Tuesday, December 20, 2011

Former Miss Venezuela dies of breast cancer at 28





Former Miss Venezuela Eva Ekvall, who appeared bald and without makeup in a recent book about her struggle against breast cancer, died in Houston on Saturday after losing her battle with the disease, according to Venezuelan TV news network Globovision. She was 28.
The former beauty queen had worked to promote cancer awareness since being diagnosed in 2010.
The hospital in Houston where she reportedly passed away, and the funeral home there where her body was taken declined to comment on news of her death.
Ekvall won the Miss Venezuela title in 2000 and was a third runner-up for Miss Universe in 2001. She also worked as an actress and television anchor.
Although known for her beauty, Ekvall was depicted bald and without makeup in her book Fuera de Foco (Out of Focus) released this year, which chronicled her fight with breast cancer for readers around the world. Photographer Roberto Mata showed the beauty queen throughout her cancer treatment and as her illness regressed. She wrote the text of the book.

Mgogoro waikumba Manispaa ya Arusha

Paul Sarwatt
Arusha
Mji wa Arusha
Mji wa Arusha
 
Ni kuhusu zabuni ya ushuru wa maegesho ya magari
MANISPAA ya Arusha imeingia katika kashfa ya kutoa zabuni ya kukusanya ushuru wa maegesho ya magari katika  mji wa Arusha kwa Kampuni ya Barack Printers Ltd, bila  kampuni hiyo kutia saini mkataba wa kukusanya ushuru  kinyume cha sheria za Jiji.
Taarifa zilizopatikana mwishoni mwa wiki na kuthibitishwa na vyanzo kadhaa zinaeleza kuwa kampuni hiyo ilipewa zabuni ya kukusanya mapato ya ushuru wa maegesho ya magari kuanzia Desemba mosi, mwaka huu, lakini makataba wake haukuwa umesainiwa na pande zote zinazohusika.
Kwa mujibu wa  sheria zinazotawala Serikali za Mitaa, zabuni yoyote ya kukusanya ushuru kati ya halmashauri, manispaa au jiji na kampuni au wakala aliyeshinda zabuni, ni lazima mkataba  wake usainiwe na pande zote kabla ya kampuni husika kuanza kazi.
Kampuni husika pia inatakiwa kupitia mchakato wa kujadiliwa na Bodi ya Zabuni na baada ya machakato kukamilika, jina la kampuni iliyoteuliwa na bodi huwasilishwa katika Kamati ya Fedha na Uchumi ya Baraza la Madiwani,  ambako hujadili na baada ya kuridhia, meya au mwenyekiti wa halmashauri husika hutia saini  mkataba kwa niaba ya halmashauri yake.
Hata hivyo, pamoja na sheria hiyo kuwa wazi,  Halmashauri ya Jiji la Arusha imekiuka sheria hiyo na badala yake, imetoa zabuni kwa kampuni hiyo ya Barack Printers  Ltd kukusanya ushuru wa maegesho ya magari wakati haina makataba wa kutekeleza kazi hiyo.
Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka ndani ya Manispaa zinaeleza kuwa, suala hilo liliwasilishwa katika kikao cha Kamati ya Fedha na Uchumi ya Baraza la Madiwani, ambayo Mwenyekiti wake ni Meya wa Jiji, Gaudance Lyimo, na kamati hiyo iliyakataa maelezo yaliwasilishwa na Mkurugenzi wa  Jiji, Estomih Chang’a kwamba hayakujitosheleza.
“Katika kikao hicho, Chang’a (Mkurugenzi wa Jiji) akiwa na timu yake ya wataalamu aliwasilisha mbele ya kamati taarifa za Kampuni ya Barack Printers kupewa zabuni ya  kukusanya ushuru wa halmashauri, lakini wajumbe wote walikataa na kuhoji mambo kadhaa,” anaeleza mtoa taarifa wetu.
Miongoni  mwa hoja za wajumbe wa kamati hiyo zilizoelekezwa kwa mkurugenzi ni pamoja wajumbe kutaka kufahamu kampuni hiyo ilishinda lini zabuni hiyo kwa vigezo gani vilivyotumika hadi kuipa wa zabuni husika.
“Mkurugenzi na watalaamu wake hawakuwa na maelezo ya kina baada ya kuhojiwa na wajumbe hao na ndipo kamati ilipopitisha azimio kumtaka meya asitie saini mkataba huo,” alieleza mtoa habari wetu.
Utata mwingine ulioibuka kuhusu kampuni hiyo ni umiliki wake, ikidaiwa kuwa inamilikiwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Moshi Vijijini, Morris Makoi, ambaye ni diwani katika halmashauri hiyo na kwa mujibu wa sheria za zabuni katika Serikali za Mitaa, diwani, mtumishi au kiongozi wa Serikali haruhusiwi kuwa mzabuni katika halmashauri yoyote.
“Kwa ujumla suala hili la ukusanyaji wa ushuru wa maegesho ya magari limezingirwa na wingu zito na hata masuala ya ufisadi na rushwa yanadaiwa kutumika kabla na baada ya kukamilika kwa mchakato wake,” kilieza chanzo chetu cha habari.
Kamati pia ilimtaka mkurugenzi huyo kutoa maelezo kuhusu vigezo vilivyotumika kuipa zabuni kampuni hiyo, inayodaiwa hata hivyo kuingia kwenye ushindani wa zabuni kwa kiwango cha chini cha fedha, ikilinganishwa na kampuni nyingine mbili zilizoshiriki na kuweka kiwango cha juu zaidi.
Kampuni nne zinaelezwa kuomba zabuni hiyo  na fedha viwango vya fedha walivyotumia wakati wa ushindani wa zabuni kwenye mabano ni pamoja na Ecco Consultant (Sh milioni 48).
Kampuni nyingine ni Consard Ltd (Sh. milioni 46), Makumira Filling Station (Sh. milioni 42) na Barack Printers (Sh. milioni 42), ambayo ndiyo imepewa ushindi unaotiliwa shaka.
Kabla ya kampuni hiyo kupewa zabuni kazi ya kukusanya mapato ilifanywa na Kampuni ya Jamahedo, iliyomaliza mkataba wake Novemba 30, mwaka huu, na mkataba huo ulikoma baada ya uongozi wa manispaa kukubaliana na kampuni hiyo kusitisha mkataba kutokana na mgogoro uliozikumba pande zote mbili.
Mgogoro huo uliodumu kwa miaka miwili na kuathiri kwa ujumla shughuli za ukusanyaji mapato, ulianza baada ya uongozi wa manispaa kuzuia Kampuni ya Jamahedo isikusanye ushuru katika maeneo tisa, kinyume cha mkataba uliosainiwa awali.
Kutokana na hatua hiyo ya manispaa, kampuni ya Jamahedo ilifungua shauri Mahakama Kuu katika kesi iliyokuwa chini ya Jaji Sambo, lakini baada ya mvutano wa muda mrefu walikubaliana kumaliza suala hilo nje ya mahakama na Jamahedo kupewa miezi minne kukusanya ushuru bila kupeleka fedha zozote manispaa ili kufidia hasara waliyopata na mkataba huo ulimalizika Novemba 30.
Habari zaidi zinaeleza kuwa Bodi ya Zabuni ilitangaza kampuni zilizoshinda zabuni mbalimbali za kukusanya ushuru katika Jiji la Arusha mapema Juni, mwaka huu, ambapo kwa upande wa ushuru wa magari, kampuni nne ziliomba kazi hiyo.
Hata hivyo, hakuna kampuni iliyopewa zabuni kutokana na mgogoro uliokuwepo mahakamani wakati huo, baina Jamahedo na manispaa hivyo, Jamahedo waliendelea kukusanya ushuru huo wa maegesho hadi walipomaliza mkataba wao Novemba 30.
“Wakati muda wa mkataba wa Jamahedo ukifikia tamati, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, aliushauri uongozi wa manispaa kujipa muda wa kutafakari kabla ya kuingia mkataba na kampuni nyingine na pia kupitia kwa kina makataba husika, ili kuondoa matatizo yaliyotokea awali” alisema moja wa maofisa wa jiji (jina linahifadhiwa) aliyezungumza na gazeti hili.
“Mkurugenzi na wataalamu wake wala hawakujipa muda wa kutafakari kama walishauriwa na Mkuu wa Mkoa. Badala yake,  walimpuuza RC na kuidhinisha Barack Printers Ltd, waanze kazi bila hata mkataba kupitiwa na Kamati ya Fedha na Uchumi, matokeo yake wananchi wa Arusha wanalipa ushuru wa maegesho kwa mkataba batili, kinyume cha sheria” alieleza ofisa huyo.
Meya wa Jiji la Arusha, Gaudance Lyimo alithibitishia Raia Mwema kuwa, mkataba huo haujasainiwa na kamati yake ilikuwa bado haijapata maelezo ya kutosha kuhusu kampuni iliyopewa zabuni na halmashauri.
“Ni kweli bado hatujasaini mkataba kutokana na sababu kadhaa kuhusu kampuni husika na tumeomba maelezo ya kina kutoka kwa mkurugenzi na watu wake na tunatarajia watafanya hivyo haraka iwezekanavyo,” alieleza Lyimo.
Meya Lyimo alisema kuwa kwa muda mrefu mikataba ya kukusanya mapato ya halmashauri imekuwa na migogoro na kwamba, mawakala waliifungulia mashtaka halmashauri kutokana na udhaifu wa watendaji wake wanaodaiwa kushiriki katika hujuma na hivyo kusababisha upotevu mkubwa wa mapato.
“Kutokana na uzoefu wa mikataba tulioupata na kesi mbalimbali tulizofunguliwa ni lazima tuwe makini na suala hili ili tutakapokubaliana basi kusiwe na dosari ambazo zinaweza kuingiza halmashauri yetu katika hasara ya kulipa fidia na gharama zisizo za lazima,” alisema Lyimo.
Kwa mujibu wa meya huyo, suala hilo sasa litajadiliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani kinachotarajiwa kukutana Desemba 16, mwaka huu, katika ukumbi wa mikutano wa Jiji. Katika kikao hicho,  madiwani watapata fursa ya kujadili kwa kina utata kuhusu kampuni hiyo.
Akizungumzia utata huo, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Estomih Chang’a, alikanusha taarifa hizo.
“Si kweli kuwa hakuna mkataba ila tumewapa barua kuwa wameteuliwa kufanya kazi ya ukusanyaji wa ushuru na barua hiyo ina halalisha wao kufanya kazi wakati tunaandaa mikataba  ya kisheria unayoizungumzia,” alisema Chang’a.
“Nawashangaa sana nyie mnaofutilia suala dogo kama hili, kuna kitu gani kipya hapa? Halmashauri imeingia mkataba na kampuni hiyo kihalali baada ya kupitishwa na Bodi ya Zabuni, kwa hiyo, hakuna tatizo,” alisema mkurugenzi huyo ambaye amekuwa akitajwa kuwa ni mtendaji dhaifu wa kazi.
Akijibu tuhuma dhidi ya kampuni hiyo inayotajwa kuwa ni mali yake, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Moshi Vijijini, Morris Makoi, alisema ni kweli wanatekeleza kazi ya kukusanya ushuru huo baada ya kampuni yake ya Mkomilo Trading, kuingia mkataba wa kibiashara na Barack Printers Ltd, kuwasaidia kazi hiyo kwa kuwa hawana uzoefu.
“Hawa Barack Printers wametu-sub contract sisi Kampuni ya Mkomilo Trading, ili tukusanye ushuru kwa niaba yao kwa sababu hawana uzoefu, lakini kazi hii wamepwa kihalali baada ya kushinda zabuni iliyotangazwa,” alieleza Makoi.
Hata hivyo, sheria za halmashauri pia zinazuia kampuni iliyopewa zabuni kuingia makataba na kampuni nyingine kutekeleza kazi walizokubaliana na maelezo hayo ya Makoi yamezidi kuongeza utata kuhusu uhalali wa zabuni hiyo ya ushuru wa maegesho.
Makoi anasema; “Tayari tumelipa bondi ya shilingi milioni 46 kwa halmashauri na tumekubaliana kuwasilisha Sh milioni 42.5, kila mwezi na makataba wetu unaisha Juni 30, mwaka 2012 na wanaolalamika ni washindani wetu wa kibiashara ambao wamekosa zabuni hii”.
Halmashauri ya Jiji la Arusha ni kati ya halmashauri zinazolalamikiwa nchini kutokana na kushamiri wa vitendo vya ufisadi. Hivi karibuni, Serikali iliwahamisha watumishi 19 wakiwamo wakuu wa idara sita, kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kushamiri kwa vitendo vya ufujaji wa fedha za miradi.
Halmashauri hiyo imekuwa ikipata hati chafu kwa miaka zaidi ya mitano mfululizo baada ya hesabu zake kukaguliwa na mabilioni ya fedha yaliyotengwa kwa ajili ya miradi mbalimbali, zinadaiwa kupotea kutokana na usimamizi duni kutoka kwa watendaji.

Ufisadi mpya kuitikisa Dar

Mwandishi Wetu
Bandari ya Dar es  Salaam
Bandari ya Dar es Salaam
 
Ni wa bilioni 600/= upanuzi wa Bandari
MRADI mkubwa wa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam, unaotarajiwa kugharimu takriban Sh. bilioni 600, umeingia dosari ikidaiwa kwamba tayari wakubwa serikalini, akiwamo mmoja wa mawaziri, wameanza mipango ya kifisadi itakayochelewesha mradi huo kuanza, Raia Mwema limeelezwa.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana, katika mipango yao, vigogo kadhaa wamepanga kutafuta kampuni itakayoendesha shughuli za ujenzi bandarini kinyume cha makubaliano ya awali, hali inayoashiria kuweza kuchelewa kuanza kwa mradi husika.
Taarifa kutoka Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), zimeeleza kwamba Serikali ya China, kupitia Benki ya Exim ya nchini humo, imekubali kutoa fedha za upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam lakini kumekuwa na vikwazo kadhaa kutoka baadhi ya vigogo hao wa Serikali, wakilenga kujinufaisha na mchakato huo.
Kwa mujibu wa habari hizo, Waziri mmoja (jina linahifadhiwa kutokana na kutopatikana kwa sasa kujibu tuhuma) amefunga safari hadi China kutafuta mwekezaji “atakayempendeza” ambaye atafanya kazi ya upanuzi wa bandari hiyo eneo la gati namba 13 na namba 14, karibu na gati la mafuta (KOJ).
Uamuzi wa waziri huyo kutafuta kampuni itakayofanya shughuli za upanuzi bandarini, unatajwa kuingilia uamuzi uliofikiwa wa kutoa jukumu hilo kwa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) ambayo ndiyo iliyopewa fedha kutoka China, na ambayo ndiyo yenye majukumu ya kupata kampuni husika ya ujenzi.
Kwa mujibu wa habari hizo, awali Waziri huyo katika juhudi zake za ‘kujitafutia’ ulaji alikuwa akifanya mawasiliano na kampuni moja ya Falme za Kiarabu (UAE), ambayo nayo imeelezwa kuwa na uhusiano mkubwa na wanasiasa kadhaa nchini.
Hata hivyo, aliahirisha juhudi zake hizo za Falme za Kiarabu baada ya kuzingatia ukweli kwamba fedha zinazogharimia shughuli hizo ni kutoka China na kwa hiyo, ni busara kwake kutafuta kampuni ya kichina, ili kupunguza kile kinachoelezwa kuwa ‘kelele’ za wadau.
“Waziri huyo baada ya kuona ukubwa wa mradi, ameamua kuingilia majukumu ya Bandari kuhusu kazi hizi, anatafuta kampuni ambayo ndiyo itafanya shughuli za upanuzi. Kwa hiyo Bandari itabaki mtazamaji tu, huyo Waziri anataraji maslahi yake yataingizwa kwenye hiyo kampuni atakayoipa kazi.
“Mwanzo akishirikiana na baadhi ya wanasiasa nchini alitafuta kampuni kutoka Falme za Kiarabu lakini wenzake wakamwambia, tutafute kampuni ya China kwa sababu fedha (mkopo) zimetoka huko China, tukitafuta kampuni isiyo ya China kelele zitakuwa nyingi,” kinaeleza chanzo chetu cha habari.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa Benki ya Exim ya China kwa maelekezo ya Serikali ya nchi hiyo, imekubali kutoa fedha hizo kwa TPA inayomilikiwa na Serikali ya Tanzania, kwa njia ya mkopo wa muda mrefu na wenye masharti nafuu ya riba ya asilimia mbili tu, lakini kwa masharti kuwa kampuni ya ujenzi ya China ndiyo itakayojenga mradi huo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopo, Serikali ya Tanzania kupitia kwa Wizara ya Fedha, ilikwisha kutoa hati ya dhamana kwa ajili ya mradi huo ambao ulianza kuasisiwa mwaka 2008, wakati huo, Dk. Shukuru Kawambwa akiwa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi.
Raia Mwema ilifanya mawasiliano na Waziri huyo bila mafanikio. Hata hivyo, kwa upande mwingine, Katibu Mkuu wa Waziri wa Uchukuzi, Omari Chambo, naye hakupatikana kueleza kuhusu masuala hayo.
Hata hivyo, gazeti hili lilifanikiwa kumpata Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraem Mgawe, na kueleza kuwa, hana taarifa za kigogo yeyote kuingilia mchakato huo.
Alisema mradi huo ni moja ya miradi muhimu kwao na kwamba inapewa kipaumbele cha juu, lakini bado hawajapata fedha walizoomba serikalini.
Alikanusha kuwa tayari wamepata fedha kutoka Benki ya Exim ya China na badala yake anasema walichopata ni barua kutoka serikalini ambayo itawawezesha kupata fedha.
Kuhusu kuwapo kwa vigogo serikalini na wanasisa wanaokwamisha, Mgawe alisema hana taarifa hizo kwa kuwa wako katika mchakato wa kuanza kwa mradi.
Mradi huo uliorodheshwa katika miradi muhimu ya TPA mwaka 2008 ukiwa na gharama za Dola za Marekani milioni 525, ambazo zitawezesha kupanuliwa kwa Bandari ya Dar es Salaam ili kuweza kushindana na Bandari ya Mombasa, nchini Kenya

Kumekuwa na madai kutoka kwa wadau mbalimbali wa sekta ya uchukuzi wakiwamo wamiliki wa kampuni za meli, mawakala na hata watumishi wa umma kwamba, matatizo makubwa katika sekta ya bandari yanatokana na ukiritimba uliopo kwa Kitengo cha Makontena ambacho kinaendeshwa na Kampuni binafsi ya Tanzania International Container Terminal Services Limited (TICTS).
Madai hayo pamoja na mengine ndiyo yameisukuma Serikali kuanza mradi wa upanuzi wa Bandari ya Dar es Salaam ambayo inategemewa na nchi kadhaa kupokea mizigo yao, zikiwamo nchi za Rwanda, Burundi na Kongo (DRC).
TICTS  ambayo iliingia nchini katika mazingira tata, imekuwa katika migogoro ya mara kwa mara na wadau na hasa wafanyakazi wake kutokana na kile kinachoelezwa ya kwamba kuna mkono wa wanasiasa wachafu, ambao wamekuwa wakiendelea kuyumbisha sekta ya uchukuzi nchini.
Katika eneo hili la Afrika Mashariki, taarifa zinasema, ni Tanzania pekee, katika hatua inayotafsiriwa kuwa ya kujinyima mapato, ndiyo imekabidhi uendeshaji wa biashara kubwa ya kupakia na kupakua mizigo bandarini kwa kampuni binafsi.

Ikulu kuwafutia posho wabunge

Mwandishi Wetu
Rais Jakaya Kikwete, Spika Anna Makinda
Rais Jakaya Kikwete, Spika Anna Makinda
 
Matanuzi yao sasa kutegemea mshahara
Upembuzi wa athari wafanyika
Siku nne tu za ‘wikiendi’ walilipwa milioni 129/-
SAKATA la nyongeza ya posho kwa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeingia katika sura mpya, na sasa uchunguzi wa Raia Mwema, umebaini kuwa si tu Rais Jakaya Kikwete hatasaini nyongeza hiyo mpya kama tulivyoripoti wiki iliyopita, bali posho hizo za ‘kukaa kitako’ (sitting allowance) zitatangazwa  kufutwa rasmi wakati wowote.
Vyanzo vya habari vya gazeti hili ndani ya Ikulu vimethibitisha ya kuwa Rais Kikwete amepewa ushauri wa kufuta posho hizo kutoka kwa baadhi ya watalaamu wake na uamuzi unaweza kufanyika na kutangazwa wakati wowote.
Inaelezwa kuwa upembuzi wa kina wa athari za kufuta posho hizo kwa wabunge na hasa kujua kama zitaathiri majukumu yao umekwishakufanyika na kukamilika na taarifa zinasema kati ya waliowasilisha takwimu za ‘kihasibu’ Ikulu, ni pamoja na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila.
“Suala lililopo mezani kwa Rais si kusaini au kutosaini waraka wa mapendekezo ya nyongeza ya posho, bali ni kufuta sitting allowance zote kwa wabunge. Huo ndio ushauri wa kitaalamu unaohusisha hesabu za wahasibu na ambao, Rais ameukubali na unatarajiwa kutangazwa karibuni.
“Kama akitangaza kufuta posho hizi maana yake, masuala mengine ya wabunge yanaweza kufanyiwa marekebisho katika mshahara, ambayo nchi itanufaika kwa kukata kodi pia, unajua walikuwa hawakatwi kodi kwenye posho.
“Wabunge hawastahili malipo ya sitting allowance, kwa sababu wanakuwa wanatekeleza wajibu wao na stahili yao ni kulipwa mishahara tu,” alisema mtoa habari wetu.
Lakini wakati hayo ya Ikulu yakiwa hivyo, uchunguzi wa Raia Mwema umebaini ya kuwa wakati wa jaribio la kutaka nyongeza ya posho mpya, Spika wa Bunge, Anne Makinda, alizungumza tu na Rais Jakaya Kikwete akiamini kuwa angeridhia wito wa wabunge na hivyo, mchakato wa malipo ya posho mpya ukianza si tatizo.
Mbali na Spika kuzungumza tu na Rais Kikwete bila kufikia muafaka, inaelezwa kuwa akishirikiana na Tume ya Bunge, walimshinikiza Katibu, Dk. Kashilila, kulipa posho mpya, naye akagoma.
Taarifa zaidi zinasema hata Spika Makinda mwenyewe aliwekwa katika shinikizo kubwa la wabunge wakitaka posho mpya na kama angeshindwa, walimtisha kumpigia kura ya kutokuwa na imani naye na hivyo, kumng’oa madarakani.
Taarifa za uchunguzi zilizotufikia zinaeleza kuwa wabunge karibu wote waliunga mkono posho mpya na kupitia Tume ya Bunge, azimio la nyongeza likapitishwa kutoka Sh 70,000 hadi 200,000.
Kutokana na azimio hilo kupitishwa, wajumbe wa Tume hiyo kwa kushirikiana na Spika, walimtaka Katibu Dk. Kashilila kuanza kuwalipa katika mkutano uliopita wa Bunge.
Lakini, kwa mujibu wa taarifa hizo, akikariri mchakato unaofutwa katika malipo ya aina hiyo ambayo yanahitaji mamlaka husika iridhie, na katika suala hili mamlaka hao ni Rais Kikwete ambaye alikuwa hajaridhia, Dk. Kashilila aligoma kuwalipa akisema bado mamlaka husika (Rais) hajaidhinisha kwa vile hakuna instrument  ama waraka idhinishi kwa ajili hiyo ambao lazima usainiwe na Rais kabla ya kwenda Hazina kuomba fungu.
“Katibu alishinikizwa sana, alipowaeleza hana instrument Spika akamwambia yeye ameongea na Rais na amekubali, lakini Katibu anajua kukubali kwa Rais si kwa maneno bali ni kutia saini waraka.
“Kwa hiyo, naye Katibu akamwambia Spika, kama Rais amekubali naomba niandikie rasmi kwa maandishi ili nifanye malipo...hapo Spika hakuandika.
“Lakini pamoja na Spika kutoandika, alisisitiza kwamba amekwishakuzungumza na Rais, na pia Tume ya Bunge iliweka shinikizo kali dhidi ya Katibu alipe posho mpya.
“Alichofanya Katibu hakulipa posho isipokuwa amelipa malipo ya wabunge kwa siku walizofanya kazi mwishoni mwa wiki, kuanzia kwenye kamati na vikao vya Bunge, si wabunge wote waliopata malipo hayo,” kinaeleza chanzo chetu cha habari.
Raia Mwema ilizungumza na Katibu wa Bunge, Dk. Kashilila kujua kama alishinikizwa lakini katika majibu yake akasisitiza akisema; “Sikulipa mbunge yeyote posho mpya, mimi ndiye mlipaji...nasema sijalipa.
“Nilicholipa ni malipo wanayostahili waheshimiwa wabunge waliofanya kazi siku za mwisho wa wiki, wengine kwenye vikao vya kamati na wengine vikao vya Bunge Dodoma.
“Tunaandaa taarifa za mchanganuo na kuwatumia wahusika wote, halafu mkawaulize nilichowalipa ni ongezeko la posho au nini?” alisema Dk. Kashilila.
Hata hivyo, gazeti hili limebaini kuwa malipo yanayotajwa kufanyika kwa wabunge kama anavyoeleza Katibu wa Bunge, yamefanywa kwa wabunge 307, kila mmoja akilipwa Sh. 420,000 zinazohusisha siku nne za mwisho wa wiki walizofanya kazi, wakati wa mkutano wa Bunge uliopita na baadhi ya vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge, kabla ya kuanza kwa mkutano huo uliofanyika Novemba, mwaka huu.
Taarifa zinaonyesha kuwa jumla ya Sh. 128,940,000 (takriban milioni 129) ndizo zilizolipwa kama fungu la ziada ambalo limesababisha wabunge kuhisi ongezeko kwenye akaunti zao.
Takwimu hizo zinapingana moja kwa moja na kauli ya Spika kuwa wabunge walilipwa posho mpya tangu mkutano uliopita.
Utata kuhusu kauli ya Spika
Uchunguzi zaidi wa gazeti hili umebaini kuwa kauli ya Spika kuwa posho zimelipwa haina ukweli isipokuwa kilichofanyika kwa wakati huo ni agizo alilotoa (Spika) kutaka hesabu za malipo ya posho mpya ziandaliwe na kama Rais angesaini, basi walipwe kwa kuongezea juu ya  posho za Sh 70,000 kwa siku walizolipwa mkutano uliopita wa Bunge.
“Spika kule bungeni aliagiza hesabu za malipo ya posho kwa viwango vipya zifanyike. Kwa hiyo, wabunge wangelipwa hizo Sh.70,000 lakini baada ya Rais kusaini, wangeongezewa (kufidiwa) ili ifikie Sh 200,000. ndiyo maana alisema wabunge wameanza kulipwa mkutano uliopita, kilichopo ni kwamba waliamini Rais angesaini tu kiurahisi,” anasema mtoa habari wetu.
Juhudi za gazeti hili kumpata Spika kuzungumzia suala hilo zimegonga mwamba kwa siku kadhaa sasa, ikiwa ni pamoja na kumpigia kwa simu yake ya mkononi iliyokuwa ikiita bila majibu.
Njama kumng’oa Katibu zasukwa
Kutokana na suala hili kuonekana kuibua mvutano wa kiutawala ndani ya Bunge, sasa kuna taarifa kwamba mkakati maalumu umeanza kusukwa ili kumng’oa Dk. Kashilila.
Mpango huo ambao Raia Mwema imeunasa, unatajwa kuhusisha baadhi ya viongozi wa Bunge, wakiwamo baadhi ya wenyeviti wa Kamati za Kudumu za Bunge.
Wenyeviti hao (majina yanahifadhiwa) wanadaiwa kuchukizwa na uamuzi wa Katibu wa Bunge, wakiamini ni kati ya wasiotaka wabunge kuongezewa posho na kwa hiyo, wanadhani ni kikwazo kwa mafanikio ya Spika Makinda.
Raia Mwema imetajiwa baadhi ya wenyeviti hao akiwamo Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mahesabu ya Serikali Kuu, Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Momose Cheyo ambaye alikataa kuzungumzia jambo hilo alipoombwa aeleze maoni yake wiki hii na mwandishi wetu.
Cheyo, ama maarufu kama Bwana Mapesa, alisema ya kuwa kama ana mawazo yake kuhusu posho anajua sehemu sahihi pa kuyawasilisha.
Kikwete awajibu kupitia CCM
Wachambuzi wa mambo wanasema ya kuwa taarifa ya Rais Kikwete ya kuukataa mpango huo wa posho kwa wabunge imejieleza wazi katika hatua ya wiki hii ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kutangaza kwamba hakiafiki posho hizo ziendelee kulipwa na kwamba ni busara suala hili liachwe kwa sasa.
CCM kupitia kwa Katibu wake wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, mwishoni mwa wiki iliyopita ilitoa tamko ikisema: “Tunaamini busara itatumika kuachana na jambo hili, kwani kuendelea  nalo kunaweza kutafsiriwa ni kuwasaliti watendaji katika sekta nyingine, wakiwamo askari, walimu na madaktari.
“Kwa kuongeza kiwango hicho cha posho kwa wabunge ni kuongeza pengo la tofauti ya kipato kati ya wenye nacho na wasionacho katika jamii yetu hasa kwa kuegemea baadhi ya makundi.
“Swali kubwa hapa linakuwa je, maisha yanapanda Dodoma peke yake na kwa wabunge tu? Kuongoza ni kuonyesha njia hivyo si sahihi kwa wabunge kuonyesha njia kwa kujiongezea posho peke yao kwa kisingizio cha ugumu wa maisha.”
Kauli ya Zitto Kabwe
Miongoni mwa wabunge, Ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, pekee mwenye msimamo wa wazi kupinga si tu ongezeko la posho za sasa, bali hata posho nyingine zinazolipwa kwa wabunge kwa kutimiza majukumu yao ya kawaida, ambayo kipato halali kwa mujibu wa tasiri ya Kabwe ni mshahara.
Alipoulizwa na gazeti hili kuhusu tafsiri yake kutokana na tofauti ya msimamo na kauli kati ya Spika Makinda na Katibu wa Bunge, Dk. Kashilila, Zitto alisema Spika amewekwa katika shinikizo na wabunge.
Speaker is under pressure (anashinikizwa), wabunge wamemtisha ili ahakikishe kunakuwapo posho mpya na asipofanya hivyo kuna vitisho kwamba anaweza kupigiwa vote of no confidence (kura ya kutokuwa na imani), ushauri wangu hapa ni kwamba Spika anatakiwa awe bold enough (imara), akatae shinikizo na aseme hakuna posho mpya.
“Najua amewekwa kwenye pressure na Tume ya Bunge na wabunge wengine, lakini kama kibali cha Rais hakuna aseme, awe jasiri,” alisema Zitto.
Waziri Mkuu achukizwa
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa kati ya viongozi walioshitushwa na kauli ya Spika Makinda kuhusu ongezeko la posho kwa kuzingatia ugumu wa maisha Dodoma, ni Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
Pinda ananukuliwa akisema; “Hili suala bado lilikuwa katika mchakato ambao uamuzi wa mwisho hautokani na Bunge, sasa kwa nini amekwenda (Spika) kueleza kabla ya kujua majibu ya mwisho?
Kuhoji huko kwa Pinda kumetafsiriwa na baadhi ya viongozi kuwa, Spika alichofanya ni kucheza mchezo wa kisiasa kwa kujivua pressure iliyokuwa ikielekezwa kwake na wabunge na kutua mzigo huo kwa Ikulu, na hususan Rais Kikwete, ambaye naye sasa amecheza ‘siasa’ kwa kutumia CCM.
Inaelezwa kuwa Spika Makinda amekuwa akishinikizwa na baadhi ya wabunge ambao wanamzongazonga wakihoji kwa nyakati tofauti; “Mbona Sitta (Samuel,  Spika aliyepita)  aliweza, wewe unashindwa nini?”

Uamuzi wa kukomoana ni ufisadi - Tendwa

MSAJILI wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa amevitupia lawama vyama vya siasa kwa kufanya uamuzi wa kukomoana na kusababisha gharama zisizo za lazima kwa taifa na kutolea mfano gharama za Uchaguzi Mdogo ambazo zinasababishwa na kuvuana uanachama,
akizifananisha na ufisadi.

Kauli yake imetokana na hatua ya mwishoni mwa wiki ya chama cha NCCR-Mageuzi kumvua uanachama mbunge wake wa Kigoma Kusini, David Kafulila, hatua ambayo ina maana amepoteza kiti hicho cha ubunge na sasa taratibu za Uchaguzi Mdogo zitafuatwa kwa mujibu wa Katiba.

Tendwa amesema ingawa yeye siyo mhusika wa gharama za uchaguzi, lakini Uchaguzi Mdogo
una gharama kubwa ambazo alisema si chini ya Sh bilioni 19 na uchaguzi kama huo unakuwa ni gharama kwa kuwa haukupangwa kufanyika.

Msajili huyo aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana baada ya kutoa mada ya uongozi kwenye mafunzo ya viongozi wa Baraza la Vyama vya Siasa kuhusu uongozi, uwajibikaji na utawala bora.

Alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu kuvuliwa uanachama kwa Kafulila, Tendwa alisema Katiba ya sasa hairuhusu mtu anapovuliwa uanachama kujiunga na chama kingine kuendelea na ubunge wake, hivyo ni lazima ufanyike Uchaguzi Mdogo kujaza nafasi hiyo.

“Sasa hizi bilioni 19 nani atakuwa amesababisha? Maana nyie ni mahodari wa kuandika
mafisadi na hili je ni ufisadi au ni nini?

Maana tusiwe mahodari wa kuisema Serikali, bali pia vyama vya siasa vinapaswa kuisaidia Serikali badala ya kuisababishia hasara,” alisema Tendwa na kuongeza:“Chama kufanya hivyo ni kupoteza sifa, nafikiri kuna adhabu nyingi ambazo zingeweza kutumika tofauti na kumfukuza
uanachama, maana hii ni hasara.

Sisi hatuingilii uamuzi wa chama, ila huo ni ushauri maana hata walichokuwa wakijadili kwenye vikao hatukijui.”

Tendwa alivitaka vyama vya siasa kutumia busara katika kufanya uamuzi badala ya kufanya
uamuzi wa kukomoana katika vikao vyao na hivyo kusababisha hasara kubwa kwa taifa ambazo si za lazima.

Msajili huyo alisema Kafulila anaweza kuomba rufaa ndani ya chama, lakini nje ya chama, pia
anao uhuru wa kwenda mahakamani na atakaposhinda kesi atakuwa mbunge wa wananchi wake.

Akizungumzia suala hilo, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC), Itikadi na Uenezi wa
Chama Cha Mapinduzi, Nape Nnauye alisema yeye si muumini wa kuwafukuza wanasiasa vijana kwenye vyama vya siasa, bali ni muumini wa kuvitumia vyama vya siasa kuwalea vijana.

“Sisi tunategemea vijana wanakosea ila tukijenga utamaduni wa kuwafukuza wanasiasa
vijana katika vyama vyetu nani atawalea na nani atawaelekeza vijana?

Mimi si muumini kabisa, mtu mzima utasema sasa huyu ameshindikana, lakini vijana hapana,”
alisema Nape na kuongeza: “Kijana akikosea leo afundishwe.

Sasa angalia suala la Kafulila, aliondoka Chadema na wakamuita sisimizi na majina mengine ya
ovyo, baadaye amekwenda NCCR nao wamemfukuza, sasa aende wapi?”

Mafunzo hayo ya siku mbili yanawashirikisha viongozi wa vyama mbalimbali vya siasa kwa
lengo la kuwaelekeza kuhusu mahusiano yao na wanachama, kuona ni jinsi gani vyama vinawajibika katika ulinzi na usalama wa taifa pamoja na kuangalia maadili ndani ya vyama vya siasa.

Kwa upande wake, Kafulila akizungumza na gazeti hili kwa simu jana, alisema hana tatizo na uamuzi uliotolewa na chama chake, bali anatulia.

Aidha, Kafulila amesema baada ya siku mbili kuanzia jana, ndipo atakapozungumzia kwa undani suala hilo kwa kuwa kwa sasa kuna taratibu zinazoendelea kufuatwa.

“Isingekuwa vizuri kuzungumza kwa sasa, najua wengi wangependa kunisikia zaidi,
lakini sisemi kwa leo (jana),” alisema Kafulila aliyevuliwa uanachama Jumamosi iliyopita na
Halmashauri Kuu.

Kisa na Mkasa na Salim Kikeke

NYOKA KITANDANI

Nyoka
Uso kwa uso na nyoka
Msichana mmoja nchini Poland aliyekuwa amelala, aliota kuwa anakumbatiana na mpenzi wake, na alipozinduka, alikuta amekumbatia nyoka.
Msichana huyo Iga Radkiewicz wa mjini Krakow, Poland, amesema aliruka kutoka kitandani huku akitetemeka. "Nilikuwa naota njozi murua kuhusu mimi na mwanaume wangu, lakini niliposhituka, nikakuta naangaliana macho kwa macho na bonge la nyoka" amesema Iga.
"Kidogo nife kwa hofu" amesema msichana huyo mwenye umri wa miaka 19, akikaririwa na gazeti la Croatian Times. Wataalam wa nyoka walimkamata nyoka huyo, ambaye hata hivyo imeelezwa kuwa sio nyoka hatari na wala hana madhara yoyote.
Msemaji wa polisi amesema nyoka huyo alitoroka kutoka katika duka moja la kuuzia wanyama wa kufuga, na alikuwa akitafuta joto tu.

WEVI WASAHAULIFU

Cr
Usisahau mafuta
Wezi wawili, wanawake hapa Uingereza waliingia katika duka moja na kuiba pombe, lakini wakasahau kuweka mafuta ndani ya gari walilotumia kubebea mali waliyoiba.
Kinamama hao Devlin mwenye miaka 59 na mwenzake Egan mwenye miaka 52 walionekana wakiiba pombe yenye thamani ya karibu dola elfu moja.
Hata hivyo baada ya kufanya wizi huo waliingia katika gari lao na kuondoka lakini hawakufika mbali, kwani gari hilo liliisha mafuta na kuzimika.
Wawili hao walilazimika kulisukuma gari lao hadi kwenye kituo cha mafuta na kununua mafuta na kisha kuondoka, bila kufahamu kuwa kila wanachokifanya kinarekodiwa na kamera maalum za usalama, CCTV. Gazeti la Metro limesema wawili hao wamekiri kufanya wizi katika mahakama ya Manchester.
Pombe walizoiba zilikuwa nyingi kiasi kwamba walipata tabu kufunga buti ya gari.

UZURI

Doctor
Daktari feki alikuwa akimdunga sindano za simenti

Mwanamama mmoja nchini Marekani aliyetaka kuutengeneza mwili wake uwe wa kuvutia zaidi amejikuta matatani, baada ya kudungwa sindani za saruji na gundi ili kuongeza ukubwa wa makalio yake.
Mwanamke huyo ambaye hakutajwa jina kutokana na sababu za kisheria, alikuwa akitaka kufanya kazi katika klabu ya usiku, na hivyo alitafuta daktari anayeweza kumbadilisha, lakini kwa bei nafuu.
Polisi wamesema mwanamke huyo alikutana na mwanamke mwingine aliyejifanya ni daktari, na kuanza kujaza mwili wake kwa saruji, gundi ya kuzibia matairi na mafuta. Msichana huyo alilipa dola mia saba ili kupatiwa hips ba makalio ya kuvutia.
Hata hivyo sindano za mchanganyiko wa saruji, na mafuta na gundi zilimsababishia maumivu makali na akalazimika kwenda hospitali. Kila alipokwenda hospitali kutokana na maumivu alikuwa akiona aibu kusema hasa chanzo cha maumivu yake.
Hata hivyo mama wa msichana huyo alimbana mwanaye hadi akasema kilichomsibu. Polisi walimkamata daktari huyo feki na kumshtaki kwa kosa la kufanya udaktari bila leseni na pia kusababisha maumivu.
Mamlaka za huko zinasema huenda kuna wasichana wengine wengi wamekubwa na jambo hilo lakini wanaona aibu kujitokeza.

DOLA KIBAO

Dollars
Mabunda ya noti

Sanduku moja linalodhaniwa kuwa na dola milioni moja liliachwa katika mgahawa mmoja mjini Sydney Australia na kusababisha tafrani.
Wamiliki wa mgahawa huo, walidhani sanduku hilo ni bomu na hivyo kuliweka nje na kuita polisi. Watu walioshuhudia wamesema waliona polisi wakifungua sanduku hilo kwa tahadhari na kukuta mabunda ya noti za dola za Kimarekani.
Taarifa zinasema inawezekana sanduku hilo liliachwa na awali mtu moja anayedhaniwa kuwa na umri wa miaka thelathini aliyeingia katika mgahawa huo na kuagiza kahawa.
Polisi wamegoma kuthibitisha ni kiasi gani cha fedha kilichokuwemo ndani ya sanduku hilo.

MBEGU ZA WIZI

Pacha
Mapacha kama hawa

Bwana mmoja nchini Marekani amedai kuwa mpenzi wake za zamani amemuibia mbegu zake za kiume, na sasa anakishtaki kituo kimoja cha afya kilichomsadia msichana huyo kupaa uja uzito.
Bwana huyo Joe Pressil amesema aligundua kuhusu mpango huo baada ya kupokea risiti kutoka katika kituo cha afya ikionesha kuwa yeye ni mteja wao, kimeripoti kituo cha TV cha KPRC cha Houston.
Bwana Pressil alishangaa kuona msichana wake alipata uja uzito miezi mitatu baada ya wawili hao kauchana. Bwana huyo amesema msichana huyo miaka yote wakiwa pamoja alikuwa akidai kuwa hawezi kupata uja uzito kutokana na sababu za kiafya.
Msichana huyo hatimaye alijifungua watoto mapacha na kumtaka bwana huyo kulipia gharama za watoto, baada ya vipimo vya damu kuonesha yeye ndio baba.
Bwana huyo amesema sasa anakumbuka kwa nini mpenzi wake huyo alikuwa akisisitiza kwenda kutupa mipira ya kiume kila baada ya wao kukutana.

Na kwa taarifa yako.....

Chakula pekee mende wasichokula ni matango
Tukutane Wiki Ijayo.... Panapo Majaaliwa...

Kabila aapishwa leo Kinshasa


Jeshi la Congo limesambaza vifaru kote jijini Kinshasa kama hatua ya kujiandaa kuapishwa kwa Rais Joseph Kabila kufuatia Uchaguzi wenye utata uliofanywa mwezi uliopita.
Ni viongozi wachache tu wa mataifa ya Afrika wameahidi kuhudhuria; na waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Ubelgiji aliyekuwa amepanga kuhudhuria sherehe hizo amefutilia mbali ziara hiyo.
Ameahidi kuwa huenda akafika nchini humo baada ya matangazo ya uchaguzi wa Bunge kutangazwa katika mazingira yaliyo bora zaidi.
Wachunguzi wa nchini na wa kimataifa wameshutumu ukiukaji mkubwa wa utaratibu wa upigaji kura katika uchaguzi wa Urais na Bunge uliofanywa Novemba 28; tayari kiongozi mkuu wa upinzani Etienne Tshisekedi amejitangaza kuwa Rais baada ya kukataa kukubali matokeo.
Tshisekedi alisema Jumamosi kuwa atajiapisha mwenyewe kuwa Rais baadaye juma hili katika uwanja mkuu wa michezo jijini Kinshasa. Kiongozi huyo wa upinzani pia alitoa wito kwa vikosi vya usalama viheshimu amri yake badala ya Rais Kabila, ambaye alisema amevunja Serikali yake. Upande wa Rais Kabila umetaja matamshi ya Tshisekedi kama ya uhaini.

Friday, December 2, 2011

RC Kandoro: Ni shetani tu, sina mkono katika vurugu zile

Fujo za machinga Mbeya
 
Felix Mwakyembe
Mbeya
MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro
MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro

MKUU wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, amevunja ukimya kuhusu vurugu za Mwanjelwa na kuweka wazi msimamo wake juu ya suala la wafanyabiashara ndogo ndogo, maarufu kama machinga.
Hatua hiyo ya Kandoro ni majibu dhidi ya shutuma mbalimbali ambazo zimekuwa zikielekezwa kwake kila kunapotokea vurugu za machinga katika mikoa aliyopata kuiongoza, ambayo ni Mwanza, Dar es Salaam na sasa Mbeya.
Akizungumza na viongozi wa madhehebu ya dini ya kikristo jijini Mbeya juma lililopita, Kandoro alisema; “Sijawahi kumwagiza mtu yeyote achukue hatua zilizosababisha ghasia zile. Unapofika mahali unachukua muda kusoma mazingira, nawahakikishia, sina mkono katika vurugu zile, ni shetani tu.”
Pamoja na kukanusha kuhusika na ghasia hizo, Kandoro alibainisha kwamba ni wajibu wao kama viongozi, kukubali changamoto kutoka kwa wananchi ambao kwa sasa kiwango cha uelewa miongoni mwao ni kikubwa.
Pamoja na ukweli kwamba vurugu hizo zilitokea akiwa ndio kwanza anajitambulisha kwenye wilaya na taasisi mbalimbali mkoani humo, mkuu huyo wa mkoa amekuwa akitajwa kutoa maagizo ya hatua za kuchukua. Ni maagizo hayo ndiyo yanayotajwa kuwa chanzo cha vurugu kubwa zaidi.
Wakati ghasia za Mwanjelwa zinatokea Kandoro alikuwa Kamsamba wilayani Mbozi katika ziara zake za kujitambulisha, hata hivyo alilazimika kukatisha ziara yake hiyo na kurudi jijini Mbeya saa kumi alasiri.
Taarifa za awali zilielezea kiini cha ghasia hizo kuwa ni hatua ya askari wa Jiji la Mbeya kuwaondoa kwa nguvu wafanyabiashara hao kwenye barabara inayoingia Kituo cha Afya cha Mwanjelwa na kwenye barabara za pembeni zilizopo eneo hilo.
Hata hivyo, mambo kadhaa yalibainika kujificha nyuma ya ghasia hizo ikiwemo wafanyabiashara wenye maduka wanaodaiwa kuwatumia machinga hao kuwauzia bidhaa zao, na kwa hiyo, kitendo cha kuwaondoa kilionekana kuathiri zaidi biashara zao.
Pamoja ushiriki wa wafanyabiashara hao kuthibitishwa na machinga wenyewe, lakini mazingira pia yanadhihirisha madai hayo, hii ni pamoja na machinga hao kupanga biashara zao kwenye mitaa yenye maduka ya nguo, masanduku ambayo ndio bidhaa maarufu za machinga walioko kwenye mitaa hiyo huku ile yenye maduka ya vifaa vya ujenzi hapo hapo Mwanjelwa ikiwa wazi bila machinga hata mmoja.
CCM lawamani
Mbali ya madai ya wafanyabiashara kuchochea ghasia hizo, baadhi ya viongozi wa Chama cha Mapinduzi katika Jiji la Mbeya wameshutumiwa kuchochea hasira ya vijana jijini humo kutokana na tabia yao ya kuendekeza siasa za chuki, ubabe na vitisho dhidi ya wale wote wanaoonekana kupingana na chama hicho.
Miongoni mwa wanaotupiwa lawama hizo ni kigogo mmoja wa CCM ndani ya uongozi wa jiji hilo anayedaiwa kuvunja sheria alizoshiriki kuzitunga, akidaiwa kuwashawishi vijana kujiunga na chama hicho ili waachiwe kuendelea na shughuli zao.
Ofisa Afya mmoja wa jiji hilo, jina linahifadhiwa, aliliambia Raia Mwema kwamba kigogo huyo huwaeleza vijana wanaoondolewa kwenye maeneo yaliyozuiliwa kuendesha baadhi ya shughuli kama vile uoshaji magari na biashara ndogo ndogo, kuwa wanaondolewa kwa sababu ya kuunga mkono CHADEMA, hivyo ili awaruhusu inabidi wajiunge na CCM.
“Vijana wa pale kwenye car wash za Mafiati, kwa Karumuna, Iyunga na Ujenzi tulikubaliana nao watafute maeneo mengine yanayofaa kwa kazi yao, jiji liwajengee miundombinu ya sehemu ya kuoshea magari, walikubali na wakaondoka, wakati wa uchaguzi mdogo wa udiwani Nzovwe na Majengo wakarudi, tena wakiwa wamepandisha bendera za CCM, tunawauliza wanasema wameruhusiwa na kiongozi mmoja wa kisiasa katika Halmashauri ya Jiji la Mbeya, amewaambia waliondolewa kwa sababu ni CHADEMA, wakitaka kurudi wachukue kadi za CCM, vijana wakachukua kadi na kupandisha bendera,” anasema ofisa afya huyo.
Hatua ya watunga sheria wa jiji hilo na madiwani, kuwazunguka watendaji wanapotekeleza uamuzi uliofikiwa kwa pamoja ni kati ya sababu za kuzingirwa kwa askari wa jiji hilo waliofika Mwanjelewa kusimamia eneo la barabara hiyo kutovamiwa tena na machinga, ambapo ikawa sababu ya kuanzisha ghasia.
Kwa mujibu wa ofisa afya huyo wale vijana waosha magari walifikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake, hivyo kuchochea zaidi hasira miongoni mwa vijana hao kwani walibaini kuchuuzwa na mwanasiasa huyo.
Mtazamo wa viongozi dini
Viongozi wa madhehebu ya dini ya kikristo wamechambua sababu zaidi kuhusu ghasia hizo, ambazo ni pamoja na mfumuko wa bei ambao umesababisha maisha kuwa ghali zaidi kiasi cha wananchi walio wengi kushindwa kuyamudu.
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Israel Mwakyolile alizitaja sababu nyingi kuwa ni pamoja na kufa kwa viwanda vya nguo (Mbeya Textile), Zana za Kilimo (ZZK) na kiwanda cha sabuni cha Hisop, ambavyo alisema kwa kiasi kikubwa vilikuwa vikichangia kutoa ajira kwa vijana.
Askofu Mwakyolile anasema pamoja na kuwepo kwa rasilimali ardhi na watu, bado kilimo hakiwavutii vijana kutokana na bei duni za mazao ya kilimo, hali inayosababisha vijana wengi wajihusishe na umachinga na baadhi yao hata kufanya vitendo vya uhalifu.
Viongozi hao wamezidi kulia na hatua ya serikali kuyauza mashamba ya Kapunga na Mbarali kwa wawekezaji ambapo wanatoa mfano wa Kapunga wakisema wakati likilimwa na wakulima wadogo lilizalisha zaidi na uchumi kusambaa kwa wananchi walio wengi zaidi.
Wanasema hali ni tofauti sana na hivi sasa ambapo uzalishaji umeshuka na kwamba mwekezaji anadaiwa na baadhi ya wakazi mkoani hapa kuwageuza wananchi manamba wake kwa kuwakodisha mashamba huku yeye akikusanya mapato tu.
Kandoro na machinga
Baada ya ghasia hizo za Mwanjelwa, sasa ni dhahiri kwamba ule mkakati ulioandaliwa tangu mwishoni mwa mwaka jana kuboresha mazingira ya wafanyabiashara ndogo ndogo jijini humo utatekelezwa muda si mrefu kuanzia sasa.
Matumani hayo yalitolewa na Mkuu wa Mkoa huo siku hiyo aliyozungumza na baadhi ya viongozi wa madhehebu ya dini ya kikristo, ambapo katika maelezo yake alibanisha kwamba machinga wapo hata katika mataifa yaliyoendelea hivyo ni suala lisilokwepeka.
“Jiji linajiandaa kuanzisha utaratibu wa kufunga baadhi ya barabara katika muda maalumu ambapo linakuwa eneo la biashara kwa wakati huo, ni utaratibu unaotumika hata na mataifa makubwa kama Marekani, utake usitake machinga ni sehemu ya jamii, unawatoa waende wapi na tukumbuke kuwa wataongezeka,” anasema Kandoro.
Pamoja na utaratibu huo, Kandoro anasema soko jipya la Mwanjelwa linalojengwa hivi sasa litakuwa na mchanganyiko wa wafanyabishara wakubwa, wa kati na wadogo na ni kwa bidhaa zote.
Kwa mujibu wa Kandoro, kipaumbele watapewa wafanyabiashara wale waliokuwepo kabla ya soko hilo kuungua.
Kauli kuhusu Soko la Mwanjelwa ilikuja kutokana na ombi la viongozi hao wa  madhehebu ya dini ya kikristo la kujengwa soko maalumu kwa ajili ya machinga.
Pamoja na Mwanjelwa Jiji la Mbeya liko katika maandalizi ya kujenga soko jingine la kisasa katika eneo lilipokuwepo soko kuu ambalo liliteketea kwa moto Desemba mwaka jana.
Ghasia za machinga wa Mwanjelwa jijini Mbeya zimesababisha hasara kubwa mkoani humo ikiwemo maisha ya watu wasio na hatia, mali, miundombinu hususani barabara kuu iendayo nchi jirani ya Zambia inayopita eneo hilo ambapo imeungua na kuchimbika na kusimama kwa shughuli mbali mbali zikiwemo biashara kwa muda wa siku mbili mfululizo.

Wafugaji watishia mgomo kuuza mifugo nchi ikose nyama

Muswada Katiba mpya
 
Paul Sarwatt
Arusha
Jamii ya wafugaji Tanzania

WAKATI Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, akitarajiwa kutia saini au la Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba kuashiria mwanzo wa mchakato wa kuandika Katiba mpya, baadhi ya wadau wameendelea kupinga Bunge kupitisha muswada huo.
Miongoni mwa wadau wa hivi karibuni kupinga muswada huo ni pamoja na baadhi ya mashirika yasiyo ya kiserikali, likiwamo Shirika la PINGOs Forum, ambalo wiki iliyopita iliandaa mdahalo wa siku mbili uliobeba maudhui ya miaka  50 ya Uhuru na changamoto ya mabadiliko ya Katiba kwa jamii za wafugaji, warina asali, waokota matunda na wakulima.
Shirika hilo lenye makao yake mjini Arusha lilifanya mdahalo huo kwa kushirikiana na shirika jingine la ALAPA (Association for, and Advocacy for Pastoralist) na uliwahusisha wadau kutoka jamii za wafugaji, wakusanya matunda, warina asali na wakulima.
Katika mdahalo huo wadau hao walipata fursa ya kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu haki watu wa jamii ya wafugaji, warina asali, wawindaji na wakusanya matunda pamoja na wakulima katika Katiba ya sasa na pia katika Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Moja wa wadau hao ni Kijolu Kakiya, mkazi wa kijiji cha Piayaya wilayani Ngorongoro ambaye alieleza kuwa Katiba  inayotumika sasa imewatenga watu wa jamii ya wafugaji hasa katika masuala ya umiliki wa ardhi kutokana na tabia ya Serikali kumega ardhi ya wafugaji kwa matumizi mengine.
Matumizi hayo yametajwa kuwa ni pamoja na uwekezaji bila ya kuwashirikisha au kuwapatia wafugaji hao ardhi mbadala.
“Kila mmoja wetu hapa ni shahidi wa matendo ya uporaji ardhi uliofanywa na Serikali katika maeneo mbalimbali ya wafugaji nchini mwetu, tumefukuzwa kama wahamiaji kutoka nchi nyingine bila ya kupewa hata nafasi ya kusikilizwa na hali hii haikubaliki,” alisema.
“Mimi nina watoto saba na wote hao wananitegemea kuwasomesha na mahitaji mengine ya kimaisha sasa nakosa nguvu za kiuchumi kuwasomesha kwa sababu  mifugo ambayo ndiyo njia kuu ya kujipatia kipato, imekufa kutokana na ukame uliotokea mwaka juzi  hivyo sina namna nyingine. Ni kama nimegeuka kuwa omba omba,” alieleza kwa masikitiko.
Mama huyo alieleza kuwa wakati wa ukame ukishika kasi katika Wilaya ya Ngorongoro, Serikali iliwazuia kuingiza mifugo yao katika eneo la pori tengefu la Loliondo ambalo liko chini ya kampuni ya Orttello Business Cooperation (OBC), inayofanya shughuli za uwindaji wa kitalii katika pori hilo na viongozi wa Serikali walijenga hoja kuwa wafugaji wangemsumbua mwekezaji.
“Matokeo ya uamuzi huo wa Serikali ni kufa kwa maelfu ya mifugo kutokana na ukosefu wa malisho, Serikali imesahau kuwa pori hilo tengefu ni eneo la wafugaji wa kimasai ambao wameishi hapo kwa miaka mingi,” alisema.
Alipendekeza kuwa iwapo  Rais Kikwete ataendelea na mipango yake ya kusaini muswada wa sasa kuhusu mchakato wa Katiba mpya na kupuuza maoni ya baadhi ya wananchi, jamii ya wafugaji inaweza kususia kuuza aina zote za mifugo kwa mwezi mzima kama njia ya kutaka kuishinikiza serikali iwasikilize.
“Tutafanya kampeni  nchi nzima kususuia uuzaji wa mifugo ya aina zote kama njia ya kufikisha ujumbe kwa Rais na Serikali yake kuwa hatujafurahishwa na hatua yake na tuone kama Serikali ina uwezo wa kuagiza nyama kutoka nje kuwalishwa watu wake,” alisema.
Kwa upande wake, mfugaji mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Kooya Timman, mkazi wa Kijiji cha Ololosokwan, wilayani Ngorongoro anasema; “Wafugaji wana tofauti kidogo na watu wa jamii nyingine kwa hiyo, waangalie Katiba ya zamani na watathmini masuala ambayo hayakuainishwa katika Katiba hiyo. Haki za msingi za kijamii kama elimu, afya na maji ziangaliwe katika Katiba hiyo mpya.”
Mkazi wa Kijiji cha Endulen, wilayani Ngorongoro, Noolosho Nakuta, naye aliunaga na wenzake akieleza kushangazwa kwake na kitendo cha Serikali kutotambua uwepo wao ndani ya eneo la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Analalamika kuwa Serikali kupitia mamlaka hiyo wamewanyima hata maeneo ya kwa ajili ya uanzishaji miradi ya kijamii, kama zahanati na shule.
Anasema; “Wakati wananchi wanabanwa katika hilo, wawekezaji wanapewa vibali vya kujenga majengo makubwa kama hoteli za kitalii ambayo yamekuwa chanzo uharibifu wa mazingira na mfumo wa asili wa maisha ya viumbe na wanyama katika  kreta ya Ngorongoro.”
Awali, akizungumza  katika   mdahalo huo  Rais wa  Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Fransis Stolla,   alisema watachukua hatua za kisheria kwa kuifikisha Serikali mahakamani kupinga Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, iwapo Rais Kikwete atausaini tayari kuanaza kutumika kama sheria rasmi.
“Tunamwomba Raia Kikwete atumie hekima yake  kwa kuurejesha upya muswada huo bungeni ili usomwe kwa mara ya kwanza na wananchi wapewe fursa pana zaidi ya kuujadili kwa kina,” alisema Stolla.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa asasi binafsi ya Jukwaa la Taifa la Katiba, Deus Kimbamba, alisema hawakubaliani na muswada huo wa mabadiliko ya Katiba mpya kwa kuwa umejaa upungufu mwingi kuliko hata Katiba ya sasa.
“Tunapoulalamikia muswada huo si kwamba tunataka kujifurahisha, tunaupinga kwa sababu hata jina lenyewe limekosewa na vipengele vingi havijazingatia mahitaji ya kweli ya Katiba mpya kwa jamii ya Watanzania,” alisema
Alitaja miongoni mwa kasoro hizo kuwa ni pamoja na muswada kuwa na kipengele kinachowanyima haki watu wasio wajumbe wa tume ya Katiba kuaandaa mikutano au majumuiko kwa lengo la kujadili, kutoa au kukusanya maoni au mapendekezo yao kuhusu Katiba mpya.
Alisema kifungu hicho kinaweka wazi kwamba anayepatikana na kosa la kuzuia tume ya kukusanya maoni ya Katiba mpya kufanya kazi yake atahukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au faini isiyozidi milioni 15 au vyote kwa pamoja.
“Hii maana yake ni kwamba kunzia tarehe moja Desemba mwaka huu  kama Rais atakuwa amesaini muswada huo basi tunaojadili masuala ya Katiba mpya hapa tumevunja sheria na tunapswa kufikishwa mahakamani na kwa tafsiri nyingine ni kwamba, magereza yetu ambayo tayari yamesheheni watuhumiwa na wafungwa yatafurika zaidi,” alisema Kibamba.
Mwenyekiti wa mkutano huo, Elfuraha Laltaika, ambaye  pia ni Mhadhiri wa Kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Tumani, tawi la Makumira, alisema malengo na maudhui ya mdahalo huo ni kufanya tathmini na marejeo kuhusu haki ya ardhi kwa jamii za wafugaji na wakusanya matunda, katika kipindi cha miaka 50 ya Uhuru na pia nafasi yao katika Katiba mpya itakayotungwa sasa.

CHADEMA njia panda kisiasa

Mabadiliko ya Katiba
 
Waandishi Wetu
Freeman Mbowe na Dr. Slaa
Freeman Mbowe na Dr. Slaa

MAKUBALIANO kati ya Serikali na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuhusu Sheria ya Mabadiliko ya Katiba inayosubiri idhini ya Rais Jakaya Kikwete, yamekiweka chama hicho njia panda kisiasa, Raia Mwema, imebaini.
Hakuna muda rasmi ulioafikiwa wa utekelezaji wa makubaliano hayo kati ya Serikali na CHADEMA kuhusu muswada huo, ambao tayari Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limekwishaupitisha na hivyo, kumaliza kazi yake kwa mujibu wa Katiba iliyopo sasa.
Kaimu Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika akiwakilisha upande wa chama hicho walitiliana saini na Serikali ikiwakilishwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Emmanuel Nchimbi. Katika makubaliano hayo, wameahidi kuendelea kuuboresha Muswada huo wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011, ili kukidhi mahitaji ya kuaminiana na mwafaka wa kitaifa.
Makubaliano hayo pia yanataka kuwashirikisha wadau wengine katika kuboresha sheria hiyo, uamuzi ambao unatajwa kuunga mkono ule ushauri uliotolewa na Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi, ambao hata hivyo ulitaka tu kushirikisha vyama vya siasa vyenye wabunge tu.
CHADEMA awali walipinga uamuzi wa kuwashirikisha katika mazungumzo ya pamoja kati yao na Rais na vyama vingine vyenye wabunge katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa kwa sasa CHADEMA kipo njia panda kisiasa ingawa msimamo wake kuhusu mchakato wa Katiba kuwashirikisha wananchi wengi unaweza kubaki kama awali.
Harakati za kisiasa za CHADEMA mwenendo wake sasa unategemea zaidi utekelezaji wa makubaliano hayo ambayo pia yanategemea namna Ikulu itakavyoshughulikia.
“Inawezekana kabisa Rais anaweza kutia saini muswada huo ili uwe sheria lakini katika uamuzi huo anaweza kutekeleza matakwa ya makubaliano hayo wakati wa maandalizi ya kanuni ambazo hutungwa na Baraza la Mawaziri kwa kumshirikisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
“Lakini katika makubaliano yale tumeona kinachopaswa kufanyiwa mabadiliko ni sheria na si muswada. Kwa hiyo kwa lugha nyingine, CHADEMA wamekubali Rais asaini muswada lakini mara utakapokuwa sheria basi ifikishwe bungeni kwa ajili ya mabadiliko,” alisema mmoja wa wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hata hivyo, hatua hiyo ya CHADEMA sasa imeanza kutofautiana na ile ya NCCR-Mageuzi ambao wabunge wake waliungana na wabunge wa CHADEMA kususia muswada huo, baadhi wakisusia hata mjadala na wengine wakishiriki mjadala lakini wakisusia upitishaji wake.
Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, tayari amenukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema; “Tulitoka nje ya Bunge ili kupinga muswada na si kutafuta njia ya kwenda kumwona Rais Ikulu. Hoja yetu ilikuwa wananchi hawajashirikishwa na bado hoja hiyo imebaki hivyo.”
Kafulila anaungwa mkono na Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia, ambao kwa pamoja wanataka muswada huo urudishwe bungeni na kusomwa kwa mara ya kwanza.
Katika muswada huo, kati ya mambo yanayolalamikiwa ni pamoja na wananchi kutoshirikishwa kikamilifu katika kutoa maoni yao kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kaitba na Sheria, malalamiko ambayo hata hivyo, yamepingwa na uongozi wa Bunge, kupitia kwa Katibu wake, Dk. Thomas Kashilila.
Katika maelezo yake kwa vyombo vya habari ambayo pia yamechapishwa katika gazeti hili kurasa za 16 na 17, Dk. Kashilila anathibitisha kuwa muswada huo umefuata hatua zote, kinyume cha malalamiko yanayoelekezwa kwa Bunge kama taasisi.
Kikao kati ya Kikwete na CHADEMA kimeelezwa kuwa ni muendelezo wa mazungumzo ya chini kwa chini ya kidiplomasia yaliyokuwa yakifanywa na viongozi wastaafu na wanataaluma mbalimbali, ambao walionekana kutaka suluhu ya kisiasa kwa maslahi ya Taifa zaidi badala ya muelekeo wa awali uliokua umejikita kwenye siasa za vyama.
Mawaziri Wakuu Wastaafu, Dk. Salim Ahmed Salim na Joseph Warioba, ambao ni wana CCM, waliripotiwa kufanya juhudi binafsi za kufanya mazungumzo na wanasiasa wa CHADEMA kuhusiana na suala la mjadala wa katiba, mazungumzo ambayo hayajawahi kurasimishwa, kabla ya kikao rasmi cha Kikwete na CHADEMA.
Tayari kumekuwa na wasiwasi kutoka kwa baadhi ya wafuasi wa CCM na CHADEMA kuhusu mazungumzo kati ya Kikwete na CHADEMA, kila mmoja ukihofia hatima ya mazungumzo hayo itakua nini na kwa maslahi ya nani kisiasa, hofu ambayo imeyakumba pia makundi mengine ya kijamii, ambayo hayakushirikishwa.