwa huyo alilazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi kutokana na hali yake kuwa mbaya na aligundulika kuwa na kipande cha risasi katika makalio na hivyo kupatiwa matibabu," alisema.

Baada ya kugundua hivyo, ndipo polisi walipoamua kumshikilia OCD huyo kwa kwa mahojiano juu ya tukio hilo na kubaini kuwa alipiga tairi risasi likapenya na kumfikia Kitururu.

Dominique Strauss-Kahn bailed for $1m and ordered to face sex trial

Dominique Strauss-Kahn was bailed for $1 million on Thursday night, after agreeing to live under house arrest with his wife at a New York flat, where he will be watched around the clock by an armed guard.

 
Anna Sinclair, wife of Dominique Strauss-Kahn, leaves Manhattan Criminal Court with daughter Camille
Mr Strauss-Kahn secured his release from Rikers Island prison as it was announced a grand jury had voted to have him prosecuted for the alleged sexual attack of a 32-year-old maid in his hotel room.

In a hearing at New York supreme court, Judge Michael Obus said he would allow the 62-year-old former head of the IMF out of jail despite the fact there was a "serious risk" he would try to flee.

He warned Mr Strauss-Kahn, who was arrested at JFK airport on a flight about to take off for Paris, that the consequences would be serious "if there is the slightest problem with your compliance".

Watched by his wife Anne Sinclair, 62, who held the hand of his daughter Camille, 26, Mr Strauss-Kahn showed little sign of emotion as the judge delivered his verdict.

He must move into an apartment in Manhattan rented by his wife, and "will be monitored 24 hours, seven days a week, electronically and by at least one armed guard", the judge said.

Obama, Netanyahu face turning point

As Prime Minister Benjamin Netanyahu of Israel heads to the White House on Friday for the seventh meeting since President Obama took office, the two men are facing a turning point in a relationship that has never been warm.
By all accounts, they do not trust each other. President Obama has told aides and allies that he does not believe that Mr. Netanyahu will ever be willing to make the kind of big concessions that will lead to a peace deal.


For his part, Mr. Netanyahu has complained that Mr. Obama has pushed Israel too far — a point driven home during a furious phone call with Secretary of State Hillary Rodham Clinton on Thursday morning, just hours before Mr. Obama’s speech, during which the prime minister reacted angrily to the president’s plan to endorse Israel’s pre-1967 borders for a future Palestinian state.

Mr. Obama did not back down. But the last-minute furor highlights the discord as they head into what one Israeli official described as a “train wreck” coming their way: a United Nations General Assembly vote on Palestinian statehood in September.

Mr. Netanyahu, his close associates say, desperately wants Mr. Obama to use the diplomatic muscle of the United States to protect Israel from the vote, not only by vetoing it in the Security Council, but also by leaning hard on America’s European allies to get them to reject it as well.


Mr. Obama has indicated that he will certainly do the first. But it remains unclear how far Mr. Obama can go to persuade Britain, France and other American allies to join the United States in rejecting the move, particularly as long as Mr. Netanyahu continues to resist endorsing the pre-1967 lines.

From the day they first met, at the King David Hotel on July 23, 2008, when Mr. Obama, then the presumptive Democratic nominee for president, visited Israel, the two men have struck, at most, an intellectual bond. Mr. Netanyahu, as the leader of Israel’s conservative Likud Party, was far more comfortable with the Republican Party in the United States than with Mr. Obama, the son of a Muslim man from Kenya whose introduction to the Arab-Israeli conflict was initially framed by discussions with pro-Palestinian academics.

“Their relationship is correct at best,” said Judith Kipper, director of Middle East programs at the Institute of World Affairs. Mr. Netanyahu “likes the status quo, and he particularly identifies with conservative Republicans.”

Abraham H. Foxman, national director of the Anti-Defamation League and a friend of Mr. Netanyahu’s, recalled that after the first meeting, Mr. Netanyahu walked out of the hotel and told him that he had been impressed with Mr. Obama’s intellect, and that the American presidency “was his to lose.”

Thursday, May 19, 2011

22 dead in plane crash in Argentine Patagonia

A Sol Air Lines plane carrying 22 people crashed and exploded Wednesday in Argentina's southern Patagonia region, killing all on board.


Sol Air Lines said its Flight 5248 carrying three crew members and 19 passengers, including a baby, communicated an emergency while flying from Neuquen near the Andes to Comodoro Rivadavia along the coast of Patagonia. The company confirmed that the wreckage was found about 25 kilometers (15 miles) southwest of the town of Los Menucos, and that local firefighers and police found no one alive.

"Unfortunately there are no survivors. We see burnt remains, everything burned," Ismael Ali, who directs the hospital in the nearest town of Los Menucos, told the Todo Noticias channel.
Sol spokesman Horacio Darre in Buenos Aires said the plane took off normally and that it's impossible to know the cause, which will be determined by accident investigators.

"It's important to clarify that right now there is no information about the cause of the crash, which will be clarified by the relevant authorities," an airline statement stressed.

Sol said it received an emergency communication from the plane at 8:50 p.m. local time, nearly halfway into the flight from Neuquen near the Andes to Comodoro Rivadavia along the coast of Rio Negro province.

The plane crashed and exploded on the rural property of a man who drove into the town of about 4,000 people to alert authorities. Los Menucos Mayor Mabel Yahuar said they would make the town's gymnasium available to support investigators and family members.

IMF Chief Resigns After Sex Attack Charges

The IMF chief charged with a sex attack on a hotel maid has resigned from his post ahead of a new bail hearing in New York.

Dominique Strauss-Kahn maintained his innocence in a formal letter to the organisation and said he was quitting with "infinite sadness".
"I think at this time first of my wife - whom I love more than anything - of my children, of my family, of my friends," he said.
"I think also of my colleagues at the fund - together we have accomplished such great things over the last three years and more.
"To all, I want to say that I deny with the greatest possible firmness all of the allegations that have been made against me."
The 62-year-old French citizen - who had been a strong contender for the country's presidency in 2012 - added he would devote "all my strength, all my time, and all my energy" to proving his innocence.
Strauss-Kahn handcuffed

Click here to see pictures related to Dominique Strauss-Kahn's arrest
There had been widespread speculation over the future of Strauss-Kahn after he was arrested following the alleged attack at the Sofitel hotel in New York at the weekend.
He faced growing pressure to quit as further claims about his private life emerged – including allegations by writer Tristane Banon that he attempted to rape her in 2002.
He is due at a fresh hearing today, where his lawyers will propose $1m bail – which was earlier refused by a judge – and electronic tagging. He has also waived his extradition rights.
Strauss-Kahn is reportedly on suicide watch at New York's Rikers Island prison, although he is not believed to have attempted to harm himself.
His lawyer, William W Taylor, said on Wednesday that his client's mood was "serious but good".
A view of the Rikers Island prison complex where Dominique Strauss-Kahn, head of the International Monetary Fund (IMF), is being held while awaiting another bail hearing on May 17, 2011 in New York City.
Strauss-Kahn is said to be on suicide watch at Rikers Island
"He is a strong man and he's committed to seeing this through," he added.
There had been fears that without a suitable figure at the helm of the IMF, the organisation - designed to maintain stability in the world economy - could be thrown into disarray just as it attempts to tackle the eurozone debt crisis.
Among the possible candidates touted to replace Strauss-Khan is former prime minister Gordon Brown.
The IMF said it would discuss in the near future the process of selecting a new managing director. For now John Lipsky remains the acting chief.
Economics editor at The Independent Sean O'Grady told Sky News he did not think Strauss-Kahn had much choice over the resignation.
"The Americans call a lot of the shots at the IMF and once he lost their support I think it was only a matter of time and so it has been proved," he said.
Strauss-Kahn faces charges of committing a criminal sexual act, attempted rape, sexual abuse, unlawful imprisonment and forcible touching, all of which he denies.
The alleged victim, a 32-year-old widow from West Africa, testified on Wednesday before a grand jury.
It will decide in secret whether there is enough evidence to formally press charges.
A mugshot of Strauss-Kahn taken more than 24 hours after he was pulled from a plane at New York's JFK airport and detained on Saturday, showed him exhausted, his eyes downcast and half-closed.

Wednesday, May 18, 2011

Al-Qaida 'appoints temporary leader'


Al Jazeera television has reported that Al-Qaida has a new leader. The terrorist group is understood to have appointed Egyptian militant Saif al-Adel as temporary leader. Mustafa al-Yemeni, whose nationality is not known, will direct operations, according to the Arabic news service.

Former leader Osama bin Laden was shot dead by US troops at a compound in Pakistan earlier this month. US prosecutors say interim leader al-Adel helped plan bomb attacks on American embassies in Nairobi and Dar es Salaam in 1998.

Polisi waua watano


POLISI wameua watu watano na kujeruhi wengine kadhaa katika mgodi wa dhahabu wa North Mara unaomilikiwa na kampuni ya African Barrick Gold, Tarime mkoani Mara.

Habari zilizopatikana kutoka eneo la tukio na kuthibitishwa na Jeshi la Polisi zilisema tukio hilo lilitokea jana alfajiri katika eneo la Nyabirama.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi Tarime/Rorya, Constantine Massawe, alisema askari walilazimika kutumia risasi za moto baada ya kutumia mabomu ya machozi bila mafanikio kutawanya kundi la watu waliojaribu kuingia kwa jinai na kupora mawe yenye dhahabu mgodini.

“Askari walilazimika kutumia risasi kukabiliana na watu wanaokadiriwa kuwa kati ya 800 na 1,000 waliokuwa wamevamia mgodi huo ili kuokota mawe yenye dhahabu,” alisema.

Kwa mujibu wa Kamanda Massawe, watu watatu walikufa katika eneo la tukio na wengine wawili walifia katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime. Majina yao hayakufahamika mara moja.

Hata hivyo, Kamanda huyo alitaja baadhi ya majina ya majeruhi waliolazwa hospitalini hapo kuwa ni Francis Emmanuel (20) mkazi wa kijiji cha Kewanja, Chacha Mwasi (23) mkazi wa kijiji cha Bisarwi wilayani Tarime na Mwikwabe Marwa (30) mkazi wa Mugumu wilayani Serengeti.

Alidai kwamba polisi wawili waliofika eneo la tukio walijeruhiwa kwa mawe yaliyokuwa yakirushwa kwa kombeo.

Akizungumzia tukio hilo kwa simu kutoka Dar es Salaam, Mbunge wa Tarime, Nyambari Nyangwine (CCM), alilaani mauaji hayo na kuahidi kuchukua hatua.

Alilaani matumizi ya nguvu kubwa yaliyofanywa na polisi kukabiliana na wananchi waliojaribu kuvamia mgodi.
“Ninalaani sana kitendo cha askari kutumia nguvu kubwa ya kuua na kujeruhi wananchi kwa tuhuma za kuvamia mgodi. Nitachukua hatua kali dhidi ya wote waliohusika katika tukio hilo la kusikitisha,” alisema Nyangwine bila kutaja aina hiyo ya nguvu alizoahidi.

Kamanda Massawe alisema ofisi yake inakusudia kuitisha mkutano maalumu wa viongozi wa mgodi wa dhahabu wa North Mara na wakazi wa vijiji vilivyo jirani kutafuta ufumbuzi thabiti wa matukio ya uvamizi na mauaji ambayo yamekuwa yakitokea mgodi hapo.

Alitoa wito kwa wananchi kuepuka vitendo vya uvamizi na uporaji mali katika mgodi huo kwa vile unamilikiwa kihalali na kampuni ya African Barrick Gold.

Wimbi la matukio ya uvamizi, uporaji mawe yenye dhahabu na mauaji ya watu katika mgodi wa dhahabu wa North Mara limeendelea kuwepo, huku baadhi ya askari, walinzi na wafanyakazi wa mgodi huo wakituhumiwa kupokea rushwa ya fedha na kuruhusu watu kuingia kuokota mawe yenye dhahabu.

Ajali ya basi yaua 16 Geita



ABIRIA 16 wamefariki dunia na wengine 120 wamenusurika baada ya mabasi mawili kugongana mkoani Shinyanga.Mabasi hayo yaligongana jana asubuhi katika Kijiji cha Kibingo, Kata ya Nyamigota wilayani Geita, moja likitokea Musoma kwenda Bukoba na jingine Mwanza likielekea Biharamulo.

Kati ya abiria hao 120 walionusurika, zaidi ya 60 walipata majeraha. Taarifa zilizopatikana kutoka wilayani Geita na kuthibitishwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Philemon Shelutete na Mganga Mkuu wa Wilaya, Dk Abdalah Dihenga zimeeleza kuwa ajali hiyo ilitokea saa 3:20 asubuhi.

Akizungumza kwa simu jana, Shelutete aliyataja mabasi hayo kuwa ni la Kampuni ya Mabasi ya Bunda lililokuwa likitokea Mwanza kuelekea Bukoba na basi la Sheratoni ambalo lilikuwa likitokea Biharamulo kwenda Bukombe.Shelutete alidai kuwa ajali hiyo ilitokea kwa uzembe baada ya dereva wa basi la Sheratoni kulazimisha kulipita roli aina ya Fuso mali ya kampuni ya vinywaji baridi Nyanza Bottling Ltd ya jijini Mwanza, ndipo likagongana na basi la kampuni ya Bunda.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Nonosius Komba alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kwamba wakati huo alikuwa akielekea eneo la tukio. Dk Dihenga alisema awali walipokea maiti za watu wanane na kwamba hadi kufikia saa 7:00 mchana walikuwa na maiti 16.

"Mpaka sasa tuna idadi kubwa ya majeruhi wa ajali hiyo, wanaendelea kutibiwa na madaktari wetu, lakini kati yao majeruhi sita hali zao ni mbaya hivyo tumelazimika kuwakimbiza katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando kwa matibabu zaidi na wengine tumewahamishia Hospitali Teule ya Sengerema kwa matibabu," alisema Dk Dihenga.

Tuesday, May 17, 2011

Strauss-Kahn arrest: IMF head detained at Rikers Island

IMF chief Dominique Strauss-Kahn has been remanded in custody at New York's notorious Rikers Island jail on charges of sexual assault.
The judge said Mr Strauss-Kahn, 62, was a flight risk. He was arrested on Saturday after boarding a plane and accused of trying to rape a hotel maid.
He faces seven charges and could be sentenced to up to 25 years in prison.
Mr Strauss-Kahn, who had been seen as a favourite in France's 2012 presidential elections, denies the charges.
His lawyer expressed disappointment at bail being denied, but said his client would be exonerated.
"This battle has just begun," defence lawyer Benjamin Brafman told the court.
Mr Strauss-Kahn had been due to attend an EU finance ministers' meeting in Brussels to discuss financial bail-outs.
The IMF has played a central role in organising rescue packages for the troubled economies of Portugal and Greece.
The BBC's Chris Morris in Brussels says the IMF chief has gained the trust of countries in Europe which are giving financial assistance, and those which are receiving it.
The European Union says the scandal should not affect bail-outs for eurozone countries.

Monday, May 16, 2011

"Mwanafunzi" anusurika kifo Chuo Kikuu cha Tumaini


Kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja alinusurika kifo baada ya kushambuliwa vikali na wananchi wenye hasira kali Katika eneo la Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa. Kijana huyo alijifanya Mwanafunzi na kuingia katika darasa mojawapo chuoni hapo na kuiba simu ya mkononi. Arobaini ya kijana huyo ilifika pale ambapo alijaribu kukimbia na kuanguka sehemu yenye mawe na matofali ambayo baadae yangesababisha kifo chake. Baada ya kipigo kibaka huyo alirudisha simu ambayo alikuwa ameiba.
Hata hivyo Polisi waliwahi kufika katika eneo hilo na kuokoa maisha ya kijana huyo aliyekuwa amejifanya mwanafunzi.
Awali ilisemwa kuwa vibaka wamekuwa wakifika eneo la chuo na kuiba mali za aina mbali mbali zikiwemo kompyuta, Projector, na vifaa vingine mali za wanachuo na chuo kikuu cha Tumaini.