Monday, August 8, 2011

Chadema yafukuza madiwani 5 Arusha

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imewafukuza uanachama madiwani watano wa chama hicho mkoani Arusha kwa kutotekeleza maagizo ya kamati hiyo na hivyo kuweka wazi kata tano za mkoa huo kwa ajili ya uchaguzi mdogo.

Aidha, madiwani watano watiifu wa chama hicho, wameamriwa kutohudhuria vikao vya Baraza la Madiwani la Jiji hilo hadi hapo muafaka mpya wa mgogoro wa umeya unaoendelezwa katika jiji hilo utakapopatikana.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza adhabu hiyo jana aliyoiita kuwa ni uamuzi mgumu wa chama hicho katika kikao na waandishi huku akisema katika uamuzi huo, chama hakikufurahi.

“Uamuzi huu ni mzito na wa majonzi, hata chama hakikufurahi kuyafanya, ila kwa kuwa tunasimamia utashi wa chama, ikifikia hatua kama hii hatuna budi kuchukua hatua,” alisema Mbowe.

Hakufafanua kutofurahi huko kwa chama na mantiki ya neno utashi katika ujenzi wa demokrasia, lakini katika duru za kisiasa, kumekuwa na hoja; kuhusu madaraka ya chama cha siasa katika kumuondoa kiongozi aliyechaguliwa na wananchi, kama ndiyo demokrasia ya kweli.

Baadhi ya wasomi na wazee, akiwemo hata Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba, alifikia hatua ya kuwataka Watanzania katika mjadala ujao wa Katiba mpya, kuhoji uhalali wa madaraka ya vyama vya siasa, vyenye wanachama wachache kutengua uamuzi wa wananchi walio wengi.

Mbali na hukumu hiyo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa alisema Kamati Kuu inaendelea na msimamo wake wa kutomtambua Meya wa Arusha, Gaudance Lyimo (CCM) hadi hapo mazungumzo ya muafaka mpya yatakapopatikana.

Katika hilo, wajumbe wa Kamati hiyo, akiwemo Dk. Slaa na Naibu Katibu Mkuu, Kabwe Zitto Alhamisi wiki hii watafanya mkutano wa hadhara kufafanua hukumu hiyo kwa wananchi.

Waathirika wa hukumu hiyo ni aliyekuwa Naibu Meya na Diwani wa Kimandolu, Estomih Mallah; Diwani wa Elerai, John Bayo; Diwani wa Themi, Reuben Ngowi; Diwani wa Kaloleni, Charles Mpanda na Diwani wa Viti Maalumu Rehema Mohamed.

Diwani wa Kata ya Sekei, Crispin Tarimo yeye hukumu yake imesogezwa mbele ili apate nafasi ya kujitetea mbele ya Kamati hiyo kwa kuwa wakati wenzake wakijitetea mjini hapa, alitoa udhuru kuwa ni mgonjwa.

Hata hivyo, wakati akina Dk. Slaa wanajipanga kufanya mkutano wa hadhara Alhamisi wiki hii, Bayo mbali na kueleza nia ya kukata rufaa, alisema mgogoro si kati ya madiwani hao na Kamati Kuu; bali na Mbunge wa Arusha, Godbless Lema (Chadema).

Aliongeza kuwa na wao watakwenda kufanya mikutano ya hadhara kuwaeleza wananchi waliowachagua kilichowatokea. Mallah alipoulizwa kwa simu, alisema anasubiri barua ya kufukuzwa uanachama na kuweka wazi kuwa hajaridhika na atakata rufaa.

Safari ya kisiasa ya kuwang’oa madiwani hao ilianzia kwa Lema (Chadema), ambaye alikuwa wa kwanza kupinga muafaka wa kisiasa kati ya Chadema na CCM mkoani Arusha. Baadaye Lema aliungwa mkono na uongozi wa juu wa Chadema, ambao ulitaka madiwani hao kuvunja muafaka huo lakini madiwani hao wakasisitiza lengo lao lilikuwa maslahi ya maendeleo ya Arusha kuliko misuguano ya kisiasa.

Mbowe katika maelezo yake jana, alikumbusha kuwa baada ya madiwani hao kukubali kumtambua Meya Lyimo (CCM) katika muafaka huo, Chadema iliwataka wajiuzulu nafasi zao walizopata baada ya muafaka na kuomba radhi.

Nafasi hizo ni pamoja na ya Naibu Meya ambayo Mallah alichaguliwa kuichukua na uongozi wa Kamati ya Huduma za Uchumi, Elimu na Afya, ambayo Bayo alichaguliwa Mwenyekiti.

Madiwani hao wakiungwa mkono na wenzao walikaidi agizo la kutakiwa kujiuzulu na kuomba radhi kwa madai kuwa hawakutaka kuendeleza msuguano wa kisiasa, walitaka kuweka maslahi ya wananchi mbele na si ya chama.

Pia walilalamikia kauli za baadhi ya viongozi wa kitaifa wa Chadema akiwemo Dk. Slaa, kuwa wamekula rushwa na wakataka kiongozi huyo wa kitaifa kuomba radhi. Mbowe alisisitiza kuwa madiwani hao watapewa barua, kwa kuwa kitendo cha madiwani hao kukaidi agizo hilo ni utomvu wa nidhamu na pia ni kuvunja maadili na kanuni za chama na kuenda kinyume na msingi mama wa Chadema wa uwajibikaji.

Kuhusu kukata rufaa, Dk. Slaa alisema, madiwani hao wanaweza kufanya hivyo kwenye Baraza Kuu la chama hicho.

Katika hatua nyingine, Kamati hiyo imepokea taarifa ya mazungumzo baina ya Mwenyekiti wao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuhusu nia na azma ya kumaliza mgogoro wa umeya jijini Arusha.

Akielezea mazungumzo hayo, Mbowe alisema wamekubaliana na Waziri Mkuu, Pinda kuunda kamati ya kushughulikia mgogoro wa umeya jijini Arusha itakayojumuisha wajumbe kutoka vyama viwili. Wajumbe hao watatoka CCM na wengine Chadema, na kamati hiyo itakuwa chini ya uenyekiti wa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa.

Saturday, August 6, 2011

Lady Gaga Sued For Ripping Off "Judas"

According to a singer named Rebecca Francescatti, Lady Gaga's hit song "Judas" is a total rip-off of her 1999 song called ... wait for it ... "Juda".

Rebecca is suing Gaga in federal court, and claims the similarities between the two songs are not a coincidence. Her theory behind that claim?
Her former bass player, Brian Gaynor, is now employed by the music company that authored 17 songs for Gaga's most recent album, Born This Way.
"Though the songs are different styles, the composition is the same and the chorus is the same melody," said an attorney for Rebecca Francescatti.
"[Rebecca] is seeking recognition for what she created." Francescatti, who sings under the name Rebecca F., is suing Gaga for unspecified damages.
No comment from Lady Gaga's camp as of yet.
Seems a bit frivolous to us, but you decide. Listen to a snippet of "Juda" (above) and compare it to the Lady's video (below) and see what you think:

Read more celebrity gossip at: http://M.thehollywoodgossip.com/#ixzz1UFgo1Jvz

Afghan helicopter crash kills 31 US troops

A US helicopter crash in eastern Afghanistan has killed 31 US special forces and seven Afghan soldiers, President Hamid Karzai's office says.

The helicopter was taking the personnel back to their base after an operation. It is not clear how the crash happened but the Taliban said they shot the helicopter down. The incident is believed to be the biggest single loss of life for US forces in Afghanistan since operations began in 2001.

The helicopter went down overnight in Wardak province, the statement from President Karzai's office said.
It was returning from an operation against the Taliban in which eight insurgents are believed to have been killed.
A senior official of President Barack Obama's administration said the helicopter was apparently shot down, Associated Press news agency said.

Nyota wa soka Japan Naoki afariki dunia

Mcheza kandanda wa Japan Naoki Matsuda amefariki dunia siku mbili baada ya kupoteza fahamu uwanjani akiwa mazoezini ikidhaniwa ni matatizo ya moyo.
Naoki Matsuda
Naoki Matsuda

Matsuda aliyekuwa na umri wa miaka 34, aliyeiwakilisha Japan katika fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2002, siku ya Jumanne alikimbizwa. Alianguka na kuzimia akifanya mazoezi na klabu yake ya Matsumoto Yamaga, na tangu wakati huo hakuweza kurejewa na fahamu.

Meneja wa zamani wa timu ya taifa ya Japan, Philippe Troussier akitoa rambirambi zake kwa familia ya mchezaji huyo, alisema alikuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha nchi hiyo kilichoshiriki Kombe la Dunia.
"Inasikitisha sana kuona mtu anafariki dunia akiwa na umri mdogo kama wake," Bw Troussier alieleza Shirika la Reuters.

"Ni pigo kubwa. Alikuwa kijana mzuri sana na nilikuwa karibu naye. Niko pamoja na jamaa zake katika msiba huu mkubwa."
Mashabiki, marafiki na wachezaji wenzake wa zamani, walikusanyika katika hospitali ya Matsumoto kumtakia apone haraka alipokuwa amepoteza fahamu.

Matsuda aliichezea Japan mara 40 na kushinda mataji mara mbili katika Ligi ya nchi hiyo katika kipindi cha miaka 15 cha uchezaji wake na timu ya Yokohama F-Marinos.
Mapema mwaka huu alijiunga na timu ya Matsumoto inayocheza ligi ya chini.

Kisa na mkasa na Salim Kikeke

Kujifungua mtihani


Mwanamama mmoja mja mzito nchini Marekani, alijizuia kujifungua kwa muda wa saa tatu ili amalize kufanya mtihani. Mwanamama huyo mwenye umri wa miaka 29, alianza kupata uchungu wa kujifungua muda mfupi tu baada ya kuanza mtihani wake uliodumu kwa saa tatu. Alilazimika kuendelea kufanya mtihani huo, kwani asingemaliza mtihani wake, basi matokeo yake hayatatambuliwa. Mwanamke huyo Nightingale Dawson wa mjini Chigago amesema alijaribu kuufanya mtihani huo kwa haraka iwezekanavyo.

Baada ya kumaliza mtihani wake, alisaidiwa na watu kupelekwa katika hospitali iliyokuwa karibu, na kufanikiwa kupata mtoto saa mbili baadaye. Alipata mtoto wa kiume na kumuita Wilson. "Nilijitahidi na kuvuta pumzi ndefu ili niweze kumaliza mtihani" amesema Bi Nightingale akizungumza na gazeti ta Chicago Tribune.

Matokeo ya mtihani alioufanya yatatoka wakati Wilson akiwa na miezi miwii na nusu.

Maumbile

Bwana mmoja nchini India aliyekwenda hospitali kutokana na maumivu ya tumbo, alifanyiwa upasuaji na madaktari kukuta bwana huyo ameota kizazi cha kike. Bwana huyo, ambaye kazi yake ni mkulima, na tayari ana watoto wawili, alitajwa kwa jina la Ryalu, na gazeti la Telegraph, ambalo limeandika taarifa hii.
Mtandao wa cnews.com umesema madaktari walidhani kuwa bwana huyo anasumbuliwa na ngiri. Hata hivyo baada ya madaktari kumfanyia upasuaji, walikuta akiwa na viungo kamili vya uzazi vya kike.

Bwana huyo alikuwa akiishi maisha ya kawaida kabisa, huku viungo vyake vya kiume vikifanya kazi kama inavyotakiwa.
"Viungo vyake vya kiume viko sawa kabisa" amesema Daktari Pramod Kumar, akizungumza na gazeti la Telegraph. Bwana huyo ameondolewa viungo visivyo vyake, na anaendelea vizuri hospitali.

Roho yaumia


Mahakama moja nchini Taiwan imetoa amri kwa mwanamke mmoja kumlipa faini mchumba wake wa zamani, kutokana na kumsababishia maumivu ya kiihisia. Mahakama hiyo imetoa amri kwa mwanamke huyo, kumlipa mchumba wake dola elfu nane, baada ya kutotokea siku ya harusi yao.

Kwa mujibu wa BBC, bi harusi huyo ambaye alikuwa na uja uzito wa miezi mitano wakati wa harusi, alihitilafiana na mume wake mtarajiwa, kutokana na mabishano ya nani wamualike, na nani wasimualike katika harusi yao. Mvutano huo ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba bi harusi akapanga kutokwenda katika harusi yake, na kumuacha bwana harusi akiwa kasimama peke yake mbele ya wageni waalikwa. Bwana harusi kuona hivyo, alimshawishi mmoja wa wasichana wasimamizi wa harusi wafunge naye ndoa ili kuepuka aibu.

Hata hivyo wakati wakifunga ndoa hiyo ya kuepuka aibu, bwana harusi alibadili mawazo na kuamua kufunga ndoa ya kikweli kweli na msimamizi huyo wa harusi.

Upasuaji nyumbani

Bwana mmoja mwenye umri wa miaka 63 nchini Marekani, aliyekuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa ngiri, aliamua kuchukua kisu na kujifanyia upasuaji yeye mwenyewe. Shirika la habari la Reuters limesema baada ya kujipasua, aliwasha sigara, na kuweka moto huo wa sigara katika jeraha lake.

Polisi katika kiunga cha Glendale cha mjini Los Angeles walimkuta bwana huyo akiwa kajilaza nje ya nyumba yake bila nguo, baada ya mke wake kupiga simu na kutoa taarifa ya mume wake kujifanyia opareshen.
"Yaani alijipasua mwenyewe kwa kutumia kisu cha jikoni" amesema Sajini Tom Lorenz, msemaji wa polisi wa Glendale.

Polisi wamesema bwana huyo alimwambia mke wake kuwa amechoshwa na maumivu na hakutaka kuendelea kusubiri kupelekwa hospitali. Polisi hata hivyo wamesema bwana huyo hajatenda kosa lolote. Hospitali ya mjini humo intarajiwa hivi karibuni kumfanyia upasuaji wa kikamilifu kumtibu ngiri.

Mtoto au...

Polisi wa hapa Uingereza walivunja kioo cha gari moja lililokuwa limeegeshwa, ili kuokoa mwanasesere aliyeachwa ndani ya gari hilo.

Mtandao wa Times of India umeripoti kuwa polisi hao walidhani ni mtoto mdogo ameachwa ndani ya gari. Mwenye gari hilo, Anastazi Cristofis amesema ameshtushwa baada gari lake kuvunjwa na polisi ili kumtoa mwanasesere aliyeachwa ndani ya gari na mtoto wake wa kike mwenye umri wa miaka mitano.
"Sikuamini polisi walipokuja huku wameshikilia mdoli huyo na kuniambia kilichotokea" amesema bwana Cristofis.

Polisi hao wamesababisha hasara ya karibu dola mia tano.
"Polisi wameniambia nisirudie tena kuacha mdoli ndani ya gari" amesema Cristofis.
Taarifa zinasema mpita njia aliona mwanasesere huyo dani ya gari, na kudhani ni mtoto wa kweli, na kuita polisi.

Senti zimesheheni

Bwana mmoja nchini Uchina alikwenda kununua gari kwa kutumia sarafu, yaani coins. Bwana huyo, Wang alikwenda katika duka la magari akiwa na magunia saba ya sarafu ambazo thamani yake ni yuan elfu sitini, sawa na dola elfu tisa.

Bwana huyo alikusanya mapeni hayo kutokana na biashara yake ya kuuza unga rejareja. Sarafu hizo zilikuwa za thamani ya senti kumi na hamsini. Bwana huyo hukusanya yuan elfu kumi za sarafu kila mwezi kutokana na biashara yake. Sarafu hizo zilikuwa na uzito wa kilo mia tatu.

Mtandao wa China daily umesema muuzaji magari alipata tabu kutafuta benki itakayokubali kuchukua fedha hizo. Hata hivyo amekubali kumuuiza bwana wang gari, lakini atalazimika kusubiri muda mrefu kwani muuza gari amesema atampa gari mara tu atakapomaliza kuhesabu senti hizo.

Na kwa taarifa yako Kucha za mkononi huota haraka, mara nne zaidi ya kucha za miguuni.

Tukutane wiki ijayo..... Panapo majaaliwa...

Al-Shabaab wanahama Mogadishu

Kikundi cha wapiganaji wa Kiislamu wa Somalia, al Shabaab, kinasema kuwa kimeondoka katika vituo vyake kadha ndani ya mji mkuu, Mogadishu.
Mogadishu, Somalia

Wakaazi wameiambia BBC kwamba waliona misafara ya wapiganaji ikiondoka katika mji huo.
Kuhama huko kunafuatia mapigano makali jana usiku.

Kikosi cha Umoja wa Mataifa kinachoisaidia serikali ya Somalia kimekuwa kikipigana na al Shabaab mjini Mogadishu katika siku za karibuni; ili kuweza kufikisha msaada wa chakula kwa wale walioathirika na ukame nchini Somalia.

Haijulikani kama wapiganaji hao wameondoka kabisa. Msemaji wa serikali alielezea huo kuwa "ushindi wa dhahabu" kwa watu wa Somalia. Lakini al Shabaab, ambayo inadhibiti sehemu kubwa ya kusini mwa nchi, ilisema wameondoka kufuatana na mikakati yao na iliahidi kufanya shambulio la kulipiza.

Baadhi ya wadadisi wanafikiri al Shabaab imepungukiwa na fedha kwa sababu wafadhili wao wa Arabuni wamewapunguzia msaada tangu al Shabaab kudhoofika kijeshi. Wadadisi wanasema al Shabaab imewahi kuwahamisha wapiganaji wake mjini Mogadishu siku za nyuma, lakini safari hii inaonesha kuondoka kwao ni ushindi mkubwa kwa serikali.

Friday, August 5, 2011

Kazi imeanza UDA Kumekucha


Alisema kutokana na hali iliyojitokeza bungeni kuhusu uuzwaji wa shirika hilo, serikali imeona ni vyema vyombo vyake vikachunguza jambo hilo. Pinda alisema baada ya uchunguzi kukamilika, serikali itachukua hatua kwa wote waliohusika katika uuzaji UDA kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.  “Tumeagiza CAG, TAKUKURU na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kuanza uchunguzi wa jambo hili, utakapokamilika tutatoa taarifa na kuchukua uamuzi wa kisheria kwa wahusika,” alisema.  Katika hatua nyingine, waziri mkuu alisema serikali ina nia ya dhati ya kuhakikisha wastaafu na wanaodai pensheni katika Shirika la TAZARA wanalipwa. Alisema hatua zimeanza kuchukuliwa ili kuhakikisha wastaafu hao kwa upande wa Tanzania, wanalipwa.

Waziri mkuu alitoa maagizo hayo siku moja baada ya wabunge kulalamikia kuuzwa UDA. Waliwahusisha Meya wa Jiji wa Dar es Salaam, Dk. Didas Massaburi, mbunge wa Kaliua, Profesa Juma Kapuya (CCM), anayedaiwa kuwa na hisa 10,000 katika kampuni ya Simon Group iliyonunua UDA na aliyewahi kuwa waziri katika serikali ya awamu ya tatu, Idd Simba, ambaye anadaiwa kuingiza fedha kwenye akaunti yake na nyingine ya asasi ya Pride.

Wabunge kutoka mkoa wa Dar es Salaam, wakizugumza na waandishi wa habari jana, walisema Dk. Massaburi, Mkurugenzi wa Jiji, Bakari Kingobi na watendaji wengine waliohusika na kadhia hiyo wasimamishwe kazi. Kwa mujibu wa wabunge hao, hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi ya Simba, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya UDA, wajumbe wa bodi na watendaji wa shirika hilo waliohusika na kashfa hiyo.

Mwenyekiti wa wabunge hao, Abass Mtemvu, alisema wanataka mkataba wa uuzaji UDA usitishwe. Alisema Dk. Massaburi na Kingobi walishiriki kikao batili kilichoitwa mkutano maalumu wa wanahisa wa UDA na kufanya uamuzi wa kukabidhi shirika la mali zake kwa Simon Group Limited.

Alisema kikao hicho kilichoitishwa na meya kilifanyika bila kuheshimu maelekezo ya barua ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya Februari 28, mwaka huu, yenye Kumb. Na. CAB. 185/295/01/27 iliyoagiza kusitisha mchakato wa kuuza hisa ambazo hazijagawiwa. Nakala ya barua hiyo  iliwasilishwa kwa Kingobi, meneja mkuu wa UDA na wizara nyingine husika.  Mtemvu alisema mkutano huo ulitanguliwa na kikao batili cha bodi ya wakurugenzi ya UDA, chini ya uenyekiti wa Simba, kilichofanyika Januari 28, mwaka huu, kilichoazimia kuuza hisa zisizogawiwa kwa Simon Group bila kuzingatia taratibu, kanuni na sheria.

Alisema serikali itoe tamko kutokana na mgogoro wa kimaslahi ulioelezwa kuhusu kamati ndogo ya Bunge iliyoundwa na Kamati ya Miundombinu, kutokana na kutozingatiwa Kanuni za Bunge katika kutoa majukumu kwa kamati husika kuhusu kashfa ya UDA. Miongoni mwa wajumbe ni Profesa Kapuya.  Wabunge hao na majimbo yao kwenye mabano ni Mtemvu (Temeke – CCM), Mussa Zungu (Ilala - CCM), Iddi Azzan (Kinondoni - CCM), John Mnyika (Ubungo - CHADEMA), Halima Mdee (Kawe – CHADEMA), Dk. Faustine Ndungulile (Kigamboni –CCM), Eugene Mwaiposa (Ukonga – CCM), Dk. Makongoro Mahanga (Segerea –CCM).

Wengine kupitia Viti Maalumu ni Zarina Madabida (CCM), Philipa Mturano (CHADEMA), Mariam Kisangi (CCM), Angellah Kairuki (CCM) na Dk. Fenella Mukangara (CCM).

Wauza mafuta wakubali kuuza

MKURUGENZI Mtendaji wa Chama cha Waagizaji Wakubwa wa Mafuta ya Petroli nchini (TAOMAC), Salum Bisarara, amesema wamekubali kuendelea kutoa huduma kwa bei elekezi.

Alitoa msimamo huo katika mkutano wa waagizaji wa mafuta hao na Serikali jana katika  Wizara ya Nishati na Madini, Dar es Salaam, uliozungumzia mgomo wa wafanyabiashara hao uliofanyika juzi na jana maeneo mengi nchini.  Mkutano huo ulikutanisha kampuni zinazoagiza mafuta nchini za Total Tanzania, NSK Oil, Nat Oil, Lake Oil, Oryx, Camel Oil Ltd, Oil Com, BP, Gapco, Engen, MGS International Ltd, Moil na TPDC.

Pamoja na makubaliano hayo, chama hicho kiliteua kamati maalumu itakayokaa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), kupitia upungufu uliosababisha wamiliki hao kusitisha kutoa huduma juzi.

Bisarara alisema kulikuwa na tatizo, kwa sababu bei iliyotangazwa na Ewura iliwashitua kwa madai kuwa haikuwa imekubaliwa katika vikao vyao vya awali vya kukokotoa bei.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Engen, Seelan Naidoo, aliipa Serikali saa 24 kufanyia kazi upungufu uliomo katika fomula ya ukokotoaji bei mpya, la sivyo, atasitisha huduma. Naidoo alidai ni vibaya kwa nchi kuendelea kuuza mafuta kwa bei hiyo elekezi na kuitaka Serikali itambue kuwa wao wanafanya biashara kwa ajili ya faida.

“Ni vema tukaruhusiwa kufanya biashara kwa njia endelevu, kwa bei hizo tutakuwa tunakusanya hasara badala ya faida na inaweza kushusha uchumi wa nchi,” alidai Naidoo.

Alisema pamoja na kufikia makubaliano kati ya waagizaji wenzake na Serikali, ya kuendelea kutoa huduma kwa bei elekezi wakati wakisubiri upungufu uliojitokeza kurekebishwa, endapo hautafanyiwa kazi kwa saa 24 kuanzia sasa, kampuni hiyo haitaendelea kutoa huduma.

Engen ni kampuni ya Afrika Kusini ambayo inamiliki asilimia kati ya nne na tano ya soko la mafuta nchini.

Mwakilishi wa Oilcom, Ameir Nahdi, aliyekuwa wa kwanza kutoa msimamo wake, alisema wamekubali kuendelea na biashara baada ya kuelezea upungufu wa upatikanaji wa bei hiyo na kuahidiwa kufanyiwa kazi.

Akijibu hoja ya Serikali kupewa saa 24, Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi aliyeitisha mkutano huo, aliwaambia waagizaji hao kuwa hawana mamlaka ya kutoa masharti kwa Serikali.

Alifafanua kuwa Serikali haipewi masharti ya aina hiyo na kuwataka waagizaji hao wafanye kazi kwa ushirikiano na kuonya kwamba kama masharti ya aina hiyo yatatolewa, Serikali pia itatoa ya kwake. Maswi aliwataka waendelee kuuza mafuta kwa bei elekezi kama ilivyotangazwa na Ewura.

Kuhusu dalili za kuwapo baadhi ya wafanyabiashara wasiotii agizo hilo, Maswi alisema sheria ziko wazi, kwamba mwagizaji anaweza kunyang’anywa leseni ingawa anaamini hawawezi kufika huko kwa kuwa tayari wamekubaliana.

Alifafanua, kuwa juzi mara baada ya mgomo, Serikali ilikutana na waagizaji na kuwataka wauze mafuta kwa kuzingatia bei elekezi kabla ya mkutano wa jana wa kuzungumzia yaliyowatatiza. Alisema baada ya kukutana na wagizaji hao jana saa 5 asubuhi, ni kweli walikiri kufanya kazi kwa hasara, lakini wakakubaliana kuendelea na biashara kama ilivyo kwa bei elekezi na palipo na matatizo, Ewura iangalie na kutoa maelekezo.

“Tumekubaliana bila masharti na tumechagua Kamati ambayo itakaa na kufuatilia hayo yote ili suluhu ipatikane.

“Tumewaelekeza wawaambie pia wauzaji wao wa mikoani kuuza mafuta kwa bei hiyo na hata magari yaliyokuwa yakisafiri yaendelee na safari ya kwenda yalikokusudiwa,” alisema Maswi.

Kaimu Katibu Mkuu huyo alisema atakagua katika maghala yao kuona kama wametekeleza agizo la Serikali la kuendelea kutoa huduma kama inavyotakiwa.

Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Haruna Masebu, alisema masuala ya waagizaji yana sura ya kisera, usalama wa Taifa na udhibiti ambayo waliyazingatia zaidi.

Hata hivyo wachambuzi wa masuala ya kisheria, wanasema wafanyabiashara hao wamekiuka sheria ya ushindani wa kibiashara ambayo hairuhusu wao kukutana na kupanga mgomo wa kuuza mafuta.

Pia wanasema hawaoni sababu ya wao kusita kuuza mafuta kutokana na bei kushushwa, huku wakiuza mafuta ya taa mwezi uliopita, kwa bei ya juu wakati wakiwa wameyaagiza kwa kodi ya asilimia 52 kwa lita kabla haijapanda hadi asilimia 400.30 zilizokusudia kukabiliana na uchakachuaji.

Njaa ya athiri maeneo zaidi Somalia

Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa sehemu zingine tatu nchini Somalia zinakabiliwa na baa la njaa. Kufikia sasa kuna maeneo tano nchini humo yanayokabiliwa na tatizo hili. Baadhi ya sehemu hizo tatu zilikuwa maarufu sana kwa uzalishaji wa vyakula. Sehemu hizo tatu mpya zinapatikana kusini mwa Somalia na karibu na mji mkuu wa Mogadishu.
Janga la njaa Somalia
Janga la njaa Somalia

Kati ya sehemu hizo tatu, Afgoye corridor ndio ilio na idadi kubwa zaidi ya watu ikiwa na urefu wa takrbani kilomita thelathini kwenye barabara kuu inayounganisha mji wa mogadishu na ule wa Afgoye. Wakati somalia ilipokuwa nchi thabiti, mji huu wa Afgoye ulikuwa na shughuli nyingi wakati wa asubuhi, malori mengi yalikuwa yakisafirisha mboga na matunda hadi kwenye soko kuu mjini Mogadishu.

Nyakati za jioni, ili kuwa jambo la kawaida kuona idadi kubwa ya mifugo ikisafirishwa, kupitia mji huo hadi soko kuu la mifugo mjini Mogadishu.

Mwaka wa 2007, eneo hili liligeuka na kuwa makao ya zaidi ya watu nusu milioni waliokimbia mapigano mjini mogadishu kati ya wanajeshi wa ethiopia na wapiganaji wa waasi. Tangu wakati huo mji wa Afgoye umekuwa kwa kiasi kikubwa kutokana na kuongezeka kwa nyumba za mabanda na zile za kifahari.

Eneo hili la Afgoye corridor limewavutia wafanyabiashara wengi, kampuni ya simu ya mkononi na kampuni kadhaa za uchukuzi zimefungua ofisi zao katika sehemu hii. Kutokana na kuongezeka kwa shughuli nyingi katika eneo hili, sasa limekuwa mji mkubwa ambao raia wake wanapata huduma za kimsingi kama vile shule na hospitali.

Mji wa pili uliotangazwa kuwa unakabiliwa na baa la njaa ni mji wa Balad, ulioko kilomita 40 kaskazini mwa mogadishu. Mto shabelle umepita katikati mwa mji huo na shughuli nyingi za kilimo zinaendelea viungani mwake. Eneo hili lilikuwa likizalisha kiasi kikubwa cha pamba ndiposa kiwanda cha kutengeneza nguo kilijengwa mjini humo.

Na mji wa tatu ni ule wa Adale, mji mdogo ulioko pwani, kaskazini mwa mogadishu. Mji huo una sehemu nyingi zenye ufuo mzuri na wakuvutia na ni maarufu kwa shughuli za uvuvi.

Miji hii mitatu kwa sasa inathibitiwa na kundi la la wapiganaji wakiislamu la al shabaab.

Rowan Atkinson 'cheats death' as 240mph supercar hits tree then bursts into flames

Actor Rowan Atkinson cheated death last night after careering off the road in his 240mph supercar. The £650,000 McLaren F1 spun several times, smashing into a tree and ploughing into a road sign before catching fire on the opposite side of the carriageway.

The Mr Bean star, 56, pulled himself free from the wreck and was looked after by a passing motorist until emergency services arrived on the A605 at Haddon, near Peterborough, Cambridgeshire, at 7.30pm.

Scroll down for video of Rowan Atkinson on Top Gear...
Smash: Rowan Atkinson's £650,000 McLaren F1 spun several times, smashed into a tree and ploughed into a road sign before catching fire on the opposite side of the carriage
Smash: Rowan Atkinson's £650,000 McLaren F1 spun several times, smashed into a tree and ploughed into a road sign before catching fire on the opposite side of the carriageway 

Smash: Rowan Atkinson's £650,000 McLaren F1 spun several times, smashed into a tree and ploughed into a road sign before catching fire on the opposite side of the carriageway
Accident: Emergency services rushed to the scene to check on Mr Atkinson who managed to free himself from the wreck

Firemen tackled the blaze and an ambulance crew took him to nearby Peterborough hospital where he was believed to be recovering last night.

It is not the first time the Blackadder star has crashed the supercar, which can sprint from 0-60mph in just three seconds.

 
In 1999, a year after buying it following the phenomenal success of his Mr Bean movie, he was in collision with a Rover Metro in Lancashire.

Recently appearing on BBC's Top Gear 'Star in a Reasonably Priced Car', he listed the vast array of cars he currently owns, before setting the fastest lap in a time of 1min 42.2 sec.


Smash: Actor Rowan Atkinson cheated death after careering off the road in his 240mph McClaren F1 supercar, pictured here in 1998
Smash: Actor Rowan Atkinson cheated death after careering off the road in his 240mph McClaren F1 supercar, pictured here in 1998


Accident: The front of the car was wrecked in a previous collision with the rear of a Rover Metro in Lancashire, in October 1999
Accident: The front of the car was wrecked in a previous collision with the rear of a Rover Metro in Lancashire, in October 1999
He beat comedian John Bishop who, in an earlier episode, notched up the time of 1.42.8.

TOP GEAR FASTEST LAPS:

Suzuki Liana (2002–2005)

1:46.7 – Ellen MacArthur
1:46.9 – Jimmy Carr
1:47.1 – Simon Cowell
Chevrolet Lacetti (2006–2010)
1:45.83 – Jay Kay
1:45.87 – Kevin McCloud
1:45.9 – Brian Johnson
Kia Cee'd (2010-present)
1:42.2 – Rowan Atkinson
1:42.8 – John Bishop
1:43.5 – Ross Noble

The segment, recorded at the Top Gear test track at the Dunsfold Aerodrome, Surrey, sees a guest driving a standard car in a bid to get the fastest lap.
A Suzuki Liana was used for the shows recorded between 2002 and 2005, and a Chevrolet Lacetti between 2006 and 2010.
Atkinson set the record in a Kia Cee'd.
In 1994, the British car magazine Autocar stated 'it has too much performance for the public road'.
But it added that it 'will be remembered as one of the great events in the history of the car, and it may possibly be the fastest production road car the world will ever see'.
Mr Atkinson, who has a passion for fast cars has written articles about different vehicles for specialist car magazines.

Though his collection of cars changes regularly, he also has a £125,000 Aston Martin Virage, a vintage Rolls-Royce, and an elderly Morris Traveller, which he regularly drives around the Oxfordshire village where he lives in a £1 million former rectory.

He also has a £2.5 million townhouse in Chelsea. Last night an East of England Ambulance Service spokesman confirmed the accident.
He said: 'A man has since been conveyed to hospital with minor injuries after the car he was driving left the road earlier this evening.'
In style: Rowan Atkinson's character Mr Bean has less of a passion for fast cars
In style: Rowan Atkinson's character Mr Bean has less of a passion for fast cars