Wednesday, March 21, 2012

Kanisa Katoliki lamshukia Wassira kuhusu Dk Slaa


LASEMA KAMA ANAO USHAHIDI WA WIZI WA FEDHA ZA PAPA AUTOE, WANASIASA WANAOCHAFUA WENZAO WAMEFILISIKA, NEC YAVIONYA CCM, CHADEMA
Na Waandishi Wetu
KANISA Katoliki nchini limemtaka Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano wa Jamii), Stephen Wassira kutoa ushahidi kuthibitisha kama Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa alifukuzwa upadre baada ya kuiba fedha za ujio wa Papa John Paul II, alipokuja nchini mwaka 1991.Akizungumza kwa simu jana, Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (Tec), Yuda Thadeus Ruwaichi alimtaka Wassira athibitishe tuhuma zake akisema kanisa hilo halijawahi kumtuhumu  Dk Slaa kwa tuhuma za wizi.

Akizungumza katika kampeni za CCM Jimbo la Arumeru Machi 19, mwaka huu, Wassira alimtupia kombora Dk Slaa akidai si mwaminifu kwa kuwa alifukuzwa ukasisi wa kanisa hilo baada ya kufanya ufisadi kwenye fedha za mapokezi ya Papa huyo ambaye sasa ni marehemu.

Hata hivyo, Wassira jana alipotakiwa kuzungumzia kauli hiyo ya Askofu Ruwaichi alijibu kwa kifupi: “Mimi nilishazungumza na yakaandikwa kwenye vyombo vya habari, hii leo siyo habari.”
Ruwaichi ambaye pia ni Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Mwanza alisema madai hayo ya Wassira hayana msingi.

“Kanisa halijawahi kumshutumu Dk Slaa kuhusu madai hayo (ya Wassira). Kama Wassira ameyatoa kwenye mkutano wa hadhara, njia sahihi ya kupata ukweli ni yeye kutupa ushahidi wa vielelezo kuthibitisha madai yake,” alisema Ruwaichi.

Askofu Ruwaichi amewaonya wanasiasa wanaofanya kampeni za kuchafuana akiwataka waache na waanze kufanya siasa za kistaarabu.

“Ukiona mwanasiasa anakurupuka na kuanza kumchafua mwenzake ujue amefilisika, vitendo hivyo vinaonyesha udhaifu kwa nchi katika nyanja za siasa,” alisema.

Askofu Ruwaichi alisema wanasiasa waliokomaa hawapaswi kufanya kampeni za kuchafuana... “Watajishughulisha katika kujadili hoja zinazozingatia mahitaji ya jamii. Kitendo cha wanasiasa wetu kufanya kampeni za kuchafuana kinaonyesha dhahiri kuwa bado tuko dhaifu katika siasa na hatuna vipaumbele.”

Askofu Ruwaichi aliwataka wanasiasa hao kuachana na kampeni chafu na badala yake wajikite katika kujadili hoja zinazotoa vipaumbele katika matatizo yanayoikabili jamii na namna ya kuyatatua ili kuwawezesha wananchi kuchagua viongozi bora.

Kauli hiyo ya Askofu Ruwaichi, imekuja siku chache baada ya Dk Slaa kuzungumza katika mkutano wa hadhara kwenye kampeni za uchaguzi mdogo Jimbo la Arumeru na kusema Wassira ni mwongo na hajui asemalo.

“Kama tangu mwaka 1991 nipo, basi kitendo cha Serikali kushindwa kunifungulia mashtaka ya wizi wa hizo fedha basi ni Serikali dhaifu na ijiuzulu,” alisema Dk Slaa.

NEC yavionya CCM, Chadema

Katika hatua nyingine, Kamati ya Maadili ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), imeonya vyama vya CCM na Chadema kuacha kampeni chafu baada ya kuthibitika kuwa vimekiuka sheria na maadili ya uchaguzi kutokana na vitendo vya uvunjifu wa amani ambavyo vinafanywa na wafuasi wao.

Msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo, Trasias Kagenzi akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema vyama hivyo vimeandikiwa barua hizo baada ya kukamilika kwa kikao cha kamati ya maadili ambacho kilipokea barua za malalamiko matano kuhusu mwenendo usioridhisha katika kampeni.

Kagenzi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, alisema CCM kimepewa barua ya onyo kutokana kitendo cha wafuasi wake kuchana picha na mgombea wa ubunge wa Chadema, Joshua Nassari siku ya uzinduzi wa kampeni zake katika Uwanja wa Ngaresero.

Mwenyekiti huyo alisema Chadema nacho kimepewa onyo kutokana na wafuasi wake kuwakashifu viongozi wa CCM katika eneo la Meru Garden ambako viongozi hao na mgombea wao, Sioi Sumari walisimama kupata chakula.

Alisema malalamiko yaliyojadiliwa ni ya Chadema na CCM na kwamba vyama hivyo viwili vinatuhumiana kwa ukiukwaji wa sheria na maadili ya uchaguzi.

Alisema Chadema katika barua yao ya Machi 12 mwaka huu, kililalamikia wafuasi wa CCM kung’oa picha za mgombea wao wakati wa uzinduzi wa kampeni zao ambazo zilikuwa zimebandikwa katika kontena lilipo jirani na uwanja kulipozinduliwa kampeni.

Alisema malalamiko mengine ya Chadema yaliwasilishwa Machi 14, mwaka huu kuhusu kukashifiwa kwa mgombea wao na CCM kwa matusi mbalimbali na Machi 19 walilalamika kutekwa kwa Mwenyekiti wao wa Kitongoji cha Magadirisho, Nuru Maeda na wafuasi wa CCM na kupigwa.

Kwa upande wa CCM, Kagenzi alisema kiliwasilisha barua ya malalamiko kwamba Machi 12 wafuasi wa Chadema walikaa njia panda kutoka eneo palipofanyika uzinduzi wa kampeni za CCM na kuanza kuwazomea viongozi wa chama hicho na kung’oa bendera za chama hicho kwenye magari na kuonyesha alama ya vidole viwili inayotumiwa na Chadema.

Alisema pia Machi 18 wafuasi wa Chadema waliufanyia vurugu
msafara wa mgombea ubunge wa CCM, katika eneo la Meru Garden na kushambulia magari kwa mawe na gari moja la CCM lilivunjwa vioo.

Kagenzi alisema ni busara vyama vyenye wagombea katika
uchaguzi huo kufanya kampeni kwa kunadi sera za kutoa ahadi wagombea wao wakichaguliwa watafanya nini, badala ya kutoa matusi wakati wote na kashfa dhidi ya wengine.

Pia amepiga marufuku machapisho yote kusambazwa katika jimbo hilo bila ridhaa yake... “Napenda kukumbusha kuwa ni marufuku kwa chama au mtu kusambaza machapisho katika kampeni bila kuwasilisha chapisho hilo ofisi yake ili yaidhinishwe.”

Tamko hilo limekuja wakati Chadema wakiwa wanalalamikia kusambazwa kwa nyaraka za uchochezi na kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Dk Slaa wamekuwa wakilalamikia polisi kusambaza vipeperushi kwenye mikutano yake ambavyo alisema vinalenga kuwatisha raia.

CCM wamgomea msimamizi
Akizungumza na gazeti Dada la The Citizen jana, Mratibu wa Kampeni wa CCM, Mwigulu Nchemba alisema chama chake hakiwezi kuacha kujibu mapigo ya Chadema na kuongeza kuwa kitaacha kufanya hivyo endapo Tume ya Taifa ya Uchaguzi itakiandikia Chadema kukanusha kashfa kilizozitoa dhidi ya mgombea wa CCM Sioi.

“Tunachokifanya sisi ni kuwaeleza wananchi ukweli dhidi ya wapinzani wetu hatutukani watu hapa… hatuwezi kubadili staili hii ya kampeni mpaka tume iwaambie Chadema wafute matusi hadharani dhidi ya mgombea wetu,” alisema Nchemba.

Alisema tume inatakiwa kutenda haki kwa vyama vyote huku pia akiwataka wapinzani kutolia katika harakati za mashambulizi ambazo wamezianzisha wenyewe.

Meneja wa Kampeni wa Chadema, Vincent Nyerere alisema chama chake hakijapokea barua yoyote kutoka tume huku akionya kwamba hata kama kutakuwa na barua hiyo, basi walengwa wake ni CCM na siyo chama chake.

Alisema amekuwa mmoja kati ya watu waliokashifiwa na viongozi wa CCM huku akiitaka Tume kuacha upendeleo na badala yake itoe adhabu stahiki kwa chama hicho tawala.

“Hebu tuwaache Sioi na Nassari wapambane katika majukwaa na sio mzee Wassira, Mkapa na Ole Sendeka kutushambulia badala ya kutangaza sera za chama chao, sisi tunaendelea na kampeni za kistaarabu,” alisema Nyerere.
Habari hii imeandikwa na Geofrey Nyang'oro Dar, Neville Meena na Mussa Juma, Arumeru.

Tuesday, March 20, 2012

Kisa na Mkasa na Salim Kikeke

Mwizi na 'haja'

DNA
Teknolojia ya DNA
Mwizi mmoja nchini Uchina aliyekuwa na tabia ya kujisaidia haja kubwa katika nyumba anazofanywa wizi wake, hatimaye amekamatwa kutokana na teknolojia ya DNA.
Polisi jijini Cixi, katika jimbo la Zhejiang wamesema mwizi huyo aitwaye Chen mwenye umri wa miaka 29 akiwa na mwenzake walivunja nyumba moja na kuingia jikoni na kula chakula, kabla ya bwana Chen kujisaidia kwenye sakafu karibu na mlango.
Baada ya kufanya hayo, wawili hao wakaanza kutafuta vitu vya kuiba ndani ya nyumba hiyo, lakini kutokana na kukuru kakara zao, mwenye nyumba alishtuka, na wezi hao kukimbia bila ya kuiba chochote. Miezi michache baadaye, wezi hao waliingia katika nyumba nyingine na kuiba kompyuta mpakato-- yaani Laptop na fedha taslimu yuan elfu moja.
Kama kawaida, waliingia jikoni na kujipakulia chakula, na bwana chen kuacha muhuri wake wa kawaida, wa kinyesi chenye harufu kali karibu na mlango wa mbele. Mtandao wa china daily umesema polisi walifanikiwa kulinganisha vipimo vya DNA na mwizi Chen, ambaye aliwahi kutupwa gerezani kwa kosa jingine mwaka 2003. Baada ya kukamatwa, bwana Chen alikiri kujisaidia katika nyumba anazofanya wizi, akisema, amekuwa akisoma katika vitabu mbalimbali jinsi wezi wanayokuwa na mitindo yao ya kipekee, wanapofanya wizi. Polisi bado wanamsaka mwizi mwenzake.

Mwizi arejesha alichoiba

Zawadi
Zawadi za Krismasi

Bwana mmoja aliyeiba zawadi za Krismasi katika nyumba moja nchini Marekani, amerejesha zawadi zote, na kuandika ujumbe wa kuomba radhi. Mike Valloney aliyeibiwa zawadi hizo amesema camera zake zilimrekodi mwizi huyo akiiba. "Alikuwa akitazama huku na huko, akihisi kama kuna mtu anamtazama" amesema bwana Mike.
Hata hivyo kituo cha televisheni cha WPIX kimesema siku mbili baada ya kuiba zawadi hizo, mwizi huyo alirejea tena, na kurudisha kila alichoiba.
Aidha, mwizi huyo pia aliandika ujumbe usemao " Naomba radhi. Heri ya mwaka mpya. Nataka kufanya mambo mazuri mwaka huu" umesema ujumbe huo. Bwana Valloney aliyeibiwa amesema hadhani kama mwizi huyo ataiba tena.

Aiba na kumuuzia aliyemuibia

iPhone
iPhone kama hii

Polisi mjini Florida Marekani wamesema wamemkamata mwizi mmoja aliyejaribu kumuuzia vitu mtu aliyemuibia vitu hivyo.
Polisi katika kiunga cha Miramar, Florida wamesema mwizi huyo baada ya kuiba simu aina ya iPhone na tabiti aina ya iPad, alimpigia alyemuibia siku mbili baadaye akitaka kumuuzia vifaa hivyo hivyo alivyomuibia.
Polisi wa Miramar wamesema bwana Hank Yan aliyeibiwa siku ya Jumatatu, alishikiwa bunduki na watu wawili waliompora simu na tabiti pamoja na dola mia tano taslimu, limeripoti gazeti la South Florida Sentinel. Polisi wamesema bwana Yan alipokea simu siku mbili baada ya kuibuiwa na alitambua sauti ya mtu anayetaka kumuuzia iPad, na hivyo kupanga kukutana naye. Wezi hao, Zachari Swindle na Devonte Suckie walikamatwa na polsi walipojitokeza katika mahala walipokubaliana na mteja wao.

Bibi na bangi

Bangi
Miche kadhaa
Mwanamama mmoja mwenye umri wa miaka sitini na saba nchini Marekani, ameachiliwa huru na mahakama baada ya kushtakiwa kwa kosa la kupanda miche ya bangi katika bustani yake.
Makachero wa polisi wamesema walikuta miche saba yenye afya na yenye urefu wa futi nne katika bustani ya mwanamama huyo mjini Uniontown, Philadelphia. Mama huyo aitwaye Alberta Kelly amesema yeye alirusha mbegu tu kwenye bustani yake baada ya kupewa mbegu hizo na mtu mmoja mwenye madevu lakini asiyemfahamu.
Bi Kelly amesema wala hakufahamu kama ni bangi, na mtu aliyempa mbegu hizo alimwambia ni mbegu za maua. Bi Kelly alikiambia kituo cha Televisheni cha WTAE kuwa majani ni majani tu.

Hujui Beyonce kaolewa na Jay Z?

Beyonce
Beyonce kaolewa na Jay Z
Polisi mjini Parma, Ohio, nchini Marekani wamesema mtu mmoja amechomwa kisu kwa sababu tu hakuwa akifahamu kwamba mwamamuziki Beyonce ameolewa na msanii Jay Z.
Kachero wa polisi Marty Compton wa kituo cha polisi cha Parma amesema mtu mmoja aitwaye Garfield Heights siku ya mwaka mpya alikuwa akibishana na Ronald Deaver, baada ya bwana Deaver kugundua kuwa Bwana Garfield hafahamu kuwa wanamuziki hao mashuhuri wa Marekani ni wanandoa, kimeripoti kituo cha TV cha WJW, siku ya Alhamisi.
Kachero Compton amesema Bwana Deaver alimchoma kisu bwana Garfield nje tu ya nyumba yake majira ya saa tano usiku saa za huko. Bwana huyo aliyechomwa kisu imeripotiwa anaendelea vizuri katika hospitali ya Metro mjini humo alipolazwa.
Bwana Deaver alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa la kushambulia.
-----------------------
Na kwa Taarifa yako...
Watu huzungumza takriban maneno mia moja na ishirini kwa dakika moja.
--------------------
Tukutane Wiki Ijayo... Panapo Majaaliwa....

Wamisri wamuaga papa Shenouda

 Idadi kubwa ya watu wamejumuika mjini Cairo katika mazishi ya Papa Shenouda wa Tatu wa Kanisa la Coptic.
Papa Shenouda alifariki Jumamosi akiwa na umri wa miaka themanini na minane.
Viongozi wa kijeshi nchini Misri wametangaza siku ya maombolezi ya kitaifa kwa heshima ya papa huyo aliyeongoza waumini wa Copti kwa zaidi ya miongo minne.
Baada ya misa mwili wa papa utasafirishwa na kuzikwa katika makao ya watawa eneo la Nile Delta.
Papa huyo alikuwa kiongozi wa kidini wa waumini hao ambao ni asilimia kumi ya idadi yote ya watu wa Misri na wamelalamika kutengwa sana nchini Misri katika miaka ya hivi karibuni.
Baada ya misa ya wafu , papa Shenouda atazikwa katika nyumba ya watawa ya St Bishoy monastery katika eneo la Nile Delta.
Wa Copti ndio jamii kubwa ya wakristo mashariki ya kati. Hii leo walipewa likizo kuweza kufanya maziko huku siku moja ya maomblozi ya kitaifa ikitangazwa.

A day in the life of a hotel test sleeper


A day in the life of a hotel test sleeper
IF SHE finds a strand of hair in a hotel bed - you'll be sure to hear of it.
Ms Zhuang has a dream job of a Hotel Test Sleeper, which involves sleeping in hotel beds to test them for quality ahead of your visit.
Many of us can be envious of Zhuang as she was selected as one of three final winners out of 7,800 candidates and started working for Qunar as a Professional Hotel Test Sleeper in March 2010.
To date, she has slept at more than 200 hotels.
"My job is to role-play travellers of different types, different ages and genders at different scenarios, and see how each hotel fits their particular needs." Zhuang said.
Her reviews help travellers make smart hotel picks and bring them a more pleasant experience on the road.
Qunar, a Chinese online travel platform, started to recruit Professional Hotel Test Sleepers in 2010.
The requirement for this new profession is to sleep at selected hotels without disclosing their real job and write expert reviews about the facilities, location, dining, services and prices of the hotels, in order to provide an independent third-party evaluation and an authoritative guide to travellers, according to the company.
[Photo: Ms Zhuang, a Hotel Test Sleeper, checks the texture of the toilet paper at a business chain hotel, in Beijing on March 6, 2012.]

Teenage brothels in Bangladesh hold dark steroid secret



TANGAIL, BANGLADESH - Their faces painted heavy with make-up, teenage girls in short, tight blouses and long petticoats loiter in squalid alleys, laughing and gesturing to potential clients who roam Tangail town's infamous red light area in the early evening.
There is no shortage of men looking for "company" in Kandapara slum, a labyrinth of tiny lanes - lined cheek-by-jowl with corrugated iron shacks - a few hours drive northeast of Bangladesh's capital, Dhaka.
But with rates as low as 50 taka (S$0.75), the need to attract as many customers as possible is desperate - prompting a rising, yet dangerous, trend of steroid abuse among adolescent sex workers to "enhance" their appearance.
"There is a huge difference between my appearance now and the malnourished look of my childhood," says Hashi, 17, who was lured into the sex trade by a trafficker when she was 10 and sold to Kandapara's brothel, where she began taking steroids.
"I am healthier than before and fit to serve a lot of customers in a day. Sometimes up to 15," she says, placing a large black bindi, or dot used by Hindu women, between her perfectly shaped eyebrows.
She sits in her tiny room with a bed, a cooking stove and posters of Bollywood stars taped across the wall.
Click on thumbnail to view (Photos: Reuters)

Dk Mwakyembe aweka hadharani ugonjwa wake


BAADA ya utata wa muda mrefu wa ama Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe amelishwa sumu au la, jana Mbunge huyo wa Kyela, aliweka hadharani ugonjwa wake akisema unafahamika kitaalamu kwa jina la Popular Scleroderma huku akisisitiza: “Sasa nimepona kabisa.”

Dk Mwakyembe amekuwa akisumbuliwa na maradhi ya ngozi ambayo mwaka jana yalizidi kumtikisa na Oktoba 9, Serikali iliamua kumpeleka Hospitali ya Appolo, India kwa ajili ya matibabu na uchunguzi zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, Dk Mwakyembe akiwa amevalia kofia ya pama alisema: “Si kwamba sijambo, bali nimepona kabisa baada ya kugundulika na maradhi hayo na kutibiwa.”

“Nimerudi juzi kutoka India na daktari wangu ameniambia nimepona, nilikuwa nasumbuliwa na maradhi ya ‘Popular Scleroderma’ iliyosababisha ‘skin disorder’ (ngozi kutokuwa katika hali ya kawaida), lakini kwa nguvu za Mungu nimepona, namshukuru Mungu.”

Kuhusu sumu
Alipoulizwa kuhusu tuhuma za kulishwa sumu, Dk Mwakyembe alikataa kuzungumzia hilo akisema anasubiri uchunguzi ulioagizwa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha.

Hata hivyo, Dk Mwakyembe alisema angependa kuona uchunguzi huo unakamilika haraka na ripoti yake inatangazwa kwa umma.

Alisema yuko tayari na anasubiri tume hiyo ya uchunguzi iliyoundwa na Waziri Nahodha imhoji ili atoa kile kilichomo katika ripoti ya daktari wake.

Dk Mwakyembe alisema anachoshukuru hadi sasa ni kwamba afya yake imeimarika kutokana na shinikizo la Rais Jakaya Kikwete ambaye aliagiza Serikali kumpa kipaumbele wakati wote akiwa nchini na India hatua ambayo imemwezesha kufika hapo alipo.

Kutokana na hali hiyo, Dk Mwakyembe aliwataka wananchi wote wakiwemo wa jimboni kwake Kyela kuondoa wasiwasi akisema sasa yupo imara kwa ajili ya ujenzi wa majukumu ya taifa.

“Ninaomba wapiga kura wangu wa Kyela waache jazba, wawe na subira juu ya matatizo yangu. Wiki ijayo nitakwenda kuzungumza nao ili niweze kuwaeleza matatizo yaliyokuwa yananisumbua, lakini sasa hivi niko fit,” alisema.

Mtaalamu auzungumzia
Mtaalamu wa afya ambaye hakutaka kutajwa gazetini alisema ugonjwa huo wa ‘Popular Scleroderma’ unasababishwa na chembechembe hai nyeupe kushambulia kitu kigeni kilichoingia kwenye mwili na kusababisha magonjwa ya ngozi.

Alisema chembechembe hizo zinaweza kusababisha ngozi ya mwili kuharibika... “Ni magonjwa yanayosababishwa na chembechembe hai nyeupe kujikataa zenyewe na kusababisha ugonjwa wa ngozi na mifupa.”
Kauli hiyo ya Dk Mwakyembe kuhusu ugonjwa wake imefungua ukurasa mpya hasa baada ya baadhi ya wanasiasa kuamini kuwa hakuwa na tatizo jingine bali, amelishwa sumu. Tayari Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba ambaye alitoa ripoti akisema Naibu Waziri huyo hakulishwa sumu kama inavyodaiwa, amefanyia uchunguzi madai hayo na kukabidhi jalada lake kwa Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma, DPP ili afungue kesi.

Kauli ya Sitta

Mmoja wa wanasiasa waliodai kuwa Dk Mwakyembe amelishwa sumu, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta alipoulizwa jana juu ya kauli hiyo mpya ya Dk Mwakyembe alisema hana cha kuzungumza.

Januari 28, mwaka huu akiwa kwenye uzinduzi wa Programu ya Neno la Hekima kutoka kwa Kiongozi iliyoanzishwa na Kanisa la Ufufuo na Uzima la Kawe, Dar es Salaam Sitta alisema Dk Mwakyembe amelishwa sumu.

Akizungumza kwa utaratibu, Sitta alisema hana mengi ya kuzungumza kuhusu ugonjwa unaomsumbua Dk Mwakyembe na kusisitiza kuwa isubiriwe ripoti kutoka India ambako alikuwa akitibiwa.

“Dk Mwakyembe si anatibiwa India?,” alihoji na kuendelea, “Nadhani umeshapata jibu, tusubiri… acha huko India waendelee na uchunguzi wao, siwezi kusema lolote zaidi ya hilo nililokuambia.”

Dk Mwakyembe alianza kuugua Oktoba 9, mwaka jana na alitibiwa Apollo hadi aliporejea Desemba 11, mwaka jana. Alirejea tena India kuendelea na matibabu hadi Ijumaa iliyopita aliporudi na kusema kuwa amepona.

Matatizo yake ya kiafya yamesababisha mvutano baina ya viongozi wa Serikali. Wakati Manumba akisema ripoti kutoka Wizara ya Afya ilionyesha hakupewa sumu, waziri mwenye dhamana na afya Dk Haji Mponda alimkana.

Pia Waziri Nahodha ambaye ana dhamana na jeshi hilo la polisi, alikana ripoti hiyo ya DCI Manumba na kutaka aulizwe mwenyewe alikoitoa huku akisema uchunguzi alioagiza bado unaendelea.

Ugonjwa wa Scleroderma

Kwa mujibu wa mtandao wa Johns Hopkins wa www.hopkinsscleroderma.org, Scleroderma ni ugonjwa unaohusisha mfumo wa kinga ambao wakati mwingine dalili zake zinaweza kuwa mtu kuwa na baridi yabisi na sugu. Ni ugonjwa unaoathiri mwili, hasa muunganiko wa tishu na kuufanya kuwa mgumu.
Mfumo wa Kinga
Scleroderma iko katika kundi la ugonjwa wa mfumo wa kinga. Hii ina maana kwamba mfumo wa kinga wa mtu hufanya kazi kwa kujitegemea. Hulinda mwili dhidi ya maadui mbalimbali kama virusi na maambukizi.
Kuwa na ugonjwa huo wa mfumo wa kinga maana yake ni tishu au kinga kuvamiwa na wageni, ama virusi au maambukizi mengine na hivyo kusababisha matatizo.Mtu anapokuwa na scleroderma, seli huathirika kwa sababu katika hali ya kawaida seli haipaswi kuwa na kitu kingine cha ziada katika mfumo wake wa utendaji kazi na kama ikitokea hivyo, mtu huyo hujikuta katika matatizo yanayosababisha mfumo wa mwili wake kutokuwa kama ulivyo kawaida.
Unawezaje kuupata?
Watu wachache hupata ugonjwa huu na hakuna anayejua unatokana na nini. Scleroderma ni ugonjwa nadra. Chini ya watu 500,000 Marekani wanasumbuliwa nao na hakuna anayejua kwa uhakika chanzo chake.
Baadhi ya wataalamu wanabainisha kuwa watu kati ya saba wenye kusumbuliwa na ugonjwa huo ni wanawake. Wenye kusumbuliwa zaidi na ugonjwa huo ni wale wenye umri wa kati ya miaka 35 na 50. Hata hivyo, watoto wadogo na watu wazima zaidi wanaweza kuupata.
Baadhi ya familia zimekuwa zikiathirika zaidi na ugonjwa huu kuliko zingine. Ingawa scleroderma hauonekani kuathiri kifamilia, lakini mara nyingi hutokea katika familia ambayo imewahi kuwa na mtu mwenye magonjwa yanayokaribiana nao kama vile tezi au mengine yanayofahamika kitaalamu kama arthritis rheumatoid au lupus ambayo msingi wake ni kuathirika kwa mfumo wa kinga.

Dalili za awali
Kwa baadhi ya watu kuna dalili mbili za kwanza:
• Vidole kuwa vya baridi na wakati mwingine kubadilika rangi au mtu kuonekana mwenye msongo wa mawazo.
• Vidole na mikono kuwa migumu na kutoa magamba au unga
Mabadiliko ya rangi ya kidole husababishwa na kupungua kwa uwezo wa mishipa ya damu kupitisha damu ipasavyo. Hii hutokea kwa sababu ya madhara yaliyotokea dhidi ya mishipa ya damu iliyoharibiwa kutokana na ugonjwa huo.
Hali ya ubaridi na mabadiliko ya rangi huitwa raynaud’s (hutamkwa ray-knowds). Watu wengi wenye hali hii wanaweza kudumu nayo bila kuwa na ugonjwa wa scleroderma.
Athari tofauti
Athari ya scleroderma inatofautiana sana kati ya watu. Wengi huanza kuona dalili za vidole kubana na hata kuvimba. Kisha kwa baadhi ya watu huchukua miezi sita wakati wengine hata zaidi ya mwaka ugonjwa kujitokeza rasmi.

Lowassa awakaanga vigogo Serikali ya JK


ASEMA WAMEKWAMA KUMALIZA TATIZO LA AJIRA, AWATAKA MAASKOFU WAINUSURU, RUWAICHI AIPONDA KUHUSU MGOMO WA MADAKTARI
Juma Mtanda, Ifakara
WAZIRI Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa amesema anashangazwa na Serikali kuendelea kulifumbia macho tatizo la ajira kwa vijana na kuwaomba maaskofu wasaidie kulimaliza akisema hilo ni bomu linalosubiri kulipuka.

Lowassa alisema hayo jana alipokuwa akitoa salamu zake kwenye sherehe za uzinduzi wa jimbo jipya la Kanisa Katoliki la Ifakara zilizofanyika katika Viwanja vya Kanisa Kuu la Mtakatifu Edward, Ifakara.

Alisema viongozi wa juu serikalini wameshindwa kulitatua na kulifumbia macho tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana hivyo kuwaomba maaskofu waliangalie kundi hilo ambalo linakabiliwa na changamoto nyingi.

“Suala la ajira kwa vijana hakuna kiongozi anayelishughulikia ipasavyo ndani ya Serikali, hivyo niwaombe maaskofu nchini walione hili. Nawaomba katika miradi yenu mlipe kipaumbele suala la tatizo la ajira kwa vijana,” alisema Lowassa na kuongeza:

“Kanisa Katoliki limekuwa likisaidia sana katika sekta ya elimu na afya kwa hiyo sasa waelekeze nguvu hizo katika kusaidia ajira kwa vijana. Wengi wanaomaliza elimu ya sekondari na vyuo wanakabiliwa na tatizo kubwa la ajira. Hili kama tunavyosema ni bomu linalosubiri kulipuka, sasa naliomba Kanisa lisaidie juhudi za Serikali kutatua tatizo hili,” alisema Lowassa huku akishangiliwa.

Ruwaichi na mgomo
Akizungumza katika sherehe hizo, Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Yuda Dadeus Ruwaichi alisema mgomo wa madaktari nchini umedhihirisha udhaifu wa Serikali katika kushughulikia migogoro na kusema ni aibu kwa Tanzania.

“Watu wengi wamekufa katika mgomo ule na hii imeonyesha Tanzania ni taifa lisilo na dira,” alisema Askofu Ruwaichi huku Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda ambaye ni Mbunge wa Ulanga Mashariki akimsikiliza.

“Hakuna hata uharaka uliochukuliwa kushughulikia mgomo ule na hii ni kwamba nchi yetu sasa imefikia pabaya kwani inaonekana imeshindwa kushughulikia matatizo,” alisisitiza.

Katika salamu hizo kwa Askofu mpya wa jimbo jipya la Ifakara, Salutaris Libena, Askofu Ruwaichi alisema kanisa litaendelea kupiga vita umasikini.

Alimtaka askofu huyo kutoogopa kukemea maovu yanayofanywa na viongozi wa Serikali na kusababisha pengo kati ya wenye nacho na wasionacho.

Mwinyi asisitiza upendo
Kwa upande wake, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi alimtaka Askofu Libena kutumia nafasi yake kuleta amani na upendo miongoni mwa waumini wa dini mbalimbali.

Mwinyi alisema uaskofu ni daraja kubwa linalofanana na nafasi ya uwaziri katika Serikali hivyo waumini wa dini ya Kikristo katika jimbo jipya la Ifakara wanapaswa kutoa ushirikiano kwa kiongozi huyo aliyesimikwa kutumikia dini hiyo na Watanzania kwa ujumla.

“Nafasi ya uaskofu haifungamani na dini wala kabila kwani daraja hilo limejaa roho ya huruma na upendo hivyo jamii ya jimbo la Ifakara ni wakati wa kutoa ushirikiano ili kumpa nafasi mhashamu Askofu Salutari Libena ya kuwahudumia katika nyanja mbalimbali za elimu, afya na tabia njema,” alisema Mwinyi.

Kadinali Pengo
Katika mahubiri yake, Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo alisema uamuzi wa kugawanya Jimbo la Mahenge ni mchakato wa muda mrefu uliotokana na ukubwa wa Jimbo la Mahenge.

“Mchakato huo uliridhiwa na Papa Benedict wa 16 Januari 14, 2012 kwa kukubali Ifakara kuwa jimbo jipya na makao makuu katika Kanisa la St Andrew lililopo mji mdogo wa Ifakara.

Sherehe hizo zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, dini na taasisi wakiwemo maaskofu wa majimbo 34.

Wengine waliohudhuria sherehe hizo ni Waziri wa Katiba na Sheria Celina Kombani, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Joel Bendera na Mkuu wa Wilaya ya Ulanga na Kilombero, Francis Miti.

Monday, March 19, 2012

Students' public trysts


SINGAPORE – More students have been ‘caught’ by netizens in brazen public displays of intimacy, just months after two students from Yuhua Secondary were chastised by school authorities for their misdemeanours.
Citizen journalism website Stomp has reported three cases in the month of March alone.
In one of the incidents, a couple in their school uniform was spotted on March 11 locking lips at a coffeehouse in Holland Village.
According to the Stomp contributor who snapped the photos, the pair, believed to be from an “elite school”, was oblivious to other people around them.
Another young couple was spotted sharing their passion aboard the MRT in full view of other commuters, on March 14.
The Stomp contributor who caught them in the act described the couple to be “young” and barely adolescent.
Earlier this month on March 5, another young secondary school couple was seen kissing in public, to the disgust of another witness close by.
Going further than tongue wrestling, a group of secondary school students were spotted in early Feb at Tampines 1 shopping mall 'all over each other'. The students were captured sitting on one another, the contributor reported.
In Jan, a pair of teenagers from Yuhua Secondary made headlines on The New Paper when they were spotted brazenly making out for two hours at a public playground.
They were pictured kissing and groping each other for two and a half hours.
A witness said that they started activities on the bench and then moved on to making out on the swing and slide. Pictures of their activities were then posted on Stomp.
The teens were then counselled by the school and their parents were informed.
A child psychiatrist  that The New Paper spoke to commented that the teens' raunchy behaviour in public suggests that they were unable to control themselves.
He added that counselling would be the best course of action.

Dk Slaa afunika kampeni Arumeru


AKWEPA KUMJIBU WASSIRA, WAZAZI WA NASSARI WATOA NENO, LEMA AMTAHADHARISHA LOWASSA
Na Waandishi Wetu, Arumeru
KATIBU Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa jana alitua Arumeru Mashariki na kuhutubia mkutano uliotikisa eneo la Kwapole – Soko la Ndizi, huku wazazi wa mgombea wa chama hicho, Joshua Nassari wakipanda jukwaani kujibu matamshi yaliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira dhidi ya mtoto wao.

Mchungaji Samuel Nassari na mkewe, waliwaambia mamia ya watu waliofika kwenye uwanja huo kuwa walitoa baraka kwa Joshua kugombea nafasi hiyo wakisema mtoto wao ni mwadilifu anayefaa kuwawakilisha wananchi wa Arumeru Mashariki bungeni.

Kauli ya Mchungaji Nassari inatokana na matamshi ambayo yamekuwa yakitolewa na Wassira katika kampeni za kumnadi mgombea wa CCM, Sioi Sumari kwamba mgombea wa Chadema hana nidhamu na kwamba amewachosha wazazi wake kwa kutokuwa na nidhamu.

Lakini jana, baba wa mgombea huyo akiwa na mkewe jukwaani alisema: “Mimi siyo mwanasiasa, lakini nimelazimika kupanda jukwaani leo kutokana na matamshi yaliyotolewa na Wassira, napenda kusema hivi Joshua alipata baraka za familia.”

Alisema kabla ya kugombea, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alifika nyumbani kwake Songoro na kuwaeleza kuwa wanamtaka Nassari kugombea tena na kusema kwamba familia ilikubali na kumpa baraka zote ikiwa ni pamoja na kuwaita wachungaji kumwombea.

Mchungaji Nassari pia alikanusha madai kwamba mwanaye alikuwa jeuri tangu shule akisema hajawahi kufukuzwa wala kusimamishwa masomo kwa utovu wa nidhamu tangu akiwa shule ya msingi hadi alipohitimu masomo ya shahada, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Mchungaji huyo alisema, mtoto wake alisoma katika shule ya msingi, Sekondari ya Bagamoyo kidato cha kwanza hadi cha nne na Shule ya Sekondari ya Wavulana Tabora kidato cha tano na sita.

“Alipokuwa chuo kikuu, ninatambua kwamba alikuwa mtetezi wa wenzake, hivyo ndugu zangu Joshua Nassari anafaa kuwa mbunge na suala kuwa hajaoa halina msingi kwani mke bora mtu anapewa na Mungu na siyo utashi wake au hamu yake, kwani mke siyo kitunguu cha kununua sokoni,” alisema Mchungaji Nassari.

Mapokezi ya Dk Slaa
Dk Slaa ambaye alihutubia mkutano wa kampeni kwa mara ya kwanza katika uchaguzi huo mdogo, alilakiwa na mamia ya watu na magari ulianzia Uwanja wa Ndege ya Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) hadi eneo la Kwapori, Kata ya Akheri ambako mkutano huo ulifanyika.

Msafara wa kumsindikiza Dk Slaa kuelekea Uwanja wa Kwapori ulianza mara tu baada ya kuwasili KIA majira ya saa tisa alasiri. Msafara huo uliokuwa umesheheni magari na pikipiki, ulifunga kwa muda Barabara ya Arusha-Moshi katika eneo hilo.

Akihutubia mkutano huo, Dk Slaa alisema Chadema kinataka wakazi wa Jimbo la Arumeru Mashariki, kumchagua Nassari si kwa sababu ana sura nzuri, bali wanataka kumtuma katika Halmashauri ya Meru na bungeni.

“Halmashauri ya Meru ina tatizo kubwa la ubadhirifu wa fedha za umma, fedha za afya, elimu na barabara zinaliwa na hili nina ushahidi nalo kwa sababu nilikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), kwa hiyo Nassari anatakiwa kwenda kufanya kazi ya kudhibiti wizi huo,” alisema Dk Slaa na kuongeza:

“Hata huko bungeni hatumtumi kwenda kufanya kazi ya Chadema wala Mbowe (Freeman) hapana, hatumtumi kwenda kusinzia wala kuzomea, anatakiwa kwenda kufanya kazi ya watu wa Arumeru ambayo kwa miaka 50 ya Uhuru CCM wameshindwa kuifanya.”

Alisema alipokuwa Mwenyekiti wa LAAC alibaini ubadhirifu wa kutisha katika Halmashauri ya Arumeru wakati huo na hadi sasa unaendelea.

“Kuna wizi mkubwa, fedha za barabara, fedha za maji, fedha na elimu, zimeliwa na hii ni kwa kuwa hakuna mbunge au diwani wa Chadema katika Halmashauri ya Meru,” alisema Dk Slaa.

Alisema wanataka Nassari awe mtetezi wa haki za Jimbo la Meru bungeni kwani wabunge wa CCM kamwe hawawezi kuisema Serikali yao bungeni.

Ujumbe wa polisi
Akizungumza katika mkutano huo, Dk Slaa alisema polisi ambao wametumwa kusimamia amani katika jimbo hilo wamemtumia ujumbe wakilalamikia kulipwa posho ya Sh10,000 kwa siku ambayo haikidhi mahitaji yao.

Dk Slaa alimwomba Nassari kuwasaidia polisi hao kwa kutetea maslahi na stahili zao pindi atakapochaguliwa kuwa mbunge.

“Wamenitumia ujumbe polisi, walimu na wafanyakazi wengine, wanajua watetezi wao ni wabunge wa upinzani, hivyo nawaomba wakazi wa Meru kumchagua Nassari ili aende kuwatetea,” alisema Dk Slaa.

Aliwaomba wakazi wa jimbo hilo, kuendelea kumchangia Nassari ili aendelee na kampeni kwani hana fedha tofauti na mgombea wa CCM.

Kuhusu tuhuma alizotoa Wassira dhidi yake, kwamba yeye (Dk Slaa) alifukuzwa upadri kutokana na kula fedha za ujio wa Papa na kuwa bado anatafutwa, alisema waziri huyo ni mwongo na hajui asemalo. Alisema ikiwa tangu mwaka 1991 bado hajakamatwa, basi Serikali iliyopo madarakani inalea wezi.

Alisema Papa alifika nchini tangu mwaka 1991 na tangu wakati huo yeye yupo nchini na hajawahi kuulizwa kama alikula fedha au kutafutwa akisema kama ni kweli anatafutwa kwa miaka yote hiyo, basi Serikali ijiuzulu kwa kushindwa kumkamata.

“Kama tangu mwaka 1991 nipo, basi kitendo cha Serikali kushindwa kunifungulia mashtaka ya wizi wa hizo fedha basi ni Serikali dhaifu na ijiuzulu,” alisema Dk Slaa.

Lema amuonya Lowassa
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema amemuonya Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kutofika Arumeru akisema akifanya hivyo, wataweka hadharani kashfa zote zinazomkabili.

“Tumesikia anakuja Arumeru, tunamkaribisha lakini tunamwonya maana tutamshughulikia ipasavyo, tunafahamu mengi sana kuhusu tuhuma zinazomkabili, akithubutu kukanyaga hapa basi imekula kwake,” alisema Lema.

Kwa upande wake, Nassari alisema: “Mimi siombi ubunge kwa ajili ya kutafuta utajiri kama wengine wanavyofanya, ninatambua tabu zetu Arumeru, kina mama wanavyobeba bidhaa zao na kuingiza sokoni lakini wanatozwa ushuru mkubwa, haya yote ni mambo muhimu ya kushughulikia.”

“Masoko mengi tunayo tangu enzi za utoto wetu, licha ya kwamba wanatoza ushuru lakini miaka yote mnafanya biashara kwenye mvua na jua. Nipeni nafasi tufanye kazi pamoja ya kukabiliana na matatizo haya.”

Chadema washambulia waandishi

Wafuasi wanaosadikiwa kuwa ni wa Chadema jana walifunga Barabara ya Moshi-Arusha eneo la Maji ya Chai na kulishambulia gari lililokuwa limebeba waandishi wa habari waliokuwa katika msafara wa CCM uliokuwa ukipita katika barabara hiyo ukitokea Kata ya Leguruki.

Wafuasi hao walilirushia mawe gari hilo na kulipasua kioo cha nyuma na kumjeruhi Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Mtanzania, Eliya Mbonea.

Muda mfupi baadaye, polisi walifika katika eneo hilo na kuwatawanya wafuasi hao.

Mlezi wa chama hicho mkoani Arusha, Steven Wassira alilaani kitendo hicho akisema hakivumiliki na kuvitaka vyombo vya sheria kuchukua mkondo wake.

Katika hatua nyingine: Gari linalodaiwa kuwa la wafuasi wa Chadema, jana lilivamia mkutano wa CCM katika Kata ya Leguruki na kutimua vumbi uwanjani hapo kwa muda kabla ya kuondoka na kutokomea kusikojulikana.

Imeandikwa na Neville Meena, Mussa Juma na Moses Mashalla.

The world's worst tourists are...

The world's worst tourists are...
AMERICANS have been deemed as the world's most annoying tourists, and surprisingly or not, they themselves agree.
Sharing the same sentiments were the Canadians and Australians who also slammed the Americans for their lousy behaviour overseas.
While the Irish pointed the finger at their British neighbours for being the most intolerable, the UK travellers, on the other hand, thought the Germans were a pain in the neck.
The list - which also places the Indians, Chinese, Japanese and French tourists among the worst behaved - ranks travellers from 16 nationalities on the basis of their behaviour.
Of the 5,600 total respondents in survey carried out by Mandala Research for LivingSocial, a majority 4,000 were Americans. The rest were from Australia, Canada and Ireland.
Perhaps, one reason why the Americans were considered "insufferable" is their lack of practice as tourists. The survey reported that Americans only get an average of 16 days of vacation each year.
In comparison, the Canadians get about 21 days off, the British get 23 days, the Australians get 27 days, and the Irish get a whopping 28 days off a year.
However, contrary to what is commonly perceived that 'only 15 per cent of Americans own passports', they seem to be globetrotting around enough for their vacation habits to be noticed.
The survey found that 78 per cent of Americans have visited at least one foreign country, 61 per cent have visited multiple countries, and 36 per cent have travelled to four or more foreign destinations. The average American has visited at least four countries," said Dave Madden, GM of LivingSocial Escapes (North America).
Far from perfect, four in ten US travellers (39%) also admitted to having pilfered something from a hotel during a visit. The most common items smuggled into suitcases were towels, bathrobes, pillows and sheets.