Sunday, August 11, 2013

New case of H7N9 bird flu confirmed in China: officials


BEIJING - A Chinese poultry worker was confirmed as having contracted the deadly H7N9 bird flu virus, health officials said, the first case in the southern Guangdong province.
The 51-year-old woman is in a critical condition after she was admitted to hospital on August 3 following signs of a fever, the Guangdong Provincial Health Department said on Saturday.
"She was a poultry slaughtering worker at a local marketplace," the local health bureau said in a statement on its website.

A total of 134 cases have now been reported on the Chinese mainland, including the Guangdong case.
State news agency Xinhua said Saturday that 44 people had died of the disease - which includes a recent fatality following the release of the latest official figures a month ago.

The virus was first reported in late March, with most cases confined to eastern China, and only one reported outside the mainland, in Taiwan.
Scientists reported last week the first likely case of direct person-to-person transmission of the H7N9.
However, they told people to "not panic" as the virus's transmissibility remained "limited and non-sustainable".

Local health authorities Saturday lifted medical observations on 54 of 96 people who were placed under monitoring after they had close contact with the Guangdong patient, Xinhua said.
The patient had worked in markets in Boluo, which is about 129 kilometres (80 miles) east of the provincial capital Guangzhou.

Many of those infected with the virus had direct contact with birds, commonly at poultry markets, which have been closed by officials across China to halt the spread of the disease.
Cases of H7N9 have dropped significantly in recent weeks.

In the southern Chinese city of Hong Kong, which borders Guangdong province, a government spokesman Sunday said the territory is closely monitoring the virus for any developments.

Waingereza waliomwagiwa tindikali waitesa Serikali


Dar es Salaam. Siku tano baada ya raia wawili wa Uingereza kumwagiwa tindikali visiwani Zanzibar, Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi imeibuka na kueleza kuwa bila wananchi kutoa taarifa za ushahidi wa uhalifu wa aina mbalimbali, ni vigumu kuwabaini wahusika.

Kauli hiyo ilitolewa kwa pamoja jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) Eliezer Feleshi, katika mkutano wao na waandishi wa habari, uliolenga kueleza mikakati ya kupambana na matumizi yasiyo sahihi ya tindikali nchini.

Katika ufafanuzi wao walisema, “Kutoa taarifa ya uhalifu wa jambo lolote siyo hiari, ni jukumu la kisheria na kikatiba,” huku Feleshi akitolea mfano jinsi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk Steven Ulimboka alivyoshindwa kutoa ushahidi wa tukio lililomkuta la kutekwa, kupigwa na kisha kutupwa katika Msitu wa Mabwepande, hivyo kufanya uchunguzi kuwa mgumu.

Agosti 7, mwaka huu raia wawili wa Uingereza, Kate Gee (18) na Kirstie Trup (18) walimwagiwa tindikali katika maeneo ya Mji Mkongwe, Zanzibar na vijana wawili waliokuwa wakiendesha pikipiki aina ya Vespa, Waingereza hao wa walisafirishwa siku tatu zilizopita kurudi kwao kwa ajili ya matibabu.

Kuhusu polisi inavyopambana na uhalifu huo aliouita kuwa ni ‘Uhalifu mpya nchini’, IGP Mwema alisema:
“Mkemia Mkuu, Polisi hawawezi kubaini matukio haya bila ushirikiano wa wananchi kwani Tanzania ni nchi kubwa na ina watu zaidi ya milioni 45. Watu wanaingiza tindikali lakini wapo ambao wanatumia tindikali hiyo kwa matumizi haramu.”

Alisema tindikali inaweza kutolewa kwa ajili ya shughuli za viwandani, maabara na usafirishaji na kwamba watu wanapotaka kuitumia kwa ajili ya kufanya uovu wanaweza kugundulika kupitia kwa taarifa zitakazotolewa na wananchi, kwa sababu wanakuwa wamezungukwa na jamii ya watu mbalimbali.
“Kama wanataka kuitumia tindikali kwa ajili ya matumizi mabaya wananchi wanaweza kugundua kwa sababu wanakuwa wanaishi karibu na watu hao, mwananchi mwema anaweza kuwa chanzo kizuri cha kuweza kuzuia na kutoa taarifa za kuwabaini wahusika,” alisema Mwema.

Alisema wananchi wanatakiwa kutambua kuwa shughuli za kibiashara za kuwawezesha kupata kipato cha kila siku hazitafanikiwa kama hakutakuwa na ustawi wa amani.
“Tishio la tindikali linaweza kutia hofu na taharuki katika jamii, hatutaki jambo hili liendelee nchini, tunaamini wazi kuwa hakuna mtu anayeweza kufanya uhalifu akawa peke yake bila kujulikana na mtu hata mmoja,” alisema na kuongeza:

“Tunaweza kubaini kupitia kwa mhusika (mwathirika), mhalifu mwenyewe (anayetenda tendo husika) na mazingira yaliyowezesha mtu ammwagie mwingine tindikali, tukitumia nafasi hizo vizuri, moja kati ya vyanzo hivyo vinaweza kutusaidia kutambua wahusika.”

Japan kujenga kiwanda cha pikipiki


Dar es Salaam. Serikali ya Japan imesema ina mpango kabambe wa kukuza uchumi wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na kampuni kubwa duniani za Honda na Panasonic kujenga viwanda vitakavyokuwa matawi yake hapa nchini.
Uamuzi na msimamo wa Japan umetangazwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa nchi hiyo, Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu.

Taarifa ya Ikulu iliyosambazwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Motegi akisema: “Kwa kuanzia kampuni mbili za Honda na Panasonic zimekubali kujenga viwanda nchini, kimoja kwa ajili ya kutengeneza pikipiki za Honda na kingine kwa ajili ya kutengeneza vifaa vya umeme.”

Akaweka msisitizo: “Huu ni mwanzo tu Mheshimiwa Rais (Kikwete) kwa sababu kama nilivyosema kuwa tunataka Tanzania kuwa nchi ya mfano ya uwekezaji wa Japan katika eneo hili la dunia, na namna hiyo kwa pamoja tutakuwa tumeshirikiana katika kuongeza ajira kwa wananchi wa Tanzania.”

Waziri huyo pia alisema kuwa baadhi ya kampuni za Japan zina mipango ya kuwekeza katika kilimo, na hasa kilimo cha pamba na kuanzisha viwanda vya nguo hapahapa nchini.
Motegi alisema mikakakati mingine ya kuisaidia Tanzania ni pamoja na kushiriki uboreshaji wa Reli ya Kati, kusaidia kupanua na kuboresha Bandari ya Dar Es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Ikulu, mkakati huo wa Japan unatokana na ziara ya Rais Kikwete nchini humo, Juni mwaka huu.
“Japan imeamua kuanzisha ushirikiano mkubwa zaidi na Tanzania ambako nchi hiyo itaifanya Tanzania kuwa nchi lengwa ya kuwekeza na kuifanya kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji katika Afrika,” inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo iliweka wazi kuwa Waziri Motegi alimweleza Rais Kikwete kuwa ametumwa na Waziri Mkuu Abe, kufuatilia mazungumzo kati yao na kutangaza rasmi kuwa Japan imeiteua Tanzania kuwa nchi lengwa na kitovu cha uwekezaji Afrika Mashariki na Afrika kwa jumla.
Waziri Motegi amesema kuwa katika kufanikisha mkakati huo aliandamana na kundi la wafanyabiashara wa Japan ambao wanaendelea kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa Tanzania, kuona jinsi gani wanavyoweza kusaidiana katika kuwekeza katika uchumi wa Tanzania.

Ponda adaiwa kujeruhiwa kwa risasi


Morogoro. Hali ya wasiwasi imetanda mjini Morogoro baada ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, kudaiwa kupigwa risasi begani wakati polisi wakiwa katika harakati ya kumkamata.
Habari kutoka katika eneo hilo zinadai kuwa Ponda alipigwa risasi saa 12:25 jioni, wakati akisindikizwa na wafuasi wake kuelekea katika Msikiti wa Mungu Mmoja Dini Moja, baada ya kumaliza kutoa mhadhara katika kongamano lilifanyika mjini Morogoro jana.
Tukio hilo lilitokea katika Barabara ya Tumbaku, baada ya kumalizika kwa mkutano wa kongamano lililoandaliwa na Jumuiya ya Wahadhiri wa Kiislamu Mkoa wa Morogoro.
Mwenyekiti wa Kongamano hilo, Sheikh Idd Mussa Msema aliliambia Mwananchi Jumapili jana kuwa Ponda alipigwa risasi sehemu ya bega, na askari polisi na kwamba aliwahishwa kutibiwa katika Hospitali ya Kiislamu iliyopo eneo Msamvu mjini Morogoro.
Hata hivyo, wakati Sheikh huyo akisema hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alikanusha madai ya kuwa polisi wamempiga risasi.
Alisema polisi walifika katika eneo hilo kwa ajili ya kumkamata Ponda, baada ya kumaliza mhadhara wake na kwamba wakati wakitaka kumkamata ndipo wafuasi wake wakawazuia polisi na kulazimika kupiga mabomu ya machozi na risasi hewani kuwatawanya.
Katika tukio hilo inadaiwa kuwa Sheikh Ponda aliyekuwa katika gari ndogo huku wafuasi wake wakimsindikiza kwa miguu, walipofika eneo la gereji mabomu ya machozi yalipigwa na polisi waliokuwa katika magari aina ya defender wakati wakijaribu kuwatawanya wafuasi hao.
Baada ya tukio hilo baadhi ya wafuasi wake walimchukua Sheikh Ponda kutoka katika gari lake na kumkimbizia katika gereji moja, kisha wakatoka wakiwa wamempakia katika pikipiki na kumpeleka katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro.
Mlinzi mmoja wa lango namba moja alisema kuwa ulifika msululu wa pikipiki zaidi ya 50, lakini pikipiki zote zilizuiliwa isipokuwa iliyokuwa imembeba Sheikh Ponda na kwenda naye mpaka mapokezi.
Aidha, alisema wakiwa katika eneo hilo magari kadhaa ya polisi yaliingia katika lango la hospitali hiyo. Hivyo wafuasi wa Sheikh Ponda wakalazimika kumbeba begani na kutoroka naye kupitia lango namba mbili.
Taarifa zilizopatikana baadaye zinadaiwa kuwa Sheikh Ponda alikimbizwa katika Hospitali ya Kiislamu ya Msamvu.
Baadhi ya watu walidai kumwona Sheikh Ponda akiingizwa katika Hospitali ya Rufaa Morogoro, lakini walishangaa alivyotoweka.

Thursday, May 23, 2013

Ghasia kubwa zazuka Mtwara


Mtwara. Hali ya usalama mkoani Mtwara ni tete. Mtu mmoja anaaminika kufariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa kutokana na vurugu kubwa zilizozuka jana huko Mtwara baada ya kusomwa hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini na Nishati bungeni Dodoma jana.
Aidha, askari wanne wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wamefariki dunia katika ajali wakitokea Nachingwea kwenda Mtwara ili kusaidia kutuliza vurugu hizo. Katika ajali hiyo, askari 20 walijeruhiwa, wengi wao vibaya na saba walinusurika.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Dk Mohamed Kodi alithibitisha kupokea maiti moja na kuomba apewe muda kutaja idadi ya majeruhi.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa alidai kwamba hakuna mtu aliyefariki dunia wala majeruhi. Alisema watu 45 wamekamatwa.
Milio ya risasi za moto na mabomu ya machozi vilisikika kila kona na hasa Mitaa ya Mdenga, Magomeni na Shengena Mjini Mtwara ambako hali ilikuwa mbaya kutokana na kuwapo kwa mapambano kati ya polisi na vijana.
Vurugu hizo zilitokana na hatua ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kusisitiza kuwa bomba la gesi kutoka Mtwara na kuja Dar es Salaam litajengwa, jambo lingine linalodaiwa kusababisha ghasia hizo ni hatua ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kutokurusha moja kwa moja matangazo ya Bunge hivyo kuwakosesha wananchi fursa ya kusikiliza bajeti hiyo.
Akizungumzia kukosekana kwa matangazo hayo ya televisheni, Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Clement Mshana alisema kukatika kwa matangazo hayo kulitokana na tatizo la satelaiti katika mji huo na Musoma.
Hata hivyo, wakazi wa Mtwara waliokuwa na ving’amuzi walipata fursa ya kuangalia matangazo hayo.
Pia vurugu hizo zilichangiwa na vipeperushi vilivyosambazwa na watu wasiojulikana wakitaka watu kuacha kufanya shughuli zozote na kukaa nyumbani ili kufahamu hatima ya mradi wa usafirishaji wa gesi kutoka Msimbati hadi Dar es Salaam kwa njia ya bomba.
Katika vurugu hizo zilizozagaa zaidi maeneo ya Mikindani na Magomeni, wananchi pia waliharibu Daraja la Mikindani linalounganisha Mikoa ya Dar es Salaam, Lindi na Mtwara.

Friday, February 22, 2013

35 Imaginative “Hands And Fingers” Photo Manipulations

By Alvaris Falcon.


Find the Perfect Stock Pictures. Royalty-Free Inspiration for Less!
Hands and fingers are the greatest assets of every human born in this world. With hands and fingers, human created great arts that shine in the human history. They are really great, but can they be artistic as well? It’s hard to answer this kind of questions with a ‘no’, especially in this technological age, when everything can possibly become an art with the might of creativity and the power of the Photoshop.
hands and fingers manipulation
In this showcase you won’t see any regular hands and fingers, as we brought to you 35 manipulation works with artistic attempts on hands and fingers. So let’s see what artists and designers can do when it comes to brush up their own hands and fingers!




25 Fingers. Aside from its seamless manipulation, this work is so great that it makes me actually think that having 30 fingers look really cool! Well I have to confess that as a developer, I will like to have a hand like this. (Image Source: Alexandre Guilbeault)
25 fingers

Multi Hands. Another really cool one with awesome manipulation applied. (Image Source: j.walsh)
multi hands

A Handful. “I would be so much better at piano…” (Image Source: pwnedbyryan)
a handful

Again, I Say… For everything you do, there might be an eye watching you. (Image Source: 0 W8ing)
again i say

Arms Break, Vases Don’t. Sometimes if you are too careless, your hand will go wrong on you! (Image Source: alltelleringet)
arms break, vases don't

Being M.C. Escher. So which one is the real hand? A nice one! (Image Source: billyboingo)
being m.c. escher

Candlehand. Looks great, and what’s greater with this photo: it’s completely real! (Image Source: Bradi)
candlehand

Chase Your Love. Killer metallic effect. (Image Source: SubhadipKoley)
chase your love

Cyborg Hand. The day you know you’re not your father’s son. (Image Source: Naikoivanenko)
cyborg hand

Don’t Preach. Which one is the real hand? Or which one is the photo? (Image Source: haribahagia)
don't preach

FingBods. “Hey man, what’s weird about me?” (Image Source: Sterzy Hunter)
fingbods

Finger Killer. It’s a magnum, for sure. (Image Source: thecolourushproject)
finger killer

Flaming Fingertips. This actually makes you think about it, wonderful piece. (Image Source: PhilipHolm)
flaming fingertips

Give Me A Hand. It’s like these hands got some personalities! (Image Source: tiagogmc)
give me a hand

Gold Fish In My Hand. Very sleek manipulation with amazing uses of colors! (Image Source: sertanarig)
gold fish in my hand

Handed. How many fingers in total? You will never get it right. (Image Source: Õri Balázs)
handed

Hands. I have to say, the 3rd hand is epic. Amusing and unique one! (Image Source: cute0designer)
hands

Hands. Could be what you’ll see when you did too much Photoshop stuff! (Image Source: justyourtype)
hands

I Love Chocolate!! The expressions are priceless, and I believe it will be troublesome to live with these kinda annoying fingers. (Image Source: Manu Pombrol)
i love chocolate

M&M’s Chocolate Candy. Cute or haunting? Different people will have different thought about this piece. (Image Source: erwin mallari)
m&m's chocolate candy

Mutant Cell Pearl. Yikes! (Image Source: Tavieo Sawyer)
mutant cell pearl

My Kind Of Angel. “As an artist, I soar high to the limitless boundaries of my imagination through art and I enable myself to fly with my bare hands.” (Image Source: Alvin Adriano)
my kind of angel

Orchestra. More hands are surely cooler. (Image Source: Manu Pombrol)
orchestra

Pyro. Great manipulation and lighting, gave me a feel that the photo is expressing something. (Image Source: Tom Miatke)
pyro

Save the Earth. Unique manipulation work with great details inside it. (Image Source: Fayaz Mohamed)
save the earth

Screaming Hand. You can’t have quiet environment with this kind of hand. (Image Source: Lintza)
screaming hand

Some Skills. I doubt its usability, great concept though! (Image Source: Julio Mello)
some skills

Spander. Never thought the evolution of the spider could be that similar with human hands. (Image Source: Coltography)
spander

Working Fingers. I always imagine if I could just lie on bed and type on the keyboard like this. Beautiful hand by the way. (Image Source: saibia)
working fingers

You Are What You Eat. Amusing idea with classic quote, well done! (Image Source: Dimaci)
you are what you eat

You Will Never Be Alone. There’s always a helping hand for you. (Image Source: Olivia Ariferiani)
you will never be alone

Reflection

So now you see, hands and fingers could not only make interesting stuff, they could also be interesting by themselves! In fact I was quite doubtful that what would be the manipulation works of hands and fingers look like when I just started to search for them here and there, and I didn’t regret to compile them into a showcase, just like they didn’t fail to inspire and/or amuse me!
Which one would you choose to customize your hand to? Oh! The question should be, which manipulation piece you like in this showcase! Do let us know your favorite(s)!

Computers Can Read Your Mind!


This site will attempt to read your mind, please follow the instructions carefully.
Click here when you are ready to start.

This will open up


I shall now attempt to read your thoughts. Please mentally select a card and concentrate on it.

After you have memorized your card, please click here.



The MASTER wizard has selected your card and has removed it from the pile.


Surprised? Try it again with another set of cards.

Tuesday, February 19, 2013

Asilimia 60 chali matokeo ya kidato cha nne


MATOKEO ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana yametangazwa. Watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata sifuri, huku wanafunzi 23,520 tu ambao ni sawa na asilimia 5.16 ndiyo waliofaulu na wengine 103,327 sawa na asilimia 26.02 wamepata daraja la nne.

Akitangaza matokeo hayo jana, Waziri wa Elimu Dk Shukuru Kawambwa alisema watahiniwa walikuwa 456,137, wa shule wakiwa 397,136 huku wa kujitegemea wakiwa 68,806.
“Matokeo ya mwaka huu yamekuwa mabaya sana, Serikali tunasikitika kutokana na hali hii lakini tuna mipango mbalimbali ya kuhakikisha tunaweza kutatua hili tatizo,” alisema Dk Kawambwa.

Dk Kawambwa alisema watahiniwa wote kwa ujumla waliosajiliwa walikuwa 480,036 kati yao wasichana 217,583 sawa na asilimia 45.33 na wavulana 262,453 sawa na asilimia 54.67 lakini waliofanya mtihani huo ni 456,137 sawa na asilimia 95.44, wengine 21,820 (asilimia 4.55) hawakufanya mtihani.

Alisema watahiniwa wa shule (school candidates) walikuwa 397,136 sawa na asilimia 96.57, miongoni mwao, 14,090 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo utoro, ugonjwa na vifo.

Ufaulu kwa madaraja
Kwa mujibu wa matokeo hayo, watahiniwa waliopata daraja la kwanza ni 1,641, wavulana wakiwa 1,073 na wasichana 568, daraja la pili ni 6,453, wavulana wakiwa 4,456 na wasichana 1,997.

Waliopata daraja la tatu ni 15,426, wavulana 10,813 na wasichana 4,613, waliopata wa daraja la nne 103,327, wavulana 64,344 na wasichana 38,983 huku waliopata sifuri wakiwa 240,903, wavulana 120,664 na wasichana 120,239.

Shule 20 bora
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, wizara ilitaja shule 20 zilizofanya vizuri badala ya 10 kama ilivyozoeleka, kati yake 18 zilikuwa za watu binafsi na mashirika ya dini na mbili za Serikali.

Shule hizo ni pamoja na St.Francis Girls ya Mbeya, Marian Boys ya Pwani, Feza Boys ya Dar es Salaam, Marian Girls ya Pwani, Rosmini ya Tanga, Canossa ya Dar es Salaam, Jude Moshono ya Arusha, St. Mar’s Mazinde Juu ya Tanga, Anwarite Girls ya Kilimanjaro na Kifungilo Girls ya Tanga.

Nyingine ni Feza Girls ya Dar es Salaam, Kandoro Sayansi Girls ya Kilimanjaro, Don Bosco Seminary ya Iringa, St. Joseph Millenium ya Dar es Salaam, St. Iterambogo ya Kigoma, St. James Seminary ya Kilimanjaro, Mzumbe ya Morogoro, Kibaha ya Pwani, Nyegezi Seminary ya Mwanza na Tengeru Boys ya Arusha.

Shule 10 za Mwisho
Kwa upande wa shule 10 za mwisho, iliyofanya vibaya zaidi ni Mibuyuni ya Lindi, Ndame ya Unguja, Namndimkongo ya Pwani, Chitekete ya Mtwara, Maendeleo ya Dar es Salaam, Kwamndolwa Tanga, Ungulu Morogoro, Kikale ya Pwani, Mkumba na Tongoni za Tanga.

Matokeo yaliyofutwa
Jumla ya watahiniwa 789 wamefutiwa matokeo kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na udanganyifu na kuandika matusi.

Baadhi ya udanganyifu huo ni karatasi za majibu kuwa na mfanano usio wa kawaida, kukamatwa na simu za mkononi kwenye chumba cha mtihani, kukutwa na karatasi au madaftari pamoja na kubadilishana karatasi za majibu.

Dk Kawambwa alisema matokeo ya watahiniwa 28,582 yamezuiwa kwa sababu ya kutolipa ada ya mtihani na wanatakiwa kulipa fedha hizo ndani ya mwaka mmoja.

Matokeo ya QT
Dk Kawambwa alisema waliosajiliwa kufanya Mtihani wa Maarifa (QT) walikuwa 21,310, wasichana 13,134 na wavulana 8,176 na waliofanya ni 17,137 sawa na asilimia 80.42... “Watahiniwa 5,984 kati ya 17,132 waliofanya mtihani huo wamefaulu.”

Kanisa lachomwa Zanzibar


SIKU tatu baada ya kuuawa kwa kupigwa risasi Padri Evarist Mushi Mjini Zanzibar, Kanisa la The Pool of Siloam lililoko katika Shehia ya Kianga, Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, limechomwa moto na watu wasiojulikana na kuharibu madhabahu yake.

Kuchomwa moto kwa sehemu ya kanisa hilo, kumetonesha kidonda cha kifo cha Padri Mushi ambaye aliuawa kwa kupigwa risasi kichwani, Jumapili asubuhi mjini Zanzibar. Padri huyo anazikwa leo.

Akizungumza katika kanisa hilo, Naibu Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai upande wa Zanzibar ambaye pia ni Naibu Kamishna wa Polisi, Yusuf Ilembo alisema tukio hilo limetokea kati ya saa tisa usiku na saa 10 alfajiri ya kuamkia jana.

“Mlinzi aliona watu watatu wakiwa ndani ya eneo la kanisa na alipowakaribia wakaendelea kupanda ngazi kwenda juu. Baadaye walirudi na kuanza kumrushia mawe akakimbilia nje kupitia dirishani. Ghafla akaona moto unawaka, kumbe walikuwa wamechoma viti vya plastiki vilivyokuwa ndani,” alisema Naibu Kamishna Ilembo.

Mlinzi huyo, Mussa Jackson alisema: “Niliona watu watatu wakipita na baadaye wakawa wanarusha mawe, mwisho nikakimbia na kumwambia jirani na kumpigia simu mchungaji msaidizi. Wakati nakwenda kwa jirani nikaona moto mkali unawaka kanisani, sikujua wameuwashaje.”

Mchungaji Msaidizi wa Kanisa hilo, Penuel Elisha alisema tukio hilo ni la pili kwa kanisa hilo kwani mwaka 2011 zaidi ya watu 80 wakiwa na mapanga, nyundo na magongo walilivamia na kulivunja kabisa.

Alilishukuru Jeshi la Polisi kwa kuwahi kuwasaidia katika tukio la jana. Licha ya kutotaka kuonyesha uhasama na msikiti uliopo eneo hilo, Penuel alisema siku moja kabla ya tukio hilo viongozi wa msikiti huo walihoji uhalali wa kujengwa kwa kanisa hilo.

“Siku moja kabla ya tukio la mwaka 2011, viongozi wa msikiti walihoji uhalali wa sisi kujenga kanisa hapa. Sisi tukawaonyesha vibali vyote. Lakini kesho yake kanisa likabomolewa. Hatuna mgogoro na msikiti, kwanza hayo matukio ni ya kawaida tu hapa Zanzibar,” alisema Penuel.

Alipoulizwa kuhusu kuwapo kwa uhasama kati ya msikiti na kanisa hilo, Imamu wa msikiti huo, Hassan Migirimu alikanusha akisema kuwa mzozo huo ulikuwa kati ya kanisa na Sheha Assed Mvita ambaye amefariki dunia.

“Sisi hatuna mgogoro na hilo kanisa aliyekuwa akihoji uhalali wake ni marehemu Assed Mvita. Hatujawahi kugombana na kanisa hilo hata siku moja,” alisema Imamu Migirimu.

Padri Mushi kuzikwa leo
Padri Mushi anatarajiwa kuzikwa leo eneo la Kitope na ibada ya mazishi itaanza saa nne asubuhi katika Parokia ya Mtakatifu Joseph Minara Miwili.

“Baada ya kikao cha Baraza la Walei tulikubaliana kuwa ibada ya mazishi itafanyika hapa Parokia ya St. Joseph Minara Miwili na mwili wake utazikwa Kitope wanakozi kwa viongozi wa kanisa,” Askofu wa Kanisa Katoliki Zanzibar, Augustino Shao alisema jana.
Akizungumzia sababu ya Padri Mushi kuzikwa Zanzibar badala ya kusafirishwa kwenda kwao Moshi mkoani Kilimanjaro, Askofu Shao: “Padri Mushi ameishi Zanzibar tangu akiwa na miaka 18 hivyo ni mkazi wa Zanzibar... Hakuna sababu ya kusafirishwa. Mimi ndiye niliyekuwa mlezi wake hivyo hakuna sababu ya kumpeleka kuzika kwa askofu mwingine.”

Mmea wa kukuza sehemu za siri wagundulika


KWA kutumia mabango, lengo likiwa kutangaza kazi zao, waganga wengi wa tiba asilia wamekuwa wakijinadi kuwa wanatoa tiba ya kurefusha maumbile ya siri ya wanaume, kukuza makalio au matiti.
Katika mitaa ya miji na majiji nchini, siyo jambo la ajabu kukutana na mabango hayo, ambayo hata hivyo kushamiri kwake kunaleta picha kwamba ni kutokana na uhitaji mkubwa wa huduma hiyo nchini, huku watoa huduma husika wakinufaika kwa kujikusanyia kiasi kikubwa cha fedha kutoka kwa wahitaji.
Pia dawa zinazodaiwa kukuza makalio maarufu kama ‘mchina’, zimekuwa gumzo baada ya kuingia nchini, huku zikielezwa kukosa ubora na kwamba zina madhara makubwa.
Lakini, sasa unaweza kuachana na dawa hizo za Kichina, baada ya kugundulika mmea wenye uwezo wa kukuza makalio, matiti, pamoja na kurefusha uume.
Taarifa za kiutafiti zinautaja mti huo kwa jina la Mvunge, ukiwa na uwezo wa kukuza makalio, matiti na kurefusha uume.
Kaimu Msajili wa Tiba Asili na Tiba Mbadala nchini, Dk Naomi Mpemba anasema kuwa mmea huo ambao huwa ni mti mkubwa upo na kwamba una uwezo mkubwa wa kukuza maumbile hayo.
Anabainisha kuwa mmea huo ambao hukua na kuwa mti mkubwa huzaa matunda yanayotumika kama dawa na unapatikana wilayani Korogwe Mkoa wa Tanga, Pwani, Mbeya, Morogoro na baadhi ya mikoa nchini.
“Tulifuatilia na kutambua kuwa mti huo upo maeneo hayo na unatumiwa zaidi na waganga, hata picha za mti huo tunazo,” anasema Dk Mpemba na kuongeza:
“Jina jingine unaitwa Miegeya, mara nyingi unastawi katika maeneo yenye ardhi ya unyevunyevu, una tabia ya kustawi kama Mwembe na matunda yake huonekana kufanana na Mbuyu.”
Hata hivyo, anasema kuwa asilimia kubwa ya waganga wa tiba asili na tiba mbadala wanaotumia dawa hiyo ni wale wasiokuwa na usajili kutoka baraza hilo, hivyo kufanya huduma hizo kinyume cha utaratibu.
“Kwa mujibu wa masharti yaliyopo katika agizo la Serikali kwa waganga hao, miiko, maadili na utendaji wa kazi zao umeelekeza kuwepo na usiri na kuaminiwa, kwa hiyo sisi tunaamini wanaojitangaza kutibu mambo hayo ni matapeli,”anasema Dk Mpemba.