Thursday, August 4, 2011

Wauza mafuta wakaidi amri ya serikali

SIKU moja baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma ya Nishati na Maji (EWURA), kupunguza bei za mafuta ya dizeli, petroli na ya taa, baadhi ya wamiliki wa vituo vya kuuza mafuta hayo nchini wamegoma kutoa huduma hiyo.

Baadhi ya vituo vilidai havina mafuta, vingine vimeharibikiwa pampu, vingine umeme umezimika huku baadhi wakitangaza mgomo waziwazi.

Dar es Salaam katika kituo cha mafuta cha Lake Oil kilichoko Manzese Big Brother, walidai kuwa wamesitisha uuzaji wa mafuta hayo kutokana na pampu zao kuharibika na si kwamba wamegoma kuuza kama ilivyo kwa wengine.

“Si kwamba tumegoma kuuza mafuta isipokuwa pampu ya kusukuma kutoka visimani iliharibika tangu jana usiku, kutokana na matatizo ya umeme,” alidai mwuzaji wa kituo hicho, ambaye hata hivyo hakuwa tayari kutaja jina lake.

Morogoro baadhi ya vituo asubuhi viligoma kutoa mafuta kwa bei mpya na vingine vikidai mafuta yaliyopo ni ya zamani hivyo haviwezi kuyauza kwa bei mpya. Walisema wakishusha watapata hasara.

Lakini katika uwanja wa maonesho wa Julius Nyerere kunakofanyika maonesho ya Nane Nane kituo cha Kobil kilikuwa kinauza huku wauzaji wakisema wanatii na kufuata bei elekezi iliyotangazwa juzi.

Rukwa, wamiliki wa vituo vya mafuta walitangaza hadharani uamuzi wa kufunga vituo vyao wakipinga bei hiyo mpya.

Kutokana na hali hiyo, bei ya mafuta ya petroli ilipanda Sumbawanga hadi Sh. 5,000 kwa lita wakati Nkasi na Mpanda mafuta hayo yaliuzwa mtaani kwa Sh. 6,000.

Hali hiyo ilimlazimu Ofisa Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Salum Chami, kuagiza wamiliki wote wa vituo vya mafuta mkoani humo, kufungua mara moja na kuendelea kuuza nishati hiyo kwa bei iliyopangwa na Serikali, vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

Mbeya jana asubuhi madereva walijikuta wakishindwa kuendelea na shughuli zao kutokana na wafanyakazi wa vituo vya mafuta kudai kuwa mafuta yamekwisha na wengine wakidai umeme umekatika.

Vituo vingi vilisitisha kuuza mafuta saa mbili asubuhi jambo ambalo lilitafsiriwa na baadhi ya wakazi wa Jiji kuwa wamiliki waliwasiliana na kuzuia uuzaji mafuta kupingana na agizo la Serikali. Dereva wa bajaj, Elias John, alisema alinunua mafuta saa moja asubuhi, lakini aliporudi saa tatu alishangaa kuambiwa umeme umekatika.

Mmoja wa wafanyakazi katika kituo cha mafuta cha BP Mwanjelwa, ambaye hakutaka kutaja jina lake, alikaririwa akisema Serikali haiwezi kushindana na wafanyabiashara. Mfanyakazi huyo kwa jeuri alisema lazima mafuta yauzwe kulingana na bei wanayotaka wafanyabiashara na si Serikali.

"Mimi sifaidiki na lolote kwa kukosekana kwa mafuta, lakini ninyi ndio mtakaoathirika kwa kuwa leo hamtafanya kazi yoyote," alisema mfanyakazi huyo hali iliyoashiria mgomo wa wazi wa uuzaji mafuta.

Akizungumzia hatua hiyo Meneja Mawasiliano Mwandamizi wa Ewura, Titus Kaguo, alisema wafanyabiashara hao wanakiuka sheria ya mafuta na sheria ya ushindani wa biashara na kwamba hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.

“Kwa atakayebainika kufanya hivyo, Ewura haitasita kumfutia leseni ya biashara licha ya kwamba si lengo letu kufanya hivyo,” aliongeza Kaguo.

Alisema inashangaza kuona wafanyabiashara hao wanalalamika kushushwa kwa bei hizo na akihoji kwa nini hawakuendelea kuuza mafuta ya taa kwa bei ya chini mara baada ya Serikali kutangaza bei mpya iliyoanza Julai mosi, licha ya kuwa walikuwa nayo tangu zamani.

Alisema kutokana na hatua hiyo, Ewura imepokea ujumbe kutoka kwa wauzaji hao wa mafuta kwa rejareja wakilalamikia punguzo na ilipanga kukutana nao.

Baadhi ya madereva waliipongeza Serikali kwa hatua hiyo, huku wakiitaka kuchukua hatua nyingine kudhibiti uchakachuaji unaoweza kujitokeza.

Mmoja wa madereva hao aliyejitambulisha kwa jina la Justin Mpanga, alisema ni vema hatua za haraka kudhibiti uchakachuaji zikaanza kuchukuliwa, ili kubana wafanyabiashara hao wenye hasira kipindi hiki.

Hata hivyo baaadhi ya wananchi ambao hawakutaka kutajwa majina, waliitaka Serikali isilegeze msimamo na badala yake iwanyang’anye leseni wafanyabiashara hao jeuri.

“Wanyang’anywe leseni na vituo likabidhiwe Jeshi la Wananchi liuze mafuta na fedha ziende serikalini, kwa sababu hawa wanataka kuua wananchi katika kipindi hiki chenye matatizo ya nishati ya umeme pia,” alisema mmoja wa wananchi hao.

Rihanna rekindles relationship with her first boyfriend, Barbadian 'Love God' Negus Sealy

Rihanna has apparently rekindled her relationship with her first boyfriend Negus Sealy after the pair were seen dancing together at a festival back in Barbados.

The 23-year-old singer is said to have become inseparable from her first love Sealy, nicknamed the 'Love God' by local ladies, since arriving back in her home country 12 days ago.

The pair first dated back in 2006, before Rihanna made her name in the music industry, and are said to have given things another go in 2009 when the Rated R singer was rebounding from her violet relationship with Chris Brown.
Rekindled: Rihanna is said to have become inseparable from her first boyfriend, Negus Sealy, after the pair danced together at a festival in Barbados this week

Rekindled: Rihanna is said to have become inseparable from her first boyfriend, Negus Sealy, after the pair danced together at a festival in Barbados this week


As they were: Rihanna and 'Love God' Negus together back in 2006
As they were: Rihanna and 'Love God' Negus together back in 2006

A source told The Sun: 'Negus has hardly left her side. He was her first true love. The ladies here all love him - they call him the Love God.

'They've hooked up in the past when she's been back in Barbados but now things have progressed into a proper relationship again.'

Rihanna and Sealy were photographed dirty dancing together at a festival to celebrate Kadooment Day earlier this week.
Who could resist? Rihanna turned up at the festival wearing an incredibly skimpy outfit of a bra, knickers and headdress
Who could resist? Rihanna turned up at the festival wearing an incredibly skimpy outfit of a bra, knickers and headdress

You need to cool down! Sealy and Rihanna chat as the singer grabs a drink of water
You need to cool down! Sealy and Rihanna chat as the singer grabs a drink of water

A partygoer told the newspaper: 'They were all over each other and their dancing got very hot and heavy.'

Rihanna flew back to her home country earlier this week, ahead of her Loud Concert tour date in Bridgetown on Friday, when her role as the official ambassador for Barbados will officially begin.
And the singer seems to be enjoying herself, tweeting fans: 'My home, my country, my people....BARBADOS!!!
New advert: Rihanna is seen in the advert for her new drink Vita Coco coconut water with tropical juice
New advert: Rihanna is seen in the advert for her new drink Vita Coco coconut water with tropical juice

'#1LOVE #SWEETfahDAYS NOTHIN' BETTER! #RihannaNavy Miss u guys tho.'
Meanwhile, Rihanna also revealed on her Twitter page that she has collaborated with Vita Coco on a new tropical flavour drink.

She explained: 'I grew up in Barbados - so when Vita Coco approached me to help develop a new flavor, I thought we should combine the natural coconut with fresh tropical fruits - two of my favorite things.
'It tastes so delicious and reminds me of home! It's delicious and so good for you!'

Waka Flocka Flame Arrested For Marijuana ... Again

The rapper was detained by police in Georgia Tuesday after cops pulled him over for a routine traffic violation and say they found marijuana in his car. When police approached the rapper's White Chevy Tahoe, they could smell weed. Waka Flocka was asked to step out of the vehicle and placed in cuffs.
Flocka
When cops searched the ride, officers found "a small amount of marijuana" on the floor. Waka was cited for possession of less than an ounce of weed. And failure to wear a seat belt. Obviously. He was eventually released and sent on his way after being "very cooperative." Earlier this month, he was arrested for drug possession in New York.

Tendwa ampinga Werema

VYAMA vya siasa nchini vitaendelea kufanya maandamano ya amani pale inapobidi kwa kuwa hatua hiyo inaruhusiwa kisheria na ni haki ya msingi ya kila mtu na chama chake katika kujitafutia haki.

Aidha, imeelezwa kuwa mpango wa kutunga sheria itakayodhibiti maandamano ya vyama vya siasa nchini unaodaiwa kutajwa bungeni na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) , Jaji Frederick Werema, ni kutaka kuvinyima vyama haki za msingi za kikatiba.

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Msajili wa Vyama, John Tendwa, alipozungumza na wanahabari kuhusu uchaguzi katika jimbo la Igunga na marejesho ya fomu za gharama za uchaguzi mkuu uliopita.

“Labda kama AG hakueleweka au alitafsiriwa vibaya, sidhani kama anaweza akasema ataleta muswada wa sheria ya kudhibiti vyama vya siasa kufanya maandamano nchini, kwa kuwa hiyo ni haki ya kikatiba na yeye ni mwanasheria anayeifahamu Katiba, sijui, sikumsikia ninyi ndio mnanieleza katika swali lenu hapa.

“Lakini kama hivyo ndivyo, basi itabidi abadilishe sheria nyingi sana, kwa sababu zipo kihalali na kwa malengo ya kujenga, endapo maandamano yanakuwa na nia nyingine hapo inawezekana kukawa na kasoro, lakini kuyadhibiti bila sababu kwa kuwa ni ya vyama vya siasa sidhani kama itakuwa sawa, ngoja tuone. Itakapotokea ndipo hapo tutajua,” Msajili alisema.

Akichangia hivi karibuni hotuba ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyotolewa bungeni na Shamsi Vuai Nahodha, Werema alisema suala la maandamano ni haki ya kikatiba, lakini pia moja ya masharti ya chama cha siasa kinapoandikishwa, ni kuhakikisha hakitumii njia ya mapambano katika kufikia malengo.

Alisema ingawa maandamano yanaruhusiwa, lakini wakati mwingine yanatumika vibaya na kutolea mfano wa mbunge kuzungumzia kuandamana kutoka Mwanza hadi Dar es Salaam na kwamba zipo baadhi ya nchi maandamano ingawa yanaruhusiwa, lakini yana utaratibu ili kutohusisha watu ambao wako kazini.

Alisema kutokana na hali hiyo, kuna haja ya kufanya marekebisho ya suala la maandamano ili yasifanyike sehemu za kazi na kuvuruga taratibu za wengine. Akizungumzia vyama vya siasa vilivyofanya marejesho ya gharama za uchaguzi, Tendwa alisema ni 12 huku NCCR-Mageuzi na UDP vikiwa vimeomba nyongeza ya wiki mbili kufanya hivyo.

“Wasipotekeleza hawa sheria itachukua mkondo wake kwa kuwafikisha mahakamani na kuwatoza faini ya Sh milioni tatu huku tukiwazuia kushiriki uchaguzi unaokuja”.

Wakati huo huo, Baraza la Vyama vya Siasa Nchini litakaa mwezi ujao kujadili namna ya kurejesha heshima na imani ya wananchi kwa vyama vyenye wabunge bungeni iliyopotea, baada ya wawakilishi hao kushindwa kutii kanuni na maadili ya uwakilishi wao ndani ya chombo hicho hasa katika Bunge la Bajeti linaloendelea sasa.

Akijibu maswali ya wanahabari kuhusu tabia mbaya za baadhi ya wabunge za kutotii kanuni za Bunge wawapo vikaoni na kutoleana maneno yasiyo na mantiki bila kutii Kiti cha Spika Tendwa alisema yeye kama Msajili wa Vyama hapaswi kuwazungumzia watu hao wanapokuwa bungeni kwa kuwa wana kiongozi wao.

“Sheria inanikataza kuwazungumzia, kuwaonya na kuwanyooshea kidole kwa jambo lolote wanapokuwa ndani ya Bunge kwa sababu wana Spika na Kamati ya Maadili vyenye jukumu la kuwaonya au kuwaondoa pindi wanapoonekana kushindikana kitabia.

“Hivyo wananchi wasinitupie lawama bure kwa kuwa ni wangu wanapokuwa nje ya jengo lile la Bunge tena kupitia kwa vyama vyao. Sana sana tulichopanga kufanya ili kunusuru heshima ya Bunge na vyama vya siasa wanavyoviwakilisha ni kukutana na Baraza la Vyama vyote vya Siasa nchini na kujiwekea msimamo wa namna ya kurekebisha tabia hizo,” Msajili wa Vyama alisema.

Aliwahakikishia wananchi kuwa Bunge la Oktoba litakuwa na tofauti kubwa, kwa kuwa wao wapo kushirikiana na Spika Anne Makinda na Kamati ya Maadili ya Bunge kuhakikisha wabunge hawawi na uwakilishi usiohitajika.

“Mimi ni mlezi wa vyama ambavyo wabunge wametoka, hivyo ni lazima tunapoona kuwa tuliyowafundisha watoto wetu hawayafuati, tuangalie namna ya kuwafanya wayatii ili aibu ya malezi yasiyo bora isitupate.

“Lakini kama wataendelea kuwa na tabia hizo hizo za kuwawakilisha wananchi kwa staili ya mizozo, kukashifiana, kutishiana, kutoleana hasira na lugha chafu na tabia nyingine mbaya, viongozi wanaowajibika nao moja kwa moja watapaswa kuwachukulia hatua kwa sababu muda wa kujifunza kanuni na nidhamu umekwisha” Tendwa alisema akiwa mwanadamu wa kawaida anaumizwa na uwakilishi huo wa sasa wenye asilimia 70 ya vijana waliotazamiwa kuleta mageuzi bora.

“Sasa unafika wakati hata mtoto mdogo anayesikia mambo ya wabunge wetu anawabeza, heshima hakuna na linakuwa Bunge lenye bora wabunge na si wabunge bora. Umuhimu wa vijana wengi bungeni unapoteza maana, kwa kuwa la zamani lenye wazee wengi ndilo lilikuwa na busara kuliko hili lenye mabadiliko haya,” alisema.

Lindsay Family Thanks Japan As Killer Jailed

The father of murdered British teacher Lindsay Ann Hawker has praised the Japanese authorities for finding her killer, who has been sentenced to life in prison.

Tatsuya Ichihashi admitted killing the 22-year-old in March 2007 but said her death was accidental. Miss Hawker's body was found buried in a sand-filled bathtub on the balcony of Ichihashi's flat in Ichikawa City, east of Tokyo. She had earlier given him an English lesson in a nearby cafe.

Miss Hawker's parents Bill and Julia and sisters Lisa and Louise were in the court in the city of Chiba to hear the verdict in the long-awaited trial.
Lindsay Hawker
Lindsay's family had called for the death sentence
Speaking after the sentencing, Mr Hawker said: "We've waited four-and-a-half years to get justice for Lindsay. We have achieved that today, and we are very pleased."

After the killing Ichihashi, 32, went on the run for over two years, living rough and even resorting to plastic surgery to change his appearance. During the manhunt, the Hawker family travelled to and from Japan to raise awareness of the case and distribute flyers about the missing suspect.

Ichihashi was finally caught when his plastic surgeon contacted police in November 2009.

Umoja wa mataifa wa laani Syria

Baraza la usalama la umoja wa mataifa kwa mara ya kwanza limetoa taarifa inayolaani ukiukaji wa haki za binadamu nchini Syria. Kauli hiyo imetolewa miezi kadhaa baada ya mashauriano ya kina ambayo yalikuwa yamesababisha migawanyiko kwenye baraza hilo kuhusu matukio nchini humo.

Jeshi la Syria
Hata hivyo Lebanon imesita kuunga mkono taarifa hiyo rasmi.
Taarifa hiyo haijatosheleza matakwa ya nchi za ulaya lakini hata hivyo imekuwa na uzito kando na ilivyo tarajiwa.

Hata hivyo baraza hilo limesisitiza kuwa suluhu ya mzozo unaoendelea nchini humo itapatikana kupitia machakato wa kisiasa utakaoongozwa na raia wa syria wenyewe. Kauli hiyo imezima matumaini kuwa dola za kigeni zitaingilia kati mzozo unaoenedelea nchini humo.

Wanadiplomasia wanasema taarifa hiyo rasmi ya baraza la usalama ni onyo kwa utawala mjini Damascas.
Lakini Lebanon, hawajaunga mkono taarifa hiyo, suala ambalo halikutarajiwa ukizingatia ushawishi mkubwa wa Syria nchini humo.

Tuesday, August 2, 2011

Kombe la Dunia 2014 makundi yapangwa

Rais wa Fifa Sepp Blatter siku ya Jumamosi ya tarehe 30 Julai, alihudhuria sherehe ya kifahari za kupanga nchi katika makundi ambazo zitakazoshiriki kuwania nafasi ya kufuzu kucheza fainali ya Kombe la Dunia zilizofanyika katika ufukwe wa pwani ya Copacabana mjini Rio nchini Brazil. Uchumi wa Brazil unakuwa kwa haraka, lakini patashika za kuelekea Kombe la Dunia hata hivyo zinaonekana kuchochea zaidi maendeleo ya uchumi.
Rais wa Fifa Sepp Blatter na Rais wa Brazil Dilma Rousseff
Rais wa Fifa Sepp Blatter na Rais wa Brazil Dilma Rousseff

Hivi sasa barabara mpya zinajengwa, viwanja vya ndege navyo vinaanza kupata sura mpya inayohitajika. Kumekuwa na kuchelewa kwa hapa na pale, lakini waandalizi hivi sasa wameonesha matumaini katika kazi za maandalizi. Na tofauti na uamuzi wa kuizawadia Qatar nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia la mwaka 2022, kwa Brazil kupata nafasi hiyo ya kuandaa, hakuna cha kutiliwa mashaka kwani kandanda ndio nyumbani kwake Brazil.

Tuangalie nchi za Afrika zilivyopangwa.

Mzunguko wa kwanza utakayo kuwa na mechi 12 za nyumbani na ugenini kati ya tarehe 11 hadi 15 mwezi wa Novemba, ambapo washindi watasonga mbele katika patashika za mzunguko wa pili.

Seychelles na Kenya
Guinea Bissau na Togo
Djibouti na Namibia
Mauritius na Liberia
Visiwa vya Comoro na Msumbiji
Equatorial Guinea na Madagascar
Somalia na Ethiopia
Lesotho na Burundi
Eritrea na Rwanda
Swaziland na jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
Visiwa vya Sao Tome na Principe na Congo
Chad na Tanzania
- - -

Kwa makundi nchi hizo zimepangwa hivi:

Kundi A
Afrika Kusini
Botswana
Jamhuri ya Afrika ya Kati
Somalia na Ethiopia
- - -
Kundi B
Tunisia, Visiwa vya Cape Verde, Sierra Leone, Equatorila Guinea na Madagascar

- - -
Kundi C
Ivory Coast
Morocco
Gambia
Chad/Tanzania
- - -
Kundi D
Ghana
Zambia
Sudan
Lesotho/Burundi
- - -
Kundi E
Burkina Faso
Gabon
Niger
Sao Tome and Principe/Congo
- - -
Kundi F
Nigeria
Malawi
Seychelles/ Kenya
Djibouti/Namibia
- - -
Kundi G
Egypt
Guinea
Zimbabwe
Comoros Islands/Msumbiji
- - -
Kundi H
Algeria
Mali
Benin
Eritrea/ Rwanda
- - -
Kundi I
Cameroon
Libya
Guinea Bissau/Togo
Swaziland/Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo
- - -
Kundi J
Senegal
Uganda
Angola
Mauritius/Liberia
Mechi zitachezwa kati ya tarehe 1 mwezi wa Juni, 2012 na tarehe 10 mwezi wa Septemba 10, 2013.

Washindi wa kila kundi watasonga mbele hadi raundi ya tatu, wakicheza mechi za nyumbani na ugenini kati ya tareh 11 hadi 15 mwezi wa Oktoba, 2013 na washindi ndio watafuzu kucheza katika fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

CCM: Bei mafuta ya taa ishushwe

KAMATI Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) imeiagiza Serikali kutafuta njia ya kushusha bei ya mafuta ya taa na kuhakikisha mafuta yote yanayoingia nchini yana ubora unaotakiwa. Pia Kamati hiyo imeitaka Serikali kutafuta suluhu ya uchakachuaji wa mafuta, kwani uwezo wa kufanya hivyo inao.

Akizungumza na waandishi wa habari , Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, alisema Kamati Kuu ya Chama hicho iliyokutana juzi pamoja na kujadili mambo mbalimbali ya chama, haijaridhishwa na kiwango cha bei ya mafuta ya taa. Alisema nishati hiyo ndiyo inayotumiwa na wananchi wengi wa kipato cha chini nchini, na kwamba kupandishwa bei kwa kisingizio cha kupunguza uchakachuaji, si sahihi.

Aliongeza kwamba, kutokana na kupanda kwa gharama za mafuta hayo Serikali inapaswa kukaa na kutafuta njia zitakazoshusha bei hiyo na kuvitaka vyombo husika kuhakikisha ubora wa mafuta yanayoingia nchini.

“Tunaitaka Serikali itafute njia ya kushusha bei ya matufa ya taa na pia kutafuta suluhisho la uchakachuaji na si kupandisha bei,“ alisema Nape.

Aidha, alisema suala la umeme ni nyeti na kwa hali ilivyo sasa si nzuri na kuishauri Serikali kuja na njia za kunusuru hali hiyo.

“Athari ya kukosekana kwa umeme nchini ni kubwa, hivyo Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini, itumie muda iliopewa kurekebisha bajeti yao vizuri na kuja na mpango wa dharura wa kunusuru hili na pia kuja na majibu ya suluhu ya tatizo hili,” alisema Nape

Aliongeza kwamba madhara yanayoipata nchi na mtu mmoja mmoja ni makubwa na inasikitisha kwa hali ilivyo na kwamba lazima Serikali ije na suluhu ya jambo hilo.

Aidha, Nape alisema Kamati Kuu pia ilijadili masuala yanayogusa wananchi likiwamo la migogoro ya ardhi, madini bei ya pamba na kuagiza Serikali iyashughulikie kabla migogoro hiyo haijawa mikubwa.

Hivi sasa mafuta ya taa yanauzwa bei kubwa kuliko dizeli na petroli ambapo katika baadhi ya vituo bei elekezi ni Sh 1,940 na kikomo ni Sh 2,086 kwa Dar es Salaam wakati kigoma elekezi ni Sh 2,117 na kikomo ni Sh 2,334 kwa lita.

Kwa hali hiyo hiyo, bei elekezi ya dizeli kwa Dar es Salaam ni Sh 1,939 na kikomo ni Sh 2084 huku kwa Kigoma elekezi ni Sh 2170 na kikomo ni Sh 2,333.

Hatua ya kupandishwa kwa bei hiyo ya mafuta ilifikiwa bungeni katika Bajeti ya Mwaka huu wa Fedha, kwa lengo la kuhakikisha kwamba kodi ya mafuta ya taa haizidiani sana na ya dizeli na hivyo kuondokana na uchakachuaji.

Hata hivyo wachambuzi wa masuala ya uchumi wanadai kwamba wachakachuaji wanafahamika na hivyo ni wajibu wa Serikali kuwabana kuliko kumwumiza Mtanzania masikini anayeishi kwa kutegemea mafuta ya taa.

Lakini pia wanasema tatizo linalosababisha yote haya ni kwamba mafuta yote yanaagizwa kutoka nje ya nchi ambako bei inatoka huko huko lakini pia kodi ya mafuta nchini ni kubwa. Wanatoa mfano kwamba lita moja ya mafuta ya taa huitozwa kodi ya Sh 400.30, ya petrioli ni Sh 534 na dizeli ni Sh 415.

Wachambuzi hao wanasema pia kwamba hata thamani ya sarafu kulinganisha na dola ya Marekani ni tatizo, “angalia Machi kiwango kilikuwa dola moja kwa Sh 1,400 leo ni Sh 1,600,” alisema mchambuzi ambaye hakuta kutajwa jina.

Asilimia 14 tu ya Watanzania ndio wanaotumia umeme huku asilimia iliyosalia ambayo wengi ni wananchi masikini waishio vijijini, wanatumia mafuta ya taa kumulikia na hata kupikia, hivyo bei ya nishati hiyo inapopanda inawaumiza.

Wakati huo huo, habari zilizopatikana jana jioni Dodoma, zilisema leo Serikali inatarajiwa kutangaza bei mpya ya mafuta nchini, baada ya Mamlaka ya Udhibiti wa Maji na Nishati (Ewura) kukokotoa kwa kuzingatia maoni ya wadau mbalimbali

Wabunge wapitisha mswada muhimu Marekani

Bunge la Congress nchini Marekani limepitisha mswada ambao utadhibiti deni la nchi hiyo na kuepusha hatari ya serikali kukosa pesa.
Rais ObamaChama cha Democratic na wapinzani wake Republicans wameridhia na Mswada huo sasa utawasilishwa mbele ya baraza la senate. Baada ya wanasiasa wa marekani kutofautiana kuhusu kuongeza kiwango cha kukopa cha serikali, bunge la Congress hatimaye limepiga kura kuunga mkono mswada utakaowezesha serikali ya nchi hiyo kuongeza kiwango cha madeni yake.

Kufuatia kupitishwa kwa mswada huo, marekani haina wasi wasi tena kuwa itashindwa kufadhili shughuli zake kuanzia hii leo, kama ilivyokuwa imetangazwa na wizara ya fedha. Mswada huo umepata kuungwa mkono na wajumbe wengi katika baraza la wawakilishi wakati ulipowasilihsiwa kupigiwa kura. Kwa hivyo sasa umevuka kikwazo chake cha kwanza. Hata hivyo matokeo hayo hayakuwa suala ambalo lilishangaza.

Jambo ambalo lililokuwa geni ni kuwasili bungeni kwa mbunge wa congress Bi Gabrielle Giffords kwa mara yake ya kwanza tangu apigwe risasi kichwani mwezi January. Wajumbe wa baraza la congress ambao wamekuwa wakivutana kwenye mijadala mikali walisimama kwa pamoja na kumshangilia alipowasili kupigia kura mswada huo.

Mswada huo ambao pamoja na kuongeza kiwango cha serikali kukopa fedha za kuendesha shughuli zake pia umependekeza hatua za kupunguza matumizi ya serikali. Kuna kila uwezekano kuwa Rais Barack Obama atakuwa anatia saini kuudhinisha saa chache tuu kabla ya pesa zilizoko kwenye mfuko wa serikali kumalizika kulingana na ushauri wa wizara ya fedha.

Hapo jana Rais Barack Obama alitangaza kuwa chini ya makubaliano kati ya chama chake na kile cha Republicans serikali itapunguza matumizi yake kwa dollar trilioni moja katika kipindi cha miaka kumi ijayo.
Kwa wiki kadhaa, viongozi wa vyama hivyo wamekuwa wakivutana kuhusu njia bora ya kufuata kukabili madeni ya marekani. Hali ambayo ilitishia kukwamihsa shughuli za serikali.

Rais Obama amesema kuwa mpango ulioafikiwa sio ule aliotarajia lakini amelazimika kuukubali ilikuwezesha huduma za serikali kuendelea na madeni yake yalipwe. Utawala wa Rais Obama ulikuwa unakabiliwa na shinikizo kali kutoka kwa wapinzani kutoka chama cha Republican ambao walikuwa wanapinga pendekezo lake la kuwepo na mpango ambao utasitiri hali hadi mwisho wa mwaka ujao.

Chama cha Republicans kilitaka mpango huo uwepo hadi katikati ya mwaka ujao. Lakini sasa vyama hivyo vimekubaliana kuunda kamati maalum itakayotoa mapendekezo mapya mwezi Novemba.

Monday, August 1, 2011

Kisa na mkasa na Salim Kikeke

Kutuma ujumbe wa simu kosa...

Jimbo moja nchini Marekani limepiga marufuku watu kutuma ujumbe wa simu huku wakiwa wanatembea barabarani. Mtu atakayekutwa akituma ujumbe mfupi wa maandishi, yaani text messege, huku akiwa anatembea, atapigwa faini ya dola mia moja na ishirini. Taarifa zinasema Jimbo la Pennsylvania limechukua hatua hiyo kukabiliana na tatizo linaloongezeka la watu kutembea huku wakiwa wanatazama simu zao badala ya kutazama wanapokwenda.

Jiji la Philadelphia limesema linataka kupambana pia na madereva wa magari, waendesha baiskeli na watembea kwa miguu ambao muda mwingi huutumia wakituma ujumbe wakiwa barabarani.

Mji wa Rexburg, uliopo Idaho, huwatoza faini ya dola hamsini watu wanaokutwa wakivuka barabara huku wakiwa wanatuma ujumbe wa simu. Hata hivyo naibu meya wa mji huo ametoa taarifa akikanusha madai ya utozaji faini, ingawa ameonya watu kuepuka kutuma text huku wakiwa wanatembea.

Taarifa hizi zimekuja kufuatia msichana mmoja aliyekuwa akituma ujumbe huku akiwa anatembea na kujikuta amedumbukia ndani ya mtaro wa pembezoni mwa barabara. Kutuma ujumbe sio kosa, lakini ni hatari, amesema naibu meya.

Jini au?

Bwana mmoja nchini Afrika Kusini aliyedhaniwa kuwa amekufa, aliamka baada ya kupigwa na baridi kali katika chumba cha kuhifadhia maiti. Bwana huyo mwenye umri wa miaka hamsini alianza kupiga kelele za kuomba msaada. Wafanyakazi wawili wa chumba cha maiti waliposikia kelele hizo walikimbia, wakidhani ni jini, vimeripoti vyombo vya habari vya Afrika Kusini.

"Ndugu zake walidhani amekufa wakampeleka mochuari" amesema Sizwe Kupelo ambaye ni afisa wa wizara ya afya, akizungumza na shirika la habari la Afrika Kusini, Sapa. Shirika la habari la Reuters limesema familia ya bwana huyo katika mji wa Libode, katika jimbo la Eastern Cape iliamua kumpeleka mochuari, baada ya kudhani amekufa.

Baada ya bwana huyo kuendelea kupiga kelele za kuomba msaada, wafanyakazi wawili waliamua kurejea ili kuhakikisha sio jini na kumkuta bwana huyo akiwa hai na mara moja kuita gari la kubebea wagonjwa.
Msemaji wa wizara ya afya amesema mtu huyo alikuwa amekaa kwenye chumba cha baridi kwa karibu saa ishirini na nne.

Afisa huyo amesema watu wasikimbilie kupeleka wagonjwa wao mochuari wakidhani wamekufa.
Amesema madaktari na polisi ndio watu pekee wenye uwezo wa kufanya vipimo na kufahamu kama watu wamekufa au la.

Kuendesha gari bila gurudumu

Dereva mmoja wa basi nchini Uchina aliendesha basi lake kwa umbali mrefu bila kujua kama matairi yote ya nyuma yamechomoka. Kutokana na msongamano wa magari katika jiji la Shaoyang, dereva huyo Shi Shao hata hakuhisi kama gari linaburura kwa sababu ya mwendo mdogo wa foleni.

Gazeti la Metro limesema ingawa alikuwa akisikia mlio usio wa kawaidia, alidhani ni mlio wa kifaa kiitwacho suspension, kimeharibika labda kutokana na mashimo ya barabarani. Hata hivyo, baada ya mlio huo kuendelea, abiria walianza kupatwa na mashaka na wao, na hivyo kutazama tatizo ni nini. Hatimaye abiria waligundua kuwa basi wanalosafiria halina matairi yote ya nyuma, na haraka walimtaarifu dereva. Dereva Shi alisimamisha basi hilo katikati ya barabara ili kusubiri kuvutwa na gari jingine, na hivyo kusababisha msongamano mwingine upya.

Polisi walipowasili hawakuamini macho yao kuona basi limesafiri umbali mrefu bila ya kuwa na matairi ya nyuma.

Yu wapi eh...bwana harusi?

Harusi moja nchini Indonesia ilisimamishwa ghafla bin vuu baada ya kugundulika kuwa bwana harusi ni mwanamke. Wageni waalikwa na wanafamilia walikuwa wamekusanyika katika sherehe ya harusi ya Kiislam, katika eneo la magharibi la Java.

Hata hivyo hali ya wasiwasi ilianza kutanda pale bwana harusi alipowasili peke yake bila ya ndugu na jamaa waliomsindikiza. Pia bwana harusi huyo hakuwa na kitambulisho chochote, zimesema taarifa kutoka Indonesia.

Wasiwasi na mashaka yalizidi pale bwana harusi alipoanza kuzungumza. Sauti iliyokuwa kama ya kiume mara ikaanza kugeuka na kuwa ya kike. "Sauti nzito ghafla ikawa ya kike" amesema mkuu wa polisi wa eneo la Krisnandi. Polisi na wageni waligundua hatimaye kuwa bwana harusi, alikuwa ni mwanamke na hivyo harusi hiyo kusitishwa kwa muda.

Wazazi wa Bi harusi mara moja walimtafuta rafiki wa zamani wa kiume wa bi harusi - yaani ex boyfriend - na kumshawishi amuoe binti yao ili kuokoa jahazi.

Ushoga nchini Indonesia haujapigwa marufuku, lakini ndoa za jinsia moja bado hazijaruhusiwa katika nchi hiyo yenye idadi kubwa ya Waisilam.

Na kwa taarifa yako.... Wanawake hutabasamu zaidi ya wanaume