Tuesday, January 3, 2012

Wawili wafa maji sikukuu ya mwaka mpya

Taarifa hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Temeke, David Misime na kusema kuwa watu hao wamekufa maji baada ya kupigwa na wimbi zito na hadi sasa miili hiyo bado haijaonekana.

Aliwataja kuwa ni Emmanuel Mwanyika (23), mkazi wa Kibada ambaye alikufa fukwe iliyopo eneo la Sunrise Beach Kigamboni kwa kupigwa na wimbi zito kuzama na kunywa maji mengi akiwa na wenzake

Wa pili ni Asha Ibrahim (14), mkazi wa Kibugumo, ambaye alizama wakati akiogelea na wenzake katika eneo la Zabada Beach Kigamboni.

Kamanda Misime amesema miili hiyo bado haijapatikana na juhudi za kuisaka bado zinaendelea

No comments:

Post a Comment