Thursday, June 14, 2012

Dk Mwakyembe awasha moto TRL


BAADA ya kusafiri kwa treni kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amebaini hujuma nzito katika Shirika la Reli Tanzania (TRL) ikiwamo ofisa mmoja kuwaibia abiria kwa kughushi viwango vya nauli na ameagiza afukuzwe kazi.

Licha ya kuagiza kutimuliwa kwa ofisa huyo, pia alitangaza kuandaliwa utaratibu wa kufanya mabadiliko kadhaa katika kuboresha usafiri huo, ikiwamo kuondoa malipo ya nusu nauli kwa watoto wadogo kuanzia miaka mitatu hadi miaka 10 na pia kuondolewa kwa utaratibu wa malipo ya mizigo midogo ya abiria.

Juzi, Dk Mwakyembe ambaye tayari amewang’oa vigogo wanne wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), aliamua kusafiri kwa treni hadi Dodoma akitokea Dar es Salaam ili kujionea utendaji kazi wa shirika hilo.

Mara baada ya kuwasili katika Stesheni ya Dodoma saa 1:30 asubuhi, Waziri Mwakyembe alizungumza na waandishi wa habari na kusema akiwa katika safari hiyo, amepata fursa za kutembelea mabehewa yote na kuzungumza na abiria.

Dk Mwayembe alisema ingawa safari ilikuwa nzuri, kuna mengi ambayo ameyabaini ambayo ni pamoja na abiria kulipa nauli kubwa na kuandikiwa tiketi tofauti jambo ambalo alisema ni wizi na kamwe wizara yake haiwezi kulifumbia macho.

“Unakuta nauli halali ni Sh9,000 lakini, abiria ameandikiwa Sh29,000. Sasa nimeagiza huyu anayehusika afuatiliwe na kujulikana na nipewe taarifa ameondolewa,” aliagiza Dk Mwakyembe.
Alisema pia katika safari hiyo, alibaini uchakavu mkubwa wa mabehewa na hakuna tofauti ya daraja la tatu na la kwanza, upungufu mwingine ni katika utendaji na taratibu jambo ambalo linapaswa kuchukuliwa hatua.

Dk Mwakyembe alisema si vyema mtoto kuanzia miaka mitatu kulipishwa nusu nauli, kwani taratibu zinapaswa kufanywa ili hadi mtoto wa miaka 10 ikiwezekana asilipishwe nauli kwani treni ndiyo usafiri wa umma.

Kuhusu mizigo, alisema kwa sasa mizigo ya abiria inalipiwa kwa kilo kama ilivyo usafiri wa ndege jambo ambalo si sawa kwani mzigo wa abiria kuanzia kilo 20 unalipishwa jambo ambalo linapaswa kuangaliwa.

“Usafiri huu mimi nasema ndiyo wa umma hivyo, tusizuie watu kupeleka hata zawadi nyumbani kwao ni vyema tuwe na utaratibu walau mizigo kidogo ya abiria isilipiwe,” alisema Dk Mwakyembe.

Safari tatu kwa wiki
Akizungumzia tatizo la ratiba za usafiri, Dk Mwakyembe alisema mipango inafanywa ili kufikia Desemba, mwaka huu walau kuwe na safari tatu za kutoka Dar es Salaam hadi  Kigoma na Tabora na kuondoa kero zilizopo sasa.

Waziri huyo alisema anaamini safari hizo zikirejea, zitapunguza wingi wa abiria na msongamano wa watu kwenye treni na pia zitasaidia kuanza kwa usafirishaji wa mizigo kwa kutumia usafiri huo.
“Tutawaomba wabunge wapitishe bajeti yetu na wapande treni ili kuona usafiri huu, nina amani tukiondoa upungufu kidogo, huu utakuwa usafiri mzuri sana,” alisema.

Hujuma
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk Charles Tzeba ambaye allimpokea Dk Mwakyembe alisema licha ya kuwepo hujuma katika nauli za abiria, pia wamebaini hujuma kubwa katika mizigo inayosafirishwa kwa reli katika mashirika yote ya TRC na Shirika la Tanzania na Zambia (Tazara).

Alisema maofisa wasio waadilifu wa mashirika hayo, wamekuwa wakisafirisha mizigo mingi lakini inayoandikiwa na kulipwa serikalini ni ile yenye uzito mdogo.

“Utakuta mzigo wa tani 40 hadi 60 unaandikiwa tani 10 au 20 fedha nyingine zinaingia mifukoni mwa wajanja, hatutakubali jambo hili,” alisema Dk Tzeba
Alisema yeye na waziri wake, pamoja na maofisa wengine, watakuwa wakisafiri kwa kushtukiza kwa reli mara kwa mara ili kubaini hujuma zote na kuwachukulia hatua wahusika mara moja.
“Mimi nilikuja hapa Dodoma kwa kiberenge na baadhi ya wabunge wa kamati ya miundombinu na leo amekuja waziri kwa treni hii haitakuwa mara yetu ya kwanza, tutasafiri sana kwa reli ili kubaini hujuma zilizopo,” alisema Dk Tzeba.

Zanzibar yaongeza kodi ya mafuta, bandari


SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) imetangaza Bajeti yake kwa mwaka 2012/13 ambayo pamoja na mambo mengine, imeongeza kodi katika maeneo manane ikiwamo mafuta, ada ya bandari na ushuru wa stempu huku ikiwa na maeneo sita ya kipaumbele.

Maeneo hayo ya vipaumbele ni afya, ajira kwa vijana, ustawi wa wazee, elimu, kuimarisha uchumi na kuhifadhi mazingira ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

SMZ katika bajeti yake hiyo, imepanga kutumia Sh307.8 bilioni kwa kazi za kawaida na Sh341.1bilioni kwa ajili ya shughuli za maendeleo huku makusanyo yakitarajiwa kuwa 648.9 bilioni.

Akiwasilisha Bajeti hiyo jana kwenye Baraza la Wawakilishi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Fedha Uchumi na Mipango ya Maendeleo), Omar Yussuf Mzee alisema kwa kuzingatia dhamira ya Serikali katika kukuza mpango wa maendeleo, imependekeza marekebisho ya viwango vya tozo ya kodi.

Mzee alitaja mabadiliko hayo kwamba yamegusa  Sheria ya Ushuru wa Stempu namba 6 ya mwaka 1996, Sheria ya Kodi za Hoteli namba 1 ya mwaka 1995, Sheria ya Ada za Bandari namba 2 ya mwaka 1999 na Sheria ya Ushuru wa Petroli namba 7 ya mwaka 2001.

Sheria nyingine ni ile ya Usimamizi na Utaratibu wa kodi namba 7 ya mwaka 2009, Sheria ya kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) namba 4 ya mwaka 1998, Sheria ya Bodi ya Mapato Zanzibar namba 7 ya mwaka 1996 na Sheria ya Mafunzo ya Amali namba 8, ya mwaka 2006.

Waziri huyo alisema kutokana na mabadiliko hayo, ada ya bandari imependekezwa kuongezwa kutoka Sh1,000 ya sasa hadi Sh2,000 kwa abiria wanaosafiri kati ya Zanzibar na Tanzania bara.
Mzee alisema abiria wanaosafiri kati ya Unguja na Pemba watatozwa Sh1,000.

Eneo jingine ni kuongeza ushuru wa mafuta kwa Sh50 kwa lita inayoingia visiwani humo kwa mafuta ya petroli na dizeli tu, hatua ambayo alisema inatarajiwa kuiingizia SMZ mapato ya Sh3.3bilioni.
Akizungumzia ongezeko la ushuru wa stempu, waziri huyo alisema Serikali inapendekeza kuongeza kutoka asilimia moja na nusu ya sasa hadi asilimia tatu, hatua ambayo itaongeza mapato kwa Serikali ya Sh2.10 bilioni.

Waziri Mzee alitaja eneo jingine ambalo limefanyiwa marekebisho kwamba ni Sheria ya Usafiri Barabarani, ambako Serikali imependekeza kurekebisha kiwango cha leseni za njia ili kiendane na uzito gari au ukubwa wa injini yake.

Alisema kiwango cha sasa cha ada ya leseni ya njia Sh24,000 kwa gari kwa mwaka, hakizingatii matumizi ya njia tofauti za gari.

Waziri huyo alisema kutokana hali hiyo, Serikali inapendekeza tozo la Sh15,000 kwa kila gari kwa mwaka na Sh3,000 kwa chombo cha moto cha magurudumu mawili au matatu.
Alisema hiyo inatokana na ongezeko la idadi ya magari nchini kila mwaka na hivyo, kuathiri mazingira kutokana na moshi unaotokana na magari hayo.

Marekebisho mengine ni yale ya viwango vya ada za huduma mbalimbali zinazotolewa na Serikali na taasisi zake baada ya kubainika kuwa zimepitwa na wakati.

Waziri huyo alisema katika mwaka wa fedha, Serikali inakusudia kufanya marekebisho kiwango cha kodi huduma za mahoteli, migahawa na kutembeza wageni.

Alisema Serikali imependekeza kuongeza kiwango cha kodi kwa hoteli, migahawa na watembeza wageni wasiosajiliwa VAT kutoka asilimia 15 ya sasa hadi asilimia 18.

Ukuaji uchumi
Kuhusu ukuaji wa uchumi, Mzee alisema uchumi wa Zanzibar unatarajiwa kukuwa kwa asilimia 7.5 kutoka  asilimia 6.8 mwaka 2011.

Alisema mfumuko wa bei unatarajiwa kushuka hadi kufikia asilimia 8.7 kwa mwaka huo wa 2012  ukilinganishwa na mwaka jana, ambao ulikuwa ni asilimia 14.7.

Alisema uchumi wa Zanzibar kwa mwaka huu unatarajiwa kuimarika zaidi kutokana na mipango mbalimbali ya Serikali katika ukusanyaji wa mapato, kutoka vyanzo mbalimbali.

Kishindo cha bajeti leo


SERIKALI, KAMATI YA BUNGE WAELEWANA, ZITTO ASEMA NI BAJETI YA KULIPA MADENI, MAMA LISHE WATAKA MFUMUKO WA BEI USHUKE, WALIA MAISHA
Waandishi Wetu
LEO ni siku ya Bajeti kwa mwaka wa fedha 2012/13. Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa anatarajiwa kuanza kusoma Bajeti ya Serikali inayosubiriwa kwa hamu na mamilioni ya Wananchi 10.00 jioni.
Hotuba ya Dk Mgimwa itatanguliwa na ile ya Mipango ya Serikali itakayosomwa asubuhi mara baada ya kipindi cha Maswali na Majibu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira.

Kutwa nzima ya jana, Dk Mgimwa na watendaji wengine wa Wizara ya Fedha walikuwa katika pilikapilika za kukamilisha maandalizi ya bajeti hiyo ya Sh15 trilioni, ambayo inatarajiwa kuwa na vipaumbele saba.

Baada ya kipindi cha maswali na majibu jana, Kamati ya Uongozi ya Wabunge wa CCM, ilikutana chini ya uenyekiti wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kufanya maandalizi ya kuwapa taarifa ya bajeti hiyo wabunge wakewaliotarajiwa kukutana kuanzia saa 10 jioni.
Kikao hicho ambacho kiliendelea hadi saa tisa alasiri, pia kilihudhuriwa na Dk Mgimwa na Manaibu wake, Janeth Mbene na Saada Mkuya Salum ambao kama alivyo waziri wao, nao wote ni wapya katika wizara hiyo.

Dk Mgimwa alisema jana kwamba maandalizi ya bajeti yalikuwa yamekamilika na tayari Serikali ilikuwa imefikia mwafaka na Kamati ya Bunge ya Fedha na Uchumi inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM), Andrew Chenge.

“Hoja za wajumbe wa Kamati ya Bunge ni kwamba Serikali iongeze Bajeti ya Maendeleo kutoka asilimia 30 hadi 35 na Bajeti ya matumizi ya kawaida ishuke kutoka asilimia 70 hadi 65, lakini tumejaribu kufanya mapitio ya pamoja imeshindikana,” alisema Dk Mgimwa na kuongeza:

“Hata hivyo, tumekubaliana kwamba kuanzia mwaka ujao wa fedha tuanze kujipanga mapema ili tuweze kufikia lengo hilo na hata ikiwezekana tuvuke hapo.”

Kwa upande wake, Chenge alisema: “Tumewasikiliza na mazingira ndiyo hayo sasa katika hatua hiyo unafanyaje? Lakini hata wao (Serikali) wameanza kuona umuhimu wa hoja yetu kwa hiyo tumeelewana nao kwamba katika bajeti ijayo ambayo nayo haiko mbali, basi wazingatie mapendekezo ya wabunge.”
Hata hivyo, Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe alisema Bajeti hiyo ya Serikali haitoi matumaini kwa Watanzania kwani itakuwa ni kwa ajili ya kulipa madeni.

“Hii yaweza kuwa Bajeti ya kulipa madeni zaidi kuliko ya kuchochea maendeleo.... yaweza pia kuwa ni Bajeti ya kukopa maana jumla ya Sh 5.1 trilioni (Dola za Marekani 3.19 bilioni), zitachukuliwa kama mikopo kwa Serikali. Mikopo ya kibiashara ambayo ni mikopo ghali sana itachukuliwa kwa wingi zaidi kuliko mwaka wa fedha uliopita.”

Hofu ya kukwama
Awali, kulikuwa na hofu kwamba bajeti hiyo ingekwama kutokana na wabunge kusisitiza kuongezwa kwa fedha maendeleo.

Hata hivyo, wabunge kupitia Kamati ya Fedha ya Uchumi walilegeza msimamo wao kutokana na maombi ya Waziri Mgimwa na Waziri Mkuu, Pinda ambao kwa nyakati tofauti, walinukuliwa katika vikao vya kujadili bajeti hiyo wakiwaomba wabunge wasiwabane kwani watendaji wa wizara hiyo walikuwa ni wapya.

Lakini kuna taarifa kwamba hata sura ya sasa ya bajeti hiyo inatokana na Dk Mgimwa kuifumua katika baadhi ya maeneo baada ya kuingia ofisini kutokana na mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanywa mapema mwezi uliopita na Rais Jakaya Kikwete na kumweka nje aliyekuwa akiongoza wizara hiyo, Mustafa Mkulo.

Pinda alinukuliwa akizungumza katika kikao cha kutoa mwongozo kwa wabunge wote (briefing) kwamba, Dk Mgimwa aliomba ridhaa ya Rais kufumua bajeti hiyo upya ili iweze kwenda sawa na mtizamo wake kama kiongozi wa wizara, hali iliyosababisha kuchelewa kwa vitabu vya bajeti kwani baadhi viliandaliwa upya.

Hata hivyo, baadhi ya wabunge wakiwamo wa CCM walisema kwa nyakati tofauti kwamba wanaiona Serikali kutokuwa na usikivu kwani mapendekezo yao kila mwaka yamekuwa hayatekelezwi.
“Ni yale yale tu, kweli Dk Mgimwa ni mpya kwenye Wizara lakini hata angekuwa Mkulo hakuna kinachotekelezwa, kila siku wanaahidi halafu hawatekelezi.” alihoji mmoja wa wabunge wa CCM jana.
Hata hivyo, wabunge wa CCM hawawezi kuzuia Bajeti Kuu ya Serikali kutokana na kubanwa na kanuni za chama hicho, lakini huenda hasira zao zikaziangukia bajeti za wizara na kuwaweka mawaziri katika wakati mgumu.

Uchambuzi wa Zitto
Uchambuzi wa Zitto unaweka wazi kwamba vitabu vya Bajeti vinaonyesha mafungu matano ya juu kwenye Bajeti hiyo kuwa ni Deni la Taifa (Sh2.7 trilioni), Wizara ya Ujenzi (Sh1 trilioni), Wizara ya Ulinzi (Sh920 bilioni), Wizara ya Elimu (Sh721 bilioni) na Wizara ya Nishati na Madini (Sh641 bilioni) ambazo jumla yake ni Sh5.982 trilioni.

“Jumla ya mafungu haya ni sawa na asilimia 40 ya Bajeti. Kwa hiyo asilimia 40 ya Bajeti yote imepangwa kwa mafungu matano tu. Fungu lenye kiwango kikubwa zaidi ya Bajeti kuliko vyote ni fungu 22 ambalo ni malipo kwa Deni la Taifa,” unaeleza uchambuzi huo uliofanywa na Zitto na kuongeza:
“Pia sehemu kubwa ya fedha zilizotengwa kwa Ujenzi na Nishati ni madeni kwa makandarasi wanaotekeleza miradi ya miaka ya nyuma. Wabunge wanapaswa kufanya uchambuzi zaidi wa Bajeti ya mwaka huu inayopendekezwa na Serikali.”

“Kuna haja kubwa ya kuharakisha kuanzishwa kwa Ofisi ya Bajeti katika Bunge na Kamati ya Bunge ya Bajeti ili kuweza kufuatilia kwa karibu, kuchunguza na kutoa taarifa kwa wabunge ili kuwezesha kuboresha Bajeti.”

Kilio cha wafanyabiashara
Wafanyabiashara katika Soko Kuu la Kariakoo, Dar es Salaam wametaka bajeti hiyo iwe ya kumaliza tatizo la mfumuko wa bei ya vyakula.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mmoja wa wafanyabiashara hao, Elizabeth Edward alisema bajeti mara nyingi imekuwa haiwalengi watu wa hali ya chini, bali wenye uwezo.
Edward alitaka Bunge litumie kipindi hiki kupunguza  mfumuko wa bei ya chakula ili wananchi waweze kuona unafuu wa maisha.

“Hivi sasa mchele mzuri unauzwa kuanzia Sh2,200 hadi Sh2,500 lakini, mimi siwezi kununua mchele wa bei kubwa. Nitanunua mchele wa Sh1,800 hadi 1,660 ambao ni mbaya una mchanga,” alisema Mama Lishe huyo na kuongeza:

“Mafuta ya kula tunauziwa lita moja Sh3,000, sukari Sh2,400 hivyo kutokana na vyakula kupanda, chai tunauza Sh200 na vitafunwa kuanzia Sh200 hivyo, watu wengi hawanunui, mtu anaona bora ale muhogo wa Sh100 na maji tu.”

Mfanyabiashara wa Soko la Mabibo, Issa Abdallah alisema bajeti hiyo haimwangalii mfanyabiashara wa chini... “Tunataka Bunge liilegeze bajeti ili kuondoa mfumuko wa vyakula hapa nchini.”
“Kama wabunge wangekuwa na umoja, nina imani huu mfumuko wa bei ya vyakula usingekuwapo hivyo, wabunge wote wanatakiwa wagomee bajeti ambayo itamkandamiza mwananchi wa hali ya chini.”

Mtaalamu wa uchumi kutoka Chuo Kikuu Mzumbe, Dk Prosper Ngowi alisema kutokana na hali ya uchumi wa nchi kukabiliwa na changamoto ya mfumuko wa bei na umaskini wa watu wake, inahitajika bajeti inayoweza kutoa majibu kwenye matatizo ya msingi.

Dk Ngowi aliyataja matatizo hayo kuwa ni pamoja na umeme, miundombinu ya umwagiliaji na ile ya usafirishaji kama barabara na reli.

Hata hivyo, alisema dalili zinaonyesha kuwa hilo haliwezi kufanikiwa, kwani katika Sh15 trilioni zinazotarajiwa kuwasilishwa kama Bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2012/13, Sh5 trilioni pekee  ndizo zinatarajiwa kutumika kwa shughuli za maendeleo.

“Kuna tetesi kuwa kati ya hizo Sh5.25trilioni zitakwenda kulipa madeni na zitakazobaki ndizo za maendeleo, hali hii inaonyesha kabisa kuwa hakuna matumaini,” alisema Dk Ngowi.

Alisema swali jingine la kujiuliza ni wapi Sh15 trilioni za bajeti zitakakopatikana akisema ukusanyaji wa kodi wa Serikali hauridhishi na pia nchi wahisani zinazotegemewa nazo pia hali yake ya kiuchumi siyo nzuri.

Tuesday, June 12, 2012

Fourth woman in sex corruption case named


SINGAPORE - The woman who is believed to have been in a "sex-for-business" deal with former Central Narcotics Bureau (CNB) chief Ng Boon Gay has been named in court today.
She is Cecillia Sue Siew Nang, who was an employee of two IT vendors, Hitachi and Oracle, when the sexual trysts took place.
Ng, 44, allegedly obtained sexual gratification on four occasions from Sue between June 2011 and December 2011.
According to the AFP, the charges state Ng had oral sex with Sue four times, twice when she was a sales manager with Hitachi Data Systems Pte Ltd and twice when she worked for Oracle Corporation Singapore Pte Ltd.
The Corrupt Practices Investigation Bureau (CPIB) said in a statement that the trysts are believed to have been in exchange for helping to 'further the business interests of the relevant IT vendor, in respect of that vendor's dealings with CNB'.
Ng pleaded not guilty to all four charges. He is currently out on a $10,000 bail.
Sue joins the other three women who have been named in court regarding the high profile case.
The three are Esther Goh Tok Mui, Lee Wei Hoon and Pang Chor Mui, who are believed to have traded sexual favours with former Singapore Civil Defence (SCDF) chief Peter Lim Sin Pang in return for him favouring their companies during IT-related tenders held by the SCDF.
At the time of the offences, Pang was a general manager at Nimrod Engineering, Lee was a director at Singapore Radiation Centre, and Goh was a director of business development at NCS. Both Nimrod Engineering and NCS were then vendors to the SCDF while SRC was a potential vendor.
Miss Pang allegedly performed oral sex on Lim on May 2, 2010, in a carpark near the Singapore Indoor Stadium.
Lee allegedly performed oral sex on Lim at a carpark at Big Splash in East Coast Park on Nov 23 last year. They also had sex some time between Oct 18 and 21 in a hotel in Paris, France.
Goh, who is single, is alleged to have had sex with Lim seven times between April 20 and Nov 13 last year. The first time was in a carpark near the Marina Bay Golf Course.
They had sex twice in Lim's apartment in Tanjong Rhu, and another tryst in a carpark near the Singapore Indoor Stadium.
They also had sex three times in a Clementi flat.
The word "obtained" used in court documents in both cases indicate that the men were the likely parties that initiated the sexual propositions.
Lim is facing a total of 10 charges and has yet to make a plea. If found guilty, the three women may also be charged.

Speeding Audi kills Chinese girl in hit-and-run


In yet another hit-and-run tragedy, an 11-year-old primary school student in Xi'an, China, was killed when an 18-year-old Audi driver rammed his car into the girl on June 5.
Zhu Qian's body was flung a distance of more than 10 metres and then dragged a further 26.5 metres.
Chinese police later arrested the young Audi driver, known only as Zhu, in his home after tracking down the car's registration number.
Witnesses said that the girl was using the pedestrian crossing when Zhu's car ran the red light and hit her. He also stopped for two seconds before speeding away.
In these pictures taken by a passer-by, the girl's relatives can be seen mourning over her lifeless body as onlookers watched helplessly.
According to witnesses, the girl's father was sobbing uncontrollably while slapping himself on the face and apologising to his daughter for not being there earlier.







Monday, June 11, 2012

Dk. Mgimwa ahaidi kutanzua kero ya kodi

WAZIRI wa Fedha na Uchumi wa Tanzania Bara, Dk. William Mgimwa, amesema suala la wafanyabiashara wa Zanzibar kutozwa kodi mara mbili wanapopeleka bidhaa Tanzania bara litapatiwa ufumbuzi katika kipindi kifupi kijacho.
Kauli hiyo alitoa jana wakati akizungumza na waandishi wa habari visiwani hapa.
Alisema kodi ni suala linalogusa maisha ya watu, hivyo manung’uniko ya wafanyabiashara kutozwa mara mbili yanapaswa kushughulikiwa.
Dk. Mgimwa alisema kuwa katika utaratibu wa kawaida wa kisheria duniani kote, ukilipia kodi upande mmoja wa Muungano hutakiwi kulipia tena upande mwingine, na kwamba si utaratibu wa kawaida, hivyo amewaagiza TRA kungalia juu ya hali hiyo.
Alisema kuwa baada ya kuangalia upya mfumo uliopo na kubaini dosari, watakaa na kujadiliana ili kutoa mapendekezo kwa viongozi na matatizo yaliyopo yaweze kupata ufumbuzi.
“Uamuzi wa kuupitia upya mfumo huo utatekelezwa na wizara zinazosimamia mambo ya fedha na sera, kwa sababu ndio wanaoguswa na masuala ya kodi kwa maana ya utendaji,” alisema.
Dk. Mgimwa aliongeza kuwa, lengo la kuupitia upya mfumo huo ni kupata muafaka juu ya mambo yanayolalamikiwa katika mfumo wa sasa wa kodi.
Akizungumzia suala la Zanzibar kulipwa asilimia 4.5 ya hisa zake katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Mgimwa alisema suala hilo pia linahitaji mabadiliko.
Alisema mabadiliko hayo yanaweza kufanyika baada ya kuangalia vigezo vilivyotumika kuweka kiwango hicho kama bado vina mantiki.
Dk. Mgimwa alisema lengo la serikali ni kupata mfumo unaotumika katika aina zote za mifumo ya muungano ili kupata utaratibu usiolalamikiwa na walipa kodi na wadau wa pande mbili za Muungano.
Alisema utekelezaji wa kazi hiyo pia utalenga kuijengea Tanzania mazingira bora ya kuingia katika ushirikiano wa masuala ya fedha na soko la pamoja la nchi wanachama wa Afrika Mshariki (EAC).

Mawaziri wafariki ajali ya helikopta


NI PROF SAITOTI, NAIBU WAKE NA MAOFISA WA JUU WA SERIKALI YA KENYA
Mwandishi wetu, Nairobi
WAZIRI wa Usalama wa Ndani Kenya, Profesa George Saitoti na Naibu wake, Orwa Ojode pamoja na maofisa wengine watano, wamefariki dunia baada ya helikopta ya Polisi waliyokuwa wamepanda kuanguka msituni.
Profesa Saitoti ambaye ni mmoja wa mawaziri waandamizi katika Serikali ya Rais Mwai Kibaki na mmoja wa wanasiasa wakongwe wanaoheshimika Kenya, aliwahi pia kuwa Makamu wa Rais kati ya mwaka 1976 hadi 1979 na alishatangaza kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwakani.
Jana, Saitoti ambaye ni mchumi aliyebobea na bingwa hisabati, akiwa na naibu wake na maofisa hao wa wizara walipata ajali wakati wakielekea katika eneo la Sotik kwa ajili ya  mkutano wa usalama.
Ajali hiyo ilitokea asubuhi katika eneo la Kibiku, karibu na Mji wa Ngong, kilometa 20  kutoka Nairobi.
Taarifa zilisema helikopta hiyo ya polisi ilikuwa imebeba abiria saba ambao wote walifariki dunia huku miili yao ikiharibika vibaya.
Profesa Saitoti alikuwa Mbunge wa Kajiado tangu mwaka 1988 hadi mauti yalipomkuta.

Mashuhuda
Walioshuhudia ajali hiyo, walisema waliona helikopta hiyo ikizunguka angani kabla ya kuanguka katika Msitu wa Ngong.
Baada ya kutokea ajali hiyo, polisi walilizingira eneo la ajali huku Kamishna wa Polisi, Mathew Iteere ambaye na yeye alikuwapo katika eneo hilo akisema atatoa taarifa kamili kuhusiana na  ajali hiyo kwa waandishi wa habari baadaye.
Ajali hiyo imetokea ikiwa ni miaka minne tu tangu kutokea kwa ajali nyingine ya helikopta Juni 10, 2008 ambayo ilisababisha vifo vya mawaziri wawili.
Mawaziri walipoteza maisha katika ajali hiyo ni pamoja na Kipkalya Kones na Lorna Laboso.

Mambo muhimu kwa Saitoti
Saitoti ambaye alizaliwa mwaka 1945 kabla ya kupatwa na mauti hayo, aliwahi kutoa wito kwa raia wa Kenya  kuwachagua viongozi ambao ni watendaji wa kazi bila ya kuangalia kabila, rangi na dini.
Kiongozi huyo ambaye kabla ya kuwa Waziri wa Usalama wa Ndani, alikuwa Waziri wa Fedha na pia Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Dunia kati ya mwaka 1990 hadi 2001, alisema Wakenya wanapaswa kuwachunguza viongozi kabla ya kuwachagua ili kuepuka kuchagua wala rushwa.
Profesa Saitoti alibainisha kuwa kuna haja ya wanasiasa wote  kutowagawa Wakenya wakati wa kampeni zao ili kuepuka kile kilichotokea katika uchaguzi 2007.
Alisema kutokana na uzoefu wake, yeye ndiye aliyekuwa na uwezo wa kumrithi Rais Mwai Kibaki.
“Mataifa yote yanatuangalia sisi sasa hivi, nini tunachokifanya wakati huu na nini kitakachotokea wakati wa uchaguzi mkuu mwakani,” alisema.
Marehemu Saitoti ndiye aliyekuwa akiongoza jeshi la nchi hiyo kwa ajali ya kuwatafuta wafuasi wa kundi la Al Shabab, Somalia

Friday, June 1, 2012

Man secretly films foreign women in S'pore to promote spy camera





In order to promote his spy cameras, a man is using them to film videos of attractive women and posting them online.

STOMPer Longnails is disgusted that a man is promoting spy cameras by shooting videos of attractive foreign women and posting them online.

The videos are posted on Youtube, all with links to a website selling a spy camera. The spy camera is modelled after a mobile phone, and can take photographs, record sound and videos.

Said the STOMPer:

"This guy is seriously twisted!

"He stalks foreign women, films them secretly, and posts the videos on Youtube.

"It is even worse that he does this to promote the sale of a spy camera.

"The spy camera is made to look like a phone, but has no mobile phone functionality.

"This means its sole purpose is to take pictures, record videos and audio clips without people knowing.

"The stuff he is selling will compromise our privacy.

"He may even corrupt our young by showing the depraved things he can do with his gadget.

"Someone better do something about this freak."

Cleaners protest by littering Barcelona airport

Travellers walk on a floor that has been littered with pieces of paper strewn by cleaning staff who protested at Barcelona's airport on May 30, 2012. Cleaning staff working for a company who have a contract with the airport demonstrated against pay and benefits cuts made by their employer.
The cleaners' strike has brought chaos to El Prat Airport in Barcelona - more than 200 workers have stopped clearing the terminal.
The Spanish Airports Authority said that it is making an effort to solve the situation.

Who is the hottest of them all?




The verdict's out on who's the most beautiful of them all. Well, this year at least.
Model Bar Refaeli has topped Maxim's new 2012 Hot 100 list as the most beautiful woman in the world.
Actresses Olivia Munn and Mila Kunis took second and third spot, respectively, while Katy Perry came in fourth.
This year marked the first year Maxim readers could weigh in on who made the list.
Battleship actress Brooklyn Decker made the top 50 at no. 42, while Kristen Stewart pipped her Snow White co-star Charlize Theron by a spot to take no. 15 on the list.