Tuesday, March 29, 2011

20 PERCENT AWAANGUSHA MASHAROBARO - KILI MUSIC AWARDS



Abbas Hamis, marufu kama “20 percent” aliwashangaza masharobaro na kuibuka mfalme pale alipojinyakulia Tuzo tano katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam, siku ya jumamosi usiku.

20 percent ambaye hakuwepo ukumbini, alijitwalia tuzo za Mwanamuziki wa mwaka wa kiume, Mwanamuziki bora wa kiume na Mwandishi bora wa Mwaka, ambapo nyimbo zake mbili “Tamaa mbaya” na “Ya nini Malumbano” zilipigiwa kura kwa Wimbo wa mwaka, na Wimbo bora wa Kiafrika. Nyota huyo ni Mwimbaji na mtunzi bora.

Tuzo za 20 percent zilipokelewa na producer wake Man Walter

No comments:

Post a Comment