Thursday, September 26, 2013

Askari alivyookoa zaidi ya watu 100 Kenya

Askari wa Kikosi Maalumu cha Anga (SAS) cha Uingereza, ameonekana shujaa katika tukio la uvamizi lililotokea katika jengo la maduka la Westgate jijini Nairobi Kenya baada ya kufanikiwa kuokoa watu 100 waliokuwa ndani ya jengo hilo.
Askari huyo ambaye jina lake halikutajwa kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni sababu za kiusalama,  wakati wavamizi hao wanavamia jengo hilo siku ya Jumamosi, naye alikuwemo ndani ya jengo hilo akinywa kahawa.
Kwenye baadhi ya mitandao, askari huyo ameonekana akiwasaidia wanawake wawili huku akiwa ameweka bastola kwenye suruali yake, ingawa sura yake imefichwa.
Habari zinasema kuwa, askari huyo ameonekana shujaa kwani licha ya hali tete iliyokuwa ndani ya jengo hilo, aliweza kuingia na kutoka zaidi ya mara 12 akiwaokoa baadhi ya watu waliokwama ndani ya jengo hilo lenye maduka na migahawa mbalimbali.
“Alichofanya ni kitendo cha kishujaa sana, alikuwa akinywa kahawa na baadhi ya rafiki zake wakati wavamizi walivyoingia.
Alirudi ndani mara 12 na kufanikiwa kuokoa zaidi ya watu 100. Fikiria kuthubutu kurudi ndani huku akijua kabisa jinsi hali ilivyo ndani ya hilo jengo,” baadhi ya mashuhuda walinukuliwa.
Habari zaidi zinaeleza kuwa, askari huyo wa Uingereza  anafanya zaidi shughuli zake Kenya na nje ya nchi hiyo ikiwa ni pamoja na kuwafuatilia raia wa nchi yake wanaojishughulisha na mambo mbalimbali.
Agosti mwaka huu, gazeti la Daily Mirror liliripoti kuwa kikosi maalumu cha SAS na askari maalumu wa kupambana na ugaidi,  wameanza kumtafuta Samantha Lewthwaite, Mwanamke anayetajwa kuwa ni raia wa Uingereza anayedaiwa kuwa gaidi ambaye pia anashirikiana na kundi la  Al-Shabaab.
Mwanamke huyu mjane anayetajwa kuwa ni gaidi, inasemekana pia alishiriki kupanga na kutekeleza uvamizi mjini Nairobi.
Kikosi hicho cha SAS, kinaelezwa kuwa kinafanya kazi kwa ukaribu na vikosi vya ulinzi vya Uingereza, Kenya na vile vya nchi nyingine za Afrika Mashariki.
Habari juu ya askari huyo zimekuja wakati milio ya risasi ikizidi kusikika ndani ya jengo hilo, huku maofisa wa usalama wa nchi hiyo wakisema kuwa wamedhibiti sehemu kubwa ya jengo hilo. Habari zaidi zinasema kuwa, bado zaidi ya watu 10 wanashikiliwa ndani ya jengo hilo kama mateka.
‘Tumeshadhibiti sehemu yote ya jengo, tuko hapa kuhakikisha tunawaadhibu vya kutosha hawa watekaji,” Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Kenya, IGP David Kimaiyo aliandika kwenye mtandao wake wa Twitter.

Licha ya maelezo hayo, mpaka jana saa 12 asubuhi bado milio ya risasi ilikuwa ikizidi kusikika ndani ya jengo hilo.
Kundi la Al-Shabaab, lililodai kuhusika na tukio hilo, juzi liliweka ujumbe wa sauti kwenye baadhi ya mitandao likidai kuendelea kushikilia sehemu kubwa ya jengo hilo. “Licha ya juhudi zinazofanywa, bado tunaendelea kushika sehemu ya jengo la Westgate,” Msemaji wa Al-Shabaab Sheik Ali Mohamud anasema.
Mtandao wa Daily Mail unasema kuwa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Amina Mohamed anasema raia watatu wa Marekani na mmoja wa Uingereza, ni kati ya watu waliovamia jengo hilo la Westgate.
“Mvamizi kutoka Uingereza ni mwanamke ambaye amekuwa akijaribu kutekeleza uvamizi kama huu mara nyingi,” anasema Mohamed akimlenga Samantha Lewthwaite, anayedaiwa kuwa gaidi wa kimataifa.
Marekani imesema kuwa, inaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini kama kuna raia wake yeyote aliyehusika kwenye tukio hilo ambalo mpaka sasa limegharimu maisha ya watu zaidi ya 60.
Makala haya yameandikwa na Fredy Azzah kwa msaada wa vyombo vya habari.

Sunday, September 1, 2013

In shock move, Obama puts Syria strike on hold

WASHINGTON - President Barack Obama has postponed threatened missile strikes against Syria in a risky gamble that he can win more support for his plan to punish Bashar al-Assad's regime.
To general surprise, the US leader broke with decades of precedent to announce that he would seek approval from Congress for action against Syria's alleged use of chemical weapons.
This effectively pushed military action back until at least September 9, when US lawmakers return from their summer recess.
Obama insisted that he reserves the right to strike regardless of Congress's decision, and a White House official said the pause would also allow him time to build international support.
The Arab League meets in Cairo on Sunday and is expected to condemn Assad, and Obama travels to Russia next week for a G20 Summit that will now be overshadowed by the crisis.
But the toughest battle, and perhaps the most dangerous for Obama's credibility, may yet be with his own former colleagues in Congress, where support for strikes is far from assured.
Indeed, observers warned that he faces the same fate as Prime Minister David Cameron, who on Thursday lost his own vote on authorizing military action in the British parliament.
"The chairman of the joint chiefs has informed me that we are prepared to strike whenever we choose," Obama warned during an address in the White House Rose Garden.
"Our capacity to execute this mission is not time-sensitive. It will be effective tomorrow or next week or one month from now."
At least five US warships armed with scores of Tomahawk cruise missiles have converged on the eastern Mediterranean ready to launch precision strikes on Syrian regime targets.

Father argues with angry crowd after child pees in Shanghai subway


A video has gone viral on the Internet, showing a father getting into a fight with other commuters after letting his infant urinate on the subway.
The six-minute long video shows a father quarrelling violently with commuters who are heard voicing their anger at the parents' actions.
The video has sparked even larger waves of condemnation by netizens after it was made public, Chinasmack reported.
Nearly all the comments made on the video were in criticism of the parents' "extremely uncivilised" behaviour, Chinese media reported.
The Chinese media reported that what is more outrageous is that upon seeing the public respond negatively to their behaviour, the father can be seen in the video taking out his handphone to say: "I've gotten into trouble in the subway, hurry and bring some people over."
His actions earned him the disapproval of even his wife, who can be heard in the video saying: "If you have the guys, fight yourself. Don't call other people."

Bastola nje nje, zauzwa mitaani nchini

Dar/Mikoani. Kukithiri kwa rushwa miongoni mwa baadhi ya maofisa wa Jeshi la Polisi nchini, kumesababisha silaha ndogondogo hususan bastola kumilikiwa na watu wasio na sifa nchini.
Uchunguzi wa kina wa gazeti hili katika mikoa mbalimbali nchini ikiwamo iliyopo mipakani inaonyesha kuwa, bastola zinamilikiwa na watu bila ya kufuata taratibu na nyingine zikitumika kwa ajili ya kufanyia uhalifu.
Hivi sasa hata vibaka ambao awali walikuwa wakitumia visu na mbao za misumari kupora mali za watu, sasa wanafanya uhalifu huo kwa kutumia bastola.
Mbali ya vibaka kumiliki bastola, wahamiaji haramu walioko ndani ya mipaka ya Tanzania inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wanadaiwa kuingiza silaha nzito, ambazo zinatumika kwa ajili ya matukio ya kihalifu.
Jinsi silaha zinavyopatikana
Uchunguzi unaonyesha moja ya njia ambayo imekuwa ikitumika watu wasiokuwa na sifa kupata bastola au bunduki ni kutumia mawakala au baadhi ya maofisa polisi, waliopo katika mikoa mbalimbali ambao huwatafutia vibali vya kumiliki.
Utaratibu wa kawaida ni kwamba waombaji wanaotaka kumiliki silaha ni lazima wajadiliwe katika kamati za ulinzi na usalama za mtaa au kijiji, wilaya na mkoa na kuhojiwa ili kujiridhisha kama mwombaji ana sifa.

Mkoa wa Kilimanjaro
Uchunguzi  umebaini kuwa baadhi ya vijana wadogo wakiwamo wafanyabiashara, wana vibali vya kumiliki bastola mkoani Kilimanjaro na hawakupitia mchakato huo.
“Unataka kibali cha kumiliki bastola? Una milioni moja na nusu nikuunganishe na jamaa Dar anakufanyia process (mchakato) zote anakuletea kitabu,”alisema kijana mmoja jina tunalihifadhi.
Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika, baadhi ya maofisa wa Jeshi la Polisi makao makuu na wale waliopo mikoani, wamegeuza suala la kumilikisha watu silaha kama mradi wa kujitajirisha.
“Tatizo la nchi hii ni corruption (rushwa) kwa sababu unajiuliza hivi hawa vijana wadogo kabisa wanamiliki bastola na hawakujadiliwa kwenye kikao chochote,”alidokeza mfanyabiashara mmoja.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwa wapo wanaojiita wafanyabiashara, lakini ni matapeli wa kimataifa nao wamepewa vibali vya kumiliki bastola na wakati mwingine huzionyesha waziwazi wakiwa baa.
“Ufyatuaji wa risasi siku hizi umekuwa holela…ninavyofahamu ukifyatua hata risasi moja, lazima uandikishe maelezo polisi ulifyatua kwa sababu zipi siku hizi lakini hilo halifanyiki,” ilidokezwa.
Inadaiwa kuwa kutokana na kuwapo kwa ulegevu wa vyombo vya dola hususan Polisi, baadhi ya wamiliki wa bastola hizo wamekuwa wakizikodisha kwa majambazi ambao huzitumia katika uporaji.
Kwa mujibu wa uchunguzi huo, ulegevu huo katika kudhibiti matumizi ya silaha, kumetoa mwanya kwa baadhi ya wamiliki kukodisha bastola zao na kurudishiwa baada ya matukio pasipo kugunduliwa.
Dar es Salaam
Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili unaonyesha kuwa kuongezeka kwa idadi ya watu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria jijini Dar es Salaam, kumeongeza matukio ya uhalifu.
Baadhi ya watu ambao wapo karibu na maofisa wa polisi makao makuu wamekuwa wakitumia nafasi hiyo kuwatafutia watu vibali vya kumiliki silaha.
Watu hao wamekuwa wakijipatia Sh600,000 hadi Sh900,000 kwa kibali kimoja cha kumiliki silaha.
Hali hiyo imesababisha wahalifu wengi wakiwamo vibaka mitaani kumiliki silaha ambazo wanazitumia kupora watu mitaani.
Mussa Radhamn Mkazi wa Kigogo jijini Dar es Salaam anasema hali ni mbaya, hivi sasa hata vijana wasiokuwa na kazi wanamiliki silaha.
Alisema hivi sasa huwezi kupita uchochoroni kuanzia saa 4:00 usiku, lazima utakutana na vibaka wakiwa na bastola.

Mkoa wa Kagera
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake, mmoja wa wakazi wa Wilaya ya Ngara alisema kuwa silaha nyingi hasa bunduki za rashasha (sub machine gun) zinanunuliwa nchini Burundi.
“Wakati kambi za wakimbizi za Lukole zikifanya kazi, silaha zilikuwa zikipatikana kwa wingi, lakini kwa sasa kwa kuwa wakimbizi hao wameondoka, silaha zinafuatwa hukohuko,” alisema na kuongeza:
“Kuna watu wana uhusiano na wenyeji wa Burundi, basi wanaziagiza tu… bunduki moja ya SMG ni kama Sh200,000 wanakuletea. Unajua kule kwa sasa kuna njaa kali kwa hiyo yale makundi ya waasi yalikuwa na silaha nyingi hayana jinsi ila kuziuza ili kujikimu kimaisha.”
Kwa upande wake Ofisa Mfawidhi wa Idara ya Uhamiaji katika mpaka wa Rwanda na Tanzania (Rusumo), Mahirande Samuel alisema ni vigumu kudhibiti wahamiaji haramu hasa katika mpaka wa Burundi kwani ni mkubwa na uwezo ni mdogo.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi alisema wahamiaji hao wamekuwa wakishiriki katika matukio ya uhalifu wakishirikiana na wenyeji.
“Wahamiaji haramu wamechangia sana katika matukio ya uhalifu. Wanaharibu mazingira kwa kuchoma misitu, kuchoma mkaa, kupasua mbao na ujangili. Tunafaya juhudi kutekeleza agizo la Rais la kuwaondoa nchini na kazi inaendelea vizuri,” alisema na kuongeza:
“Hadi sasa tumeshakamata silaha aina ya bunduki za gobori 50 ambazo zimesalimishwa, ila wanaosalimisha hatuwajui maana huzitupia kwa viongozi wa vijiji na kukimbia. Silaha tulizokamata ni mbili ambazo ni SMG ikiwa na risasi 70 na gobori moja.
Akizungumzia tukio la Juni 15, mwaka huu, ambapo mabasi mawili yalitekwa na majambazi na kuwapora abiria katika pori la Kasindaga, Kamana Kalangi alisema bado uchunguzi unafanyika, lakini kuna kuhusika kwa wahamiaji haramu wakishirikiana na wenyeji.
Naye Mkuu wa Mkoa huo, Kanali Fabian Massawe alisema kuwa majeshi ya Tanzania kwa sasa yanajipanga kwa ajili ya operesheni ya kuwaondoa wahamiaji haramu mkoani humo.
Kwa sasa majeshi yetu yanajipanga kwa ajili ya operesheni, alisema na kuongeza:
Kama Serikali itasaidia tunataka operesheni hii iwe endelevu, ila hatuwezi kuweka kambi za jeshi mipakani kwa sababu sheria za kimataifa haziruhusu. Operesheni hii ni kwa wahamiaji wa nchi zote zinazotuzunguka. Nashangaa Rwanda peke yao wanalalamika.

Moshi anasema ukiritimba katika upatikanaji silaha serikalini si sababu ya watu kununua silaha kwa njia za siri, bali ukosefu wa ajira kwa vijana na mmomonyoko wa maadili ndivyo vilivyoifikisha hali ya kutokuwa na usalama mahali ilipo leo.
“Taratibu za upatikanaji wa silaha serikalini siyo tatizo, migogoro katika nchi jirani ndiyo inayofanya silaha zipatikane kwenye mipaka yetu,” anasema.
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Profesa Tolly Mbwete alisema suala la upatikanaji silaha haramu si la Tanzania peke yake, nchi inapaswa kushirikiana na nchi zote na kushauri serikali za mitaa kushirikiana na vyama vya siasa kudhibiti tatizo hilo.
Naye, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Gaudence Mpangala alisema upatikanaji wa silaha kiholela unatokana na kubadilika kwa mfumo wa maisha na kwamba baadhi ya watu siku hizi wanamiliki silaha kama njia mojawapo ya kujipatia fedha kwa njia za uhalifu.
“Kuna mianya mingi ya kumiliki silaha kinyume na sheria, Serikali imeweka sheria ambazo ni lazima zifuatwe,” alisema.

Sunday, August 11, 2013

Miss Hong Kong finalist denies being girl inside nude photo


First, they were criticised for being 'ugly' and 'weird'. Then, they were mocked for having a fleshy midriff.
But a majority of the Miss Hong Kong finalists probably don't have it as tough as Tammy Ouyang, who was blasted for having undergone plastic surgery and also for being flirtatious when interacting with people online.
The task of reversing that negative impression was made even more insurmountable after she was recently embroiled in a nude photo scandal.

According to a report by Hong Kong media outlet Nownews, Tammy Ouyang was said to resemble a girl who posed topless with a guy hugging her from behind in a photo that has been circulating online.
When grilled over the photo, the 20-year-old vehemently denied that she was the girl at the centre of this controversy, and swore that she was innocent.

Despite that, she found herself under the spotlight once more after she posted a photo which showed off her chest, accompanied by a comment that read "Do you want to kiss my ball?"
Her post received flak from netizens, which led to her coming out to apologise for her actions.
But it leaves one to wonder if Tammy will finally be able to let her beauty and wit do the talking for her, or if she is just one step away from self-destruction.
SYDNEY - Two commercial planes collided on the tarmac at Australia's Melbourne airport on Saturday, officials said, damaging the aircraft but causing no injury to passengers. The crash, between a reversing Virgin Australia 737 and an A320 Jetstar craft, saw one jet lose part of its tail cone and the other suffer wing damage, according to engineers who witnessed the damage.
"There were no injuries from (an) accident involving two aircraft which made contact while taxiing this morning, (which is) now under investigation," Melbourne Airport said on its Twitter feed.
"Airport operations as normal. Two gates temporarily out of use pending investigation."
The Virgin aircraft, bound for Maroochydore and carrying 175 passengers, hit an empty Jetstar plane as it was leaving the gate for take-off at about 9:30am, Virgin said.
Its wing-tip was damaged but the Jetstar aircraft lost the end of its tail cone, said engineer Paul Cousins, who described it as a lucky escape and put the damage bill at at least A$3 million for each airline.
"They were very lucky that the winglet did not go into the (tail cone's) auxiliary power unit, which is a small jet engine that runs in the back of the aircraft," Cousins, who is president of the national aircraft engineers' union, told The Age newspaper.
"It could have caused that engine to rupture... bits and pieces could have come out it and gone flying everywhere."
Disembarking Virgin passenger Luke Grima said there was a serious thud and exclamations of "Oh my God we've just hit another plane" as the jets collided.
"It was as if we ran over something," Grima told the Herald Sun newspaper.
"When we looked out the wing, we could just see the end of the wing had come off and the other Jetstar plane has got some pretty serious damage to its rear."
The Australian Transport Safety Bureau said there were "very well-practised procedures in place" for aircraft gate manoeuvres and it had launched a probe.
"The ATSB is investigating the ground collision in Melbourne," the authority said.
- See more at: http://www.relax.com.sg/article/news/2-planes-collide-at-australia-airport#sthash.dmisMb08.dpuf

New case of H7N9 bird flu confirmed in China: officials


BEIJING - A Chinese poultry worker was confirmed as having contracted the deadly H7N9 bird flu virus, health officials said, the first case in the southern Guangdong province.
The 51-year-old woman is in a critical condition after she was admitted to hospital on August 3 following signs of a fever, the Guangdong Provincial Health Department said on Saturday.
"She was a poultry slaughtering worker at a local marketplace," the local health bureau said in a statement on its website.

A total of 134 cases have now been reported on the Chinese mainland, including the Guangdong case.
State news agency Xinhua said Saturday that 44 people had died of the disease - which includes a recent fatality following the release of the latest official figures a month ago.

The virus was first reported in late March, with most cases confined to eastern China, and only one reported outside the mainland, in Taiwan.
Scientists reported last week the first likely case of direct person-to-person transmission of the H7N9.
However, they told people to "not panic" as the virus's transmissibility remained "limited and non-sustainable".

Local health authorities Saturday lifted medical observations on 54 of 96 people who were placed under monitoring after they had close contact with the Guangdong patient, Xinhua said.
The patient had worked in markets in Boluo, which is about 129 kilometres (80 miles) east of the provincial capital Guangzhou.

Many of those infected with the virus had direct contact with birds, commonly at poultry markets, which have been closed by officials across China to halt the spread of the disease.
Cases of H7N9 have dropped significantly in recent weeks.

In the southern Chinese city of Hong Kong, which borders Guangdong province, a government spokesman Sunday said the territory is closely monitoring the virus for any developments.

Waingereza waliomwagiwa tindikali waitesa Serikali


Dar es Salaam. Siku tano baada ya raia wawili wa Uingereza kumwagiwa tindikali visiwani Zanzibar, Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi imeibuka na kueleza kuwa bila wananchi kutoa taarifa za ushahidi wa uhalifu wa aina mbalimbali, ni vigumu kuwabaini wahusika.

Kauli hiyo ilitolewa kwa pamoja jana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, Mkemia Mkuu wa Serikali, Profesa Samwel Manyele na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) Eliezer Feleshi, katika mkutano wao na waandishi wa habari, uliolenga kueleza mikakati ya kupambana na matumizi yasiyo sahihi ya tindikali nchini.

Katika ufafanuzi wao walisema, “Kutoa taarifa ya uhalifu wa jambo lolote siyo hiari, ni jukumu la kisheria na kikatiba,” huku Feleshi akitolea mfano jinsi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk Steven Ulimboka alivyoshindwa kutoa ushahidi wa tukio lililomkuta la kutekwa, kupigwa na kisha kutupwa katika Msitu wa Mabwepande, hivyo kufanya uchunguzi kuwa mgumu.

Agosti 7, mwaka huu raia wawili wa Uingereza, Kate Gee (18) na Kirstie Trup (18) walimwagiwa tindikali katika maeneo ya Mji Mkongwe, Zanzibar na vijana wawili waliokuwa wakiendesha pikipiki aina ya Vespa, Waingereza hao wa walisafirishwa siku tatu zilizopita kurudi kwao kwa ajili ya matibabu.

Kuhusu polisi inavyopambana na uhalifu huo aliouita kuwa ni ‘Uhalifu mpya nchini’, IGP Mwema alisema:
“Mkemia Mkuu, Polisi hawawezi kubaini matukio haya bila ushirikiano wa wananchi kwani Tanzania ni nchi kubwa na ina watu zaidi ya milioni 45. Watu wanaingiza tindikali lakini wapo ambao wanatumia tindikali hiyo kwa matumizi haramu.”

Alisema tindikali inaweza kutolewa kwa ajili ya shughuli za viwandani, maabara na usafirishaji na kwamba watu wanapotaka kuitumia kwa ajili ya kufanya uovu wanaweza kugundulika kupitia kwa taarifa zitakazotolewa na wananchi, kwa sababu wanakuwa wamezungukwa na jamii ya watu mbalimbali.
“Kama wanataka kuitumia tindikali kwa ajili ya matumizi mabaya wananchi wanaweza kugundua kwa sababu wanakuwa wanaishi karibu na watu hao, mwananchi mwema anaweza kuwa chanzo kizuri cha kuweza kuzuia na kutoa taarifa za kuwabaini wahusika,” alisema Mwema.

Alisema wananchi wanatakiwa kutambua kuwa shughuli za kibiashara za kuwawezesha kupata kipato cha kila siku hazitafanikiwa kama hakutakuwa na ustawi wa amani.
“Tishio la tindikali linaweza kutia hofu na taharuki katika jamii, hatutaki jambo hili liendelee nchini, tunaamini wazi kuwa hakuna mtu anayeweza kufanya uhalifu akawa peke yake bila kujulikana na mtu hata mmoja,” alisema na kuongeza:

“Tunaweza kubaini kupitia kwa mhusika (mwathirika), mhalifu mwenyewe (anayetenda tendo husika) na mazingira yaliyowezesha mtu ammwagie mwingine tindikali, tukitumia nafasi hizo vizuri, moja kati ya vyanzo hivyo vinaweza kutusaidia kutambua wahusika.”

Japan kujenga kiwanda cha pikipiki


Dar es Salaam. Serikali ya Japan imesema ina mpango kabambe wa kukuza uchumi wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na kampuni kubwa duniani za Honda na Panasonic kujenga viwanda vitakavyokuwa matawi yake hapa nchini.
Uamuzi na msimamo wa Japan umetangazwa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa nchi hiyo, Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Jakaya Kikwete, Ikulu.

Taarifa ya Ikulu iliyosambazwa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Motegi akisema: “Kwa kuanzia kampuni mbili za Honda na Panasonic zimekubali kujenga viwanda nchini, kimoja kwa ajili ya kutengeneza pikipiki za Honda na kingine kwa ajili ya kutengeneza vifaa vya umeme.”

Akaweka msisitizo: “Huu ni mwanzo tu Mheshimiwa Rais (Kikwete) kwa sababu kama nilivyosema kuwa tunataka Tanzania kuwa nchi ya mfano ya uwekezaji wa Japan katika eneo hili la dunia, na namna hiyo kwa pamoja tutakuwa tumeshirikiana katika kuongeza ajira kwa wananchi wa Tanzania.”

Waziri huyo pia alisema kuwa baadhi ya kampuni za Japan zina mipango ya kuwekeza katika kilimo, na hasa kilimo cha pamba na kuanzisha viwanda vya nguo hapahapa nchini.
Motegi alisema mikakakati mingine ya kuisaidia Tanzania ni pamoja na kushiriki uboreshaji wa Reli ya Kati, kusaidia kupanua na kuboresha Bandari ya Dar Es Salaam.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo ya Ikulu, mkakati huo wa Japan unatokana na ziara ya Rais Kikwete nchini humo, Juni mwaka huu.
“Japan imeamua kuanzisha ushirikiano mkubwa zaidi na Tanzania ambako nchi hiyo itaifanya Tanzania kuwa nchi lengwa ya kuwekeza na kuifanya kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji katika Afrika,” inasema sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo iliweka wazi kuwa Waziri Motegi alimweleza Rais Kikwete kuwa ametumwa na Waziri Mkuu Abe, kufuatilia mazungumzo kati yao na kutangaza rasmi kuwa Japan imeiteua Tanzania kuwa nchi lengwa na kitovu cha uwekezaji Afrika Mashariki na Afrika kwa jumla.
Waziri Motegi amesema kuwa katika kufanikisha mkakati huo aliandamana na kundi la wafanyabiashara wa Japan ambao wanaendelea kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa Tanzania, kuona jinsi gani wanavyoweza kusaidiana katika kuwekeza katika uchumi wa Tanzania.

Ponda adaiwa kujeruhiwa kwa risasi


Morogoro. Hali ya wasiwasi imetanda mjini Morogoro baada ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda, kudaiwa kupigwa risasi begani wakati polisi wakiwa katika harakati ya kumkamata.
Habari kutoka katika eneo hilo zinadai kuwa Ponda alipigwa risasi saa 12:25 jioni, wakati akisindikizwa na wafuasi wake kuelekea katika Msikiti wa Mungu Mmoja Dini Moja, baada ya kumaliza kutoa mhadhara katika kongamano lilifanyika mjini Morogoro jana.
Tukio hilo lilitokea katika Barabara ya Tumbaku, baada ya kumalizika kwa mkutano wa kongamano lililoandaliwa na Jumuiya ya Wahadhiri wa Kiislamu Mkoa wa Morogoro.
Mwenyekiti wa Kongamano hilo, Sheikh Idd Mussa Msema aliliambia Mwananchi Jumapili jana kuwa Ponda alipigwa risasi sehemu ya bega, na askari polisi na kwamba aliwahishwa kutibiwa katika Hospitali ya Kiislamu iliyopo eneo Msamvu mjini Morogoro.
Hata hivyo, wakati Sheikh huyo akisema hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alikanusha madai ya kuwa polisi wamempiga risasi.
Alisema polisi walifika katika eneo hilo kwa ajili ya kumkamata Ponda, baada ya kumaliza mhadhara wake na kwamba wakati wakitaka kumkamata ndipo wafuasi wake wakawazuia polisi na kulazimika kupiga mabomu ya machozi na risasi hewani kuwatawanya.
Katika tukio hilo inadaiwa kuwa Sheikh Ponda aliyekuwa katika gari ndogo huku wafuasi wake wakimsindikiza kwa miguu, walipofika eneo la gereji mabomu ya machozi yalipigwa na polisi waliokuwa katika magari aina ya defender wakati wakijaribu kuwatawanya wafuasi hao.
Baada ya tukio hilo baadhi ya wafuasi wake walimchukua Sheikh Ponda kutoka katika gari lake na kumkimbizia katika gereji moja, kisha wakatoka wakiwa wamempakia katika pikipiki na kumpeleka katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro.
Mlinzi mmoja wa lango namba moja alisema kuwa ulifika msululu wa pikipiki zaidi ya 50, lakini pikipiki zote zilizuiliwa isipokuwa iliyokuwa imembeba Sheikh Ponda na kwenda naye mpaka mapokezi.
Aidha, alisema wakiwa katika eneo hilo magari kadhaa ya polisi yaliingia katika lango la hospitali hiyo. Hivyo wafuasi wa Sheikh Ponda wakalazimika kumbeba begani na kutoroka naye kupitia lango namba mbili.
Taarifa zilizopatikana baadaye zinadaiwa kuwa Sheikh Ponda alikimbizwa katika Hospitali ya Kiislamu ya Msamvu.
Baadhi ya watu walidai kumwona Sheikh Ponda akiingizwa katika Hospitali ya Rufaa Morogoro, lakini walishangaa alivyotoweka.

Thursday, May 23, 2013

Ghasia kubwa zazuka Mtwara


Mtwara. Hali ya usalama mkoani Mtwara ni tete. Mtu mmoja anaaminika kufariki dunia na wengine kadhaa kujeruhiwa kutokana na vurugu kubwa zilizozuka jana huko Mtwara baada ya kusomwa hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Madini na Nishati bungeni Dodoma jana.
Aidha, askari wanne wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wamefariki dunia katika ajali wakitokea Nachingwea kwenda Mtwara ili kusaidia kutuliza vurugu hizo. Katika ajali hiyo, askari 20 walijeruhiwa, wengi wao vibaya na saba walinusurika.
Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Dk Mohamed Kodi alithibitisha kupokea maiti moja na kuomba apewe muda kutaja idadi ya majeruhi.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Linus Sinzumwa alidai kwamba hakuna mtu aliyefariki dunia wala majeruhi. Alisema watu 45 wamekamatwa.
Milio ya risasi za moto na mabomu ya machozi vilisikika kila kona na hasa Mitaa ya Mdenga, Magomeni na Shengena Mjini Mtwara ambako hali ilikuwa mbaya kutokana na kuwapo kwa mapambano kati ya polisi na vijana.
Vurugu hizo zilitokana na hatua ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kusisitiza kuwa bomba la gesi kutoka Mtwara na kuja Dar es Salaam litajengwa, jambo lingine linalodaiwa kusababisha ghasia hizo ni hatua ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kutokurusha moja kwa moja matangazo ya Bunge hivyo kuwakosesha wananchi fursa ya kusikiliza bajeti hiyo.
Akizungumzia kukosekana kwa matangazo hayo ya televisheni, Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Clement Mshana alisema kukatika kwa matangazo hayo kulitokana na tatizo la satelaiti katika mji huo na Musoma.
Hata hivyo, wakazi wa Mtwara waliokuwa na ving’amuzi walipata fursa ya kuangalia matangazo hayo.
Pia vurugu hizo zilichangiwa na vipeperushi vilivyosambazwa na watu wasiojulikana wakitaka watu kuacha kufanya shughuli zozote na kukaa nyumbani ili kufahamu hatima ya mradi wa usafirishaji wa gesi kutoka Msimbati hadi Dar es Salaam kwa njia ya bomba.
Katika vurugu hizo zilizozagaa zaidi maeneo ya Mikindani na Magomeni, wananchi pia waliharibu Daraja la Mikindani linalounganisha Mikoa ya Dar es Salaam, Lindi na Mtwara.