Sunday, April 8, 2012

Joyce Banda aapishwa urais Malawi


Makamu wa rais wa Malawi Joyce Banda ameapishwa kuwa rais wa nchi hiyo kufuatia kifo cha Bingu wa Mutharika.
Banda anakuwa rais wa kwanza wa kike kusini mwa Jangwa la Sahara, na aliapishwa mbele ya bunge katika mji mkuu wa Malawi, Lilongwe.
Bi Banda, ambaye alikuwa makamu wa rais tangu mwaka 2009, alishangiliwa na kupigiwa kofi kabla na baada ya shughuli hiyo.
Bw Mutharika, 78, alipatwa na mshtuko wa moyo siku ya Alhamis, ingawa kifo chake hakikuthibitishwa hadi Jumamosi.
Kuchelewa kutangazwa kifo chake kulisababisha wasiwasi kuhusu nani anaongoza nchi hiyo.
Kulikuwa na tetesi kuwa watu wa karibu wa rais Mutharika walikuwa wakitaka kubadili katiba ya nchi ili kuzuia Bi Banda kuchukua madaraka, na badala yake kumpa ndugu yake, Peter Mutharika ambaye ni waziri wa mambo ya nje.
Bi Banda alifarakana na rais Mutharika mwaka 2010 na kuwa mkosoaji mkubwa wa rais. Alifukuzwa kutoka chama cha DPP na kuunda chama chake cha Peoples Party.

Kanumba afariki


MAELFU ya wapenzi wa sanaa ya filamu nchini, alfajiri ya kuamkia jana waliduwaa mithili ya watu waliopigwa sindano ya ganzi baada ya kuenea kwa taarifa za kifo cha ghafla cha msanii namba moja wa filamu nchini, Steven Charles Kanumba (28).

Taarifa za kifo cha Kanumba zilisambaa kwa kasi mithili ya moto katika nyika kavu na kuikuta alfajiri ya jana, ikigeuka kibarua kigumu kwa idadi kubwa ya watu, kusaka stesheni mbalimbali za redio, televisheni mitandao ya kompyuta huku wengine wakihangaika kupiga simu huku na kule, kutafuta ukweli wa tukio hilo,lililotikisa si Tanzania tu bali ukanda mzima wa Afrika Mashariki na Afrika kwa ujumla.


Kanumba alifariki usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake, Sinza Vatican, jijini Dar es Salaam.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Kamanda wa Polisi, Kanda ya Kinondoni, Charles Kenyela, ziinaeleza kuwa kifo cha msanii huyo kilitokana na ugomvi uliotokea kati yake na mpenzi wake ndani ya nyumba yake.

Taarifa za kifo cha Kanumba zilianza kusambaa kuanzia saa 10.00 alfajiri na kuenea kwa kasi ambapo hadi kufikia saa moja asubuhi, mamia ya watu walikuwa wamejazana nyumbani Kanumba kutaka kuthibitisha habari hizo.

Kadri muda ulivyozidi kusogea ndivyo idadi ya watu ilizidi kuongezeka nyumbani kwa msaani huyo ambaye amejizolea umaarufu mkubwa kutoka na filamu zake kuuzwa na kuoneshwa katika vituo mbalimbali vya televisheni, ndani na nje ya nchi.

Miongoni mwa watu waliomiminika kwa haraka nyumbani kwa kanumba jana ni wasanii wa fani mbalimbali nchini,  wanasiasa na viongozi mbalimbali wa Serikali

Chanzo cha kifo chake

Kwa mujibu wa maelezo ya mdogo wake aitwaye Seth ambaye alikuwepo eneo la tukio, alisema kaka yake alishinda nyumbani na baada ya kula chakula cha jioni, alimwambia wajiandae kutoka.

Seth alisema kuwa wakati Kanumba akiwa tayari amejiandaa, walisikia mlio wa gari lifunga breki nje ya nyumba.

Alisema gari hilo lilikuwa limemleta mpenzi wa kaka yake msanii wa filamu, Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu ambaye aliingia ndani na kwenda moja kwa moja chumbani kwa Kanumba.

Baada ya kuingia ndani, muda mfupi alisikia sauti zilizoashiria kuwa kulikuwa na ugomvi kati ya wapenzi hao.

“Ghafla ulizuka mzozo ndani na dakika chache baadaye, Lulu alitoka na kuja kuniambia kuwa Kanumba amedondoka baada ya kujigonga ukutani na kwamba yupo taabani hajitambui,” alisema Seth.

Alisema alipoingia chumbani, alimkuta kaka yake akiwa katika hali mbaya hivyo akaamua kumpigia simu daktari wake, ambaye alipofika na kuwashauri wampeleke haraka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kupatiwa matibabu.

Seth alisema kabla ya kufika Muhimbili  walipitia Kituo cha Polisi cha Oysterbay kupatiwa Fomu ya matibabu (PF3).

Hata hivyo, baada ya polisi kupata maelezo ya awali ya ugomvi huo, walimshikilia Lulu kituoni hapo na kumwacha Seth akimpeleka Kanumba hospitali.

Alisema walipofikia Hospitali ya Muhimbili, madakati waligundua kuwa tayari Kanumba alishaaga dunia.

Kamanda Kenyela

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alisema Kanumba alikufa kutokana na ugomvi uliotokea kati yake na rafiki yake wa kike Lulu.

 "Kanumba amefariki usiku wa kuamkia leo (jana) majira ya saa tisa usiku, kwa kile kilichoelezwa kuwa ni ugomvi kati yake na rafiki yake wa kike anayejulikana kwa jina la Elizabeth Michael 'Lulu' mwenye umri wa miaka 18.

Alisema kabla ya ugomvi huo kutokea kati yao wakiwa chumbani, simu ya Lulu iliita na akaamua kutoka nje kupokea kitendo kilichomuudhi Kanumba.

Kamanda Kenyela alisema Kanumba aliamua kumfuata Lulu nje huku akifoka kwa sauti akitaka aelezwe kwanini alitoka nje kupokea simu huku akimtuhumu kuwa huenda alikuwa akizungumza na mwanaume mwingine.

Aliongeza baada ya Lulu kuona Kanumba akimfuata aliamua kukimbia kutoka nje ya geti , lakini kabla hajafanikiwa kufungua geti, Kanumba  alimkamata na kumrudishwa ndani.

Kamanda Kenyela, alisema Kanumba akiwa amemshikilia waliingia wote chumbani na kufunga mlango.

Hata hivyo, alisema haijulikani nani aliyefunga mlango, ingawa maelezo ya Lulu anadi kuwa aliyefunga mlango ni Kanumba.

Kamanda huyo alisema Lulu anaeleza kuwa baada ya Kanumba kufunga mlango, alimuona akilegea na kujigonga kisogo chake kwenye ukuta wa chumba hicho kabla ya kuanguka chini.

Alibainisha kuwa uchunguzi wa awali unaonyesha kuwa Kanumba alikuwa amekunywa Whisky (pombe kali) aina ya Jacky Daniel, hata hivyo, bado wanachunguza zaidi kujua kama kweli Kanumba alilegea tu na kuanguka, ama alipigwa na kitu kizito kichwani au alisukumwa kwa nguvu na kumfanya aangukie kisogo.

“Uchunguzi ukikamilika tutampeleka mahakamani kwa tuhuma za mauaji,” aliongeza Kamanda Kenyela.

Rais Kikwete atoa pole

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania –TAFF kuomboleza kifo cha Kanumba,

Katika taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, Rais Kikwete ameelezea kushtushwa na kuhuzunishwa na kifo cha msanii huyo ambaye amemtaja kuwa mahiri na mwenye kipaji kikubwa.

“Nimepokea kwa mshtuko na huzuni nyingi taarifa za kifo cha Ndugu Steven Charles Kanumba. Kupitia filamu zake, ameburudisha na kuelimisha jamii yetu kwa namna ambayo haiwezi kupimika. Alikuwa msanii mahiri na mwenye kipaji kikubwa ambaye mchango wake mkubwa katika kuanzisha, kukuza na kuimarisha sanaa ya filamu nchini hautasahaulika,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Rais Kikwete alisema Kanumba ametoa mchango mkubwa kupitia sanaa ya filamu na kutokana na uwezo mkubwa wa kisanii, Watanzania wataendelea kumkumbuka kwa mchango wake.

“Nakutumia wewe Rais wa TAFF salamu zangu za rambirambi na kupitia kwako kwa wasanii wote wa filamu na sanaa nyingine kufuatia msiba huu mkubwa kwa fani yetu ya sanaa.

Mama wa Kanumba azungumza

Mama mzazi wa Kanumba, Flora Mutegoa amesema alizungumza na Kanumba kwenye simu saa chache kabla ya kifo chake, huku akimtaka arudi Dar es Salaam haraka, kutoka Kagera alikokwenda kumsalimia mama yake (bibi wa Kanumba), ili aje amuage kabla hajasafiri kwenda Marekani.

 Akizungumza na Mwananchi Jumapili jana katika Uwanja wa Ndege wa Bukoba wakati akijiandaa kusafi kwenda jijini Dar es Salaam, Flora alisema alizungumza na mwanawe  kwa simu usiku huo huo saa chache kabla ya kufikwa na mauti kumkuta.

Mama huyo ni mzaliwa wa Kijiji cha Itoju, Kata ya Izigo, Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera lakini kwa sasa anaishi  Dar es Salaam .

 "Mwanangu niliongea naye usiku akiwa mwenye furaha na tulitaniana sana,alisema anatuma nauli nirudi Dar es Salaam tuagane, kwani alikuwa na safari ya kwenda Marekani,"alisema Flora.

 "Sina cha kuongea naomba mniombee katika kipindi hiki kigumu jana nimeongea naye kwenye simu leo naambiwa mwanangu amekufa,"alisema huku akibubujikwa machozi.
Aliongeza kuwa Kanumba aliwahi kumdokeza kuhusu ndoto zake za baadaye kuwa alikuwa na matarajio ya kufika mbali zaidi katika sanaa ya uigizaji.

Maneno ya mwisho ya Kanumba

Siku za hivi karibuni Kanumba alikuwa akichapisha habari mbalimbali katika mitandao ya kijamii zilizokuwa zikisisitiza  upendo.

Katika mtandao wake wa Twiter na Blog yake  juzi saa sita mchana alichapisha habari akiwasi watu kufanya mambo mema kwa watu wengine ili wapate baraka.

"Tunavyofanya kwa ajili yetu huwa yanakufa nasi, lakini tunayoyafaya kwa ajili ya wengine hubaki duniani," sehemu ya maneno yake ya mwisho aliyoyaweka katika Balog yake juzi kabla ya kifo chake .


Mbali na ujumbe alioandika siku moja kabla ya kufikwa na mauti, Kanumba amekuwa akichapisha katika mitandoa yake ya kijamii maneno ya busara na kukemea chuki miongoni mwa jamii tangu mwanzoni mwa mwaka huu.

Maneno ya mwisho kwa wasanii wenzake

Kanumba mbali ya kutoa maneno ya busara kwa jamii, pia alikuwa akitumia mitandao yake kutoa maneno ya kuwapa moyo wasanii wenzake.

Kwa mfano Januari 24 mwaka huu baada ya kutwaa Tuzo ya ZIFF, aliandika kwenye mtandao maneno aliyoyaelekeza kwa wasanii wenzake akisema,:

 "Maneno yangu ya mwisho, hata tukiwa na uwezo wa kuhamisha milima kama hatupendani katika tasnia ni kazi bure,kile kilicho moyoni ndio kioneshe usoni na si vinginevyo".

"Kama wanichukia moyoni basi onyesha usoni na kama wanipenda moyoni basi onyesha usoni na si vinginevyo,Isiwe moyoni wanichukia halafu usoni wanichekea,Hii sanaa ni karama tuliyobarikiwa na Mungu tuitumie vyema kwa ajili ya utukufu wake maana ipo siku atatuuliza na kutudai,kama katupa bure basi anao uwezo wa kutuny'ang'anya pia','soma Wakorintho uone jinsi Mungu alivyogawa karama hizi na ni kwanini katugawia." sehemu ya maneno yake kwa wasanii wenzake nchini.

Mamia wafurika nyumbani kwake

Mamia ya watu jana walifurika nyumbani kwa msanii huyo kiasi cha barabara ya Sinza Uzuri inayopita karibu na nyumba hiyo kufungwa.

Watu kutoka kona mbalimbali za jiji la Dar es Salaam baadhi yao wakiwa wanabubujikwa, machozi walifika kushuhudia kwa macho yao kile wanachokisikia kwenye vyombo vya habari. Kulikuwa na msongamano mkubwa pia wa magari katika eneo hilo.

Historia yake

Kanumba alizaliwa Januari 8, 1984  mkoani Shinyanga,  ni mtoto wa tatu katika familia yao akiwa na dada zake wawili.

Alisoma Shule ya Msingi Kaboya, mjini Bukoba na baadaye akahamia Shinyanga ambako alimalizia elimu yake ya msingi katika Shule ya Bugoi.

Alijiunga kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari, Christian Seminari iliyopo Kongowe na baadaye akaendelea na masomo ya kidato cha tano na sita katika Shule ya Sekondari ya Jitegemee.

Dada wa marehemu

Dada wa marehemu, Abela Kajumolo alisema kuwa mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Sinza Vatican.

Alisema familia imepanga mazishi ya Kanumba yatafanyika Jumanne wiki ijayo na kwamba bado hawajaamua kama atazikwa Dar es Salaam au Bukoba," alisema.

Tayari kamati ya mazishi imeundwa na ikiwajumuisha Gabriel Mtitu,  Stephen Jacob (JB) William Mtitu na Issa Mussa (Cloud) ambao wote ni wasanii wa filamu nchini.

Kamati ya usafiri itakuwa na Meneja wa  Clouds Media Group,  Ruge Mutahaba na Vincent Kigosi (Ray).

Enzi za Uhai wake

Marehemu alianza uigizaji miaka ya 2000 akiwa na Kundi la Kaole na baadaye kuingia katika fani ya filamu wakati huo akifanya kazi zake chini ya Kampuni ya Game First Quality.

Hata hivyo, alifanya kazi na kampuni hiyo hadi alipofanikiwa kumiliki kampuni yake binafsi ya Kanumba The Great Film.

Marehemu Kanumba pia ameshirikiana na wasanii wakubwa barani Afrika katika uingizaji akiwamo Ramsey Nouah wa Nigeria ambaye amecheza naye filamu ya Devil’s Kingdom na ambayo imezinduliwa mapema mwezi huu nchini Ghana.

Pia hadi mauti yanamkuta, Kanumba alikuwa akiendelea kutengeneza filamu ya Ndoa yangu ambayo alikuwa akiiandaa na mwigizaji mahiri wa kike, Jackline Wolper.

Kuingia kwenye siasa

Marehemu Kanumba pia katika siku za hivi karibuni aliwahi kukaririwa akisema atagombea Ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, akini hakuweka bayana kupitia chama gani wala jimbo.

Kanumba amekuwa  msanii wa kwanza nchini kuitangaza Tanzania ndani na nje ya bara la Afrika kupitia filamu.

Wasanii wenzake wanasemaje?

Suzan Lewis maarufu kama 'Natasha'  ambaye ni msanii mkongwe anasema kifo cha Kanumba kimemwachia kumbukumbu ambayo haiwezi kusahaulika.

“Nitamkumbuka Kanumba daima katika maisha yangu, alikuwa ni mtu wa watu alikuwa ni msanii pekee aliyepiga hatua na kuishi maisha ya wasanii wa kimataifa.

Yvonne Cherryl (Monalisa): “Kifo cha Kanumba kimefifisha ndoto zangu za kuigiza pamoja na wasanii maarufu kutoka Hollywood, tulikuwa na maandalizi hayo na Kanumba ndio alikuwa kila kitu katika suala hilo sikutegemea kama hili lingetokea.”

Wema Sepetu: "Siamini, na sitaki kuamini kabisa, nipo ndotoni sijui niseme nini,"alisema Wema huku akiangua kilio kilichomfanya ashindwe kuendelea kuongea.

Hatman Mbilinyi: " Alikuwa ni mcheshi sana, alipenda watu waliofanya naye kazi, nimepokea kwa ugumu, siamni kwa sababu ni saa chache tu tulikuwa pamoja, hakuumwa ni bora angeumwa tukajua aliumwa."

Jerison Tegete ambaye ni Mchezaji wa Yanga alisema alikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kupata habari za msiba, na kwamba ameguswa sana na kifo cha Kanumba.

"Inasikitisha sana kwani tumepoteza kijana mdogo na ambaye alikua na nafasi kubwa katika kuielimisha jamii kupitia filamu zake.
Single Mtambalike maarufu Richie alisema ana mwachia Mungu kuhusu kifo cha Kanumba. "Sijui nizungumze vipi kuhusu marehemu kwanza siamini kama kweli Kanumba hatutakua naye katika tasnia hii na si filamu tu hata katika kazi nyingine ambazo tumekua naye karibu yote namwachia Mungu.”

Jacob Steven  amarufu JB alisema ni vigumu kuamini kuwa kanumba kafa kwa vile saa chcahe walikuwa pamoja.

“Ni pigo lisiloelezeka kwa sasa na ni vigumu kuamini kilichotokea kwani saa chache kabla ya kifo chake tuliwasiliana na alioongea kwa furaha bila kutambua nini kitatokea mbele yake katika muda mchache ujao.”

Tangana Iringa wamlilia
Naye Burhani Yakub kutoka Tanga anaripoti kuwa waandaaji wa filamu wa Mkoa wa Tanga wameleza kuguswa kwao na taarifa za kifo cha Kanumba na kuwataka wasanii wa tasnia hiyo kuwa watulivu katika kipindi hiki cha majonzi.
Wakizungumza na Mwananchi Jumapili mara baada ya kusikika taarifa za kifo cha Kanumba jana asubuhi, walisema kifo cha Kanumba ni pigo kubwa kwa tasnia hiyo nchini.
Mtunzi Mkongwe  wa riwaya na mwandishi wa hadithi za Filam wa Jijini Tanga, Faki A. Faki  alisema taarifa za kifo cha Kanumba zimeshtua kwa kuwa ni msanii aliyeikuza sanaa ya filamu nchini.

Tumaini Msowoya anaripoti kutoka Iringa kuw Tumaini Msowoya, Iringa
Wakazi wa Mkoa wa Iringa wakiwamo wasanii wa filamu wamesema kuwa wamepokea kwa masikitiko msiba wa msanii nyota wa filamu Tanzania, Steven Kanumba na kwamba taifa limepata pigo kwa kumpoteza mtu muhimu aliyeweza kutangaza filamu za Kitanzania ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya maduka, kati kati ya mji wa Iringa wameamua kuomboleza kifo cha msanii huyo kwa kutoa nje televisheni zao ili kusaidia watu kuona filamu ambazo zimeigizwa na msanii huyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wananchi hao walisema msiba huo umewashtua na kwamba msanii huyo alikuwa na mchango mkubwa kwenye sanaa sanaa kupitia filamu zake.
Katibu wa kundi la sanaa la Mundu, mkoani Iringa, Athanas Kipera alisema hata kundi lake limepata mchango mkubwa kutoka kwa marehemu Kanumba.

Basata wahuzunika
Katibu Mkuu wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) amesema kuwa baraza lake limepokea kwa masikitiko makubwa  kifo cha Kanumba.
"BASATA inaungana na familia za wafiwa na wasanii wote nchini kwa maombolezo  ya msiba huu mkubwa na wa kihistoria, kufiwa na msanii huyu mahili kwenye tasnia ya filamu ni pengo kubwa kwa familia, Sekta ya sanaa na Taifa kwa ujumla kutokana na ukweli kuwa, aliweza kuutangaza utamaduni na sanaa yetu nje ya mipaka,"alisema Gonche Materego ambaye ni katibu mkuu wa Basata.

Alisema Kanumba atakumbukwa kwa moyo wake wa kujituma na kuthamini kazi ya Sanaa toka akiwa Kundi la Maigizo la Kaole ambapo moyo wake huo ulimfanya awe miongoni mwa wasanii walioleta mageuzi kwenye tasnia ya filamu kwa kuifanya kuanza kupendwa na wadau wengi zaidi.

Police to probe 'Chapel Party' incident

The police are investigating the 'Chapel Party' incident which caused an uproar this week due to the provocative images used to promote it
In a statement released to the media, the Ministry of Home Affairs (MHA) noted that the event had been cancelled but said investigations will be conducted as a police report has been made against the organisers for putting up insensitive advertisements that could have offended the Catholic faith.
It said that if the event had been carried out as originally publicised, the organiser could also have breached one of the conditions of its licence and be liable for sanction.
Its licence could also be revoked.
"While organisers can be creative in organizing events, there is no excuse for breaking the law, or for insulting or denigrating any racial group or religion in Singapore.
"MHA does not condone any behavior that denigrates any religion in Singapore. Mutual respect, tolerance and restraint are critical to maintaining communal peace and harmony in our multi-ethnic, multi-religious society," the statement said.
The organisers had used an image of two young women dressed in skimpy nun-like habits. While habits normally cover the whole leg, the outfits the women wore were shorter than mid-thigh length.
It was posted on the Facebook page of 'Escape Chapel Party', with the caption "A sneak peek at what some of our girls will be wearing on the 7th of April."
The page also featured an event poster, with a woman also dressed in a habit-like outfit.
The page was set up two to three weeks ago by events organiser Creative Insurgence. The party is organised by the company and Escape, a club from Swansea in Britain.

Friday, April 6, 2012

Men get high from hiring wild young students


He has 10 girls in his books who are young students and there is hot demand for them.
William (not his real name) runs an online "escort service" pairing up male clients with young women for dates.
Business, he tells The New Paper on Sunday, is "good": He gets up to 20 requests per week for his stable of students, some of whom are as young as 18.
He has heard of call girls even younger, but the industry has become very cautious recently and they've stopped taking bookings for women who are "too young".
William says: "The recent police action has made me very careful about the way I work."
He is referring to the online vice ring bust last December.
About 60 men were arrested and later released on police bail. They are accused of having had sex with a "social escort".
Prostitution is legal here, but it is a crime to solicit by approaching a customer or promoting the trade. This also means it is an offence to be a pimp.
It is also illegal to have paid sex with a girl under 18. Anyone who does so may be jailed for up to seven years, fined up to $10,000, or both.
Anyone who makes or organises travel arrangements for another person to engage in paid sex with someone under 18 outside Singapore is also committing a crime.
In William's case, he's careful not to include underage girls in his books, though he knows that the demand for them is "high".
But having young girls in his stable is not without its headaches.
"Sometimes, these girls are busy with school, so I have to know who is available and make the recommendations to the customers," he says.
It is understood these girls are Singaporeans and studying in tertiary institutions.
"But the truth is these young girls don't stay in the business for very long and only do it when they need the money," he adds.
The price for their services ranges from $200 to $800 and is set by the girls themselves.
He also claims that the girls in his stable are all acquaintances introduced to him "by friends because they want to earn extra cash".
These friends, he claims, would forward them his contacts. Most of his dealings with these girls are via SMS, he adds.
Pimps, however, are known to recruit the young women through advertisements online.
But while some escorts prefer to have someone like William making their arrangements, some - like Celine (not her real name) - prefer to work alone.
That way, she's less likely to be implicated in any vice busts.
"Working alone also give me the chance to pick and choose my own clients," says the attractive 19-year-old, who is charming and exudes a confidence which attracts a lot of male attention.

Was a 22-year-old woman raped by a man she met at a nightclub or did she have sex with him willingly?

 
That was the issue before the High Court on Friday when it heard the appeal of convicted rapist Ong Ming Wee, 29, who is fighting his conviction and sentence of seven years' jail and eight strokes of the cane for rape.

He had failed to convince a district court during the trial last year that the woman had consented to having sex hours after they met at Zouk disco in 2009.

On Friday, his lawyer Subhas Anandan argued that the woman, who cannot be named, had consented to sex.

Mr Anandan pointed out that surveillance footage in the club showed that she had danced very closely to his client, who felt that she was trying to seduce him.

The lawyer said the pair had kissed during the taxi ride back to Ong's Toa Payoh flat after leaving the club. Mr Anandan said she was crying rape only because Ong threw her out after they had sex and she was angry at being treated as a tool.

He added that Ong - who helps run a family-owned mini-mart in Toa Payoh North - did not use violence or any weapon against the woman.

But Deputy Public Prosecutor Leong Wing Tuck pointed out that the rape took place more than two hours after the dancing and there was a 'cooling-off period'.

While Ong had not used physical violence or threatened her explicitly, he was in a position of dominance over the woman, who was intoxicated, said the DPP.

The DPP pointed out that Ong had told her that he would allow her to make a phone call to her mother if she had sex with him; this showed he was in control.

The DPP said the woman's mindset was that of a 'trapped animal' and that she was 'overawed into submitting' to Ong.

Justice Quentin Loh reserved judgment.

However, he told both sides to make written submissions on a provision in the Penal Code which states that a person has not committed an offence if he had acted in mistaken belief.

Teacher's party lifestyle draws parent's concern


Photo: Stomp
SINGAPORE - A Physical Education (PE) teacher who posted photographs of his clubbing exploits on Facebook has drawn the ire of a parent.
In a posting on citizen journalism website Stomp, the parent, identified only as Anon, said she stumbled upon the teacher's profile when her daughter forgot to log out of the social media site.
The pictures she saw showed the teacher posing with various female companions, some with their arms around him.
The parent was upset that the teacher was pictured regularly with various female companions.
The parent said, "He had many photographs taken when clubbing and with different girls (seemingly of different nationalities) on different days in his profile pictures and mobile uploads which have attracted likes and comments from students.
"Exactly what message is he trying to send across with those photos on his profile?"
The parent's comment seems to have drawn the flak of netizens who have jumped to the teacher's defence.
A Stomp reader by the moniker of 'blackjix' said: "Over here you are complaining about the teacher taking photos with women and you invade your daughter's privacy.
"Look at yourself before you complain about others. Did you discuss with your daughter regarding this issue?"
Another known as SingaporeanMummy also voiced concern about the parent not respecting the teacher's privacy, "Teachers are humans too and need to enjoy themselves outside of work.
"They do not need to stress about how their students have done badly, misbehaving in class or getting complaints from parents all the time!"
But Anon does not stand alone with her views.
Another Stomp reader, princess11 believes that the teacher should have better protected himself by keeping his personal life, well, personal.
"The teacher must know what to post when there are children around. It is common sense.
"He could have created a separate Facebook account for his personal life."

Woman receives kidney from husband's lover

unbelievable organ transplant stories


Recently, the world's largest series of organ transplants took place, where 60 patients exchanged 30 kidneys in a domino chain of events across 11 states in the US.
The arrangement involved a number of people agreeing to give a kidney to a stranger in return for their sick relative receiving one matching their blood and antibody type.
Think the strange tale is like an episode right out of popular hit show "House"?
If this makes your jaw drop, read on for more unbelievable organ transplant stories, compiled by oddee.com:

1. Woman receives kidney from husband's lover
When a 34-year-old Turkish woman discovered that she would die without a kidney transplant, her unlikely saviour came in the form of her husband's mistress. 
Meliha Avcı's kidneys had both failed her 12 years ago, resulting in the need for dialysis three times a week, four hours per session.
During this time, her husband of 16 years, Mehmet Avcı, met another woman while accompanying his wife on a hospital trip.
After getting to know 34-year-old Ayse Imdat, Mehmet asked her to move to his mother's home, under a pretence that she was the new babysitter for the couple's son.
After his wife found out about the affair, she pleaded with her husband to marry Imdat after she died.
As Meliha's condition continued to deteriorate, Imdat made the suggestion that Meliha be saved with one of her kidneys, as the two women shared the same blood type.
Upon Imdat's insistence that she take her kidney, Meliha agreed.
"We shared a husband, and now we shared a kisney," she reportedly said.
She added that she has her husband and Imdat to thank for completely changing her life. Imdat on her part has promised to continue taking care of Meliha after the surgery.

Woman dies after being hit by SBS bus


SINGAPORE - A 66-year-old woman has died after being hit by a SBS bus this morning at the junction of Sengkang Eastway and Compassvale Road.
According to The Straits Times, the unnamed woman was dragged under the bus for nearly half a minute before motorists alerted the bus driver and the bus stopped.
Eyewitnesses say the bus driver then got on the phone. After which, he told the bus passengers to disembark the bus. This happened about two to three minutes after the bus had stopped.
Reports say she was crossing the road when she was hit by the bus which was making a right turn at the junction.
The Singapore Civil Defence Force (SCDF) and police told AsiaOne that they received a call at 11.20am regarding an accident between a bus and a pedestrian.
SCDF said that an ambulance arrived at the scene in five minutes, but the woman was pronounced dead at 11.35am.
According to news reports, eyewitnesses said the woman was was run over by SBS Transit Bus service 159. Shin Min Daily News said she was dragged for almost 10m under the bus before it stopped.
Her legs were also crushed. She was bleeding profusely.
Police investigations are underway.
SBS Transit said it is very saddened by the incident and extends its deepest condolences to the family of the victim.
It also said it will try and extend all possible assistance to them during this very difficult time.
A spokesperson for the company also said the bus driver has been suspended with immediate effect and is assisting with the investigations.

Bingu wa Mutharika afariki dunia


Rais wa Malawi Bingu wa amefariki dunia baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo, akiwa na miaka 78. Duru kutoka kwa serikali zimethibitisha kifo hicho kwa BBC. Mwili wa wa kiongozi huyo umepelekwa Afrika Kusini. Hata hivyo serikali haijatoa taarifa rasmi kuhusu kifo cha Wa-Mutharika. Mmoja wa madaktari waliokuwa wakimhudumia kiongozi huyo ameambia BBC, Wa-Mutharika alikufa baada ya moyo wake kusimama.
Wadadisi wameonya kifo cha rais huyo huenda kikazua mgogoro wa uwongozi. Katiba ya nchi inampa nafasi Makamu wa Rais kuongoza nchi endapo Rais atafariki au kuugua kiasi cha kushindwa kuongoza taifa.Hata hivyo Makamu wa Rais nchini Malawi, Joyce Banda alitofautiana na Wa-Mutharika kufuatia mzozo wa urithi wa uongozi ambapo alifukuzwa kutoka chama tawala,Democratic People's Party (DPP).
Kakake rais ambaye ni Waziri wa mambo ya nje Peter Mutharika aliteuliwa kugombea urais hapo mwaka wa 2014.Mwandishi wa BBC mjini Blantyre Raphale Tenthani amesema mawaziri wamekuwa na kikao usiku mzima kujadili hali ya sasa. Rubaa za serikali zimenukuliwa zikisema kwamba maiti ya Rais imesafirishwa Afrika Kusini huku maafisa wakitafakari hali ya sasa.
Bingu wa Mutharika aliingia madarakani mwaka wa 2004. Baadaye alikihama chama chake cha United Democratic Front (UDF) kwa tuhuma za wanachama kuhujumu harakati za kupambana na ufisadi. Alichaguliwa tena mwaka 2009, lakini katika siku za karibuni wakosoaji wake wamemlaumu kwa kuegemea sera za kiimla.
Rais huyo alikumbwa na shinikizo za kuachia madaraka kwa tuhuma za kupendelea ukoo wake, na kuharibu madaraka.Wa Mutharika aliwakera wafadhili wa kigeni hasa baada ya kumfukuza balozi wa Uingereza Fergus Cochrane-Dyet, na kufanya utawala wa Uingereza kusimamisha msaada kwa Malawi.

Pigo Chadema


LEMA AVULIWA UBUNGE ARUSHA MJINI, JAJI AMZUIA KUGOMBEA MIAKA MITANO, VILIO MAHAKAMANI
Waandishi Wetu, Arusha
MAKAHAMA Kuu Kanda ya Arusha,  imetengua matokeo ya ubunge yaliyompa ushindi mgombea wa Chadema, Godbless Lema baada ya kuridhika kuwa alitumia lugha ya kashfa na udhalilishaji dhidi ya aliyekuwa mpinzani wake katika uchaguzi huo wa mwaka 2010, Dk Batilda Burian.

Lema ni mbunge wa nne nchini kuvuliwa ubunge na mahakama katika kipindi cha miaka 16 iliyopita kutokana na kasoro zilizojitokeza katika mchakato wa uchaguzi.

Akisoma hukumu yake jana iliyochukua zaidi ya saa nzima, Jaji Gabriel
Rwakibarila alimtia hatiani Lema kwa makosa mawili kati ya manne
aliyokuwa akikabiliwa nayo, huku akitupa mawili kwa kukosa ushahidi.

Ndani ya ukumbi wa mahakama uliojaa wanachama, wafuasi na wapenzi wa Chadema, Jaji Rwakibarila alimvua ubunge Lema baada ya kuridhika na ushahidi kuwa alitumia maneno ya kashfa na ubaguzi wa jinsia dhidi ya aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk Batilda Burian.

Jaji Rwakibarila katika hukumu yake hiyo, pia alimwamuru Lema kulipa gharama za kesi hiyo na kwamba ana haki ya kukata rufaa ikiwa hajaridhika na hukumu hiyo.

Uamuzi wa Jaji huyo ni kama umetia doa shamrashamra za Chadema ambazo zilikuwa zikiendelea baada ya chama hicho kushinda kiti cha ubunge katika uchaguzi mdogo wa Arumeru Mashariki, kupitia kwa mgombea wake, Joshua Nassari.

Makosa ya Lema
Lema alitiwa hatiani kwa kudaiwa kusema kuwa Dk Burian hakustahili kuchaguliwa kuwa mbunge kwa sababu mila na desturi za makabila ya Waarusha (Wamaasai na Wachaga), mwanamke hawezi kuongoza wazee.

Sababu ya pili aliyotumia Jaji kutengua ubunge wa Lema kutoa maneno ya kashfa dhidi ya Dk Burian kuwa ni mwanamke asiye mwaminifu, aliyezaa nje ya ndoa na alikuwa na mimba nyingine na bwana huyo aliyezaa naye ambaye siyo mumewe.

Jaji Rwakibarila alitupilia mbali madai mawili ya kutumia lugha na maneno yenye mwelekeo wa ubaguzi wa kidini na ubaguzi wa makazi.

Kuhusu ubaguzi wa kidini alikataa madai ya walalamikaji Mussa Mkanga,
Agness Mollel na Happy Kivuyo kuwa kauli ya Lema kuwataka wapiga kura wa Arusha kujihadhari na wanaovaa vitambaa na hijabu wasije kujikuta wanachagua Al Qaida kuwa haihusiani na dini ya Kiislamu.

“Mwanamke kuvaa kitambaa kichwani haina uhusiano wowote na dini ya
Kiislam wala Al Qaida kwani ni dhahiri wanawake wengi ambao baadhi yao
siyo Waislam wanavaa vitambaa. Kwanza ni heshima kwa wanawake kuvaa vilemba hivyo madai haya nayatupilia mbali,” alisema Jaji Rwakibarila katika hukumu yake.

Kuhusu tofauti ya ukaazi kati ya Lema na Dk Burian aliyedaiwa kuolewa
na kuishi Zanzibar, Jaji huyo alisema hoja hiyo isingeharibu wala kwenda
kinyume na maadili ya kampeni kwani kisheria Mtanzania ana haki ya
kuishi upande wowote wa Jamhuri ya Muungano, yaani Bara na Visiwani.

Katika shauri hilo namba 13/2010, wadai waliowakilishwa mahakamani na Mawakili Alute Mughwai na Modest Akida, waliomba mahakama kutengua matokeo yaliyompa ushindi Lema kwa madai kuwa alitumia lugha na kauli za matusi, kashfa na udhalilishaji dhidi ya Dk Burian wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu uliopita.

Jaji Rwakibarila alisema baada ya kupitia ushahidi wa mashahidi 14 wa
upande wa wadai na wanne wa upande wa utetezi, aliridhika kuwa Lema alitamka maneno ya kibaguzi, kijinsia na kashfa dhidi ya Dk Burian katika mikutano yake minane ya kampeni kati ya mikutano zaidi ya 60 aliyofanya.

Kabla ya kuanza kusikilizwa mbele ya Jaji Rwakibarila, shauri hilo
lilikuwa mbele ya Jaji Aloyce Mujulizi aliyejitoa baada ya Lema kueleza kutokuwa na imani naye kutokana na wabunge wa Chadema kuwahi kuituhumu kampuni yake ya uwakili ya IMMA aliyokuwa akifanyia kazi
kabla ya kuteuliwa kuhusika na ufisadi wa akaunti ya EPA katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT)

Jaji Rwakibarila alianza kusikiliza shauri hilo mfululizo kuanzia mapema Februari kutokana na kutakiwa kulimazika kabla ya Mei 3, mwaka huu kutokana na mahitaji ya kisheria inayoelekeza kesi za uchaguzi zisikilizwe na kuamuliwa ndani ya mwaka mmoja tangu kufunguliwa.

Licha ya kuibuka washindi kwa uamuzi wa Jaji jana, wadai katika shauri
hilo pamoja na mawakili wao walionekana kupigwa bumbuwazi mahakamani bila kuamini kilichotokea hadi watu walipoanza kuondoka baada ya Jaji kutoka ndipo waliposimama na kuanza kukumbatiana na kupongezana.

Baada ya mwaka mmoja kukamilika Novemba, mwaka jana, Msajili wa Mahakama Kuu, Herbert George aliandika barua kwa Waziri mwenye dhamana ya sheria ambaye aliongeza kipindi cha ziada cha miezi sita
kinachomalizika Mei 3, mwaka huu.


Mkanganyiko kwenye hukumu

Jaji Rwakibarila kwa upande mwingine anadaiwa kujichanganya katika vifungu vya sheria alivyotumia katika uamuzi wake.

Akitoa uamuzi wake jana, Jaji huyo alisema Lema alithibitika kutenda kosa la kutumia maneno yasiyostahili kwenye kampeni zake za Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.

Kwa kauli ya kisheria, Jaji alisema Lema anatiwa hatiani kwa kosa la
‘Illegal Campaign’ kwa kutoa kauli za kumbagua kijinsia Dk Burian
akitumia tofauti yao ya kimaumbile ya yeye kuwa mwanamme na mwenzake mwanamke aliposema mila na desturi za Waarusha na Wachaga haziruhusu mwanamke kuongoza wanaume.

Alisema hata kauli ya Lema kuwa Dk Burian siyo mwanamke mwaminifu
aliyezaa nje na kupata mimba nje ya ndoa ilikuwa ya kashfa dhidi ya
mgombea huyo wa CCM na kutafsiri kosa hilo kama ‘Illegal Campaign’
aliyosema inatosha kutengua matokeo ya uchaguzi.

Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi, makosa yote mawili yanaangukia
kwenye kifungu cha 108, kifungu kidogo cha pili aya ‘A’ ambayo
humruhusu aliyevuliwa ubunge kugombea kwenye uchaguzi mdogo
utakaoitishwa.

Lakini katika majumuisho ya hukumu yake, Jaji Rwakibarila alitumia
kifungu cha 114 cha sheria ya uchaguzi inayozungumzia “Illegal
Practice” ambayo yanaangukia kwenye makosa yanayohusiana na vitendo vya rushwa kwa wapiga kura, watendaji wa Serikali na watumishi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Wakili wa Lema, Method Kimomogoro  alithibitisha utata huo na kusema atafuatilia kujua iwapo Jaji Rwakibarila alijichanga katika kutaja vifungu hivyo vyenye maana na adhabu tofauti kisheria.

“Anayehukumiwa kwa makosa yanayoangukia kwenye kifungu cha 108 (II) (A) kama ilivyotokea kwa mteja wangu (Lema) anaruhusiwa kugombea kwenye uchaguzi, lakini kwa mshangao wakati akihitimisha hukumu yake jaji alitaja kifungu cha 114 ambacho ni kinyume na makosa aliyokutwa nayo Lema,” alidai Wakili Kimomogoro.

Bila kutaka kuingia kwa undani katika suala hilo hadi atakapopata
nakala ya hukumu hiyo, Kimomogoro alidai hadi jana jioni alikuwa
hajapata maelekezo yoyote kutoka kwa mteja wake kuhusu hatua za
kuchukua dhidi ya uamuzi huo.

Kimomogoro alieleza kuwa iwapo hukumu hiyoitaachwa kubakia kwenye kifungu hicho cha 114 ina maana mteja wake Lema hataruhusiwa kugombea ubunge kwa kipindi kisichopungua miaka mitano, jambo ambalo siyo haki kwa sababu hakushtakiwa wala kukutwa na hatia ya kujihusisha na rushwa wakati wa kampeni.

Kwa upande wake, wakili wa wadai Alute Mughwai aliyekuwa akisaidianana Modest Akida alieleza kuridhishwa na uamuzi huo ingawa aliahidi kuwasiliana na wateja wake kuangalia uwezekano wa kukatia rufaa hoja mbili za ubaguzi kimakaazi na kidini zilizotupwa na mahakama.

Happy Kivuyo aliyekuwa mdai wa tatu katika shauri hilo nambo 13/2010
alieleza kufurahishwa na hukumu hiyo aliyodai imewatendea haki wote
waliochukizwa na matusi, kashfa na udhalilishaji uliofanywa na Lema
dhidi ya Dk Burian.


Kauli ya Mbowe
Mwenyekiti wa  Chadema, Freeman Mbowe, amevitaka vyombo vyenye Mamlaka ya Maamuzi nchini, ikiwepo Mahakama kusoma alama za nyakati kabla ya kutoa uamuzi ambao unaweza kusababisha nchi kuingia katika machafuko.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi za Chadema Mkoa wa Arusha, eneo la Ngarenaro, kuhusu hukumu ya Jaji Rwakibarila, Mbowe alisema ni hatari pale watu wanapoanza kutilia shaka vyombo vya uamuzi kama Mahakama Kuu.

“Sitaki kuingilia uamuzi ya mahakama, lakini ni kweli kuwa uamuzi wa hukumu hii ulivuja hata kabla ya kusomwa, tulipewa taarifa za ubunge wa Lema kutenguliwa, sasa hili ni jambo la hatari kama tutaendelea kuvujisha uamuzi wa kisheria, nchi inaweza kuingia kwenye machafuko pale watawala wanapoingilia vyombo vya kisheria,”alisema Mbowe.

Alisema Serikali na vyombo vingine vyenye Mamlaka, ni lazima wajue kuwa, enzi za kuwaburuza watu zimepitwa na wakati.

“Mahakama zisifikiri zinaweza kufanya kila ambacho zinataka bila kuzingatia, sheria, taratibu na matakwa ya  umma, mimi sitaki tukife huko,”alisema Mbowe.

Alisema katika kesi hiyo ya Lema, wanaamini uamuzi ya mahakama umeingiliwa na chombo kingine jambo ambalo ni hatari katika utawala wa Sheria.

Kukata rufani
Kuhusu Chadema kuukatia rufaa uamuzi wa Lema kuvuliwa ubunge, Mbowe alisema bado wanasubiri nakala ya hukumu ya kesi hiyo na wanafanya majadiliano kupitia mawakili wa chama hicho na viongozi wengine na kisha watatoa uamuzi ambao utatangazwa kesho Jumamosi kwenye mkutano wa hadhara.

Mbowe alisema, ingawa wananchi wengi wa Arusha wanataka kurejewa haraka kwa uchaguzi, lakini, hawafahamu kama Mbunge wao Lema, kulingana na hukumu hiyo ataruhusiwi kugombea tena.

“Kabla ya kufikia uamuzi wowote  tumeona ni busara kwanza, tukae kwani Lema ambaye wanamtaka kwa hukumu hii ni lazima tukate rufani,”alisema Mbowe.

Hata hivyo, aliwaomba wananchi wa Arusha, kutulia kwa sasa na kutofanya vurugu zozote ili kuthibitisha Chadema sio chama cha vurugu na ni chama cha wanademokrasia wa kweli.

Alisema katika mkutano wa Jumamosi, watatoa tamko la pamoja kama watakata rufani au watatoa nafasi kwa wanachama wengine wa Chadema kujitokeza kumrithi Lema.

Kabla ya kukutana na waandishi wa habari, Mbowe alizungumza na mamia ya wakazi wa Jiji la Arusha nje ya Uwanja wa ofisi za Chadema, ambao pia aliwataka kutulia wakati chama hicho kinatafakari uamuzi wa kuchukua.

Chaguzi zilizowahi kutenguliwa
Mwaka 1996 aliyekuwa mbunge wa Temeke, Ramadhani Ali Kihiyo alivuliwa ubunge baada ya Mahakama kumtia hatiani kwa kosa la kughushi cheti na nafasi yake ilichukuliwa na Augustine Mrema, wakati huo akiwa Mwenyekiti wa Chama cha NCCR- Mageuzi.

Vivyo hivyo Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba ilitengua ubunge wa aliyekuwa mbunge wa Biharamulo Magharibi kwa tiketi ya Chama Cha Tanzania Labour (TLP), Phares Kabuye.

Kabuye aliyefariki dunia kwa ajali ya gari akiwa njiani kuelekea jijini Dar es Salaam, alivuliwa ubunge baada ya mahakama kuthibitisha kuwa katika mchakato wa uchaguzi mwaka 2005, alimdhalilisha mgombea mwenzake, Anatoly Choya.

Desemba 28, 2007 Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, kupitia kwa Jaji Josephat Mchome ilitengua matokeo ya aliyekuwa mbunge wa Mwibara Charles Kajege kutokana na kutiwa hatia kwa rushwa.

Kesi ya kupinga matokeo ya hayo ilifunguliwa na aliyekuwa mgombea wa jimbo hilo kupitia TLP, Mtamwega Mgaywa, (TLP) aliyeshindwa katika Uchaguzi Mkuu wa 2005.

Hata hivyo, Septemba 25, 2009, Mahakama ya Rufaa chini ya majaji watatu, wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania wakati huo, Agustino Ramadhani, January Msofe na Jaji Mbaruku, walimrejeshea Kajege ubunge kutokana na rufaa aliyokata dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu.