Monday, May 16, 2011

"Mwanafunzi" anusurika kifo Chuo Kikuu cha Tumaini


Kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja alinusurika kifo baada ya kushambuliwa vikali na wananchi wenye hasira kali Katika eneo la Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa. Kijana huyo alijifanya Mwanafunzi na kuingia katika darasa mojawapo chuoni hapo na kuiba simu ya mkononi. Arobaini ya kijana huyo ilifika pale ambapo alijaribu kukimbia na kuanguka sehemu yenye mawe na matofali ambayo baadae yangesababisha kifo chake. Baada ya kipigo kibaka huyo alirudisha simu ambayo alikuwa ameiba.
Hata hivyo Polisi waliwahi kufika katika eneo hilo na kuokoa maisha ya kijana huyo aliyekuwa amejifanya mwanafunzi.
Awali ilisemwa kuwa vibaka wamekuwa wakifika eneo la chuo na kuiba mali za aina mbali mbali zikiwemo kompyuta, Projector, na vifaa vingine mali za wanachuo na chuo kikuu cha Tumaini.


























1 comment:

  1. wananchi wabaya we jamaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa duhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh wangemtoa roho

    ReplyDelete