Monday, May 28, 2012

Kisumo: Ngeleja, Maige wanamdhalilisha rais


MWANASIASA mkongwe nchini, Peter Kisumo amehoji hatua ya mawaziri wawili waliong'olewa na Rais Jakaya Kikwete kutokana na kuhusishwa na tuhuma za rushwa, kupokelewa majimboni kwao kama mashujaa.

Kauli hiyo ya Kisumo ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa CCM, imekuja kipindi ambacho kumekuwa na utaratibu kwa baadhi ya watu kufanya sherehe na kupokelewa kama mashujaa baada ya kujiuzulu au kung'olewa.

Akizungumza na Mwananchi jijini Dar es Salaam jana, Kisumo alisema kitendo kilichofanywa na waziri wa zamani wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Ezekiel Maige wa Maliasili na Utalii,  kupokelewa kama mashujaa ni kumdhalilisha rais.

Kisumo alisema kama CCM kingekuwa na Kamati ya Maadili iliyo hai ilipaswa kuwaita wabunge hao na kuwahoji juu ya kitendo hicho.

"Siamini kama mapokezi yao hayakuwa na mkono wao, siamini hata kidogo..., kama kamati yetu ya maadili ingekuwa hai lazima ingewaita wajieleze," alisema Kisumo.

Alisema kama CCM na Serikali yake itaacha utamaduni huo uanze kujengeka katika jamii wa kuwapokea kishujaa viongozi waliondolewa madarakani kwa kuhusishwa na vitendo viovu, itakuwa ni jambo la hatari kwa mustakabali wa nchi.

Kisumo alisema hata mapokezi ya kishujaa waliyopewa Waziri mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa na Waziri wa zamani wa Miundombinu, Andrew Chenge yalikuwa si sahihi na ni kumweka rais na serikali katika majaribu makubwa.

"Yeye rais anasimamia suala la maadili, watu wengine wanaona ni kero, hapa kuna tatizo kubwa la kimaadili... tukifika mahali wananchi hawaoni rushwa na ufisadi kama ni dhambi na wanawapokea kama mashujaa, ni jambo la hatari," alionya.

Alisema kuondolewa kwa mawaziri hao kuliridhiwa na vikao vya juu ndani ya CCM na serikali, hivyo wananchi katika majimbo yao kuwapokea kishujaa kunatia mashaka kama viongozi hao hawakushiriki kuwahamasisha kufanya hivyo.

"Haiwezekani kijana mdogo kama Ngeleja umepata uwaziri katika umri mdogo unaondoshwa unaanza kufanya wana CCM jimboni wanung'unike kana kwamba umeonewa, kwani rais alipokuchagua aliwaconsult (aliwaomba ushauri) wananchi waliokupokea kishujaa? "alihoji Kusumo.

Kwa mujibu wa Kisumo, kwa hali inayoendelea sasa ni kama CCM imenyimwa haki yake kukabiliana na ukiukwaji wa maadili kwa wanachama wake, na hata jitihada inazozifanya hazionekani waziwazi kwa wananchi.

"Suala la kufikiri usimamiaji wa maadili ya viongozi ni lazima kuwe na ushahidi kama wa kimahakama, ni udhaifu na lazima viongozi wetu sasa wajue chama kinahitaji dhamira ya kweli katika hili," alisema.

Kudhibiti fedha chafu
Katika hatua nyingine, CCM kimetangaza rasmi kuanzisha kampuni za biashara na kuimarisha mapato kwenye miradi yake ili kuwa na nguvu ya kifedha na hivyo kujiepusha na fedha chafu zinazoweza kutoka kwa wafadhili.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisi ndogo za CCM Lumumba, Kisumo alitangaza mpango huo ambao sasa chama kitajikita katika kufufua vitega uchumi vyake.

“Kuna wafadhili ambao wamekuwa wakiichangia CCM na Chadema hadharani kama akina Sabodo, lakini wako wengine wanachangia kwa siri, sasa kuna hatari ya kupokea fedha chafu kutoka kwao,” alionya Kisumo.

Alisema chama hicho kinahitaji fedha lakini siyo fedha chafu ambazo zimepatikana kwa kukwepa kodi.

Hata hivyo, alisema,  “Tunawashukuru watu marafiki ambao wamekuwa wakikisaidia chama.”

Kisumo aliongeza kusema,"Tunahitjai fedha lakini hatuhitaji fedha chafu tunataka fedha zitakazopatikana kwa uwazi na sio kama kampuni fulani (anaitaja) inakupa fedha ili uipe upendeleo."

Alisema ili kuondokana na utegemezi, chama hicho kitafungua kampuni zake na kuingia ubia na kampuni nyingine za kitaifa na kimataifa.

“Kampuni hizo zitakuwa huru kufanya biashara kwa kufuata sheria na kanuni huku zikiwa chini ya wadhanimi, lakini utendaji wake hautaingiliwa na chama,” alisema.

Alisema pia chama hicho kinataka kuimarisha usimamizi wa mapato kwenye miradi yake iliyoko kwenye mikoa mbalimbali nchini.

Kisumo alisema kwa mujibu wa tathimini iliyofanywa mwaka 2007, chama hicho kina miradi yenye thamani ya Sh 57 bilioni lakini mapato yake ni madogo ilikinganishwa na thamani ya miradi.

“Tunataka kuimarisha usimamizi kwenye miradi ya chama ili kuongeza mapato,” alisema Kisumo ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) katika utawala wa Mwalimu Julius Nyerere.

Alisema miradi ina thamani kubwa lakini, inashindwa hata kulipa mishahara badala yake baadhi ya mikoa inapelekewa ruzuku.

Kisumo alisema chama hicho hakiwezi kuendelea kuwategemea wafadhili kwani, kuna uwezekano mkubwa wa kupokea fedha chafu.

“Wako marafiki wanaoweza kutupatia fedha walizozipata kihalali, lakini wakataka upendeleo fulani, pia wapo wengine ambao wanaweza kutupatia fedha ambazo zimepatikana kwa njia zisizo halali, hizo zote ni chafu hatuzihitaji,” alisema Kisumo.

Alisema utaratibu huo wa kuanzisha miradi badala ya kutegemea ada za wanachama na wafadhili, wamejifunza kutoka Msumbiji, Afrika Kusini na Namibia.

“Chama cha Swapo Namibia, ANC cha Afrika Kusini na Frelimo cha Msumbiji vyote vinamiliki kampuni na kuendesha biashara. Hawategemei ada za wanachama wala wafadhili kama sisi, ingawa sisi ni wakongwe kwao imebidi tujifunze kutoka kwao,” alisema Kisumo. 

Mwenyekiti huyo alisema michango ya wanachama bado ni midogo ambayo haiwezi kukiendesha chama hicho.

Alisema kwa siasa za hivi sasa, chama hakiwezi kujiendesha kwa kutegemea ada za uanachama pekee yake.

Alipoulizwa CCM itawezaje kuendesha miradi wakati ilishindwa kuendesha shirika lake la uchumi (Sukita), Kisumo alisema katika kipindi hicho mashirika mengi yalikufa kwa sababu ‘yalidekezwa’ na serikali.

“Mashirika yale yakitetereka kidogo yalikuwa yanapata fedha kutoka hazina, sasa hivi utapata wapi, ndiyo maana tukianzisha tunaweka waendeshaji wenye sifa kibiashara,” alisema.

Zanzibar yalipuka


MAKANISA YACHOMWA, WABARA WATAKIWA KUONDOKA
Salma Said, Zanzibar
ZANZIBAR imechafuka. Baada ya kuwapo kwa amani kwa takribani mwaka mmoja tangu kuundwa kwa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, vurugu na hali ya wasiwasi zimeibuka tena baada ya wanaharakati wa Kiislam kufanya maandamano kutaka uhuru wa visiwa hivyo.
Zanzibar ilijikuta katika hali tete kiusalama tangu mwaka 1995 baadaya kutangazwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa Rais, ambayo Chama cha Mapinduzi (CCM) kiilibuka kidedea na Chama cha Wananchi (CUF) kupinga, lakini uhasama huo ulizikwa Julai 31 mwaka 2010, baada ya kura ya maoni ya kuunda Serikali hiyo ya umoja wa kitaifa.

Lakini kuanzia juzi usiku hadi jana jioni mji wa Unguja na viunga vyake ulitikiswa na mabomu ya kutoa machozi ambayo polisi waliyatumia kutawanya mamia ya wanaharakati hao wa Kiislam wakiongozwa na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar (JUMIKI).

Mabomu ya machozi yalipigwa mfululizo juzi usiku na kuendelea kutwa nzima jana, hivyo kuathiri shughuli za biashara, ibada katika makanisa mbalimbali na kusababisha hofu kwa wananchi.

Kwa muda wa saa takriban mbili hivi kati ya saa 3:00 na saa 5:00 asubuhi, helkopta ya polisi ilikuwa ikipasua anga la Zanzibar ambalo lilikuwa limetandwa na moshi uliotokana na mabomu ya machozi pia uchomaji wa matairi ya magari. 
Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar, Mussa Ali Mussa aliwaambia waandishi wa habari kuwa wafuasi hao wamefanya uharibifu mkubwa ikiwa pamoja na kuchoma moto makanisa mawili na kwamba, watu saba akiwamo Imamu wa Msikiti wa Bizeredi, Maalim Mussa Juma wanaotuhumiwa na matukio hayo wamekamatwa na jeshi hilo.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi Kiongozi wa Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG), Askofu Dickoson Maganga alisema watu wasiojulikana walivamia kanisa lao eneo la Kariakoo Mjini Zanzibar mnamo saa 4.30 usiku na kuvunja ukuta, kuchoma viti vya plasitiki pamoja na gari yake.

Chanzo cha vurugu hizo kinatajwa kuwa ni wanaharakati hao juzi kufanya mkusanyiko na maandamano makubwa ya kushtukiza ambayo yalizistua mamlaka za usalama visiwani humo, lakini baada ya kutawanyika jioni baadhi ya viongozi wa maandamano hayo walitiwa mbaroni.

Baada ya kukamatwa kwao, wafuasi wao walikusanyika makao makuu ya polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Madema, kushinikiza kutolewa kwa viongozi hao wanaoshikiliwa kituoni hapo.

Habari zaidi zinasema kutokana na hali ilivyo, askari polisi walitarajiwa kuongezwa visiwani humo, ili kusaidia kuimarisha hali ya usalama pia kuwadhibiti wahalifu ambao walikuwa wameanza kuelekea nje ya maeneo ya mji.

Tayari kuna taarifa kuwa askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kutoka Tanzania bara jana mchana walingia Zanzibar kwa ajili ya kuongeza ulizi katika mji wa Unguja.

Hata hivyo, katika hali ya kushangaza hakuna kiongozi yoyote wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) aliyetoa kauli kuhusu hali hiyo.

Kauli ya Polisi
Kamishna Mussa alisema jeshi lake litaendelea kuwasaka na kuwatia mikononi wote waliopanga fujo hizo pamoja na viongozi wote wa JUMIKI.

“Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar ndio iliyohusika na kuwachochea vijana kukusanyika na kufanya uharibifu ikiwemo kuchoma moto gari, kupanga mawe barabarani na kufanya hujuma mbalimbali kinyume cha sheria. Tutaendelea kuwasaka kwa gharama zote,” aliapa Kamishna Mussa.

Alifafanua kwamba kwa sasa mikusanyiko yote ya mihadhara ya kidini na vyama vya siasa, lazima ipate kibali cha polisi vyinginevyo jeshi lake litatumia nguvu za ziada kutawanya mikusanyiko hiyo ili kulinda sheria za nchi, amani na utulivu.

Hata hivyo, kamishna huyo wa polisi alijizuia kuhusisha harakati za Uamsho na chama cha siasa wala kutaja majina ya viongozi ambao tayari wanashikiliwa na jeshi lake.

“Mpaka sasa hivi sina majina yao kwa jumla, lakini tumewakamata viongozi wa Uamsho na tunatendelea kuwasaka lakini jina moja tu ndio ninalo ambalo ni Mussa Abdallah Juma,” alisema Kamishna huyo.

Hali bado tete
Wakati jeshi la polisi litoa onyo hilo, hali ya usalama ilionekana kuwa bado tete huku maeneo kadhaa ya Mji wa Zanzibar hasa Darajani na Michenzani ambako muda wote ni sehemu zenye harakati nyingi za biashara, jana zilikuwa zimebakia bila pilikapilika kutokana na askari waliojihami kufanya doria katika mitaa yote na kulipua mabomu kila penye kikundi cha watu waliokusanyika wakinywa kahawa.

Mitaa hiyo ilikuwa imechafuliwa kwa mawe, matofali na magogo yaliowekwa barabarani ili kuziba njia kwa ajili kuzuia magari yasipite huku mipira ya magari ikiwashwa moto na vijana hao.

Kwa upande wake Askofu Maganga akizungumzia uvamizi kisha uhalifu uliofanywa kanisani kwake alisema:
“Nasikitika sana kwa tukio hili ambalo tayari tumeiarifu polisi ambao jana (juzi), usiku walifika hapa wakishirikiana na kikosi cha kuzima moto na kufanikiwa kuuzima moto huo ambao kwa habati nzuri haujaathiri paa la kanisa letu,” alishukuru kiongozi huyo.

Alisema kundi la watu ambalo lilikuwa likitoa maneno ya kashfa na kutishia maisha ya waumini waliokuwa wakifanya ibada usiku huo, lilikatisha ibada hiyo pamoja na kusababisha uharibifu wa mali ya kanisa hilo yenye thamani ya zaidi ya Sh 100 millioni.

Kauli ya JUMIKI
Kutokana na hali hiyo, jumuiya hiyo jana ilitoa taarifa yake kwa vyombo vya habari ikikanusha kuhusika na kuchochea watu kuchoma kanisa wala kuharibu mali za watu.

Hata hivyo, Katibu wa Jumuiya hiyo, Abdallah Said alisema katika taarifa hiyo kwamba jeshi la polisi linapaswa kubeba lawama kwa yote yaliotokea kutokana na kuvunja sheria na kuwakamata viongozi bila ya utaratibu wa busara.

“Uislamu ni dini ya amani na inahimiza ushirikiano na utulivu na hatuwezi kuwatuma watu kwenda kuvunja makanisa na kuharibu mali, kwa sababu ndani ya imani zetu tunajua hilo ni kosa na jambo ambalo halifai katika maamrisho ya dini yetu,” alisema Sheikh Abdallah.

Taarifa hiyo ilisema pia kwamba jumuiya hiyo imekuwa wazi katika kudai maslahi ya Zanzibar na sio vinginevyo na kuahidi kufanya hivyo kwa njia za amani, na iwapo watakuwa wamekosea basi wapo tayari kufikishwa katika vyombo vya sheria.

“Ni lazima polisi wajue kwamba tupo tayari kufanya kazi kwa misingi ya kisheria na hata kwa kujisalimisha tupo tayari, lakini ukamataji bila kufuata busara na sheria haukubaliki. Tunachokitaka ni kura ya maoni haraka na hilo tutaendelea kulidai,” alisisitiza katibu huyo wa JUMIKI.

Wakati viongozi wa Uamsho wakiendelea kutafutwa na jeshi la polisi, nyumba ya kiongozi aliyeongoza maandamano juzi Sheikh Farid Hadi Ahmed inadaiwa kuvunjwa milango usiku wa manane alipokuwa akiswakwa jeshi hilo.

Hata hivyo, taarifa hizo hazikuthibitishwa iwapo ni polisi waliofanya kitendo hicho au la,  wanafamilia wanasema waligongewa milango na kutakiwa wafungue baada ya kutofungua walisikia kishindo kikubwa cha kusukumwa milango katika eneo la Mbuyuni Mjini Unguja.

Vijana katika mitaa ya Zanzibar jana walionekana wakiwa na hamasa kubwa wakidai kuendelea kuungana na viongozi wao kudai haki ya Zanzibar, pamoja na kutaka Zanzibar huru kutoka ndani ya mikono ya Muungano.

“Sisi tunachokitaka Zanzibar yetu watupige mabomu, watuue, watukamate lakini tunataka Zanzibar yetu na hatusikii lolote,” walisikika baadhi ya vijana.

Hada jana jioni vurugu katika badhi ya maeneo hususan Kwelekwe na njia ya Baa ya Amani zilikuwa zikiendelea na gari moja lilichomwa moto karibu na ofisi ya CCM.

Matukio kabla
Zanzibar imekuwa ikitawaliwa na matukio ya ghasia ambayo licha ya mihadhara hiyo ya Kiislam ilikuwa ni uhasama wa kisiasa kati ya vyama vikuu vya CUF na CCM, hatua ambayo iliwahi kusababisha mauaji ya Januari 27, mwaka 2001.

Lakini, uhasama huo wa kisiasa ambao ni wa kihistoria ulizikwa baada ya kura hiyo ya maoni na uchaguzi mkuu wa 2010 hatua ambayo imemfanya Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharrif Hamad kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa SMZ huku baadhi ya mawaziri pia wakitoka katika chama hicho.

Hata hivyo, wanaharakati hao wa Kiislam wameanza upya kuilipua Zanzibar wakishinikiza visiwa hivyo viwe taifa huru kwa kujitenga katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Zitto ataka tume ya uchunguzi
Katika hatua nyingine Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe amemtaka Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein aunde kikosi kazi maalum kwa ajili ya kudhibiti
vurugu hizo na kuanza mazungumzo na pande zote kwa kuwa, "Hiki sio kitendo cha kudharau
kabisa."

Alifafanua kwamba waliochoma nyumba za ibada wasakwe na kufikishwa mbele ya sheria mara
moja na kuongeza, "Tusiruhusu hata kidogo wapuuzi wachache kutuingiza katika vurugu za
kidini ili kufikia malengo yao ya kisiasa."

Thursday, May 24, 2012

Mnyika ambwaga tena Hawa Ngh'umbi mahakamani


Habari zilizotufikia muda si mrefu zinasema mbunge wa Jimbo la Ubungo John Mnyika (Chadema)  amemshinda tena Hawa Ng'humbi (CCM) baada ya Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam kutoa hukumu  kuwa ushindi wa Mbunge Mnyika  uliofanyika Oktoba 31, 2010 ulikuwa wa halali.Kwa taarifa zaidi ungana nasi baadaye.

=====================
Mbunge John Mnyika wa Chadema
NI KATIKA HUKUMU YA KESI KUPINGA MATOKEO YA UBUNGE WA JOHN MNYIKA
James Magai
MAHAKAMA Kuu, Kanda ya Dar es Salaam, leo itawaliza au kuwafurahisha wapenzi na wanachama wa Chadema wakati itakapotoa hukumu ya kesi ya kupinga matokeo ya ubunge yaliyompa ushindi Mbunge wa Jimbo la Ubungo kupitia chama hicho, John Mnyika.

Kesi hiyo namba 107 ya 2010, ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa CCM, Hawa Ngh’umbi dhidi ya Mnyika ambaye ni mdaiwa wa pili katika kesi hiyo akitetewa na Wakili Edson Mbogoro.

Mdaiwa wa kwanza katika kesi hiyo iliyoko mbele ya Jaji Upendo Msuya ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na aliyekuwa Msimamizi wa Uchaguzi (RO) katika jimbo hilo, (aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni) ambao walikuwa wakitetewa na Wakili Mkuu wa Serikali (PSA), Justice Mulokozi.

Katika uchaguzi huo, uliofanyika Oktoba 31, 2010, Msimamizi wa Uchaguzi, Raphael Ndunguru alimtangaza Mnyika kuwa mshindi Novemba 2, 2010 baada ya kupata kura 66,742. Ngh’umbi alipata kura 50,544.

Hata hivyo, Ngh'umbi hakuridhishwa na matokeo hayo akaamua kufungua kesi Mahakama Kuu kuyapinga, akimtumia Wakili Issa Maige.

Katika hati yake ya madai na wakati akitoa ushahidi  mahakamani, Ngh’umbi na mashahidi wake walidai kuwa kulikuwa na ukiukwaji mkubwa wa taratibu na kisheria katika ujumlishaji wa kura na utangazaji wa matokeo ambao umeathiri matokeo hayo.

Hoja za kuzingatia
Katika hukumu ya leo, Jaji Msuya atazingatia hoja tano ambazo zinatokana na madai katika hati ya Ngh’umbi alizozitoa wakati akitoa ushahidi wake mahakamani pamoja na mashahidi wake wawili, kuhusu ukiukwaji huo wa sheria.

Hoja hizo zitakazozingatiwa katika hukumu ya Jaji Msuya ni pamoja na kama mkanganyiko wa takwimu za kura katika Fomu namba 24B (Fomu za matokeo ya jumla ya ubunge), zimeathiri matokeo hayo ya uchaguzi mzima.

Hoja nyingine ni kama mlalamikiwa wa pili (Mnyika), aliingia na kompyuta (laptop) tano katika chumba cha majumuisho ya kura na kama ndizo zilizotumiwa na wasimamizi wa uchaguzi kuhesabu na kujumlishia kura.

Nyingine ni kama marekebisho ya kura katika baadhi ya fomu namba 21B, (Fomu za matokeo ya kura za ubunge vituoni), yalifanyika katika chumba cha majumuisho na mlalamikiwa Mnyika kuingia na kundi la wafuasi wake katika chuma cha majumuisho kinyume cha sheria.

Hoja nyingine ni kama mlalamikiwa wa pili (Mnyika) alitoa kauli za kashfa dhidi ya mlalamikaji (Ngh’umbi) kwa kumuita fisadi, akimtuhumu kuuza jengo la Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT).
Wakati akitoa ushahidi wake mahakamani, Ngh’umbi alidai kuwa matokeo hayo siyo sahihi kwa sababu pamoja na mambo mengine, katika fomu ya matokeo yaliyotangazwa kuna kura 14,854, zisizojulikana mahali zilikotoka ambazo upande wa mashtaka unadai ni kura hewa.

Alisema kwa mujibu wa fomu hiyo, kura halisi zilikuwa ni 119,823, kura halali zilikuwa ni 117,639 huku kura zilizokataliwa (zilizoharibika) zikiwa ni 2,184.
Lakini alidai kuwa ukijumlisha kura zake na za Mnyika wote kwa pamoja kisha zikitolewa kutoka katika kura halali zilizopigwa, zinabaki kura 353 ambazo ndizo zitagawanywa kwa wagombea wengine 14, jambo ambalo alisema si sahihi.

Hata hivyo, wakati akijitetea, Mnyika alikanusha madai hayo yote licha ya kukiri kuwepo kwa mkanganyiko wa usahihi na uwiano wa kura katika Fomu namba 24B.
Lakini, bado alidai kuwa dosari hiyo zinaweza kurekebishwa na kwamba haziathiri matokeo kiasi cha kuyafanya yawe batili.
Shahidi wa kwanza upande wa wadaiwa (DW1), aliyekuwa Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Gaudence Kadiarara alikiri kuwa Mnyika aliingiza kompyuta hizo japo alidai kuwa hata hivyo, hawakuzitumia, tofauti na Mnyika ambaye alidai hakuingia na kompyuta yoyote.

Shahidi huyo na mashahidi wengine wa utetezi akiwemo Msimamizi wa Uchaguzi (Mkurugenzi wa Manispaa), pia walikiri kuwepo kwa mkanganyiko katika fomu ya matokeo hayo ya ubunge lakini, wakasisitiza kuwa dosari hizo haziathiri matokeo jumla.

Hoja hizo ndizo ambazo ama zitamshawishi Jaji Msuya katika hukumu yake kutengua matokeo ya ubunge huo au kuthibitisha kwamba matokeo hayo ni halali.

Mawakili wa utetezi, PSA Mulokozi kwa niaba ya AG na RO na Mbogoro kwa niaba ya Mnyika, walidai kuwa mlalamikaji ameshindwa kuthibitisha madai yake na hivyo kuiomba mahakama iyatupilie mbali.

Lakini, Wakili Maige anayemtetea Ngh’umbi alisema wamethibitisha madai yao kwa kiwango kinachohitajika kisheria na kuiomba Mahakama itengue matokeo hayo yaliyompa ushindi Mnyika.

Alisema madai mengine yameungwa mkono na mashahidi wa utetezi hususan DW1 aliyekiri Mnyika kuingia na kompyuta katika chumba cha majumuisho ingawa alikanusha kuzitumia tofauti na Mnyika aliyekana kuingiza kompyuta hizo katika chuma hicho.
Pia Wakili Maige alihoji sababu ya mawakili wa Serikali kutowaita mahakamani baadhi ya mashahidi ambao walitajwa na upande wa madai na wa wadaiwa kuhusika kwa namna moja au nyingine katika mchakato wa uchaguzi huo.

Wakili Maige aliwataja mashahidi hao ambao alidai walikuwa ni muhimu kuitwa mahakamani kujibu madai na kutoa ufafanuzi wa masuala yaliyowagusa kuwa ni pamoja na Mkurugenzi wa Uchaguzi na Mtaalamu wa Teknolojia ya Mawasiliano wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec).

Mkurugenzi huyo alidaiwa kuwa ndiye aliyekagua kompyuta zilizotumika kufanyia majumuisho ya kura ambazo zilidaiwa kuwa zilitoka Manispaa ya Kinondoni, baada ya mfumo wa awali ulioandaliwa na Nec kuonekana kuwa haufai.

Lakini, Wakili Maige alidai kuwa kitendo cha kushindwa kumuita mkurugenzi huyo wa Nec mahakamani kutoa maelezo ya ukaguzi alioufanya na mbinu alizozitumia kuithibitishia mahakama kuwa katika kompyuta hizo zisingewezekana kuingizwa taarifa za kughushi ni kinyume cha sheria.

Akirejea kesi ya Stanbic Bank (T) Ltd dhidi ya Woods (T) Ltd namba 48 ya mwaka 2002, alidai kuwa Mahakama ilishatoa mwongozo kuwa ushahidi wa kitaalamu hauwezi kuthibitishwa kwa maneno matupu mpaka mtaalamu huyo atakapoitwa kuutolea ufafanuzi.

Wakili Maige alidai kuwa upande wa madai umethibitisha kuwa kompyuta zisizostahili kisheria ndizo zilizotumika kufanya majumuisho na kwamba ndizo zilizosababisha kuwepo kwa mkanganyiko uliojitokeza katika fomu ya matokeo wa kura zaidi 14,000, zisizo na maelezo.

Mawaziri wote waitwa Dodoma



SIKU chache baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangaza Baraza jipya la Mawaziri, mawaziri wote wameitwa mjini Dodoma, huku taarifa zikisema pamoja na mambo mengine, wanatarajiwa kujadili Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2012/13.

Tangu Rais alipotangaza Baraza hilo Mei 4, mwaka huu timu hiyo nzima haijawahi kukutana na hicho ni kikao cha kwanza kwa mawaziri wote chini ya uenyekiti wa mkuu huyo wa nchi.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue amethibitisha kuwepo kwa kikao hicho akisema ni cha kwanza tangu kuteuliwa kwao.

“Ni kikao cha kawaida cha Baraza la Mawaziri. Ndiyo ni cha kwanza kwani tangu kuteuliwa kwa mawaziri hakuna kikao ambacho kimewahi kufanyika. Ni cha kawaida tu katika utendaji kazi wa baraza,” alisema Balozi Sefue.

Habari zaidi zinasema kuwa karibu mawaziri wote waliondoka jana kuelekea Dodoma kwa ajili ya kikao hicho ambacho kinafanyika kabla ya kuanza kwa Bunge la Bajeti mnamo Juni 12, mwaka huu.

“Wapo ambao wanaweza wakawa Dar es Salaam au nje kwa kazi maalumu. Hawa wanaweza kupata kibali cha Waziri Mkuu. Lakini, karibu mawaziri wote waliondoka jana kuelekea Dodoma,” kilidokeza chanzo kingine.

Hoja ya Bajeti
Kikao hicho kinatarajiwa kujadili bajeti hiyo ya mwaka 2012 ambayo pamoja na mambo mengine, inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo namna ya kupunguza mfumuko wa bei.

Ingawa takwimu za mwezi huu kuhusu mfumuko wa bei zilizotolewa na Taasisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), zinaonyesha kupungua kwa mfumuko huo kutoka asilimia 19 hadi 18.7, bado Watanzania wengi wamekuwa wakilalamikia ukali wa maisha.

Mfumuko huo ambao unagusa bidhaa muhimu kama sukari, pia unagusa nishati ya mafuta ikiwemo petroli na mafuta ya taa, hivyo kuongeza gharama za usafiri kuanzia kwa watu binafsi na abiria wanaotumia usafiri wa umma.

Tayari Chama cha Wamiliki wa Daladala Mkoa wa Dar es Salaam (Darcoboa), kimepeleka maombi Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), wakitaka ongezeko la nauli kwa kiwango cha asilimia 150.

Lakini, kwa upande wa wafanyakazi, tayari kumekuwa na shinikizo la kutaka nyongeza ya mishahara kwa kiwango kinachoendana na mfumuko wa bei na ukali wa maisha unaotikisa nchi kwa sasa huku Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), likiwa tayari limetoa angalizo kwa Serikali kutopuuza kilio hicho.

Changamoto nyingine ambayo Baraza hilo la Mawaziri inapaswa kukabiliana nayo katika kujadili Bajeti hiyo kabla ya kuwasilishwa bungeni ni kuhusu namna ya kupunguza gharama za uzalishaji wa chakula, ikiwemo kuhakikisha upatikanaji wa urahisi wa pembejeo za kilimo, ili kutekeleza kwa kasi Mpango wa Kilimo Kwanza.
Pia, Baraza hilo Mawaziri linapaswa kupitia kwa kina  vyanzo vipya vya mapato ya kodi ambavyo havitajikita katika vyanzo vilivyozoeleka ambavyo ni pamoja na kodi katika mishahara ya wafanyakazi huku baadhi ya wafanyabiashara wakubwa wakikwepa kodi.

Why Kikwete has retained Mwandosya


Dar es Salaam. The recent appointment of ailing Prof Mark Mwandosya as a Minister in the President’s Office is linked with the 2015 General Election, according to a cross-section of political analysts.They told The Citizen yesterday that President Jakaya Kikwete’s decision to appoint Prof Mwandosya was a strategy to capture the support of the ailing politician, who has a big following both in the Southern Highlands and Chama Cha Mapinduzi (CCM).

The soft spoken electrical engineer-turned-politician came third in CCM’s 2005 presidential nomination race, having been beaten at the game by Mr Kikwete and runner-up Dr Salim Ahmed Salim.

Though his health has been failing, Prof Mwandosya still enjoys enough political clout to reckon with.
There is also the possibility that Mr Kikwete is courting Prof Mwandosya in order to get a guarantee of his backing should the president have a preferred successor in 2015.

When asked yesterday to comment on President Kikwete’s choice of the ailing minister, Chief Secretary Ombeni Sefue responded that it was the prerogative of the Head of the State to appoint his assistants.
The people should not worry, he added, because “even if Prof Mwandosya were to attend various check-ups, he will not go with his office”.

Though Prof Mwandosya himself has not given a firm indication that he will run for the top office in 2015, there are those who argue that this appointment gives him an edge should he decide to go for it.

A political science lecturer at the University of Dar es Salaam, Mr Richard Mbunda, said this appointment would be a big plus for Mr Mwandosya if he were to take a shot at the presidency, his health notwithstanding. “Along with his record as a hardworking and a committed public servant, he will be better equipped than anyone else since he will have gained a lot of experience working as the president’s right hand man,” Mr Mbunda added.

Mr Mbunda played down suggestions that Prof Mwandosya would not have any work to do in his new docket. Rather, he said, Prof Mwandosya would be second in line to the Prime Minister and his role wouldl cut across all ministries and government operations in Parliament.

Mr Emmanuel Mallya, a doctoral student in Portugal, said the president’s decision to appoint Prof Mwandosya would help heal divisions within the party. He added: “Among the scenarios which I think the president considered prior to his decision was uniting the party ahead of 2015… if he had left out Prof Mwandosya, many CCM members and other people outside CCM would have been dissapointed… certainly, Mr KIkwete didn’t want to do such a thing.”

Similar comments came from Mr Hamad Salim, head of political science and public administration at the Open University of Tanzania, who suggested that the president, who is also the CCM national chairperson, was doing everything in his power to make sure that the party did not disintegrate in his hands.

“For now, he is afraid that the party might die in his hands,” Mr Salim said.  “As a result, he is making sure that the groups are dissolved immediately, so as to strengthen party unity at large.”

According to Mr Salim, the president is fully aware that what matters come the 2015 will be party unity rather than individual strengths. And the president is also sensitive to the fact that 2015 election will be different from previous elections as there is no “leadership legacy” to fall back on.  Elaborating, he said: “In 1995, the late father of the nation (Mwalimu Julius Nyerere) picked Mr (Benjamin) Mkapa because President Kikwete wasn’t mature enough. Mr  Kikwete was mature and ready to take over in 2005, but things are very different now.”

Mr Mallya does not, however, rule out Prof Mwandosya from the contest for the top office, his current health status notwithstanding. He adds: “Even Prof Mwandosya himself says that he is getting stronger. When asked, he did not say that he would not contest. He said he is focusing on his health. What happens if his health stabilises before the nomination process?”

University of Dar es Salaam political science lecturer Alexander Makulilo declined to associate the appointment with the Kikwete succession. “I can’t predict whether or not the president is seeking his (Prof Mwandosya’s) backing for his (president’s) preferred candidate come 2015,” he said. “What I am sure of is that, in being the president’s right hand man, Prof Mwandosya would be a big factor in 2015 whether or not he vies for the presidency.”

Prof Mwandosya was flown to India for medical treatment at the end of last year. He then had surgery at Apollo Hospital and has been in and out of the country recuperating since then. The MP for Rungwe constituency since 2000, he has served as a minister in various dockets in the third and fourth phase governments.
Reported by Frank Kimboy and Alex Bitekeye

Wednesday, May 23, 2012

Few know the EAC and what it stands for: study


By Zephania Ubwani
The Citizen Bureau Chief
Arusha. Many Tanzanians, including small and medium entrepreneurs, are not aware of the East African Community (EAC) and what it has to offer, a survey has indicated.The problem is more acute in the southern highland regions, where farmers and crop traders have little information on markets for their produce.

It is sometimes easier for local entrepreneurs to trade with Europe than with neighbouring countries because of lack of information, according to Mr Allan Nswila, a business consultant based here.

During a forum convened to discuss challenges facing the bloc, he said the problem has been compounded by a poor transport network. “Very few Tanzanians know about the EAC and its potentials for doing business,” he pointed out. “People are much more aware of markets abroad than those within the region.”

Farmers in Mbeya, Iringa, Rukwa and Ruvuma regions, for example, were unaware of opportunities to sell their surplus produce at a time Kenya and parts of Tanzania were in dire need of food.Transporting maize to regions within the country that have been afflicted by drought and food shortages has also been difficult.

“There are also cases where the government had no money to buy maize when it was needed in neighbouring regions,” he said during a forum organised by a new lobby group, Friends of East Africa.The survey, carried out early this year, also covered small and medium enterprises in the northern regions including Arusha, where EAC has its headquarters.

Mr Nswila noted that very few cross-border traders consulted the East African Business Council and the Tanzania Chamber of Commerce, Industry and Agriculture on matters to do with regional trade.

“Even in Arusha, some business people do not seem to be aware of the business potential in neighbouring countries, especially EAC member countries,” he told an audience at the Arusha City Complex hall.Other speakers echoed his sentiments, wondering why the Arusha region authorities appeared indifferent to the presence of the EAC secretariat in the town.

Dr Firmin Nguma, a retired public servant, accused the Arusha region, district and municipal officers of distancing themselves from regional affairs. “It’s unfortunate that some people here do not want to get involved in EAC matters,” he said. “As a result, Tanzania has always been left behind in negotiations on critical issues on regional integration.”
In response, EAC Secretary General Richard Sezibera said the secretariat was keen to work with Arusha authorities to champion the regional integration agenda. He pointed out, though, that the community comprised five partner states and it could not dictate terms to Tanzanian officials. He also denied that the EAC was pushing for land to become an economic asset under the Common Market Protocol.
Land was listed among the contentious issues under the Common Market Protocol signed in November 2009, the others being travel documents and right of residence. “But these were successfully ironed out by the partner states,” the secretary general added.

The EAC boss admitted, though, that there had been fears in Tanzania that the common market arrangement would arbitrarily open up land to outsiders and landless people from other East African states. “This is not true,” he stressed. “Land remains a national issue.”

He cautioned, however, that Tanzanians would have to put their vast land resources to full use for economic development of the country. According to the secretary general, Tanzania can become an economic giant in Africa if it exploits its vast economic resources such as minerals, natural gas, wildlife, livestock and arable land.

He also implored the Tanzanian business community not to fear the economic dominance of Kenya. There have been economic disparities among the EAC member states since the early days of the community, he said, and this has been reflected in education, skills and enterprise development.

A study conducted three years ago established that issues that needed to be sorted out to ease the process of integration included improving the way business is done by fine tuning the customs clearance procedures and introducing a single currency.

Respondents in the study commissioned by EAC also wanted service enhanced at border points. This would involve introducing a 24-hour work schedule, fast clearing services especially for large trucks and reducing time spent on verifying documents.

They also asked for freedom of movement of goods by removing border restrictions, accepting one common EAC identification document and ensuring the same standards for document verification at all borders. Taxation and non-tariff barriers also need to be dealt with by ensuring that taxation is standardised and paid once.

jalada la Mkulo latua kwa Hoseah


ASEMA ALIANZA KULISHUGHULIKIA JANA, LINAHUSU TUHUMA ZA UUZWAJI WA KIWANJA KWA MOHAMMED ENTERPRISES
Patricia Kimelemeta na Raymond Kamnyoge
MKURUGENZI Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah jana alikuwa akichambua majalada ya baadhi ya mawaziri waliong’olewa baada ya wizara zao kutajwa kuhusika na ufisadi katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Tayari Dk Hoseah alikwishatangaza kwamba Takukuru imeanza uchunguzi dhidi ya tuhuma za mawaziri hao kabla hata ya Rais Jakaya Kikwete hajawang’oa katika mabadiliko yake ya Baraza la Mawaziri aliyofanya mapema mwezi huu huku Ikulu nayo ikiagiza uchunguzi kwa watendaji wa wizara husika.

Mawaziri walioondolewa ni pamoja na aliyekuwa wa Fedha, Mustafa Mkulo, Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), William Ngeleja (Nishati na Madini), Dk Cyril Chami (Viwanda na Biashara), Dk Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii) na Omary Nundu (Uchukuzi).

Jana, akizungumza na gazeti hili, Dar es Salaam, Dk Hoseah alisema tangu CAG alipowalisha ripoti hiyo serikalini walianza uchunguzi wa tuhuma hizo ili kuwafikisha wahusika kwenye vyombo vya sheria.
Alisema jana hiyo alikuwa akipitia tuhuma za Mkulo kuhusu na uuzaji wa Kiwanja Namba 10 kwa Kampuni ya Mohamed Enterprises (MTeL).

“Tangu CAG alipowasisha ripoti yake Serikalini tulianza mchakato wa kuwachunguza kulingana na tuhuma zinazowakabili kwa kila mmoja kwa nafasi yake ili tutakapomaliza zoezi hilo tuwasilishe kwenye vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua zaidi,” alisema Dk Hoseah.

Mkulo aishangaa Takukuru

Alipoulizwa kuhusu madai hayo ya kuchunguzwa, Mkulo alisema anachojua ni kwamba uchunguzi au mahojiano ya Takukuru na mawaziri ni wa kimaadili na ni jambo la siri.

“Huwezi kusimama sokoni Kariakoo kwenye watu wengi na kutangaza kwamba tunamchunguza au tunamhoji Mkulo ni kwenda kinyume na maadili ya Takukuru,” alisema Mkulo.

Alisema uchunguzi unaweza kuvurugika kama unawekwa hadharani ukiwa katika hatua za mwanzo.

“Ndiyo maana nasema hata kama ninachunguzwa au nimehojiwa kuna umuhimu gani kutangaza? Kwa nini Takukuru wasisubiri ili kupata uhakika katika uchunguzi wao?”

Mkulo alikuwa akirejea Sheria ya Takukuru ya mwaka 2007, Kifungu cha 37 ambacho kinazuia mtu yeyote kueleza kwa kina mchakato wa uchunguzi unaofanywa na Takukuru dhidi ya mtuhumiwa.

Watendaji nao

Dk Hoseah alisema uchunguzi unaoendelea hivi sasa siyo kwa mawaziri hao pekee, bali unagusa pia baadhi ya watendaji wakuu wa Serikali ambao wamehusishwa kwa namna moja au nyingine kwenye Ripoti ya CAG hivyo kusababisha kuwajibishwa kwa mawaziri.

Alisema ripoti zilizopo kwenye ofisi yake ni za viongozi mbalimbali ambao wameshindwa kutimiza majukumu yao na kuisababishia Serikali hasara.

Katika Mkutano wa Saba wa Bunge uliomalizika hivi karibuni, wabunge wa upinzani pamoja na wa CCM walifikia uamuzi wa kusaini fomu ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda lengo likiwa kumshinikiza kuwawakijibisha mawaziri waliotajwa katika ripoti hiyo vinginevyo, ajiuzulu.

Hatua hiyo iliibua mvutano mkali ndani ya CCM huku wabunge wa chama hicho wakishikilia msimamo wa kuitaka Serikali kuwawajibisha mawaziri hao hali iliyomfanya Rais Kikwete kupangua Baraza lake la Mawaziri na kulipanga upya huku akiwatosa mawaziri sita kati ya wanane waliotajwa katika ripoti hiyo.

Ripoti ya CAG

Katika shinikizo hilo la wabunge, Mkulo alikuwa wa kwanza kutakiwa ajiuzulu, kutokana na kashfa ya kuvunja Bodi ya Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC) ili kuficha tuhuma zake ikiwemo uuzaji wa Kiwanja hicho Na.10 kwa MeTL.

Kilichomponza Dk Mponda ni kashfa ya Bohari ya Dawa (MSD) ambako ukaguzi maalumu katika bohari hiyo ulibaini kuwapo tofauti ya Sh658.9 milioni ikiwa ni pungufu ya kiasi ambacho kilipokewa na kuripotiwa wizarani kwenda MSD, bila ya ushahidi wa kuzipokea.

Pia, uchunguzi unaonyesha kuwapo Sh100 milioni zilizopelekwa MSD kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na kutumiwa na Bohari hiyo bila kuwepo kwa mchanganuo wa matumizi.

Ukaguzi pia ulibaini kuwepo kwa kiasi cha Sh4.5 bilioni zilizotoka Hazina kwenda Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa ajili ya kununulia dawa na vifaa vya hospitali, lakini kiasi cha Sh4.344 bilioni ndicho kilichopelekwa MSD  ukiondoa Sh196 milioni ambazo zilitumika bila kuwapo kwa ushahidi wa kupokewa MSD kutoka wizarani.

Kwa upande wa Maige, pamoja na mambo mengine, Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira ilitaka awajibishwe kwa madai ya kutengeneza mazingira ya rushwa katika ugawaji wa vitalu vya uwindaji kwa kampuni ambazo hazina sifa na kusafirishwa nje kwa wanyama wakiwamo twiga na tembo kinyume cha sheria.

Nundu alidaiwa kuipigia kifua kampuni ya China Merchant ili apate zabuni ya ujenzi wa magati mawili katika Bandari ya Dar es Salaam huku Ngeleja akidaiwa kukaa kimya wakati Tanesco ikifanya ununuzi wa Sh300 hadi 600bilioni kwa mwaka mmoja.

Profesa Jumanne Maghembe ambaye alihamishiwa Wizara ya Maji akitokea Kilimo, Chakula na Ushirika, alituhimiwa kwa kuchelewa kwa mikopo ya pembejeo kwa wakulima huku George Mkuchika ambaye sasa yuko Ofisi ya Rais (Utawala bora), akituhimiwa kuwa akiwa Waziri wa Nchi Ofidi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), halmashauri nyingi zilifanya ufisadi wa kutisha ukitolewa mfano wa Kishapu ambayo inadaiwa kufuja fedha za umma kiasi cha Sh6bilioni.

Mkandarasi amvunja mguu polisi kwa risasi

Kwirinus Mapunda, Songea
MKANDARASI mmoja wa Manispaa ya Songea, Ruvuma (jina tunalihifadhi) anashikiliwa na Polisi mkoani hapa kwa tuhuma ya kumpiga risasi askari polisi na kumvunja miguu yote miwili.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa Ruvuma, George Chipos alimtaja askari aliyepigwa risasi kuwa ni Lucas Komba ambaye kituo chake cha kazi ni Mkoa wa Tabora. Alikuwa hapa kwa mapumziko na kwamba tukio hilo lilitokea Mei, 20 mwaka huu saa 2.45 usiku katika grosari iliyopo Seedefarm Barabara ya Namtumbo.

Chipos alisema mkandarasi huyo aliyepewa kazi ya kutengeneza Barabara za vijijini, alimpiga risasi askari Komba mwenye No.E 9507 PC kutokana na kile kinachodaiwa ni mtuhumiwa kulewa kupita kiasi hivyo kuanza kufyatua risasi hewani bila utaratibu.

Alisema askari Komba alishambuliwa baada ya kujaribu kumzuia. Alimfyatulia risasi miguuni na kumpiga sehemu ya paja la mguu wa kushoto.

Kaimu kamanda huyo alisema askari Komba amelezwa katika Hospitali ya Mkoa Ruvuma akipatiwa matibabu na mtuhumiwa atapandishwa kizimbani baada ya upelelezi kukamilika.

Katika tukio jingine: Watu wawili wanashikiliwa na polisi kwa tuhuma za mauaji ya mtu mmoja, Esau Kapinga yaliyotokea katika Kijiji cha Mkumbi Wilaya ya Mbinga, Ruvuma. Marehemu aliuawa kwa kukatwakatwa kwenye goti la kulia na kupigwa na kitu kizito mgongoni.

Kamanda Chipos alisema tukio hilo lilitokea Mei 21, mwaka huu saa 7:00 usiku na kuwa chanzo chake ni ugomvi wa kifamilia wa kugombea mashamba ya kahawa. Alisema watuhumiwa watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kukamilika.

Mwandosya: Afya kwanza urais baadaye


Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya, jana aliapishwa Ikulu kushika wadhifa huo huku akikataa kuzungumzia mipango yake ya baadaye ya kisiasa.  Profesa Mwandosya akijibu moja ya maswali ya waandishi wa habari baada ya kuapishwa, lililohusu iwapo bado ana nia ya kugombea urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, alisema hawezi kuzungumzia suala hilo mpaka hapo afya yake itakapotengemaa.

“Mbona mnapenda sana kuniuliza suala hili? Maana kila mwandishi akiniona anapenda kuuliza hili au leo mmeuliza kwa sababu mmeona nimekuja karibu na jengo hili? (Ikulu)…” alihoji huku akicheka na kuongeza:  “Ngoja kwanza tuangalie afya…. Eeh! Afya kwanza halafu hayo mambo mengine yatafuata.” Profesa Mwandosya alihamishiwa Ofisi ya Rais kutoka Wizara ya Maji aliyokuwa akiiongoza awali, baada ya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanywa na Rais Jakaya Kikwete, Mei 4, mwaka huu.

Hata hivyo, waziri huyo ambaye aliomba kugombea urais kupitia CCM akipamba na Rais Kikwete mwaka 2005, hakuweza kuapishwa na mawaziri wenzake Mei 7, mwaka huu kwa kuwa ndiyo kwanza alikuwa amerejea kutoka India alikokuwa kwa muda mrefu akipatiwa matibabu kutokana na ugonjwa ambao hata hivyo, haujawahi kuwekwa hadharani.

Katika mchakato wa kinyang’anyiro hicho ndani ya CCM, Profesa Mwandosya alishika nafasi ya tatu, nyuma ya Rais Kikwete na Dk Salim Ahmed Salim.  Jana, Profesa Mwandosya alizungumzia afya yake kwa kusema kuwa anaendelea vizuri... “Afya yangu ni kama mnavyoiona, naendelea vizuri tu, mwaka jana nilikuwa nikitembea kwa msaada wa magongo lakini leo nimeweza kutembea mwenyewe bila msaada wa magongo, kwa kweli naendelea vizuri,” alisema Waziri huyo.

  Kuhusu wadhifa wake mpya alisema anafahamu kwamba kazi aliyonayo ni kubwa na kwamba yuko tayari kumsaidia Rais katika majukumu mbalimbali ya kitaifa yanayomkabili.  “Mnafahamu Rais ana majukumu mengi sana ya kitaifa, yanamhitaji kwenda hapa na pale, kwa hiyo mimi kwanza nashukuru kwa kupewa wadhifa huu na niko tayari kumsaidia mheshimiwa Rais katika majukumu hayo,” alisema.
Ugonjwa wake  Profesa Mwandosya alikwenda katika Hospitali ya Apolo, India kwa ajili ya matibabu Mei, mwaka jana ambako alikaa huko kwa miezi ipatayo sita kabla ya kurejea Novemba 29, 2011.

 Desemba 3, 2011 zikiwa zimepita siku sita tangu aliporejea, alifanya mkutano na waandishi wa habari katika makao makuu ya Wizara ya Maji na kusema kwamba alikuwa bado ana kiu ya kuwatumikia wananchi.  Katika mkutano huo, Profesa Mwandosya alikataa kuzungumzia suala la urais wa 2015 kwa maelezo kwamba yapo mambo mengi ya kufanya na kwamba haukuwa wakati mwafaka.

“Kama kuna watu wana fedha za kuwekeza katika kutafuta uongozi ni wao, lakini mimi bado nahitaji kuwahudumia wananchi kwa kutatua matatizo ya maji,” alisema na kuongeza:

 “Bado kuna mambo mengi, vilivyopo kwenye ajenda za Wizara ya Maji sijavikamilisha. Kwa hiyo siwezi kuzungumzia masuala ya urais wakati bado nina majukumu mazito ya kuwahudumia wananchi.”   Januari mwaka huu, Profesa Mwandosya alikwenda tena India kuendelea na matibabu kabla ya kurejea nchini siku chache zilizopita.

Sitta, Lowassa wazungumzia kujiunga na Chadema


*SITTA ADAI WANAOKIMBILIA HUKO NI MAGAMBA YEYE SI MMOJA WAO, LOWASSA AMSHANGAA LEMA, ASEMA KUHAMIA CHADEMA SI SIRI,

Waandishi Wetu

SIKU chache baada ya aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema kuwataja mawaziri wawili na mmoja aliyewahi kuwa Waziri Mkuu kwamba, wameomba kujiunga na chama hicho cha upinzani, wawili kati yao wamejitokeza na kuzungumzia madai hayo.

Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta ambao walitajwa na Lema, jana kwa nyakati tofauti walibeza madai hayo.

Jumamosi iliyopita, Lema akiwa wilayani Sengerema, Mwanza alisema mawaziri watatu, akiwamo mmoja aliyewahi kuwa waziri mkuu wameiomba kujiunga na Chadema lakini mmoja kati yao amekataliwa na wengine mchakato wa kuyakubali maombi yao unaendelea.

Katika mkutano huo, Lema aliwataja mawaziri hao kwa jina moja kuwa ni Sitta, Lowassa na waziri mwingine ambaye tunahifadhi jina lake kwa kuwa hakupatikana jana kuzungumzia madai hayo.

Msimamo wa Sitta
Sitta alipuuza madai hayo akiyaita ya kitoto na kueleza kuwa kwa hadhi yake, hawezi kuomba kujiunga Chadema na kusubiri majibu kama amekubaliwa au la.

“Yaani mimi niombe kwenda Chadema halafu nikae kabisa huku nikisubiri wanijibu! Huo ni upuuzi na jambo hili haliwezekani na si kweli hata kidogo. Kama Lema kasema hivyo, basi huo ni utoto na siasa za kihuni,” alisema Sitta.

Sitta huku akicheka aliongeza: “Sasa nimeomba kwa nani na kwa njia ipi ya mdomo au maandishi? Mimi siyo gamba. Ni mtu mwadilifu siwezi kujiunga katika utaratibu wa kuchukua magamba ndani ya CCM.”

“Wao Chadema wanachukua tu kila mtu. Wakienda kwenye mikutano pia wanachukua tu watu, sasa hivi wanachukua magamba CCM. Mimi nawatakia kila heri katika kuchukua magamba CCM.”

Sitta alisema yeye ni mwanasiasa makini na mwadilifu hawezi kukaa chungu kimoja na magamba... Wanalofanya kuchukua magamba ya CCM ni faraja hata kwa Katibu Mkuu Wilson Mukama.”

Mbunge huyo wa Urambo Mashariki, alisema kuchukua magamba CCM ni sawa na mtu ambaye anakwenda kwa jirani ambaye nyumba yake imezungukwa na takataka kisha akamsaidia kuzisomba kwenda kuzitupa... Hapo si lazima ufurahie bwana?

Alisema kama angekuwa anajiunga na Chadema wangemkumbatia akisema: “Kama wanakwenda watu wadogo wanaandaa sherehe kubwa, nikienda mimi...?

Majibu ya Lowassa
Jana, Lowassa naye alipuuza madai hayo ya Lema akisema hajawahi kuomba kujiunga na Chadema huku akisisitiza: “Kama ingekuwa hivyo isingekuwa siri. Ningetangaza uamuzi wangu kupitia vyombo vya habari.”

Lowassa alitoa kauli hiyo baada ya gazeti hili kumtaka azungumzie madai ya Lema kwamba aliomba kujiunga na chama hicho cha upinzani lakini akakataliwa.

“Kama ningeomba kuingia Chadema ningetangaza kwenye vyombo vya habari. Sijasikia hayo na sitaki kusema chochote zaidi,” alisema  Lowassa na kisha kukata simu.

Slaa amshangaa Lema

Alipoulizwa kuhusu madai hayo ya Lema, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa alisema hawezi kuzungumzia kauli ya mtu.

“Tabia yangu huwa sipendi kuzungumzia kauli aliyoitoa mtu hivyo alichokisema Lema mtafuteni yeye mwenyewe afafanue kwani atakuwa anajua alichokisema kina maana gani,” alisema Dk Slaa.

Dk Slaa alisema: “Badala ya kukaa na kuzungumzia kauli ya mtu, kinachotakiwa ni kujadili jinsi gani ya kuhakikisha tunapunguza ugumu wa maisha kwa mwananchi wa hali ya chini.”

“Tuache kuzungumza kauli za watu hapa sasa kinachotakiwa kila mmoja wetu kwa nafasi yake  atizame ni jinsi gani atahakikisha anamkomboa mwananchi kwa kupunguza gharama za maisha.”

Lema ang’ang’ana

Hata hivyo, jana alipotakiwa kufafanua kauli yake baada ya kuelezwa kwamba aliowataja wabeza madai yake, Lema aliendelea kusisitiza kwamba alichosema ni cha kweli.

“Wanakataa tu kisiasa, lakini nilichosema ni cha kweli na (kesho), leo katika mkutano wangu wa Singida, pamoja na kuwarudia hawa niliowataja nitawataja wengine pamoja na wabunge wa CCM ambao wapo tayari kujiunga na Chadema.”

Katika madai yake ya kwanza aliyotoa Jumamosi iliyopita katika mkutano uliofanyika kwenye Viwanja vya Mnadani, Lema alisema viongozi wenye uchungu na taifa hili ndani ya CCM na ambao wamekuwa hawafurahishwi na ubadhirifu wa mali za nchi, wamekuwa wakifanya mazungumzo kutaka kujiunga na Chadema.

Alisema kwa vile chama chake kimejiandaa kuingia madarakani kwa kutumia nguvu ya umma, ndiyo maana mawaziri wa Serikali ya CCM wameomba kujiunga nacho ili kusaidiana kwa pamoja kwenda kuingia madarakani mwaka 2015.

“Lakini, Lowassa tumemkataa. Tunataka wachapa kazi na wenye mioyo ya kweli katika mapambano ya kupigania haki na kuondoa dhuluma kwa Watanzania,” alisema Lema.

Lema alidai kuwa mawaziri hao (waliokubaliwa) wanasubiri muda muafaka ufike waweze kutangaza rasmi kujiunga na chama hicho, kutokana na kile kilichodaiwa kuchoshwa na mwenendo mzima wa uongozi na utendaji serikalini na ndani ya CCM, hususan suala la kuwalinda watu wanaotuhumiwa kwa ubadhilifu.