Thursday, September 26, 2013

Askari alivyookoa zaidi ya watu 100 Kenya

Askari wa Kikosi Maalumu cha Anga (SAS) cha Uingereza, ameonekana shujaa katika tukio la uvamizi lililotokea katika jengo la maduka la Westgate jijini Nairobi Kenya baada ya kufanikiwa kuokoa watu 100 waliokuwa ndani ya jengo hilo.
Askari huyo ambaye jina lake halikutajwa kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni sababu za kiusalama,  wakati wavamizi hao wanavamia jengo hilo siku ya Jumamosi, naye alikuwemo ndani ya jengo hilo akinywa kahawa.
Kwenye baadhi ya mitandao, askari huyo ameonekana akiwasaidia wanawake wawili huku akiwa ameweka bastola kwenye suruali yake, ingawa sura yake imefichwa.
Habari zinasema kuwa, askari huyo ameonekana shujaa kwani licha ya hali tete iliyokuwa ndani ya jengo hilo, aliweza kuingia na kutoka zaidi ya mara 12 akiwaokoa baadhi ya watu waliokwama ndani ya jengo hilo lenye maduka na migahawa mbalimbali.
“Alichofanya ni kitendo cha kishujaa sana, alikuwa akinywa kahawa na baadhi ya rafiki zake wakati wavamizi walivyoingia.
Alirudi ndani mara 12 na kufanikiwa kuokoa zaidi ya watu 100. Fikiria kuthubutu kurudi ndani huku akijua kabisa jinsi hali ilivyo ndani ya hilo jengo,” baadhi ya mashuhuda walinukuliwa.
Habari zaidi zinaeleza kuwa, askari huyo wa Uingereza  anafanya zaidi shughuli zake Kenya na nje ya nchi hiyo ikiwa ni pamoja na kuwafuatilia raia wa nchi yake wanaojishughulisha na mambo mbalimbali.
Agosti mwaka huu, gazeti la Daily Mirror liliripoti kuwa kikosi maalumu cha SAS na askari maalumu wa kupambana na ugaidi,  wameanza kumtafuta Samantha Lewthwaite, Mwanamke anayetajwa kuwa ni raia wa Uingereza anayedaiwa kuwa gaidi ambaye pia anashirikiana na kundi la  Al-Shabaab.
Mwanamke huyu mjane anayetajwa kuwa ni gaidi, inasemekana pia alishiriki kupanga na kutekeleza uvamizi mjini Nairobi.
Kikosi hicho cha SAS, kinaelezwa kuwa kinafanya kazi kwa ukaribu na vikosi vya ulinzi vya Uingereza, Kenya na vile vya nchi nyingine za Afrika Mashariki.
Habari juu ya askari huyo zimekuja wakati milio ya risasi ikizidi kusikika ndani ya jengo hilo, huku maofisa wa usalama wa nchi hiyo wakisema kuwa wamedhibiti sehemu kubwa ya jengo hilo. Habari zaidi zinasema kuwa, bado zaidi ya watu 10 wanashikiliwa ndani ya jengo hilo kama mateka.
‘Tumeshadhibiti sehemu yote ya jengo, tuko hapa kuhakikisha tunawaadhibu vya kutosha hawa watekaji,” Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Kenya, IGP David Kimaiyo aliandika kwenye mtandao wake wa Twitter.

Licha ya maelezo hayo, mpaka jana saa 12 asubuhi bado milio ya risasi ilikuwa ikizidi kusikika ndani ya jengo hilo.
Kundi la Al-Shabaab, lililodai kuhusika na tukio hilo, juzi liliweka ujumbe wa sauti kwenye baadhi ya mitandao likidai kuendelea kushikilia sehemu kubwa ya jengo hilo. “Licha ya juhudi zinazofanywa, bado tunaendelea kushika sehemu ya jengo la Westgate,” Msemaji wa Al-Shabaab Sheik Ali Mohamud anasema.
Mtandao wa Daily Mail unasema kuwa, Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Amina Mohamed anasema raia watatu wa Marekani na mmoja wa Uingereza, ni kati ya watu waliovamia jengo hilo la Westgate.
“Mvamizi kutoka Uingereza ni mwanamke ambaye amekuwa akijaribu kutekeleza uvamizi kama huu mara nyingi,” anasema Mohamed akimlenga Samantha Lewthwaite, anayedaiwa kuwa gaidi wa kimataifa.
Marekani imesema kuwa, inaendelea kufanya uchunguzi ili kubaini kama kuna raia wake yeyote aliyehusika kwenye tukio hilo ambalo mpaka sasa limegharimu maisha ya watu zaidi ya 60.
Makala haya yameandikwa na Fredy Azzah kwa msaada wa vyombo vya habari.

Sunday, September 1, 2013

In shock move, Obama puts Syria strike on hold

WASHINGTON - President Barack Obama has postponed threatened missile strikes against Syria in a risky gamble that he can win more support for his plan to punish Bashar al-Assad's regime.
To general surprise, the US leader broke with decades of precedent to announce that he would seek approval from Congress for action against Syria's alleged use of chemical weapons.
This effectively pushed military action back until at least September 9, when US lawmakers return from their summer recess.
Obama insisted that he reserves the right to strike regardless of Congress's decision, and a White House official said the pause would also allow him time to build international support.
The Arab League meets in Cairo on Sunday and is expected to condemn Assad, and Obama travels to Russia next week for a G20 Summit that will now be overshadowed by the crisis.
But the toughest battle, and perhaps the most dangerous for Obama's credibility, may yet be with his own former colleagues in Congress, where support for strikes is far from assured.
Indeed, observers warned that he faces the same fate as Prime Minister David Cameron, who on Thursday lost his own vote on authorizing military action in the British parliament.
"The chairman of the joint chiefs has informed me that we are prepared to strike whenever we choose," Obama warned during an address in the White House Rose Garden.
"Our capacity to execute this mission is not time-sensitive. It will be effective tomorrow or next week or one month from now."
At least five US warships armed with scores of Tomahawk cruise missiles have converged on the eastern Mediterranean ready to launch precision strikes on Syrian regime targets.

Father argues with angry crowd after child pees in Shanghai subway


A video has gone viral on the Internet, showing a father getting into a fight with other commuters after letting his infant urinate on the subway.
The six-minute long video shows a father quarrelling violently with commuters who are heard voicing their anger at the parents' actions.
The video has sparked even larger waves of condemnation by netizens after it was made public, Chinasmack reported.
Nearly all the comments made on the video were in criticism of the parents' "extremely uncivilised" behaviour, Chinese media reported.
The Chinese media reported that what is more outrageous is that upon seeing the public respond negatively to their behaviour, the father can be seen in the video taking out his handphone to say: "I've gotten into trouble in the subway, hurry and bring some people over."
His actions earned him the disapproval of even his wife, who can be heard in the video saying: "If you have the guys, fight yourself. Don't call other people."

Bastola nje nje, zauzwa mitaani nchini

Dar/Mikoani. Kukithiri kwa rushwa miongoni mwa baadhi ya maofisa wa Jeshi la Polisi nchini, kumesababisha silaha ndogondogo hususan bastola kumilikiwa na watu wasio na sifa nchini.
Uchunguzi wa kina wa gazeti hili katika mikoa mbalimbali nchini ikiwamo iliyopo mipakani inaonyesha kuwa, bastola zinamilikiwa na watu bila ya kufuata taratibu na nyingine zikitumika kwa ajili ya kufanyia uhalifu.
Hivi sasa hata vibaka ambao awali walikuwa wakitumia visu na mbao za misumari kupora mali za watu, sasa wanafanya uhalifu huo kwa kutumia bastola.
Mbali ya vibaka kumiliki bastola, wahamiaji haramu walioko ndani ya mipaka ya Tanzania inayopakana na Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wanadaiwa kuingiza silaha nzito, ambazo zinatumika kwa ajili ya matukio ya kihalifu.
Jinsi silaha zinavyopatikana
Uchunguzi unaonyesha moja ya njia ambayo imekuwa ikitumika watu wasiokuwa na sifa kupata bastola au bunduki ni kutumia mawakala au baadhi ya maofisa polisi, waliopo katika mikoa mbalimbali ambao huwatafutia vibali vya kumiliki.
Utaratibu wa kawaida ni kwamba waombaji wanaotaka kumiliki silaha ni lazima wajadiliwe katika kamati za ulinzi na usalama za mtaa au kijiji, wilaya na mkoa na kuhojiwa ili kujiridhisha kama mwombaji ana sifa.

Mkoa wa Kilimanjaro
Uchunguzi  umebaini kuwa baadhi ya vijana wadogo wakiwamo wafanyabiashara, wana vibali vya kumiliki bastola mkoani Kilimanjaro na hawakupitia mchakato huo.
“Unataka kibali cha kumiliki bastola? Una milioni moja na nusu nikuunganishe na jamaa Dar anakufanyia process (mchakato) zote anakuletea kitabu,”alisema kijana mmoja jina tunalihifadhi.
Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika, baadhi ya maofisa wa Jeshi la Polisi makao makuu na wale waliopo mikoani, wamegeuza suala la kumilikisha watu silaha kama mradi wa kujitajirisha.
“Tatizo la nchi hii ni corruption (rushwa) kwa sababu unajiuliza hivi hawa vijana wadogo kabisa wanamiliki bastola na hawakujadiliwa kwenye kikao chochote,”alidokeza mfanyabiashara mmoja.

Uchunguzi zaidi umebaini kuwa wapo wanaojiita wafanyabiashara, lakini ni matapeli wa kimataifa nao wamepewa vibali vya kumiliki bastola na wakati mwingine huzionyesha waziwazi wakiwa baa.
“Ufyatuaji wa risasi siku hizi umekuwa holela…ninavyofahamu ukifyatua hata risasi moja, lazima uandikishe maelezo polisi ulifyatua kwa sababu zipi siku hizi lakini hilo halifanyiki,” ilidokezwa.
Inadaiwa kuwa kutokana na kuwapo kwa ulegevu wa vyombo vya dola hususan Polisi, baadhi ya wamiliki wa bastola hizo wamekuwa wakizikodisha kwa majambazi ambao huzitumia katika uporaji.
Kwa mujibu wa uchunguzi huo, ulegevu huo katika kudhibiti matumizi ya silaha, kumetoa mwanya kwa baadhi ya wamiliki kukodisha bastola zao na kurudishiwa baada ya matukio pasipo kugunduliwa.
Dar es Salaam
Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili unaonyesha kuwa kuongezeka kwa idadi ya watu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria jijini Dar es Salaam, kumeongeza matukio ya uhalifu.
Baadhi ya watu ambao wapo karibu na maofisa wa polisi makao makuu wamekuwa wakitumia nafasi hiyo kuwatafutia watu vibali vya kumiliki silaha.
Watu hao wamekuwa wakijipatia Sh600,000 hadi Sh900,000 kwa kibali kimoja cha kumiliki silaha.
Hali hiyo imesababisha wahalifu wengi wakiwamo vibaka mitaani kumiliki silaha ambazo wanazitumia kupora watu mitaani.
Mussa Radhamn Mkazi wa Kigogo jijini Dar es Salaam anasema hali ni mbaya, hivi sasa hata vijana wasiokuwa na kazi wanamiliki silaha.
Alisema hivi sasa huwezi kupita uchochoroni kuanzia saa 4:00 usiku, lazima utakutana na vibaka wakiwa na bastola.

Mkoa wa Kagera
Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake, mmoja wa wakazi wa Wilaya ya Ngara alisema kuwa silaha nyingi hasa bunduki za rashasha (sub machine gun) zinanunuliwa nchini Burundi.
“Wakati kambi za wakimbizi za Lukole zikifanya kazi, silaha zilikuwa zikipatikana kwa wingi, lakini kwa sasa kwa kuwa wakimbizi hao wameondoka, silaha zinafuatwa hukohuko,” alisema na kuongeza:
“Kuna watu wana uhusiano na wenyeji wa Burundi, basi wanaziagiza tu… bunduki moja ya SMG ni kama Sh200,000 wanakuletea. Unajua kule kwa sasa kuna njaa kali kwa hiyo yale makundi ya waasi yalikuwa na silaha nyingi hayana jinsi ila kuziuza ili kujikimu kimaisha.”
Kwa upande wake Ofisa Mfawidhi wa Idara ya Uhamiaji katika mpaka wa Rwanda na Tanzania (Rusumo), Mahirande Samuel alisema ni vigumu kudhibiti wahamiaji haramu hasa katika mpaka wa Burundi kwani ni mkubwa na uwezo ni mdogo.
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi alisema wahamiaji hao wamekuwa wakishiriki katika matukio ya uhalifu wakishirikiana na wenyeji.
“Wahamiaji haramu wamechangia sana katika matukio ya uhalifu. Wanaharibu mazingira kwa kuchoma misitu, kuchoma mkaa, kupasua mbao na ujangili. Tunafaya juhudi kutekeleza agizo la Rais la kuwaondoa nchini na kazi inaendelea vizuri,” alisema na kuongeza:
“Hadi sasa tumeshakamata silaha aina ya bunduki za gobori 50 ambazo zimesalimishwa, ila wanaosalimisha hatuwajui maana huzitupia kwa viongozi wa vijiji na kukimbia. Silaha tulizokamata ni mbili ambazo ni SMG ikiwa na risasi 70 na gobori moja.
Akizungumzia tukio la Juni 15, mwaka huu, ambapo mabasi mawili yalitekwa na majambazi na kuwapora abiria katika pori la Kasindaga, Kamana Kalangi alisema bado uchunguzi unafanyika, lakini kuna kuhusika kwa wahamiaji haramu wakishirikiana na wenyeji.
Naye Mkuu wa Mkoa huo, Kanali Fabian Massawe alisema kuwa majeshi ya Tanzania kwa sasa yanajipanga kwa ajili ya operesheni ya kuwaondoa wahamiaji haramu mkoani humo.
Kwa sasa majeshi yetu yanajipanga kwa ajili ya operesheni, alisema na kuongeza:
Kama Serikali itasaidia tunataka operesheni hii iwe endelevu, ila hatuwezi kuweka kambi za jeshi mipakani kwa sababu sheria za kimataifa haziruhusu. Operesheni hii ni kwa wahamiaji wa nchi zote zinazotuzunguka. Nashangaa Rwanda peke yao wanalalamika.

Moshi anasema ukiritimba katika upatikanaji silaha serikalini si sababu ya watu kununua silaha kwa njia za siri, bali ukosefu wa ajira kwa vijana na mmomonyoko wa maadili ndivyo vilivyoifikisha hali ya kutokuwa na usalama mahali ilipo leo.
“Taratibu za upatikanaji wa silaha serikalini siyo tatizo, migogoro katika nchi jirani ndiyo inayofanya silaha zipatikane kwenye mipaka yetu,” anasema.
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Profesa Tolly Mbwete alisema suala la upatikanaji silaha haramu si la Tanzania peke yake, nchi inapaswa kushirikiana na nchi zote na kushauri serikali za mitaa kushirikiana na vyama vya siasa kudhibiti tatizo hilo.
Naye, Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Gaudence Mpangala alisema upatikanaji wa silaha kiholela unatokana na kubadilika kwa mfumo wa maisha na kwamba baadhi ya watu siku hizi wanamiliki silaha kama njia mojawapo ya kujipatia fedha kwa njia za uhalifu.
“Kuna mianya mingi ya kumiliki silaha kinyume na sheria, Serikali imeweka sheria ambazo ni lazima zifuatwe,” alisema.