Showing posts with label chadema. Show all posts
Showing posts with label chadema. Show all posts

Monday, August 8, 2011

Mchungaji Msigwa: Tuna viongozi legelege

Mchungaji Peter  Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini
HANA makeke. Ni mpole, lakini mwenye msimamo thabiti wa kutetea anachokiamini. Si mwingine, bali Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Bunge la Muungano katika jimbo la Iringa Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Katika mahojiano yake na MwanaHALISI wiki hii, pamoja na mambo mengine, Mchungaji Msigwa anasema kuna tofauti kubwa kati ya wabunge wa CHADEMA na wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Anasema: “Wabunge wa CHADEMA wanalazimika kufanya kazi mara kumi zaidi ya ile inayofanywa na wabunge wa CCM, kwa sababu, wabunge wa CCM wamekuwa na utamaduni mchafu wa kutanguliza mbele maslahi ya chama chao kuliko maslahi ya taifa. Unapokuwa mbunge wa CHADEMA unakuwa pia mbunge wa wananchi wote wa Tanzania.

“Unapofikiri uwafanyie nini wapiga kura wa jimbo lako, papo hapo unatakiwa kufikiri uifanyie nini nchi yako. Unatakiwa ufikiri utawasaidiaje Watanzania wengine kutatua matatizo yao. Ni kwa sababu wabunge wa CCM wamekuwa wakiutumia wingi wao vibaya kupitisha mambo ambayo kila mwenye kulitakia mema taifa hili anaona si sahihi.

“Hata wale wachache miongoni mwao wanaotaka kujitutumua kutetea maslahi ya taifa, wanabanwa na chama chao kukubaliana na kila linaloletwa na serikali hata kama halina maslahi na taifa.”

Mchungaji Msingwa anasema, pamoja na changamoto hiyo kubwa inayowakabili wabunge wa chama chake, bado wanajivunia wajibu huo mkubwa waliojitwisha kuwakilisha Watanzania.

Alizungumzia kilichomsukuma kujitumbukiza katika ulingo wa kisiasa, tena kupitia vyama vya mageuzi, wakati yeye ni kiongozi wa kidini, Mchungaji Msigwa anasema: “Nimeingia kwenye siasa ili wasio na sauti waweze kusikika.

“Katika maandiko matakatifu walikuwapo watumishi wa Mungu waliosimamia haki na kuonya watawala walioenda kinyume cha maagizo ya Mungu. Mfumo tulionao unakandamiza wanyonge. Kwa hiyo, mimi kama Mchungaji napaswa kufanya kila niwezalo kuhakikisha haki za wanyonge zinasikilizwa na kuheshimiwa.”

Mchungaji Msigwa ni miongoni mwa wabunge 48 wa chama hicho wanaochangamsha Bunge kwa hoja nzito.
Akiwa ameingia Bungeni kwa mara ya kwanza, Mchungaji Msigwa anatambua changamoto tatu zinazomkabili. Anasema:
“Kwanza, changamoto kubwa ninayokumbana nayo ni jinsi ya kuwawakilisha wananchi wa Iringa Mjini na Watanzania kwa wakati mmoja.
“Ni changamoto ya kupambana na kasi ya muda, ili kuutumia vizuri katika kushughulikia masuala yote ya kijimbo na ya kitaifa.
“Nikiwa Waziri Kivuli wa Wizara ya Nishati na Madini, nina majukumu mengine zaidi ya kuhakikisha utajiri wa utalii na maliasili ya nchi hii vinatumika vizuri kuwanufaisha Watanzania, na kuishitaki serikali kwa wananchi pale inapoendeleza ufisadi na sera mbovu zisizowanufaisha wananchi.

“Pamoja na changamoto hiyo kubwa inayotukabili wabunge wa CHADEMA, bado tunajivunia wajibu huo mkubwa tuliojitwisha wa kuwakilisha Watanzania.
“Ndiyo maana Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alipotumia magari zaidi ya 50 ya kifahari na ndege mbili katika ziara yake ya kikazi mkoani Iringa, nilisimama kupinga hatua hiyo. Niliona huu ni ubadhirifu unaochangia kurudisha nyuma maendeleo ya wananchi kwa sababu, fedha zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo zinatumika kwa safari za anasa. Hili nililifanya bila kuujali Pinda ametembelea mkoa wa Iringa.
“Pili, kuna changamoto ya kubadilisha mtazamo wa wananchi (mind set) kuhusu majukumu ya mbunge. Baadhi ya wananchi wanamtazama mbunge kama mfadhili badala ya kumtazama kama mwakilishi na mtetezi wao.
“Baadhi wanafikiri kazi ya mbunge ni kutumia fedha zake binafsi kujenga barabara, shule au kugharamia shughuli nyingine za kimaendeleo. Hiyo si kazi ya mbunge, na hata ingekuwa ndiyo kazi ya mbunge basi isingewezekana kwa mshahara wa mbunge kufanya shughuli kubwa za kimaendeleo kwa ajili ya wananchi.
“Mbunge kama mtu namba moja anayeguswa na kero na matatizo ya watu wa jimbo lake, anaweza tu kuchangia baadhi ya shughuli za kimaendeleo kama watu wengine, lakini majukumu ya msingi ya mbunge, mbali na kuwasilisha kero na matatizo bungeni, ni kuhakikisha kodi inayolipwa na wananchi wote pamoja na mapato yatokanayo na raslimali za nchi, vinatumika kuwaletea maendeleo. Kwa hiyo, wakati nashughulikia kero na matatizo ya wananchi, nachukua pia wajibu wa kuwabadili mtazamo.
“Tatu, changamoto nyingine ni mbunge aliyenitangulia (wa CCM) ambaye alikuwa anapenda kuwapa baadhi ya wananchi vitu vidovidogo kama mchele, maharage, na kuwafanya baadhi yao waamini kuwa hayo ndiyo maendeleo, na hiyo ndiyo kazi pekee na ya msingi ya Mbunge, kumbe sivyo.
“Mimi sitawarubuni wananchi wa jimbo langu kwa kuwapa vitu vidogo vidogo. Badala yake, nitahakikisha napigania mgawo mzuri wa fedha zao kutoka kwenye bajeti kuu ya serikali na ile ya halmashauri, ili wapate maendeleo ya kweli na endelevu kwa manufaa ya vizazi vya leo na kesho, kama nilivyowaahidi katika kampeni zangu. Kazi hiyo nimeshaanza.”

Ingawa amekaa Bungeni kwa miezi saba tu, Mchungaji Msigwa anasema amejifunza mambo kadhaa, na ana matarajio kadhaa.
“Mwanzoni tulidhaniwa kuwa hatujui kitu kwa sababu ya ugeni wetu, lakini kama nilivyojibu swali lako la kwanza, ni kujifunza mfumo huu uliopo, na wakati unaendelea kujifunza unapaswa kuwawakilisha wananchi wa Iringa na Watanzania kwa ujumla.

Matarajio yangu ni kuwa na bunge linalojadili mambo ya msingi yanayolihusu taifa bila kuoneana aibu. Bunge la sasa halinifurahishi kabisa kwa sababu wenzetu kutoka CCM wanaweka ushabiki wa kichama ndani ya Bunge hata kwenye mambo ya msingi,” anasema.

Hata hivyo, Mchungaji Msigwa anasema anatumaini wabunge hawa watabadilika.Anakiri kwamba licha ya uchanga wake Bungeni, yu miongoni mwa wabunge wachache wanaoheshimika kwa wananchi kutokana na kuichachafya serikali. MwanaHalisi lilitaka kujua siri ya mafanikio yake.
“Siri ya mafanikio yangu ni huduma ya kichungaji. Mtu moja aliwahi ‘kama kuna jambo muhimu linaendelea kukaa kimya ni kuenzi uwongo; na kama utaamua kukaa kimya maana yake nawe ni mwongo.’
“Kwa kuwa namheshimu Mungu siwezi kukaa kimya ninapoona mambo hayaendi inavyopaswa kwenda, utakuwa ni uwongo nami pia nitakuwa mwongo.
“Taifa hili tuko katika kipindi ambacho maadili ya uongozi yametoweka, viongozi wanasema wasiyoyaamini. Naomba ieleweke sipo bungeni kuichachafya serikali, nipo bungeni kusimamia na kuishauri serikali bila kumuonea mtu. Viongozi tuna sehemu muhimu sana katika jamii.

“Ukiwa na baba dhaifu utakuwa na familia dhaifu. Vilevile ukiwa na kiongozi dhaifu tarajia taifa dhaifu. Kwa bahati mbaya viongozi wetu hawataki mabadiliko ambayo yatatupelekea kupevuka.”
Anazungumzia pia matarajio ya wana Iringa mjini katika miaka mitano ya ubunge wake.
“Kwanza, watarajie mabadiliko makubwa ya kimtazamo na kifikra. Bunge ni kioo cha taifa. Ni maombi yangu kuwa uwakilishi na fursa hii niliyoipata iwe ni baraka kwa kila Mtanzania. Mchango wowote nitakaoutoa uwe na faida kwa Watanzania na mustakabali wa taifa letu.
“Pili, watarajie kuwa sitaweza kukaa kimya pale ambapo Bunge litatumika kama mhuri wa kupitishia mambo ya serikali.”

Kwa mujibu wa Mchungaji Msigwa, CHADEMA ndilo tumaini pekee la Watanzania, kwa maana ndicho chama chenye mwelekeo. Anawataka wananchi kwa wakiunge mkono kwa hali na mali, maana yeye na wenzake tayari wameshajitoa kikamilifu kukitumikia chama na taifa. Ameoa na ana watoto.

Chadema yafukuza madiwani 5 Arusha

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imewafukuza uanachama madiwani watano wa chama hicho mkoani Arusha kwa kutotekeleza maagizo ya kamati hiyo na hivyo kuweka wazi kata tano za mkoa huo kwa ajili ya uchaguzi mdogo.

Aidha, madiwani watano watiifu wa chama hicho, wameamriwa kutohudhuria vikao vya Baraza la Madiwani la Jiji hilo hadi hapo muafaka mpya wa mgogoro wa umeya unaoendelezwa katika jiji hilo utakapopatikana.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza adhabu hiyo jana aliyoiita kuwa ni uamuzi mgumu wa chama hicho katika kikao na waandishi huku akisema katika uamuzi huo, chama hakikufurahi.

“Uamuzi huu ni mzito na wa majonzi, hata chama hakikufurahi kuyafanya, ila kwa kuwa tunasimamia utashi wa chama, ikifikia hatua kama hii hatuna budi kuchukua hatua,” alisema Mbowe.

Hakufafanua kutofurahi huko kwa chama na mantiki ya neno utashi katika ujenzi wa demokrasia, lakini katika duru za kisiasa, kumekuwa na hoja; kuhusu madaraka ya chama cha siasa katika kumuondoa kiongozi aliyechaguliwa na wananchi, kama ndiyo demokrasia ya kweli.

Baadhi ya wasomi na wazee, akiwemo hata Waziri Mkuu mstaafu, Joseph Warioba, alifikia hatua ya kuwataka Watanzania katika mjadala ujao wa Katiba mpya, kuhoji uhalali wa madaraka ya vyama vya siasa, vyenye wanachama wachache kutengua uamuzi wa wananchi walio wengi.

Mbali na hukumu hiyo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa alisema Kamati Kuu inaendelea na msimamo wake wa kutomtambua Meya wa Arusha, Gaudance Lyimo (CCM) hadi hapo mazungumzo ya muafaka mpya yatakapopatikana.

Katika hilo, wajumbe wa Kamati hiyo, akiwemo Dk. Slaa na Naibu Katibu Mkuu, Kabwe Zitto Alhamisi wiki hii watafanya mkutano wa hadhara kufafanua hukumu hiyo kwa wananchi.

Waathirika wa hukumu hiyo ni aliyekuwa Naibu Meya na Diwani wa Kimandolu, Estomih Mallah; Diwani wa Elerai, John Bayo; Diwani wa Themi, Reuben Ngowi; Diwani wa Kaloleni, Charles Mpanda na Diwani wa Viti Maalumu Rehema Mohamed.

Diwani wa Kata ya Sekei, Crispin Tarimo yeye hukumu yake imesogezwa mbele ili apate nafasi ya kujitetea mbele ya Kamati hiyo kwa kuwa wakati wenzake wakijitetea mjini hapa, alitoa udhuru kuwa ni mgonjwa.

Hata hivyo, wakati akina Dk. Slaa wanajipanga kufanya mkutano wa hadhara Alhamisi wiki hii, Bayo mbali na kueleza nia ya kukata rufaa, alisema mgogoro si kati ya madiwani hao na Kamati Kuu; bali na Mbunge wa Arusha, Godbless Lema (Chadema).

Aliongeza kuwa na wao watakwenda kufanya mikutano ya hadhara kuwaeleza wananchi waliowachagua kilichowatokea. Mallah alipoulizwa kwa simu, alisema anasubiri barua ya kufukuzwa uanachama na kuweka wazi kuwa hajaridhika na atakata rufaa.

Safari ya kisiasa ya kuwang’oa madiwani hao ilianzia kwa Lema (Chadema), ambaye alikuwa wa kwanza kupinga muafaka wa kisiasa kati ya Chadema na CCM mkoani Arusha. Baadaye Lema aliungwa mkono na uongozi wa juu wa Chadema, ambao ulitaka madiwani hao kuvunja muafaka huo lakini madiwani hao wakasisitiza lengo lao lilikuwa maslahi ya maendeleo ya Arusha kuliko misuguano ya kisiasa.

Mbowe katika maelezo yake jana, alikumbusha kuwa baada ya madiwani hao kukubali kumtambua Meya Lyimo (CCM) katika muafaka huo, Chadema iliwataka wajiuzulu nafasi zao walizopata baada ya muafaka na kuomba radhi.

Nafasi hizo ni pamoja na ya Naibu Meya ambayo Mallah alichaguliwa kuichukua na uongozi wa Kamati ya Huduma za Uchumi, Elimu na Afya, ambayo Bayo alichaguliwa Mwenyekiti.

Madiwani hao wakiungwa mkono na wenzao walikaidi agizo la kutakiwa kujiuzulu na kuomba radhi kwa madai kuwa hawakutaka kuendeleza msuguano wa kisiasa, walitaka kuweka maslahi ya wananchi mbele na si ya chama.

Pia walilalamikia kauli za baadhi ya viongozi wa kitaifa wa Chadema akiwemo Dk. Slaa, kuwa wamekula rushwa na wakataka kiongozi huyo wa kitaifa kuomba radhi. Mbowe alisisitiza kuwa madiwani hao watapewa barua, kwa kuwa kitendo cha madiwani hao kukaidi agizo hilo ni utomvu wa nidhamu na pia ni kuvunja maadili na kanuni za chama na kuenda kinyume na msingi mama wa Chadema wa uwajibikaji.

Kuhusu kukata rufaa, Dk. Slaa alisema, madiwani hao wanaweza kufanya hivyo kwenye Baraza Kuu la chama hicho.

Katika hatua nyingine, Kamati hiyo imepokea taarifa ya mazungumzo baina ya Mwenyekiti wao na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kuhusu nia na azma ya kumaliza mgogoro wa umeya jijini Arusha.

Akielezea mazungumzo hayo, Mbowe alisema wamekubaliana na Waziri Mkuu, Pinda kuunda kamati ya kushughulikia mgogoro wa umeya jijini Arusha itakayojumuisha wajumbe kutoka vyama viwili. Wajumbe hao watatoka CCM na wengine Chadema, na kamati hiyo itakuwa chini ya uenyekiti wa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa.

Saturday, July 16, 2011

Lowassa aweka mambo hadharani

MBUNGE wa Monduli, Edward Lowassa, amesema atatangaza uamuzi kuhusu nyadhifa zake ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakati muafaka ukifika. Amesema ameshitushwa na kitendo cha aliyekuwa mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, kutangaza kuachia nafasi hiyo na ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM.

Lowassa aliyewahi kuwa waziri mkuu wa Serikali ya Muungano, alisema hayo baada ya kutakiwa kutoa maoni kuhusu uamuzi wa Rostam kujiuzulu nyadhifa hizo. "Ninachoweza kusema ni kuwa, Rostam kujiuzulu ni haki yake lakini nimeshituka kuona amejiuzulu na ubunge. Nimeguswa pia na wananchi wake walivyopokea uamuzi huo," alisema. Rostam akitangaza uamuzi wa kuachia ngazi juzi, alisema amefikia uamuzi huo ili kulinda maslahi ya Chama. Kwa upande wake, Lowassa alipoulizwa ana mpango gani wa yeye kujiuzulu alisema: "Nitazungumza wakati muafaka ukifika."

Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama, kwa upande wake alisema kwa kufuata utaratibu wa kawaida ndani ya Chama, hakina taarifa za kujiuzulu Rostam. Hata hivyo, alisema jambo hilo litazungumzwa katika vikao vya juu vya Chama na baadaye taarifa zitatolewa.  "Chama hakina taarifa yoyote, tumeona kwenye vyombo vya habari ametangaza kujiuzulu kwake akiwa Igunga," alisema Mukama na kuongeza kuwa, CCM bado inalihitaji jimbo la Igunga.

Naye mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA), aliibuka bungeni na kuomba muongozo wa Spika Anne Makinda, akitaka atangaze kuwa jimbo la Igunga lipo wazi. Spika Anne alisema hana taarifa rasmi kuhusu kujiuzulu kwa Rostam, na kama ilivyo kwa wengine ameona habari hizo kwenye mitandao.
"Sisi tuna taratibu zetu, Rostam hajaniandikia barua, tutatoa taarifa wakati muafaka utakapowadia," alisema. Katika hatua nyingine, wanasiasa na wasomi nchini wameendelea kuwa na maoni tofauti kuhusu uamuzi wa Rostam, wengine wakipongeza hatua hiyo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti , walisema uamuzi huo ni mzuri ingawa umechelewa.  Mwenyekiti wa TLP na mbunge wa Vunjo, Augustino Mrema, alisema Rostam amechukua uamuzi mzuri. “Ni uamuzi mzuri ingawa amechelewa,  hasa kutokana na tuhuma zake kuwa za muda mrefu,’’ alisema. Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Hajji Semboja, alisema Rostam anapaswa kupigiwa mfano na wafanyabiashara wengine.
“Ni sawa tu kuondoka, nina hakika CCM haiwezi kuyumba, ikizingatiwa kuwa wameondoka wakongwe kama hayati Julius Nyerere na Mzee Rashidi Kawawa na CCM bado ipo,’’ alisema. Alisema CCM ni chama chenye wanachama wengi, hivyo kinachopaswa kufanyika ni kwa wafanyabiashara wengine kujitoa na kuwaachia watu wa siasa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Mohamed Bakari, alisema CCM inapaswa kuwa makini kutokana na Rostam kushika nafasi kubwa, hivyo ni lazima alikuwa na wafuasi. “Suala hili ni kubwa na lina faida na hasara, hivyo kinachotakiwa ni kujipanga vyema ili kuepusha matatizo yatakayoweza kujitokeza baadaye,’’ alisema.

Wednesday, July 13, 2011

Sitta: Wabunge wa upinzani wanafiki

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema mambo mengi ya wapinzani ni ya kinafiki na wamekuwa wakiibeza Serikali kwa kauli nyepesi nyepesi.

Sitta alitoa kauli hiyo jana bungeni mjini Dodoma alipokuwa akijaribu kutuliza Bunge lililokuwa limechafuka baada ya Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila (NCCR-Mageuzi), kudai kuwa Serikali iliyoko madarakani ni legelege na imeshindwa kukusanya kodi.

"Nawasihi wenzangu hasa wa CCM, hawa wapinzani hii (kupinga mambo) ndiyo kazi yao, wanabeza kila tunachofanya kwa lugha nyepesi nyepesi na mambo mengi wanayozungumza ni unafikinafiki hivi, sisi tuwaachie wananchi wawahukumu.

Kauli hiyo ilisababisha baadhi ya wabunge hasa wa upande wa upinzani kusimama na kuomba mwongozo wa Mwenyekiti na wengine wakizomeana, huku Sitta ambaye ni Kaimu Kiongozi wa Shughuli za Serikali Bungeni, akiwa amesimama akiomba kuendelea.

"Subirini nitoe mfano ... wanazungumza posho za vikaoni ni kuibia wananchi na baadhi yao wamekuwa wabunge kwa miaka mitano iliyopita na walikuwa wakizichukua, kama kweli ndivyo hivyo, basi warudishe," alisema Sitta.

Kauli hiyo ilisababisha wabunge zaidi, karibu 10 wakiwamo wa CCM kusimama kuomba Mwongozo wa Mwenyekiti, lakini Mwenyekiti Jenista Mhagama akaahirisha shughuli za Bunge kwa mapumziko ya mchana, kwa kuwa muda ulikuwa umefika, huku akiwaacha wabunge wakipiga kelele za kuomba Mwongozo.

Kabla ya kuibuka tafrani hiyo, Kafulila aliyekuwa akichangia hotuba ya Makadirio ya Matumizi ya Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, alisema tangu Uhuru moja ya maadui waliopigwa vita ni maradhi; lakini akashangaa bajeti ya Afya ni ndogo na kuongeza kuwa inatokana na Serikali legelege kushindwa kukusanya mapato.

"Miaka 50 ya Uhuru asilimia 90 ya bajeti ya maendeleo ya afya inategemea fedha za nje, tatizo hamkusanyi kodi na Nyerere (Baba wa Taifa) alisema Serikali legelege inashindwa kukusanya kodi," alisema Kafulila.

Kauli hiyo ilipingwa na Mbunge wa Nzega, Dk. Hamisi Kigwangala (CCM) aliyesema Kafulila alitumia neno la kuudhi kwa kuiita Serikali ya CCM legelege.

Dk. Kigwangala alifafanua kuwa Kafulila hakuwa na taarifa sahihi, kwa kuwa katika miaka mitatu iliyopita, Serikali ilikuwa ikikusanya karibu Sh bilioni 200, lakini mpaka mwaka huu, makusanyo yaliongezeka na kufikia karibu Sh bilioni 400.

Baada ya ufafanuzi huo, Mwenyekiti wa Bunge, Mhagama alimtaka Kafulila kufuta usemi, lakini mbunge huyo alipinga akisema ni kauli ya Baba wa Taifa, ambaye kila mtu anamuenzi bila kujali anatoka chama gani.

"Tunapoteza muda kujadili suala ambalo liko wazi, mwaka 2005/06 Serikali ilikuwa ikikusanya wastani wa Sh bilioni 260 lakini dola moja ilikuwa sawa na Sh 1,000.

"Leo mnakusanya karibu Sh bilioni 400 kwa mwezi, dola moja ni Sh 1,600 ni hesabu rahisi, hakuna kilichoongezeka ... sifuti usemi, niko tayari kufia ukweli huu," alisema Kafulila na kusababisha Sitta kuamka na kuwaita wapinzani wanafiki huku akiwataka CCM kuwavumilia.

Hata hivyo, Mwalimu Nyerere alisema chama legelege huzaa Serikali legelege na pia aliwahi kusema "Serikali corrupt (inayokula rushwa) hushindwa kukusanya kodi," na si Serikali legelege hushindwa kukusanya kodi.

Awali, kabla ya tafrani hiyo, Kafulila alimtaka Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hadji Mponda, ikibidi ajiuzulu kuliko kukubali kuwasilisha bajeti ya fedha ndogo bungeni huku ikitegemea fedha nyingi za wahisani.

Alisema hiyo inatokana na wabunge na familia zao kuwa na uwezo wa kutibiwa sehemu yoyote ndani na nje ya nchi, ndiyo maana hawawekezi katika hospitali za vijijini.

Wakati akisema hayo, mmoja wa wabunge ambaye hakufahamika lakini mwanamke, aliwasha kipaza sauti akasema: "Pamoja na wewe (Kafulila) na Mbunge wa Mpanda Mjini Chadema (Said Arfi ambaye alilazwa India hivi karibuni)."

Hata hivyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uwekezaji na Uwezeshaji, Dk. Mary Nagu, alisimama na kupinga kauli ya Kafulila, akisema: "Hili ni Bunge Tukufu, tuzungumze kwa heshima."

Mbunge mwingine mwanamume akawasha kipaza sauti na kuhoji: "Nani ana heshima?" Nagu akaendelea kufafanua kuwa mwanawe ni daktari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili ambayo ni ya Serikali na hata baba yake mzazi alilazwa katika hospitali ya Katesh ambayo ni ya vijijini.

Hata hivyo, sauti ile ya kiume iliendelea kumkatisha Nagu na safari hii Mbunge huyo alisema, "so what(kwa hiyo?"

Kutokana na kauli hizo za kukatishana, Mhagama alisimama na kusema ameisikiliza sauti ya mmoja wa wabunge wanaotoa kauli hizo za kejeli huku akimkatisha waziri aliyekuwa akizungumza na kubaini kuwa sauti hiyo inafanana na ya Mbunge wa Nyamagana, Ezekia Wenje (Chadema).

Alionya kuwa wanachofanya wabunge kuwasha vipaza sauti holela ili kuzuia hoja za wenzao kusikika au kuwakatiza, ni kinyume na Kanuni za Bunge na akifuatilia anaweza kuwabaini na kuwachukulia hatua.

Thursday, June 30, 2011

Ex-spy chief backs Chadema protests






Dar es Salaam. Former Intelligence chief Hassy Kitine yesterday came out in support of the opposition Chadema’s stance on various issues.He told journalists in Dar es Salaam that demonstrations organised by Chadema across the country in protest at the spiralling cost of living and the party’s demand for the scrapping of sitting allowances were pertinent issues which the country’s leadership should take seriously.

Dr Kitine is the first prominent CCM cadre to have publicly supported Chadema’s cause, which has in recent months been roundly criticised by the ruling party and some opposition parties. He said it was a fact that the high cost of living was a heavy burden on Tanzanians, adding that something should urgently be done to address the situation.

Dr Kitine, a former Cabinet minister and MP, said whatever Chadema was doing to draw attention to such issues deserved support, and added that the opposition party should not be demonised for practising its democratic rights.
He made the remarks when journalists sought his comments on various national issues at the end of a meeting organised by Faidika, a microfinance institution in which he is a director.

Dr Kitine said he had also been closely following the debate on whether or not MPs and other holders of public office deserved sitting allowances.“What Chadema is doing is healthy for our democracy because everyone is entitled to their own opinion, but the views should be constructive…they should not be aimed at destroying the country.”

Dr Kitine warned that the widening gulf between the rich and poor was “very dangerous”, saying it posed a serious threat to peace and stability in Tanzania.He said the country could not expect to remain peaceful forever when a few individuals controlled 99 per cent of the economy.

Dr Kitine said he was only trying to speak the “truth”, although he was aware that his comments would not go down well in some quarters.“I, like other Tanzanians, am giving my views on various national issues, but I know that some people are not happy with my comments. But even if I don’t say what I am saying, other people will say it.”

On the Chadema demonstrations, Dr Kitine said what the opposition party was doing was a challenge to the government and other political parties.

“What we need to look at is what they (Chadema) are advocating in their demonstrations. If you talk of life having become unbearably tough, that’s reality because many people are feeling the pinch...I support the demonstrations although I’m a CCM member,” he said.

Comparing the reign of retired President Benjamin Mkapa and President Jakaya Kikwete’s Fourth Phase government, Dr Kitine said he had not noticed any major difference between the two phases.He said, however, that things had gone from bad to worse after principles enshrined in the Arusha Declaration were abandoned, adding that people were now freely buying their way into elective office.

“In the past, when I was appointed Director of Intelligence by Mwalimu Nyerere and later a minister before I became an MP, the sole motive for seeking leadership was to serve the people,” he said.

Dr Kitine said the political landscape had changed dramatically since the Arusha Declaration was shunted aside. It was very difficult in the past for people who had amassed wealthy and failed to explain its source to be allowed to seek elective office, he said.

In a swift response, CCM Publicity Secretary Nape Nnauye told The Citizen that there was nothing wrong with convincing people to fight for their rights, adding that the issue was how this was done.

“Even CCM has been doing a lot to raise people’s awareness and sensitise them on their rights. Take for instance the decision to construct a secondary school in every ward across the country…this aims at increasing people’s awareness by giving them education,” he said when he toured Mwananchi Communications Limited head office in Dar es Salaam.

“The difference is that while we (CCM) are empowering the people by educating them, Chadema stops people from engaging in economic activities by holding demonstrations daily and deceiving them that this is a shortcut to State House,” he said.

Wednesday, June 29, 2011

Mbunge aibua Deci bungeni

NAIBU Waziri wa Fedha, Gregory Teu, leo ameshindwa kujibu swali lililomtaka aeleze hatua zilizochukuliwa na Serikali kuhusu maofisa walioshindwa kutekeleza wajibu wao hadi taasisi ya Development Entrepreneurship for Community Initiative (DECI) ikafanya shughuli zake kinyume cha sheria.

Swali hilo liliulizwa na Mbunge wa Kawe Halima Mdee (Chadema) ambaye awali aliuliza swali la msingi kuhusu DECI.

Katika swali hilo la nyongeza, Mdee alisema, DECI ilifanya shughuli zake kwa miaka mitatu za kuchukua amana za wananchi bila kuwa na kibali cha kufanya hivyo.

“Serikali inatoa kauli gani juu ya maafisa wake ambao walikuwa wanajua suala hilo
lakini hawakuchukua hatua zozote? alihoji Mdee.

Katika swali lingine la nyongeza Mbunge huyo aliuliza kuwa, kwa kuwa fedha zinazoshikiliwa ni za wanachama na waliofanya uhalifu huo ni watu watano, na kwa vile thamani ya fedha inashuka kwa nini wanachama ambao hawakuwahi kuvuna hata mara moja wasikabidhiwe fedha hizo?

Katika majibu yake alisema: “Fedha zinazodaiwa na wanachama ni nyingi wakati fedha zilizoko kwenye akaunti za wakurugenzi ni kidogo.”

Baada ya kujibu hivyo alienda kukaa ndipo Spika wa Bunge Anne Makinda akamkumbusha kuwa hajajibu sehemu nyingine ya swali hilo kuwa maofisa wa serikali ambao walizembea hadi Deci wakaendesha shughuli zao kinyume cha sheria wamechukuliwa hatua gani?

Ndipo Naibu huyo aliporudi kwenye eneo la kujibia na kusema “Nafikiri walikuwa bado
hawajaandikishwa,” alisema naibu waziri huyo na kuwafanya wabunge kuangua kicheko.

Awali akijibu swali la msingi la Mbunge huyo, Teu alisema Serikali haijachukua fedha za Deci bali fedha hizo, Sh bilioni 14.81 zimezuiliwa katika akaunti zilizomilikiwa na wakurugenzi wa Deci katika benki mbalimbali nchini.

Katika swali hilo Mdee alitaka kufahamu hatma ya fedha za wananchi. Alisema fedha hizo ni asilimia 37.77 ya ambazo zinadaiwa na wanachama wa Deci ambazo ni Sh bilioni 39.3.

Alisema, uamuzi wa kuzizuia uliotolewa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali ikiwa ni hatua mojawapo ya uchunguzi dhidi ya Deci ambayo ilikuwa inaendesha mchezo wa upatu.

“Napenda kuliarifu Bunge lako kuwa kesi ya Deci iliyofunguliwa mwaka juzi katika mahakama ya Kisutu inaendelea kusikilizwa,” alisema Teu na kuongeza: “Hivyo hatma ya fedha hizo za wananchi itategemea hatma ya kesi hiyo kwani Deci ilikuwa na matawi 40 katika mikoa 18 ya Tanzania Bara”.

Alisema, usikilizwaji wa mashahidi wa Dar es Salaam umekamilika na hatua za kuwapata mashahidi kutoka mikoa mingine zimeanza.

Alisema, Deci ilikuwa na wanachama 649,859 na sehemu ya wanachama hao watahitajika kutoa ushahidi mahakamani.

Friday, June 17, 2011

Allowances here to stay, says PM


Prime Minister Mizengo Pinda yesterday ruled out the possibility of allowances budgeted for in the 2011/12 financial year being scrapped.Answering a question in Parliament, Mr Pinda said those advocating the scrapping of allowance allocations in the Budget should understand that it was a constitutional issue.
“This is a constitutional issue, and there is no way the government can act without following due procedure, which can take a long time,” Mr Pinda said when answering Mr Mohamed Habib Mnyaa (Mkanyageni-CUF), who had asked the Prime Minister to state the government’s stand on the debate on whether or not MPs should receive sitting allowance.

Mr Pinda said Article 73 of the Constitution talked about MPs’ benefits, making parliamentarians’ sitting allowances a constitutional matter that could not be changed through the pressure of one person. He added, however, there was no problem if an MP chose to forfeit his or her allowance, saying the money could be used for other purposes.

“I think there is no problem if an MP directs that his or her allowance be kept by the Treasury for other uses... this is not the first time that such a decision has been made,” Mr Pinda said. Chadema legislators, led by Mr Zitto Kabwe, have been demanding for the scrapping of sitting allowance, saying it was not justified.

Mr Kabwe, the Kigoma North MP, has argued that MPs and civil servants were being paid salaries monthly, and do not deserve extra payment when they go about their official duties. But Mr Pinda said he doubted whether Chadema arrived at the decision out of patriotism. Earlier, Mr Mnyaa said the allowance debate had caused hostility between MPs and voters, with the latter thinking that parliamentarians were squandering public resources.

He accused some MPs and the media of misleading the public, and asked the Prime Minister to clarify on the matter. Mr Pinda said there were two types of allowances –discretionary and non-discretionary. He added that the government had no powers to suspend payment of discretionary allowances, but could do so with discretionary allowances.

Mr Pinda said MPs’ sitting allowance was discretionary, and was recognised under the law and therefore could not be scrapped arbitrarily. The Prime Minister said Chadema MPs were being insincere by claiming that they do not need allowances.
“Chadema MPs may be supporting the idea, but they know deep down that they desperately need the money,” he said, adding that there was nothing wrong if MPs used their allowances to help their voters. On whether the government would take legal measures against those opposed to allowances, which were enshrined in the Constitution, Mr Pinda said there was no need to reach that stage.

“I don’t think that we need to reach that stage as the issue is not as big as some people think…it is a very minor issue.”Mr Pinda added his voice to the debate that has attracted the attention of a number of prominent individuals, including former German president Horst Kohler, who on Wednesday warned that the government’s image was at stake.

Prof Kohler said in Dar es Salaam that donors were closely monitoring the debate, adding that it might end up tarnishing the government’s image before development partners if it was not handled properly. Responding to a question during a dialogue at Movenpick Hotel, he said the debate did not present a good picture of the country’s expenditure priorities.

Prof Kohler felt that it was not in order for a country like Tanzania, which received substantial assistance from donor countries, to set aside huge sums as allowances for government officials, who were also being paid salaries. Giving an example of his own country, he said: “In Germany, such officials have to foot their own bills while attending official duties.” He added that payment of allowances was not a proper way of spending taxpayers’ money.

Prof Kohler said at the Maendeleo Dialogue, organised by Konrad Adenauer Stiftung (KAS) and the Tanzania Development Initiative Programme (Tadip), that Western countries were likely to react once they had all the facts on the allowances debate.

Opposition MP Zitto Kabwe has written to the Clerk of National Assembly, declining sitting allowance during Parliament’s ongoing Budget meeting in Dodoma.

Prof Kohler urged the government to uphold transparency and accountability.  He noted that Tanzania had made great strides in development, but added that a lot more needed to be done to promote the rule of law, saying this would enhance the public’s confidence in the government.

Mbowe: Kesi zimeniletea msongo wa mawazo

  • Kapteni Komba adai jina lake limekatwa


MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe, ameliambia Baraza la Maadili ya Viongozi wa Umma kuwa, ameshindwa kujaza fomu za kutangaza mali zake kutokana na msongo wa mawazo.

Akihojiwa kwenye baraza hilo jana, Mbowe alisema tangu umalizike Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, amekumbwa na mambo mengi, ikiwa ni pamoja na kesi mbalimbali ambazo zimemsababishia msongo wa mawazo na kumwathiri kifamilia. Alisema alifikishwa katika mahakama tatu tofauti, zikiwamo Mahakama Kuu, Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha na Hai kwa tuhuma mbalimbali ambazo zimemsababishia msongo wa mawazo.

“Katika kipindi chote hicho nimekuwa kwenye mahakama tatu tofauti nikituhumiwa kwa mambo mbambali ambayo ni matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana na matokeo ya kazi yangu,”alisema Mbowe na kuongeza:
“Siilaumu Tume kwa lolote, naiheshimu sana na naheshimu kazi yao, niliona kuliko kujaza kwa makosa ni bora nichelewe kuileta,”alisema.

Mwenyekiti huyo wa Chadema alisema pia kutokana na mali na biashara alizonazo alishindwa kujaza fomu hizo kwa wakati kwa sababu ana makazi sehemu tatu na kote huko kuna mali zake.
“Naliomba radhi Baraza, ratiba yangu imekumbwa na mambo mengi sana. Mimi ni mbunge na ni kiongozi wa chama cha siasa hivyo, nilikosa utulivu wa kujaza fomu kwa wakati,”alisema.

Kapteni Komba adai jina lake limekatwa

Katika hatua nyingine, Mbunge wa Mbinga Magharibi, John Komba amesema ameshangazwa kuitwa katika baraza hilo wakati yeye alijaza fomu na kuirejesha kwenye Ofisi ya Bunge.

“Sina mali za kutisha hadi niogope kujaza fomu, mimi nina vijihela tu kidogo kama Mtanzania mwingine wa kawaida,”alisema Komba na kuongeza kuwa:
“Nina marafiki wengi kama kina Bakili Muluzi wamenipa mahela sasa ningeyafanyia nini,”:
Komba pia alilalamikia jina lake kukatwa katika orodha ya wabunge wengine ambao walikuwa wamerejesha fomu na kudai kuwa hiyo ni hujuma.

“Wana lao jambo haiwezekani jina langu liwemo kwenye orodha ya wabunge waliorejesha fomu halafu lionekane limekatwa,”alisema.
Mbunge huyo aliitaka tume hiyo iwasiliane na viongozi husika moja kwa moja badala ya kupitia kwa spika kwa sababu katika suala la kutangaza mali hawawajibiki kwa spika. Mwenyekiti wa baraza hilo, Jaji Damian Lubuva alisema baada ya kusikiliza utetezi wa viongozi hao watatoa uamuzi na mapendekezo yao kwenye mamlaka zinazohusika.

Wednesday, June 15, 2011

CCM WAFUTA POSHO ZA VIKAO


HOJA ya kutaka kufutwa kwa posho za vikao za wabunge na watumishi wengine wa umma imechukua sura mpya baada ya jana Mbunge wa Bumbuli (CCM), Januari Makamba kuliambia Bunge mjini hapa kuwa suala la kufutwa kwa posho ni la kitaifa na ni sehemu ya Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano uliowasilishwa na serikali.

Kauli hiyo ya Makamba ambaye pia ni Katibu wa Mambo ya Nje wa Sekretarieti ya CCM imekuja huku kukiwa na malumbano makali baina ya Spika wa Bunge, Anne Makinda na Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe kuhusu suala hilo la posho za vikao vya wabunge.

Juzi, Spika Makinda alisema Zitto ambaye ni Naibu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, anaweza kufukuzwa ubunge kwa kutosaini karatasi za mahudhurio, hatua ambayo Zitto alisema ataichukua ili asilipwe posho za vikao.

Spika alisema Zitto anaweza kukumbwa na adhabu hiyo iwapo hatasaini karatasi za mahudhurio ambazo ndizo zinathibitsha uwepo wa mbunge katika mikutano na vikao vya bunge na kwamba kanuni zinamwadhibu mbunge kwa kumfukuza asipohudhuria mikutano mitatu. Hata hivyo, Zitto amepuuza kauli hiyo ya Spika kwa kusema kwamba kama ni kwa ajili ya kukataa posho, yuko tayari kufukuzwa bungeni.

"Nitafanya hivyo tuone, Kanuni inasema mikutano mitatu mfululizo na siyo vikao vitatu mfululizo. Nitatumia uzoefu wangu wa siasa za wanafunzi kukwepa mtego wake. Lakini kama anadhani ni sawa kunifukuza ubunge kwa kukataa posho, nipo tayari," alisema.

Kauli ya jana ya Makamba pia inaonekana kutofautina na mawazo ya wabunge wengi wa CCM akiwamo Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo ambaye amesema wanashabikia suala hilo wanajitafutia umaarufu.

Akichangia huo wa maendeleo wa miaka mitano jana, Makamba alionekana kupigia chapuo suala la kufutwa au kuangaliwa upya kwa posho za vikao huku akisema kwamba ni la kitaifa na ni sehemu ya mpango huo.

Makamba alisema kuwa suala la nidhamu na usimamizi wa matumizi ya fedha za umma ni muhimu na kwamba mpango huo umeliona katika ukurasa wa 17 wa kitabu kilichochapishwa kwa Kiingereza na kutoa mapendekezo ya kufutwa kwa posho za vikao na zile za usafiri.

"Mpango unabainisha kwamba kuna umuhimu wa kufutwa kwa posho za vikao na usafiri hivyo iwapo wabunge mtalisikia likiwasilishwa hapa kwa mbwembwe kesho (leo), basi msije mkashangaa kwani ni sehemu ya mpango huu," alisema Makamba.

Kujadiliwa bungeni leo

Mjadala kuhusu malipo ya posho ambao umekuwa ukiendelea kwa wiki moja sasa hasa zaidi nje ya Bunge, leo unatarajiwa kuingizwa rasmi bungeni wakati Bajeti ya Serikali iliyowasilishwa na Mkulo Jumatano iliyopita itakapoanza kujadiliwa.

Suala hilo ni dhahiri litajitokeza katika bajeti mbadala itakayowasilishwa na kambi ya Upinzani Bungeni na Waziri Kivuli wa Fedha, Zitto Kabwe ambaye amekuwa katika mvutano usio rasmi na Spika kutokana na kukataa kulipwa posho za kikao.

Mwenyekiti wa Chadema ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alisema jana kuwa kambi yake inatarajiwa kutoa ushauri mgumu ambao haujazoeleka kwa watendaji wa serikali na kwamba suala la kufutwa kwa posho ni sehemu ya mapendekezo hayo.

Alisema kufutwa kwa posho hizo kunaweza kuokoa zaidi ya Sh900 bilioni ambazo zinaweza kuelekezwa katika maeneo mengine ya huduma kwa wananchi.

Uhalisia posho za wabunge

Mmoja wa wabunge wa CCM ambaye hakutaka kutaandikwa jina lake alisema anasikia kuhukumiwa katika nafsi yake kutokana na kupokea posho za vikao ambazo kimsingi ni sawa na "kuwaibia wananchi".

"Ujue bwana sisi ndani ya CCM mambo hayaendi kama kwa wenzetu (Chadema), wale wanaweza kukaa leo na kuamua, sisi ni tofauti lazima kuwepo na mchakato lakini ukweli ni kwamba hoja yao ni nzuri," alisema mbunge huyo.

Uchunguzi uliofanywa umebaini kuwa malipo ya wabunge yamegawanyika katika sehemu nne ambazo ni pamoja na mshahara ambao ni Sh2,300,000 kwa mwezi, posho ya ubunge kila mwezi ambayo ni Sh5 milioni, posho ya kujikimu (per-diem) Sh80,000 wawapo nje ya majimbo yao kikazi na posho ya vikao (sitting allowance) ambayo huwa ni Sh70,000 kwa kila mbunge.

Kwa maana hiyo, kwa kawaida mbunge hulipwa Sh7.3 milioni kila mwezi kabla ya kukatwa kodi na wawapo Dodoma na Dar es Salaam kwa ajili ya vikao vya kamati na bunge au mikoani kwa ajili ya kukagua shughuli zilizopo chini ya kamati zao. Hulipwa kiasi cha Sh150,000 kila mmoja kwa siku ambazo ni Sh70,000 kwa ajili ya vikao na Sh80,000 kwa ajili ya kujikimu.

Kwa maana hiyo bunge linatarajiwa kutumia kiasi cha Sh1.788 bilioni kwa ajili ya kugharamia vikao 73 vya Bunge la Bajeti iwapo wabunge wote 350 waliopo watahudhuria vikao hivyo.

Kwa hesabu hizo, kila mbunge katika mkutano wa Bunge la Bajeti anatarajiwa kuondoka na kikita cha Sh5.1 milioni mbali na Sh 5.58 milioni ambazo ni malipo kwa ajili ya kujikimu, fedha ambazo ni mbali na mshahara wake kwa mwezi na posho ya ubunge.

CCM yakataa posho

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeanza machakato wa kufuta posho hizo ikiwa ni hatua ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Habari kutoka ndani ya CCM, Dodoma na Dar es Salaam zinasema kuwa mkakati wa kufutwa kwa posho ulianzishwa takriban mwezi mmoja uliopita na sekretarieti mpya inayoongozwa na Katibu Mkuu, Wilson Mukama.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, baadhi ya wajumbe wa sekretarieti walihoji uhalali wa posho wanazolipwa hata pale vikao vinapofanyika katika sehemu ambako ni makazi yao na kwamba hoja hizo ndizo zilizozaa wazo la kufutwa kwa posho katika vikao.

"Hoja ilikuwa kwamba kama chama hakina fedha na tunataka kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, basi posho za vikao zifutwe kwa sababu hakuna ulazima wa posho hizo hasa kwa wajumbe wa sekretarieti ambao kazi zao ni za kila siku," kilieleza chanzo chetu na kuongeza:

"Hivi sasa mpango huo uko kwenye mchakato wa kuwekewa mwongozo na nadhani baada ya kupitia katika vikao vyetu utaanza kutekelezwa. Lakini kimsingi ni kama utekelezaji wake umeshaanza kwa sababu baadhi ya wajunbe wamekataa kabisa kusaini posho hizo."

Habari zaidi zinadai kuwa waraka wa mapendekezo ya kupunguza matumizi ndani ya CCM unakwenda mbali zaidi hadi katika matumizi ya magari na kwamba pale usafiri unapohitaji wa kuelekea kwenye mkutano mmoja, basi viongozi watumie magari machache kwa maana ya usafiri wa pamoja badala ya utaratibu wa sasa ambao unamruhusu kila kiongozi kutumia usafiri wake.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alipoulizwa kuhusu sekretarieti kufuta posho katika vikao vyake, hakukanusha wala kuthibitisha, badala yake akadai kuwa hayo ni mambo ya ndani ya chama ambayo hayana faida yoyote kwa umma.

"Hivi ninyi waandishi wa habari, haya mambo mnayapata kwa nani! Haya ni mambo ya ndani ya chama sidhani kama yana tija yoyote kwa umma, maana haiwezi kusaidia chochote," alisema Nape kwa kwa simu.

Alipoelezwa kwamba suala hilo lina uhusiano na sakata linaloendelea bungeni, Nape alisema: "Bunge ni bunge na chama ni chama. Kila taasisi inajitegemea na ina uamuzi wake, lakini pia sisi kama chama tulishatoa kauli mara nyingi kwamba suala la posho kwa wabunge na watumishi wengine wa serikali linazungumzika, ni la kisera na wanaohusika wapo waulizeni hao."

Mwishoni mwa wiki iliyopita Nape akizungumzia malumbano miongoni mwa wabunge kuhusu suala la posho alisema suala hilo linajadilika na kwamba si vyema kulipinga kwa sababu tu linatokea kambi ya upinzani.

Kwa upande wake, Makamba alipoulizwa kuhusu kufutwa kwa posho katika vikao vya Sekretarieti ya CCM naye kama ilivyokuwa kwa Nape, hakukanusha wala kuthibitisha.

"Wewe si unamfahamu msemaji wa chama ni nani? Mwulizeni Nape tena nadhani anakuja Dodoma. Akija mwulizeni, mimi siwezi kulizungumzia.... lakini ninyi waandishi haya mambo ya ndani ya chama huwa mnayapata wapi? Anyway, mwulizeni mwenezi atawaambia," alisema Makamba.

Chanzo: Mwananchi 15/6/2011

Monday, June 6, 2011

Hali tete: Chadema, Polisi wakwaruzana

Askari polisi wakilinda kwenye kituo kikuu cha polisi kati anakoshikiliwa mwenyekiti wa Chadema Freeman MbowePicha na Fidelis Felix/Silvan Kiwale


















JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, jana lililazimika kuimarisha ulinzi katika Kituo chake Kikuu (Central) na baadhi ya maeneo ya jiji kukabiliana na tishio la wanachama wa Chadema kuandamana ili kushinikiza Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe aliyekamatwa juzi aachiwe.Mbowe ambaye alikamatwa juzi ikiwa ni kutekeleza amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha iliyoamuru akamatwe popote alipo na afikishwe hapo kwa kutotii amri ya kufika mahakamani katika kesi inayomkabili, alitarajiwa kupelekwa huko wakati wowote kuanzia jana akiwa chini ya ulinzi.

Jana, vijana wa Chadema walikusanyika katika kituo hicho huku wakilaani kitendo cha kukamatwa kwa mwenyekiti wao huku wengine wakijikusanya katika vikundi vidogovidogo katika maeneo mbalimbali katika Barabara za Morogoro na Nyerere, lengo likiwa kushinikiza kiongozi huyo atolewe rumande na asisafirishwe kupelekwa Arusha.

Taarifa kutoka Arusha ambako kesi ya kiongozi huyo inatarajiwa kuendelea leo asubuhi zinaeleza kuwa polisi jana jioni waliendesha msako wa wanachama wa Chadema waliokuwa wakihamasishana kuhudhuria kwa wingi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Arusha.

Wanachama na mashabiki hao wa Chadema walidai kwamba kitendo cha kukamatwa kwa kiongozi huyo wa kambi ya upinzani bungeni ni mpango uliobuniwa na CCM wa kubinya demokrasia ya vyama vingi nchini.

Mbowe na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, Zitto Kabwe walikamatwa katika maeneo tofauti nchini juzi. Wakati Mbowe alidaiwa kutotii amri ya mahakama, Zitto alidaiwa kuzidisha muda wakati wa kuhutubia mkutano wa hadhara mkoani Singida.

“Tumeongea na polisi, bado wanamng'ang'ania Mbowe. Msimamo wao ni kumpeleka Arusha, tuangalie utaratibu utakaotumika katika kumsafirisha,” alisema Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Chadema, John Mnyika.

Baada ya kauli hiyo ya Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Ubunge, vijana wa chama hicho wakiongozwa na Diwani wa Kata ya Ubungo, Boniface Jacob walianza kuimba nyimbo za kulaani kukamatwa kwa mwenyekiti wao huku wakisema muziki wa Chadema polisi hawauwezi.

Ofisa mmoja mwadamizi wa Polisi Ilala ambaye hakujitambulisha jina aliwaambia vijana hao kuwa polisi  walishakubaliana na viongozi wa Chadema kuwa mtuhumiwa huyo amepangiwa utaratibu wa kusafirishwa kwenda Arusha kuhudhuria kesi yake.Ofisa huyo aliwataka wananchi waliokuwa kwenye eneo hilo kuondoka ili kupisha jeshi hilo kuendelea na kazi ya kutoa huduma kwa watu wengine.

“Tumeshaongeza na wakubwa wenu, hiki ni kituo cha polisi watu mbalimbali wanakuja kupata huduma hapa. Mtu haji kuangaliwa kwa aina hii ya hamasa na nyimbo, tunaomba muondoke,” alisema ofisa huyo.Kauli hiyo ilipingwa na vijana hao wakisema ofisa huyo ni mtu wa kawaida hawezi kuwaeleza mambo kama hayo.

“Sisi hapa tuna viongozi wetu mambo kama hayo tungeelezwa na kuelewa kama yangesemwa nao na si mtu wa kawaida kama wewe,”alisikika mmoja wa wanachama hao akisema kwa sauti.

Kauli hiyo ilimshangaza ofisa mwingine wa polisi aliyeibuka na kuhoji: “Mnasema huyu ni mtu wa kawaida? Akajibiwa “ndiyo”, “huyo siyo mtu wa kawaida."Vijana hao waliendelea na msimamo wao: “Sisi tunasema huyo ni mtu wa kawaida kwa sababu siyo kiongozi wetu, ndiyo maana tunasema angekuwa kiongozi wetu tungemwelewa.”

Kauli hiyo ilimlazimisha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Faustine Shilogile kujitokeza na kuwataka watu hao kuondoka katika eneo hilo kwa sababu kulikuwa na shughuli mbalimbali zilizokuwa zikiendelea.

“Tumeongea na viongozi wenu, tumeshakubaliana tunawaomba mtawanyike na sisi tuendelee na kazi, sitaki mkusanyiko wowote katika kituo cha polisi,” alisema Shilogile. Mara baada ya kauli hiyo gari la maji ya kuwasha lilianza kusogea walipokuwa wafuasi hao wa Chadema likitanguliwa na Polisi wa Kutuliza Ghasia waliokuwa wakiwafukuza katika eneo hilo.

Kundi hilo liliondoka na kuelekea makao makuu ya Chadema ambako Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa alikuwa na mkutano na waandishi wa habari.

Msimamo wa Kamanda Kova
Akizungumzia mvutano huo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema jeshi lake haliwezi kumwachia Mbowe kwa sababu wanaheshimu amri ya Mahakama.

Kova aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba jeshi hilo lilipokea amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha ya kumkamata kiongozi huyo wa Chadema na kwamba hawaruhusiwi kuhoji lolote juu ya amri hiyo.

“Sisi kama jeshi la Polisi tumepokea amri ya mahakama ya kumtia hatiani Mheshimiwa Mbowe na hatuna mamlaka ya kumwachia huru hadi mahakama itoe amri ya kumwachia,”alisema.

Alisema sheria hairuhusu kuhoji sababu za amri inayotolewa na mahakama na kufafanua kuwa hizo ni sheria zilizotungwa na wabunge wenyewe. Alisema Mbowe anatarajiwa kusafirishwa chini ya ulinzi wa Polisi kwenda mkoani Arusha kujibu kesi inayomkabili na kwamba taratibu zote za safari tayari zimekamilika.

“Tunachokifanya ni maagizo ambayo yametoka ngazi ya juu kuhusu suala hili kwa hiyo Mbowe atapelekwa Arusha chini ya ulinzi wa polisi muda wowote kuanzia sasa alimradi awahi muda wake wa mahakama,”alisema Kova.

Alisema atapelekwa Arusha chini ya ulinzi wa polisi kwa sababu amekiuka masharti yake ya dhamana na kwamba tayari wamezungumza na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani waliokwenda kumuona kiongozi huyo wa kambi ya upinzani bungeni jana.

Kova alisema kulingana na taratibu na sheria za Tanzania, mahakama ikitoa amri hakuna mtu anayeweza kuipinga.

Aliwataka wananchi watulie na kuipa fursa mahakama itekeleze sheria zilizotungwa na Bunge. Akizungumzia kukamatwa kwa Mbowe, Mnyika alisema hizo ni njama za kuudhalilisha upinzani na pia mbinu za kumtaka Mbunge huyo wa Hai asihudhurie kwenye Kikao cha Bunge la Bajeti.

“Endapo watashindwa kutumia busara za mazungumzo tuliyoyafanya kumwachia Mbowe, jambo hili tutalirudisha kwa wananchi na nguvu ya umma itatumika kusuluhisha tatizo hilo,” alisema.

Alisema amani ni tunda la haki lakini inaweza kupotea kama haki haitatendeka na kuongeza kuwa kuna watu ambao wanashutuma nzito za ufisadi, lakini hawachukuliwi hatua zozote isipokuwa viongozi wa upinzani.


Tamko la Dk Slaa
Dk Slaa alisema kesi zinazowakabili viongozi wa chama hicho na wabunge wa vyama vya upinzani vinalifedhehesha Bunge la Tanzania kimataifa.

“Ili mtuhumiwa akamatwe sheria iko wazi, notisi zilitakiwa kutolewa kwa mdhamini wake na pia kwa wakili, lakini kwa Mbowe haikuwa hivyo na hiyo inaonyesha ni agizo kutoka mahali Fulani,” alidai.

“Polisi mkoa wa Mwanza wametuma barua kwa Katibu wa Bunge kuomba kibali cha kwenda kumhoji Mbunge wa Jimbo la Busega, Dk Titus Kamani, iweje kwa wabunge wa upinzani kukamatwa bila utaratibu? Alihoji Dk Slaa.

Alisema kutokana na mazingira hayo kama Mbowe hatafikishwa leo mahakamani wabunge wa Chadema hawataingia bungeni.

Kuhusu uwakilishi kwenye kamati ya uongozi alisema hata kama Zitto atakuwa nje ya mahabusu, hataingia kuwakilisha upinzani kwa sababu anayetakiwa kumpa kibali cha kufanya hivyo yupo ndani.

Kuhusu kosa la Zitto kukamatwa na polisi alisema inashangaza kwa sababu alikuwa kwenye mkutano wa hadhara kama mbunge na alizidisha dakika 20 kwenye mkutano huo.

Alisema hiki siyo kipindi cha kampeni na Zitto ni kiongozi mwenye haki ya kufanya hivyo na kusisitiza kilichofanyika kimelenga kufifisha demokrasia nchini.

Friday, June 3, 2011

Mahakama yaamuru Mbowe akamatwe

















 MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha, imetoa amri ya kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe popote alipo na kufikishwa mahakamani hapo kwa kile kilichoelezwa kuwa ni kutotii amri ya kufika mahakamani hapo. Mahakama hiyo pia imemtaka mdhamini wa Mbowe aliyetajwa kwa jina la Julius Isaya Magwe, kufika mahakamani hapo mara moja ili kuieleza mahakama hiyo sababu za kutotii amri ya mahakama pale anapohitajika.

Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Charles Magesa alisema jana kuwa kimsingi Mahakama inakubaliana na hoja ya wakili upande wa Serikali kuitaka mahakama kutoa amri ya kukamatwa kwa Mbowe kwa sababu ya kutotii amri ya kufika mahakamani au kumtuma mdhamini wake. Alisema sababu iliyotolewa mahakamani hapo kwamba mshtakiwa huyo ni mbunge na yupo kwenye vikao vya Kamati za Bunge haina uzito kwa kuwa hiyo ni moja ya shughuli zake kama ilivyo shughuli nyingine kwa watumishi wa serikali.

“Hivyo basi kama ni shughuli zake za kawaida, haimzuii kutii amri ya mahakama pale anapoitwa bila kujali anaitiwa nini,” alisema Magesa. Hakimu Magesa alisema kuwa anachokumbuka ni kwamba Mahakama hiyo kweli ilipokewa maelezo ya kuwa washtakiwa hawatahudhuria mahakamani hapo Mei 27 mwaka huu kwa sababu ya kuwa katika vikao vya Kamati za Bunge na kuagiza waje wadhamini wao siku kesi inapotajwa. Ndiyo sababu Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini alimpeleka mdhamini wake mahakamani hapo.

Lakini, kabla ya kuhitimisha agizo hilo, hakimu huyo, awali alitoa amri ya kutaka kukamatwa kwa Mbunge wa Moshi Mjini, Philimon Ndesamburo, ambaye naye hakutii amri ya mahakama kwa kutofika Mei 27, 30 na 31 na hata jana.

Hata hivyo, baada ya kutoa amri ya kukamatwa kwa Ndesamburo ambaye naye ni mshtakiwa, ghafla alijitokeza mdhamini wake, Rubeni Ngowi na kuiambia mahakama hiyo kuwa alikuwapo Mei 30, ila hakuweza kusogea mbele kwa sababu ya woga wa mahakama na kwa kuwa hakuitwa. Baada ya maelezo hayo, Hakimu Magesa alimhoji mdhamini huyo akitaka kujua alikuwa wapi Mei 27 mwaka huu kesi hiyo ilipotajwa. Ngowi alijitetea kuwa alikwenda jijini Dar es Salaam kwa familia yake ambayo ilikuwa ina matatizo, lakini Mei 30 alifika mahakamani hapo na kuomba kuondoa amri hiyo ya kukamatwa kwa mshtakiwa wake.

“Basi kwa sababu nakumbuka ulikuwapo Mei 30 na nilikuona hapa mahakamani ukimnong’oneza wakili Kimomogoro, basi naondoa amri hii. Ila naomba utii amri ya mahakama pale mshtakiwa anapokosa uje kutoa sababu za kukosa kwake,” alisema Magesa.

Hakimu Magesa pia alitoa onyo kwa washtakiwa wengine wakiongozwa na Dk Willibrod Slaa wasiache kufika mahakamani, kila siku kesi yao inapotajwa na pale wanapokuwa na sababu ya kutofika, wahakikishe wadhamini wao wanakuwapo kutoa sababu za kukosekana kwao.

Akitoa uamuzi wa hatima ya dhamana za washtakiwa wa kesi inayowakabili viongozi wa Chadema, Godbless Lema, Joseph Selasini na wafuasi wao, Hakimu Mkazi Magesa, alisema Mahakama hiyo imeondoa hati ya kukamatwa kwa washtakiwa hao kama ilivyoamriwa awali na kutupilia mbali ombi la wakili wa serikali la kutaka wafutiwe dhamana.

Alisema kuwa kutokana na kupitia kwa makini maelezo ya utetezi wa pande zote mbili kwa Wakili wa Serikali, Edwin Kakolaki na wakili upande wa utetezi, Medhod Kimomogoro, Mahakama hiyo imeamua kuwapatia dhamana ya kudumu washtakiwa ambao ni Dk Slaa na wenzake, kwa kutii amri ya Mahakama.

“Mahakama hii imeamua kufuta amri ya dhamana ya muda na kuacha dhamana ya awali kwa sababu mara mahakama hii ilipotoa amri ya kuwakamata Mei 27 mwaka huu, washtakiwa hao walifika mahakamani hapa kujisalimisha wenyewe na wengine, akiwamo Mbunge Joseph Selasini, alituma mdhamini wake, hivyo nawaachia dhamana zao,” alisema Magesa.

Kesi hiyo ilifunguliwa na Serikali, Januari 5 mwaka huu ambapo washtakiwa 19 walifikishwa mahakamani hapo na kusomewa shtaka la kufanya kusanyiko pasipo na kibali na kutoa maneno ya uchochezi. Washtakiwa walikana makosa yao na kwa sasa wako nje kwa dhamana hadi Juni 24 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Akizungumza na Mwananchi jana jioni, Mbowe alisema anatarajia kutoa tamko kuhusu suala hilo leo saa tano asubuhi jijini Dar es Salaam, lakini alikataa kutaja ni wapi mkutano wake na waandishi wa habari utafanyika.

“Nitatoa tamko kesho, lakini nasikitishwa na tafsiri hii ya Mahakama kwamba mimi nimekaidi amri ya kufika katika vikao vya mahakama. Nasema hivyo kwa sababu mara ya mwisho tulipokuwa mahakamani, tulipewa ruhusa ya kuhudhuria vikao vya Kamati za Bunge,” alisema Mbowe na kuongeza:
“Sasa sijui tafsiri yake ni nini, lakini niseme tu kwamba haya yote kuhusu sakata la Arusha na amri za polisi kuwakamata wabunge wa opposition (upinzani) nitalizungumza kesho (leo) kwa vyombo vya habari”.

Kwa mujibu wa Mbowe, waliomba ruhusa ili kuwawezesha kushiriki vikao vya Kamati za Bunge kutokana na umuhimu wa masuala ya bajeti kwa umma ambayo pia yanawagusa mahakimu na Idara ya Mahakama kwa jumla.

“…hebu kama mnakumbuka, katika Bunge lililopita tulijadili ule muswada wa sheria unaogusa idara ya mahakama sisi wabunge wa upinzani tulitumia nguvu kubwa kuwatetea mahakimu katika mambo mengi. Sasa katika suala hili la bajeti si vizuri tukikosekana kwenye vikao na ndiyo maana tuliomba ruhusa siku ile na tukaruhusiwa, ”alisema Mbowe.

Monday, May 30, 2011

Mtikila: Ridhiwani nenda mahakamani




Mchungaji Christopher Mtikila
LICHA ya mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani kuwaandikia barua ya kusudio la siku 10 kuwafikisha mahakamani Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa na Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameambiwa aende huko mahakamani.

Katika kusudio lake Ridhiwani amedai kuwa endapo watashindwa kumwomba radhi na kumlipa Sh2 bilioni atakwenda mahakamani.Katika kusudio hilo, Ridhiwani amewataka wanasiasa hao wamwombe radhi na kumlipa fidia hiyo ndani ya siku kumi kuanzia Mei 13, kwa madai waliyoyatoa hadharani kuwa yeye ni bilionea aliyetajirika kifisadi.

Katika kusudio hilo, Ridhiwani pia amehusisha gazeti la Tanzania Daima ambalo amedai limechangia kumchafua kwa kuripoti madai ya wanasiasa hao dhidi yake.

“Tumeelekezwa na mteja wetu kuwataka wote kwa pamoja kukanusha na kusahihisha tuhuma zote na kuchapisha habari hiyo ya kuomba radhi kwa uzito na herufi kubwa (bold print) katika kurasa za mbele  wa gazeti hilo (Tanzania Daima) kwa siku tatu mfululizo hadi Mei 23, 2011," alieleza wakili Sam Mapande wa Law Associates, anayemwakilisha Ridhiwani.Wakili huyo aliendelea, "Pia, wote kwa pamoja mnatakiwa kulipa fidia ya Sh2 bilioni kwa madhara ya jumla aliyopata mteja wetu.”

Barua hiyo ya kurasa sita  imetaja baadhi ya maneno yaliyoandikwa kwenye matoleo mawili ya gazeti la Tanzania Daima yakimkariri Dk Slaa na Mchungaji Mtikila, wakimhusisha pia Rais Jakaya Kikwete na mwanaye (Ridhwani) na watu wengine walio karibu yake na matukio ya ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka na ofisi ya umma. Kwa mujibu wa Ridhiwani, madai hayo yamemchafulia jina, kumdhalilisha, kumshushia hadhi na heshima yake katika jamii inayomzunguka.

Mhariri wa gazeti la Tanzania Daima, Absalom Kibanda amekiri kupokea barua hiyo, lakini akasema hawezi kusema chochote kwa jambo ambalo ni la kisheria. “Kwa kuwa bado hatujafikishwa mahakamani, siwezi kusema tumejiunga vipi. Tunasubiri tufikishwe mahakamani kwanza,” alisema Kibanda.

Mchungaji Christopher Mtikila amemtaka mtoto huyo wa rais kwenda mahakamani haraka akidai kuwa hana shaka kwa kuwa ana ushahidi mzito kuthibitisha madai yake.Mtikila aliwaambia waandishi wa habari mjini Arusha jana kuwa, kesi hiyo itakuwa ni ukombozi kwa taifa kwa sababu itampa yeye na mwenzake, Dk Slaa muda wa kueleza kile alichokiita madudu yanayofanywa na mtoto huyo wa rais.
Mtikila aliendelea kudai kuwa Ridhwani anatumia vibaya ofisi na madaraka ya baba yake (Rais Kikwete) kujilimbikizia mali kinyume cha sheria.

“Kitendo cha Ridhwani kutaka aombwe radhi na fidia ni njia na ngazi muhimu itakayosaidia mambo mengi yaliyojificha kuwekwa hadharani," alisema Mtikila na kuongeza:"Tutatumia sheria zilizopo kuwabana wote ambao majina yao yameandikishwa kwenye mali za vigogo nchini waeleze walivyopata mali hizo na hapo ndipo watakapowataja wahusika halisi,” alisema Mtikila.

Kiongozi huyo wa DP aliendelea kudai kuwa viongozi wengi nchini wamejilimbikizia mali kupitia wizi na ufisadi, wakitumia nafasi zao za umma huku wakiandikisha majina ya watu wengine kwenye mali hizo kuficha umiliki wao.

Alidai kuwa kesi anayotaka kuifungua Ridhiwani itaibua mambo mengi kwani walioandikishwa majina kwenye mali hizo, watawataja wamiliki halisi badala ya kufungwa jela kwa kumiliki mali inayodhaniwa kuwa ya wizi au kupatikana isivyo halali.

Kwa upande wake, Dk Slaa jana hakupatikana kuzungumzia kusudio hilo la Ridhiwani kutokana na simu yake ya kiganjani kutopatikana kwa siku nzima.

Jana, Ridhiwani alipotakiwa kueleza nini kinafuata baada ya muda aliotoa kuisha alijibu kwa ufupi kuwa asingependa kuzungumzia suala hilo kwa kuwa ni jambo la kisheria na kwamba sheria ina kanuni zake.

"Ndugu yangu, sitaki kuzungumzia hili kwa kuwa sheria ina kanuni zake. Hili litazungumzwa mahakamani."
Dk Slaa na Mtikila walikaririwa mwanzo wa Mei wakisema kuwa mtoto huyo wa rais ana utajiri mkubwa licha ya kumaliza shule miaka ya karibuni huku wakimtuhumu kutumia cheo na madaraka ya baba yake kujitajirisha.
 

Thursday, May 26, 2011

Lissu na wenzake marufuku Nyamongo

Maiti wazikwa, wananchi wataka kurejesha majeneza polisi



 
















MBUNGE wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Katiba na Sheria, na wenzake saba ambao juzi walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Tarime na kusomewa mashtaka matatu ya kuingia eneo la hospitali bila kibali, kufanya mkutano na kuzuia watu kufanya kazi, wamepata dhamana lakini wamezuiwa kutembelea maeneo ya Nyamongo hadi kesi inayowakabili itakapokwisha.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya hiyo, Yusto Roboroga alitoa uamuzi huo akisema ni kwa mujibu wa kifungu cha Sheria Namba 148 cha Makosa ya Jinai, kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2002, ambacho kinatoa haki kwa watuhumiwa kupata dhamana. Alitoa uamuzi huo baada ya kupitia pingamizi lililowekwa na upande wa mashtaka kutaka wasipewe dhamana. Hata hivyo, alisema: “Washtakiwa wanazuiwa kutembelea maeneo ya Nyamongo mpaka kesi hiyo itakapokuwa imekwisha."

Hakimu huyo alisema kwa kuwa washtakiwa hao ni viongozi wakubwa wa chama walizuiwa ili kupunguza shinikizo la wanachama kutokana na tukio lililojitokeza, lakini kwa kuwa mazishi yameshafanyika, alisema wanaweza kudhaminiwa kama watakidhi masharti.

Hakimu Ruboroga alitaja masharti  ya dhamana hiyo kuwa ni kusaini mkataba wa dhamana wa Sh5 milioni kwa wadhamini wawili wanaoaminika.

Kwa wasio wakazi wa Tarime, alisema watatakiwa kupeleka mahakamani hati za mali isiyohamishika. Washtakiwa wote walikidhi masharti na kuachiwa kwa dhamana hadi Juni 26, mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Juzi, Lissu na wenzake, Waitara Mwita Mwikwabe, Stanslaus Nyembea, Anderson Deogratias Chacha, Andrew Andalu Nyandu, Mwita Marwa Maswi, Bashiri Abdalllah Selemani na Ibrahimu Juma Kimu walifikishwa mbele ya mahakama hiyo na kusomewa mashtaka hayo matatu na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Casmir Kiria ambaye alisema, waliyatenda Mei 23, majira ya saa nne usiku. Wote walikana mashtaka hayo.

Wakati huo huo maiti wote waliokuwa wametelekezwa barabarani wamezikwa na ndugu zao huku baadhi ya familia zikikataa kuwazika kwa majeneza ya polisi na kutumia yale yaliyokuwa yameandaliwa huku wengine wakipanga kuyarudisha kwa Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Tarime, Constantine Massawe.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kewanja, Om’tima Tanzania alisema kuwa mmoja wa marehemu hao, Chacha Ngoka alizikwa na jamii. Hata hivyo, alisema polisi waliweka mwili wake ndani ya jeneza bila kuweka sanda hali ambayo iliwalazimu kumweka ndani ya jeneza lao na kumvika sanda. Hilo lilifanyika pia katika eneo la Nyakunguru alikozikwa marehemu Emmanuel Magige.

Katika Kijiji cha Bonchugu, Serengeti, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Mwikwabe Makena alidai kwamba walilazimika kuzika mwili wa marehemu Chawali Bhoke uliotelekezwa na polisi.


Alidai kwamba kabla ya kuutelekeza, walifyatua mabomu ya machozi na risasi hewani baada ya wananchi waliokuwa wamebeba pinde, mishale, mikuki na mapanga kujaribu kuzuia gari la polisi. Alisema walilazimika kuzika bila kuwapo kwa ndugu wa marehemu waliokuwa wameachwa Tarime.Hata hivyo, Kamanda Massawe na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Robert Boaz hakuwa tayari kuzungumzia madai hayo.

Wednesday, May 25, 2011

Polisi 'wapora' maiti mochwari

*Tundu Lisu akamatwa, afikishwa kortini Tarime

JESHI la Polisi limewakamata na kuwafikisha mahakamani Mbunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) pamoja na maofisa wengine wa chama hicho baada ya kudaiwa kufanya mkusanyiko usio halali na kuzuia watu kuzika ndugu zao.

Sambamba na hatua hiyo jeshi hilo limedaiwa kuingia mochwari ya Hospitali ya Wilaya ya Tarime na kuchukua kwa nguvu maiti nne za watu waliouawa na polisi hivi karibuni na kwenda kuzitelekeza maeneo mbalimbali ili kuzuia mkusanyiko wa kuaga maiti hizo kwa pamoja, kwa kile wanachoeleza ni kuzuia uvunjifu wa amani.

Bw. Lisu na wenzake wanadaiwa kukutwa katika Hosptali ya Wilaya ya mjini hapo wakilinda miili hiyo baada ya kusikia tetesi kuwa polisi walikuwa na mpango wa kuichukua na kuisafirisha kusikojulikana.

Akizungumza na waandishi wa habari nje ya mahakama, Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Bw. Casmil Kria alisema watuhumiwa wanakabiliwa na mashtaka matatu, yaliyosomwa mbele ya Hakimu wa Wilaya, Bw. Yusto Ruboroga.

Mashtaka hayo ni kuingia eneo la hospitali bila kibali, kufanya mkusanyiko usio halali na kuzuia watu kuchukua miili ya ndugu zao.

Watuhumiwa hao ambao wanadaiwa kukutwa eneo hilo saa 4:00 usiku baada ya kusomewa mashtaka na kuyakana, walirudishwa rumande kwa 'sababu za kiusalama', na kesho watafikishwa tena mahakamani kwa ajili ya kupewa dhamana, endapo miili ya waliouawa itakuwa imeshazikwa.

Walioshtakiwa ni Mbunge wa Singida Magharibi, Bw. Tundu Lissu (43), Bw. Mwita Mwikwabe (36), Bw. Stancelaus Nyembea (33), Anderson Deogratias (35), Bw. Andrew Andaru (63), Bw. Mwita Marwa (48) Bw. Bashiri Abdallah Seremani (35) pamoja na Ibrahimu Juma Kimi (27) ambaye ni dereva wa Bw. Lissu.

Wakati huo huo, waandishi wanne wa habari pamoja na Mbunge Viti Maalumu, Bi. Ester Matiko (CHADEMA) nao walishikiliwa na Jeshi la Polisi katika Kituo Kidogo cha Nyamwaga na baadaye kuachiwa huru baada ya mahojiano.

Wandishi hao ni Bi. Beldina Nyakeke wa The Citizen, Anna Mroso (Nipashe), Bw. Anthony Mayunga (Mwananchi) pamoja na Mabere Makubi wa Chanel Ten ambao walikuwa kwenye msafara wa Bi. Matiko.

Waandishi wengine wa habari waliofika katika mahakama ya wilaya kufuatilia tukio hilo walizuiliwa kuingia na kutishiwa kupigwa
risasi na ofisa mmoja wa polisi.

Ofisa huyo ambaye hakufahamika jina aliwatimua waandishi hao, huku akiomba bunduki kutoka kwa askari mwenzake na kuiandaa mithili ya kupambana na adui.

“Toka! Toka! Naombeni bunduki yangu hapa naona nyinyi hamjui kufanya kazi, hatukuja kufanya mchezo hapa waondoe na wale watu upesi mahali hapa wasongee mbali huko hatutaki mtu hapa!” alisema.

Askari hao wakiwa wameziba njia huku ofisa huyo akiendelea kuelekeza bunduki yake kwa raia waliokuwa eneo hilo.