Friday, January 6, 2012

Wabunge Dar ‘wafyata mkia’ kwa Dk Magufuli

WABUNGE wa Mkoa wa Dar es salaam wamenywea kwa Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, huku wakieleza kusubiri majibu ya malalamiko yao kutoka kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.Mwenyekiti wa wabunge hao, Abbas Mtemvu, alisema kinachofanywa na Waziri Magufuli ni maoni yake, lakini wao wanasubiri majibu ya Pinda.

Mtemvu alisema uwezo wa kumjibu wanao, lakini kutokana na kuandika malalamiko yao kwa waziri mkuu watakuwa wanavunja kanuni.Alisema alisikiliza kwa makini hoja za Dk Magufuli, lakini kutokana na kumwandikia barua Pinda watajibu pindi watakapopata majibu hayo.

Mbunge huyo alisema Ofisi ya Waziri Mkuu inatarajia kutoa majibu kuazia kesho, hivyo baada ya kupitia majibu hayo watatoa msimamo wao. Hata hivyo, wakati wabunge hao wakipinga kupanda kwa nauli hiyo ya Sh200, kifuko cha Misungwe mkoani Mwanza kinatoza Sh400.

“Sasa nitazungumza nini maana anachoongea waziri sijajua, lakini ninachosema hapa hebu tusubiri waziri mkuu ili tuweze kumjibu maana tuanalo la kujibu,” alisema.Aliwataka wananchi wawe watulivu maana kuanzia kesho majibu yatatolewa na Pinda kutokana na malalamiko yao.Dk Ndungulile akata tamaa

Naye, Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndungulile, alisema Dk Magufuli amebeza wananchi wa Kigamboni, maana kinacholalamikiwa siyo tangazo la kupandisha nauli, bali mchakato uliotumika kufikia uamuzi huo.
Dk Ndungulile kinachosubiriwa hapa na wananchi siyo kushuka kwa nauli, bali  kuangalia makundi maalumu yanayotumia kivuko hicho jinsi yatakavyosaidiwa.

“Nimemsikiliza Waziri Magufuli kwa makini sana, lakini ameshindwa kujua watu gani wanokwenda kufaidika na watu gani watakaoathirika na ongezeko hilo,” alisema.

No comments:

Post a Comment