Friday, August 26, 2011

Aishi na maiti ndani kwa siku saba

MZEE wa jijini Mbeya, Sadick Salehe, mkazi wa mtaa wa Ilolo Kata ya Luanda, anashikiliwa na Polisi baada ya wakazi wa mtaa anaoishi kukasirishwa na hatua yake ya kukaa ndani na mwili wa mwanawe kwa siku saba na majirani kujenga hisia za kuwa huenda alimwua.

Hisia za wakazi hao zilikuja baada ya kuoanisha kifo hicho na cha mkewe kilichotokea miaka ya themanini, ambapo mzee huyo alimwua kwa kumkata mapanga na kuficha maiti kwenye uvungu wa kitanda kwa siku nne huku akiendelea kulalia kitanda hicho.

Ilielezwa, kuwa tukio la mauaji ya mkewe, lilikuja kubainika baada ya majirani kubaini zimepita siku nyingi hawamwoni mkewe huyo na walipomwuliza hakuwa na jibu la kuwaridhisha hivyo ikawalazimu waombe uongozi wa mtaa upekue ndani ya nyumba hiyo na ndipo wakakuta mwili huo uvunguni na akashitakiwa na kutumikia kifungo cha miaka minane jela.

Akizungumzia tukio la jana, Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Ilolo, Benson Mbwana, alisema juzi akiwa katika mizunguko yake ya kawaida, alipigiwa simu na mkazi wa mtaani hapo ambaye alimjulisha kuwapo tatizo la kushitua nyumbani kwa Mzee Salehe.

Mbwana alisema baada ya kwenda eneo la tukio saa 12 jioni, alimkuta Salehe akiwa na viongozi wa Msikiti wa Soweto, wakijadiliana, na alipouliza akapelekwa katika chumba chenye mwili wa kijana huyo; Salehe Sadiki (38).

Alisema mwili huo ulikuwa umeharibika hali iliyodhihirisha kuwa kijana huyo alifariki dunia muda mrefu na baada ya kumwuliza mzee huyo, akasema aligundua kifo hicho alipoingia katika chumba cha mtoto wake akifuata beseni ili aweke maji.

Jambo lililowashitua wengi ni kuwa eneo la kuzunguka nyumba hiyo lilikuwa na harufu kali hali iliyowafanya wahisi kuwapo mzoga wa mnyama ndani ya nyumba hiyo, lakini wakashindwa kwenda kumhoji mzee huyo, kwa kuwa hakuna jirani ambaye amekuwa akiingia nyumba hiyo.

Hata hivyo, Mwenyekiti huyo wa Mtaa alisema pamoja na harufu hiyo kali, bado mzee huyo ambaye yuko kwenye Mfungo wa Ramadhani, siku zote hizo aliendelea kupika na kula karibu na mlango wa chumba chenye maiti bila kujua mtoto wake alipo.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti baada ya Mzee Salehe kuulizwa, alisema alionana kwa mara ya mwisho na mtoto wake, ambaye alikuwa kiafya amedhoofu kwa muda mrefu.

Jumatano wiki jana na baada ya hapo hakujua yuko wapi, hivyo akabaki na hisia ya kuwa kijana huyo alikuwa kwa wenzake.

“Tulimwuliza unatambua kuwa kijana wako, alikuwa anaumwa na hakumwona kwa siku
hizo zote, iweje usifungue mlango wa chumba hicho kumwangalia. Akajibu kuwa
walikuwa wakiishi kila mmoja na zake, hivyo hata alipokuwa hamwoni hakushtuka,”
alisema.

Mwenyekiti huyo alisema baada ya kuona hayo, aliliarifu Jeshi la Polisi na baada ya askari kufika hapo saa mbili usiku walishindwa kuuchukua mwili kwakuwa ulikuwa umeharibika kiasi cha kupasuka na kila kiungo kilichoshikwa kilikuwa kikinyofoka.

Kufuatia hasira ya wakazi wa eneo hilo ililazimu Jeshi la Polisi kuondoka na mzee huyo, hivyo hakushuhudia maziko ya mwanawe huyo jana kwenye makaburi ya Isanga yakiendeshwa na Serikali ya Mtaa wa Ilolo.

Gazeti hili jana lilifika eneo la tukio na kukuta vijana na wakazi wengine wakitoka makaburini kuzika lakini hali katika chumba alimokuwa maiti bado ilikuwa mbaya kutokana na harufu kali.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Anaclet Malindisa, alikiri kumshikilia Sadiki kwa kuhofia usalama wake na kuongeza kuwa mtuhumiwa huyo anaonekana anasumbuliwa na matatizo ya akili.

Zitto kujiuzuru ubunge

MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, Kabwe Zitto amelieleza Bunge kuwa, endapo itabainika kwamba, mjumbe yeyote wa kamati hiyo alipewa rushwa katika suala la kuiongezea muda taasisi ya Serikali inayosimamia ubinafsishaji wa mashirika ya umma (CHC), si tu atajiuzulu uenyekiti wa kamati hiyo lakini pia atajiuzulu ubunge.

Zitto ametoa ahadi hiyo leo bungeni mjini Dodoma wakati Bunge lilipokaa kama kamati kupitia vifungu vya bajeti ya Wizara ya Fedha kwa mwaka 2011/2012.

Amemtaka Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo naye aliahidi Bunge kuwa ikibainika viongozi wa Serikali walipewa rushwa ya shilingi milioni 60 ili CHC waruhusiwe kufanya kazi hiyo moja kwa moja atajiuzulu.

Mkulo hajatoa ahadi ya kujiuzulu, amesema kwanza uchunguzi ufanyike ndipo lije suala la kujiuzulu au la.

Kwa mujibu wa Zitto, katika hadidu za rejea alizopewa Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) za kuchunguza tuhuma za ubadhirifu CHC, suala la rushwa hiyo halipo.

Mbunge huyo alimtaka Mkulo aagize tuhuma hizo za rushwa ziingizwe kwenye hadidu za rejea alizopewa CAG, na pia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), aagize Taasisi ya Kudhibiti na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ichunguze tuhuma hizo kwa uwazi.

Mkulo amesema, suala hilo litafanyiwa kazi kwa mujibu wa taratibu za Serikali, na kwamba, Bunge litapewa taarifa.

Spika wa Bunge, Anne Makinda, amesema, amepata malalamiko ya wafanyakazi wa CHC lakini hakukuwa na tuhuma za rushwa inayosemwa.

Awali, wakati anajibu hoja za wabunge waliochangia bajeti ya Wizara hito, Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo amelieleza Bunge kuwa, Waziri Kivuli wa Wizara hiyo, Kabwe Zitto ni muongo na mzushi.

Waziri Mkulo amesema, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa CHC, Mathusela Mbajo, hajafukuzwa kazi, kapewa likizo ili CAG amchunguze. Mkulo amewaeleza wabunge kuwa, hajaagiza kiongozi huyo wa CHC afukuzwe kazi ila tuhuma dhidi yake kuhusu ubadhirifu ni nzito.

Jana wakati anawasilisha hotuba ya Kambi ya Upinzani kuhusu bajeti ya Wizara ya Fedha, Zitto alisema, Mathusela amesimamishwa kazi kwa tuhuma zilizozaa majungu kutoka kwa wanaojiita wafanyakazi wa CHC.

“Kufuatia maagizo ya Waziri wa Fedha kwa Bodi ya Wakurugenzi wa CHC Mtanzania huyu kazimamishwa kazi na kwamba, CAG ameombwa kuchunguza majungu yale kutoka kwa mwanaojiita wafanyakazi wa shirika la CHC” alisema Zitto.

Kambi hiyo imepinga uamuzi wa Mkulo kwa maelezo kuwa, amekiuka Sheria namba 3 ya mwaka 1988 ya Haki, Kinga na Madaraka ya Bunge na ilitaka maelezo ya Mkulo kwa nini ameamuru Kaimu Mkurugenzi wa CHA aende likizo wakati anafahamu kuwa suala hilo lipo mezani kwa Spika wa Bunge.

“Bunge hili linapaswa kusimama imara kuzuia kuingiliwa kwa mamlaka yake na tawi la utendaji. Mijadala ndani ya Bunge inalindwa na Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Tusipokuwa makini Bunge litaendelea kudharauliwa na hivyo kushindwa kufanya kazi yake ya kuwawakilisha wananchi, kutunga sheria na kuisimamia Serikali ipasavyo” alisema.

UN yaonya dhidi ya kulipiza kisasi

Waasi nchini Libya
Waasi nchini Libya
Umoja wa Mataifa umetoa wito kwa pande zinazozozana nchini Libya kuchukua hatua za kuhakikisha kuwa visa vya uhalifu na vya kulipiza kisasi havitokei.
Wito huo umetolewa huku ripoti za ukiukaji wa haki za binadamu zikiibuka ambazo zinadaiwa kutekelezwa na pande hizo mbili, upande wa waasi na wanajeshi watiifu kwa Kanali Gaddafi.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya haki za binadamu Rupert Colville amesema kuwa ni vigumu kuthibitisha ripoti hizo za mauaji na unyanyasaji wa watu.
''Tunawasihi wale wote walioko kwenye nafasi za utawala nchini Libya, ikiwa ni pamoja na makamanda wa jeshi, wachukue hatua za dharura kuhakikisha kuwa uhalifu au visa vya kulipiza kisasi havitekelezwi'', Muakilishi huo alisema.

Uhalifu unatekelezwa na pande zote

Shirika la kimataifa kuhusu haki za binadamu, Amnesty International limesema ''linaushahidi wenye nguvu'' wa uhalifu uliotekelezwa na pande hizo mbili pwani mwa mji wa Zawiya, ikiwa ni pamoja na madai ya ghasia zilizotekelezwa na waasi dhidi ya wahamiaji wa Afrika, waliodaiwa kuwa mamluki.
Na Umoja wa Mataifa umekubali kutoa dola billioni moja na nusu amana ya Libya, baada ya kuondoa jina la baraza hilo la kitaifa (NTC), na badala yake kuweka kuwa pesa hizo zitaelekezwa kwa utawala mbadala nchini Libya.
Afrika Kusini ilikuwa imekwamisha hatua hiyo ikidai kuwa ilikuwa na wasiwasi kuwa iwapo Baraza la Mpito la Kitaifa (NTC) litapewa pesa hizo itamaanisha ni kuwatambua waasi hao kama utawala wa Libya, jambo ambalo Muungano wa Afrika haukuwa umekubaliana.

NTC kuhamisha makao yao

Baraza hilo la Mpito la Kitaifa(NTC) limetangaza kuwa linapanga kuhamisha makao yao makuu ya kisiasa kutoka ngome yao ya Benghazi hadi mji mkuu Tripoli.
Mapigano bado yanaendelea mjini Tripoli, mji ambao kwa kiasi kikubwa unadhibitiwa na waasi.
Waasi hao sasa wanajaribu kufika mji wa Sirte, alikozaliwa Kanali Muammar Gaddafi, lakini wamekabiliwa na upinzani mkali.
Kulikuwa na taarifa kuwa ndege za kivita za NATO zilitekeleza mashambulio ya angani usiku kucha mjini humo.

Vigogo Chadema kizimbani

KATIBU wa Jumuiya ya Vijana ya Chadema (BAVITA), Anold Kamunde na aliyekuwa Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema, Gervas Mgonja wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za wizi wa kutumia silaha na kupora vitu na fedha vyote vikiwa na thamani ya Sh milioni 3.5.

Mbali na hilo pia askari Polisi, Salumu Idefonce (23) wa Kituo kikuu cha Polisi Mkoa wa Arusha amefikishwa mahakamani kwa madai ya mauaji ya mlinzi wa kampuni ya kuuza na kununua madini ya Classic Gems, Joseph Kisuda.

Wakisomewa mashitaka na Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Agustino Kombe, ilidaiwa mahakamani hapo, kuwa Mgonja na Kamunde, walifanya hayo wakitumia bunduki aina ya SMG na bastola katika tukio lililotokea Ngarenaro jijini hapa Juni 8.

Kombe alidai hivyo mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha, Rose Ngoka, kuwa
watuhumiwa hao walitenda kosa hilo kwa kumpora Elizabeth Mkuka, fedha taslimu Sh milioni 1.8 na simu mbili.

Aliendelea kudai kuwa Mgonja na Kamunde walitenda kosa hilo saa 3 usiku kwa kiasi hicho cha fedha na simu mbili za Sumsung na BlackBerry zote zikiwa na thamani ya Sh milioni 1.6.

Viongozi hao walikana mashitaka yao na kesi yao itatajwa Septemba 8 na walirudishwa rumande kwani upelelezi haujakamilika na walinyimwa dhamana kutokana na uzito wa kesi yenyewe kisheria.

Katika kesi ya Idefonce, Mwendesha Mashitaka wa Serikali, Sabina Slayo, mbele ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Arusha, Devotha Msofe, alidai kuwa mtuhumiwa anashitakiwa kwa mauaji pamoja na wenzake wawili katika tukio la Mei 21 katika kampuni hiyo ya madini.

Wenzake ambao wako rumande ni Abdul Philipo ‘Baba Salimu’ na Prosper Saimoni ‘Otieno’.

Mshitakiwa hakutakiwa kujibu lolote kwani Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi za mauaji ila Mahakama ya juu yake.

Kesi hiyo itatajwa mahakamani hapo Septemba 6 na alirudishwa rumande hadi siku hiyo.

Habari za nje ya Mahakama zilidai kuwa viongozi wa Chadema wataunganishwa na washitakiwa wengine waliokuwa walisomewa mashitaka juzi katika Mahakama hiyo kwa mashitaka hayo hayo.

Wednesday, August 24, 2011

Indonesian airline Garuda under fire for near-naked interview

Female job applicants were ordered to take off their clothes to be checked for breast implants.
Indonesian airline Garuda under fire for near-naked interview


Would-be flight attendants in South Korea have accused Indonesia’s national airline of making them strip nearly naked and have their breasts handled in medical check-ups, provoking a storm of criticism.
Several dozen candidates for 18 highly-coveted female flight attendant positions with Garuda Indonesia were required to strip down to their panties to screen out those with tattoos or breast implants, one applicant told AFP.

She declined to be named, saying she was still waiting to hear whether she had got a job after the tests last month.
“The hand examination on breast was held since those with implants can have health issues when air pressure falls during flights,” Yonhap news agency quoted an airline official as saying.
Cabin crew are banned from having tattoos and workers hired in other countries such as Japan and Australia were also subject to a similar process, the agency quoted the official as saying.
But the move baffled industry peers and angered women’s rights groups, which called the process unnecessary and intrusive.





Kim Da-Mi, a Seoul-based activist with the Sexual Violence Relief Centre, urged the state human rights agency to take action, telling AFP: “I wonder if such a practice is acceptable in Indonesia.”
Indonesia has the world’s largest Muslim-majority population.
“We’ve never heard of or done such checkup on flight attendants,” said a spokesman for South Korea’s flag carrier Korean Air, calling the Jakarta-based airline’s tests “bizarre”.
“I wonder if that means passengers with breast implants should not fly also,” he told AFP.

A spokesman for Garuda Indonesia’s Seoul office said the medical tests should have followed routine procedures, which do not include such examinations.

“We are investigating the matter by questioning managers and the doctor who was in charge of the checkup... This is very embarrassing,” Park Sung-Hyun told AFP.
Competition for flight attendant jobs is fierce in South Korea, where the role is seen as offering high pay and travel opportunities, and thousands of young women prepare for years before applying for vacancies.

Girl climbs over barbed-wire fence to flee school

She is spotted by an eyewitness, who snaps photographs of her daring escape attempt.
Girl climbs over barbed-wire fence to flee school

Click on thumbnails to view media.


A secondary school girl was seen climbing over her school’s barbed-wire fence in an apparent attempt to play truant.

According to an eyewitness who sent in photographs to citizen journalism website Stomp, the incident took place in Woodlands at around 9.35am on Monday.

He claimed he saw the girl “moving to the edge of the gate” after she had climbed over the fence, and later running away.
“I called the school an hour later to inform them about the dangerous escape but to my surprise the office was not aware of the missing student.
“And I was told there wasn't a CCTV at that gate hence the escape,” he added.
“The security of the school could be improved.”

Photographs show the girl perched precariously on the top of the fence, with a fellow classmate looking on.
The name of the secondary school was not identified in the report.

Russians who gang-raped M'sian student filmed attack on their phones


LONDON: Four wealthy Russians who used an iPhone to film themselves gang-raping a Malaysian student at an exclusive private college in London are facing jail terms.

The group had been in Britain for just two weeks when they carried out the horrific two-and-a-half hour attack on the Malaysian teenager at the £30,000-per-year (RM146,000) college.

The Daily Mail reported that the Russians, aged between 19 and 23, gave a sickening running commentary - and even filmed themselves boasting about what they were going to do to the victim the day before the attack.
 The prosecution fear that she may have had her drinks spiked as she was too drunk to consent.

Oleg Ivanov, 23, Norayr Davtyan, 22, Armen Simonyan, 19, and 23-year-old Gregory Melnikov all denied rape but were unanimously convicted by a jury at Woolwich Crown Court yesterday.
Davtyan described the girl as a "machine" and in the witness box referred to her as a "sl**".
The court heard that Ivanov expressed "pity" for the victim when they noticed she was crying but was talked out of it by his friend Davtyan.

Prosecutor Peter Clement said the four watched and encouraged each other during the attack, and gave a running commentary as to what they had done and what they were going to do to their fellow student.
They referred to her merely in the abstract as "her" or "she" and in the course of the incident one of the four even had to ask another, "What's her name?''

International water polo player Davtyan was holding a party at his dorm at the exclusive college in South London on Jan 21 this year which the girl attended. She had a shot of whisky at the party before going to a disco at the school.

Although there is no concrete evidence her drink was spiked, she felt "funny, dizzy and peculiar" and was clearly intoxicated before going back to the party and vomiting, then falling asleep. The next time she awoke, a man was having sex with her but she was unable to move, the jury heard.

She told police: "I just wanted him to stop, I couldn't wake up, I couldn't stand up, I felt really, really, really tired, I couldn't do anything. I couldn't move my hand...
"I just wanted to close my eyes, I just wanted to die, I did not consent to it."

The four men were all unanimously found guilty of rape at Woolwich Crown Court.
They sat emotionless in the dock as the verdicts against them were read out but a cry was heard from the family members in the public gallery.

Davtyan was convicted on two counts of rape, Melnikov was guilty of rape and attempted rape while Ivanov and Simonyan were both convicted of one count of rape.

They were remanded in custody until they are sentenced.

Jairo asafishwa

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, amerejeshwa kazini baada ya tuhuma dhidi yake zilizotolewa bungeni kutothibitishwa.

Katibu Mkuu Kiongozi, Phillemon Luhanjo, aliwaambia waandishi wa habari jana Dar es Salaam, kwamba Jairo anarejea kazini leo, kuendelea na nafasi iliyokuwa ikikaimiwa na Eliakim Maswi.

Alipewa likizo Julai 21 kupisha uchunguzi dhidi yake. Luhanjo alisema matokeo ya uchunguzi wa awali uliofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), haukuthibitisha kuwapo kwa usahihi tuhuma zilizokuwa zimetolewa dhidi yake.

Luhanjo aliyefuatana na CAG, Ludovick Utouh na Naibu wake, Jumaa Mshihiri katika mkutano huo, alisema utaratibu wa taasisi kuombwa kuchangia fedha kwa ajili ya kuwezesha
bajeti za wizara zao ni wa kawaida.

Alisema waziri anayepeleka bajeti ya Serikali, hutakiwa kufuatana na maofisa wake. “Kuomba mchango ni suala la kawaida,” alisema Luhanjo ambaye alimpa nafasi CAG aeleze kwa ufasaha matokeo ya uchunguzi huo.

Matokeo ya uchunguzi yaliyosomwa na Utouh yalionesha kuwa ukaguzi maalumu ulibaini kuwa fedha zilizochangwa kwa mtindo unaotuhumiwa hazikufikia Sh bilioni moja na taasisi zilizohusika katika uchangiaji huo si 20 kama tuhuma zinavyodai.

Kuhusu madai kwamba fedha hizo zilitumika kushawishi wabunge kupitisha bajeti ‘kiulaini’, Utouh alisema ukaguzi wake haukupata ushahidi wowote juu ya matumizi hayo.

Alisema timu ya ukaguzi ilitumia mbinu zikiwamo za mifumo ya kielektroniki ya kuchambua data na kupata jumla ya malipo kwa kila ofisa.

Katika uchambuzi huo, ilibainika kuwa malipo yaliyofanyika ni kwa ajili ya posho za kujikimu, takrima na posho za vikao, kwa maofisa walioshiriki shughuli nzima ya kuwasilisha bajeti.

“Hakuna ushahidi wowote wa malipo kwa waheshimiwa wabunge,” alisisitiza. Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo (CCM), ndiye aliyeibua tuhuma hizo bungeni Julai 18, kwa
kuwasilisha barua iliyoandikwa na Jairo ikizitaka idara na taasisi zote za wizara hiyo, kila moja ichangie Sh milioni 50, kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti.

Wabunge walihoji uhalali wa michango hiyo na matumizi ya fedha hizo zilizopitishwa kwenye akaunti ya Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) katika Benki ya NMB tawi la Dodoma, na kuzua hisia kuwa zililenga kuhonga wabunge kwa kuwashawishi ili bajeti ipite kirahisi.

Akifafanua zaidi juu ya uchunguzi, Utouh alisema walibaini kuwa jumla ya fedha zilizochangwa ni Sh 578,599,100 na si Sh bilioni moja iliyotajwa kwenye tuhuma.

Alisema taasisi nne za wizara zilichangia jumla ya Sh 149,797,600. Alizitaja taasisi hizo na fedha zilizochangiwa kwenye mabano kuwa ni Wakala wa Nishati Vijijini –REA (milioni 50/- ), Shirika la Umeme Tanzania –Tanesco (milioni 40/-), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania –TPDC (milioni 50/-) na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) iliyochangia Sh 9,797,610.

Idara ya Uhasibu ilichangia Sh 150,720,000 na Idara ya Mipango Sh 278,081,500. Hata hivyo, Utouh alisema Ewura ambayo ilikuwa imeombwa Sh milioni 40 haikutuma mchango wake GST kama ilivyokuwa imeagizwa, bali ilijitolea kugharimia chakula cha mchana na kiasi cha Sh 3,656,000 kilicholipwa kwa Kampuni ya African Conference Centre Ltd na kupokewa kwa stakabadhi namba 917 ya Julai 18, 2011.

Utouh alisema Ewura ililipia gharama za tafrija iliyofanyika Julai 18 jioni katika ukumbi wa St Gaspar kwa gharama ya Sh 6,141,600.

Alifafanua kuwa taarifa ya benki ya Julai 29, kuhusu akaunti namba 505100068 ya GST iliyotumika kukusanya fedha zilizochangwa, inaonesha kuwa jumla ya Sh 99,438,380 zilirejeshwa kwenye akaunti hiyo Julai 20.

Pia taarifa hiyo ya benki inaonesha kuwa Sh 14,860,000 zilirejeshwa kwenye akaunti hiyo Julai 27. Baada ya kupitia vitabu vya hesabu vya GST pamoja na kuhoji wahusika, ilibainika
kuwa Sh 99,438,380 zilisalia kutokana na fedha za kuwasilisha bajeti ya wizara kupokewa.

Ilibainika pia kwamba Sh 14,860,000 zilikuwa ni bakaa ya fedha za kikao cha kazi cha kuandaa uwasilishaji wa bajeti, fedha ambazo zilipokewa Julai 27.

Hivyo hadi Julai 29, bakaa ya fedha zilizochangwa kwa ajili ya kuwasilisha bajeti bungeni ilikuwa Sh 195,235,567.33.

Gaddafi:Nitapambana hadi kifo.

sanamu ya Gaddafi
Waasi wakikanyanga sanamu ya Gaddafi

Kanali Muammar Gaddafi ameapa kupigana na waasi hadi kifo au ushindi, ripoti zimesema, baada ya waasi kudhibiti makazi yake mjini Tripoli.

Televisheni inayomuunga mkono Kanali Gaddafi, al-Urubah, imesema Kanali Gaddafi ambaye bado hajulikani alipo, ametoa hotuba akisema kuondoka kutoka kwa makazi yake kulikuwa ni ''mpango''.
Makazi hayo ndiyo yaliyokuwa maeneo ya mwisho chini ya udhibiti wa Kanali Gaddafi mjini Tripoli.
Waasi wamekuwa wakisheherekea mafanikio yao katika bustani ya Green Square, mjini Tripoli.

Sanamu ya Gaddafi yaharibiwa.

Picha za televisheni pia zimeonyesha wapiganaji wakivunja sanamu ya kiongozi huyo na kuipiga mateka baada ya kuuteka Bab al-Aziziya siku ya Jumanne. Waasi hao pia walichukua vifaa mbalimbali katika makazi hayo ya Kanali Gaddafi.

Hata hivyo bado mapambano yanaripotiwa katika mji huo, mkiwemo katika maeneo ya Abu Salim na Hadba na karibu na hoteli ya Rixos, ambapo waandishi wa kigeni wanapoishi.

Mwandishi wa BBC Rana Jawad mjini Tripoli amesema kuwa kuna hisia kuwa huu ndio mwisho wa utawala wa Kanali Gaddafi, lakini sherehe kamili hajitaanza hadi pale yeye na jamaa wake watakapo kamatwa.

Akizungumza na redio moja mjini Tripoli, Kanali Gaddafi ameahidi''kifo au ushindi'' katika mapigano dhidi ya majeshi ya NATO na waasi wa Libya, redio ya al-Urubah ilisema.

Kanali Gaddafi aidha amesema makazi yake yameharibiwa na mashambulio 64 ya angalini ya NATO.
Jumanne asubuhi, wapiganaji wa waasi waliokuwa wamejihami vilivyo walimiminika katika mji mkuu kushiriki katika mashambulio ya Bab al-Aziziya.

Baada ya saa tano ya mapigano makali, walivunja lango kuu na kuvamia makazi hayo.
Waasi walionekana wakiharibu masanamu, mkiwemo sanamu ya dhahabu, ya mkono unaovunja ndege ya kivita ya Marekani. Hema ya Kanali Gaddafi ambayo aliitumia kupokea wageni pia iliteketezwa.

Wametoroka kama panya.

''Tumeshinda makabiliano'' Abdul Hakim Belhaj, kamanda wa ngazi ya juu wa waasi mjini Tripoli aliliambia shirika la al-Jazeera.''Wametoroka kama panya''.

Haijulikani iwapo kanali Gaddafi na jamaa wake walikuwa katika makazi hayo ya Bab al-Aziziya, lakini inaripotiwa kuwa ina mahandaki ya chini kwa chini, yanayounganisha na maeneo mengine ya mji.

Hali sio wazi katika katika mji wa Sirte, alikozaliwa Kanali Gaddafi, ambayo imekuwa ngome ya maafisa wanaomuunga mkono. Ripoti zinasema wanajeshi waliorudishwa nyuma wanaelekea huko.

Wabunge- Bunge limedhalilishwa, Pinda kafedheheshwa

BUNGE limesema, Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo amelidhalilisha na pia amemdhalilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa kumuamuru Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo arudi kazini.

Wabunge wamesema, taarifa ya uchunguzi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu tuhuma kwamba, Jairo alichangisha shilingi bilioni moja ili kuwezesha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini ipitishwe bungeni ilistahili kupelekwa bungeni waijadili kabla Serikali kutoa uamuzi.

Wabunge leo wamejadili kauli ya Luhanjo kama jambo la dharura baada ya wabunge kukubali hoja ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto aliyoitoa asubuhi kabla ya kipindi maswali na majibu na kuifafanua baada ya Kamati ya Bunge ya Uongozi kukutana katika ukumbi wa Spika.

Spika wa Bunge, Anne Makinda aliongoza kikao hicho cha dharura wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

Kabla ya kamati hiyo kukutana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, alisema, kwa kutumia kifungu cha 51 cha Kanuni za Bunge alichotumia Zitto kuwasilisha hoja yake, inamtaka Mbunge aiwasilishe mapema kwa Spika wa Bunge ili atoe uamuzi.

Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai, alimjibu Lukuvi kwamba, kabla ya kuanza kwa kikao cha leo, Zitto alipeleka taarifa fupi kwa Spika wa Bunge kuhusu hoja hiyo kwa hiyo utaratibu umefuatwa.

“Hoja hii nzito kweli…na ndiyo hoja iliyoungwa mkono” amesema Ndugai baada ya Zitto kuiwasilisha kwa mara ya kwanza kabla ya.

Zaidi ya robo tatu ya wabunge waliokuwa ukumbini wakiwemo kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameunga mkono hoja ya Zitto. Ndugai, amesema bungeni kuwa, hoja ya Zitto ni ya msingi kwa kuwa Bunge limedharauliwa.

“Kwa sababu Bunge ni mhimili, hatuwezi kudharauliwa kirahisi”amesema Ndugai na kusisitiza kwamba, Wabunge hawawezi kukaa kimya wakati Waziri Mkuu anadhalilishwa.

“Kama dharau inaweza ikatokea basi huko huko lakini sio ndani ya Bunge hili” amesema Ndugai baada ya wabunge kuijadili hoja ya Zitto na kusisitiza kwamba, kwa kuwa suala hilo lilianzia bungeni, taarifa ya CAG ingepelekwa kwanza kwenye mamlaka hiyo kabla ya uamuzi wa Serikali.

Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Zainab Vullu, wabunge wamepewa jukumu la kuisimamia na kuishauri Serikali kwa niaba ya wananchi hivyo kauli ya Luhanjo imewadhalilisha, na limepokwa mamlaka yake.

Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, amesema, suala hilo lina maslahi kwa Taifa, taarifa ya CAG ingepelekwa kwanza bungeni itendewe haki.

Sendeka amesema bungeni kuwa, Waziri Mkuu amefedheheshwa kwa kuwa Kiongozi huyo wa Shughuli za Serikali Bungeni alisema, kama angekuwa yeye angemchukilia hatua Jairo, na pia Bunge limedhalilishwa.

Kwa mujibu wa Sendeka, kauli ya Luhanjo imelilidhalilisha Bunge na imekiuka Sheria ya Kinga na Madaraka ya Bunge na ibara ya 100 ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Mbunge huyo ametumia Kanuni 117 ya Bunge kuomba iundwe kamati teule ya Bunge kuchunguza jambo hilo ukiwemo utaratibu wa Jairo kukusanya fedha za kupitishia bajeti hasa ikizingatiwa kuwa, kila Waziri huwa na fungu la kugharamia bajeti kila idara zikiwemo fedha za kununulia mafuta.

Sendeka aliomba Bunge liunge mkono hoja yake ili kulinda hadhi ya Bunge, takribani wabunge wote walikubali isipokuwa mawaziri na manaibu mawaziri.

Wakati anatoa hoja hiyo, Zitto amesema, kwa kuwa jambo hilo lilianzia bungeni wakati Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo (CCM) alipolieleza Bunge kuwa ana barua ya Jairo kuzitaka idara katika Wizara za Nishati na Madini zichangie shilingi milioni 50 kila moja, wabunge walistahili kuijadili ripoti ya CAG kabla ya Serikali kufanya uamuzi.

Zitto amelieleza Bunge kuwa, kauli ya Luhanjo ni dharau kwa Waziri Mkuu, na imeingilia hadhi, kinga na madaraka ya Bunge kwa kuwa wabunge ndiyo wana mamlaka ya kuisimamia Serikali.

Zitto alipendekeza kwamba, shughuli na hoja zote za Serikali bungeni zisitishwe, kwanza wabunge waijadili taarifa za CAG kwa kuwa Bunge limepokwa nafasi yake.

Ndugai amewaeleza wabunge kuwa, Spika wa Bunge, Makinda, ataunda tume kuchunguza kudharauliwa kwa Bunge, na kukusanywa kwa fedha kwa ajili ya kupitishwa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2011/2012.

Kwa mujibu wa kiongozi huyo wa Bunge, tume hiyo itapaswa kufanya kazi haraka ili taarifa yake ijadiliwe katika mkutano ujao wa Bunge.

Luhanjo jana alimuagiza Jairo arudi kazini leo aendelee na madaraka yake katika Wizara ya Nishati na Madini kwa kuwa tuhuma zilizotolewa dhidi yake hazikuthibitika.

Leo asubuhi, Jairo alikwenda ofisini kwake wizarani jijini Dar es Salaam, wafanyakazi wakampokea kwa shangwe na vigelegele huku wakiimba kwamba wana imani naye.