Wednesday, February 23, 2011

Kwa nini makundi ya wasanii huvunjika?

Tanzania kuna makundi mengi sana ya wasanii, hasa wa filamu, muziki wa kizazi kipya, na ngoma. Makundi haya huwa na malengo ya kuendeleza vipaji vyao na kujipatia ajira. Utakuta kundi limetoa filamu au album yao na kuanza kupata mafanikio. La kushangaza ni pale ambapo baada ya muda mfupi tu wanaanza malumbano, ugomvi na hatimaye kundi kuvunjika. Napenda kufahamu kama kuna mtu ameona au imetokea kwenye kundi lake atuambie sababu ilikuwa nini, na wengine wachangie nini kifanyike ili mambo hayo yasijirudie na hatimaye tuendeleze sanaa na ajira nchini.

No comments:

Post a Comment