Showing posts with label pinda. Show all posts
Showing posts with label pinda. Show all posts

Monday, August 8, 2011

Mchungaji Msigwa: Tuna viongozi legelege

Mchungaji Peter  Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini
HANA makeke. Ni mpole, lakini mwenye msimamo thabiti wa kutetea anachokiamini. Si mwingine, bali Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Bunge la Muungano katika jimbo la Iringa Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Katika mahojiano yake na MwanaHALISI wiki hii, pamoja na mambo mengine, Mchungaji Msigwa anasema kuna tofauti kubwa kati ya wabunge wa CHADEMA na wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Anasema: “Wabunge wa CHADEMA wanalazimika kufanya kazi mara kumi zaidi ya ile inayofanywa na wabunge wa CCM, kwa sababu, wabunge wa CCM wamekuwa na utamaduni mchafu wa kutanguliza mbele maslahi ya chama chao kuliko maslahi ya taifa. Unapokuwa mbunge wa CHADEMA unakuwa pia mbunge wa wananchi wote wa Tanzania.

“Unapofikiri uwafanyie nini wapiga kura wa jimbo lako, papo hapo unatakiwa kufikiri uifanyie nini nchi yako. Unatakiwa ufikiri utawasaidiaje Watanzania wengine kutatua matatizo yao. Ni kwa sababu wabunge wa CCM wamekuwa wakiutumia wingi wao vibaya kupitisha mambo ambayo kila mwenye kulitakia mema taifa hili anaona si sahihi.

“Hata wale wachache miongoni mwao wanaotaka kujitutumua kutetea maslahi ya taifa, wanabanwa na chama chao kukubaliana na kila linaloletwa na serikali hata kama halina maslahi na taifa.”

Mchungaji Msingwa anasema, pamoja na changamoto hiyo kubwa inayowakabili wabunge wa chama chake, bado wanajivunia wajibu huo mkubwa waliojitwisha kuwakilisha Watanzania.

Alizungumzia kilichomsukuma kujitumbukiza katika ulingo wa kisiasa, tena kupitia vyama vya mageuzi, wakati yeye ni kiongozi wa kidini, Mchungaji Msigwa anasema: “Nimeingia kwenye siasa ili wasio na sauti waweze kusikika.

“Katika maandiko matakatifu walikuwapo watumishi wa Mungu waliosimamia haki na kuonya watawala walioenda kinyume cha maagizo ya Mungu. Mfumo tulionao unakandamiza wanyonge. Kwa hiyo, mimi kama Mchungaji napaswa kufanya kila niwezalo kuhakikisha haki za wanyonge zinasikilizwa na kuheshimiwa.”

Mchungaji Msigwa ni miongoni mwa wabunge 48 wa chama hicho wanaochangamsha Bunge kwa hoja nzito.
Akiwa ameingia Bungeni kwa mara ya kwanza, Mchungaji Msigwa anatambua changamoto tatu zinazomkabili. Anasema:
“Kwanza, changamoto kubwa ninayokumbana nayo ni jinsi ya kuwawakilisha wananchi wa Iringa Mjini na Watanzania kwa wakati mmoja.
“Ni changamoto ya kupambana na kasi ya muda, ili kuutumia vizuri katika kushughulikia masuala yote ya kijimbo na ya kitaifa.
“Nikiwa Waziri Kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini, nina majukumu mengine zaidi ya kuhakikisha utajiri wa utalii na maliasili ya nchi hii vinatumika vizuri kuwanufaisha Watanzania, na kuishitaki serikali kwa wananchi pale inapoendeleza ufisadi na sera mbovu zisizowanufaisha wananchi.

“Pamoja na changamoto hiyo kubwa inayotukabili wabunge wa CHADEMA, bado tunajivunia wajibu huo mkubwa tuliojitwisha wa kuwakilisha Watanzania.
“Ndiyo maana Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alipotumia magari zaidi ya 50 ya kifahari na ndege mbili katika ziara yake ya kikazi mkoani Iringa, nilisimama kupinga hatua hiyo. Niliona huu ni ubadhirifu unaochangia kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi kwa sababu, fedha zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo zinatumika kwa safari za anasa. Hili nililifanya bila kuujali Pinda ametembelea mkoa wa Iringa.
“Pili, kuna changamoto ya kubadilisha mtazamo wa wananchi (mind set) kuhusu majukumu ya mbunge. Baadhi ya wananchi wanamtazama mbunge kama mfadhili badala ya kumtazama kama mwakilishi na mtetezi wao.
“Baadhi wanafikiri kazi ya mbunge ni kutumia fedha zake binafsi kujenga barabara, shule au kugharamia shughuli nyingine za kimaendeleo. Hiyo si kazi ya mbunge, na hata ingekuwa ndiyo kazi ya mbunge basi isingewezekana kwa mshahara wa mbunge kufanya shughuli kubwa za kimaendeleo kwa ajili ya wananchi.
“Mbunge kama mtu namba moja anayeguswa na kero na matatizo ya watu wa jimbo lake, anaweza tu kuchangia baadhi ya shughuli za kimaendeleo kama watu wengine, lakini majukumu ya msingi ya mbunge, mbali na kuwasilisha kero na matatizo bungeni, ni kuhakikisha kodi inayolipwa na wananchi wote pamoja na mapato yatokanayo na raslimali za nchi, vinatumika kuwaletea maendeleo. Kwa hiyo, wakati nashughulikia kero na matatizo ya wananchi, nachukua pia wajibu wa kuwabadili mtazamo.
“Tatu, changamoto nyingine ni mbunge aliyenitangulia (wa CCM) ambaye alikuwa anapenda kuwapa baadhi ya wananchi vitu vidovidogo kama mchele, maharage, na kuwafanya baadhi yao waamini kuwa hayo ndiyo maendeleo, na hiyo ndiyo kazi pekee na ya msingi ya Mbunge, kumbe sivyo.
“Mimi sitawarubuni wananchi wa jimbo langu kwa kuwapa vitu vidogo vidogo. Badala yake, nitahakikisha napigania mgawo mzuri wa fedha zao kutoka kwenye bajeti kuu ya serikali na ile ya halmashauri, ili wapate maendeleo ya kweli na endelevu kwa manufaa ya vizazi vya leo na kesho, kama nilivyowaahidi katika kampeni zangu. Kazi hiyo nimeshaanza.”

Ingawa amekaa Bungeni kwa miezi saba tu, Mchungaji Msigwa anasema amejifunza mambo kadhaa, na ana matarajio kadhaa.
“Mwanzoni tulidhaniwa kuwa hatujui kitu kwa sababu ya ugeni wetu, lakini kama nilivyojibu swali lako la kwanza, ni kujifunza mfumo huu uliopo, na wakati unaendelea kujifunza unapaswa kuwawakilisha wananchi wa Iringa na Watanzania kwa ujumla.

Matarajio yangu ni kuwa na bunge linalojadili mambo ya msingi yanayolihusu taifa bila kuoneana aibu. Bunge la sasa halinifurahishi kabisa kwa sababu wenzetu kutoka CCM wanaweka ushabiki wa kichama ndani ya Bunge hata kwenye mambo ya msingi,” anasema.

Hata hivyo, Mchungaji Msigwa anasema anatumaini wabunge hawa watabadilika.Anakiri kwamba licha ya uchanga wake Bungeni, yu miongoni mwa wabunge wachache wanaoheshimika kwa wananchi kutokana na kuichachafya serikali. MwanaHalisi lilitaka kujua siri ya mafanikio yake.
“Siri ya mafanikio yangu ni huduma ya kichungaji. Mtu moja aliwahi ‘kama kuna jambo muhimu linaendelea kukaa kimya ni kuenzi uwongo; na kama utaamua kukaa kimya maana yake nawe ni mwongo.’
“Kwa kuwa namheshimu Mungu siwezi kukaa kimya ninapoona mambo hayaendi inavyopaswa kwenda, utakuwa ni uwongo nami pia nitakuwa mwongo.
“Taifa hili tuko katika kipindi ambacho maadili ya uongozi yametoweka, viongozi wanasema wasiyoyaamini. Naomba ieleweke sipo bungeni kuichachafya serikali, nipo bungeni kusimamia na kuishauri serikali bila kumuonea mtu. Viongozi tuna sehemu muhimu sana katika jamii.

“Ukiwa na baba dhaifu utakuwa na familia dhaifu. Vilevile ukiwa na kiongozi dhaifu tarajia taifa dhaifu. Kwa bahati mbaya viongozi wetu hawataki mabadiliko ambayo yatatupelekea kupevuka.”
Anazungumzia pia matarajio ya wana Iringa mjini katika miaka mitano ya ubunge wake.
“Kwanza, watarajie mabadiliko makubwa ya kimtazamo na kifikra. Bunge ni kioo cha taifa. Ni maombi yangu kuwa uwakilishi na fursa hii niliyoipata iwe ni baraka kwa kila Mtanzania. Mchango wowote nitakaoutoa uwe na faida kwa Watanzania na mustakabali wa taifa letu.
“Pili, watarajie kuwa sitaweza kukaa kimya pale ambapo Bunge litatumika kama mhuri wa kupitishia mambo ya serikali.”

Kwa mujibu wa Mchungaji Msigwa, CHADEMA ndilo tumaini pekee la Watanzania, kwa maana ndicho chama chenye mwelekeo. Anawataka wananchi kwa wakiunge mkono kwa hali na mali, maana yeye na wenzake tayari wameshajitoa kikamilifu kukitumikia chama na taifa. Ameoa na ana watoto.

Friday, August 5, 2011

Kazi imeanza UDA Kumekucha


Alisema kutokana na hali iliyojitokeza bungeni kuhusu uuzwaji wa shirika hilo, serikali imeona ni vyema vyombo vyake vikachunguza jambo hilo. Pinda alisema baada ya uchunguzi kukamilika, serikali itachukua hatua kwa wote waliohusika katika uuzaji UDA kwa kufuata sheria na taratibu za nchi.  “Tumeagiza CAG, TAKUKURU na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) kuanza uchunguzi wa jambo hili, utakapokamilika tutatoa taarifa na kuchukua uamuzi wa kisheria kwa wahusika,” alisema.  Katika hatua nyingine, waziri mkuu alisema serikali ina nia ya dhati ya kuhakikisha wastaafu na wanaodai pensheni katika Shirika la TAZARA wanalipwa. Alisema hatua zimeanza kuchukuliwa ili kuhakikisha wastaafu hao kwa upande wa Tanzania, wanalipwa.

Waziri mkuu alitoa maagizo hayo siku moja baada ya wabunge kulalamikia kuuzwa UDA. Waliwahusisha Meya wa Jiji wa Dar es Salaam, Dk. Didas Massaburi, mbunge wa Kaliua, Profesa Juma Kapuya (CCM), anayedaiwa kuwa na hisa 10,000 katika kampuni ya Simon Group iliyonunua UDA na aliyewahi kuwa waziri katika serikali ya awamu ya tatu, Idd Simba, ambaye anadaiwa kuingiza fedha kwenye akaunti yake na nyingine ya asasi ya Pride.

Wabunge kutoka mkoa wa Dar es Salaam, wakizugumza na waandishi wa habari jana, walisema Dk. Massaburi, Mkurugenzi wa Jiji, Bakari Kingobi na watendaji wengine waliohusika na kadhia hiyo wasimamishwe kazi. Kwa mujibu wa wabunge hao, hatua kali za kisheria zichukuliwe dhidi ya Simba, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya UDA, wajumbe wa bodi na watendaji wa shirika hilo waliohusika na kashfa hiyo.

Mwenyekiti wa wabunge hao, Abass Mtemvu, alisema wanataka mkataba wa uuzaji UDA usitishwe. Alisema Dk. Massaburi na Kingobi walishiriki kikao batili kilichoitwa mkutano maalumu wa wanahisa wa UDA na kufanya uamuzi wa kukabidhi shirika la mali zake kwa Simon Group Limited.

Alisema kikao hicho kilichoitishwa na meya kilifanyika bila kuheshimu maelekezo ya barua ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya Februari 28, mwaka huu, yenye Kumb. Na. CAB. 185/295/01/27 iliyoagiza kusitisha mchakato wa kuuza hisa ambazo hazijagawiwa. Nakala ya barua hiyo  iliwasilishwa kwa Kingobi, meneja mkuu wa UDA na wizara nyingine husika.  Mtemvu alisema mkutano huo ulitanguliwa na kikao batili cha bodi ya wakurugenzi ya UDA, chini ya uenyekiti wa Simba, kilichofanyika Januari 28, mwaka huu, kilichoazimia kuuza hisa zisizogawiwa kwa Simon Group bila kuzingatia taratibu, kanuni na sheria.

Alisema serikali itoe tamko kutokana na mgogoro wa kimaslahi ulioelezwa kuhusu kamati ndogo ya Bunge iliyoundwa na Kamati ya Miundombinu, kutokana na kutozingatiwa Kanuni za Bunge katika kutoa majukumu kwa kamati husika kuhusu kashfa ya UDA. Miongoni mwa wajumbe ni Profesa Kapuya.  Wabunge hao na majimbo yao kwenye mabano ni Mtemvu (Temeke – CCM), Mussa Zungu (Ilala - CCM), Iddi Azzan (Kinondoni - CCM), John Mnyika (Ubungo - CHADEMA), Halima Mdee (Kawe – CHADEMA), Dk. Faustine Ndungulile (Kigamboni –CCM), Eugene Mwaiposa (Ukonga – CCM), Dk. Makongoro Mahanga (Segerea –CCM).

Wengine kupitia Viti Maalumu ni Zarina Madabida (CCM), Philipa Mturano (CHADEMA), Mariam Kisangi (CCM), Angellah Kairuki (CCM) na Dk. Fenella Mukangara (CCM).

Thursday, July 28, 2011

Wabunge waghushi saini ya Pinda

BUNGE la Tanzania linakoelekea sasa si kuzuri. Pengine ndivyo inavyoweza kuzungumzwa kuhusu mambo yanavyokwenda ndani ya chombo hicho cha kutunga sheria na kuisimamia Serikali. Hali hiyo inatokana na tukio la juzi usiku baada ya wabunge au Mbunge asiyefahamika, kughushi saini ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakati kikao kikiendelea.

Aliyeweka wazi aibu hiyo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, muda mfupi baada ya Bunge kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika kwa Mwaka 2011/12 yaliyowasilishwa Jumatatu na Waziri Profesa Jumanne Maghembe, ambapo Sh. bilioni 258.3 ziliidhinishwa.

Baada ya Mwenyekiti wa Bunge, ambaye pia ni Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene (CCM) kuzungumzia kupitishwa kwa bajeti hiyo na kumpongeza Waziri na wabunge, huku akijiandaa kusitisha shughuli za Bunge ikiwa ni karibu saa 2:15 usiku, alisimama Waziri Lukuvi na kuomba Mwongozo wa Mwenyekiti.

Katika maelezo yake ya kuomba Mwongozo, Lukuvi alisema kumeibuka tabia ndani ya Bunge ambayo si ya kistarabu, kwani baadhi ya wabunge wamekuwa wakiandika ujumbe kwenye vikaratasi kuonesha mhusika fulani anaitwa wakati hakuna jambo kama hilo.

“Kwa leo (juzi) hapa yametokea matukio mawili ya wabunge Joseph Selasini (Rombo-Chadema) na Leticia Nyerere (Viti Maalumu-Chadema) kupelekewa ujumbe kwa nyakati tofauti ukionesha umesainiwa na Waziri Mkuu akiwaita.

“Lakini jambo la ajabu Waziri Mkuu mwenyewe hajui lolote na anashangaa jambo hili maana hakuandika ujumbe kuwaita,” alisema Waziri Lukuvi na kusababisha mshangao kwa baadhi ya wabunge.  Kutokana na mazingira hayo, aliomba suala hilo liachwe na kwamba si tabia nzuri ambayo imeanza kujitokeza.

Akizungumzia suala hilo, Simbachawene naye alilaani jambo hilo na kusema kwa vile karatasi iliyoandikwa alikuwa nayo, itakuwa rahisi kumbaini mhusika na kumshughulikia.

“Karatasi yenyewe imeandikwa hivi: Mheshimiwa Joseph Selasini, naomba uje kuna jambo tujadili, nahitaji ufafanuzi kutoka kwako - Mizengo Pinda,” alisema Simbachawene na kuongeza kuwa karatasi hiyo imesainiwa kuonesha aliyesaini ni Waziri Mkuu.

“Ndiyo maana nilimwona Mheshimiwa Selasini amekwenda kwa Waziri Mkuu akiwa amejikunyata kistaarabu kuona ameitiwa kitu gani, lakini Mheshimiwa Waziri Mkuu wala alikuwa hamfuatilii, alikuwa ameelekeza mawazo yake katika majibu ya Waziri,” alisema Mwenyekiti huyo.

Alieleza kuwa jambo hilo ni la aibu kubwa kwa wabunge, kufikia hatua ya kughushi saini ya Waziri Mkuu na kusisitiza lazima ichukuliwe uzito unaostahili.

Tangu Bunge la 10 lianze, kumekuwa na malalamiko kutoka kwa wadau mbalimbali kwamba limepoteza heshima kutokana na baadhi ya wabunge kufanya mambo ambayo hayaendani na chombo hicho – ya kitoto.

Masuala ya kuzomeana, kupigana vijembe na wakati mwingine kuzungumza bila mpangilio, ni baadhi ya mambo yanayopigiwa kelele na wadau kwamba yanakivunjia heshima chombo hicho, ambacho ni moja ya mihimili mikuu mitatu ya Dola.

Sunday, July 24, 2011

Mwanamke aolewa na wanaume wawili


MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, zilifanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Wakiwa kijijini hapo mume wake aliendelea kufanya kazi ya ukulima wakati yeye mama (Veronica), pamoja na kilimo hujihusisha na upishi na uuzaji wa pombe ya kienyeji ya iitwayo kayoga.

Mwanamke huyo ambaye amesema ana watoto wanne, Alfred (20), binti mwenye miaka 16 (ambaye ameolewa) na wengine wawili wa kiume, mmoja akisoma darasa la sita na mdogo ana miaka saba, amesema hana shida na waume wake.

Ingawa wanandoa hao walizungumza kwa hadhari, majirani walikiri kuwa mwanamke huyo anaishi na wanaume hao wawili kwa amani na kwamba mwanamke huyo ndiye mwenye sauti na si waume zake.

“Si siri tena sasa, tumeshawazoea, kwani wanaishi kwa amani ila yule mume mdogo anaishi kwenye nyumba aliyoachiwa na marehemu baba yake, lakini anashinda kwa mume mkubwa, ambapo inajulikana kijijini hapa kuwa ni nyumba kubwa. “Basi pale ni mambo yote, kula na kunywa, mama huyu amewapangia zamu wanaume hao kama afanyavyo mume mwenye wake wengi. Ama kweli ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni,” alisema mkazi mmoja kwa masharti ya jina lake kutoandikwa gazetini. Ilielezwa, kwamba wanaume hao wana akili timamu na hawatumii kilevi cha pombe kama ilivyo kwa mke wao.

Hata hivyo, mume mkubwa anapewa sifa za upole tofauti na mume mdogo anayetajwa kuwa mkorofi kiasi cha mara kadhaa kumchapa makofi mkewe anapomuudhi.

Majirani wanadai kwamba Mama Kaela na mumewe Paulo, walipofika kijijini hapo, walipokewa na kuishi maisha ya kawaida, lakini baadaye mama huyo alianza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Arcado, ambaye naye alilazimika kuachana na mkewe wa ndoa anayefahamika kijijini hapo kwa jina la Mama Pere.

Ilielezwa na mashuhuda hao kwamba mume mkubwa alipobaini uhusiano huo, alikuja juu, lakini mwanamke huyo inadaiwa alimweleza mumewe huyo, atake asitake lazima wataishi wawili, vinginevyo ataachana naye, ndipo mume mkubwa alipokubali kuishi na mume mwenza.

Katika maisha ya kawaida katika familia hiyo, inaelezwa kwamba katika baadhi ya siku ikitokea kuwa mama huyo amechoka kupika, mume mdogo huchukua jukumu la kupika na kumwandalia chakula na maji ya kuoga mume mkubwa.

“Lakini mara nyingi kwa mfano, ikiwa ni zamu ya mama huyo kulala kwa mumewe mkubwa, basi humfulia nguo zake kisha anakwenda kwa mumewe mdogo nako anamfulia nguo.

“Ndivyo wanavyoishi, nasi sasa tumewazoea ila yule mama ni mkali na ana sauti pale kwake kwa wanaume wale ila tunaona kama ana wivu sana kwa huyu mdogo ambaye naye pia ana wivu kwa mkewe huyo, labda anahofia kuwa mama huyo anaweza kuongeza mwanamume mwingine,” anasema mmoja wa majirani hao.

Hakuna mazuri yasiyokuwa na machungu, japo familia hiyo inaelezwa kuwa na amani, mtoto wao mdogo nusura avuruge uhusiano wa wanandoa hao, baada ya kuibuka mzozo wakati wa maandalizi ya ubatizo wake.

Kwa sababu anazojua mama, ingawa inafahamika kuwa wote ni watoto wa mume mkubwa, mke huyo katika hati za ubatizo aliandikisha ubini wa mtoto huyo kuwa ni Mlele (akimaanisha kuwa mtoto wa mume mdogo), lakini mume mkubwa aliweka pingamizi kanisani akidai yeye ndiye baba halali wa mtoto huyo.

Kwa mujibu wa mwanamke huyo, yeye na Arcado ni waumini wa madhehebu ya Katoliki wakati Paulo ni Mpentekoste. Madai ya mzozo wa uhalali wa `ubaba’ wa mtoto huyo, yalithibitishwa na baadhi ya wakazi wa kijiji hicho, akiwamo mwalimu wa dini wa Kigango cha Kanisa Katoliki Uruira, Mashaka Abel. Walisema miaka sita iliyopita, mtoto huyo akiwa na umri wa mwaka mmoja, alifanyiwa taratibu za ubatizo, lakini ilishindikana, kutokana na wanaume hao, kila mmoja kudai ndiye baba mzazi wa mtoto.

“Lilikuwa jambo la kustaajabisha sana, kwani familia hiyo ilifanya maandalizi yote ya sherehe ya ubatizo wa mtoto huyo, lakini siku hiyo kanisani wakati huo ilikuwa ni kigango cha Katumba ambacho sasa ni Uruira, sakata lilianzia pale Padri alipomwuliza mama wa mtoto huyo ubini wa mtoto naye akasema ni Mlele.

“Hapo ndipo mume mkubwa alipopinga na kudai kuwa mtoto yule si wa Arcado bali wake na yeye ndiye baba halali. Padri hakuamini, aliuliza tena na tena na majibu yakawa ni yale yale, ndipo ubatizo ukashindikana,” alisema Katekista Abel.

Kazi ya kutafuta undani wa ndoa hiyo haikuwa rahisi kutokana na mazingira ya woga na usiri uliokusudiwa kubaki, ambapo awali mama alisema kwamba mume wake ni Paulo pekee japo siku ambayo mwandishi wa habari hizi alifika kijijini hapo na baadaye nyumbani kwa wanandoa hao na kumkuta mume mdogo (Arcado akimsaidia mkewe kukoroga pombe. Awali katika utambulisho, walidai kuwa ni mtu na mdogo wake na kusita kuzungumzia maisha yao ya kifamilia.

Mke wao ambaye alionekana wazi kuwa ni msemaji mkuu alifoka na kuja juu, akidai kuwa hayuko tayari kuzungumzia uhusiano wake na wanaume hao wawili, ingawa alikiri kuwa wanaishi pamoja.

"Kwa hiyo umefunga safari yote hii kutoka huko ulikotoka ili uje kwangu mie Veronica … nasema sitaki kabisa mtu kuja hapa na kutaka kunivurugia mpangilio wa maisha yangu, kwanza nani alikueleza hayo, wambea wakubwa hao yanawahusu nini watu hao?” alihoji.

“Mie mume wangu ni huyu Paulo basi … sasa leo umeniachia vurugu ndani ya nyumba nitapigwa na huyo mume wangu Paulo, kwani mmenishikisha ugoni?” alifoka Mama Kaela. Hata hivyo, mume mkubwa alidai kuwa hatamwadhibu mkewe huyo na kwamba wataendelea kuishi pamoja na mdogo wake Arcado kwa amani. Hata hivyo, akina mama wengi kijijini hapo wanalaani kitendo cha mama huyo kuishi na wanaume wawili ambapo waliomba uongozi wa Kanisa uingilie kati, ili mama huyo aweze kufunga ndoa na mume mmoja.

Lakini kwa upande mwingine, baadhi walimpongeza mwanamke huyo wakidai kuwa kitendo hicho ni cha kijasiri kwa mwanamke, kumudu kuishi na wanaume wawili na kuwa na mamlaka juu yao.

Ndugu wa Arcado wao wanalaani kitendo cha ndugu yao kuolewa na mama huyo, wakidai kuwa walishamshauri na kumuahidi kuwa endapo ataachana na mama huyo watamwozesha mwanamke mwingine, lakini yeye Arcado, amedai kuwa yuko tayari kufa, lakini si kuachana na mama huyo, kwani ndiye ubavu wake wa maisha.

“Sasa tumebaki tunamwangalia tu huyu ndugu yetu Arcado, tumemshauri, lakini mkaidi, hatusikilizi. Basi nasi hatuna la kufanya zaidi ya kumwangalia,“ alisema mmoja wa ndugu wa karibu wa Arcado. Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kijiji hicho, Florence Katobasho, alikiri kuwa mwanamke huyo anaishi kinyumba na wanaume wawili na wanaishi kwa amani kwani hajawahi kufikishiwa malalamiko yoyote kuhusu wanandoa hao.

“Ni ukweli usiopingika, kwamba Mama Kaela anaishi na wanaume hao wawili … lakini kwa kuwa sijafikishiwa malalamiko yoyote kuhusu maisha ya wanandoa hao, mimi kama kiongozi hapa sina la kufanya na siwezi kuwafukuza, kwa kweli wanaishi kwa amani, mengine ni yao,” alisema Mwenyekiti wa Kijiji.

Saturday, July 23, 2011

Jairo awekwa benchi


SERIKALI imemsimamisha kazi Katibu Mkuu  wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo.  Hatua hiyo inalenga kutoa nafasi ya   ufanyika uchunguzi dhidi ya tuhuma  zinazomkabili zilizoibuliwa bungeni. Jairo anadaiwa kuziandikia barua idara na  taasisi zilizo chini ya wizara ili kila moja itoe  sh. milioni 50 kwa ajili ya kufanikisha  uwasilishaji wa makadirio ya matumizi ya  wizara kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012. Anadaiwa pia kuwalipa posho za safari  watumishi wa wizara waliofuatana na  viongozi wa juu licha ya kuwa walishalipwa  na idara na taasisi zao. 
Wabunge Beatrice Shellukindo (Kilindi-CCM)  na Christopher Ole Sendeka (Simanjiro  -CCM), ndio walioibua tuhuma hizo  walipojadili makadirio ya wizara, kabla ya  serikali kuyaondoa bungeni.  Serikali iliyaondoa makadirio hayo bungeni  kutokana na hoja za wabunge kuwa  haijajipanga kukabiliana na tatizo la umeme.  Bunge limetoa wiki tatu kwa serikali  kujipanga na kuyarejesha. 
Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo,  akizungumza na waandishi wa habari jana  mjini hapa, alisema amemwagiza Mdhibiti  na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG), kufanya uchunguzi wa kina, ambao  anatakiwa kuukamilisha ndani ya siku 10  kuanzia alipopewa kazi hiyo. "Wakati uchunguzi ukiendelea, Jairo   amesimamishwa kazi.
Hatua nyingine  zitafanyika baadaye kulingana na matokeo  ya uchunguzi," alisema. Luhanjo alisema anatarajia kufanya uteuzi  wa mtu atakayekaimu nafasi hiyo katika  kipindi kisichozidi siku tatu. Luhanjo alisema baada ya uchunguzi  kukamilika na endapo tuhuma dhidi ya Jairo  zitathibitika, uamuzi dhidi yake utachukuliwa  na rais kwa kuwa ndiye mamlaka yake ya  uteuzi.

Alisema amechukua uamuzi huo dhidi ya  Jairo kwa kuwa sheria ya  utumishi wa  umma inampa uwezo wa kushughulikia  nidhamu serikalini. "Kwa sababu suala hili ni zito nimeamua  aende likizo, lakini baada ya uchunguzi na  nikipata matokeo ya uchunguzi huo nitampa  taarifa itakayoambatana na hati ya  mashitaka," alisema.
Akizungumzia utaratibu alisema baada ya  matokeo ya uchunguzi kupatikana, Jairo  atapatiwa taarifa itakayoambatana na hati  ya mashitaka, itakayoeleza kwa kifupi kosa  alilotenda na namna alivyolitenda ili atoe  majibu.  Luhanjo alisema katika kipindi hicho,  atakuwa amesimamishwa kazi na kuanza  kulipwa nusu mshahara.  Kwa mujibu wa Luhanjo, katika majibu,  anaweza kukubali au kukana tuhuma dhidi  yake, ambapo mamlaka ya nidhamu  itaendelea kutoa adhabu kulingana na uzito  na kwamba, kwa kuwa Jairo ni mteule wa  rais, ndiye atakayeamua hatima dhidi yake.

Awali, kabla Luhanjo hajatangaza uamuzi  huo, wabunge waliibua hoja hiyo wakitaka  kufahamu hatua zilizochukuliwa dhidi ya  Jairo. Hoja hiyo iliibuliwa wakati wa kipindi cha   maswali ya papo kwa hapo kwa waziri mkuu  bungeni, ambapo Rashid Ali Abdalah  (Tumbe -CUF), alihoji hatua ya Waziri Mkuu  Mizengo Pinda, kudai hana mamlaka ya  kumwadhibu Jairo. Katika swali la msingi Rashid alitaka  kufahamu ni kwa nini waziri mkuu alitoa  kauli kuwa hawezi kumwajibisha Jairo hadi  Rais Jakaya Kikwete atakaporudi wakati  makamu wake na yeye wapo.
Akiwasilisha hoja ya kuondoa bungeni  makadirio ya Wizara ya Nishati na Madini,  Waziri Mkuu Pinda alisema Rais Kikwete  ndiye atakayeamua kuhusu hatima ya Jairo  kwa kuwa ndiye aliyemteua. Waziri Mkuu Pinda akijibu swali la Rashid,  alisema makamu wa rais au waziri mkuu  hawana mamlaka kikatiba ya kumwajibisha  Jairo, kwani mwenye uamuzi wa mwisho ni  rais wa nchi.
"Naomba niwaambie waheshimiwa wabunge  kwamba, si kila jambo linalotokea wakati  rais anapokuwa hayupo au yupo nje ya nchi  linaweza kutolewa uamuzi na makamu wa  rais au waziri mkuu," alisema. Alisema ni kweli kwa mujibu wa Katiba ya  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kifungu  cha 47 (1) (c), rais anapokuwa nje ya nchi  makamu wake ndiye anayeshika madaraka  ya kuongoza taifa. Pinda alisema kuna wakati hata waziri mkuu  hupewa nafasi hiyo, kama na makamu wa  rais hayupo, lakini wote wawili wana ukomo  katika utekelezaji wa majukumu yao,  ikiwemo kuamua mambo ambayo ni rais  pekee anayepasa kuyaamua.

Thursday, July 21, 2011

Kikwete amweka kiporo Jairo

RAIS Jakaya Kikwete amemweka kiporo Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo akisema ataona cha kufanya baada ya ziara yake ya Afrika Kusini.

Akizungumza jana nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu uvumi wa kujiuzulu kwa Jairo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema hakuwa amepata taarifa rasmi ya kujiuzulu kwake.

Lakini alisema kilichopo ni kuwa alimjulisha Rais Kikwete mambo yaliyotokea Jumatatu bungeni kuhusu mjadala wa Makadirio na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini ambapo baadhi ya wabunge walitaka Jairo aondolewe.

“Amenijibu kuwa ‘sawa, nisubiri nitakaporudi Afrika Kusini tuone tunafanyaje’,” alisema Pinda akimnukuu Rais Kikwete.

Jumatatu wakati wa mjadala wa makadirio hayo, wabunge waliibua kashfa wakituhumu wizara hiyo kuchangisha Sh bilioni moja kutoka idara na taasisi zake kwa ajili ya kufanikisha uwasilishaji wa makadirio hayo.

Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo (CCM), ndiye aliyeibua sakata hilo wakati akichangia hotuba ya Makadirio hayo kabla hayajaondolewa bungeni.

Katika kuthibitisha kashfa hiyo, Shelukindo aliwasilisha barua bungeni iliyoandikwa na Jairo ikizitaka idara na taasisi zote za wizara hiyo, kila moja ichangie Sh milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti.

Mbunge huyo wa Kilindi pamoja na wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka (CCM) kwa nyakati tofauti, walihoji bungeni mantiki ya fedha hizo, takribani Sh bilioni moja na wakataka wizara ifafanue zimekusanywa kwa ajili gani.

Pinda katika hoja yake bungeni, alikiri kwamba Jairo aliudhi na kutibua wabunge na akaahidi kuwasilisha suala hilo kwa Rais Kikwete aliyemteua ili achukuliwe hatua.

“Lazima nikiri hata mimi nilishtuka sana tena si kidogo, kwani suala hili limegubikwa na maswali mengi hakuna namna ya kutetea,” alisema Pinda siku hiyo.

Friday, June 17, 2011

Allowances here to stay, says PM


Prime Minister Mizengo Pinda yesterday ruled out the possibility of allowances budgeted for in the 2011/12 financial year being scrapped.Answering a question in Parliament, Mr Pinda said those advocating the scrapping of allowance allocations in the Budget should understand that it was a constitutional issue.
“This is a constitutional issue, and there is no way the government can act without following due procedure, which can take a long time,” Mr Pinda said when answering Mr Mohamed Habib Mnyaa (Mkanyageni-CUF), who had asked the Prime Minister to state the government’s stand on the debate on whether or not MPs should receive sitting allowance.

Mr Pinda said Article 73 of the Constitution talked about MPs’ benefits, making parliamentarians’ sitting allowances a constitutional matter that could not be changed through the pressure of one person. He added, however, there was no problem if an MP chose to forfeit his or her allowance, saying the money could be used for other purposes.

“I think there is no problem if an MP directs that his or her allowance be kept by the Treasury for other uses... this is not the first time that such a decision has been made,” Mr Pinda said. Chadema legislators, led by Mr Zitto Kabwe, have been demanding for the scrapping of sitting allowance, saying it was not justified.

Mr Kabwe, the Kigoma North MP, has argued that MPs and civil servants were being paid salaries monthly, and do not deserve extra payment when they go about their official duties. But Mr Pinda said he doubted whether Chadema arrived at the decision out of patriotism. Earlier, Mr Mnyaa said the allowance debate had caused hostility between MPs and voters, with the latter thinking that parliamentarians were squandering public resources.

He accused some MPs and the media of misleading the public, and asked the Prime Minister to clarify on the matter. Mr Pinda said there were two types of allowances –discretionary and non-discretionary. He added that the government had no powers to suspend payment of discretionary allowances, but could do so with discretionary allowances.

Mr Pinda said MPs’ sitting allowance was discretionary, and was recognised under the law and therefore could not be scrapped arbitrarily. The Prime Minister said Chadema MPs were being insincere by claiming that they do not need allowances.
“Chadema MPs may be supporting the idea, but they know deep down that they desperately need the money,” he said, adding that there was nothing wrong if MPs used their allowances to help their voters. On whether the government would take legal measures against those opposed to allowances, which were enshrined in the Constitution, Mr Pinda said there was no need to reach that stage.

“I don’t think that we need to reach that stage as the issue is not as big as some people think…it is a very minor issue.”Mr Pinda added his voice to the debate that has attracted the attention of a number of prominent individuals, including former German president Horst Kohler, who on Wednesday warned that the government’s image was at stake.

Prof Kohler said in Dar es Salaam that donors were closely monitoring the debate, adding that it might end up tarnishing the government’s image before development partners if it was not handled properly. Responding to a question during a dialogue at Movenpick Hotel, he said the debate did not present a good picture of the country’s expenditure priorities.

Prof Kohler felt that it was not in order for a country like Tanzania, which received substantial assistance from donor countries, to set aside huge sums as allowances for government officials, who were also being paid salaries. Giving an example of his own country, he said: “In Germany, such officials have to foot their own bills while attending official duties.” He added that payment of allowances was not a proper way of spending taxpayers’ money.

Prof Kohler said at the Maendeleo Dialogue, organised by Konrad Adenauer Stiftung (KAS) and the Tanzania Development Initiative Programme (Tadip), that Western countries were likely to react once they had all the facts on the allowances debate.

Opposition MP Zitto Kabwe has written to the Clerk of National Assembly, declining sitting allowance during Parliament’s ongoing Budget meeting in Dodoma.

Prof Kohler urged the government to uphold transparency and accountability.  He noted that Tanzania had made great strides in development, but added that a lot more needed to be done to promote the rule of law, saying this would enhance the public’s confidence in the government.

Thursday, June 16, 2011

Wanafunzi 9,000 Udom watimuliwa


ZAIDI ya wanafunzi 9,000 wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) wamefukuzwa kwa muda usiojulikana kuanzia jana kwa madai ya kuhamasisha mgomo usio halali.Habari zilizopatikana mjini hapa zimeeleza kuwa wanafunzi hao ni wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii na Sayansi Asilia. Walitakiwa kuondoka chuoni hapo kabla ya saa 8:00 mchana.

Baada ya amri hiyo, Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) walionekana wakiwa wanarandaranda katika maeneo ya chuo hicho.hali hiyo ilichangia pia kuharakisha wanafunzi hao kuondoka chuoni hapo wakihofia kukumbana na kipigo.

Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Profesa Idriss Kikula alithibitisha kufukuzwa kwa wanachuo hao na kusema kuwa suala la kuwarejesha litatokana na utaratibu watakaoupanga baadaye.

Kufukuzwa huko kumekuja siku mbili baada ya kuanzisha maandamano yaliyoshinikiza kujiuzulu kwa viongozi waandamizi wa Serikali, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Waziri wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa kwa madai kwamba wamewadanganya kuhusu malipo yao ya masomo kwa vitendo.

“Ni kweli kabisa kuwa tumewasimamisha kwa muda usiojulikana. Tutawarudisha kwa muda ambao tutaona unafaa,” alisema Profesa Kikula na kuongeza mtindo utakaotumika ni wa kuchambua na kurudisha mwanafunzi mmoja mmoja.

Katika madai yao, wanafunzi hao walisema wanasoma bila ya kufanya mazoezi ya vitendo kama ilivyo kwa vyuo vingine. Madai mengine ni pamoja na mazingira mabovu chuoni hapo pamoja na kutosoma baadhi ya masomo ambayo wanachuo wengine wanasoma.

Msimamo wa wanafunzi

Wakizungumza mara baada ya agizo hilo jana baadhi ya wanafunzi hao walisema kuwa hawaoni tabu kufukuzwa wakisema wao ni waathirika wanaotumika kwa maslahi ya wengine. Walisema kuwa kufukuzwa kwao ni kwa ajili ya kudai maslahi ambayo wamekuwa wakiyatafuta wakati wote bila ya mafanikio na kwamba kama itabidi itakuwa bora waondoke.

“Sisi tunaondoka na wenzetu wengine walishaondoka katika Kitivo cha Sayansi ya Kompyuta kwa hiyo kwa hali hii lazima chuo chote kitafungwa maana hali inakokwenda chuoni hapa ni siasa tupu,” alisema mmoja wa wanafunzi hao na kuongeza:

“Ni bora turudi nyumbani kwa kuwa huwezi kusoma bila ya kufanya mafunzo kwa vitendo. Ni bora tukae nyumbani tu,” alisema mmoja wa wanafunzi hao huku akiungwa mkono na wenzake.

Wanafunzi wa Kitivo cha Teknolojia ya Habari na Elimu Angavu walifukuzwa baada ya kugoma wakitaka walipwe fedha kwa ajili ya vifaa vya kujivunzia kwa vitendo.

Kufukuzwa kwa wanafunzi hao kulikuwa faraja kwa madereva wa teksi na pikipiki maarufu kama bodaboda ambao walifurika chuoni hapo kufanya kazi ya kuwasafirisha kwa malipo ya Sh10,000 kwa pikipiki na teksi Sh15,000.

Tuesday, June 14, 2011

Polisi yapiga wanafunzi mabomu



Jeshi la Polisi limetumia mabomu kuwatawanya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom). Milio ya mabomu ilisikika katika eneo la Bunge mjini Dodoma, baada ya polisi kuwatawanya wanafunzi wa Chuo cha Sayansi ya Jamii cha Udom, kuandamana hadi bungeni wakitaka kumuona Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, kushinikiza kulipwa posho za mafunzo kwa vitendo.

Mapema asubuhi, wanafunzi hao walikusanyika katika viwanja vya Nyerere Square mjini hapo na ilipofika saa 4.00 asubuhi walianza kuandamana hadi bungeni wakishinikiza kumuona Pinda na Kawambwa. Hata hivyo, jitihada zao zilishindikana baada ya polisi kuwaamuru kuondoka katika eneo hilo na walipokaidi amri hiyo ndipo walipopigwa kwa mabomu ya machozi yaliyofanya wanafunzi hao kukimbia ovyo.

Katika maeneo mbalimbali ya mji wa Dodoma hususan bungeni kulikuwa na ulinzi mkali wa askari wa Kikosi cha Kuzuia Fujo (FFU), waliokuwa wamebeba bunduki na mabomu ya kurusha kwa mkono.

Rais wa Serikali ya Wanafunzi Kitivo cha Sanaa ya Lugha na Sayansi za Jamii, Mwakabinga Philipo, alisema wameamua kuandamana kutokana na kutotekelezewa madai yao ambayo ni kupatiwa fedha za mafunzo kwa vitendo ambazo wamekuwa wakiahidiwa, lakini hawapatiwi.

Alisema Seneti ya Udom Juni 8, mwaka huu ilitoa taarifa kuwa tatizo la madai ya fedha za mafunzo kwa vitendo halitatokea tena. Alifafanua kuwa licha ya ahadi hiyo, wanashangazwa kuona mpaka sasa haitekelezeki ndio maana waliamua kwenda bungeni kuonana na viongozi hao.

Mwakabinga alisema kutokana na ahadi zilizotolewa na viongozi hao ndio maana waliamua kwenda kuonana na Pinda na Kawambwa ili kupata ufumbuzi wa fedha hizo. Baada ya kutawanywa na polisi, ilipofika majira ya saa 6:00 mchana, wanafunzi hao walikusanyika tena katika viwanja vya Nyerere wakidai kuwa Waziri Kawambwa angekwenda kuzungumza nao.

Baada ya wanafunzi hao kukusanyika, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, James Msekela, alifika katika eneo hilo kwa lengo la kuwatuliza, lakini jitihada zake ziligonga mwamba baada ya kumzomea na kumwambia “hatukutaki wewe, tunamtaka Waziri.” Baada ya Dk. Msekela kuzomewa, askari wa FFU walianza kuwatawanya wanafunzi hao na kukimbizana nao katika mitaa mbalimbali na kufanikiwa kuwakamata baadhi yao.