Thursday, September 6, 2012

Wachimba migodi waliosalia waachiliwa


Wachimba migodi 106 waliosalia kuzuiliwa na polisi nchini Afrika Kusini wameachiliwa baada ya kesi tatanishi dhidi yao kutupiliwa mbali kufuatia shinikizo za umma.
Wachimba migodi hao wanatarajiwa kurejea katika mgodi wa Marikana ambako polisi waliwapiga risasi na kuwaua wenzano 34 waliokuwa wanagoma mwezi jana.
Chama kimoja cha wafanyakazi kiimekataa kutia saini mktaba wa amani na serikali pamoja na wamiliki wa mgodi huo, Lonmin,wakisisitiza kuwa wataendelea kugoma hadi matakwa yao yatakapotimizwa.
Mgomo huo uliitishwa na chama cha wafanyakazi wa migodini na wale wa ujenzi. wadadisi wansema kuwa hatua ya chama hicho kukataa kutia saini mktaba huo, heunda isiathiri kivyovyote mgogoro unaoendelea
Chama cha wafanyakazi cha NUM ambacho kina uhusiano na chama tawala, ANC, kilitia saini mkataba huo ulioafikiwa kwa usaidizi wa viongozi wa makanisa.
Hapo awali, mwanaharakati wa kisiasa nchini Afrika Kusini, Julius Malema, alitoa wito wa wachimba migodi kuendelea na mgomo wao hadi matakwa yao yatakapotimizwa na waajiri wao.
Tamko la Malema linakuja wakati mgogoro wa mishahara kati ya wachimba migodi wa Marikana na waajiri wao ukitokota.
Bwana Malema hata hivyo anasema kuwa tamko lake sio uchochezi wa ghasia.
Takriban wachimba migodi, 34 waliuawa kwa kupigwa risasi na polisi tarehe kumi na sita mwezi Agosti.
Wachimba migodi zaidi walioshtakiwa kwa madai ya kusababisha mauaji hayo, wanatarajiwa kuachiliwa baadaye leo.
Vyama kadhaa vya wafanyakazi, vimetia saini makubaliano yatakayowafanya kurejea kazini, kulingana na wamiliki wa migodi hiyo.
Bwana Malema anatarajiwa kuzuru mgodi wa Marikana hii leo, siku moja baada ya wachimba migodi 3,000 kuandamana kuunga mkono wachimba migodi wenzao
Aidha Malema, ambaye alikuwa kiongozi wa chama cha ANC tawi la vijana, alifukuzwa chamani baada ya kuonekana kutofautiana kwa sera na Rais Jacob Zuma.
Bwana Malema awali aliwataka wachimba migodi hao kuendelea kutatiza shughuli za migodi.
Aliambia BBC kuwa '' Watu wametafsiri visivyo wito wangu kwa wachimba migodi kutatiza kabisa shughuli za migodi. Nilicho maanisha ni kwamba waendelee kugoma. Sipendekezi, ghasia wala vurugu wala sitoi wito wa mauaji. Wafanyakazi hawapaswi kukubali kunyanyaswa. Hatutaki dhulma tena, ila ikiwa tu serikali itakubali kuwalipa pesa za kutosha ''
Malema alisema muwa waekezaji wa kigeni wameiba kila kitu nchini Afrika Kusini na akasema kuwa wako tayari kufanya kila hali kurejeshewa kila kilicho chao.
Alisema jibu lililosalia kwa matatizo ya migodini ni kutaifisha migodi.
Siku ya Jumatano, wachimba migodi wa Marikana, walifanya maandamano makubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa tangu mauaji ya wafanyakazi wenzao kuzua hisia kali.
Wachimba migodi hao wanaolipwa kati ya dola miatatu na mianne wanataka nyongeza ya hadi dola miasaba au mianane kwa mwezi.

Kisa na mkasa na Salim Kikeke

Nzi wawili tu

Mamlaka nchini Uchina zimeanzisha sheria mpya ya vyoo vya umma.
Sheria hiyo inakataza choo kuwa na zaidi ya nzi wawili kwa wakati mmoja.Sheria hiyo iliyowekwa na halmashauri ya mannispaa ya jiji la Beijing inalenga kuhakikisha hali ya usafi katika vyoo vinavyotumiwa na jamii.
Hata hivyo haijawekwa wazi ni hatua gani zitachukuliwa iwapo nzi wa watu atakutwa chooni.
Sheria nyingine ni kuhakikisha vyoo vinasafishwa kila mara na matumizi ya vifaa vyakisasa na mafunzo ya kutosha kwa watu wanaovitazama vyoo hivyo.
Mwandishi wa BBC mjini Beijing amesema sheria hizi mpya ni mahsusi kusaidia watu wengi mjini humo ambao hawana vyoo majumbani mwao na wanategemea vyoo vya umma. Bila shaka watakuwa wakitazama huko na huko kutafuta nzi wa tatu yuko wapi..

Tembo kuwa pweza

Tembo mmoja nchini Poland anatarajiwa kuchukua nafasi ya Pweza Paul kwa kutabiri matokeo ya michuano ya maataifa ya Ulaya yanayoanza hivi karibuni.
Tembo huyo anayejulikana kama Citta mwenye umri wa miaka thelathini na mitatu atakuwa akitumia mkonga wake kubashiri timu itakayoshinda.
Habari kutoka Warsaw zinasema ubashiri wa kwanza utafanywa tarehe sita mwezi Juni, siku mbili kabla ya kuanza kwa michuano hiyo. Tembo huyo alifanya kituko wakati akitambulishwa kwa waandishi wa habari, baada ya kuumeza mpira wa miguu uliokuwepo mezani.
Mkurugenzi wa hifadhi ya wanyama ya mjini Warsaw Teresa Grega amesema tembo huyo alitabiri ushindi wa Chelsea dhidi ya bayern Munich katika fainali ya Klabu Bingwa Ulaya hivi karibuni. Tembo huyo atatabiri mshindi kati ya Poland watakaopambana na Ugiriki Juni nane.
Atapewa matunda matatu, mawili yakiwa na majina ya timu hizo mbili, na tunda la tatu kwa ajili ya kutabiri sare. Tembo huyo alizaliwa India, akaishi Ujerumani kabla ya kwenda Austria, halafu Uhispania na hatimaye kuhamia Poland. Bi Gregga amesema tembo huyo anapenda sana kutazama soka.

Noti taka

Bwana mmoja nchini Marekani ameingia matatani baada yakudondosha noti ya dola moja barabarani.
Bwana huyo, John davis wa Cleveland, amesema alikuwa akijaribu kutoa sadaka kwa mtu aliyekuwa barabarani.
Davis ambaye alikuwa ndani ya gari yake, alifungua dirisha na kutoa noti kadhaa za fedha ili kumpa mtu aliyekuwa akiomba msaada.
Kwa bahati mbaya, moja kati ya noti alizokuwa akizitoa ilipeperushwa na upepo. Muda si mrefu, alitoea polisi na kumkamata bwana Davis kwa kosa la kurusha taka barabarani.
"Nimekuona ukitupa karatasi" amekaririwa polisi huyo akimwambia bwana Davis. Msamaria mwema huyo amepigwa faini pamoja na gharama za mahakama zinazofika dola mia tano.

Atoroka na gari la wagonjwa

Mwanamama mmoja aliyekuwa amelazwa hospitali, alichoshwa na maisha ya hospitalini na kuamua kuiba gari la wagonjwa na kutoroka nalo.
Mwanamama huyo Heather Sullivan wa Buffalo, New York, alikataliwa kwenda nyumbani kwa kuwa hali yake haikuwa njema sana kiafya, ingawa mwenyewe alikuwa akitaka kuondoka.
Taarifa zinasema mwanamama huyo alinyata na kuiba gari la kubebea wagonjwa la hospitali ya Erie County, na kuondoka kwa kasi kubwa. Alianza kufukuzwa na polisi.
Mwanamama huyo alikuta gari la kubebea wagonjwa likiwa limeegeshwa nje ya hospitali huku fungua za gari hilo zikinin'ginia kwenye kiwashio.
Polisi wa Buffalo wamesema mwanamke huyo aliokuwa akiendesha gari hilo kwa mwendo wa kasi na wa hatari, huku akikosa kosa kugonga wapita njia. Hatimaye gari hilo lilipoteza mwelekeo na kupunduka, na mwanamama huyo kukamatwa.
Ameshtakiwa kwa kuhatarisha maisha ya watu, na kuiba gari. Hasara aliyosababisha imefika dola laki moja.

Faini kwa mluzi

Mwanamama mmoja nchini Ujerumani amepigwa faini, baada ya kupiga mluzi kwenye simu yake na kusababisha maumivu kwa mtu aliyekuwa akizungumza naye.
Mwanamama huyo mwenye umri wa miaka sitini na moja, alikuwa amechoshwa kupigiwa simu na kampuni zilizokuwa zikimshawishi anunue bidhaa mbalimbali.
Mwanamama huyo wa Pirmasens, katika eneo la Rhineland amesema alikuwa amechoshwa na bughudha za wauza bidhaa waliokuwa wakimpigia simu kila mara kumshawishi anunue bidhaa zao. Siku ya siku alipopigiwa simu, aliamua kupiga mluzi kwa nguvu kwa mtu aliyempigia simu kiasi cha kumsababishia maumivu ya masikio. Mwanamama huyo amepigwa fani ya karibu dola mia tisa.
Alipofikishwa mahakamani alimwambia jaji kuwa alikuwa amechukizwa mno na simu za wafanyabiashara.
Na kwa taarifa yako.........Fani kongwe zaidi duniani ni ukunga na uganga wa kienyeji.
Tukutane wiki ijayo.... panapo majaaliwa....

Chadema says No to team on Mwangosi

By Fariji Msonsa, The Citizen Reporter
Dar es Salaam. Chadema has expressed serious doubts on the five-man commission formed by the Home Affairs minister, Dr Emmanuel Nchimbi, to investigate circumstances that led to the death of Iringa-based journalist, Mr Daudi Mwangosi, on Sunday.
Talking to reporters at party headquarters, the Chadema director of Legal, Constitution and Human Rights department, Mr Tundu Lissu attacked the commission, alleging that some of its members’ competency was questionable.
But in a quick rejoinder, Dr Nchimbi dismissed Chadema’s concern, noting that he has already fulfilled his responsibility as minister and at this point, he wouldn’t entertain suggestions on the probe team’s set up. “What I am waiting for now is a report on what happened until the journalist was killed; I won’t entertain anything that’s bent on diverting us from this task,” he said.
But discrediting the team, Mr Lissu, a lawyer by profession, singled out the chairman of the commission, Court of Appeal Judge Stephen Ihema, as a person who wasn’t fit to head such an important task. “The team has been formed on the basis of personal friendship,” he claimed, noting that this would hinder free and competent investigation.
He said his party was also not satisfied with the terms of reference for the commission, since most of those issues are known to the public through photos published in newspapers and aired through television stations.
“Most of the things are clear to the public. What we want is the top officials including the minister and the Inspector General Police (IGP) to be investigated if they ordered the police to kill,” said Mr Lissu.
He said that the probe team itself is inefficient since most of its members are not familiar with that field, calling on President Jakaya Kikwete to intervene and form a new team “comprising respected judges from the Court of Appeal and may be the High Court but not judge Ihema.”
Furthermore, he said, Chadema would like to see Dr Nchimbi take political responsibility over the killing by stepping  down or alternatively, the President should fire him. The Union of Tanzania Press Clubs (UTPC) president, Mr Kenneth Simbaya, warned yesterday they would be watching to see if anyone is attempting to give misleading information to the commission.
“Basically, we all know what happened. We don’t expect an entirely different version of what happened,” Mr Simbaya said.
And residents of Busoka Village appealed to Dr Nchimbi to closely follow up the performance of the commission so that it comes up with the truth.
Meanwhile, the Trade Union Congress of Tanzania through union’s assistant secretary general Mr Hezron Kaaya wondered why the team has been given “a whole 30 days to accomplish the work while most of the facts and details of what happened were a public knowledge.”
From Mwanza, CCM issued a statement condemning brutal killing of the Channel Ten reporter. Ideology and Publicity secretary, Nape Nnauye, issued the party’s statement at CCM Regional office here that expressed “grave concern” at the escalation of violence whenever the opposition does its ‘operations’.
Additional reporting by Hawa Mathias (Mbeya), Mulemwa Mulemwa and Lasteck Alfred (Dar).
“CCM takes this opportunity to offer condolences to the bereaved, members of press and all those touched by this tragedy in one way or another. We call upon the various agencies and commissions created to investigate this with great professionalism and find out the cause of the violence and the circumstances that led to the death of Mwangosi,” said Nnauye in a statement to media.
Additional reporting by Hawa Mathias (Mbeya), Mulemwa Mulemwa and Lasteck Alfred (Dar).

Siri mauaji Iringa zaanza kufichuka


POLISI WALIOTEKELEZA OPERESHENI WADAIWA KUSAFIRISHWA KUTOKA MIKOA MINGINE, WAANDISHI WA HABARI IRINGA WASUSIA MKUTANO WA DCI MANUMBA
Waandishi wetu, Dar, mikoani
INADAIWA kwamba askari waliokuwa katika operesheni ya kuzuia mkutano wa Chadema katika eneo la Nyololo wilayani Mufindi, Iringa na ambayo ilisababisha kifo cha Mwandishi wa Habari, Daudi Mwangosi walitolewa katika mikoa ya Dodoma, Morogoro na Mbeya.

Tayari tukio hilo limeibua mjadala mzito kiasi cha kumfanya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi kuunda tume huru kubaini chanzo cha tukio hilo. Marehemu Mwangosi alizikwa juzi nyumbani kwao Tukuyu, mkoani Mbeya.

Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili jana zilisema kuwa polisi hao kutoka mikoa hiyo mitatu wakiwa wamesheheni vifaa mbalimbali likiwamo gari la maji ya kuwasha, walisafiri siku moja kabla ya mkutano huo wa Chadema na baadaye kuzuka vurugu zilizosababisha kifo hicho.
Marehemu Mwangosi aliuawa kwa mlipuko unaodhaniwa kuwa ni wa bomu ambao ulisambaratisha vibaya sehemu kubwa ya mwili wake.

Chanzo cha habari kutoka mkoani Dodoma kilisema: “Hapa kwetu kuna askari 10 na tunawafahamu kwa majina. Waliondoka hapa siku moja kabla ya tukio hilo wakiwa na gari la washawasha.”
Chanzo hicho kilisema kwamba awali, hawakuwa wakifahamu kama baadhi ya wenzao walichukuliwa na kupelekwa Iringa. “Tulikuja kuona kwenye gazeti picha na tulipofuatilia tukaelezwa kuwa ni kweli Dodoma ilitoa askari kwenda Iringa.”

Askari mwingine aliyekuwa katika operesheni hiyo ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sababu za kitaaluma, alikiri kuwa hadi jana baadhi yao walikuwa bado wako Iringa na kwamba walikwenda kwa agizo la wakubwa wake wa kazi.
“Sisi ni Watanzania, lakini tumelazimika kuyafanya hayo kwa sababu ya mkate (malipo). Kwa kweli haikuwa haki, kuwatoa askari na silaha kutoka mikoa mitatu kana kwamba wanakwenda kupigana vita!”

Alidokeza kwamba, askari wote waliotoka Dodoma walikuwa njiani kurudi mkoani humo, jana lakini gari la maji ya kuwasha liliendelea kubaki huko Iringa likiwa na dereva wake na askari mmoja mwenye cheo cha inspekta. Askari huyo alisema kwamba gari hilo lililazimika kubaki kutokana na hitilafu.

“Wengine wamerudi lakini, kuna wengine wenye gari la kuwasha bado walikuwa Iringa, gari lao limepata hitilafu kidogo,” kilisema chanzo hicho kutoka mjini Dodoma.

Mmoja wa askari hao alidaiwa kwamba hiyo inaweza kuwa moja ya sababu ya askari hao kumshambulia marehemu Mwangosi wakati mwenzao anayemfahamu akijaribu kuwazuia. "Hii inaonyesha kuwa askari hao waliompiga walikuwa hawamjui na huyu aliyekuwa akiwazuia, alimjua.”

Makamanda watupiana mpira

Alipoulizwa kuhusu taarifa hizo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Zelothe Stephen hakukubali wala kukanusha na badala yake alisema: “Mambo yote hayo yanatakiwa kujibiwa na Kamanda wa Iringa.”
Aidha, alisema sakata la kifo cha mwandishi huyo kwa sasa liko katika vyombo vya uchunguzi hivyo asingekuwa tayari kulizungumzia.

“Siwezi kusema kama askari wangu walikwenda huko au hawakwenda, isipokuwa ninachoweza kusema ni kwamba suala hilo lipo katika vyombo husika hivyo waachiwe wao au Kamanda wa Iringa ndiye mwenye majibu.”
Alipotajiwa jina la mmoja wa askari aliyeonekana katika picha za video na magazeti za tukio hilo kwamba anatokea  katika moja ya vituo vyake, kamanda huyo alisema: “Mimi yakitokea Dodoma nitazungumza wala siyo mtu mwingine kwa hiyo, mambo ya Iringa siwezi kuyazungumza na kama tutaanza kila Kamanda kuzungumza jambo hilo hamuoni kuwa itakuwa ni kama vurugu?”

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Michael Kamuhanda alipopigiwa simu yake iliita tu bila kupokewa.
Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro Faustine Shilogile alisema kwa kuwa tukio hilo limefanywa na polisi, mambo mengi yatazungumzwa lakini akasisitiza kwamba hajapeleka askari Iringa.
Alisema hakukuwa na agizo kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Polisi wala ombi kutoka Polisi Iringa kutaka askari wa kuongeza nguvu... “Taarifa hizo ni za uzushi kwani hazina ukweli wowote.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani alikanusha pia kuwapeleka askari wake Iringa akisema: “Hizo taarifa siyo za kweli. Hakuna askari yeyote aliyekwenda Iringa wakati wa vurugu zile.”

Mkutano wa DCI wavunjika

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba hakutaka kuzungumzia suala hilo akisema: “Hayo yote yameundiwa tume ngoja tuiachie ifanye kazi yake.”
Awali, DCI Manumba aliitisha mkutano na waandishi wa habari mkoani Iringa, ambao hata hivyo, ulivunjika baada ya kutokea kutoelewana baina yao.

Manumba alitaka kueleza ripoti ya uchunguzi wa kifo cha Mwangosi, lakini waandishi hao walikataa kumsikiliza wakisema hawauamini uchunguzi huo kwa kuwa ulifanywa na polisi peke yao.

Kabla Manumba, hajaanza kuzungumza, Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Iringa (IPC), Frank Leonard alisema kutokana na msimamo wa waandishi wa habari wa mkoa huo hakutakuwa na uhusiano wa kikazi na polisi hadi pale tume zilizoundwa kuchunguza kifo hicho zitakapotoa taarifa sahihi juu ya mauaji hayo.

“Msimamo wetu ni kusitisha uhusiano wa kikazi baina yetu na jeshi la polisi hususan Mkoa wa Iringa, tumekuja hapa kwa sababu DCI umetuita na kama unataka kutupa taarifa ya kifo cha ndugu yetu basi waambie hao maofisa wa jeshi wa Iringa watoke nje,” alisema Leonard.

Akijibu madai hayo Manumba alisema: “Nia yangu ni kutoa taarifa ya uchunguzi wa kifo cha Mwangosi, ndiyo maana niliwasiliana na mwenzenu ili tuweze kuzungumza, Polisi Iringa wataendelea kuwepo na waandishi wa habari mtaendelea kuwepo, matukio kama haya yapo na yataendelea kuwepo.”
Licha ya maelezo hayo, hakuna mwafaka uliofikiwa na mkutano huo ukavunjika.
Akizungumza kwa simu na gazeti hili baadaye, DCI Manumba alisema: "Ni vyema wao wangenisikiliza kujua ninataka kuwaambia nini. Lakini, kwa kuwa kuna mkanganyiko, nimeona ni vyema jambo hili lisubiri tume ndipo watakuja kulizungumza.”

Waikataa Tume ya Nchimbi
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeiponda tume ya Dk Nchimbi kikieleza kuwa imeundwa ili kurudisha uhusiano kati ya Polisi na waandishi wa habari na si kutafuta chanzo cha tatizo.

Juzi, Dk Nchimbi alitangaza kamati ya kuchunguza mauaji hayo inayoongozwa na Jaji Mstaafu, Steven Ihema na wajumbe, Mwakilishi wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Theophil Makunga, Mwakilishi wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Pili Mtambalike, Mtaalamu wa milipuko kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Kanali Wema Wapo na Naibu Kamishna wa Polisi (DCP), Isaya Mngulu.

Mkurugenzi wa Sheria, Katiba na Haki za Binadamu wa Chadema, Tundu Lissu alisema Dar es Salaam jana kwamba: “Hii si tume ya kuchunguza mauaji, bali ina lengo la kurudisha uhusiano mzuri kati ya Jeshi la Polisi na waandishi wa habari ili kuwasahaulisha wananchi kwa sababu imeundwa na waziri ambaye naye anatakiwa kuhojiwa.” “Tunamwomba Rais Jakaya Kikwete ateue tume kama anavyoelekezwa na Sheria ya Tume za Uchunguzi ya mwaka 1992, ambayo inaruhusu kumhoji yeyote kasoro yeye Rais.”

Lissu alisema Rais Kikwete angeunda tume hiyo na Waziri Nchimbi na IGP Said Mwema wanatakiwa kujiuzulu ili kupisha uchunguzi akidai kwamba kuna uwezekano mkubwa kwamba walitoa amri ya mauaji hayo.
“Dk Nchimbi anatakiwa kumuiga Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi ambaye alijiuzulu akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani baada ya kutokea mauaji, akijiuzulu atajijengea heshima tofauti na sasa kwani wananchi wamesikitishwa na mauaji hayo,” alisema Lissu.

Mwanasheria wa Chadema, Mabere Marando alidai kwamba kuna mkakati uliowekwa na Serikali wa kukidhoofisha Chadema baada ya kuonekana kwamba ni tishio kwa CCM.

Mbali na Chadema, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), pia limesema halina imani na kamati hiyo likisema imekuwa kawaida kwa Serikali kuunda tume ambazo hazileti ripoti kwa wananchi.
“Tume zimekuwa zikiundwa bila faida yoyote, huku zikipewa muda kuchunguza yaliyotokea lakini matokeo yake huwa hakuna ripoti wanayorudisha,” alisema Kaimu Katibu Mkuu wa Tucta, Hezron Kaaya.

Kaaya alisema tume zimekuwa zikiundwa na kuigharimu Serikali fedha nyingi za walipa kodi, lakini ripoti zake zinaendelea kuwa siri.

Imeandikwa na Habiel Chidawali, Dodoma, Hamida Sharrif Morogoro, na Tumaini Msowoya, Iringa na
Lasteck Alfred na Juliana Malondo.

Friday, August 10, 2012

VACANCIES/ JOB OPPRTUNITIES/ NAFASI ZA KAZI/ AJIRA


Nursing Officer/Midwife
Date Listed: Jul 19, 2012
Application Deadline: Sep 28, 2012


Work Experience / Skills:
·        Have experience in communicating effectively especially with patients, doctors and other staff respectively  (E)
·        Have experience in preparing the room and all necessary equipment for the clinic  (E)
·        Good interpersonal skills  (E)

Qualifications:
·        Diploma In Nursing
 E – Essential, P – Preferred
Application Instructions:
We are an equal opportunities employer, people with disabilities are encouraged to apply Please submit a letter of Application or curriculum vitae with two references and maximum one page cover letter on why you believe you are the right candidate for this position.  Please send it via email to: recruitment@ccbrt.or.tz or by post to the Human Resources Department,P.O Box 23310, Dar es Salaam, Tanzania. Tel:  +255 (0) 22 260 1543, +255 (0) 22 260 2192, Fax: +255 (0) 22 260 1544. Website: www.ccbrt.or.tz, www.baobabhospital.or.tz
 Closing date for Applications: 28th  September 2012.  Only shortlisted candidates will be contacted

Program Officer- Grants
Date Listed: Aug 7, 2012
Application Deadline: Aug 17, 2012
Desired skills, knowledge and qualifications
·        Master’s degree in social sciences with background in accounting and at least three years experience in grants or project management, monitoring and evaluation, policy and development
·        Strong analytical and problem solving skills

Application Instructions:
The Executive Director
The Foundation for Civil Society
Haidery Plaza, 5th Floor
Upanga/ Kisutu Street,
P. O. Box 7192
DAR ES SALAAM
Head – Communication Information &Publicity
Date Listed: Aug 6, 2012
Application Deadline: Aug 17, 2012
Desired skills, knowledge and qualifications
·        Master’s degree in Journalism, Mass Communication or any related qualifications
·        At least 3 years of experience in Mass communication

Application Instructions:
The Executive Director
The Foundation for Civil Society
Haidery Plaza, 5th Floor
Upanga/ Kisutu Street,
P. O. Box 7192
DAR ES SALAAM
Poultry Technicians (6 Posts)
Date Listed: Aug 6, 2012
Area: Moshi
Application Deadline: Aug 20, 2012
Education Requirement
A holder of Diploma or degree in animal production, or animal science from a recognized college or university
Experience / Knowledge and Exposure
·        A minimum of 10 years experience in poultry operation
·        Experience in poultry breeding is an added advantage.
·        Ability to work independently but as a part of a team
·        Ability to work with people from wide range of nationalities and willing to share skills and knowledge wit others.

 Application Instructions:
Personnel Assistant
P.O box 8733
MOSHI

ICS Programme Volunteer
Date Listed: Aug 6, 2012
Application Deadline: Aug 20, 2012
Closing Date:20 August 2012
Successful applicants must:
·        Be Tanzanian citizens living in Kagera or Mwanza;
·        Have completed secondary school up to Form 6; u be aged 18 to 25;
·        Be able to communicate in English and Swahili;
·        Have been involved in community development through clubs, youth groups, community based organizations or volunteering; U be able to work well in a team;
·        Be able to commit to a full-time 11-week programme away from home;
·        Be available for training 3 weeks before the program starts.

 Application Instructions:
For application forms please visit www.jitoleetanzania.com
Return your form by email or post to the address below:
ICS Programme Manager
VSO Tanzania
Plot No 997 Msasani
P.O Box 6297
Dar Es Salaam
Email Link above or call: +255 (0) 22 260 072/87 Ext 111
Deadline: 17:00 Mondav 20 August 2012
Interview Dates: 7 & 8 September 2012
Due to anticipated interest in these posts, only short listed candidates will receive a response.

Finance Manager
Date Listed: Aug 6, 2012
Application Deadline: Aug 20, 2012


Daily News, August 6, 2012
Qualifications
·        Relevant university degree from a reputable/accredited Institution OR other relevant educational background combined with relevant professional experience;
·        At least 5 years experience of finance management;
·        Relevant Accounting Qualification(s) a must e.g. CPA;
·        Solid experience of work with windows-based computer software and modern accounting- systems;
·        Ability to plan for different sets of scenarios in relation to budgets and plans;
·        Proven skills and experience in report writing;
·        Strong communication; interpersonal, analytical and negotiation skills; Fluency in written and spoken English, fluency in spoken Kiswahili a must

The President, Tanganyika Law Society
P.O Box 2148,
Dar es Salaam.
An electronic copy of ONLY the application letter and CV should also be sent to the Email Link above 
Surveyor
Date Listed: Aug 6, 2012
Application Deadline: Aug 15, 2012
Skills & Abilities:
·        Good IT skills;
·        DGPS post processing software experience; Ability to work independently;
·        Good reporting capability;
·        Good oral and written communication skills, with reasonable English reading and writing;
·        Driver's licence.

Human Resources
Intra Energy Tanzania 16th Floor, PPF Tower, Plot No. 20121
Ohio Street / Garden Avenue
P.O. Box 23066
Dar es Salaam

Physiotherapist
Date Listed: Jul 19, 2012
Application Deadline: Sep 28, 2012

Work Experience / Skills:
·        At least 2 years experience in a Hospital. Strong communication skills both verbal and written (E)
·        Experience in keeping records and monitoring progress of patients (E)
·        Proficient  computer skills (E)

Qualifications:
·        A bachelor degree or diploma   in Physiotherapy
 E – Essential, P – Preferred
 Please send it via email to: recruitment@ccbrt.or.tz or by post to the Human Resources Department,P.O Box 23310, Dar es Salaam, Tanzania. Tel:  +255 (0) 22 260 1543, +255 (0) 22 260 2192, Fax: +255 (0) 22 260 1544. Website: www.ccbrt.or.tz, www.baobabhospital.or.tz

Closing date for Applications: 28th September 2012.  Only shortlisted candidates will be contacted
Deputy of Disability Hospital
Date Listed: Jul 19, 2012
Application Deadline: Aug 31, 2012

Work Experience / Skills:
·        Minimum of five years working experience in a health institution (E)
·        Have strong leadership and excellent interpersonal skills (E)
 Qualifications:
·        Master Degree or Postgraduate Diploma General Management
 E – Essential, P – Preferred.
Please send it via email to: recruitment@ccbrt.or.tz or by post to the Human Resources Department,P.O Box 23310, Dar es Salaam, Tanzania. Tel:  +255 (0) 22 260 1543, +255 (0) 22 260 2192, Fax: +255 (0) 22 260 1544. Website: www.ccbrt.or.tz, www.baobabhospital.or.tz
Internal Auditor
Date Listed: Aug 7, 2012
Application Deadline: Aug 17, 2012
Desired skills, knowledge and qualifications
·        Must be a CPA holder
·        He/she must be strong in Systems audit and experienced
·        Strong analytical and problem solving skills
·        Excellent, well developed interpersonal and organizational skills.
·        Highest level of integrity, honesty and sense of responsibility.
·         A proven ability to work under pressure to achieve visible results
·        Excellent report writing skills and analytical skills
·        Computer literate with proficiency in MS Office Applications
·        Excellent communication skills, verbally and writing, both in English and Swahili
The Executive Director
The Foundation for Civil Society
Haidery Plaza, 5th Floor
Upanga/ Kisutu Street,
P. O. Box 7192
DAR ES SALAAM
Assistant Program Officer- Grants
Date Listed: Aug 7, 2012
Application Deadline: Aug 17, 2012
Desired skills, knowledge and qualifications
·        Degree in Social Sciences  with background in accounting or any related degree course
·        At least two years experience in grants or project management
·        Writing and documentation skills (reports and minutes)
·        Fluency in written and spoken English and Kiswahili
·        Computer literate with competency in MS Office Applications
·        Possess time management and planning skills
·        A high level of integrity, honesty and sense of responsibility

The Executive Director
The Foundation for Civil Society
Haidery Plaza, 5th Floor
Upanga/ Kisutu Street,
P. O. Box 7192
DAR ES SALAAM
Program Officer - Monitoring & Evaluation
Date Listed: Aug 6, 2012
Application Deadline: Aug 17, 2012
·        Desired skills, knowledge and qualifications
·        Master’s degree in social sciences with at least three years experience in grants or project management, monitoring and evaluation, policy and development
·        Strong analytical and problem solving skills
·        Excellent, well developed interpersonal and organizational skills.
·        Must be a team player, very self motivated and able to make balanced judgment and prioritize work load with minimum supervision
·        An in depth knowledge of the civil society sector and development processes in Tanzania
·        Highest level of integrity, honesty and sense of responsibility
·        A proven ability to work under pressure to achieve visible results
·        Strong work ethics and sensitive to people from different countries/cultures
·        An in depth knowledge of MKUKUTA/MKUZA
·        Excellent report writing skills and analytical skills
·         Fluency in written and spoken English and Kiswahili
·        Computer literate with proficiency in MS Office Applications

The Executive Director
The Foundation for Civil Society
Haidery Plaza, 5th Floor
Upanga/ Kisutu Street,
P. O. Box 7192
DAR ES SALAAM
Secretary / Chief Executive Secretary
Date Listed: Aug 6, 2012
Application Deadline: Aug 20, 2012
Daily News, August 6, 2012
Qualifications
·        Masters in Business administration or other qualification from Chartered Institute of
·        Secretaries and Administration;
·        At least a Bachelor degree in law from a recognized University;
·        LL.M will be an added advantage;
·        At least 5 years experience in administration;
·        Experience in planning, coordination and monitoring of programs;
·        Excellent analytical, writing, oral presentation and organizational skills;
·        Possess strong knowledge of current development issues;
·        Demonstrate leadership ability;
·        Excellent knowledge of the Tanzanian judicial system and administrative structure of the judiciary; and
·        Experience in building and managing teams and creating an enabling environment.

The President, Tanganyika Law Society
P.O Box 2148,
Dar es Salaam.

Paediatric Oncology Ward Administrator
Date Listed: Aug 1, 2012
Phone: +255 22 277 5965
Application Deadline: Aug 17, 2012
Start Date: Oct 01, 2012


Essential Requirements:

  • Diploma or degree in a relevant field such as administration, communication or accountancy
  • Strong communication skills, with excellent written and spoken English and Swahili
  • 3-years work experience in an administrative position
  • Financial management experience which includes operating a petty cash system
  • Proven computer skills in Microsoft Office applications with advanced skills in Excel
  • Strong organisational and time management skills
  • Ability to take initiative, prioritise and be proactive
  • Flexibility and experience of working within a challenging and fast paced environment
  • The ability to work within a culturally diverse team spread across different functions
If are interested in any of these roles, please visit our website www.tumainilamaisha.orgwhere you can view and download the job description.  CV’s and covering letter should be returned via email to: the Email Link above by 12:00 noon EAT on 17th August 2012.
Only candidates shortlisted for interview will be contacted. 
Maintenance Engineer
Date Listed: Jul 31, 2012
Email Address: Click to Email
Phone: +255 776 529 877
Area: Zanzibar
Application Deadline: Aug 24, 2012


Application Instructions:
·        Atleast 3 years experience, degree of engineering, above 28 years
Operation Manager 
Zainab Bottlers Ltd
P o Box 271, Mombasa area, Zanzibar. 

Programme Co-ordinator
Date Listed: Aug 1, 2012
Phone: +255 22 277 5965
Application Deadline: Aug 17, 2012
Start Date: Oct 01, 2012

Essential Requirements:
  • University Degree or Higher Diploma
  • Strong communication skills, with excellent written and spoken English and Swahili
  • 3-years work experience in leading programmes within a childcare setting
  • Proven computer skills in Microsoft Office applications
  • Proven skills in programme management and project administration
  • Ability to lead a programme and support an international volunteer team
  • Skills & experience in project/programme monitoring review, reporting
  • Ability to work with limited supervision, take initiative, prioritise and be proactive
  • Strong organisational and time management skills
  • Flexibility and experience of working within a challenging and fast paced environment
  • The ability to work within a culturally diverse team spread across different function
If are interested in any of these roles, please visit our website www.tumainilamaisha.orgwhere you can view and download the job description.  CV’s and covering letter should be returned via email to: the Email link aboveby 12:00 noon EAT on 17th August 2012.
Only candidates shortlisted for interview will be contacted. 
Paediatric Oncology Patient Liaison Officer
Date Listed: Aug 1, 2012
Phone: +255 22 277 5965
Application Deadline: Aug 17, 2012
Start Date: Oct 01, 2012


Essential Requirements:
  • Senior nurse or social worker who has minimum 3 years experience in managing children with cancer.
  • Strong communication skills, with excellent written and spoken English and Swahili
  • Experience of establishing strong working relationships with colleagues from different functions and cultures
  • The ability to work in a busy and stressful environment.
  • Experience of a flexible approach to managing and prioritising a high workload and multiple tasks
  • Experience of proactively identifying and addressing issues 
If are interested in any of these roles, please visit our website www.tumainilamaisha.orgwhere you can view and download the job description.  CV’s and covering letter should be returned via email to: to the Email Link above by 12:00 noon EAT on 17th August 2012.
Only candidates shortlisted for interview will be contacted. 
Project Engineer
Date Listed: Aug 1, 2012
Phone: +255 22 285 1212
Application Deadline: Aug 20, 2012


The Managing Director
Tanzania Petroleum Services Limited
Box 72376
Dar Es Salaam

Project Manager
Date Listed: Jul 31, 2012
Application Deadline: Aug 15, 2012
Position Description:
Intelectual Property Lawyer preferably specialized in Biotech and pharmaceutical Patent law. The applicant should be a self starter with a minimum of 2 years work experience.
Send your application by email attaching copies of your professional/academic certificates to mnshangeki@costech.or.tz and copy to daf@costech.or.tz
Executive Director
Date Listed: Jul 31, 2012
Phone: +255 717 781 524
Application Deadline: Aug 15, 2012


 General qualifications
A bachelors degree/advanced diploma in social science from a recognized university preferably social work, sociology, project planning. Candidates with a fairly good working experience (at least two to three years) with children’s issues are highly encouraged to apply. Other qualities include:
  • Good communication in spoken and written Kiswahili and English language.
  • Good judgment and analytical skills.
  • Proposal writing skills, Project planning and management experience
  • Good interpersonal and demonstrative ability to work independently
 Closing date: 15th August 2012,
ANPPCAN – Tanzania chapter
New Bagamoyo road Makumbusho area. DSM
E-mail: anppcantanzania@gmail.com
Exploration and Mining Geology Tutor
Date Listed: Jul 26, 2012
Phone: +255 755 646 470
Application Deadline: Aug 24, 2012


Qualification and Experience:
·        Holder of a degree in geology or geo-sciences from a recognized institution.
·        Must be computer literate with good command in English language.
·        A Masters degree in the related field will be an added advantage.
Executive Secretary,
Earth Sciences Institute of Shinyanga,
P. O. Box 1026,
SHINYANGA.
Or
by email to:
info@esis.ac.tz
For more details visit our website www.esis.ac.tz

Tuesday, July 17, 2012

Wabunge wote vijana kupigishwa kwata JKT


NI KUANZIA MWAKA HUU WA FEDHA,PIA WAMO WA  KIDATO CHA SITA
Neville Meena na Boniface Meena, Dodoma
WABUNGE vijana walioko katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania watapaswa kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa Mujibu wa Sheria kuanzia mwaka huu wa fedha wa 2012/13.
Waziri wa Ulinzi na JKT, Shamsi Vuai Nahodha alisema hayo alipokuwa akiwasilisha hotuba ya makadirio ya wizara yake bungeni jana. Alisema wabunge vijana watakuwa sehemu ya kundi la kwanza la vijana 5,000 katika mafunzo yatakayoanza Machi, mwakani.

Alisema wizara hiyo imelifanyia kazi ombi la kuandaa mafunzo ya JKT kwa wabunge vijana kama ilivyoombwa mwaka jana na kwamba wabunge hao wameandaliwa mafunzo hayo ya wiki tatu.
“Nafurahi kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba Wizara yangu imelifanyia kazi ombi hilo na kuandaa utaratibu wa mafunzo maalumu ya wiki tatu kwa waheshimiwa wabunge vijana,” alisema Nahodha na kuongeza:

“Kwa hiyo wabunge vijana wataungana na kundi la kwanza la vijana 5,000 niliowaeleza hapo juu… naomba waheshimiwa wabunge mjiorodheshe kwa maandalizi ya mafunzo haya.”
Waziri Nahodha alisema ni imani yake kuwa, pamoja na wabunge kunufaika na mafunzo hayo, watahamasisha urejeshwaji wa mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria na kutoa taswira nzuri ya mafunzo hayo kwa jamii.

Alisema JKT tayari imefanya maandalizi ya kutosha na kwamba kambi tano zenye uwezo wa kuchukua vijana 20,000 kwa wakati mmoja zimeshaandaliwa kwa ajili hiyo.
Alizitaja kambi hizo kuwa ni Bulombora na Kanembwa za mkoani Kigoma, Mlale ya Ruvuma, Msange mkoani Tabora na Oljoro hukoArusha.

Hata hivyo, alisema gharama ya kuendesha mafunzo hayo ni kubwa hivyo JKT haitaweza kuchukua vijana wote na ndiyo maana imeamua kuanza na hao 5,000.
“Vijana hao ni miongoni mwa vijana 41,348 ambao watahitimu mafunzo ya kidato cha sita katika mwaka 2013,” alisema Nahodha.

Kuhusu utaratibu wa kujiunga na kambi hizo, Nahodha alisema uandikishaji wa vijana shuleni utafanyika kati ya Desemba mwaka huu na Januari 2013 na kwamba kambi zitawapokea kati ya Machi 7 na 16, mwakani.Alisema mafunzo hayo ya miezi sita yataanza Machi 17 mwakani na kuendelea hadi Agosti 16.

Wanajeshi Syria

Katika hatua nyingine, Nahodha alisema wanajeshi wa Tanzania kati ya 100 na 200 wanatarajiwa kwenda Syria kuwa waangalizi wa amani ikiwa ni kuitikia ombi la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa Serikali.

Alisema ombi hilo linatokana na utendaji mzuri wa jeshi hilo na kwamba tayari Serikali imelikubali.
Nahodha alisema tayari Makao Makuu ya Jeshi yameanza maandalizi ya kuwapeleka waangalizi hao.
Alisema Tanzania ina wajibu wa kushirikiana na nchi nyingine kulinda amani duniani na imekuwa ikishiriki katika operesheni mbalimbali za kulinda amani.

Katika hatua nyingine; Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Christowaja Mtinda alilalamikia kitendo cha Wahindi kuuza bidhaa za maduka ya jeshi kwa gharama za juu, wakati bidhaa hizo hazilipiwi kodi.
Alisema ni lazima Serikali ieleze Wahindi hao wanauzaje bidhaa za kwenye maduka ya jeshi kwa gharama kubwa wakati maduka hayo yanatakiwa yauze bidhaa hizo kwa bei ya chini.

“Ukienda sasa hivi wanauza sukari Sh1,800 wakati nje ya maduka hayo sukari kilo ni Sh2,000, hili haliwezekani. Wanauza friji, tv kwa bei ya juu na TRA, maofisa wa jeshi wa ngazi za juu wote wanajua,” alisema.

Mtinda alitaka suala hilo litafutiwe ufumbuzi ili bidhaa ziuzwe kwa bei inayotakiwa. Pia alilalamikia nyumba za maofisa wa jeshi akisema haziridhishi na kwamba zinahitaji kukarabatiwa upya.

“Nyumba za maofisa wa jeshi zinatia aibu, hazijakarabatiwa kitu ambacho kinasababisha wafanye ukarabati kwa fedha zao wenyewe,” alisema.

Wapinzani wang’aka

Kwa upande wake, Msemaji wa Kambi ya Upinzani kuhusu wizara hiyo, Mchungaji Israel Natse aliitaka Serikali kutoa maelezo ya matumizi ya Sh4.048 bilioni ambazo zilitumika kuondoa matrekta bandarini.
“Hakika fedha hizi ni nyingi sana kwa kazi ya kuondoa tu matrekta bandarini, Kambi ya Upinzani inataka kupata majibu ni matrekta mangapi yaliondolewa na gharama ya kuondoa trekta moja ilikuwa kiasi gani?” alisema Natse alipokuwa akitoa maoni ya kambi hiyo.

Natse ambaye pia ni Mbunge wa Karatu (Chadema) alisema malipo hayo yanatia shaka na kwamba Serikali lazima ieleze fedha hizo zilikuwa ni kwa ajili ya matumizi gani.
Kuhusu migogoro ya ardhi, mbunge huyo alisema kumekuwapo na migogoro kwa muda mrefu baina ya wanajeshi na wananchi kwenye maeneo mbalimbali ya nchini na kwamba ni kama hakuna dalili kwamba kuna nia ya dhati ya kumalizwa kwa matatizo hayo.

“Migogoro hii imesababisha kuwapo kwa mvutano baina ya wananchi na jeshi letu kwa upande mmoja na viongozi wa wananchi kwa upande wa pili,” alisema Natse.
Alitoa mfano wa maeneo hayo kuwa ni Ilemela, Tarime, Kunduchi na mengine mbalimbali ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na wabunge kwa muda mrefu.

“Mara zote Serikali imekuwa ikitoa majibu kuwa itawalipa fidia wananchi ili waweze kuondoka na kuyapisha maeneo hayo kwa ajili ya jeshi, kwa mwaka huu wa fedha 2012/13 zimeombwa kiasi cha Sh1 bilioni kwa ajili ya kulipa fidia ya ardhi maeneo ya Mapinga, Shinyanga na Arusha.”
Alisema kutokana na fedha hizo ni dhahiri kwamba hakuna nia ya dhati ya kumaliza migogoro baina ya jeshi na wananchi kwani kiasi hicho kilichotengwa ni kidogo na ni kwa ajili ya kulipa fidia na sehemu chache tu.

“Tunaitaka Serikali iwe na nia ya dhati ya kuwalipa wananchi fidia ili kumaliza migogoro hii ambayo inawafanya wananchi walichukie jeshi lao,” alisema.