Wednesday, September 7, 2011

Msafara wa Libya wavuka mpaka kuingia Niger

Vikosi vinavyompinga Gaddafi 

Msafara wa magari wenye ulinzi na silaha kutoka Libya umevuka mpaka kuingia nchini Niger, ripoti zinasema.
Msafara huo unaaminika ni wa wapiganaji wa Tuareg waliopewa mafunzo na Kanali Muammar Gaddafi aliyekimbia nchi kupigania utawala wake ukielekea katika mji wa Agadez.

Haijafahamika wazi iwapo kuna mwanafamilia yeyote wa Kanali Gaddafi katika msafara huo. Msemaji wake alisema Gaddafi mwenyewe bado yuko Libya.

Kanali Gaddafi ameapa atapigana mpaka kufa, ingawa amepoteza sehemu kubwa ya udhibiti wake nchini Libya.

Nato, ambayo imekuwa ikiendesha harakati za kijeshi za anga kuunga mkono Maamuzi ya Umoja wa Mataifa kuwalinda ria wa Libya, imekataa kusema chochote katika ripoti yake.
'katika ari yahali ya juu'

Msafara huo wenye silaha umevuka mpaka na kuingia Niger na kufika mji wa Agadez Jumatatu, taarifa za kijeshi kutoka Ufaransa na Niger zimelifikia Shirika la Habari la Reuters.
Wamesema msafara huo una magari kati ya 200 na 250 na unasindikizwa na jeshi la Niger.
Wasemaji kutoka Agadez wameiambia BBC kuwa kati ya magari hayo 200, 60 ni ya Libya na yaliyosalia ni kutoka Niger.

Baadaye afisa mmoja kutoka Baraz la Mpito la Taifa Libya (NTC) aliliambia Shirka la Habari la Reuters kuwa msafara huo umebeba dhahabu na fedha na umevuka kuingia Niger kutoka katika mji unaoshikiliwa na Gaddafi wa Jufra.
"Usiku wa Jumatatu, magar 10 yaliyokuwa yamebeba dhahabu, fedha za Euro na dola na kuvuka mpaka kutoka Jufra na kuingia Niger wakisaidiwa na wapiganaji wa Tuaregs kutoka kabila moja Niger," Fathi Baja alisema.
Madai haya hayajathibitishwa na vyombo huru.
Msafara wa waasi

Mwandishi wa BBC Kevin Connolly, aliyeko mjini Tripoli, anasema kuna tetesi kuwa msafara huo unaweza kuwa umebeba washirika wa karibu wa Kanali Gaddafi huku njia ya jangwani inaonekana kuwa ni pekee kuweza kukimbia vikosi vya waasi wanaounda utwawala mpito nchini Libya.

Nchi ya Burkina Faso iliyoko Afrika Magharibi, haina bandari, inachangia mpaka na Niger, imekubali kumpa hifadhi Kanali Gaddafi.
Waasi wengi wa zamani wa Tuareg kutoka Mali na Niger walipewa mafunzo nchini Libya kati ya miaka ya 1970 na 80.

Kanali Gaddafi alisaidia kufikiwa makubaliano ya amani mwaka 2000 kati ya serikali ya Niger na kundi la waasi wa Tuareg linaloongozwa na Rissa ag Boula, ambaye alikimbilia Libya.
Watu wengi walioshuhudia wanasema wamemuona Rissa ag Boula katika msafara huo, lakini amekanusha taarifa hizo akiiambia AFP: "Mimi niko Niamey [Mji mkuu wa Niger]."

Msemaji wa NTC mjini London, Guma el-Gamaty, ameiambia BBC kuwa Niger italipishwa faini iwapo itathibitika kuwa imemsaidia Kanali Gaddafi kutoroka.
"Niger ni jirani na Libya kutoka Kusini na haina budi kufikiria uhusiano wake na Libya siku za usoni," Bw Gamaty alisema. "Hili – iwapo litathibitishwa - litaathiri sana uhusiano kati ya Libya na Niger."
Mke wa Kanali Gaddafi na watoto wake wawili wa kiume na binti yake tayari wamekimbilia Algeria.
Mke wa Gaddafi, Safiya na watoto

Mwandishi wa BBC Jon Leyne, mjini Benghazi, yalipo makao makuu ya waasi, anasema kwa msafara mkubwa kama huo usingeweza kukatisha jangwa bila ya Nato kutokuuona.

Nato imekataa kusema chochote kuhusu masuala yake ya kijasusi, msemaji wake ameiambia BBC
Kanali Roland Lavoie amesema kazi kubwa ya muungano wa Nato ni kuwalinda raia sio kufuatlia ‘viongozi wa zamani wanaokimbia nchi, mamluki,makamanda wa jeshi na watu waliopoteza makazi yao ".

Wakati waasi wanaimarisha ngome yao nchini Libya, Nato imeendelea na harakati zake za kijeshi za anga na uangalizi kama ilivyopewa majukumu na UN ya kuwalinda raia wa Libya.
Mapema Jumatatu, msemaji wa Kanali Gaddafi Moussa Ibrahim alisema kiongozi wa Libya ‘yuko vizuri na mwenye ari kubwa’
‘Yuko mahali ambako hataweza kufikiwa na vikundi cha watu tu walioasi nab ado yuko’ Bw Ibrahim ameiambia televisheni ya ya Arrai.

Tuesday, September 6, 2011

Uhusiano wa Libya na Uingereza Kuchunguzwa

David Cameron
Waziri mkuu wa Uingereza David Cameron amesema uchunguzi utaanza dhidi ya tuhuma kwamba majajusi wa Uingereza walihusika na mateso dhidi ya wafungwa katika jela wakati kanali Muammar Gadafi alipokuwa madarakani.

Bwana Cameron amesema ni muhimu kwa uchunguzi huo kuangazia madai kwamba kulikuwa na uhusiano wa karibu kati ya maafisa wa upelelezi wa Uingereza na Libya hasa baada ya shambulizi la septemba kumi na moja.

Kulingana la stakabadhi zilizofichuliwa mjini Tripoti hivi majuzi, inadaiwa kuwa huduma za ujasusi nchini Uingereza huenda zilitumiwa kuwahamisha washukiwa wawili wa ugaidi hadi nchini Libya mnamo mwaka 2004.

Akizungumza katika Bunge, Bwana Cameron alisema madai hayo sasa yatachunguzwa pamoja na madai mengine kuwa Serikali ya Uingereza iliyopita iliruhusu uhusiano wake na Libywa kuwa karibu kupita kiasi. Lakini hata hivyo Waziri Mkuu alitahadharisha kuwa watu hawapaswi kuharakisha kulaumu huduma za kijasusio za Uingereza.

Akizungumza dakika chache tu baadaye katika Bunge la Commons, Waziri wa Mashauri ya Kigeni katika Serikali iliyopita ya Labour, Jack Straw, alikariri madai ambayo yamerudiwa mara kadhaa sasa kuwa yeye na Mawaziri wengine walipinga mateso ya washukiwa walipokuwa mamlakani.

Monday, September 5, 2011

Ngeleja: Makali ya mgawo kupungua Desemba

Na Stella Aron

SERIKALI imewaomba wananchi kuwa wavumilivu kutokana na mgawo wa umeme unaoendelea maeneo mbalimbali nchini na kuahidi ifikapo Desemba mwaka huu, tatizo hilo
litakuwa limepungua kwa kiasi kikubwa.

Waziri wa Nishati na Madini, Bw. William Ngeleja, aliyasema hayo Dar es Salaam jana baada ya kutembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Symbion, Aggreko na Jacobsen iliyopo Ubungo.

Alisema Serikali inaendelea na jitihada za kupunguza mgawo kwa kuhakikisha inafanya kazi usiku na mchana.

“Tunaelewa kutokana mgawo huu, uchumi wa nchi umeyumba, watu wanapoteza ajira hivyo tunalazimika kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha mgawo huu unakwisha kabisa na ifikapo Desemba utakuwa umepungua,” alisema Bw. Ngeleja.

Aliwaomba wananchi kuwa wavumilivu na kumtaka Mkurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Bw. William Mhado, kutoa taarifa yanapotokea mabadiliko.

“Kama kuna mabadiliko ya ratiba ya mgawo ni vyema mtoe taarifa kwa umma badala ya kukaa kimya, hili ni tatizo la wote sio nyinyi peke yenu,” alisema Bw. Ngelena na kuongeza kuwa, ahadi ya kupunguza makali ya mgawo aliitoa bungeni kwa kuhakikisha ifikapo Desemba mwaka huu, mitambo yote mitatu itakuwa ikizalisha umeme.

Kwa upande wake, msimamizi wa mtambo wa Symbion Bw. Moses Mwandenga, alisema mtambo huo ambao unatumia gesi na mafuta una uwezo wa kuzalisha megawati 112 za umeme na kuna mitambo minne yenye uwezo wa kuzalisha megawati 20.

“Mtambo huu wa Symbion ambao unazalisha megawati 112 tunauwasha kesho (leo), hivi sasa unazalisha megawati 75,” alisema.

Msimamizi wa miradi hiyo kutoka TANESCO, Bw. Saimon Jirima, alisema mradi wa Jacobsen ambao unasimamiwa na Bw. Marrkko Rapo, ulitarajiwa kukamilika Juni 2012 lakini kutokana na dharura iliyopo, mradi huo unatarajiwa kukamilika kabla ya kipindi hicho.

Alisema mradi huo wenye mashine tatu zenye uwezo wa kuzalisha megawati 35 kila moja, tayari umeanza kufungwa vifaa ambapo mtambo wa Aggreko, una mashine 63 zilizokamika katika kituo cha Ubungo badala ya 50 zilizokuwa kwenye mkataba wa makubaliako.

“Vituo viko viwili, kimoja Ubungo na kingine Tegeta, kila kimoja kinatakiwa kuwa na mashine 50 lakini wameleta na mashine za  ziada ili kuziba pengo kama litatokea tatizo,” alisema Bw. Jirima.

Hata hivyo, Bw. Mhando alisema hadi sasa kuna megawati 570 za umeme ambazo zinazalishwa nchi nzima na bado jitihada zinaendelea kufanyika ili kupunguza kero iliyopo ambapo mitambo hiyo inatarajiwa kuanza kuzalisha umeme mwezi huu.

Wakati huo huo, Bw. Ngelaja aliwashukuru waumini 200 wa madhehebu mbalimbali ambao walikwenda kufanya maombi ya kuomba mvua katika Bwawa la Mtera, mkoani Iringa.

Alisema maombi hayo yaliongozwa na mchungaji Charles Gadi kutoka Kanisa la Goodnews For All ambapo Serikali imetambua mchango wao na kuwaomba waumini wengine kuendelea kufanya hivyo ili mvua zinyeshe.

Fresh worries over Loliondo

Retired pastor,Rev Ambilikile Mwasapila
By The Citizen Correspondent
Arusha. One year after retired pastor, the Rev Ambilikile Mwasapila started dispensing his purported miracle cure, the mugariga, in Samunge village of Loliondo in Arusha Region, medical experts are worried the concoction, which is still administered to patients, albeit at a lesser extent now, might be fatal.

In the recent past, Samunge village and Rev Mwasapila commonly referred to as Babu (Kiswahili for grandfather), have become a household name in Tanzania and beyond, thanks to enthusiastic media coverage, of both locally and internationally.

However, it has been reported that over 100 people died in the process of going to Samunge to get the “wonder” cup provided by the Rev Mwasapila, 76, of the Evangelical Lutheran Church in Tanzania (ELCT).

The tedious journey mostly involved critically ill patients determined to get a cupful of the herbal drink. Some of them were forced to trek long distances to Samunge as vehicles would at times be overfilled or were too expensive.

Media reports indicate that about four million people have already taken the cup, made from “mugariga”, a tree which was identified in Samunge village by the Maasai as “engamuriaki” or “olmuriaki” and Sonjo (Batemi) as “engamuriaga”. Plant Taxonomists identified the plant as Carissa spinarum (formerly Carissa edulis) which belongs to the family Apocynaceae.

Of serious concern to physicians in the country is the suspected large number of patients having abandoned conventional medication in favour of Babu’s mysterious cupful of concoction, believed to cure chronic diseases.
This is feared to happen as patients are likely to subscribe to the spiritual aspect of the medicine that requires the patient to have “faith”.

After some outcry by concerned observers, the Rev Mwasapila came out and urged his patients not to abandon their medicines prescribed by their doctors.

“If someone is on medication for a chronic diseases such as hypertension, diabetes, heart disease, cancer, epilepsy, Aids and decides to go for traditional treatment, it is important to discuss with their respective doctor before withdrawing from their conventional medicines suddenly as this may be fatal,” said Dr Kaushik Ramaiya, Honorary Secretary of Tanzania Diabetic Association.

Apparently, the Rev Mwasapila was neither the first nor would he be the last to claim a discovery of cure for chronic diseases.

What made him stand out and grab headlines in newspaper’s front pages and prime time news in the electronic media is how he discovered his “cure”.

Did it come after years of painstaking scientific research and product development? No, thank you; it was revelation from the heavens above, according to Rev Mwasapila who announced to the nation that God gave him the “mugariga” herb instructions through a dream in 1991: composition, dosage (the now-famous cup) and the amount to charge patients – a paltry Sh500!

The pastor prays to God before boiling the herbs in clean water, leaving it cool after which it is decanted and then given to patients who flock to his simple homestead from all over the country, neighbouring countries and beyond.

The controversy over Babu’s “miracle cure” is not only about the divine revelation aspect; it is also about the effectiveness of the cup that, according to him, could enable even barren women to conceive and bear children to fill the world.

Mashauriano yamevunjika, Libya

Wanajeshi wa serikali ya mpito nchini Libya, ambao wameuzingira mji wa Bani Walid ambao ni mji wa miwsho unaothibitiwa na wanajeshi watiifu kwa kanali Muammar Gadaffi, wamesema mazungumzo kati yao yamesambaratika.
Kanali Gadaffi
Kanali Gadaffi

Mmoja wa wapatanishi wakuu wa upinzani ameiambia BBC kuwa raia katika mji huo hawawezi kutembea kwa sababu wanahofia kupigwa risasi au kutekwa nyara na kutumiwa kama ngao.
Amesema wanajeshi watiifu kwa Gadaffi wamewataka wanajeshi hao wa upinzani kutoingia mjini humo huku wakiwa na silaha.

Amesema lililosalia sasa ni kwa makamanda wa jeshi la serikali hiyo ya mpito kuamua hatua watakayochukua.
Serikali ya mpito nchini Libya imesema ina uhakika kuwa mwanawe Kanali Gadaffi, Khamis Gadaffi ameuawa.
Wapiganaji wa waasi nchini Libya
Wapiganaji wa waasi nchini Libya

Baraza hilo la kitaifa la mpito NTC limesema Khamis aliuawa kwenye mapigano makali karibu na mji mkuu wa Tripoli na kuzikwa karibu na mji wa BANI Walid.
Muhammad, ambaye ni mwanawe mkurugenzi mkuu wa zamani wa idara ya ujasusi Abdullah Senussi, pia amaeirpotiwa kuuawa.
Hakuna habari zozote zimetolewa kuhusu kifo chake. Kifo cha Khamis kimeripotiwa mara mbili lakini baadaye akajitokeza tangu ghasia za kisiasa kuanza nchini Libya.

Mji wa Bani Walid, ulioko 150km Kusini mashariki mwa mji mkuu wa Tripoli, ni moja ya miji minne inayothibitiwa na wanajeshi watiifu kwa kanali Gadaffi. Miji mingine ni pamoja na mija ya Jufra, Sabha na Sirte

Mwenyekiti wa baraza hilo la NTC Mustafa Abdel Jalil amesema wanajeshi hao watiifu kwa kanali Ghadafi wanapewa msaada wa kibinadam kujisalimisha ili kuepusha umwagigaji zaidi wa damu nchini humo.

Sunday, September 4, 2011

Kisa na mkasa na Salim Kikeke

MITA KWA MAKAHABA

Makahaba nchini Ujerumani wanatakiwa kununua tiketi maalum kutoka katika mita maalum wakati wakifanya shughuli zao katika mitaa mbalimbali nchini humo.
Mita
Mita mpya za makahaba

Makahaba katika jiji la Bonn watakabiliwa na faini kali kutoka katika mamlaka za mji iwapo watakutwa wakifanya shughuli zao bila kulipia.Nchini Ujerumani, wanawake wanaouza miili yao hutakiwa kulipa kodi ya mapato. Kiwango cha kodi hiyo hutofautiana kulingana na mji na mji.

Mita hizi mpya nchini Ujerumani zinaruhusu makahaba kununua tiketi kwa dola tisa ambayo itadumu kwa usiku mmoja. Msemaji wa jiji la Bonn amesema mita hizi zitahakikisha kodi inakusanywa bila tatizo lolote.
Iwapo kahaba atakamatwa akifanya shughuli zake bila tiketi, atawekwa rumande, na kukabiliwa na faini, na hata uwezekano wa kupigwa marufuku. Takriban makahaba mia mbili wanafanya shughuli zao mjini Bonn.
Kutokana na malalamiko kutoka kwa wakazi wa mji huo, maeneo maalum yametengwa kwa ajili ya shughuli hizo, na jiji pia limejenga mabanda ya mbao yaitwayo "maeneo ya mlo" ili wateja wenye magari waweze kujificha na makahaba.

KULA KULIPA

Bwana mmoja nchini Canada aliingia hotelini kula, na alipotakiwa kulipa, alimwambua mhudumu amsubiri kidogo. Bwana huyo alitoka hotelini na kwenda katika kituo kimoja cha kuuzia mafuta, na kuiba fedha, na kurudi na kulipia chakula chake.
Lipa
Usisahau kulipa

Gazeti la Metro limesema bwana huyo Cory Henderson alikwenda kula katika hoteli ya Browns Kaskazini mwa Vancouver siku ya Ijumaa na kutakiwa kulipa dola thelathini na nane. Polisi wamesema wahudumu wa hoteli walipomtaka alipe fedha hizo, aliwajibu kuwa anatoka mara moja na atarejea baada ya muda mfupi.
Taarifa za polisi zimesema bwana huyo alikweda katika kituo cha mafuta na kumtishia muuzaji kwa kutumia screwdriver, na kisha kurejea hotelini na kulipa na fedha alizoiba. hata hivyo haijafahamika aliiba fedha kiasi gani.

Bwana Henderson sasa anashitakiwa kwa kosa la wizi, kujipatia chakula kwa njia za wizi, na kumiliki silaha hatari.

JESHI NA KITAMBI

Madaktari wa jeshi nchini Czech wamegundua kuwa nusu ya wanajeshi wa nchi hiyo wameota vitambi.
Kitambi
Jeshi na kiriba tumbo.. wapi na wapi..

Shirika la habari la Reuters limesema jeshi hilo lina wanajeshi wapatao elfu ishirini na mbili. Taarifa zinasema nusu ya wanajeshi hao wana uzito uliozidi na wengine takriban elfu tatu na mia tano wana viriba tumbo.
Jeshi hilo limeamua kuchukua hatua za haraka maraka, ambapo wanajeshi watatakiwa kuacha kula, yaani kufanya diet. Taarifa zinasema jeshi huenda pia likaagiza vidonge maalum vya kupunguza uzito. hata hivyo wizara ya ulinzi ya nchi hiyo imesema vidonge hivyo vitatumika kama suluhu ya miwsho kabisa, baada ya mpango wa kupunguza kula, na kufanya mazoezi kushindikana.
Czech ni mwanachama wa NATO na ina wanajeshi wapatao mia saba nchini Afghanistan.

BILA PESA INAWEZEKANA

Mwanamama mmoja nchini Ujerumani amefikisha miaka 15 sasa akiishia maisha yake bila kutumia fedha. Mama huyo mwenye umri wa miaka sitini na tisa aliacha kutumia fedha mwaka 1996.
Pesa
Si lazima pesa..

Mwanamama huyo amesema tangu aachane na kutumia fedha kununua na kuuza bidhaa, amekuwa akiishi kwa furaha bila kifani.

Hadithi ya mwanamama huyu ilianza miaka ishirini na mwili iliyopita wakati akiwa mwalimu wa shule ya sekondari. Amesema alipoahamishwa kutoka jiji la Dortmund kwenda eneo la Ruhr, alikutana na jambo ambalo lilibadilisha maisha yake.

Amesema kitu cha kwanza alichokiona ilikuwa idadi kubwa ya watu wanaoishi mitaani bila makazi. Amesema hali hiyo ilimshtua sana kiasi kwamba akaamua kuchukua hatua.
Amesema aliamini kuwa watu masikini wasio na makazi hawahitaji na huwa hawatumii fedha ili kukubalika katika jamii, bali kinachohitajika ni nafasi ya kuwezeshwa.
Amesema baada ya hapo, alifungua duka la kubadilishana bidhaa, liitwalo Gib und Nimm, ikiwa na maana ya Toa na Chukua. Unatoa bidhaa, unaewa bidhaa.

Na kwa taarifa yako

...Wanaume wana damu nyingi mwilini kuliko wanawake. Wanawake wana takriban lita nne na nusu, wakati wanaume wana lita tano na nusu.

Magufuli akingiwa kifua bomoabomoa

UAMUZI wa Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, kuendelea na bomoabomoa kwa watu wote waliojenga katika hifadhi ya barabara nchini umeungwa mkono na wanazuoni ambao walisema siasa ziwekwe kando katika utekelezaji wake.

Wasomi hao ambao walizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, walisema mkakati wa Magufuli kubomoa nyumba zote zilijengwa kwenye hifadhi ya barabara ni halali kwa sababu ni makosa kisheria watu kujenga katika maeneo hayo. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Jumatano wiki hii, Waziri Magufuli aliwatahadharisha watu waliojenga kwenye hifadhi ya barabara kwamba nyumba zao zitabomolewa kwa operesheni bomoabomoa itakayoanza hivi karibuni.Magufuli alisisitiza kuwa, hakuna atakayemzuia kutekeleza azma yake hiyo kwa vile anafuata sheria ya nchi ambayo Rais Jakaya Kikwete ameibariki kutumika wa kutia saini.

Agizo hilo la Dk Magufuli linakuja takribani miezi mitano baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Rais Kikwete kwa nyakati tofauti kumzuia kuendelea na bomoabomoa aliyokuwa anaitekeleza sehemu mbalimbali nchini.

Machi 6, mwaka huu, akiwa ziarani mkoani Kagera, Waziri Mkuu Pinda alisimamisha bomoabomoa katika hifadhi ya barabara nchi nzima hadi itakapoamuliwa vinginevyo na Baraza la MawaziriMachi 20 mwaka huu, Rais Kikwete alipotembelea Wizara ya Ujenzi akamshauri Magufuli kuzingatia utu na historia ya eneo wakati akitekeleza bomoabomoa.Alisema litakuwa jambo la ajabu kama kubomoa nyumba ya sanaa au kihistoria iliyopo katika hifadhi ya barabara.

Kutokana na maagizo hayo ya wakuu wake wa kazi, Dk Magufuli alisimamisha bomoabomoa zilizokuwa zinaendeshwa nchi  nzima.  Hata hivyo, wakati Rais Kikwete akizindua Barabara ya Singida-Manyoni, Dk Magufuli alisisitiza kuwa atafufua bomoabomoa kwa maeneo yote ya hifadhi za barabara kwa kutumia sheria zinazomruhusu kufanya.Wakiunga mkono tangazo jipya la bomoabomoa lililotolewa na waziri Dk Magufuli, wanazuoni waliozungumza na Mwananchi Jumapili walisema kwamba, hifadhi za barabara zimewekwa kisheria hivyo zinatakiwa kuheshimiwa na hatua ya kubomoa nyumba zilizojengwa katika maeneo hayo ni halali.

Profesa Ngowi
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Dk Honest Ngowi, alisema wakati umefika kwa viongozi wa Serikali kuacha siasa, akisisitiza kuwa maamuzi yanayotakiwa kutolewa na wataalamu yasiingiliwe.
“Unajua kila kiongozi akiwa anasema lake katika mambo ya kisheria kama hili la bomoabomoa ujue wazi kwamba, siasa zinaanza kuingizwa katika utendaji,” alisema Dk Ngowi.
Alifafanua kwamba, sheria ya Tanzania inaeleza wazi kuwa si ruhusa kujenga katika hifadhi ya barabara, hivyo wanapoibuka watu na kupingana na sheria hiyo ni kinyume na taratibu zilizowekwa ili zifuatwe.

Profesa Rwegasira
Profesa Delfin Rwegasira wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) alisema uamuzi juu ya ubomoaji wa nyumba zilizopo katika hifadhi ya barabara, ni halali lakini lazima lifanywe na wataalamu tena kwa umakini wa hali ya juu.“Jambo hili la upanuzi wa miji na ujenzi wa barabara lina mambo mengi…, lazima wingi wa watu utazamwe, pamoja na taratibu za kuwafidia watakaobomolewa nyumba zao,” alisema Rwegasira.Alitahadharisha kuwa katika utekelezaji wa suala hilo siasa hazitakiwi kuingizwa, badala yake waachiwe wataalamu.

Profesa Safari
Naye Profesa Abdallah Safari, ambaye kitaaluma ni mwanasheria alisema kuwa, kila kitu kilichopo katika hifadhi ya barabara kinatakiwa kubomolewa kwa mujibu wa sheria.
“Nakumbuka wakati wakipanua barabara ya kwenda Mbagala, kuna msikiti ulibomolewa, watu walilalamika lakini baadaye mambo yakaisha.  Hiyo ndiyo maana ya sheria, lazima itekelezwe,” alisema Safari.
Alisema Rais anachoweza kufanya ni kutoa msamaha kwa wafungwa na si kwa waliojenga katika hifadhi ya barabara, kwani kwa kufanya hivyo atakuwa amekiuka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hata hivyo, pamoja na kuunga mkono hatua ya Dk Magufuli, baadhi ya wahadhiri walisema inaonekana kuna mgongano wa maamuzi katika Serikali ambayo yanatakiwa kusahihishwa haraka.

Profesa Wangwe
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mkurugenzi  wa Taasisi ya Utafiti Kuhusu Kuondoa Umaskini (Repoa),  Profesa Samweli Wangwe, amesema haoni kama huko ni kugongana kwa kauli ila ni ushauri.Hata hivyo, alisema kutoa ushauri kama huo katika majukwaa ya siasa inaleta picha mbaya kwa wananchi.“Mimi ninachoona ni kwamba alipewa ushauri siyo mgongano, sema huo ushauri siyo vizuri kuutolea kwenye majukwaa, ingepaswa aambiwe wakiwa wenyewe,” Profesa Wangwe alisema na kuongeza:
“Sheria inataka nyumba zibomolewe, zisipobomolewa itakuwa ni kuvunja sheria, kwa hiyo ingebidi aambiwe jinsi ya kuzivunja ili kusiwe na athari sana.” 

Kulipa fidia
Alipoulizwa kuhusu fidia kwa watakaokumbwa na bomoabomoa hiyo,  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, alisema waliojenga kwenye hifadhi ya barabara hawatalipwa fidia, isipokuwa wale barabara itawafuata watalipwa.Akizungumza kwa njia ya simu  na Mwananchi Jumapili jana, Prof Tibaijuka alisema kuwa, kazi ya wizara yake ni kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata haki , lakini akaonya kuwa watakaokuwa wamevunja sheria kwa kujenga ndani ya hifadhi ya barabara hawana haki.
Januari 13, mwaka huu Magufuli aliagiza kuwa wananchi waliojenga katika hifadhi ya barabara waaanze kubomoa nyumba hizo mapema na kwamba wasitegemee kulipwa fidia.
Pia alimtaka Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam pamoja na madiwani kujipanga na kuondoa nyumba zilizopo katika maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya njia ya mabasi yaendayo kasi ili kuwawezesha makandarasi kuanza kazi hiyo.Waziri Magufuli amekuwa akisisitiza kwamba waliojenga ndani ya barabara wamevunja sheria namba 13 ya mwaka 2007  na kwamba hawastahili kulipwa fidia.

Surfing for danger


The latest craze among some teenagers in Mumbai, India, is a dangerous one - train surfing.
It has already caused injuries to one teen and the Indian Government Railway Police (GRP) want to put a stop to it.

To make matters worse, a video of the boys doing stunts has gone viral on YouTube.
It shows two young men skidding along a station platform while hanging on to the handrail of a moving train.
As the train leaves the station, they jump up on to a ledge, and then leap out to slap each passing pylon, reported the Telegraph.

It also shows them jumping on top of a steel viaduct and running on it while hanging on to the train before jumping back on again.

The stunts appeared to be staged to impress travellers in the trains' women-only carriages between Mumbai's Cotton Green and Reay Road stations.

The stunts take to new levels of risk the Mumbai tradition of fare-dodging passengers sitting on the train roof.
Those caught "travelling dangerously" can be fined 500 rupees (S$13) or jailed for three months.
The GRP said one young person recently fell off a train after being hit by a pole while trying to perform the stunts.

Doctors at the state-run St George Hospital, where Zahid Ansari, 13, who was hit by a pole while performing the stunts, is undergoing treatment, said he is in a stable condition.
He has suffered facial fractures and will have to undergo surgery.
"There is a facial bone fracture below his right eye. There is also a lot of blood collection in his cheek due to the fracture," surgeon Narsing Mane told the Times of India.

Coloured chicks: Cute or cruel?

Chicken eggs are being injected with dye in order to produce vibrantly-coloured chicks upon hatching.
Further findings revealed an online video of someone who had a similar encounter with the multi-coloured chicks, and these chicks are said to be commonly sold by street vendors in China, India, Malaysia, Morocco, Yemen, and even the US.

Questions of animal cruelty have arisen as a result of the embryos being injected with dye while still developing within the egg, as dyes consist of hydrogren peroxide and ammonia. Food colouring could also be used, but while it is harmless for humans, it might not be the same for chicks. Many have been intoxicated and have died before hatching.

However, the colour is not permanent. As the chicks grow, undyed feathers will replace the coloured ones, causing the birds to lose their visual appeal, and therefore running the risk of being discarded by their owners.

Wapiganaji Libya wajongelea Bani Walid

Wapiganaji wa Libya wanajongelea mji ulioko jangwani wa Bani Walid -- moja kati ya ngome ya mwisho la wanajeshi wa Kanali Gaddafi -- baada ya kutoa ilani kwa mji huo kusallim amri ama sivyo, utashambuliwa.

Mpiganaji wa Libya anapokea bendera mpya kutoka raia, nje ya Bani Walid
Mamia ya wapiganaji kwenye magari wakiwa na silaha nzito, wanasogelea mji huo kutoka pande tatu.
Lakini mwandishi wa BBC alioko nje ya Bani Walid anasema haijulikani kama wapiganaji wamepewa amri ya kufanya shambulio.

Inafikiriwa kuwa watu wa familia ya Gaddafi pengine wameshakimbia kwa kupitia Bani Walid wakati walipoondoka Tripoli.

Taarifa zinaonesha pengine baadhi yao wangali wamejificha katika mji huo.