Showing posts with label kikwete. Show all posts
Showing posts with label kikwete. Show all posts

Monday, August 8, 2011

JK amuangukia Rostam

Rais Kikwete na Rostam Aziz

RAIS Jakaya Kikwete sasa anapanga kumuangukia aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, MwanaHALISI limeelezwa.

Taarifa kutoka ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zinasema tayari chama hicho kimepanga kumuita Rostam katika mkutano wa Kamati Kuu (CC) uliopangwa kufanyika 30 Julai 2011 kwa lengo la kumwangukia.

Kada mmoja wa chama hicho aliye karibu na Rostam anasema kumekuwapo na shinikizo kutoka kwa baadhi ya viongozi wajuu wa CCM na serikali wakitaka Rais Kikwete awasiliane na Rostam ili amwombe kuhudhuria kikao cha CC kwa lengo la kumwomba msamaha ili hatimaye asaidie kampeni za uchaguzi mdogo katika jimbo la Igunga utakapotangazwa.

“Ni kweli kuna mpango wa kumuita katika Kamati Kuu. Lengo ni kumuomba atusaidie kufanikisha kampeni za Igunga, ambako kwa kweli CCM kinakabiliwa na kibarua kigumu kutetea kiti hicho kutokana na kutokuwa na maandalizi ya uchaguzi katika kipindi hiki,” ameeleza mtoa taarifa wa gazeti hili.

Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja wiki mbili baada ya mwanasiasa huyo kujiuzulu nyadhifa zake zote za uongozi ndani ya chama hicho kwa madai ya kuchoshwa na siasa uchwara. Mara baada Rostam kujivua nyadhifa hizo na kuandika barua kwa Spika wa Bunge la Jamhuri Anne Makinda na Rais Kikwete, akiwataarifu uamuzi wake huo aliokwishautangaza mbele ya vyombo vya habari, aliondoka nchini kuelekea Uswisi kwa kile kilichoitwa “safari ya mapumziko.”

Rostam aliondoka tarehe 14 Julai 2011 saa 10.40 alasiri, kwa ndege Na. EK 725 ya Shirika la Ndege la Emirates la Nchi za Falme za Kiarabu, siku moja baada ya kutangaza kujiuzulu ubunge na ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya chama chake.

Kiongozi mmoja wa ngazi ya juu ndani ya CCM aliliambia gazeti hili: “Uamuzi wa Rostam kuachia nafasi zake zote za uongozi umelenga kupeleka ujumbe maalum kwa Rais Kikwete, kwamba hakufurahishwa na hatua yake ya kumtumia Nape Nnauye kumshambulia yeye na wenzake majukwaani.”

Rostam alikuwa mbunge wa Igunga, mkoani Tabora tangu mwaka 1994 na mjumbe wa NEC kwa vipindi viwili.

Hata hivyo, habari zinasema hata kama mkakati wa kumuita kada huyo kwenye CC utashindwa kufanikiwa, Rais Kikwete ataendelea kumuomba asaidie kampeni za uchaguzi mdogo wa Igunga.

Tayari Makinda ameijulisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kujiuzulu kwa Rostam, na hivyo kuwapo uwezekano mkubwa wa kufanyika uchaguzi wa jimbo hilo ndani ya kipindi cha miezi mitatu ijayo.

MwanaHALISI limenukuu vyanzo kadhaa vya taarifa, akiwamo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano ya Umma), Steven Wasira, akitaka Rostam aitwe kusaidia kampeni za CCM. Wasira, ambaye alikuwa mstari wa mbele kutaka Rostam aondoke kwenye chama hicho, alimweleza mjumbe mmoja wa NEC, siku moja baada ya Rostam kujiuzulu, “…Kama tunataka kushinda Igunga, sharti tumuombe Rostam atusaidie. Nimeongea naye na amekubali kusaidia kampeni za Igunga.”

Hata hivyo, wachambuzi wa mambo ya kisiasa wanasema hatua ya CCM kutaka kumuangukia mwanasiasa huyu anayekabiliwa na tuhuma za ufisadi kutazidi kukichafua chama hicho mbele ya wananchi na jumuiya ya kimataifa.

Hata hivyo, zipo taarifa kuwa Rostam hataki kabisa kujihusisha na uchaguzi mdogo wa Igunga. Inaeleweka kuwa ndiye amekuwa nguzo ya CCM mkoani Tabora, kwa kutumia ushawishi wake na nguvu ya kipesa kuhakikisha wapinzani hawapiti.

Hofu ya makada na viongozi wa CCM inatokana na ukweli kwamba Rostam aliwashtukiza, kwani walipokuwa wakimtaka aondoke kwenye NEC, hawakutarajia kwamba angejiondoa kwenye ubunge.
Kutokana na hali hiyo, sasa wameanza kushikwa na ‘kigugumizi’ cha kuwachukulia hatua makada wengine wawili, Edward Lowassa na Andrew Chenge ambao, kama Rostam, wamekuwa wanashambuliwa na kuambiwa waondoke, kama njia ya utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba.

Lowassa na Chenge wanadai Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, anatumia vibaya dhana hiyo kuwashambulia. Habari zinasema Lowassa hatafuata nyayo za Rostam za kuachia ngazi, lakini kama chama kitaamua kumfukuza atajivua nafasi zote za uongozi ndani ya chama hicho, ukiwamo ubunge wa Monduli.
Iwapo hilo litatokea, CCM kitakuwa kimejiingiza katika mgogoro kama wa Igunga.

Kwa uchache, habari zinasema wabunge tisa wakiwamo waziri mmoja na manaibu mawaziri wawili wameapa kumfuata Lowassa. Majina ya mawaziri na manaibu mawaziri hao tunayahifadhi kwa sasa.

Wakati Lowassa akiapa kutoachia ngazi, habari zinasema CCM inajiandaa kumlazimisha ajiuzulu. Aliyepangwa kuendesha kampeni ya kusimamia hatua hiyo ni Waziri Mkuu Mstaafu, Cleopa Msuya.
Hata hivyo, wapo wanaodai iwapo Lowassa ataondolewa kwenye uongozi kutaibuka mgogoro ndani ya Bunge kwani ana ushawishi mkubwa miongoni mwa wabunge wengi wa CCM. Baadhi ya maswahiba zake ni wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge. Kwa sasa Lowassa yuko safarini nje ya nchi kikazi. Anatarajiwa kurejea nchini kabla ya vikao vya chama vinavyotarajia kumjadili.

Wakati hayo yakitendeka, mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (UV-CCM), uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Dodoma, ulimalizika kwa wajumbe wa pande za Lowassa na Kikwete kushambuliana. Wakati kundi la Kikwete likitaka chama kichukue hatua kwa kupongeza maamuzi ya NEC ya kujivua gamba, upande wa Lowassa ulipinga kwa madai kuwa dhana ya kujivua gamba imetafsiriwa vibaya, na inakiangamiza chama.

Mtoa taarifa aliyekuwa ndani ya mkutano huo amemweleza mwandishi wa habari hizi kuwa mvutano huo uliishia kwa wajumbe “kumshambulia” kwa maneno makali Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama.
Miongoni mwa wengi, mjumbe wa Baraza Kuu, John Nchimbi, alinukuliwa akimweleza Mukama amejiingiza katika vita ya makundi bila ya kujua.

“Umekuja hapa kuponda kauli ya Mheshimiwa Lowassa juu ya serikali kushindwa kufanya maamuzi magumu, ukatoa mfano wa kesi ya City Water. Umesema kesi ile imegharimu serikali Sh.9 bilioni zikiwa gharama za kulipa wanasheria. Lakini mbona hukusema kiasi ambacho serikali imelipwa kutokana na kushinda shauri hilo mahakamani?” alihoji Nchimbi kwa sauti ya ukali.

Alisema, “Acheni unafiki. Mtaangamiza chama. Kama wewe ni mkweli, mbona hujasema kama serikali ilishinda kesi ile na imelipwa mamilioni ya shilingi? Au kwa sababu, Mheshimiwa Lowassa amesema serikali haifanyi maamuzi magumu?”

Nchimbi pia alisema Nape ni “mropokaji” anayevuruga chama.
Wengine walioshupaliwa kwa kuchangia kukidhoofisha chama ni Samwel Sitta na Dk. Harrison Mwakyembe ambao ni miongoni mwa waasisi wa Chama cha Jamii (CCJ) huku wakiwa bado viongozi na wanachama wa CCM. Hata hivyo, CCJ kilinyimwa usajili wa kudumu.
Aliyetoa hoja hiyo ni Hussen Bashe ambaye anajitambulisha ni kutoka kundi la Lowassa na Rostam. Habari zinasema kwamba Mukama alimwita Bashe na kumwomba agombee ubunge Igunga, lakini Bashe alimgomea kwa maelezo kuwa hana mizizi ya kisiasa katika jimbo hilo.
“Nilitaka ubunge wa Nzega, si Igunga. Huko si kwetu. Siwezi kwenda Igunga kwa sababu nataka mshindwe ili tuheshimiane,” Bashe alinukuliwa akimweleza Mukama.

Vile vile, vijana hao walimtaka Mukama aagize serikali imwondoe Sitta katika nyumba ya spika, kwa maelezo kwamba kitendo chake kung’ang’ania nyumba hiyo huku akijua alishaachia uspika ni kinyume cha utaratibu, na kinagombanisha wananchi na serikali yao.

Pengo: Nitawachunguza mapadri wauza "unga"

ASKOFU Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam, Mwadhama Policarp Kardinari Pengo, ametangaza kuwachunguza viongozi wa kanisa lake ili kujua kama wanajihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

Hatua hiyo imekuja miezi michache baada ya Rais Jakaya Kikwete kuwatuhumu hadharani viongozi wa dini kujihusisha na biashara hiyo.

Akizungumza mwishoni mwa wiki katika kipindi maalumu cha kuadhimisha miaka 67 ya kuzaliwa kwake kilichorushwa hewani kupitia Redio na Tv Tumaini, Mwadhama Pengo alisema kuna haja kwake kama kiongozi wa kanisa kulifanyia kazi suala hilo.

"Kuna changamoto ambayo imejitokeza siku za hivi karibuni nchini, kwamba tunajua kuwa kuna viongozi wa dini wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya, dawa ambazo huangamiza vijana, lakini serikali inawanyamazia, inawaonea aibu kwa kutowachukulia hatua.

"Kwangu mimi ndani ya kanisa ni lazima nianze kuona kama kuna ukweli wa hili kwa mapadri wangu, watawa na makatekista. Kama kuna yeyote anajihusisha na biashara hiyo sintamuonea aibu, ni lazima tuwe na ujasiri katika kupambana na haya.

"Kumwonea aibu mtu wa aina hiyo ni kusema aendelee kunipenda japokuwa ni muovu, huo ni ubinafsi kwa upande wa kiongozi," alisema Askofu Pengo ambaye ameonyesha kukerwa na suala hilo ambalo hii ni safari ya pili kulizungumza hadharani kwani wiki iliyopita alilizungumzia akiitaka serikali ya Jakaya Kikwete kutaja majina ya viongozi hao.

Alisema hakubaliani na kauli ya serikali kwamba haiwezi kutaja majina yao kwa hofu ya kulinda sifa na utukufu wao.

Alishangazwa na uvumilivu wa serikali kusikiliza kilio cha viongozi hao wa dini wanaojisalimisha wenyewe na kuomba wasitangazwe, ili kutunza heshima zao mbele ya makanisa wanayoyaongoza.
Pamoja na mambo mengine, askofu huyo ambaye analiongoza kanisa Katoliki kwa miaka 19 sasa tangu achaguliwe kushika wadhifa huo aliwataka viongozi kupambana na ubinafsi kuanzia katika nafsi zao pamoja na walio chini yao kwa kutowaonea aibu.

Alisema ubinafsi ni kizuizi kikubwa kinachokwamisha maendeleo ya watu iwe kikanisa hata kitaifa, hivyo inakuwa changamoto kwa yeyote anayekuwa kiongozi ndani ya serikali au sehemu nyingine na ili kuiondoa ni lazima suala hilo likafanyiwa kazi kikamilifu.

Akizungumzia miaka 50 ya Uhuru, alisema enzi za Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliliwekea taifa ari ya kutaka kutenda mambo kwa manufaa ya taifa na si kwa kujinufaisha binafsi.
Alihoji ni kwa kiasi gani moyo huo wa kutaka kujitoa ili kuendeleza taifa upo hivi sasa na akalitaka taifa kuomba kwa Mungu moyo huo usife na kwamba hali hiyo ndiyo itakayoleta maana ya uhuru ambao nchi inauadhimisha.

Alieleza kuwa wakati nchi inapata Uhuru alikuwa na umri wa miaka 17 na wakati huo alikuwa akisoma katika Seminari ndogo ya Kaengesa iliyopo Sumbawanga na wakati huo alisikia namna Mwalimu Nyerere alivyokuwa akipigania harakati za nchi kupata uhuru.
"Wakati huo wapo waliobeza hatua yake wakisema kuwa nchi ikipata uhuru Wazungu wangekasirika", wengine walisema tutakufa njaa, lakini kwetu sisi seminarini tuliona ni kitu cha fahari kwani tuliona kwamba tungeweza kupata manufaa kwa kujiendeleza zaidi kielimu," alisema Askofu Pengo.

Alitegua kitendawili na kusema kuwa akiwa shule alikuwa na ndoto nyingi kwani wakati mwingine aliwaza kuwa mwalimu wa chuo kikuu, rubani au hata mwanasheria.
"Nilikuwa na ndoto nyingi kiasi kwamba leo hii nisingekuwa mwangalifu msingekuwa nami, kwani mngekuwa na wengine lakini hata hivyo kwa neema za Mungu leo tuko pamoja," alisema Askofu Pengo.
Alisema pia darasani kwao walikuwa wanne waliokuwa na wito wa kuwa mapadri, lakini kwa bahati mbaya amebaki peke yake kwani wenzake walishafariki.

Saturday, July 23, 2011

Jairo awekwa benchi


SERIKALI imemsimamisha kazi Katibu Mkuu  wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo.  Hatua hiyo inalenga kutoa nafasi ya   ufanyika uchunguzi dhidi ya tuhuma  zinazomkabili zilizoibuliwa bungeni. Jairo anadaiwa kuziandikia barua idara na  taasisi zilizo chini ya wizara ili kila moja itoe  sh. milioni 50 kwa ajili ya kufanikisha  uwasilishaji wa makadirio ya matumizi ya  wizara kwa mwaka wa fedha wa 2011/2012. Anadaiwa pia kuwalipa posho za safari  watumishi wa wizara waliofuatana na  viongozi wa juu licha ya kuwa walishalipwa  na idara na taasisi zao. 
Wabunge Beatrice Shellukindo (Kilindi-CCM)  na Christopher Ole Sendeka (Simanjiro  -CCM), ndio walioibua tuhuma hizo  walipojadili makadirio ya wizara, kabla ya  serikali kuyaondoa bungeni.  Serikali iliyaondoa makadirio hayo bungeni  kutokana na hoja za wabunge kuwa  haijajipanga kukabiliana na tatizo la umeme.  Bunge limetoa wiki tatu kwa serikali  kujipanga na kuyarejesha. 
Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo,  akizungumza na waandishi wa habari jana  mjini hapa, alisema amemwagiza Mdhibiti  na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG), kufanya uchunguzi wa kina, ambao  anatakiwa kuukamilisha ndani ya siku 10  kuanzia alipopewa kazi hiyo. "Wakati uchunguzi ukiendelea, Jairo   amesimamishwa kazi.
Hatua nyingine  zitafanyika baadaye kulingana na matokeo  ya uchunguzi," alisema. Luhanjo alisema anatarajia kufanya uteuzi  wa mtu atakayekaimu nafasi hiyo katika  kipindi kisichozidi siku tatu. Luhanjo alisema baada ya uchunguzi  kukamilika na endapo tuhuma dhidi ya Jairo  zitathibitika, uamuzi dhidi yake utachukuliwa  na rais kwa kuwa ndiye mamlaka yake ya  uteuzi.

Alisema amechukua uamuzi huo dhidi ya  Jairo kwa kuwa sheria ya  utumishi wa  umma inampa uwezo wa kushughulikia  nidhamu serikalini. "Kwa sababu suala hili ni zito nimeamua  aende likizo, lakini baada ya uchunguzi na  nikipata matokeo ya uchunguzi huo nitampa  taarifa itakayoambatana na hati ya  mashitaka," alisema.
Akizungumzia utaratibu alisema baada ya  matokeo ya uchunguzi kupatikana, Jairo  atapatiwa taarifa itakayoambatana na hati  ya mashitaka, itakayoeleza kwa kifupi kosa  alilotenda na namna alivyolitenda ili atoe  majibu.  Luhanjo alisema katika kipindi hicho,  atakuwa amesimamishwa kazi na kuanza  kulipwa nusu mshahara.  Kwa mujibu wa Luhanjo, katika majibu,  anaweza kukubali au kukana tuhuma dhidi  yake, ambapo mamlaka ya nidhamu  itaendelea kutoa adhabu kulingana na uzito  na kwamba, kwa kuwa Jairo ni mteule wa  rais, ndiye atakayeamua hatima dhidi yake.

Awali, kabla Luhanjo hajatangaza uamuzi  huo, wabunge waliibua hoja hiyo wakitaka  kufahamu hatua zilizochukuliwa dhidi ya  Jairo. Hoja hiyo iliibuliwa wakati wa kipindi cha   maswali ya papo kwa hapo kwa waziri mkuu  bungeni, ambapo Rashid Ali Abdalah  (Tumbe -CUF), alihoji hatua ya Waziri Mkuu  Mizengo Pinda, kudai hana mamlaka ya  kumwadhibu Jairo. Katika swali la msingi Rashid alitaka  kufahamu ni kwa nini waziri mkuu alitoa  kauli kuwa hawezi kumwajibisha Jairo hadi  Rais Jakaya Kikwete atakaporudi wakati  makamu wake na yeye wapo.
Akiwasilisha hoja ya kuondoa bungeni  makadirio ya Wizara ya Nishati na Madini,  Waziri Mkuu Pinda alisema Rais Kikwete  ndiye atakayeamua kuhusu hatima ya Jairo  kwa kuwa ndiye aliyemteua. Waziri Mkuu Pinda akijibu swali la Rashid,  alisema makamu wa rais au waziri mkuu  hawana mamlaka kikatiba ya kumwajibisha  Jairo, kwani mwenye uamuzi wa mwisho ni  rais wa nchi.
"Naomba niwaambie waheshimiwa wabunge  kwamba, si kila jambo linalotokea wakati  rais anapokuwa hayupo au yupo nje ya nchi  linaweza kutolewa uamuzi na makamu wa  rais au waziri mkuu," alisema. Alisema ni kweli kwa mujibu wa Katiba ya  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kifungu  cha 47 (1) (c), rais anapokuwa nje ya nchi  makamu wake ndiye anayeshika madaraka  ya kuongoza taifa. Pinda alisema kuna wakati hata waziri mkuu  hupewa nafasi hiyo, kama na makamu wa  rais hayupo, lakini wote wawili wana ukomo  katika utekelezaji wa majukumu yao,  ikiwemo kuamua mambo ambayo ni rais  pekee anayepasa kuyaamua.

Thursday, July 21, 2011

Kikwete atoa ufafanuzi wa umeme


Katika mahojiano maalum na Rais Kikwete, mwandishi wa BBC, Omar Mutasa, kwanza alitaka kujua, pamoja na kutafuta wawekezaji ambao kimsingi watahitaji nishati ya umeme ya uhakika, kwa nini tatizo la umeme halijapatiwa ufumbuzi.

"Serikali haina uwezo wa kufanya mvua inyeshe", alisema Rais Kikwete.

Habari zaidi
http://www.bbc.co.uk/swahili/habari/2011...

Kikwete amweka kiporo Jairo

RAIS Jakaya Kikwete amemweka kiporo Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, David Jairo akisema ataona cha kufanya baada ya ziara yake ya Afrika Kusini.

Akizungumza jana nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma, baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu uvumi wa kujiuzulu kwa Jairo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, alisema hakuwa amepata taarifa rasmi ya kujiuzulu kwake.

Lakini alisema kilichopo ni kuwa alimjulisha Rais Kikwete mambo yaliyotokea Jumatatu bungeni kuhusu mjadala wa Makadirio na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini ambapo baadhi ya wabunge walitaka Jairo aondolewe.

“Amenijibu kuwa ‘sawa, nisubiri nitakaporudi Afrika Kusini tuone tunafanyaje’,” alisema Pinda akimnukuu Rais Kikwete.

Jumatatu wakati wa mjadala wa makadirio hayo, wabunge waliibua kashfa wakituhumu wizara hiyo kuchangisha Sh bilioni moja kutoka idara na taasisi zake kwa ajili ya kufanikisha uwasilishaji wa makadirio hayo.

Mbunge wa Kilindi, Beatrice Shelukindo (CCM), ndiye aliyeibua sakata hilo wakati akichangia hotuba ya Makadirio hayo kabla hayajaondolewa bungeni.

Katika kuthibitisha kashfa hiyo, Shelukindo aliwasilisha barua bungeni iliyoandikwa na Jairo ikizitaka idara na taasisi zote za wizara hiyo, kila moja ichangie Sh milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya uwasilishaji wa hotuba ya bajeti.

Mbunge huyo wa Kilindi pamoja na wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka (CCM) kwa nyakati tofauti, walihoji bungeni mantiki ya fedha hizo, takribani Sh bilioni moja na wakataka wizara ifafanue zimekusanywa kwa ajili gani.

Pinda katika hoja yake bungeni, alikiri kwamba Jairo aliudhi na kutibua wabunge na akaahidi kuwasilisha suala hilo kwa Rais Kikwete aliyemteua ili achukuliwe hatua.

“Lazima nikiri hata mimi nilishtuka sana tena si kidogo, kwani suala hili limegubikwa na maswali mengi hakuna namna ya kutetea,” alisema Pinda siku hiyo.

Thursday, June 30, 2011

Ex-spy chief backs Chadema protests






Dar es Salaam. Former Intelligence chief Hassy Kitine yesterday came out in support of the opposition Chadema’s stance on various issues.He told journalists in Dar es Salaam that demonstrations organised by Chadema across the country in protest at the spiralling cost of living and the party’s demand for the scrapping of sitting allowances were pertinent issues which the country’s leadership should take seriously.

Dr Kitine is the first prominent CCM cadre to have publicly supported Chadema’s cause, which has in recent months been roundly criticised by the ruling party and some opposition parties. He said it was a fact that the high cost of living was a heavy burden on Tanzanians, adding that something should urgently be done to address the situation.

Dr Kitine, a former Cabinet minister and MP, said whatever Chadema was doing to draw attention to such issues deserved support, and added that the opposition party should not be demonised for practising its democratic rights.
He made the remarks when journalists sought his comments on various national issues at the end of a meeting organised by Faidika, a microfinance institution in which he is a director.

Dr Kitine said he had also been closely following the debate on whether or not MPs and other holders of public office deserved sitting allowances.“What Chadema is doing is healthy for our democracy because everyone is entitled to their own opinion, but the views should be constructive…they should not be aimed at destroying the country.”

Dr Kitine warned that the widening gulf between the rich and poor was “very dangerous”, saying it posed a serious threat to peace and stability in Tanzania.He said the country could not expect to remain peaceful forever when a few individuals controlled 99 per cent of the economy.

Dr Kitine said he was only trying to speak the “truth”, although he was aware that his comments would not go down well in some quarters.“I, like other Tanzanians, am giving my views on various national issues, but I know that some people are not happy with my comments. But even if I don’t say what I am saying, other people will say it.”

On the Chadema demonstrations, Dr Kitine said what the opposition party was doing was a challenge to the government and other political parties.

“What we need to look at is what they (Chadema) are advocating in their demonstrations. If you talk of life having become unbearably tough, that’s reality because many people are feeling the pinch...I support the demonstrations although I’m a CCM member,” he said.

Comparing the reign of retired President Benjamin Mkapa and President Jakaya Kikwete’s Fourth Phase government, Dr Kitine said he had not noticed any major difference between the two phases.He said, however, that things had gone from bad to worse after principles enshrined in the Arusha Declaration were abandoned, adding that people were now freely buying their way into elective office.

“In the past, when I was appointed Director of Intelligence by Mwalimu Nyerere and later a minister before I became an MP, the sole motive for seeking leadership was to serve the people,” he said.

Dr Kitine said the political landscape had changed dramatically since the Arusha Declaration was shunted aside. It was very difficult in the past for people who had amassed wealthy and failed to explain its source to be allowed to seek elective office, he said.

In a swift response, CCM Publicity Secretary Nape Nnauye told The Citizen that there was nothing wrong with convincing people to fight for their rights, adding that the issue was how this was done.

“Even CCM has been doing a lot to raise people’s awareness and sensitise them on their rights. Take for instance the decision to construct a secondary school in every ward across the country…this aims at increasing people’s awareness by giving them education,” he said when he toured Mwananchi Communications Limited head office in Dar es Salaam.

“The difference is that while we (CCM) are empowering the people by educating them, Chadema stops people from engaging in economic activities by holding demonstrations daily and deceiving them that this is a shortcut to State House,” he said.

Saturday, June 18, 2011

President names new BOT Deputy Governor


President Jakaya Mrisho Kikwete has appointed Dr Natu El-Maamry Mwamba the new Deputy Governor of the Bank of Tanzania effective this week.

A State House statement released yesterday by State Chief Secretary Philemon Luhanjo said Dr Mwamba takes over from Dr Enos Bukuku, who was appointed Deputy Secretary General of the East African Community (EAC) in April this year.

His term in office commenced on Monday June 13, according to the State House briefing.
Before his appointment, the BoT economist served as a Senior Lecturer at the Department of Economics at the University of Dar es Salaam (UDSM).

Friday, June 17, 2011

MP advises govt to provide video on Balali`s burial


The government has been advised to provide video proof on the funeral and burial of former Governor of the Bank of Tanzania (BoT), Daudi Balali, who died and buried in the US about four years ago.
Speaking during the House question and answer session yesterday, Masoud Salim (Mtambile, CUF) asked the government whether the former governor was dead or alive, and if it is true that he died, then it should furnish the video detailing his funeral and burial.

Salim said it was necessary for the government to provide the video on the late governor’s funeral as evidence so that people could refrain from relating the incident to that of Osama bin Laden, the Al-Qaeda leader whom the American government claims it buried at sea. In a supplementary question, Salim had wanted to know when the government would seriously deal with the embezzlers of government funds.

In his response to the first question, Deputy Finance minister Gregory Teu said according to a report the government received from its embassy in the US, Balali died and he was buried in the States.
“What I am aware of and the information obtained from our embassy in the US, Balali died and everything concerning him had better be taken as bygone,” Teu said.

The Bank of Tanzania made an official announcement of Dr Balali’s death and burial in the US on May 2008.
However, the announcement has left suspicion among many Tanzanians, who have been questioning whether Dr Balali really died or not and have been asking for evidence on his burial. Dr Balali, who was former Governor of the Bank of Tanzania was seriously implicated in a massive corruption scandal involving embezzlement of more than USD116.5m (133bn/-) while in office during the third phase government.
Prior to his death however, a drama ensued that led to his resignation as he proceeded abroad allegedly for medical examination.

Pressured largely by the public, Dr Balali let it go, but in December 2007, a senior government official said he was not aware of the resignation.
“We have just read about the alleged resignation of the governor through the press” State House Director of Information Salva Rweyemanu said in a telephone interview.
He added: “If there is a letter to that effect, then its existence will be known later because the President is on leave.”
Leakage of Balali`s resignation became vivid when the resignation letter he submitted to President Kikwete detailing the reasons for his resignation surfaced.

In the letter, Dr Balali is alleged to have cited the reasons for resignation as having undergone a major operation at a Boston Hospital in the US where he had been admitted for “over three months.”
Some months later, it transpired that he was not going to come back to Tanzania. This was followed by the announcement that he died and had been buried in the US.

Answering the second question, the minister said the government has been taking serious measures to check theft and embezzlement of its funds, adding that between 1998 and 2010, it dismissed a total of 75 council directors besides taking action on 33 councils including filing cases against them in court.

In the basic question Salimu had wanted to know the loss the government has incurred in monetary terms due to negligence, theft and embezzlement in the period between January and October 2010.
In his answer, the minister said according to the Controller and Auditor General’s report 5.1bn/- was lost through theft, negligence and embezzlement in the 2009/ 2010 financial year.

He further said that after the ministry received the 2009/2010 CAG report, it took measures including informing the Prevention and Combating of Corruption Bureau and the Directorate of Criminal Investigation for further action.
 
SOURCE: THE GUARDIAN

Tuesday, May 31, 2011

Marando: Tunamtaka Rais Kikwete mahakamani
















Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, WAKILI Mabere Marando anayemtetea Profesa Costa Mahalu aliyekuwa na Balozi wa Tanzania nchini Italia, amesema ataiomba mahakama imlazimishe Rais Jakaya Kikwete kufika mahakamani kumtetea mteja mteja wake iwapo hatakubali kwenda kutoa ushahidi baada ya kuombwa kufanya hivyo kwa barua.Marando ametoa kauli hiyo wakati Profesa Mahalu na mwenzake Grace Martin wakianza kujitetea leo.

Mbali na utetezi wao binafsi, wanatarajia pia kuwa na mashahidi kadhaa wa kuwatetea akiwamo Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa pamoja na Rais Kikwete.Tayari Rais Mkapa amewasilisha mahakamani hapo hati yake ya kiapo akimtetea Profesa Mahalu na mwenzake kuhusiana na tuhuma zinazowakabili huku akibainisha kuwa yuko tayari kufika mahakamani iwapo italazimu.

Lakini hadi jana, Rais Kikwete alikuwa hajajibu barua aliyoandikiwa na Wakili Marando kwa niaba ya wateja wake wakimwomba akubali wa kufika mahakamani kuwatetea au kuwasilisha kiapo chake ambacho kitatumika kama ushahidi wa utetezi dhidi yao.

Marando alisema jana kuwa Rais Kikwete alikuwa hajajibu barua hiyo, lakini akasema ikiwa Profesa Mahalu atamaliza kujitetea pamoja na mashahidi wengine kabla Rais Kikwete hajakubali, wataiomba mahakama imkumbushe.

“Kama atakaidi hata baada ya mahakama kumwandikia, basi tutaomba kesi hiyo iahirishwe hadi mwaka 2016 (wakati atakapokuwa amemaliza muda wake wa urais) ili imlazimishe kuja kutoa ushahidi huo,” alisema Marando.

Mei 3, mwaka huu Wakili Marando alimwandikia barua Rais Kikwete yenye kumbukumbu namba MM/PCRM/2011/1 kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, akibainisha kuwa ni miongoni mwa mashahidi muhimu ambao wateja wao wamewaagiza wamwite.

Barua hiyo inabainisha kuwa umuhimu wa Rais Kikwete katika ushahidi huo wa utetezi unatokana na ukweli kwamba nyumba hiyo ya Ubalozi wa Italia ilinunuliwa wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na kwamba alikuwa na taarifa zote kuhusu mchakato wa ununuzi wake.

Mchakato huo, kwa mujibu wa barua hiyo ni pamoja na nguvu ya kisheria aliyopewa mteja wao ambayo ilisainiwa na Rais Kikwete wakati huo akiwa Waziri Septemba 24, 2004 pamoja na hotuba yake aliyoitoa Bungeni Agosti 3, 2004 akithibitisha kuwa ununuzi wa jengo hilo haukuwa na mushkeli wowote.

Pia barua hiyo inaweka wazi kuwa kuna barua nyingi tu ambazo Profesa Mahalu alimwandikia Kikwete akiwa waziri, pamoja na katibu mkuu wa wizara hiyo, ambazo anapaswa kuzitambua mahakamani wakati wa utetezi.

“Kwa hiyo tunaomba kwa unyenyekevu kabisa, uweke barua yetu hii mbele ya Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania; aisome na akueleze utujibu kama hana pingamizi kuja kueleza ukweli mahakamani. Kama muda wake hauruhusu, kulingana na ratiba zake za kitaifa, tunaomba aturuhusu tumwandalie kiapo (affidavit) kitakachoeleza yaliyotekea ili tukiwasilishe mahakamani badala ya kumwita yeye mahakamani”, inasisitiza barua hiyo na kuongeza kuwa hakuna kifungu cha Katiba kinachozuia Rais kuitwa kutoa ushahidi mahakamani.

Katika kiapo chake alichokiwasilisha mahakamani, Mkapa anamtetea Mahalu na akidai kuwa amefanya naye kazi kwa muda mrefu na anamjua kuwa ni mtu mwaminifu, mtiifu na mchakapakazi. Mkapa alieleza katika hati yake hiyo kuwa mchakato wa ununuzi wa jengo hilo ulifanyika wakati wa uongozi wake na kwamba alikuwa akijua kila kilichokuwa kikiendelea kuhusiana na ununuzi huo na kwamba ulifanyika kwa mujibu wa sheria.

Alifafanua kuwa mpango wa ununuzi wa jengo hilo ulikuwa ni utekelezaji wa sera ya serikali wa kuwa na majengo yake ya kudumu katika kila ubalozi kwa kununua au kujenga ikiwa ni njia ya kupunguza gharama za upangaji. Aliongeza kuwa serikali yake ilimpa Profesa Mahalu mamlaka yote kupitia nguvu ya kisheria ya kusimamia na kutekeleza mchakato wa ununuzi wa jengo.

Mkapa alisisitiza kuwa kupitia utaratibu wa serikali, alikuwa akijua kuwa taarifa ya uthamini wa jengo hilo iliyofanywa na Wizara ya Ujenzi ilikuwa ni Dola za Marekani 3.0 milioni wakati Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ilikadiriwa Euro 5.5 milioni: “Kupitia utaratibu wa serikali nilifahamu kuwa jengo hilo lilinunuliwa kwa gharama ya Dola za Marekani 3.0milioni sawa na Euro 3,098,741.40,” alisema Mkapa.
Pia Mkapa alisisitiza kuwa alikuwa na bado anatambua taarifa ya serikali bungeni ya Agosti 3, 2004 iliyoeleza na kuthibitisha kuwa taratibu zote za ununuzi wa jengo hilo zilifuatwa kwa mujibu wa maelekezo ya serikali na kwamba dalali alilipwa kikamilifu.

“Kwa kipindi chote ambacho nimefanya kazi na Balozi Mahalu katika nafasi mbalimbali za utumishi wa serikali ameonyesha tabia thabiti na za dhati, uaminifu, utiifu, uchapakazi na ubora," alisema Mkapa.

Alisema kuwa sifa hizo zilimfanya atunukiwe na Rais wa Italia, Tuzo ya Heshima ya Juu wakati wa kuadhimisha Siku ya Taifa hilo, muda mrefu baada ya kuwa ameondoka nchini humo.

Profesa Mahalu na mwenzake, Martin aliyekuwa Ofisa Utawala wa ubalozi huo wanakabiliwa na mashtaka hayo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakidaiwa kuhujumu uchumi kwa kuisababishia Serikali hasara ya Euro 2,065,827.60. Wanadaiwa kusababisha hasara hiyo kupitia mchakato wa ununuzi wa jengo la ubalozi huo, wakati wa utumishi wao.

Kutokana na mashtaka hayo, leo wanadiplomasia hao wanaanza kujitetea baada ya mahakama hiyo kuwaona kuwa wana kesi ya kujibu.Mahalu na Martin wanadaiwa kula njama na kutenda makosa hayo katika tarehe tofauti na katika maeneo tofauti huko Italia, likiwamo la kumpotosha mwajiri wao katika hati ya matumizi.

Miongoni mwa mashtaka hayo ni kwamba Septemba 23, 2002 huko Rome, washtakiwa wakiwa waajiriwa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walisaini vocha yenye namba D2/9/23/9/02 ikionyesha kuwa bei ya ununuzi wa jengo la ubalozi ni Euro 3,098,741.58, maelezo ambayo yalikuwa ni ya uongo na yenye nia ya kumdanganya mwajiri wao.

Monday, May 30, 2011

Mtikila: Ridhiwani nenda mahakamani




Mchungaji Christopher Mtikila
LICHA ya mtoto wa Rais Jakaya Kikwete, Ridhiwani kuwaandikia barua ya kusudio la siku 10 kuwafikisha mahakamani Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa na Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameambiwa aende huko mahakamani.

Katika kusudio lake Ridhiwani amedai kuwa endapo watashindwa kumwomba radhi na kumlipa Sh2 bilioni atakwenda mahakamani.Katika kusudio hilo, Ridhiwani amewataka wanasiasa hao wamwombe radhi na kumlipa fidia hiyo ndani ya siku kumi kuanzia Mei 13, kwa madai waliyoyatoa hadharani kuwa yeye ni bilionea aliyetajirika kifisadi.

Katika kusudio hilo, Ridhiwani pia amehusisha gazeti la Tanzania Daima ambalo amedai limechangia kumchafua kwa kuripoti madai ya wanasiasa hao dhidi yake.

“Tumeelekezwa na mteja wetu kuwataka wote kwa pamoja kukanusha na kusahihisha tuhuma zote na kuchapisha habari hiyo ya kuomba radhi kwa uzito na herufi kubwa (bold print) katika kurasa za mbele  wa gazeti hilo (Tanzania Daima) kwa siku tatu mfululizo hadi Mei 23, 2011," alieleza wakili Sam Mapande wa Law Associates, anayemwakilisha Ridhiwani.Wakili huyo aliendelea, "Pia, wote kwa pamoja mnatakiwa kulipa fidia ya Sh2 bilioni kwa madhara ya jumla aliyopata mteja wetu.”

Barua hiyo ya kurasa sita  imetaja baadhi ya maneno yaliyoandikwa kwenye matoleo mawili ya gazeti la Tanzania Daima yakimkariri Dk Slaa na Mchungaji Mtikila, wakimhusisha pia Rais Jakaya Kikwete na mwanaye (Ridhwani) na watu wengine walio karibu yake na matukio ya ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka na ofisi ya umma. Kwa mujibu wa Ridhiwani, madai hayo yamemchafulia jina, kumdhalilisha, kumshushia hadhi na heshima yake katika jamii inayomzunguka.

Mhariri wa gazeti la Tanzania Daima, Absalom Kibanda amekiri kupokea barua hiyo, lakini akasema hawezi kusema chochote kwa jambo ambalo ni la kisheria. “Kwa kuwa bado hatujafikishwa mahakamani, siwezi kusema tumejiunga vipi. Tunasubiri tufikishwe mahakamani kwanza,” alisema Kibanda.

Mchungaji Christopher Mtikila amemtaka mtoto huyo wa rais kwenda mahakamani haraka akidai kuwa hana shaka kwa kuwa ana ushahidi mzito kuthibitisha madai yake.Mtikila aliwaambia waandishi wa habari mjini Arusha jana kuwa, kesi hiyo itakuwa ni ukombozi kwa taifa kwa sababu itampa yeye na mwenzake, Dk Slaa muda wa kueleza kile alichokiita madudu yanayofanywa na mtoto huyo wa rais.
Mtikila aliendelea kudai kuwa Ridhwani anatumia vibaya ofisi na madaraka ya baba yake (Rais Kikwete) kujilimbikizia mali kinyume cha sheria.

“Kitendo cha Ridhwani kutaka aombwe radhi na fidia ni njia na ngazi muhimu itakayosaidia mambo mengi yaliyojificha kuwekwa hadharani," alisema Mtikila na kuongeza:"Tutatumia sheria zilizopo kuwabana wote ambao majina yao yameandikishwa kwenye mali za vigogo nchini waeleze walivyopata mali hizo na hapo ndipo watakapowataja wahusika halisi,” alisema Mtikila.

Kiongozi huyo wa DP aliendelea kudai kuwa viongozi wengi nchini wamejilimbikizia mali kupitia wizi na ufisadi, wakitumia nafasi zao za umma huku wakiandikisha majina ya watu wengine kwenye mali hizo kuficha umiliki wao.

Alidai kuwa kesi anayotaka kuifungua Ridhiwani itaibua mambo mengi kwani walioandikishwa majina kwenye mali hizo, watawataja wamiliki halisi badala ya kufungwa jela kwa kumiliki mali inayodhaniwa kuwa ya wizi au kupatikana isivyo halali.

Kwa upande wake, Dk Slaa jana hakupatikana kuzungumzia kusudio hilo la Ridhiwani kutokana na simu yake ya kiganjani kutopatikana kwa siku nzima.

Jana, Ridhiwani alipotakiwa kueleza nini kinafuata baada ya muda aliotoa kuisha alijibu kwa ufupi kuwa asingependa kuzungumzia suala hilo kwa kuwa ni jambo la kisheria na kwamba sheria ina kanuni zake.

"Ndugu yangu, sitaki kuzungumzia hili kwa kuwa sheria ina kanuni zake. Hili litazungumzwa mahakamani."
Dk Slaa na Mtikila walikaririwa mwanzo wa Mei wakisema kuwa mtoto huyo wa rais ana utajiri mkubwa licha ya kumaliza shule miaka ya karibuni huku wakimtuhumu kutumia cheo na madaraka ya baba yake kujitajirisha.
 

Friday, May 27, 2011

CUF yamtaka Nahodha ajiuzuru

*Ni kutokana na mauaji ya wananchi  watano Tarime 
*Yalaani, yasema huo ni ukiukwaji wa haki za binadamu


BARAZA Kuu la Chama cha Wananchi (CUF) limemtaka Waziri wa Mambo ya Ndani kuwajibika kutokana na mauaji yaliyotokea wilayani Tarime lakini pia kufanyika kwa uchunguzi wa kina juu ya tukio hilo.

Hatua hiyo ilifikiwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mapendekezo mbalimbali yaliyoazimiwa na kikao cha baraza hilo.

Alisema kuwa baraza hilo linalaani vitendo vya ukiukaji na uvunjaji wa haki za binadamu hususan mauaji ya raia yanayofanywa na Jeshi la Polisi ambayo yamekuwa yakiripotiwa kila mara.

"Inatuumiza sana kwa kuwa inaonekana jambo hili ni la kawaida kwa sababu watendaji wake hawachukuliwi hatua yoyote," alisema.

Prof. Lipumba alisema kuwa baraza hilo pia linamtaka Rais Jakaya Kikwete kutambua kuwa jukumu la kuleta maendeleo ya Watanzania ni la watu wote hivyo serikali yake isisite kutumia sera mbadala za CUF kwa maendeleo ya taifa.

Alisema serikali kupitia wizara ya Fedha na Uchumi na Wizara ya Nishati na Madini inatakiwa kuchukua hatua za kuhakikisha nchi na wananchi wake wananufaika na rasilimali za madini zilizopo hapa nchini hususani madini ya dhahabu ambayo bei yake katika soko la dunia imepanda.

"Dhahabu inayouzwa nje ni dola bilioni 1.5 kwa mwaka sawa na  asilimia 40  ya bidhaa za Tanzania zinazouzwa nje ya nchi," alisema.

Alisisitiza kuwa baraza hilo linataka kuona utajiri wa nchi unawanufaisha wananchi na kuisaidia nchi kujikomboa kutoka katika dimbwi la umasikini na kuacha kutegemea misaada kutoka nje ambayo imeifanya nchi kuwa tegemezi kwa miaka mingi.

Aliongeza kuwa baraza hilo linamtaka Waziri wa Nishati na Madini Bw.William Ngeleja kujiuzulu kwa kuwa ameshindwa kutumia vyanzo vya umeme vilivyopo nchini ili kukabiliana na tatizo sugu la nishati linaloikumba nchi yetu kwa sasa.

Alisema nchi imejaliwa vyanzo vingi ya umeme na maeneo mengi ya maporomoko ya maji, makaa ya mawe, madini na hata umeme wa jua ambao hauna gharama kubwa ya kufua.

"Ni miaka 50 tangu tupate uhuru hatuna sababu yoyote  ya kutokuwa na umeme wa uhakika, ni ufisadi tu ambao umekithiri katika serikali yetu," alisema.

Alisisitiza kuwa serikali ni lazima itambue kuwa hali ya kutokuwa na umeme wa uhakika imezorotesha uzalishaji viwanda,biashara,huduma katika hospitali na shule hivyo kusababisha uchumi wa nchi kuzorota.

Aliitaka serikali kuzingatia mapendekezo na hoja zinazotolewa na kamati ya Nishati na Madini ya Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania zinazolenga kupata ufumbuzi wa matatizo ya umeme.

Pia alisema baraza hilo linaitaka serikali kuwa makini katika suala zima la utunzaji na uhifadhi wa silaha nzito za kivita zenye madhara makubwa na kutaka zihifadhiwe mbali na makazi ya watu ili matukio ya milipuko ya mabomu ambayo yameshatokea mara mbili yasijirudie tena.