Monday, January 30, 2012

Urais CCM 2015 balaa


KIGOGO AMWAGA MAMILIONI, ATUMA MAKADA MIKOANI KUMNYOSHEA NJIA
Na Mwandishi Wetu
WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikionya wanachama wake kuacha ndoto za urais wa mwaka 2015, kauli hiyo sasa imeonekana kupuuzwa na kugeuka kichocheo cha kuongeza kasi ya kujipanga kwa baadhi ya makada wenye nia ya kusaka nafasi hiyo ya juu ya uongozi wa taifa.Hivi karibuni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM, Nape Nnauye, alionya kwamba chama hicho hakiko tayari kuendelea kuwakumbatia wanachama wake wanaunda makundi ndani ya chama, kwa lengo la kusaka umaarufu wa kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu ujao mwaka 2015.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jijini Dar es Salaam, Nape alisisitiza kuwa endapo mwanachama yeyote atabainika kuvuruga mshikamano ndani ya chama kutokana na kigezo hicho, CCM haitasita kuchukua hatua kali dhidi yake.

Pamoja na CCM kutoa onyo hilo kali, mbio za urais wa mwaka 2015 ndani ya chama hicho, zimeelezwa kuingia katika sura mpya baada ya mmoja wa makada anayetajwa kuwania nafasi hiyo, kufanya kikao kizito jijini Arusha, kwa lengo la kuweka mikakati ya kujipanga na kuimarisha kambi yake.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na baadhi ya wana CCM mjini Arusha, zinaeleza kuwa, kigogo huyo alifanya kikao chake wiki chache zilizopita katika moja ya majengo ya mfanyabiashara mmoja kutoka Kanda ya Ziwa, yaliyopo nje kidogo ya jiji.

Kikao hicho kilichohudhuriwa na baadhi ya viongozi wa CCM kutoka mikoa mbalimbali nchini, wakiwamo baadhi ya wenyeviti wa mikoa wa chama hicho na baadhi ya viongozi wa Serikali, pamoja na mambo mengine, kilifanya tathmini ya kina kujua maeneo ambayo mgombea huyo hakubaliki.

Chanzo chetu kilidokeza kwamba tathmini hiyo ilionyesha kuwa kada huyo hakubaliki sana katika mikoa ya Lindi , Mtwara pamoja na maeneo ya mikoa ya Kanda ya Ziwa, ukiwemo Mkoa wa Mara.

Kutokana na hali hiyo, ilikubaliwa kuwa fedha nyingi zitumike na watu mahiri wenye ushawishi, watumwe katika maeneo haya ili kuwalainisha baadhi ya viongozi wa CCM ambao wanaonekana kuwa mbali na mgombea huyo, na jambo hilo lifanyike haraka kabla ya kuanza kwa chaguzi mbalimbali ndani ya CCM mwaka huu.

Kauli ya Nape
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alipoliuzwa kuhusiana na kikao hicho, alisema hana taarifa zozote lakini alionya kuwa endapo itathibitika kuwa kuna makada wa chama hicho wanafanya ‘rafu’ hizo, watachukuliwa hatua za kisheria za chama kwani huu si muda wa kufanya kampeni za urais.

Aliwataka wanachama wa CCM kuipa nafasi  Serikali yao kutekeleza majukumu yake na ilani kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania.Awali, pia Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi, aliwahi kukaririwa akisema kuwa wanaotarajia kutumia fedha kupata urais kupitia chama hicho wanajidaganya, ni bora watafute kazi nyingine za kufanya.


 Kikao cha mkakati
Habari zaidi kutoka ndani ya kikao hicho, zililidokeza Mwananchi Jumapili  kuwa makada watakaotumwa kuzunguka mikoani, baada kukamilisha kazi yao, watatakiwa  kurejesha ripoti itakayofanyiwa kazi, ili kundi hilo liweke mikakati zaidi ya kufanikisha lengo lake.

Inaelezwa kuwa hofu kuu ya kundi hilo, ni kutoka kwa baadhi ya makada wengine wa CCM, wanaotajwa kuonyesha nia ya kuwania nafasi ya urais, kukubalika zaidi ndani ya chama katika mikoa hiyo, ambapo baadhi yao  wanatoka huko.
Chanzo chetu kilidokeza pia kuwa mbali ya kuweka mikakati hiyo kabambe ya kuwania urais, pia wajumbe wa kikao hicho ‘kizito’, walifanyiwa sherehe kubwa ambapo nyama na vinywaji mbalimbali vilimwagwa kwa wingi, ndani ya majengo ya mfanyabiashara huyo, ambayo yamezungushiwa ukuta mrefu.

“Aisee! kikao kilikuwa kizito mno mikakati mizito imewekwa , jamaa yuko serious (makini) kuutaka urais, “alidokeza kada mmoja aliyekuwa ndani ya kikao hicho kwa sharti la kutoandikwa jina gazetini.
Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umebaini kuwa tayari, makada waliotumwa kwenda mikoani ‘kumnyoshea njia’ mgombea huyo wa urais, hivi sasa wanavinjari kwenye maeneo hayo, wakiwa na fedha za kutosha na vitendea kazi vingine, yakiwemo magari ya uhakika.

Waliotumwa kufanya kazi hiyo, ni wenyeviti  wa baadhi ya mikoa ambao imeelezwa kuwa watatumia nafasi zao kufanya ushawishi huo kwa urahisi.

Ingawa hadi sasa hakuna kada ndani ya CCM ambaye ametangaza hadharani  kutaka kuwania urais, inadaiwa kwamba kuna kundi kubwa la watu ambao tayari wanapigana vikumbo chini chini kutaka nafasi hiyo, kutokana na Rais wa sasa Jakaya Kikwete, kufikia ukomo wake kikatiba mwaka 2015.

Hatua hiyo imedaiwa kuibua makundi yanayosabisha nyufa zinazoweza kuleta mgawanyiko mkubwa ndani ya chama hicho.
Tayari CCM kimekiri kupitia Katibu Mkuu wake, Wilson Mukama kuwa harakati za kuwania urais ndani ya chama hicho, zinakivuruga.

Taarifa ya Kamati Kuu ya CCM iliyosomwa ndani ya Kikao cha Halmashuari Kuu (NEC) ya CCM mjini Dodoma Novemba mwaka jana ,pamoja na mambo mengine, ilikiri kuwa mbio za kuwania urais mwaka 2015 ndani ya chama hicho, ndicho kiini kikuu cha mgawanyiko.

Kamati Kuu ilionya kuwa wanaotaka kuwania nafasi ya urais kupitia chama hicho, wanapaswa kudhibitiwa na kwamba matumizi ya fedha katika kampeni hayatakubalika.

Ushauri wa Kinana
Alhamisi wiki hii, Mjumbe wa Kamati Kuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alikaririwa na gazeti la Mwananchi akieleza kuwa vigogo wa chama hicho walioanza kampeni za urais, sasa wanavuruga  utendaji wa Serikali ya Rais Kikwete.
Akiwa kwenye ziara ya kutembelea matawi ya CCM Mkoa wa Dar es Salaam, Kinana alisema vigogo hao ni wabinafsi, wanaivuruga nchi na hawana lolote wanalolifanya kwa maslahi ya chama hicho tawala.

Kinana ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa Kampeni za Rais Jakaya Kikwete wakati akigombea urais kwa CCM katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010, alionesha kukerwa na watu hao na kueleza kuwa si sahihi kuanza kuzungumza masuala ya urais sasa wakati Rais Kikwete bado ana miaka minne ya kutekeleza Ilani ya chama hicho.

“Sasa hivi Rais Kikwete ana miaka mingine minne mbele kabla ya kumaliza uongozi wake na CCM ina kero nyingi za kushughulikia ili kutekeleza ilani yake, halafu wengine wanazungumzia urais sasa,” alikaririwa akisema Kinana.
Alisema anasikitishwa na hali hiyo hasa ikizingatiwa kuwa wanaoanza kupiga kampeni za urais ni watu wazito ndani ya nchi na ni wajumbe wa vikao vikuu ndani ya CCM.

Tishio lingine
Mbali ya chama hicho kukabiliwa na tishio la mgawanyiko kutokana na urais wa 2015, pia kinakabiliwa na kazi ngumu ya utekelezaji wa mkakati wake, kuwavua gamba baadhi ya makada wake wanaohusishwa na kashfa za ufisadi.

Kikao kilichopita cha NEC ambacho kilitarajiwa kuchukua maamuzi magumu ya kuwavua gamba wanachama hao, kilishindwa kufanya hivyo,  badala yake kikatoa muda kwa wanachama  hao kujitathmini wenyewe na kuchukua uamuzi kabla ya CCM kuwachukulia hatua.

Serikali yageuka mbogo


• MADAKTARI WASEMA HAWATAENDA KAZINI, KESHO KUKUTANA
SERIKALI imetangaza kuwafuta kazi madaktari wote watakaoendelea na mgomo huku ikiviamrisha vyombo vya dola kuwakamata watakaodiriki kufanya mikutano kwenye maeneo mbalimbali.
Msimamo huo ulitangazwa jana jijini Dar es Salaam katika Ukumbi wa Karimjee na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana mara baada ya madaktari kushindwa kufika kwenye mkutano ulioandaliwa kuzungumzia madai na mgomo wa wataalamu hao.
Pinda aliwaamaru madaktari wanaoendelea na mgomo katika mikoa saba nchini kurejea kazini mara moja leo asubuhi huku akiweka wazi watakaokiuka agizo hilo watapoteza ajira zao.
Alisema serikali inatambua madaktari hao wanaongozwa na kamati ya mpito isiyotaka suluhu licha ya juhudi zilizofanywa za kuwaita kushughulikia madai husika.
“Serikali tayari imechukua tahadhari ya kukabiliana na hali hii kwa kuagiza Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kupeleka madaktari wake katika hospitali za mkoa wa Dar es Salaam ili kusaidia wagonjwa walioko hospitalini. Kwa hiyo huduma zitaendelea kama kawaida,” alisema Pinda.
Katika mkutano huo Pinda aliongozana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Haji Mponda na Naibu wake, Dk. Lucy Nkya; Waziri wa Nchi Ofsi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawa Ghasia; Waziri wa Ulinzi, Dk. Hussein Mwinyi; Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha; na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, George Mkuchika.
Akionekana kukerwa na kitendo hicho cha madaktari hao kushindwa kukutana naye, Pinda alisema kuanzia leo ameviagiza vyombo vya dola kuzuia mikutano yote ya madaktari hao, akisema ni kinyume cha sheria ingawa serikali ilikuwa ikiwavumilia tu.
“Mgomo wao si sahihi kwa sababu haukufuata taratibu za kuuitisha. Wao walipaswa kutangaza mgogoro na kisha kutoa notisi ya siku 60, jambo ambalo hawakufanya,” alisema Pinda na kukipongeza Chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali Kuu (Tughe) kwa kutambua hoja za madaktari hao lakini wakasema njia iliyotumika si sahihi.
Pinda ambaye aliwasili ukumbuni hapo saa 6:12 mchana badala ya saa 4:00 kama ratiba ilivyokuwa, alianza kwa kufafanua chimbuko la mgomo huo na hatua kadhaa zilizochukuliwa na serikali kuutatua.
Alisema tangu mwishoni mwa Desemba mwaka jana, kulikuwa na madai ya wataalamu mbalimbali waliokuwa kwenye mazoezi kwa vitendo (interns) kwamba wangeitisha mgomo kwa sababu ya kucheleweshewa posho zao; alisema juhudi zilifanyika na wakalipwa madai hayo yaliyokuwa yakifikia sh milioni 876.
Waziri Mkuu aliongeza kuwa baada ya malipo kufanyika, mgogoro ulihama kutoka kwa interns na kuwahusisha wataalamu wa kada nyingine za afya wakiwemo madaktari na kwamba kwa kuwa interns hao nafasi zao zilikuwa zimezibwa wakati wakiwa wamegoma, serikali iliona ni vyema kuwasambaza kwenye hospitali nyinge jijini hapa.
“Uhamisho huo ulifanywa kwa nia njema ila wenzetu waliutafsiri kama adhabu ya kuwakomoa interns hao na kupitia Chama chao cha Madaktari (MAT), walileta madai kuwa tuwarejeshe Muhimbili wakitoa sababu nyingi ambazo kimsingi tuliona zina mantiki,” alisema Pinda.
Aliongeza kuwa wakati wakiwa kwenye majadiliano ya hoja hiyo na yeye kuonyesha nia ya kukutana nao, MAT walienguliwa na jukumu hilo kupewa Jumuiya ya Kamati ya Mpito iliyoongozwa na Dk. Stephen Ulimboka, ambayo ilitoa madai nane.
Katika madai yao walitaka posho ya kulala kazini ya sh 10,000 kwa siku, ilipwe kwa kiwango cha asilimia 10 ya mshahara wa mwezi, posho ya kufanya kazi katika mazingira hatarishi iwe asilimia 30 ya mshahara wa mwezi; na posho ya nyumba walipwe asilimia 30 ya mshahara wa mwezi.
Madai mengine ni kupandishwa kwa posho ya kufanya kazi katika mazingira magumu zifikie asilimia 40 ya mshahara, kupatiwa posho za usafiri kwa asilimia 10 ya mashajara iwapo itashindikana wapatiwe usafiri wa kwenda na kurudi kazini.
“Wanadai mshahara wa sh 700,000 ni mdogo sana kwa daktari anayeanza kazi, hivyo wanapendekeza alipwe sh 3,000,000 kwa mwezi. Wanataka kupatiwa bima ya afya pamoja na familia zao kwa kupewa kadi za kijani na wanataka interns warejeshwe Muhimbili bila masharti yoyote,” alisema Pinda.
Hata hivyo, akichambua madai hayo alisema serikali haiwezi kuyapatia ufumbuzi mara moja madai hayo ila taratibu za kuyapatia ufumbuzi zinaendelea huku akikanusha kuwa daktari anayeanza kazi analipwa sh 700,000 bali ni sh 957,7000.
Alisema madaktari hao wamependekeza wanaoajiriwa hivi sasa walipwe mshahara wa sh milioni 3.5 wakati watumishi wa kada nyingine kama wahandisi wanaanza na sh 600,000 na wahasibu wanaanza na mshahara wa sh 300,000; kwamba posho zote wanazodai zikijumuishwa zinafikia asilimia 120 ya mshahara wa daktari mmoja.
“Kwa mujibu wa mapendezo yao ina maana kiwango cha kuanzia mshahara wa mhudumu wa afya kitakuwa sh 670,316 na mshahara wa juu utakuwa sh mil. 8.1 kwa mwezi. Utekelezaji wa pendekezo hili utagharimu sh bil 83.5 kwa mwezi ambayo ni sawa na sh bil. 417.5 kwa kipindi kilichobaki cha miezi mitano,” alisema.
Pinda alifafanua kuwa kwa mujibu wa mapendekezo hayo mshahara na posho, daktari anayeanza kazi atapata sh mil. 7.7 na daktari mshauri mwandamizi atapata sh mil. 17.2 kwa mwezi.
“Endapo madai hayo yatatekelezwa kwa mwaka mmoja jumla ya mishahara yao itakuwa sh bil. 799.7 badala ya sh bil. 222. 2 hadi kufika Juni 2012.
Kiongozi wao si daktari
Katika hatua nyingine, Pinda alisema kuwa katika uchunguzi wao walibaini kuwa kiongozi wa mgomo, Dk. Ulimboka alihitimu shahada ya udaktari katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 2004 na kupata usajili wa muda No. 2022 wa Baraza la Madaktari mwaka huu na kupangiwa internship Muhimbili.
Alisema kuwa Novemba 2005, aliongoza mgomo wa madaktari nchini na usajili wake ulisitishwa na kushtakiwa mbele ya baraza hilo kwa ukiukaji wa maadili ya taaluma ya madaktari kwa kutishia na kufanya mgomo.
Mwaka 2006 Rais alimsamehe na hivyo kurejeshewa usajili na baraza na kuruhusiwa kuendelea na internship.
“Katika kumpa taarifa za msamaha wa Rais, Wizara ya Afya na Baraza la Madaktari walimtaka Dk. Ulimboka kutojihusisha na migomo au suala lolote kinyume na maadili ya udaktari ambapo Februari 2, 2007 alikiri sharti hilo kwa maandishi.
Hadi sasa hakuna taarifa kama alimaliza internship kwa kuwa hajawasilisha cheti cha kumaliza mazoezi hayo na hatuna taarifa anafanya kazi wapi ila si mtumishi wa serikali na hajasajiliwa kama daktari, alisema Pinda.
Dk. Ulimboka anena
Mwenyekiti wa Kamati ya Muda ya Jumuiya ya Madaktari, Dk. Steven Ulimboka, alisema hakuna sheria ya kumfukuza mfanyakazi asiyeenda kazini kwa siku moja na hivyo kuwataka madaktari waendelee kukaa nyumbani.
Alisema leo wanafanya taratibu za kisheria ili kesho wakutane kuzungumzia mgomo huo ambao sasa serikali inaonekana kutaka kutumia nguuvu kuwasambaratisha.
Alibainisha kuwa sababu ya wao kushindwa kwenda kukutana na Waziri Mkuu jana ni kuchelewa kupata barua ya wito wa kuitwa kwenye mkutano.
“Sisi tulipata barua saa 11 jioni na tukaandika barua kumjibu Pinda kuwa hawawezi kukutana leo kwa kuwa wenzao wengine wameshatawanyika, pia tulifanya hivyo kwa kuwa jana tulitarajia wenzetu kutoka mikoani wangewasili Dar es Saalam.”
Kuhusu kutohitimu mafunzo ya udaktari, alisema huo ni uongo kwa kuwa alimaliza mafunzo kwa vitendo katika Hospitali ya Muhimbili na kutunukiwa cheti chake cha udaktari mwaka 2007.

Saturday, January 21, 2012

CCM, CUF wapinga muswada wa mafao ya viongozi

WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi kutoka CCM na CUF wameupinga muswada wa maslahi ya mafao ya viongozi wa kisiasa na kusema kwamba utawabebesha wananchi wa Zanzibar mzigo mkubwa.

Mwakilishi wa Jimbo la Magomeni ambaye pia ni Katibu wa wajumbe wa CCM katika Baraza la Wawakilishi Salmin Awadh alisema wananchi wameukubali mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa kwa matarajio makubwa ya kuimarisha hali zao za uchumi na maendeleo.

Lakini Salmin alisema kwa mujibu wa hali inavyokwenda inaonesha wazi wazi kwamba matarajio ya wananchi katika kupiga hatua ya maendeleo yameanza kuyeyuka kidogo kidogo.

“Mimi siungi mkono mswada huu kwa sababu hauna maslahi ya wananchi wa Zanzibar...huu si wakati wa kuanza kujipangiya maslahi makubwa ya viongozi wakitaifa wakati wananchi wetu hali zao ni duni,”alisema Awadh.

Mwakilishi wa Jimbo la Chonga kwa tiketi ya CUF, Abdallah Juma Abdallah yeye alisema wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wanavunja Katiba kwa sababu wanatakiwa kuupitisha mshahara wa Rais lakini kazi hiyo haifanyiw na wajumbe.

“Kwa mujibu wa Katiba, mshahara wa Rais unatakiwa kuidhinishwa na Baraza la Wawakilishi lakini mimi nipo mwaka wa 14 sasa sijapata kusikia kuidhinishwa kwa mshahara huo,” alisema.

Alisema wananchi wanakabiliwa na matatizo mbalimbali ambayo ni ya msingi ikiwemo huduma za afya na elimu ambazo bado hazijatekelezwa kwa ufanisi. Mwakilishi wa Viti Maalumu, Raya Suleiman (CCM) alisema huu si wakati muafaka wa kupitisha mafao makubwa na manene ya viongozi wastaafu wa serikali.

“Tusubiri hadi uchumi wetu utakapokuwa mzuri na kustawi ndipo tuanze kuwekeana maslahi makubwa ya mafao ya viongozi wastaafu wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar,” alisema Raya.

Madaktari wapiga hodi kwa Pinda

 BAADA ya vuta nikuvute baina ya madaktari wanaoendelea na vikao vya kutaka nyongeza ya posho na mishahara na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, hatimaye madaktari hao wametangaza kuisusa Wizara hiyo na kubisha hodi kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakimwomba asikilize madai yao.

Hatua hiyo imekuja siku moja baada ya juzi kutokea kutokuelewana baina ya Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Lucy Nkya na madaktari hao baada ya kutofautiana juu ya mahali wanapotakiwa kuonana ili kujadiliana.

Wakati Dk. Nkya alikwenda katika ukumbi wa mikutano wa Arnatouglo Mnazi Mmoja ili kuonana na madaktari hao, wao walikusanyika ukumbi wa Don Bosco nao wakimsubiri.

Kutokana na hatua hiyo, madaktari hao chini ya Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), jana waliendelea na vikao vyao vya kudai nyongeza hiyo ya mishahara na posho wakiwa Don Bosco na baadaye Makamu wa Rais wa MAT, Dk. Primus Saidia alitangaza azma ya kukutana na Pinda ili kutafuta jibu la madai yao.

“Napenda kuwafahamisha kwamba baada ya jana (juzi) Naibu Waziri wa Afya kushindwa kukutana nasi, sasa tumeona Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii haina dhamira ya dhati ya kusikiliza hoja zetu.

“Naibu Waziri aliamua kwenda Arnatouglo kukutana nasi wakati hakukuwa na mawasiliano yoyote rasmi ya sisi kuonana naye kule, sisi tulikusanyika hapa (Don Bosco) kumsubiri, kwa vile tulikuwa na mawasiliano rasmi ya kuonana naye hapa.

“Baada ya kutafakari, sasa tumeona suala hili tulifikishe kwa Waziri Mkuu, kwani ndiye kiongozi pekee ambaye sasa tumeona anaweza kutusikiliza na kujibu hoja zetu. Hapa tunaandika barua rasmi kwenda kwa Waziri Mkuu. Rais wetu (Dk. Namala Mkopi) atakwenda kwa Waziri Mkuu na ataambatana na baadhi ya madaktari kati yetu,” alisema Dk. Saidia.

Alisema chama hicho kina imani kubwa na Waziri Mkuu Pinda, kuwa ana uwezo na utashi wa dhati wa kutatua matatizo yao kutokana na kuwa na uhusiano mzuri na chama hicho.

“Nikukumbusheni tu kwamba mara zote Waziri Mkuu amekuwa mtu makini na msikivu sana kwetu. Kama mtakumbuka Novemba mwaka jana Waziri Mkuu alifanya mazungumzo na viongozi wa MAT Mwanza alipokuwa kwenye hafla Chuo Kikuu cha Bugando. Baadhi ya mambo tunayoyatoa leo tulimpa wakati ule, hivyo anafahamu kwa dhati madai yetu,” alisema.

Gazeti hili jana jioni liliwasiliana na mmoja wa viongozi wa madaktari hao ambaye alisema Ofisi ya Waziri Mkuu, ilikuwa tayari imeanza kujibu hoja zilizowasilishwa na madaktari hao kupitia barua maalumu waliyomwandikia Pinda.

“Waziri Mkuu hataweza kuja, lakini ofisi yake imeanza kujibu hoja zetu na viongozi wetu wapo huko wanasubiri majibu tutakayojibiwa ingawa tuna imani kubwa ya kupewa majibu mazuri.

“Tumeambiwa kwamba huenda Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Peniel Lyimo) atakuja kuzungumza na sisi ili kutafuta muafaka. Uwezekano wa kuonana naye kesho (leo) ni mkubwa sana,” alisema kiongozi huyo wa MAT.

Kutoka Mwanza, Grace Chilongola, anaripoti kwamba MAT Kanda ya Ziwa imeiomba Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuacha malumbano na madaktari na badala yake isimamie matatizo yaliyopo ili kuboresha sekta ya afya.

Walitoa ombi hilo jana baada ya kikao cha pamoja kilichojumuisha madaktari wa Kanda ya Ziwa kilichokuwa kikiunga mkono madai ya madaktari wenzao wa Muhimbili.

Akizungumza Katibu wa MAT, Dk. Rodrick Kabangila alisema Serikali iangalie mambo ya msingi katika sekta ya afya kama ya milipuko ya surua inayoendelea kutokea wakati chanjo zinatolewa, ukosefu wa dawa na vifaa badala ya kuendeleza malumbano na madaktari.

Kabangila ambaye pia ni Mwenyekiti wa MAT, Kanda ya Ziwa alisema Serikali inapoendeleza malumbano na madaktari, inaamsha machungu ya madaktari ya siku za nyuma na kutaka kuyafanyia kazi madai yao ya mishahara, posho na kusomeshwa, ili waweze kufanya kazi pamoja.

Aidha, aliiomba Serikali kuangalia ugumu wa shule ya madaktari, gharama kubwa wanayosomea pamoja na changamoto wanazokumbana nazo kazini, kwa kuwalipa kile kinachostahili na si kusingizia kuwa Serikali haina fedha.

Dk. Godfrey Mbawala alisema madaktari hawataki wafikie kwenye mgomo, kwani itakuwa ni vita na watakaoathirika ni wananchi wenye wagonjwa hospitalini.

“Hofu ni kwa wagonjwa watakaokufa na kuziacha familia zao zikihangaika na ugumu wa maisha na ukiuliza sababu ni madaktari kulumbana na Serikali, inatia uchungu sana, hatutaki kufika huko,” alisema na kuiomba Serikali ichukulie suala la madai ya madaktari kwa uzito unaostahili.

Alisema jamii inapaswa kuwaunga mkono ili nao wasiathirike na mgomo unaoweza kutokea .

“Hatutaki kufikia mgomo kutokana na athari zake kuwa kubwa kiuchumi, kidini na kijamii, lakini kwenye mgomo tutafikishwa na Serikali iwapo itashindwa kutusikiliza,” alisema Dk. George Adriano.

Mchakato kutafuta mrithi wa Regia Mtema waanza


Aziza Masoud na Ellen Manyangu
WIKI moja tangu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Regia Mtema kilipotokea, mchakato wa kumtafuta mrithi wa nafasi yake umeanza.

Regia alifariki dunia Jumamosi iliyopita kwa ajali ya gari katika eneo la Ruvu mkoani Pwani na kuzikwa Jumatano wiki hii nyumbani kwao Ifakara, mkoani Morogoro.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili jana zinasema tayari maofisa husika ndani ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) wameanza kushughulikia suala hilo la kuziba nafasi ya mbunge huyo kijana ambaye pia alikuwa mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Julius Mallaba alisema jana kwamba ofisi yake itatumia orodha ya majina yaliyopendekezwa na Chadema mwishoni mwa mwaka juzi.

“Nadhani tunayo orodha ya mapendekezo ya Chadema, basi kwa jinsi taratibu zilivyo, tutarejea katika orodha hiyo na pale tulipopitisha msitari ndipo tutakapoanzia, lakini lazima huyo anayefuata katika orodha awe na sifa za kuwa mbunge,” alisema Mallaba kupitia simu yake ya kiganjani.

Hata hivyo, Mallaba alisema hivi sasa ni mapema mno kufahamu ni lini uteuzi huo utafanyika na kwamba taratibu za ndani zikikamilika, mamlaka husika zitaarifiwa ili umma pia uweze kufahamu.

Awali, Mallaba alikataa kuonana na waandishi wa habari na mmoja wa maofisa wa Tume hiyo alisema: “Amesema majina yametoka hukohuko Chadema ndipo yakaja huku kwa hiyo kama mnayahitaji mnapaswa kwenda katika ofisi za Chadema ili muweze kupata majina hayo.”

Dk Slaa, Zitto wanena
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willbrod Slaa alisema chama chake hakifahamu atakayechukua nafasi hiyo na kwamba hiyo inatokana na ukweli kwamba jukumu hilo liko mikononi mwa NEC.

“Majina ya wagombea wa viti maalumu yapo NEC na wao ndiyo wanaoangalia kuchagua nani anayefuata katika orodha iliyopo Tume, kwa utaratibu, mgombea anayefuata ndiye atakayechukua nafasi hiyo,” alisema Dk Slaa.

Alisema Chadema kilipeleka NEC orodha ya majina 28 ya wabunge wa viti maalumu, Desemba 30, 2010 na kati ya hayo majina 25 tayari wameshachaguliwa ni jukumu la NEC kuangalia jina gani linalofuata kwenye orodha hiyo iliyopo.

Alisema kati ya hayo majina matatu yaliyobaki yeyote atakuwa na uwezo wa kuchukua nafasi hiyo kulingana na vigezo vya NEC na kulingana na utaratibu na Katiba ya Chadema.

“Sina mamlaka ya kujua nani anayefuata na ofisini kwangu hata majina sina majina yapo NEC mimi nawategemea wao waniletee  jina kwa mujibu wa taratibu zao nitaliangalia kama muhusika bado ni mwanachama hai nitawajibu na nitawarudishia na ndiyo watalitangaza kwa wananchi,” alisema Dk Slaa.

Alisema kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi, jina watakalopewa kama muhusika atakuwa amefukuzwa katika chama, basi jina litakalofuata baada ya huyo mwanachama ndilo litakaloandikwa na kufanyiwa kazi.

Alisema si rahisi kwa NEC kumtangaza mrithi wa nafasi hiyo bila kuwasiliana kwanza na chama na kuthibitisha kuwa bado ana sifa za kushika nafasi hiyo.

Alisema NEC inajua wazi kuwa haiwezi kumtangaza mtu moja kwa moja pasipo baraka za chama kwa sababu siku hizi kumekuwa na wimbi la migogoro ndani ya vyama vya siasa nchini na wengine kujivua uanachama au kufukuzwa.

Wakati Dk Slaa akisema jukumu hilo ni la NEC, Naibu Katibu wake,  Zitto Kabwe alitaja jina la mmoja wa madiwani wa viti maalumu wa chama hicho kuwa ndiye anayefuata katika orodha iliyopelekwa NEC.

Akizungumza jana, Zito alisema kwa mujibu wa orodha yao ya viti maalumu anayefuata baada ya wabunge walioteuliwa mwaka juzi ni diwani huyo ambaye jina lake tunalihifadhi kwa sasa.

“Kwa mujibu wa orodha tuliyonayo ya wabunge wa viti maalumu anayefuata baada ya Regia ni diwani kutoka (anataja wilaya na jina lake), ndiye atakayechukua nafasi ya kiti hicho kilichoachwa na marehemu,” alisema Zitto.

Mabadiliko makubwa yaja uchaguzi CCM


WABUNGE WAPIGWA ‘STOP’,TAKUKURU WATANGAZA VITA
Waandishi Wetu
MABADILIKO makubwa yanatarajiwa katika uchaguzi wa ngazi zote ndani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambao mchakato wake umepangwa kuanza mwezi ujao.Miongoni mwa mabadiliko hayo ni pamoja na wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuzuiwa kugombea nafasi yoyote ndani ya chama, ikiwa ni hatua ya kufanya mageuzi yenye lengo la kuondoa tatizo la baadhi ya watu kujilimbikizia madaraka.

“Ikiwa mbunge au mjumbe wa Baraza la Wawakilishi anataka kugombea uongozi wa chama, basi lazima apate kibali cha Kamati Kuu ya CCM na si vinginevyo,” kilisema chanzo chetu kutoka ndani ya chama hicho.

Habari ambazo Mwananchi lilizipata na kuthibitishwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), Nape Nnauye zinasema uchaguzi ndani ya chama hicho tawala unatarajiwa kufanyika kwa kuzingatia marekebisho yanayofanywa katika katiba yake.

Nape alikiri jana kwamba kuna mchakato wa marekebisho ya katiba ya CCM. Hata hivyo, hakuwa tayari kuzungumzia kwa undani marekebisho hayo.

Jumatano wiki hii, CCM kilitangaza ratiba ya uchaguzi huo wa ndani ya chama pamoja na jumuiya zake, ambao uchukuaji  fomu utaanza Februari 4, mwaka huu kwa ngazi ya shina, tawi na kata.
 Ratiba iliyotolewa na Ofisi Ndogo ya CCM Lumumba, Dar es Salaam inaonyesha kwamba katika uchaguzi wa ngazi ya wilaya, mkoa na taifa, fomu zitaanza kutolewa Juni 2, mwaka huu.  Uchaguzi huo unapewa umuhimu mkubwa na wachunguzi wa masuala kisiasa ambao wanauchukulia kama sehemu ya maandalizi ya chama hicho kutwaa tena dola katika Uchaguzi Mkuu wa 2015.

“Mchakato wote uchaguzi huo kwa ngazi zote, unatarajiwa kukamilika Novemba 11,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo iliyotangazwa wiki hii na Radio Uhuru inayomilikiwa na CCM.

Mabadiliko ya Katiba
Katika mabadiliko ya katiba yanayofanywa na chama hicho, imeelezwa kwamba hatua ya kuwaengua wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi katika kinyang’anyiro cha nafasi za uongozi wa chama ni kuondoa tatizo la baadhi ya watu kujilimbikizia madaraka.
Kazi hiyo inafanywa na Kamati ya Marekebisho ya Katiba ya CCM chini ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Tanzania Bara, Pius Msekwa na inatarajiwa kuwasilisha matokeo ya kazi yake katika vikao vya juu vya CCM vinavyotarajiwa kukutana Dodoma mwezi ujao.

Nape alikiri kwamba kuna mabadiliko yanayotarajiwa na kutaja moja tu kwamba ni lile la kufutwa kwa nafasi za wajumbe wa NEC wa mikoa na badala yake nafasi hizo kurejeshwa katika ngazi za wilaya.

Katibu huyo wa Itikadi na Uenezi alisema pia wajumbe wa NEC kutoka katika jumuiya za chama wanapendekezwa kuchaguliwa na jumuiya husika badala kupigiwa kura na Mkutano Mkuu wa CCM kama ilivyo sasa.

Alipoulizwa kuhusu kupitishwa kwa mabadiliko hayo na vikao husika Nape alisema: “Najua  unachotaka kufahamu ni iwapo kuna mgogoro wa kikatiba, haupo kwani katiba yetu ina vipengele ambavyo vinaruhusu NEC kutekeleza jukumu hilo.”

“Kwa hiyo mapendekezo yatapelekwa kwenye kikao kijacho cha NEC na yakishapitishwa, basi yataanza kutumika isipokuwa tu kwa mujibu wa katiba lazima Mkutano Mkuu wetu uarifiwe kuhusu hatua hiyo.”

Juzi, Nape alinukuliwa akiwataka watu wanaoona kwamba anakivuruga na kukigawa chama hicho kutokana na kauli zake za kutilia mkazo miongozo na kanuni, watoke CCM na kuanzisha chama chao.  Alitoa kauli hiyo alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Televisheni ya Taifa ya TBC1 juu ya maadhimisho ya miaka 35 ya CCM, uchaguzi ndani ya chama na matembezi ya mshikamano, mwaka huu. 
“...Mimi navuruga ulaji wa wachache, si kuvuruga chama, naamini nipo sahihi kwa sababu natetea wengi. Kama ninakigawa chama kwa kuvuruga ulaji wa wachache, basi nitaendelea kukigawa, wachafu waanzishe chama chao cha wachafu na wasafi wabaki upande wao (CCM).”  Alisema sasa ni wakati wa kukirejesha chama hicho katika misingi yake na siyo wachache kukitumia kujinufaisha. 
Ratiba ya uchaguzi
Ratiba inaonyesha kuwa uchaguzi huo umegawanyika katika sehemu kuu mbili; uchaguzi wa viongozi wa chama na ule wa Jumuiya zake.  Kwa mujibu wa ratiba hiyo, wanachama watakaowania uongozi kwenye jumuiya katika ngazi ya shina, wataanza kuchukua fomu kuanzia Februari 4 na uchaguzi utafanyika Februari 29, mwaka huu.
Kwa upande wa uongozi wa chama ngazi hiyo ya shina, uchukuaji fomu, utaanza Machi 23 na uchaguzi utafanyika Aprili 30.

Katika ngazi ya tawi, fomu kwa wagombea wa jumuiya zitaanza kutolewa Machi 3 na uchaguzi wake utafanyika Aprili 22, wakati fomu za kuwania uongozi wa chama zitaanza kutolewa Februari 20 na uchaguzi utafanyika Machi 31.

Katika ngazi ya kata, wagombea wa jumuiya wataanza kuchukua fomu Mei 4 na uchaguzi wake ni Juni 30, wakati kwa wagombea wa chama fomu zitaanza kutolewa Mei 13 na uchaguzi utafanyika Julai 4.  Ngazi nyingine
Visiwani Zanzibar, fomu kwa ajili ya uchaguzi wa majimbo zitaanza kutolewa Juni 2 na uchaguzi wake kufanyika Julai 26 kwenye jumuiya na Agosti 2 kwa wagombea wa uongozi wa chama.
Kwa upande wa wilaya, ratiba hiyo inaonyesha kwamba fomu za uchaguzi wa viongozi wa wilaya wa jumuiya Tanzania Bara, zitaanza kutolewa Juni 2 na uchaguzi wake kumalizika Agosti 22, huku fomu kwa ajili ya viongozi wa chama, zikipangwa kuanza kutolewa Juni  2 na uchaguzi kufanyika Septemba 26. 
Taarifa hiyo ilifafanua kwamba  katika ngazi ya mkoa, uchaguzi wa jumuiya utaanza Juni 2 na uchaguzi utafanyika Septemba 26 na fomu za uchaguzi wa viongozi wa chama, zitaanza kutolewa Juni 2 na uchaguzi wake kufanyika Oktoba Mosi mwaka huu.
Ngazi ya taifa, fomu zitaanza kutolewa Juni 2 kwa wagombea wa jumuiya na uchaguzi wake utafanyika Oktoba 5 na fomu kwa ajili ya wagombea wa ngazi ya chama, zitaanza kutolewa Oktoba 25  na uchaguzi utafanyika Novemba 11.  Mkutano Mkuu wa taifa unatarajiwa kufanyika Oktoba 9 ili kukamilisha Uchaguzi Mkuu na kuunda Sekretarieti ya Taifa.
 Takukuru waonya  Wakati hayo yakiendelea, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imetangaza vita kwa  wote watakaotoa na kupokea rushwa ili kushinda katika nafasi mbalimbali za uchaguzi huo ndani ya CCM.

Kaimu Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, ambako uchaguzi ngazi ya taifa unatarajiwa kufanyika, Sostenes Kibwengo amesema kuwa taasisi hiyo imejipanga kukabiliana na vitendo vya rushwa vitakavyojitokeza.
“Hatutamwonea haya mtu yeyote hata kama ni mkubwa kiasi gani, maana uchaguzi huo huwa unajaa vibweka ukizingatia mwaka huu wanapanga safu zao kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu wa 2015,’’alisema Kibwengo na kuongeza:   “Tusipokuwa makini na jambo hilo, CCM kitaingiza viongozi wabovu na wazembe ambao mwisho wa siku, wataifanya Serikali yote kuwa ni ya wala rushwa.’’
Kauli hiyo imeungwa mkono na Takukuru Taifa. Msemaji wa Takukuru, Doreen Kapwan alisema kimsingi suala hilo limo ndani ya taasisi hiyo mkoani Dodoma hasa kwa kuzingatia kuwa mkutano huo unafanyika kwenye eneo lake.

Woman refuses to leave toilet bowl for 2.5 years

She sat down on the toilet bowl in her master bedroom bathroom on March 25, 2009.
For the next 902 days, the small, white-tiled room became Madam Leong Mee Yan's home.
She ate her meals there and slept there. And no amount of cajoling from her husband would make her leave the toilet bowl.
Madam Leong, now 58, claimed that she felt a strong force holding her down every time she tried to get up.
She also imagined stones being hurled and water sprayed at her by people she could not see, preventing her from leaving the bathroom.
Said Madam Leong, who was naked throughout the 902 days, in Mandarin: "I didn't understand what was happening, I only felt all the sensations which prevented me from standing or leaving the bathroom."
During her two-and-a-half year stay in the bathroom, Madam Leong showered a total of 18 times, said her husband, Mr Ong Kian Ann.
Those were the only occasions that she would move from the toilet bowl.
Mr Ong, 64, said: "I had to take a stool into the bathroom for her. Then I would slowly help her shift from the toilet bowl to the stool, and she would bathe herself with the shower head."
Aside from her husband, Madam Leong, a Malaysian who's a permanent resident here, did not see anyone during those years, including her only child, Mr Ong Jiing Yih, 27.

Underwater dragon dance to welcome the Water Dragon


The 37-year-old is part of a team that will perform Singapore's first underwater dragon dance on the first two days of Chinese New Year to welcome in the Year of the Water Dragon.

Made especially for the occasion in neon pink, complete with bushy eyebrows, the three-metre dragon twists and turns to traditional drum beats.

Friday, January 20, 2012

Kisa na Mkasa na Salim Kikeke

Mwizi na Mlegezo

Saggy
Mtindo wa Kata K
Mwizi mmoja hapa London aliyekuwa akijaribu kukimbia baada ya kufanya wizi wake, aliuhisi mkono wa sheria ukimkamata baada ya kuanguka, kwa kuwa alikuwa amevaa suruali yake katika mtindo uitwao mlegezo, au kata K.
Gazeti la Metro limesema John O'Dell alisimamishwa na polisi katika eneo la harringey, kaskazini mwa London siku ya Jumapili, lakini badala yake akaamua kukimbia.
Hata hivyo, kwa kuwa alikuwa amevaa suruali yake bila mkanda na katika mtindo wa mlegezo, suruali hiyo iliteremka na kumfanya adondoke na kukamatwa na polisi mara moja. Tukio hilo lilishuhudiwa na wapita njia. Mpita njia Harry Robbins aliyeshuhudia sakata hilo amesema, kwa kuwa hakuwa amevaa mkanda, ilikuwa ni kichekesho jinsi suruali yake mwenyewe ilivyomuangusha na kusababisha kukamatwa. Wote tuliokuwepo tulibaki tukicheka, amesema Robbins. Mwizi huyo baada ya kukamatwa alikiri kuiba laptop ya karibu dola mia tano -- atafikishwa mahakamani Januari 31.

Mimba ya Mochuari

Mochuari
Mfanyakazi wa mochuari

Mwanamama mmoja nchini Marekani anayefanya kazi mochuari ameingia matatani baada ya kupata uja uzito kwa kujamiiana na mtu aliyekufa. Mtandao wa habari wa dead serious news umesema tukio hilo linadhaniwa kutokea katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Mourning Glory, nje ya Lexington, Missouri.
Polisi wa mjini humo wamemshtaki mama huyo aitwaye Felicity Marmaduke kwa kosa la kunajisi na kuchezea maiti. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na polisi, kiungo cha kiume cha mwili wa mtu aliyekufa kilihamasika wakati mwili ukioshwa. Taarifa zinasema, kwa kuwa mwanamama huyo alikuwa peke yake, aliamua kujamiiana na mwili huo.
Kwa mshangao hata wa mwanamama huyo, maiti huyo alitoa mbegu za kiume. Wiki chache baadaye Bi Marmaduke alijikuta ni mja mzito. Baada ya kumwambia daktari wake mfululizo wa matukio, daktari huyo aliwataarifu polisi.
Bi Marmaduke alikamatwa na polisi akiwa nyumabni kwake, si mbali sana na mochuari anayofanyia kazi. Katika tukio la kushangaza zaidi, mwanamama huyo amesema anapanga kudai urithi kutoka kwa familia ya mtu huyo aliyekufa.

Wasiolia kupewa adhabu?

Kim
Mazishi ya Kim Jong-il
Mamlaka za Korea kaskazini zinadaiwa kuwaadhibu wananchi wake kwa kuwapeleka jela na kazi ngumu-- wale wote ambao hawakulia vya kutosha katika msiba wa kiongozi wao Kim Jong-il.
Gazeti la kila siku lenye makao yake makuu Korea Kusini NK limesema yeyote ambaye hakushiriki misa ya kihistoria ya kumuenzi Kim au ambaye alihudhuria lakini hakulia kiasi cha kutosha au kuonekana kulia kwa uongo, atapelekwa katika kambi maalum na kufanyishwa kazi ngumu kwa miezi sita, limeripoti gazeti hilo.
Gazeti hilo limedai huku likikariri chanzo ambacho haikukitaja kuwa yeyote aliyejaribu kutoka nje ya nchi wakati huo atashtakiwa katika mahakama mbele ya kadamnasi. Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa kwenye mtandao wa cnews.com, wengine watapelekwa katika kambi na kupewa elimu upya ya utaifa.
Hakuna taarifa rasmi kutoka Korea kaskazini iliyothibitisha taarifa hizi. Hata hivyo shirika la habari la Korea Kaskazini limeripoti wiki iliyopita kuwa kifo cha Kim Jong-il kiliombolezwa hadi na wanyama wa porini.
"Dubu mmoja akiwa na wanae walionekana wakiwa wanalia kwa nguvu" imesema taarifa ya shirika hilo. Madubu hao sio wanyama pekee ambao wameripotiwa kumuomboleza kiongozi huyo.
Shirika hilo liliripoti mwezi uliopita kuwa mamia ya kunguru aina ya Magpies walionekana wakipeperuka kuzunguka sanamu la Rais Kim katika wilaya ya Magyondae.

Polisi mwizi

Police
Polisi wa Moscow

Polisi katika mji wa St Petersburg wamesema wamemkamata afisa wa polisi akiwa anaendesha gari la wizi.
Gazeti la RIA Novosti limeripoti siku ya Alhamis kuwa polisi huyo kapteni Andrei Makononeko alikutwa akiendesha gari ya wizi aina ya Lexus na huenda akafunguliwa mashtaka. Kamati ya uchunguzi ya Urusi imesema polisi huyo alikamatwa Januari 10. Gari hilo liliibiwa mwezi Novemba, wamesema polisi. Uchunguzi unafanyika kutazama iwapo mashtaka yafunguliwe dhidi ya afisa huyo.

Usipige 999 hovyo

Police
Polisi wa Uingereza
Polisi wa Uingereza wamewataka wananchi wake kutotumia hovyo namba ya dharura, baada ya mtu mmoja kupiga simu na kuripoti ugomvi uliokuwa ukitokea kwenye TV.
Mtandao wa MSN umesema bwana mmoja alipiga simu polisi baada ya ugomvi kuzuka katika tamthilia aliyokuwa akitazama kwenye TV.
Taarifa zinasema bwana huyo alikuwa akitazama tamthilia maarufu Uingereza iitwayo EastEanders, na kipande hicho chenye mzozano kilirekodiwa mwaka 2009. Taarifa za polisi zimetolewa ili kuwafahamisha wananchi umuhimu wa kutumia simuza dharura, na kuainisha zipi ni dharura na zipi sio dharura.

Na kwa Taarifa yako....

Huwezi kujiua kwa kushikilia pumzi yako mwenyewe.

Tukutane wiki ijayo...... Panapo Majaaliwa...
Taarifa kutoka mitandao mbalimbali ya habari duniani

'Posters are insulting, demeaning'

Party posters misusing CHIJ school crest anger past and current students.
'Posters are insulting, demeaning'
[Above: CHIJ alumnus K. Tan said the misuse of the school's badge in the poster, as seen in the Internet picture, was in poor taste.]
The poster was probably created to grab attention, and grab attention it did - but of the wrong sort.

It aroused anger among current and former CHIJ students.
Seen in Filter Members Club last Saturday during a theme party, the poster showed the CHIJ school crest with a slogan around it that read: "In need of a one night stand: CHIJ girls please stand up!"
The New Paper saw the poster in a photograph posted online yesterday. In the picture, a few girls were seen posing with the poster, smiling.
The picture was sent to the CHIJ School Board of Management of the 11 IJ schools here.
Said board chairman Vivienne Lim: "The use of the CHIJ school badge in the context of the picture is highly inappropriate and demeaning."
She added that it was also "insulting" to the "thousands of CHIJ alumni and current CHIJ students, some of whom are as young as six years old".
The Filter Members Club is on Nanson Road, next to Gallery Hotel.
On the club's Facebook page, the get-up for the party was stated as "scandalous school girls" and "East Coast preppy school boys".

Famous people born in Year of Dragon

The Dragon is the most coveted sign of the Chinese zodiac, but what makes a Dragon? Here's a look at famous dragon people and key characteristics of the mythical creature.

Click on thumbnail to view (Photos: 20th Century Fox, AFP, Apple Daily, Columbia Pictures, Paramount Pictures, Reuters, SingTel, Scorpio East, ST, Star Chinese Movies, Stomp, TNP)

Driver, 21, wrecks car after crashing into Lornie Rd divider

An accident involving two cars along Lornie Road to Upper Thomson this morning caused a traffic gridlock in both directions, The Straits Times reported today.
A grey Toyota Corolla Altis ended up mounting the road divider along Lornie Road.
Its bonnet was completely wrecked and the front right tyre was torn off due to the impact.
Gridlock on both sides of Lornie Rd

One motorist was injured in the accident, the report said. According to a police spokesman, the injured motorist was about 21 years old. The driver was taken to Tan Tock Seng Hospital.
No one was seriously injured.