Monday, November 28, 2011

Msichana ajinyonga akibisha kupika chakula

MWANAFUNZI wa darasa la nne katika Shule ya Msingi Mbezi Juu, Kinondoni mkoani Dar es Salaam, amejinyonga kwa kutumia kitenge baada ya kubishana na kaka yake kuhusu nani apike chakula cha mchana.

Mwanafunzi huyo wa kike mwenye amri wa miaka 11 (jina limehifadhiwa), alikutwa amejinyonga chumbani kwake juzi akiwa amejitundika kwa kutumia kitenge kilichofungwa katika nondo ya dirisha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema jana kuwa msichana huyo kabla ya kuchukua uamuzi huo, alibishana na kaka yake mwenye umri wa miaka 12 (jina limehifadhiwa) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tano katika shule hiyo.

Alisema inavyoonekana, msichana huyo alichukua uamuzi huo baada ya kugombana kuhusu nani apike chakula cha mchana kwa kuwa baada ya ugomvi, aliingia ndani ya chumba chake
na ndipo baadaye mwili wake ukakutwa ukining’inia.

Katika tukio lingine, mfanyabiashara Ahmed Mguni (27), mkazi wa Mbagala Charambe amekutwa juzi amekufa na mwili wake umelala kitandani bila jeraha lolote.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, David Misime alisema sababu ya kifo chake haijafahamika na kwamba Polisi wanaendelea na uchunguzi huku mwili wake ukiwa umehifadhiwa katika Hospitali ya Temeke.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile alisema Polisi inamtafuta dereva
na gari lililomgonga fundi ujenzi aliyetambuliwa kwa jina moja la James (35) na kufa papo hapo.

Shilogile alisema fundi huyo aliyekuwa akitembea kwa miguu aligongwa na gari juzi asubuhi
katika eneo la Mvuti kwenye barabara ya kwenda Msongola.

Egypt gas pipeline blown up hours before key election

 
Egyptian protesters gathering for a demonstration calling for the interim military rulers to step down in Tahrir Square in Cairo on November 27, 2011.
CAIRO, Egypt - Saboteurs on Monday blew up a pipeline that supplies gas to Israel, the official MENA news agency reported, just hours before the first election since Hosni Mubarak was ousted.
Masked gunmen planted explosives under the pipeline west of the town of El-Arish in the north of the Sinai peninsula, MENA said.
A second blast occured seconds later around 100 metres away from the first explosion, a security official told AFP.
Witnesses said they saw the masked men driving away from the area just minutes before the blasts, which sent raging flames into the sky, visible from miles away.
Emergency services were rushed to the scene to try to control the blaze, the official said, adding that there were no immediate reports of casualties.
The attack- the ninth of its kind this year- came just hours before polling was due to start in landmark parliamentary elections.
The pipeline, which carries gas through the Sinai and on to Jordan and Israel, has already been attacked eight times this year, the first during the mass uprisings that drove president Hosni Mubarak from power in February. The last attack was carried out on Friday.
Gas deliveries to Israel, agreed under Mubarak, have come under heavy criticism in Egypt.
Israel generates 40 per cent of its electricity using natural gas, and Egypt provides 43 per cent of its gas supplies.
Egyptian authorities have on several occasions announced measures to step up protection of the pipeline and try to arrest those behind the attacks.
Egyptian gas also covers 80 per cent of Jordan's electricity production demand - 6.8 million cubic metres a day.
Egypt's Sinai region is particularly security sensitive due to tensions with the Bedouin community living there.
Many goods are smuggled to the Palestinian enclave of Gaza through the Sinai, which the Israelis also charge is a rear base for militant attacks against its territory.

Uchaguzi mkuu wafanyika nchini DRC

Shughuli ya upigaji kura katika uchaguzi mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, inatarajiwa kuanza asubuhi leo.
Uchaguzi huo wa rais na wabunge ni wa pili kufanyika nchini humo baada ya kumalizika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka minane iliyopita.
Kulikuwa na wasiwasi kuwa upigaji kura ungechelewa kwa sababu ya matatizo ya miundombinu na ghasia kati ya wafuasi wa wagombea wenye upinzani.
Lakini jana Tume ya Uchaguzi imesema 99% ya vituo vya kupigia kura vilikuwa tayari kwa shughuli hiyo kuanza na kufanikiwa kwake ni ushindi wa demokrasia.

vifaa vya kura

Malori yamekuwa yakisambaza karatasi za kupigia kura katika mji mkuu Kinshasa, wakati ambapo majeshi ya Umoja wa Mataifa na helikopta za jeshi hilo zilisaidia kusambaza vifaa vya uchaguzi katika maeneo ya pembezoni mwa nchi hiyo.
Rais Joseph Kabila wa Congo
Rais Joseph Kabila wa Congo
Rais anayetetea kiti hicho, Joseph Kabila anakabiliwa na wapinzani wengine kumi katika kinyang'anyiro cha kuingia Ikulu, huku mpinzani wake mkuu akiwa mwanasiasa mkongwe Etienne Thisekedi.
Zaidi ya wagombea 18,000 nao wanawania viti 500 vya ubunge.

Lowassa: Nitashinda vita hii

 Habel Chidawali, Singida

WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu na Mbunge wa Monduli (CCM), Edward Lowassa jana alitoa kile kilichokuwa kikimsibu moyoni mwake kwa muda mrefu na kusema kuwa atashinda vita dhidi yake.

Akitumia vifungu vingi vya Biblia, Lowassa ambaye amekuwa katika misukosuko mingi ya kisiasa tangu alipojiuzulu Februari 2008, alisema kuwa sasa yamekwisha baada ya kuvumilia kwa muda mrefu sana huku akisemwa maneno ya ovyo.

Alitoa kauli hiyo jana wakati wa kuchangia ujenzi wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri (KKKT), Usharika wa Amani mjini hapa.

“Wamesema maneno mengi ya ovyo sana juu yangu lakini nilivumilia siasa hizo kwa kiasi kikubwa sana hadi leo nimesimama katika imani na bila shaka nitashinda,’’ alisema Lowassa na kushangiliwa na umati wa waumini waliohudhuria.

Kauli ya Lowassa imekuja siku tatu baada ya kutoa ya moyoni kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) kuhusu kile alichosema kuwa ni baadhi ya viongozi wa chama kutumia fedha nyingi kuzunguka nchini na kumtukana ovyo.

“Mwenyekiti kwanza napongeza uamuzi huu wa kurejesha jambo hili katika taratibu za kawaida, lakini napenda kufahamu kwa miezi saba nimetukanwa nikiitwa fisadi, watu wamezunguka nchi nzima kwa fedha za chama wakinitukana, hivi hatukujua kwamba kuna kamati hizo za maadili,” Lowassa alinukuliwa akihoji baada ya NEC kuridhia ombi la Kamati Kuu ya chama hicho (CC) kwamba suala la mageuzi ndani ya CCM maarufu kama kujivua gamba lirejeshwe katika kamati hiyo ili lifanyiwe kazi kwa taratibu za kawaida za kinidhamu baada ya wahusika kukataa kuachia nafasi zao.
Katika kikao hicho, Lowassa alinukuliwa akiwataja Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, John Chiligati kwamba wamekuwa wakitukana watu ovyo kwa fedha wanazopewa na CCM.
Jana akihutubia katika hafla ya kuchangia usharika huo, Lowassa alisema: “Siku moja nilikuwa nyumbani na mke wangu tukiangalia televisheni... katika kipindi cha uchambuzi wa magazeti tukakutana na habari ambayo hata wachambuzi wa magazeti wenyewe walishindwa kuisoma kutokana na mambo mabaya ambayo yaliandikwa juu yangu.’’
Alisema mke wake alichukua Biblia na kusoma katika kitabu cha Isaya sura ya 41 mstari wa 10 na kisha akamtia moyo na kumfanya avumilie kwa kipindi chote cha misukosuko hiyo huku akimuomba Mungu.

Maneno katika kitabu hicho yanasomeka: “Usiogope kwa maana mimi ni pamoja nawe, usifadhaike kwa maana mimi ni Mungu wako nitakutia nguvu, nitakusaidia na kukushika mkono wa kuume wa haki yangu.’’

Lowassa alisema kuwa katika kipindi chote hicho amekuwa akiishi kwa matumaini ya neno hilo lililosomwa na mke wake na hata yalipokuwa yakisemwa maneno mengi juu yake aliamini kuwa yote yatapita kwa kuwa yalilenga kumchafua tu na hayakuwa na ukweli ndani yake.

Alitumia pia maneno ya Biblia katika kitabu cha Warumi 8:31 ambayo yanasema: “Basi tuseme nini juu ya hayo, Mungu akiwapo upande wetu ni nani aliye juu yetu.’’

Tofauti na alivyokuwa akionekana baada ya kujiuzulu, Lowassa jana alikuwa mwenye furaha zaidi akionyesha ujasiri wakati wote wa shughuli hiyo ya uchangiaji ambayo alisimama kwa zaidi ya saa nne akichangisha fedha za ujenzi wa kanisa hilo.

Awali, ilitarajiwa kwamba kiasi cha Sh100 milioni tu ndicho kingechangishwa katika hafla hiyo lakini lengo hilo lilivukwa na kupatikana Sh138 milioni. Lowassa alichangia Sh10 milioni.

Mbunge huyo alisema kuwa kila jambo linalomjia binadamu huwa ni la muda na baada ya hapo ukweli huonekana mbele yake na hivyo akawasihi Watanzania kuwa wavumilivu juu yake na maisha yao kwa ujumla.

“Nawashukuru sana mashehe, viongozi wa dini, wana maombi, wake kwa waume, pamoja na viongozi mbalimbali bila ya kuwasahau marafiki zangu ambao kwa namna moja au nyingine walifunga kwa maombi juu yangu, nasema asanteni sana.’’

Kwa upande wake, Askofu wa Kanisa hilo Dayosisi ya Kati, Eliufoo Sima alisema hata kama mawingu yatapita juu ya jua, haina maana kuwa jua limekwisha.

“Tunakutia moyo kwamba wale waliosema kuwa mapambano katika maisha hayatakwisha na suluhisho si kuyaogopa, bali kuyatafutia jawabu kwa upole, hekima na utulivu,’’ alisema Askofu Sima.

Alisema kuwa wanadamu wamezoea kushangilia maovu siku zote lakini umefika wakati ambao wanatakiwa kushangilia hata kwa mema pia ikiwemo masuala ya utoaji michango kwa ajili ya masikini na walio na mahitaji.

Akitumia maneno kutoka katika Biblia, Askofu Sima alimtaka Lowassa kutokata tamaa katika utumishi wake.

JK apokea kabrasha la Chadema


RAIS Jakaya Kikwete jana alikutana na ujumbe wa Chadema na kukabidhiwa kabrasha la mapendekezo ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini na kisha kujadili mchakato wa utungwaji wa Katiba Mpya.

Rais alikutana na viongozi hao kuanzia saa 9:30 alasiri mpaka saa 12:00 jioni. Mara baada ya ujumbe huo wa Chadema ulioongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe kuwasili Ikulu, ulipokewa na Rais Kikwete na muda mfupi baadaye wote wakatoka nje na kupiga picha za pamoja kabla ya kurejea ndani ambako pia walipiga picha nyingine za makabidhiano ya kabrasha hilo la mapendekezo ya Chadema na hatimaye kuendelea na majadiliano.

Taarifa iliyotolewa jana na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu imesema kwamba kikao cha jana hakikumalizika na kimeahirishwa hadi leo saa nne.

“Pande zote mbili zimekubaliana kukutana tena asubuhi ya kesho (leo), ili kuipa nafasi Serikali iweze kutafakari mapendekezo hayo,” ilisema taarifa hiyo.

Mbowe alithibitisha kwamba kikao hicho kitaendelea leo na taarifa zote zitatolewa baada ya hapo... “Ndugu waandishi wa habari tumekutana na Rais na baadhi ya mawaziri na wasaidizi wake. Kikao kilianza saa 9:30 mchana na kiliahirishwa saa 12:00 jioni. Kikao kitaendelea kesho asubuhi saa nne. Taarifa kamili ni baada ya kikao.”

Hata hivyo, taarifa ya Ikulu imesema pande hizo mbili zimekubaliana kuwa Katiba ya sasa ni nzuri iliyolilea Taifa kwa miaka 50 iliyopita na ndiyo iliyoliwezesha Taifa la Tanzania kuwa na amani, utulivu.

Mbali ya kukubaliana katika hilo, Ikulu imesema Kikwete na ujumbe huo wa Chadema wamekubaliana juu ya umuhimu wa kutunga Katiba Mpya kama Rais Kikwete alivyoliahidi taifa wakati wa salamu zake za mwaka mpya Desemba 31, mwaka jana.

“Katika mazungumzo hayo, Mheshimiwa Rais aliwahakikishia wajumbe hao wa Chadema kuwa ni dhamira yake na ya Serikali yake kuhakikisha kuwa Tanzania inapata Katiba Mpya,” ilisema taarifa hiyo ya Ikulu na kuongeza:

“Katika mkutano huo, pande zote mbili zimekubaliana kuwa ni jambo muhimu kwa mchakato mzima wa kutungwa kwa Katiba Mpya kuendeshwa kwa namna ya kulinda na kudumisha tunu za taifa za amani, utulivu na umoja wa kitaifa.
Aidha, pande zote mbili zimekubaliana kuwa mchakato huo uendeshwe kwa kuzingatia misingi ya mambo mengine muhimu kwa taifa la Tanzania kama vile kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani, kuligawa Taifa kwa misingi ya udini na ukabila ama kutugawa kwa misingi ya maeneo.”

Mbowe aliongozana na wajumbe wa kamati maalumu iliyoteuliwa na Chadema kwa ajili ya kuonana na Rais Kikwete ambayo wajumbe wake ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema (Bara) Said Arfi, Makamu Mwenyekiti (Zanzibar) Said Issa Mohamed, Mshauri wa Masuala ya Siasa wa chama hicho, Profesa Mwesiga Baregu, Profesa Abdallah Safari na Mnadhimu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lisu, ambaye alikuwa Katibu wa Kamati hiyo. Pia alikuwapo John Mrema lakini Katibu Mkuu, Dk Willibrod Slaa ambaye ni mjumbe hakuwepo.

Kwa upande wa Serikali, mbali ya Rais Kikwete alikuwapo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Mathias Chikawe, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi.

Wengine ni Waziri wa Katiba na Sheria, Celina Kombani na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

Mkutano huo umefanyika baada ya Rais Kikwete kuafiki ombi la Chadema la kutaka kuonana naye kwa lengo la kumweleza kasoro zilizopo kwenye Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba ambao tayari umeshapitishwa na Bunge ukisubiri kusainiwa na Rais ili kuwa sheria.

Posho za wabunge zapanda kimyakimya


ZAPANDA KUTOKA SH70,000 HADI 200,000, NI ZAIDI YA ASILIMIA 150
Fredy Azzah
HUKU mjadala wa kufutwa au kwa posho za wabunge na watumishi wengine wa Serikali ukiwa umefifia, posho za vikao (sitting allowance) za wabunge zimepanda kutoka Sh70,000 kwa siku hadi Sh200,000, imefahamika.
“Zimeongezeka kutoka Sh70,000 mpaka 200,000, wameanza kulipwa Bunge lililopita hili ni ongezeko la karibu mara tatu, yaani asilimia 154,” kilieleza chanzo chetu kutoka ndani ya Ofisi za Bunge.

Kutoka na ongezeko hilo, kwa sasa kila mbunge atakuwa akilipwa Sh80,000 ikiwa ni posho ya kujikimu (perdiem) anapokuwa nje jimbo lake, posho ya vikao (sitting allowance) Sh200,000 na mafuta ya gari Sh50,000 kila siku, ambazo jumla yake ni Sh330,000 kwa siku.

Kutokana na ongezeko hilo, Bajeti ya Bunge kwa ajili ya posho za vikao vya wabunge imepanda na kufikia Sh28 bilioni kwa mwaka.

Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah alipoulizwa kuhusu taarifa hizo alisema hawezi kuzungumzia jambo hilo kwa sababu siyo msemaji wa wabunge, bali Ofisi ya Bunge.

“Ni nani kawapa hizo taarifa bwana, au ni vyanzo vyenu vya habari?” alihoji Dk Kashililah.

Baada ya kuelezwa kuwa taarifa hizo zimetoka kwenye vyanzo vyetu vya kuaminika alisema “Hao wana utaratibu wao bwana, labda mtafute Spika ndiye msemaji wa Wabunge.”

Juhudi za kumpata Spika, Anne Makinda kutoa ufafanuzi wa suala hili, hazikufanikiwa baada ya simu yake kuita wakati wote bila kupokewa hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi wa simu (sms) hakujibu. Hata simu zote za Naibu wake, Job Ndugai hazikupatikana.

Hata hivyo, Mbunge wa Ludewa (CCM), Deo Filikunjombe alisema kuongezeka kwa posho hizo kunatokana na wabunge kuwa wanalipwa mishahara midogo kulingana na kazi wanayofanya.

Alisema endapo wawakilishi hao wa wananchi wangekuwa wanalipwa mishahara inayolingana na kazi wanayofanya, kusingekuwa na sababu ya kuongezeka kwa posho hizo.

“Ninachosema mimi, siyo wabunge peke yao, lakini watumishi wote wa umma wanalipwa mishahara midogo sana mimi binafsi sitegemei posho za Bunge, kabla ya kuingia bungeni nilikuwa nimefanya kazi kwa miaka 14 na nilikuwa napata mshahara mzuri tu,” alisema Filikunjombe.

Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa alisema amezisikia taarifa hizo za kuongezeka kwa posho lakini siyo kwa undani. Hata hivyo alisema hakuwa katika nafasi nzuri ya kuzungumza suala hilo.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema walivyokuwa wakipinga posho hizo wakati zilivyokuwa Sh70,000 waandishi wa habari walichukua suala hilo kama ajenda ya Chadema, hivyo kupandishwa kwa posho hizo ni matokeo ya watu kuwapuuza walivyokuwa wakizipinga.

“Msimamo wetu sisi tulishautoa tangu wakati posho zikiwa Sh70,000 wakati sisi tukipinga hizi posho waandishi wa habari na Watanzania mlichukulia suala hili kama ajenda ya Chadema, sisi wenyewe tupo wachache bungeni, tulichotaka ni kuonyesha jinsi fedha za Watanzania zinavyotumika vibaya,” alisema na kuongeza:

“Achilia mbali hizo 200,000 za wabunge kuna watu huko serikalini wanalipwa mpaka Sh400,000 au Sh1 milioni kwa siku nyie ulizeni.”

Alipoulizwa kama amechukua posho hiyo ya Sh200,000 alisema hajafanya hivyo kwa sababu hazifuatilii.

“Sijui hata kama zimeanza kulipwa au la kwa sababu huwa sizifuatilii na haka kama suala la posho hilo zilijadiliwa wakati wa vikao vya mwanzo mimi sikuwepo kwa sababu tulikuwa kwenye kesi yetu Arusha na bungeni tulikuja mwishoni wakati wa Muswada wa Katiba,” alisema Mbowe.

Ongezeko hili la posho za wabunge limekuja wakati Watanzania wakiendelea kuishi kwenye maisha magumu yanayochangiwa na mfumuko wa bei ambao mpaka mwisho mwa Oktoba ulikuwa umefikia asilimia 17.9.

Pia ongezeko hili limekuja wakati Watanzania wakiwa na matumaini ya posho hizi kupunguzwa baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutangaza bungeni kuwa Serikali imekubali pendekezo la kutafakari na kuziangalia upya posho mbalimbali wanazolipwa wabunge na watumishi wote umma.

Mbunge wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali alisema kuwa hawezi kuzungumza chochote juu ya posho hizo kwa kuwa hajapata barua rasmi juu ya kupanda kwake.

“Sijapata barua yoyote, nikiuliza na kupata majibu kwa wahusika nitakuwa na uhakika na nitakupa maoni yangu na msimamo wangu vizuri kabisa, lakini kwa sasa siwezi kusema chochote,” alisema Mkosamali.

Juni 7, mwaka huu Naibu Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Zitto Kabwe, aliwasilisha barua Ofisi ya Bunge akikataa posho akisema watumishi wa Serikali na wabunge, hawastahili kulipwa posho wanapohudhuria vikao rasmi vya uwajibikaji wao wa kawaida.

Zitto alisema posho hiyo haistahili kulipwa kwake, wabunge wengine wala watumishi wa umma kwa kuwa kuhudhuria vikao ni sehemu ya kazi zao.

Alisema kitendo cha Waziri Mkuu kueleza kuwa watatafakari na kuangalia upya na kwamba suala la posho ni sera ya taifa na Ilani ya Uchaguzi ya CCM, ni ishara ya kiongozi huyo wa juu kukubali wazo la Chadema na safari ya kufuta posho hizo.

Awali, mara baada ya Chadema kutangaza msimamo huo, Spika Makinda alipinga uamuzi wa kususia posho akisema suala hilo lipo kisheria na kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kuamua kuliondoa.

Alisema wabunge wa Chadema wataendelea kulipwa posho za vikao kupitia akaunti zao za benki na watatakiwa kusaini fomu ya mahudhurio ya Bunge, vinginevyo watajiweka katika wakati mbaya.

Hata hivyo, akihitimisha hoja za wabunge katika hotuba yake ya makadirio ya matumizi ya ofisi yake na zilizo chini yake juzi, Pinda alisema suala la posho lipo kwenye mchakato wa kuangaliwa upya.

Saturday, November 26, 2011

Michelle Chong: Famous but unhappy


by Kwok Kar Peng


You can say Michelle Chong has found fame, 13 years after she took her first step into showbiz as a finalist in the 1998 talent search Fame Awards, organised by the then-Television Corporation of Singapore (TCS).
Now, after an uphill climb involving countless rejections by those in the industry, the local star has reached the peak of her career.
The versatile comedienne-actress-host, known for her hilarious impersonations and alter egos Barbarella and Leticia Bongnino on the Channel 5 skit show The Noose, is in high demand and appears on Mandarin TV channels too.
She can command a five-figure sum for a night's work performing at private events, owns a condominium apartment on Thomson Road and drives a Porsche Cayman.
And on Dec 1, she will be making it on to the big screen with Already Famous, a film she wrote, directed and starred in.
But now that she's, well, already famous, the 34-year-old MediaCorp star says she is deeply unhappy.
She didn't shy away from revealing to the media in June that she was seeking professional help for her depression - what her doctor terms a chronic chemical imbalance - and is taking medication for it.
Chong feels the main reason for her unhappiness is the lack of a long-term creative outlet.
.She also thinks her loneliness contributes to her unhappiness.
She has never been romantically linked to anyone or spoken to the media about her love life.
"I do crave for love and companionship. I can't wait to get married and have kids. I'm not dating anyone now and I am lonely," said Chong, who then broke into the classic Bobby Vinton song Mr Lonely.

Michelle Chong has found fame, 13 years after she took her first step into showbiz as a finalist in the 1998 talent search Fame Awards, organised by the then-Television Corporation of Singapore. (Photo: ST)

‘Gamba’ laendelea kuisumbua CCM

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekiri kuwa mwito wa ‘kujivua gamba’ kwa viongozi wake wanaotuhumiwa kwa ufisadi haujaitikiwa kiasi cha kuridhisha na walengwa.

Kutokana na hali hiyo kimeagiza kamati za maadili na usalama katika ngazi zote nchi nzima kuwachukulia hatua haraka watuhumiwa wote.

Aidha, watuhumiwa wa ngazi ya kitafa nao mbali na kutakiwa kushughulikiwa na Kamati ya Maadili na Usalama ya Taifa inayoundwa na viongozi wakuu wa Chama na baadhi ya wajumbe wa Kamati Kuu, pia tuhuma zao zitachunguzwa.

Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, alisema hayo jana wakati akisoma maazimio ya kikao cha siku mbili cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kilichomalizika juzi na kuongeza kuwa watuhumiwa hao watachunguzwa na Kamati Ndogo ya Uchunguzi itakayosimamiwa na Makamu Mweyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa.

Mbali na Msekwa, wajumbe wengine wa Kamati hiyo itakayofanya kazi hiyo na kuwapa nafasi ya kujitetea kabla ya kuwachukulia hatua watuhumiwa hao, ni Mukama mwenyewe na wajumbe wengine wanne; wawili kutoka Zanzibar na wawili Tanzania Bara.

Mukama pia alikiri kuwapo harakati za urais wa mwaka 2015 huku akilaani viongozi wanaoacha majukumu yao ya kiserikali na kujikita katika harakati hizo.

Pia alikiri uwepo wa alichokiita saratani ya kupanga safu za viongozi katika uchaguzi na kuelezea hatua zitakazochukuliwa kukabiliana na hali hiyo.

Mukama alirejea moja ya maazimio ya NEC Aprili mwaka huu; "Kwa kutambua kuwa suala la ufisadi limekuwa mzigo mkubwa sana kwa chama licha ya juhudi kubwa ambazo Serikali imezifanya kupambana nalo, Nec ilielekeza kuwa CCM lazima ipige vita ufisadi kwa nguvu kubwa zaidi na ionekane inafanya hivyo ndani yake
yenyewe.

"Nec iliamua kuwa viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi watafakari, wajipime na kuchukua hatua wenyewe kwa maslahi ya chama. Wasipofanya hivyo, chama kiwawajibishe bila kuchelewa," alimaliza kunukuu azimio hilo la Nec.

Alisema azimio hilo lilikuwa sehemu ya mageuzi ya kukipa chama sura mpya maarufu ‘kujivua gamba’, lakini akafafanua kuwa utekelezaji wake baada ya miezi saba tangu litolewe, haujaridhisha.

"Hali ilivyo sasa, takribani miezi saba baada ya azimio hilo kupitishwa, bado hatujapata mwitikio wa kuridhisha kutoka kwa viongozi wa ngazi zote za chama chetu, ambao ni walengwa wa azimio hilo.

"Bila shaka wakati umefika kwa chama kutekeleza ile sehemu ya pili ya azimio husika kwa kuwawajibisha wahusika ... kwa kufuata utaratibu uliowekwa na kanuni za CCM za uongozi na maadili," alisema Mukama.

Alisema, mbali na Kamati Ndogo ya Uchunguzi ambayo iko chini ya Kamati Kuu ya CCM, pia Nec iliagiza kamati za maadili na usalama nchi nzima, kuwachukulia hatua viongozi wanaotuhumiwa kwa haki na kuwapa fursa ya kujitetea na kupeleka taarifa kwa mamlaka za uteuzi za viongozi hao.

Mukama alifafanua, kuwa wako watakaochukuliwa hatua na mamlaka za wilaya, za mkoa na Taifa na hilo litatekelezwa wa kuzingatia Mamlaka iliyomteua au kumwidhinisha kiongozi husika.

Katibu Mkuu aliyefuatana na Msekwa na Katibu wa Nec, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alifafanua kuwa hali ya siasa ndani ya chama hicho ni shwari, lakini si shwari sana.

Alisema chama kinakiri kuwapo harakati za viongozi wake kugombea urais mwaka 2015 na kuongeza kuwa hazina madhara kwa chama huku akinukuu kauli za kiongozi wa China, Mao Dze Dung kuwa waache mawazo na fikra 100 zishindane na fikra pevu
zitajidhihirisha, jambo lililoonesha kuwa harakati hizo zimeruhusiwa.

Hata hivyo, alionya kuwa harakati hizo zinatakiwa kufuata utaratibu, kuepuka kugawa wanachama katika makundi na kuepuka kuchafuana, kama njia ya kujitangaza, huku akilaani viongozi walioweka pembeni majukumu ya kiserikali na kujikita katika harakati za kutafuta urais.

Pia alikiri kuwapo alichokiita saratani ya kupanga safu ya viongozi huku akionesha kuwa inaweza kutokea katika uchaguzi wa ndani ya chama mwakani.

Alisema ili kuepuka harakati za urais zisilete madhara na kumaliza saratani ya kupanga safu, CCM inajipanga kuwa wazi katika uchaguzi wa ndani wa mwakani ili kipate viongozi watakaohaghaika na wavuja jasho.

Mbali na uongozi katika chama, Mukama alisema pia CCM inatafuta utaratibu mzuri wa kumpata mgombea urais usiotegemea makundi na fedha na kuongeza kuwa mgombea atapimwa kwa msimamo wake katika itikadi ya chama hicho na hoja zake za kupambana na umasikini wa Watanzania.

Kwa mujibu wa Mukama, ajenda ya mageuzi imepokewa vyema hasa na viongozi kwa kuwa kabla ya kuanzisha kwa ajenda hiyo, viongozi wa CCM walifikia mahali wakawa kama kuku kwenye tenga ambao wakifunguliwa watoke, hubakia wamezubaa.

Hata hivyo, alisisitiza umuhimu wa mageuzi hayo kufanyika kwa utaratibu, ili kuzuia mpasuko huku akionekana kutofautiana na falsafa ya Nape ya kuoga kwa kuanzia kichwani kwenda mwili mzima, kwa kusema kuwa watu wanaoishi kando ya ziwa, huanza kujaribu maji kwa mguu na kuingia kuanzia chini kwenda juu.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Martine Shigella, amekana taarifa za kuwapo mkakati wa kuasi ndani ya chama hicho, huku akikiri kuwa taarifa hizo za uasi 'zimechangia' wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama hicho kuzingatia maslahi ya chama.

Akizungumza jana muda mfupi baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama kutoa taarifa ya maazimio ya kikao cha Nec kilichomalizika juzi, Shigella alisema hata taarifa za uasi hazikutolewa na kiongozi wa umoja huo na kwamba kwa kuwa jumuiya hiyo ni ya CCM haiwezi kuasi chama.

Alipotakiwa kueleza sababu za wenyeviti wa umoja huo kutoka mikoa 17 nchini na makatibu wao kupiga kambi Dodoma wakati wa kikao cha Nec, alisema hana taarifa ya ujio wa viongozi hao, wala sehemu waliyosaini ingawa gazeti hili lilishuhudia wakiletwa na mabasi yenye bendera za chama hicho.

Hata hivyo, pamoja na kukana kuwapo kwa viongozi hao, Shigella pia alikiri kuwaona baadhi na kuongeza kwamba walikuja kusikiliza yanayoendelea katika vikao hivyo kwa karibu.
Shigella pia alimpongeza Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, kwa kuongoza vema vikao vya Kamati Kuu na Nec, kwa maelezo kuwa watu walichotarajia hakikutokea, lakini bila kufafanua.

Madiwani CHADEMA, CCM wala njama kumpindua Meya Moshi

Meya wa Moshi
Meya wa Moshi

ULEVI  wa madaraka umeanza kukisumbua  Chama cha Demokrasia  na Maendeleo (CHADEMA)  katika  Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro Kutokana na mgogoro  wa chini kwa chini unaofukuta  miongoni mwa madiwani wa  chama  hicho wanaotaka kufanya mapinduzi ili kumwondoa madarakani Meya, Michael Jaffary.
Katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka 2010, CHADEMA kilishinda nafasi ya ubunge kwa kishindo katika Manispaa ya Moshi kwa Philemon Ndesamburo kuwabwaga washindani wake.
Chama hicho pia kilishinda  viti  vya   udiwani katika  kata 17 kati ya 21 vya Chama cha Mapinduzi hivyo CHADEMA kupata fursa ya kuongoza halmshauri hiyo.
Hata hivyo, pamoja na kupata mafaniko hayo katika kile kiinachoonekana kuwa ni kulewa madaraka baadhi ya madiwani wanadaiwa kuanza kusuka mipango ya kumwondoa Meya katika nafasi yake, wakimtuhumu kuwa hakidhi mahitaji ya kisiasa ya chama na wananchi wa Manispaa ya Moshi.
Taarifa zilizolifikia Raia Mwema mjini Moshi na baadaye kuthibitishwa na vyanzo kadhaa zilieleza kuwa madiwani wanaoongoza harakati za kutaka kumwondoa Meya huyo wametoka katika kata tatu za manispaa hiyo na mwingine wa viti maalumu pamoja na wale wa Chama cha Mapinduzi.
Habari zaidi zinaeleza kuwa madiwani hao wanajenga hoja kuwa Meya Michael Jaffary alihusika na operesheni ya kuvunja vituo vya kuoshea magari (car wash) iliyofanyika miezi mitatu iliyopita. Katika operesheni hiyo zaidi ya vituo 20 vilivyunjwa na askari wa manispaa hiyo.
Vituo hivyo ni vile vilivyojengwa kinyume cha utaratibu na sheria zinazosimamia mipango miji kwa kujengwa katika makazi ya watu, hifadhi ya barabara na maeneo yenye majengo ya umma kama shule.
Manispaa ya Moshi iliendesha operesheni ya kuvunja vituo hivyo vya kuoshea magari katika kata za Bondeni, Mawenzi, Kilimanjaro na Kiusa na operesheni hiyo ilitekelezwa usiku wa manane kwa kutumia askari wa manispaa hiyo
Akizungumza na Raia Mwema moja wa madiwani  wa CHADEMA katika Wilaya ya Moshi (jina linahifadhiwa) alisema wanazo taarifa za uhakika kuwa madiwani hao wamekuwa wakifanya vikao katika hoteli moja mjini hapa kupanga mipango ya kumwondoa meya  madarakani.
“Ni kweli kuna madiwani wenzetu  wameungana na wale wa CCM kusuka mipango ya kumwondoa meya katika nafasi yake na tayari taarifa hizo tunazo na tumeshaanza kuzifanyia kazi,” alisema diwani huyo.
Kiongozi huyo alisema kuwa sababu nyingine inayotolewa na madiwani hao ni hatua ya Manispaa ya Moshi kuvunja pia baadhi ya majengo yaliyojengwa bila kufuata taratibu za ujenzi katika maeneo ya miji.
“Wao wanadai kuwa hatua ya kuvunjwa kwa vituo hivyo vya kuoshea magari na pia baadhi ya majengo kutaondoa umaaarufu wa chama hicho mkoani Kilimanjaro  hivyo meya awajibishwe kwa kuruhusu kuvunjwa kwa vituo hivyo,” alisema.
Diwani huyo alisema baada ya kufanya vikao vya kusuka mpango huo madiwani hao wamekuwa wakiendelea kufanya ushawishi kwa madiwani wengine ili hoja  ya kumwondoa meya itakapoletwa basi iungwe mkono na madiwani wengine.
“Kinachowasukuma hao madiwani ni uroho wa madaraka tu kwani  hoja zao hazina mashiko na masuala wanayoyatetea hayana msingi wala maslahi kwa wananchi wa mji wa Moshi,” aliongeza diwani huyo katika mazungumzo yake na gazeti hili.
Mwenyekiti wa Madiwani wa CHADEMA katika Manispaa hiyo, Jomba Koi, alikanusha kuwapo kwa mgogoro wowote na kumtaka mwandishi wa RaiaMwema kuachana na habari za aina hiyo.
“Mimi ni mwenyekiti wa madiwani na hatuna mgogoro wowote ila nakushauri uachane na habari za aina hiyo haina maana yoyote zaidi ya kuleta hali ya vurugu ndani ya chama,” alisema Koi.
Akizungumzia madai hayo Meya wa Manispaa hiyo Michael Jaffary alishindwa kuthibitisha au kukanusha njama hizo za kutaka kumuondoa katika wadhifa huo.
“Siwezi kuzungumzia hatua hiyo ila nataka nikueleze kuwa kutofautiana kimtazamo ni masuala ya kawaida katika uongozi wa umma na ninachoweza kusema tofauti zilizopo ni za kimtazamo tu ila suala la kutaka kuniondoa madarakani siwezi kulisemea,” alisema meya huyo.
Alisema uamuzi wa kuvunja vituo vinavyolalamikiwa ulifikiwa na vikao halali vya halmashauri na wala si uamuzi wake binafsi hivyo wanaoalalamika kama wapo walikuwa pia sehemu ya uamuzi huo wa pamoja katika halmashauri.
“Mimi kama Meya siwezi kujiamulia majengo na mali nyingine za wananchi zivunjwe ila hayo ni maamuzi (uamuzi) halali yaliyofikiwa katika vikao vya halmashauri hivyo anayelalamika kuhusu mimi atakuwa hanitendei haki,” alisema.
Kuhusu kuvunjwa kwa baadhi ya majengo Meya huyo alisema kimsingi uamuzi huo pia ulifikiwa katika vikao vya Baraza la Madiwani na hatua hiyo inatokana na matayarisho ya maombi ya mji huo kutaka kuwa jiji.
“Unajua tumejiwekea malengo ya kuugeuza mji wa Moshi kuwa jiji katika kipindi cha miaka miwili ijayo kuanzia sasa na moja ya sifa zinazotakiwa ni mji kuwa katika mpangilio unaokubalika hivyo Baraza la Madiwani limeazimia kukomesha ujenzi holela usiozingatia sheria za mipango miji,” alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Kilimanjaro, Philemon Ndesamburo, hakuwa tayari kuzungumzia mgogoro huo akisema bado haujafikishwa rasmi ofisini kwake.
“Sisi ngazi ya mkoa bado hatujapata rasmi taarifa hizo lakini naomba ungeacha kwanza kuandika suala hilo hadi hapo tutakapokutana kwa vikao rasmi na unajua migogoro hii inapokuwa kwenye media (vyombo vya habari) haileti picha nzuri na unavuruga chama,” alisema Ndesamburo ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini.
Naye Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Kilimanjaro, Basil Lema, alikuwa na maoni tofauti na Ndesamburo akieleza kuwa kutofautiana kwa madiwani hao ni hatua nzuri katika kukuza wigo demokrasia ndani ya chama chao.
“Sisi kama mkoa bado hatujapata rasmi malalamiko dhidi ya meya au madiwani lakini kama madiwani wanaona kuna dosari miongoni mwao na wakazungumza si jambo baya bali ni katika kupanua wigo wa demokrasia ndani ya chama chetu,” alisema Lema.
Alisema hata hivyo malalamiko hayo yakiwasilishwa yatashughulikiwa kwa mujibu wa kanuni na taratibu za kichama na muafaka wake utapatikana kwani CHADEMA ni chama kilichokomaa na kimeshakumbana na matatizo ya aina hiyo.

Tunahitaji Mamlaka ya Gesi na Mafuta – Zitto

Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini
Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Kaskazini

Haya ni maoni ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, kuhusu sekta ya gesi na mafuta. Ili kujua zaidi mawazo yake, endelea kusoma makala haya.
MKUTANO wa tano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na mambo mengine ulijadili taarifa ya Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, kuhusu sekta ndogo ya gesi nchini.
Taarifa hii ilitokana na kazi iliyofanywa na kamati ndogo iliyoundwa na Kamati ya Nishati na Madini, chini ya uongozi wa Mbunge wa Bumbuli, Januari Makamba.
Miongoni mwa hadidu rejea za kamati ndogo zilikuwa ni kubainisha kama mikataba, taratibu na kanuni zinazotawala shughuli za gesi zinazingatia maslahi ya taifa na hazitiliwi shaka na wadau na kubainisha kama uamuzi unaoendesha shughuli za gesi kama vile gharama za ujenzi, uendeshaji na mambo mengine yanayoweza kuathiri gharama na usalama wa shughuli yanafikiwa kwa ufanisi na yanazingatia maslahi ya taifa.
Taarifa ya kamati iliwasilishwa bungeni na kupitishwa na Bunge ili Serikali iweze kutekeleza maazimio zaidi ya 26 yaliyopendekezwa.
Miongoni mwa maazimio hayo ni azimio namba mbili ambalo linasema; “Kamati imejiridhisha bila shaka kwamba  kwa kipindi cha 2004 hadi 2009 Kampuni ya Pan African Energy Tanzania Ltd (PAT) imejirudishia isivyo halali gharama zinazofikia jumla ya dola za Marekani milioni 28.1 sawa na fedha za Tanzania Sh. bilioni 46.3.
“Kutokana na kujirudishia fedha hizo isivyo halali kumefanya Serikali kukosa gawio lake linalofikia dola za Marekani milioni 20.1.  Aidha, mpaka wakati Kamati inaandaa ripoti hii, Kampuni ya Pan African Energy Tanzania Ltd (PAT) imeshindwa kuwasilisha uthibitisho wa uhalali wa kujirudishia gharama nyingine zinazofikia dola za Marekani milioni 36.
Hali hii inaonyesha mashaka makubwa katika uendeshaji wa sekta hii muhimu ya gesi.
Azimio hili ni moja ya maazimio yanayopaswa kuangaliwa kwa umakini mkubwa tunapojadili namna Tanzania inavyosimamia na kufaidika na sekta ya mafuta na gesi.
Taifa linafaidika kwa kiwango gani na wawekezaji wanafaidika kwa kiwango gani ndio msingi wa mikataba ya mafuta na gesi nchini. Bado hakuna mijadala mikali katika eneo hili ukilinganisha na mijadala katika sekta ya madini kwa mfano. Kukosekana kwa mijadala hiyo kunaachia kila kukicha Shirika la Maendeleo ya Mafuta Tanzania (TPDC), kusaini mikataba ya kutafuta na kuchimba mafuta na gesi (Production Sharing Agreements – PSAs) bila Watanzania kujua haswa ni jambo gani linasainiwa. Hivi sasa kuna mikataba hii 23 hapa nchini.
Duniani kote kuna familia mbili za mikataba ya mafuta na gesi. Familia ya kwanza inaitwa ‘concessionery’ ambapo kampuni binafsi ya mafuta inapewa haki zote za mchakato mzima wa kutafuta, kuchimba, kusafirisha na kuuza mafuta au gesi.
Umiliki wa mafuta (rights) unakuwa ni wa kampuni binafsi na si Serikali. Katika mfumo huu kampuni hulipa mrabaha serikalini na kodi zinazopaswa. Nchi kama Marekani, Uingereza na Canada hutumia mfumo huu.
Familia ya pili ni mikataba ya uzalishaji au kwa Kiingereza Production Sharing Agreements (PSAs). Katika mfumo huu haki (right) inabaki kuwa mali ya taifa husika na kampuni ya mafuta huwa ni kama mkandarasi tu wa kutafuta na kuchimba mafuta. Akipata mafuta, anaondoa gharama za kuzalisha na faida inagawiwa kati ya kampuni hiyo na nchi husika kupitia Shirika la Mafuta.
Huu ndiyo mfumo unaotumika Tanzania na ulianzia huko Indonesia na Venezuela miaka ya sitini. Kutokana na mfumo huu ndiyo tunapata masuala haya ambayo Kamati ya Nishati na Madini imegundua kama nitakavyofafanua kwa ufupi hapa chini.
Mkataba wowote wa mafuta na gesi ni lazima uzingatie uzalishaji na mapato kwa ujumla, mrabaha kwa nchi, urejeshaji wa gharama za uzalishaji na kodi mbalimbali na namna faida inavyogawanywa.
Kampuni ya Pan Africa Energy kujirejeshea gharama isizostahili za zaidi ya Sh. bilioni 46 ni sehemu ya mianya iliyopo katika mikataba yetu. Jumla ya shilingi bilioni 110 zimeonekana kuwa na mashaka makubwa katika hesabu ya kampuni hii.
 
Taarifa inaonyesha kwamba kampuni hii imeweka pia gharama zao za uzalishaji kwa miradi ya nje ya Tanzania. Kwa kuwa Kampuni ya Pan Africa Energy Tanzania Limited ni kampuni tanzu ya Pan Africa Energy iliyosajiliwa ‘offshore’ Mauritius ambayo nayo ni kampuni tanzu ya Orca ambayo pia imesajiliwa visiwa vya Jersey, Tanzania isingekwepa kubambikiwa gharama ambazo si zake ili kupunguza mapato ya Serikali yake.
Imewahi kuelezwa huko nyuma kwamba hizi njia za kukwepa kodi zimeshamiri sana kutokana na kampuni kubwa zinazofanya biashara hapa nchini kufanya ‘tax planning’ na hivyo kuhamisha mapato yao kwenda nchi zisizo na kodi kubwa kama Mauritius, Isle of Man, Jersey au hata Jiji la London.
Aprili, mwaka 2009 katika taarifa yake ya mwaka, Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma ililieleza Bunge kwamba mkataba kati ya TPDC na Pan Africa Energy ni moja ya mikataba mibovu kuliko yote nchini.
Hii ilitokana na ukweli kwamba kwa mujibu wa PSA kati ya TPDC na Pan Africa Tanzania, mrabaha wa mafuta wa asilimia 12 unalipwa na TPDC na pia kodi ya mapato inakokotolewa kutoka katika mrabaha huo. Kwa maana hiyo, kampuni hii hailipi mrabaha na pia hailipi kodi ya kampuni (corporate tax) kwa mujibu wa mkataba.
Suala hili Kamati ya Nishati na Madini haikuliangalia (labda kwa kuwa ni la kihesabu). Kamati ya POAC ilitaka mikataba yote ya mafuta iangaliwe upya ili kuondoa mazonge haya yanayokosesha taifa mapato makubwa sana.
Uwezo wa TPDC kukagua hesabu za kampuni za utafutaji mafuta ni mdogo au haupo kabisa. Kama TPDC wangekuwa na uwezo huu leo Kamati ya Nishati na Madini isingekuta madudu haya katika kampuni.
Pia kama Kamati ya Nishati na Madini ingeangalia mikataba ya kampuni zote za kutafuta mafuta wangekuta madudu mengi zaidi. Kuna kampuni moja yenye kisima pale Mkuranga (mkoani Pwani), wamesema gharama za kuchimba visima vile ni dola za Marekani milioni 240 ilhali gharama halisi ni dola za Marekani milioni 60 tu. Hivyo gesi ikianza kuchimbwa itabidi warejeshe gharama zao kwanza.
Tanzania haitapata lolote mpaka gesi ile itakwisha.
Kuna haja ya kufanya marekebisho makubwa sana katika uendeshaji na usimamizi wa sekta ya Gesi Tanzania. Shirika la TPDC lirekebishwe kwa kuanzisha Mamlaka ya Mafuta na Gesi yenye uwezo na nguvu ya kusimamia uwekezaji katika sekta hii.
Vilevile kuanzishwe Shirika la Mafuta na Gesi (PetroTan – National Oil and Gas Company) ambalo litashiriki katika uwekezaji  kikamilifu na kampuni binafsi. Tusiposimamia vema sekta hii, taifa letu litaingia kwenye matatizo makubwa miaka ijayo.
Maneno ya gwiji wa uchumi, Joseph Stiglitz, ni ya kuzingatia. Anasema; “Mara zote nchi zinazoendelea zijue, wanapojadiliana na kampuni kubwa za mafuta, kampuni hizi hufikiria jambo moja tu. Jambo hilo ni kuongeza mapato yao kwa kupunguza mapato ya mataifa husika.”
Tanzania ni lazima ihakikishe kwamba inapangua mbinu zote za kampuni hizi kubwa kwa kujenga uwezo wa wananchi wake kupitia Shirika la Mafuta na Gesi, ili hatimaye kuweza kuwa na mikataba yenye kujali faida kwa nchi. Hili la Pan Africa Energy litufumbue macho.

Pinda, Makinda ‘wavuta’ za Jairo

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
 
Wabunge ‘wakunja’ milioni 16
Ripoti Kamati Teule ina utata

SEHEMU ya mamilioni ya fedha zilizochanganishwa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo, zimelipwa pia kwa wabunge kupitia semina, akiwamo Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, baadhi ya mawaziri na Spika, Anne Makinda, Raia Mwema, imebaini.
Pinda na Makinda walikua katika kundi moja na Diana Chilolo (Mwenyekiti wa semina), John Joel (Mwakilishi wa Katibu wa Bunge) na January Makamba, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, ambaye hata hivyo jina lake lilikatwa na hakuwa amesaini karatasi ya malipo hayo ya Shilingi 280,000 kila mmoja.
Mbali na Spika na Waziri Mkuu, wengine waliosaini fedha hizo ni mawaziri na wabunge kadhaa wa wakiwamo wale maarufu wa vyama vya CUF, CHADEMA, NCCR-Mageuzi na CCM, katika semina iliyofanyika Juni 26, mwaka huu, mjini Dodoma kuhusu sekta ya umeme nchini ambao wao walilipwa Sh.110,000 kila mmoja.
Miongoni mwa wabunge wakiwamo maarufu ambao hata hivyo utaratibu wa malipo kwao katika semina ni wa kawaida ni pamoja na Mchungaji Israel Natse (Karatu), Augustino Masele (Shinyanga Mjini) na Diana Chilolo (Vitimaalumu mkoani Singida).
Wengine ni Hamad Rashid Mohamed (Wawi), Philemon Ndesamburo (Moshi Mjini), Binilith Mahenge (Makete), David Kafulila (Kigoma Kusini), Davidi Silinde (Mbozi Magharibi), Moses Machali (Kasulu Mjini), Grace Kiwelu (Vitimaalumu-Kilimanjaro), Augustino Mrema (Vunjo), Profesa David Mwakyusa, Kassim Majaliwa na Kheri ali Khamis.
Wabunge wengine kwenye orodha hiyo ni Naomi Kaihula, Maria Hewa, Cynthia Ngoye, Peter Msolla, Juma Nkamia, Esther Matiko, Joseph Selasini, Mohummad Sanya, Tundu Lissu, Stela Manyanya, Lucy Owenya, Ezekia Wenje, Cristina Mughwai, Leticia Nyerere, Livingstone Lusinde, George Simbachawene na Gosbert Blandes.
Mawaziri katika orodha hiyo ni pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu- Bunge na Uratibu, William Lukuvi, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Hawan Ghasia, Naibu Waziri wa Fedha, Gregory Teu, Naibu Waziri wa Uchukuzi, Athumani Mfutakamba na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Uwekezaji na Uwezeshaji, dk. Mary Nagu.
Wengine ni Naibu Waziri wa Maji, Gerson Lwenge, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanry, Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Dk. Milton Mahanga na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sofia Simba.
Wakati malipo hayo ya posho kwa viongozi hao yakiwa hayana utata, hali imekuwa tofauti kwa watumishi wengine wa Serikali waliolipwa fedha hizo. Baadhi wakiwa wamelipwa na kusaini Sh. 20,000 tu, tarakimu hizo zimeghushiwa na wahasibu husika na kuonekana wamelipwa Sh 120,000.
Kutokana na kasoro kubainika katika mchakato wa matumizi ya fedha hizo ambazo ukusanyaji wake haukidhi vigezo vya kisheria na taratibu, Kamati Teule iliyoundwa kuchunguza sakata hilo, imependekeza sasa Bunge kujadiliana na Serikali ili hatimaye kutenga fungu maalumu kwa ajili ya semina za wabunge, badala ya sasa ambapo fedha hazikujulikani zimepatikana vipi na kisha kulipwa kwa wabunge au viongozi wengine wakiwamo mawaziri.
Kamati hiyo teule iliyoongozwa na Mbunge, Ramo Makani inaeleza katika ripoti yake; “Kamati Teule inapendekeza Bunge lijadiliane na Serikali kuhusu namna bora ya kuendesha semina kwa wabunge, ikiwamo kutenga kasma mahususi ndani ya Mfuko wa Bunge na kusisitiza uwazi, uwajibikaji na ufanisi katika matumizi ya fedha.
Utata ripoti ya Kamati Teule
Kwa upande mwingine, ripoti ya Kamati Teule ya Bunge, imetoa taarifa yenye mgongano na hasa mapendekezo yake kuhusu kuwachukulia hatua Waziri William Ngeleja na Naibu wake, Adam Malima.
Utata unajitokeza pale ambapo kamati hiyo licha ya kupendekeza viongozi hao wachukuliwe hatua lakini inakiri kuwa hawajabaini ushiriki wa viongozi hao katika uchotaji wa fedha hizo.
Sehemu ya ukurasa wa 144 wa taarifa hiyo inasomeka; “Katika suala la uchangishaji fedha uliofanywa na Wizara ya Nishati na Madini, kamati teule baada ya kukamilisha uchunguzi kwa kupitia nyaraka mbalimbali na kufanya mahojiano na watu mbalimbali, haikuweza kuthibitisha moja kwa moja ushiriki wa Waziri au Naibu Waziri, katika kubariki au kuidhinisha uchangishaji huo.”
Hata hivyo, kamati hiyo licha ya kukiri kushindwa kuthibitisha uhusika wa Waziri na Naibu wake, imependekeza wachukuliwe hatua kwa kujificha katika ‘kichaka’ kuwa viongozi hao walipaswa kujua kila kinachoendelea katika wizara yao.
Hali hiyo ya utata ndiyo iliyotumiwa na Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo, kumtetea Waziri Ngeleja na Naibu wake, Adam Malima, kwamba hakuna uthibitisho wa kuhusika kwao katika uchotaji wa fedha hizo.
Wengine waliochangia katika mwelekeo huo ambao pia walionesha wazi kuwa tatizo la msingi ni mfumo na si mtu ni pamoja na Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka, Mbunge wa Same Mashariki na Anne Kilango Malecela.
Wabunge hao kila mmoja kwa wakati wake walipokuwa wakijadili ripoti hiyo bungeni wiki iliyopita mjini Dodoma walieleza kuwa ni wakati muafaka kwa mfumo mzima wa Serikali kubadilishwa na hasa katika eneo la matumizi ya fedha za umma.
Katika hatua nyingine imebaini kuwa Wizara ya Nishati na Madini ndiyo inayoongoza kujilipa posho kubwa katika masuala ya shughuli zake za kibajeti ndani ya Bunge, ikilinganishwa na wizara nyingine.

Lowassa apambana

'Fainali’ Uvuaji Gamba CCM

Edward Lowassa
Edward Lowassa
 
Hatima yake na Andrew Chenge mashakani
Wafuasi wake wamfananisha na Rais Jacob Zuma
January amkera Rais Kikwete, hoja yake yazimwa
UVCCM vurugu tupu Dodoma
UPEPO wa hali ya kisiasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unazidi kuvuma, na sasa watu wanaotajwa kuwa na nguvu kubwa ndani ya chama hicho, Edward Lowassa na Andrew Chenge, wamebanwa na wanapambana ‘kufa au kupona’.
Japokuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, juzi Jumatatu, alilaumu vyombo vya habari kwa kupandisha joto nchini kuhusiana na matukio  ndani ya chama hicho, ukweli ni kwamba kuna upepo mbaya unavuma ndani ya CCM, na kila kitu kinachofanyika ndani ya vikao kinaleta hisia mchanganyiko.
Tayari imethibitika kwamba Lowassa na Chenge wako vitani kujibu mapigo wakisaidiwa na kundi kubwa la wafuasi wao wakiwamo viongozi wa Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM) waliofika Dodoma kuwasaidia kuokoa jahazi, hatua ambayo nayo imeiweka jumuiya hiyo katika hatari ya kuvunjwa kwa muda.
January Makamba amkera Kikwete
Mjumbe mmoja wa  Kamati Kuu ya CCM, January Makamba anaelezwa kuwa aliwasilisha mada, juzi Jumatatu, inayozungumzia hali ya kisiasa nchini akipendekeza uamuzi wa kuwachukulia hatua kina Lowassa na Chenge usitishwe ili kuepuka mgawanyiko ndani ya chama.
Katika kujenga hoja, mjumbe huyo alitoa mfano wa mjadala wa Katiba na nguvu kubwa ya CHADEMA nchi nzima kuwa inabidi CCM iepuke mgawanyiko unaoweza kutokea kwa kuwang’oa wenzao wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Hata hivyo, mapendekezo hayo yalionekana kumkera Mwenyekiti, Rais Kikwete, ambaye alihoji ni nani aliyesababisha mgawanyiko, na nini madhara ya kisiasa kwa CCM kutokua na msimamo katika kukemea uovu.
Rais Kikwete alipoonyesha kupinga moja kwa moja mawazo ya kuahirisha ‘uvuaji gamba’, alibadili hali ya hewa ndani ya kikao hicho kilichoahirishwa Jumatatu usiku na kuendelea Jumanne asubuhi.
Lowassa, Chenge wakataa kujiondoa NEC
Taarifa kutoka kwa watu walio karibu na Lowassa na Chenge, mjini Dodoma, zinaeleza kwamba awali wanasiasa hao walielezwa wazi wazi kujiondoa wenyewe kutoka NEC na kubakia na ubunge, ushauri ambao waliupinga moja kwa moja.
Imeelezwa kwamba pamoja na kukiri udhaifu na kuomba kuwapo kwa suluhu, Lowassa anaelezwa kujitetea kwa kuhoji ni kwa nini achukuliwe hatua peke yake wakati wapo baadhi ya viongozi ambao wanatuhumiwa na wengine wamekwisha kufikishwa mahakamani kwa makosa mbalimbali, na kutoa changamoto kwa Serikali kumchukulia hatua za kisheria kama inaona yeye ni fisadi.
“Wanasema yeye ni fisadi ajivue gamba, yeye akawaambia; mbona kuna wengine hadi mahakama imewatia hatiani lakini hawachukuliwi hatua zozote na kusema kama kweli ana makosa kwanini hafikishwi mahakamani?” , alisema mfuasi mmoja wa Lowassa ambaye yuko mjini Dodoma.
Hata hivyo, utetezi huo wa Lowassa ulikwisha kupatiwa majibu na Nape ambaye aliwaambia waandishi wa habari kwamba suala la ‘uvuaji gamba’ si la watu watatu tu, lakini ni lazima pawepo pa kuanzia.
Utetezi wa Lowassa umekuwa na nguvu kubwa na hapa Dodoma, kuna makundi makubwa ya watu; hasa vijana wanaodai ni wafuasi wa CCM, wakiwa na fedha nyingi, wanaendesha vikao kwenye mahoteli na mabaa na wanataja baadhi ya ajenda zilizowaleta hapa.
Kati ya ajenda hizo ni kuhakikisha kwamba ile dhana ya ‘kujivua gamba’ iliyoasisiswa na Mwenyekiti wao, Rais Jakaya Kikwete, mwanzoni mwa mwaka huu, inakomea hapo ilipofikia, isiwaguse watu wengine, na hasa Lowassa - Waziri Mkuu aliyejiuzulu kwa kashfa ya umeme mwaka 2008 na Mbunge wa Monduli; na Andrew Chenge, Mwanasheria Mkuu wa zamani na Mbunge wa Bariadi Magharibi.
Baadhi ya vijana hao wamekuwa wakimfananisha Lowassa na Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma, ambaye aliandamwa na kashfa za rushwa na ukosefu wa maadili kabla ya kushinda kesi mahakamani na baadaye kushinda uchaguzi ndani ya chama chake na kuwa Rais.
Lowassa afananishwa na Zuma
“Wameanza kumfananisha Lowassa na Zuma na kwamba atashinda tuhuma zinazoelekezwa kwake na kuwa Rais wa Tanzania baadaye,” anasema mmoja wa vijana wa UVCCM aliyeko Dodoma.
Vijana hao, wakiwamo viongozi wa karibu mikoa yote wa Umoja wa UVCCM, wanasema wako Dodoma kushinikiza mpango wanaodai unaandaliwa wa kuuvunja umoja wao, uachwe.
Ukiacha taarifa zinazosema kuna hali ya kuvutana ndani ya CCM na hata katika vikao vyake vya juu vilivyoanza hapa mwishoni mwa wiki iliyopita, kuhusu hatua za kuchukuliwa dhidi ya Lowassa na Chenge, ambao maazimio ya mkutano uliopita wa Halimashauri Kuu (NEC) yanasema wachukue hatua ya kujiondoa ama vinginevyo chama kitaamua wao wakishindwa, yapo maoni kwamba UVCCM ya leo haina msaada kwa chama.
Ni umoja unaoonekana kuendeshwa kwa kufuata matakwa ya watu kadhaa ambao wamekuwa wafadhili wakuu wa baadhi ya viongozi wa umoja huo .
Inasemwa kwamba baadhi ya viongozi wa UVCCM sasa nao wana fedha na mali ambazo kwa kazi na kipato chao, hawawezi kuthibitisha wamezipata wapi.
Mwishoni mwa wiki iliyopita na mwanzoni mwa wiki hii, umoja huo ulizua tafrani kubwa hapa Dodoma pale ziliposambazwa taarifa kwamba ulitaka kuitisha kikao cha dharura cha Baraza lake ili kutoa tamko kwamba hauko tayari kuvunjwa, na ikitokea ukavunjwa, basi,vijana wote watahamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Taarifa za ndani ya CCM zinasema kwamba ni kweli mwenendo wa UVCCM umekuwa hauwaridhishi wengi, na kwa ajili hiyo baadhi ya viongozi wa umoja huo waliitwa mbele ya Kamati ya Maadili kutoa maelezo ya baadhi ya matamshi na matendo yao.
Bashe na wenzake waitwa kuhojiwa
Kati ya wanaotajwa kuitwa mbele ya Kamati ya Maadili Jumapili iliyopita ni Hussein Bashe, mjumbe wa Baraza Kuu la Vijana. Ukiacha nafasi hiyo ndani ya UVCCM, Bashe ni mwajiriwa wa kampuni ya magazeti ya New Habari inayomilikiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz na mbunge wa zamani wa Igunga aliyejiondoa katika siasa miezi kadhaa iliyopita akidai amechoshwa na siasa chafu. Bashe ni mtendaji mkuu katika kampuni hiyo ya Rostam.
Kama walivyo Lowassa na Chenge, Rostam naye alikuwa akituhumiwa na chama chake kuwa kwa matendo yake na kutajwa sana katika matukio ya ufisadi; ya kampuni iliyochota fedha Benki Kuu ya Kagoda na kashfa ya kampuni ya kufua umeme ya Richmond, anakikosesha mvuto mbele ya jamii jambo ambalo lilichangia kupungua kwa kura za mgombea wa CCM wa nafasi ya rais, Kikwete, ambaye aliporomoka hadi kufikia kura asilimia 61 katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana kutoka katika asilimia 82 za mwaka 2005.
Bashe amekuwa akidaiwa kwamba alitoa matamshi mabaya dhidi ya chama chake akiwa wilayani Nzega alipoashiria kudai kwamba CCM isingeshinda katika uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi ya Rostam, Igunga, na hiyo ingesaidia kuweka heshima.
Imefahamika kwamba kamati hiyo pia ilimwita Katibu wa  Mkoa wa Dar es Salaam, Kirumbe Ng’enda, ambaye anatuhumiwa kusababisha mtafaruku katika zoezi la kura za maoni kiasi cha kumshusha mmoja wa wagombea nafasi za udiwani wa viti maalumu vya wanawake kutoka nafasi ya juu hadi ya chini katika mazingira yanayoashiria ufisadi.
Kamati ya Maadili ina wajumbe wazito, baadhi yao ni: Mwenyekiti Kikwete, Makamu wenyeviti, Pius Msekwa na Amani Karume, Makamu wa Pili wa SMZ, Balozi Seif Iddi,Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Katibu Mkuu, Wilson Mukama na Manaibu Katibu Mkuu, Kapteni mstaafu John Chiligati na Vuai Ali Vuai.
Hakuna taarifa zilizokuwa zimepatikana kuhusiana na hatima ya Bashe na Ng’enda na baadhi ya wanachama wa UVCCM wanaodaiwa kutoa matamshi ya kashfa kwa Mwenyekiti ambao nao waliitwa.
Kwa kawaida, kamati hiyo ina mamlaka ya kuchukua hatua, lakini pia inaweza kupendekeza hatua za kuchukuliwa na vikao vya juu zaidi, yaani Kamati Kuu ambayo sehemu ya wajumbe wake ni haohao wa kwenye Kamati ya Maadili na NEC.
Baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa nchini  wanasema kwamba kwa kuchoshwa na matatizo ya UVCCM, CCM inaweza kufanya kama ilivyopata kufanya huko nyuma.
Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1995, UVCCM iliweka msimamo uliokuwa unachagiza wagombea vijana wapewe nafasi ya kuwania urais. Majina yaliyokuwa yakitajwa wakati huo ni pamoja na ya kina Kikwete na Lowassa, waliokuwa wakiungwa mkono na kina Anne Makinda na wengineo. Joto lilipozidi, uongozi wa juu wa UVCCM uliondolewa na hali ikabaki salama.
Baadhi ya waliokuwa katika uongozi wa UVCCM wakati huo ni pamoja na John Guninita ambaye leo ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam. Vijana wengine wa enzi hizo ni pamoja William Lukuvi ambaye sasa ni mjumbe wa Kamati Kuu, Leonidas Gama ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Muhammed Seif Khatibu, John Henjewele na Said Mwambungu ambaye sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
Aidha, wachambuzi hao wanasema hata ‘kujivua gamba’ kulikwishakufanyika ndani ya CCM japo kwa msamiati mwingine, lakini wenye maana karibu na huo.
“Mwaka 1984 walisema hali ya kisiasa ilikuwa imechafuka na kuchafuka huko kukaondoka na aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Aboud Jumbe Mwinyi. Baadaye mkono huo wa CCM ukamfikia Maalim Seif Shariff Hamad na wenzake.
“Lakini hata huko nyuma, miaka ile kati ya 1960 watu kama Wilfreim Mwakitwange, Fortunatus Masha, Choga na Kasanga Tumbo  ambao walikuwa wabunge maarufu, walifukuzwa ndani ya TANU na chama hakikutetereka,” anasema mmoja wa wachambuzi hao.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi kuhusu joto hilo la kisiasa hapa na nchini kwa ujumla, Nape alisema hakuna haja ya kuwa na hofu ya mageuzi yanayofanyika sasa ndani ya CCM kwa vile yanalenga kukiboresha chama hicho.
"Kama kwa kusimamiavyema  rasilimali na kupiga vita rushwa na ufisadini kutaleta mpasuko, nadhani mpasuko huo utakuwa ni mwema kwa vile utaondoa dhambi ndani ya chama," alisema Nape akiomba vyombo vya habari kuwa na subira.
Aliongeza Nape: “Ikifika hatua ya wananchi kuwa na shaka ya uadilifu wa mtu au chama,ni lazima kuhakikisha shaka hiyo inatoka kwa kufanya mageuzi."
Kikao cha Kamati Kuu kilianza hapa juzi na kilitarajiwa kuendelea jana kabla ya cha  NEC kilichopangwa kuanza leo Jumatano na kukamilika kesho Alhamisi.
NEC inakutana baada ya kikao chake cha mwisho cha Aprili mwaka huu ambacho kiliazimia ya kuwa wanaokishusia chama mvuto wajuvue gamba.
Uamuzi huo ulikuwa umechangiwa kwa kiasi kikubwa na maoni shawishi ya mmoja wa Wenyeviti wa Mikoa, Mwenyekiti  wa Mkoa wa Mara, Charles Makongoro Nyerere, aliyesema watu wa kawaida walikuwa wakishangazwa na CCM kuendelea kukumbatia watu waliokuwa wakionekana  wanashiriki katika ufisadi.
Akichangia wakati huo katika tathmini na mapendekezo ya Kamati Kuu ya kutaka Chenge, Lowassa na Rostam wawajibike, Makongoro  Nyererealisema isingewezekana Chenge, Lowassa na Rostam kuendelea kuwa na nafasi za uongozi ndani ya chama.
Alisema wakati huo mtoa habari wetu: “ Kwanza alianza kwa kumwambia Mwenyekiti kwamba japo yeye ni Mwenyekiti wa Taifa, yeye (Makongoro)  naye ni Mwenyekiti wa Mara na kwamba NEC ndio waajiri wa Mwenyekiti Taifa.
“ Akasema anapokaa Mwenyekiti wa Taifa ni mahala patakatifu na kwa ajili hiyo pasingeweza kusogelewa na shetani, hata kama siku moja Mungu alipata kukutana na shetani barabani.
“ Akasema kule site (kwenye eneo la ujenzi ambako yeye ndiko anakoshinda akichanganya zege na kupiga bati) wanasema na wanataka watuhumiwa wote wa ufisadi watoke kwenye nafasi zao.
“Lowassa ni ndugu yangu.Sina matatizo naye.Najua ananipenda, nami nampenda.Lakini kule site wanasema hapana.Atoke. Tena nawe Mweyekiti ulipokwenda Monduli, ukainua mkono wake juu, ukasema hujapata kuona kama yeye (Lowassa), kule site wakauliza, sasa hii  ndiyo nini?
“Rostam simfahamu vizuri. Ninakotembelea yeye hawezi kuja na  mimi siwezi kwenda anakotembelea. Sina ugomvi naye.Lakini kule site wanasema naye hapana. Ulipokwenda Igunga ukamuamsha mkono ukasema ni kama timu ya mpira iliyokamilika watu kwenye site wakauliza sasa hii ndiyo nini?
“Nasikia Chenge wanamwita Mzee wa Vijisenti. Ni ndugu yangu. Sina hakika kama anavyo vijisenti kiasi hicho. Lakini kwenye site, si mimi, watu wanasema naye hapana, “ alikaririwa akisema Makongoro.
Mifano aliyoitaja Makongoro kwa kumhusisha Kikwete ilijitokeza wakati akiwa katika kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2010, katika majimbo ya Igunga alikokuwa akigombea ubunge Rostam na Monduli alikogombea ubunge Lowassa.
Akiwa katika majimbo hayo, Kikwete aliwanadi viongozi hao waliokuwa wamepitishwa na chama chake kuwania ubunge, licha ya tuhuma za ufisadi zilizokuwa zikielekezwa kwao.
Mwingine ambaye alichangia sana katika uamuzi wa NEC wa Aprili ni Mwanasheria Mkuu, Jaji Frederick Werema, aliyekuwa amealikwa kwenda kusaidia katika fafanuzi kadhaa ndani ya Kamati Kuu.
Ufafanuzi huo wa Werema ulihusu mchakato wa kupata katiba mpya ambao umepitishwa na Bunge wiki iliyopita.
Mpasha habari wetu wakati huo alisema:  “Kuondoka kwakina Lowassa, Rostam na Chenge kimeharakishwa na Werema. Aliletwa na Mwenyekiti kuja kufafanua mambo kadhaa kama mchakato wa katiba mpya.
“Katika mchango wake kama mtu aliyeko nje ya chama alizungumzia mambo ambayo yeye alisema hayaendi sawa ndani ya CCM. Kwanza alianza kwa kusema yeye si mwana CCM japo huko nyuma, kama walivyokuwa wengi, alipata kuwa mwanachama.
“Akasema kwao anakotoka (Jaji Werema anatoka Mkoa wa Mara)  mwanamume anapaswa kusema ukweli hata kama ukweli huo unauma kiasi gani.
“ Akasema kwamba alikuwa anaona tatizo kwamba taarifa nyingi za vikao kama hicho alichokuwa ameitwa kuzungumza, zilikuwa zinavuja sana.
“ Akasema hata hayo ambayo angeyasema, jioni yangekuwa yamewafikia watu wa nje, na wahusika wakubwa wa kuvujisha taarifa hizo walikuwa ndani ya Kamati Kuu hiyo hiyo.
“ Akiachana na hilo akahoji kwa nini, chama hicho kinalialia kuwa haiba yake imeshuka na wakati huo huo kikikumbatia vitu kama Richmond na Dowans ambavyo vinaichefua jamii na ambavyo wahusika wake wakuu wamo katika uongozi wa juu wa chama,” alisema mjumbe mmoja wa Kamati Kuu aliyezungumza na Raia Mwema.
Hadi tunakwenda mitamboni jana hakukuwa na taarifa mpya ya mwenendo wa kikao cha Kamati Kuu na maandalizi ya kikao cha NEC leo.
Raia Mwema hata hivyo ilishuhudia wajumbe kadhaa wa NEC waliokwisha kuwasili na kama ilivyo kawaida ya CCM, walikuwa katika vikundi vikundi wakiteta.

Wanasheria wamtega JK muswada sheria ya katiba

 Peter Saramba, Arusha

CHAMA cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kimetishia kwenda mahakamani kupinga Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba iwapo Rais Jakaya Kikwete atapuuza malalamiko na hoja za wananchi kupitia makundi mbalimbali wanayoupinga licha ya kupitishwa na Bunge wiki iliyopita.

Rais wa TLS, Francis Stolla aliwaambia waandishi wa habari mjini hapa jana kuwa upitishwaji wa muswada huo haukuzingatia taratibu na kanuni za Bunge na kumwomba Rais, akiwa sehemu ya Bunge kurekebisha makosa hayo kwa kukataa kuutia saini.

Chama hicho kimemtaka Rais Kikwete kuurejesha upya muswada huo bungeni ili usomwe kwa mara ya kwanza na wananchi wapewe fursa ya kuujadili kwa kina kwa lengo la kuupa uhalali kisheria, kijamii na kisiasa.

Stolla alikuwa akitoa mada wakati wa kujadili Miaka 50 ya Uhuru na changamoto ya mabadiliko ya Katiba kwa jamii za wafugaji, warina asali, waokota matunda na wakulima.
Akizungumza kwenye mkutano huo ulioandaliwa na Jukwaa la Umoja wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali yanayotetea Haki za Wafugaji (PINGO's Forum), Stolla alisema Rais Kikwete anapaswa kusikiliza kilio cha wananchi ili kuliepusha taifa na vurugu.

Alisema vurugu hizo zitatokana na sheria inayopendekezwa na muswada huo aliodai ulipitishwa kwa kuzingatia utashi wa kisiasa wa vyama badala ya mahitaji ya taifa na jamii.

Alisema sheria hiyo ikipitishwa, itakuwa imejadiliwa na wananchi wa mikoa mitatu pekee, miwili kutoka Tanzania Bara ambayo ni Dar es Salaam na Dodoma na Mkoa mmoja wa Zanzibar.

Alionya kuwa Tanzania ina mikoa zaidi ya 25 hivyo “Uwakilishi mdogo namna hii haukubaliki kwenye jambo kubwa na muhimu kama hilo la Katiba ya nchi inayobeba maisha na maslahi ya watu wote.”

Alisema licha ya muswada huo kutofikishwa kwa wananchi kwa lugha na wakati muafaka, pia umebeba maudhui yenye lengo la kuminya haki ya msingi wa watu kutoa maoni. Alisema haki hiyo imeminywa kutokana na Bunge kupitisha kifungu kinachonyima watu wasio wajumbe wa tume ya katiba kuandaa mikutano au majumuiko ya kujadili, kutoa, kukusanya na kuandaa maoni na mapendekezo yao kuhusu Katiba Mpya.
Isitoshe akasema kifungu hicho kinaweka wazi kwamba anayepatikana na kosa hilo atahukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au faini isiyozidi milioni 15 au vyote kwa pamoja.

Alisema ili kuitendea haki jamii na umma wa Watanzania, TLS imeunda kamati maalumu ya wanasheria zaidi ya watano inayoongozwa na Profesa Angelo Mapunda wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Kamati hiyo itakuwa na jukumu la kufanya utafiti juu ya vipengele vya sheria vilivyokiukwa na kuhakikisha wanashinda shauri watakalofungua mahakamani iwapo Rais atapitisha sheria hiyo.

Stolla alitaja upungufu mwingine kwenye muswada huo kuwa ni uwepo wa miswada miwili, wa Kiingereza uliowasilishwa bungeni Aprili, mwaka huu na kusomwa kwa mara ya kwanza kabla ya wabunge kuagiza ukaandikwe kwa Kiswahili ili kutoa mwanya kwa Watanzania wengi kuweza kuusoma na kuulewa.

Alisema muswada ulioandikwa kwa Kiswahili uliwasilishwa bungeni kwa mara ya kwanza mwezi huu lakini kwa makusudi na kwa kutumia uwingi wa wabunge wa CCM na CUF. Alisema kitendo cha kupitishwa kwa muswada huo ni cha aibu kwa Bunge na kinapaswa kurekebishwa na Rais kwa kukataa kutia saini.

Stolla alitaja kasoro nyingine katika muswada huo kuwa ni muundo wa Bunge la Katiba unaopendekeza wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kuwa wajumbe wa Bunge la Katiba hali itakayosababisha mjadala na upitishwaji wa Katiba Mpya kumilikiwa au kutawaliwa na wanasiasa.

Alisema hali hiyo ni hatari kwa sababu wanasiasa hao watapitisha kwa kuhakikisha wanalinda maslahi ya vyama na itikadi zao kisiasa.

WBaada ya makosa haya yote, kimbilio pekee la wananchi kurekebisha makosa haya yaliyofanywa kwa makusudi na Bunge letu ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mheshimiwa Jakaya Kikwete,” alisema na kutoa wito:

“Tunamuomba asikilize kilio cha watu wake, atafakari hoja zao na kukataa kusaini sheria hii kwa maslahi ya kizazi cha sasa na kijacho. Atumie nafasi yake ya sehemu ya pili ya Bunge kurekebisha udhaifu huu.”

“Sifa muhimu kwenye haki siku zote ni kuwa na uwezo wa kuidai na hili litafanyika kikamilifu bila kujali vitisho vya kisheria au nguvu ya vyombo vya dola kwani Katiba tuliyonayo sasa imetoa haki kwa kila mtu kukutana na wenzake na kutoa maoni,” alisema na kuongeza:

“Watapaza sauti kwa njia wanayoona inafaa na pengine ikaleta machafuko nchini. Rais anapaswa kuzingatia hili.”

Alisema muswada huo umeacha mianya mingi inayoweza kutumiwa na watawala kufikia malengo na maslahi yao kama vile kutoweka wazi uwakilishi wa makundi mbalimbali, idadi ya wajumbe pamoja na uundwaji wa tume kukabidhiwa mikononi mwa Rais pekee.

Alisema muswada huo pia unampa Rais mamlaka kuipa tume hadidu rejea na ripoti kuwasilishwa kwake bila kuwepo fursa ya umma kuhoji hata uteuzi na uadilifu wa wajumbe.

Wakichangia mjadala huo, wengi wa washiriki walielezea upungufu wa sheria katika ugawaji na umilikaji wa ardhi maeneo ya vijijini na kutaka Katiba Mpya ianishe ushiriki wao.

Walisema wananchi wamekuwa wakiondolewa kwenye maeneo yao kuwapisha wawekezaji ambao baadhi yao hawafiki hata kwenye uongozi wa Serikali za Mitaa kujitambulisha kwa madai kuwa wamepewa ardhi hizo na mamlaka za juu.

Mkazi wa Kijiji cha Endulen, Ngorongoro, Noolosho Nakuta alieleza kushangazwa na kitendo cha Serikali kutotambua uwepo wao ndani ya eneo la Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa kuwanyima hata maeneo ya kujenga miradi ya kijamii kama zahanati na shule.
Alisema wakati wananchi wanabanwa katika hilo, wawekezaji wanapewa vibali vya kujenga majengo makubwa kama hoteli.

Bunge: Muswada wa Katiba unaweza kufutwa, kubadilishwa


OFISI ya Bunge imesema kuna uwezekano wa kubadilishwa au kufutwa kabisa kwa Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Katiba wa mwaka 2011, endapo itaonekana kuna sababu za msingi.Hayo yamebainishwa katika taarifa kwa umma iliyotolewa jana na Idara ya Habari, Elimu kwa Umma na Ushirikiano wa Kimataifa ya Ofisi ya Bunge.

“Muswada huo, ambao Bunge liliupitishwa baada ya kuusoma kwa mara ya tatu, ambao unasubiri kuwa sheria baada ya Rais kutia saini na kuwa sheria utaendelea kusimamiwa na kutekelezwa kama sheria nyingine yoyote ambayo utekelezwaji wake unaweza kusababisha mtizamo tofauti na hivyo kupelekea kufanyiwa marekebisho endapo itaonekana kuwa ipo sababu ya kufanya hivyo na mbunge yeyote, kamati au Serikali,” ilisema taarifa hiyo na kuongeza:

“Kwa hiyo endapo sababu zitaonekana kuwa za msingi, basi  kubadilishwa au kufutwa wote na Bunge. Kwa hiyo kwa taratibu za uendeshaji, Bunge haikuwepo sababu ya msingi kuzuia muswada huo usisomwe kwa mara ya pili na pia hapakuwa na kanuni zozote, zilizozuia usisomwe kwa mara ya pili kwa kuwa ulikidhi mahitaji yote kikanuni.”

Ilisema baada ya kusomwa kwa mara ya kwanza Bungeni, wananchi hupata fursa ya kushiriki kutunga sheria ama kwa kushiriki wao wenyewe kutoa maoni au kupitia wabunge ambao ndiyo wawakilishi wao.

“Wakati wa kujadili muswada huu mara baada ya kusomwa kwa mara ya pili na kabla haujasomwa kwa mara ya tatu, wabunge walikuwa na nafasi ya kuwasilisha mawazo yao kwa kuchangia,” ilieleza taarifa hiyo.

Imeeleza kuwa baadhi ya wabunge walitekeleza demokrasia hiyo kwa kuwasilisha mapendekezo yao pamoja na jedwali la mabadiliko.

Taarifa hiyo ya Bunge ambayo imekuja huku kukiwa na shinikizo kubwa kutoka kwa baadhi ya wanasiasa wakiongozwa na chama kikuu cha upinzani cha Chadema na na wanaharakati chini ya Jukwaa la Katiba, ilifafanua kuwa muswada huo ulilenga kuweka chombo ambacho kitafanya kazi ya kuchukua maoni ya wananchi ili kuyapeleka katika Bunge la Katiba ambalo litakuwa na nafasi ya uwakilishi wa kila mtu katika jamii.

Pia imesema muswada huo ni kama mingine iliyopitishwa na Bunge na unaweka utaratibu wa kuwafikia wananchi, kuwasikiliza na kupata utashi wao juu ya mapendekezo ya kuandika Katiba Mpya ili kila Mtanzania aweze kushirikishwa.

“Lakini muswada wenyewe hauhitaji ushiriki wa moja kwa moja wa wananchi isipokuwa kupitia kwa wawakilishi wao; wabunge, walipitisha kwa kauli moja kuwa Sheria na siyo Katiba kama inavyoelezwa na baadhi ya wadau.”

“Bunge limeuchambua Muswada wa Sheria na kuupitisha kuwa sheria na siyo muswada wa kubadilisha katiba. Katiba sasa haitobadilishwa, bali itaandikwa upya na Serikali iliyopo madarakani kwa sasa na Bunge lake.”

CCM: Mbio za urais, makundi vinatutesa


CHASEMA KUJIVUA GAMBA,VITA YA UFISADI VIKO PALEPALE
Neville Meena na Habel Chidawali, Dodoma
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kwa mara ya kwanza kimekiri hadharani kuwa mbio za Urais wa mwaka 2015 ni miongoni mwa mambo yanayokitikisa na sasa kinachukua hatua za kuwadhibiti makada wake wenye nia hiyo ili harakati zake zisikiathiri.Kadhalika, CCM kimesema dhana ya kujivua gamba kiliyoiasisi iko palepale na kwamba utekelezaji wake unaanza mara moja kwa kuwachukulia hatua wanachama wake wote wanaotuhumiwa kwa rushwa na ufisadi.

Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama aliwaambia waandishi wa habari jana Mjini Dodoma kuwa si vibaya makada wa chama hicho kuanza kufikiria urais wa 2015 lakini tatizo ni njia ambazo zinatumika katika harakati hizo.

“Sisi hatuna shida na watu hao kwa kuwa ni haki yao, lakini lazima watumie njia sahihi ambazo hazitaleta shida kwa chama na tumeona iko haja ya kutengeneza mfumo mzuri wa kupata mgombea urais ambaye hatatokana na fedha isipokuwa akubalike kwa uwezo wake wa kujenga hoja, itikadi yake na kile anachokiamini,” alisema Mukama.

Mukama alikiri kuwa mbali na mbio za urais 2015, pia CCM kinateswa na siasa za makundi ambayo yamekuwa yakitumika kushambuliana, kinyume cha maadili yake.

Alisema CCM kinachukua hatua za kukabiliana na makundi ambayo misingi yake hujengwa katika chaguzi za ndani ya chama, na kwamba watahakikisha hilo halitokei wakati wa uchaguzi wake unaotarajiwa kufanyika mwakani.

“Kwa maneno ambayo tuliyatumia tulisema, hii kansa ya kupangana safu inaweka mtu ambaye hata sifa wala hana habari kabisa na matatizo ya wananchi, wala haumii lakini anapanga safu… lazima tuondokane na kansa hii ili tupate viongozi wanaojali na wanaohangaika na maisha ya wavuja jasho wa nchi hii,” alisema.

Kujivua gamba

Kuhusu suala la kujivua gamba, akimaanisha kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa wa makosa mbalimbali ukiwemo ufisadi na rushwa, Katibu Mkuu huyo alisema kati ya maazimio 26 yaliyotolewa na NEC Aprili mwaka huu, Azimio namba 27 “linahitaji kutekelezwa haraka iwezekanavyo.”

“Dhana hiyo ya kukipatia chama chetu sura mpya ndiyo iliyopewa jina la kujivua gamba na Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa imekwishatengeneza mpango wa utekelezaji wa uamuzi huo,’’ alisema Mukama.

Alisema katika kikao chake kilichomalizika juzi, NEC imeamua kuwa viongozi wa CCM wanaotuhumiwa kwa ufisadi ndani ya chama walipaswa kujipima na kujitafakari wenyewe na ikibidi wachukue hatua jambo ambalo halijatekelezwa hadi sasa.

Alisema Azimio hilo liliwalenga viongozi katika ngazi zote za chama kuanzia taifa hadi tawi na kilichokusudiwa ni kujenga utamaduni wa kusimamia maadili ya viongozi na wanachama wake.

“Takriban miezi saba baada ya Azimio hilo kupitishwa, bado hatujapata mwitikio wa kuridhisha kutoka kwa viongozi wa ngazi yoyote wa chama chetu ambao ni walengwa wa azimio,’’ alisema na kuongeza:

“Bila shaka sasa wakati umefika wa chama kutekeleza ile sehemu ya pili ya azimio husika kwa kuwawajibisha wahusika, lakini utekelezaji wake hauna budi ufanyike kwa kufuata utaratibu uliowekwa ndani na kanuni za CCM za uongozi na maadili.’’

Msingi wa mpango wa kujivua gamba umejengwa katika azimio la NEC linalosema: “Viongozi wanaotuhumiwa kwa ufisadi watafakari, wajipime na kuchukua hatua wao wenyewe kwa maslahi ya chama, wasipofanya hivyo, chama kiwawajibishe bila kuchelewa.”

Lakini tangu kupitishwa kwa mpango huo Aprili mwaka huu, ni kada mmoja tu, Rostam Aziz aliyechukua hatua za kujiuzulu Ubunge wa Jimbo la Igunga na Ujumbe wa NEC huku wengine wakiwa kimya.

Mukama alisema sehemu ya pili ya azimio hilo inayosema: “Wasipofanya hivyo chama kiwawajibishe bila kuchelewa,” ndiyo msingi wa NEC kurejesha suala hilo kwa Kamati Kuu na kwamba sasa litafanyika katika ngazi zote.
Alisema NEC imeziagiza kamati za siasa kupitia kamati za ulinzi usalama na maadili kwa ngazi zote kuanza mara moja, mchakato wa kutekeleza azimio hilo kwa mujibu wa kanuni na taratibu za chama.

Alisema NEC iliagiza kazi hiyo kufanyika haraka bila kuchelewa na baada ya kukamilika kwa kazi hiyo, taarifa zipelekwe kwenye vikao vya kikatiba vya uamuzi kwa hatua za utekelezaji.

Alisema chama hicho kitahakikisha kwamba ajenda hiyo haitekwi na makundi yanayokinzana na kwamba lengo zima ni kuhakikisha kwamba CCM kinaongeza uwezo wa kusimamia mambo yake na Serikali zake zote.

“Lazima kifike mahali (CCM), kiwe na uwezo wa kuzisimamia na kuhakikisha kwamba Serikali zinatekeleza matakwa ya wananchi na siyo vinginevyo, ndiyo maana watu wanajiunga na vyama kwani huwa wanatarajia watapata utetezi,” alisema Mukama.

Kuhusu vurugu na migomo ya vyuo vikuu CCM kiliagiza Serikali kuchukua hatua za haraka kukabiliana na hali hiyo na kuitaka kusimamia sheria inayokataza uendeshaji wa shughuli za kisiasa katika taasisi za elimu nchini. Kimetaka wanafunzi na watumishi wabanwe ili waendeshe shughuli hizo nje ya taasisi husika.

Kuhusu suala la Nishati nchini, Mukama alisema NEC imeiagiza Serikali kuhakikisha kuwa inapunguza bei za mafuta na hasa ya taa ambayo yanatumiwa na wananchi wengi wenye kipato cha chini.

Juzi, Mawaziri Wakuu wa zamani, Edward Lowassa na Frederick Sumaye, waliwashambulia kwa maneno makali wajumbe wawili wa Sekretarieti ya CCM kwamba wamekuwa wakikivuruga chama na kusababisha mgawanyiko uliopo kwa jinsi ambavyo wamekuwa wakisimamia mpango wa kujivua gamba.

Lowassa aliyejiuzulu Uwaziri Mkuu, kutokana na kashfa ya Richmond ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzungumzia suala hilo wakati wa mjadala wa hali ya siasa, pale alipowataja Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Tanzania Bara, John Chiligati kwamba wamekuwa wakitukana watu ovyo kwa fedha wanazopewa na CCM.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Lowassa alitumia zaidi ya dakika saba kumshambulia Nape kwamba amekuwa akifanya mambo nje ya utaratibu na kwamba mwenendo huo umekuwa ukikibomoa chama badala ya kukijenga.

Sumaye alisimama na kuhoji sababu za chama hicho kunyamazia ukiukwaji wa taratibu ambao umekuwa ukifanywa na watendaji hao.

Thursday, November 24, 2011

SMZ yaahidi uhuru wa habari

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imesema itahakikisha inafungua milango zaidi ya uhuru wa vyombo vya habari kwa ajili ya wananchi kupata taarifa mbalimbali kwa mujibu wa Katiba.

Hayo yalisemwa na Makamu wa Kwanza wa Rais, Maalim Seif Sharif Hamad wakati wa sherehe
za kukabidhiwa leseni ya matangazo kwa kituo cha StarTimes cha China visiwani hapa.

Maalim Seif alisema Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, inatambua kuwepo kwa umuhimu wa
kila raia wa Zanzibar kupata taarifa mbalimbali za habari ndani na nje ya nchi kwa lengo la kukidhi matakwa ya Katiba.

“Kwa ajili ya kukidhi matakwa ya Katiba, ndiyo maana tumeamua kufungua milango na
kuzikaribisha kampuni mbalimbali za nje na ndani ya nchi kuwekeza Zanzibar katika sekta ya mtandao wa kisasa wa mawasiliano,” alisema Makamu wa Kwanza wa Rais.

Hata hivyo, alisisitiza na kutoa tahadhari kwamba kampuni zote zitakazokuja kuwekeza katika sekta ya habari ya mawasiliano, zinatakiwa kwanza kuzingatia maadili na utamaduni wa
wananchi wa Zanzibar.

Alisema Serikali haitakubali kuona utamaduni na silka za wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba unapotoshwa kwa kisingizio cha uhuru wa vyombo vya habari pamoja na utandawazi wa teknolojia ya mawasiliano.

“Hayo ndiyo masharti yetu makubwa katika uwekezaji wa sekta ya habari na mawasiliano nchini... utamaduni lazima uzingatiwe na kulindwa kwa nguvu zote kwani ndiyo utambulisho wa wananchi wa Zanzibar,” alisema.

Kampuni ya StarTimes kutoka China imepewa leseni ya kuendesha shughuli za televisheni Zanzibar na kuwa kampuni ya kwanza ya kigeni kupata fursa hizo.

Kampuni hiyo imepewa leseni ambayo itaiwezesha kuwekeza katika mitambo ambayo hatimaye itagawa mawimbi kwa kampuni za redio na televisheni nchini.

Amazon, Halong Bay, Iguazu Falls among new 7 natural wonders

Amazon, Halong Bay, Iguazu Falls among new 7 natural wonders
A GLOBAL poll has named the world's new seven wonders of nature, with Vietnam's Halong Bay and South Korea's Jeju Island among the initial list of winners. Organised by Swiss foundation New7Wonders, the poll saw an initial list of 440 nominees trimmed down to 28 finalists, who were put through a final phase of worldwide voting. The provisional results, which will be confirmed in early 2012, were announced on Nov 11. We present, in photos, the list of seven winners and the 21 other finalists:

Merc-driving man seen dumping cat into bin


Footage from closed-circuit television (CCTV) security cameras showing a man dumping a cat into a rubbish bin has raised concern among outraged netizens and the Society for the Prevention of Cruelty to Animals (SPCA).
The video was posted on YouTube and citizen journalism website Stomp on Tuesday by Miss Chee Siew Luan, reported The Straits Times.
The SPCA is appealing for more information on the video and netizens have commented on their Facebook page after it posted the appeal yesterday morning.
Miss Chee is an administrative assistant at the James Tan Veterinary Centre in Whitley Road and the bin is located on the premises of the veterinary centre.
Miss Chee, 26, told The Straits Times that a staff member discovered the cat in the bin at about 2pm on Tuesday.
After tracing back events on the CCTV, they saw a man emptying something into the bin from a cat carrier at 9.47am. She added that the cat had a collar but no tag or microchip.
In the 45-second video, a man wearing a striped shirt is seen getting out of a silver Mercedes-Benz, holding a cat carrier.
A young girl, who looks about four years old, is seen accompanying the man.
He walks towards the bin, opens the lid, fidgets with the door of the cat carrier and tips something in - presumably the cat, as it is not clear from the video.
No one had opened the bin since that time.
Miss Chee said it appeared that the cat had been trying to jump out of the bin for hours as "the bin moved slightly, many times".
A spokesman for the SPCA said it had also made a police report.
"We're hoping that more information will come to pass,' she said. 'Let's leave this in the hands of the police", said the spokesman to The Straits Times.
The cat is between one and three years old, and is a male tabby which has been sterilised.
It is currently being taken care of by vets at the centre but staff say it is in shock and has not eaten since it was discovered.

Yishun murders: Quarrel over crabs sparks off killing spree



At the second day of a murder trial involving the deaths of three Chinese nationals in Yishun, accused Wang Zhijian revealed that a quarrel over money for crabs sparked off the slashing frenzy.

The prosecution yesterday read out what Wang had told the police in the immediate hours and days after the incident which happened at a Block 349, Yishun Avenue 11.

Wang is accused of killing Zhang Men, 42, her daughter Feng Jianyu, 17, and their flatmate, Madam Yang Jie, 36. Madam Yang's daughter, Li Meilin, now 18, survived despite being slashed repeatedly.

According to local media reports, Wang told the police that his girlfriend, Madam Zhang had approached him on the night of September 18, 2008 and asked him how much money he had with him.

When Wang, 45, asked her why she wanted the money, Madam Zhang, 42, said she wanted to eat crabs.

He said that they should save the money instead of spending it on crabs, especially since she had eaten the dish just a few days before.

She then called him a pauper, the court heard.

The New Paper reported that he told her to spend her own money. Madam Zhang retorted that it was only right that she spent his money.

This sparked off a quarrel in which she used vulgarities on him and humiliated him by calling him a poor fellow and that he was produced by dogs and donkey.

She spends 73 cents to get 10-cent refund


By Joyce Lim
She has been overcharged for her bus rides more than five times this year alone.
Each time, Miss Lee Hwee Teng, 39, made a claim, even though the amount could be as little as 10 cents.
She would do this even if she had to take a bus - and pay a fare costing more than the claim amount - to a bank to deposit the refund cheques.
This is because she does not have a bank account with DBS or POSB, the banks to which TransitLink can credit the refunds.
Just last week, on Nov 17, Miss Lee received yet another cheque, refunding her the extra 10 cents that was deducted from her Cepas (Contactless ePurse Application Standard) card on Nov 8.
Miss Lee, who is self-employed in the biotechology sector, submitted this latest claim - her fifth - through TransitLink's website and received her cheque refund within a week.
The first 10-cent cheque that she received from TransitLink after she was overcharged.
WHY BOTHER?
Although the cheques were mailed to her home in Yishun Street 61, Miss Lee had to take a bus to the OCBC bank branch in either Yishun or Ang Mo Kio Town Central, the nearest branches to her home, to deposit them.
She said: "It would cost 73 cents for me to take a bus from home to Yishun Central."
So why go through all that trouble?
Said Miss Lee: "It is a matter of principle...
"Most people I know wouldn't bother to get a 10-cent refund. I have shared my experience with my friends, but they told me that it's only 10 cents and asked me to forget it.
"But just imagine a whole busload of people being overcharged 10 cents for the ride."

Woman cheated at Sim Lim Square


Lianhe Wanbao



A woman says she was cheated when she tried to buy a mobile phone at Sim Lim Square.

On 9 November, Mdm Kun Tong (age 60s), a Thai Chinese tourist, went to an electronics shop in Sim Lim Square to look at the iPhone 4S mobile phone.

She described what happened, "The shop assistant demonstrated the functions of the iPhone 4S to me. I was happy with it and asked him the price. He quoted $1,490 but I felt it was too expensive and quoted him $1,200 instead."

After the shop assistant accepted the price, Mdm Kun Tong handed the man her passport to help her process the Goods and Services Tax (GST) exemption for the purchase.

While waiting, her husband suggested that she check her purchase. It was then that she found she was given a Samsung phone instead of the iPhone 4S.

Mdm Kun Tong immediately asked for a refund but the shop assistant refused and instead challenged her to bring him to court.

She called the police immediately, but police officers could do nothing to help her.

The shop assistant had apparently copied her details onto a receipt for a Samsung phone and insisted that she was purchasing the Samsung phone for $1,200.

Mdm Kun Tong shops in Singapore several times a year and often visits electronics shops in Sim Lim Square and Pearl's Centre in Chinatown.

She is outraged at the shop's claim and has made a complaint to the Consumers Association of Singapore (CASE).

With the help of CASE, the shop eventually agreed to give her a refund, but insists on charging her $120 for a Goods and Service Tax (GST) processing fee.

Mdm Kun Tong refuses to pay the fee.

"The transaction did not go through, why should I pay a processing fee to them?" she asked, "They are trying to cheat me!"

She will also be writing to the Singapore Tourism Board and the Thai Embassy about the shop's unethical practices.

MAMA SALMA KIKWETE AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA KUNAWA MIKONO DUNIANI



Baadhi ya watoto pamoja na wanafunzi wa shule mbalimbali za mkoa wa Dar es salaam wakipita mbele ya mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya kunawa mikono duniani  leo. Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mama Salma Kikwete (hayupo pichani) ndiye aliyekuwa mgeni kwenye sherehe hizo katika viwanja vya Karimjee jijini Dar leo
  
 Watoto wakicheza ngoma ya msewe ya Zanzibar
 Wasanii wa Kikundi cha Orijino Comedy kikionyesha zoezi la kunawa mikono wakati wa maadhimisho ya siku ya kunawa mikono duniani lililofanyika leo  jijini Dar es salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA Mama Salma Kikwete hayupo pichani
 Mama Salma Kikwete akiwaonyesha watoto zoezi la jinsi ya kunawa mikono kwa sabuni wakati wa maadhimisho ya siku ya kunawa mikono duniani 
 Sehemu ya tukio lilifanyika sherehe ya maadhimisho ya siku ya kunawa mikono duniani 
 Baadhi ya watoto wa shule za msingi jijini Dar es Salaam wakiangalia aina ya kibuyu chirizi ambacho hutumika kuweka maji kwaajili ya kuoshea mikono.
Watoto wakitoa burudani.
Picha na Mwanakombo Jumaa – MAELEZO